Kipindi 01, Ripoti ya Moja kwa Moja Kuhusu Maisha ya Kanisa: Injili ya Ufalme Inanawiri: Kanisa la Mwenyezi Mungu Limeenea kwa Zaidi ya Nchi 120

04/11/2025

Mnamo 1991, Mungu alianza rasmi kazi ya Enzi ya Ufalme na kuanzisha Kanisa la Mwenyezi Mungu. Tangu injili ya ufalme ilipoanza kuenea rasmi huko Uchina ya bara mnamo mwaka wa 1995, watu kutoka dini na madhehebu yote waliotamani sana kuonekana kwa Mungu waliisikia sauti Yake, walikubali kazi Yake ya siku za mwisho, na kutiririka kurudi katika nyumba ya Mungu. Katika sehemu nyingi palitukia dini zote kuungana na kuwa moja, na watu wote wakimiminika kwenye mlima wa nyumba ya Mungu. Ulimwengu wa kidini ulikuwa ukingoni mwa kuporomoka kabisa. Baadaye, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilipata shutuma na mashambulizi kutoka ulimwengu wa kidini, na serikali ya CCP ilianzisha kampeni ya kikatili zaidi ya ukandamizaji na mateso dhidi yake. Licha ya haya, kwa mwongozo wa Mungu, watu wengi wateule Mungu walivumilia magumu mengi na kupita vizuizi vingi. Mnamo 2007, hatimaye walieneza injili ya Mungu ya ufalme ughaibuni. na Kanisa la Mwenyezi Mungu la kwanza lilianzishwa nchini Taiwani. Kwa kuwa injili ya ufalme imeenea kwa kasi kutoka Asia hadi Ulaya, na kisha hadi Amerika, Afrika, na Oshenia, Kanisa la Mwenyezi Mungu sasa limeanzisha makanisa katika zaidi ya nchi 120 kote duniani. Injili ya ufalme inaendelea kuenea kama moto mkali katika kila bara.

Katika kipindi hiki, tutakupeleka katika maisha ya kanisa la Kanisa la Mwenyezi Mungu nchini Italia.

00:10 Maelezo ya Mwenyeji

02:03 Injili ya Ufalme Inanawiri Ulaya, Kituo Chake cha Kwanza Kikiwa Italia

02:57 Injili ya Ufalme Inaenea kwa Upana Barani Amerika, na Kanisa la Mwenyezi Mungu Limeanzisha Makanisa Katika Nchi Moja Baada ya Nyingine

04:04 Injili ya Ufalme Inakita Mizizi Barani Afrika: Kanisa la Mwenyezi Mungu Linastawi Kote Barani

05:05 Injili ya Ufalme Imefika Oshenia, na Kanisa la Mwenyezi Mungu Limeanzisha Makanisa katika Nchi Moja Baada ya Nyingine

06:06 Mwanahabari Mwitaliano Eneo la Tukio

09:04 Kutazama Video ya Densi ya Kikristo: Wimbo wa Ufalme: Ufalme Washuka Duniani

09:46 Ushuhuda wa Kupitia wa Cristian

12:25 Ushuhuda wa Kupitia wa Enrico

14:08 Ushuhuda wa Kupitia wa Enzo

18:31 Mungu Anatamani Mwanadamu Afuatilie Ukweli na Aendelee Kuishi

19:47 Wakristo Wakitoa Baraka

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp