592 Kufanya Kazi kwa Uzembe Si Kutekeleza Wajibu

1 Kwa kufanya kazi kwa namna isiyo ya dhati ni kitu kichukiwacho sana kwa wajibu. Ukiendelea tu kutenda kwa namna isiyo ya dhati, hutaweza kutekeleza wajibu wako kiasi cha kutosha. Lazima uwe na shauku ya kuutekeleza! Fursa ya mtu kufanya wajibu wake ni jambo adimu, na asipochukua fursa hiyo ambayo Mungu amempa, basi itapotea. Siku moja akijaribu tena kutafuta nafasi ya kutekeleza wajibu wake, haitakuwa rahisi; kwa kweli, yawezekana fursa kama hiyo haitatokea hata kidogo. Kazi ya Mungu haimsubiri mtu yeyote, vilevile nafasi ya kutekeleza wajibu wa mtu. Si fursa nyingi ambazo huja, kwa hivyo lazima uzichukue.

2 Watasema kwamba wewe hufanya kila kitu kwa namna ya shaghalabaghala, ukipuuza chochote unachofanya; wewe si mwangalifu hata kidogo katika kazi yako. Ukilazimishwa kufanya jambo, basi wakati huo tu ndipo unapotia bidii kidogo; kama kuna mtu anayeangalia iwapo kazi yako imefikia kiwango kinachotakiwa, wakati huo unafanya kazi nzuri zaidi—lakini iwapo hapana mtu wa kuangalia, unazembea kidogo. Ukishughulikiwa, basi unajitahidi; vinginevyo, unasinzia kila wakati kazini na kujaribu kukwepa lawama kadiri uwezavyo, ukidhani kuwa hakuna atakayegundua. Muda unapita, na watu wanagundua. Watu watambaini kabisa, na atakuwa amepoteza kabisa heshima na uadilifu. Iwapo hakuna mtu anayeweza kumwamini, basi Mungu anawezaje kumwamini? Mtu kama huyo haaminiki.

3 Kwa upana, iwapo mtu kama huyo hufanya tu wajibu wake kwa namna isiyo ya dhati kila mara, na akiendelea kuwa mzembe kwa Mungu, basi yeye yuko katika hatari kubwa! Je, matokeo ya kuwa mdanganyifu kwa makusudi ni yapi? Kwa muda mfupi, utakuwa na tabia potovu, utafanya dhambi za mara kwa mara bila kutubu na hutajifunza jinsi ya kutenda ukweli wala hutautia katika vitendo. Kwa muda mrefu, unapofanya mambo hayo siku zote, matokeo yako yatatoweka; jambo hili litakuingiza matatani. Hali hii inajulikana kama kutofanya makosa makubwa bali kufanya makosa madogo siku zote. Mwishowe jambo hili litakusababishia athari zisizorekebishika. Hilo litakuwa jambo baya sana!

Umetoholewa kutoka katika “Uingiaji Katika Uzima Lazima Uanze na Uzoefu wa Kutenda Wajibu wa Mtu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 591 Utoe Uaminifu Wako kwa Ajili ya Nyumba ya Mungu

Inayofuata: 593 Kipimo cha Mungu cha Kupima Mema na Maovu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp