382 Mwisho Wako Utakuwa Upi?

1 Hii ni kwa sababu mwisho u karibu kwa vitu vyote na mbingu zote na dunia zimefikia hatima yake. Mwanadamu anawezaje kukwepa hatima ya maisha yake? Ni vipi ambavyo wale wanaomcha Mungu na kutamani sana Aonekane watakosa kuona siku ya kuonekana kwa haki ya Mungu? Wanawezaje kukosa kupokea thawabu ya mwisho ya wema? Je, wewe ni yule atendaye mema, au yule atendaye maovu? Je, wewe ni yule akubaliye hukumu yenye haki na kisha kutii, au kisha hulaaniwa? Umekuwa ukiishi katika nuru mbele ya kiti cha hukumu, au katika giza jahanamu? Je, wewe mwenyewe si unayejua kwa dhahiri sana kama mwisho wako utakuwa wa thawabu au wa adhabu? Je, wewe si unayejua kwa dhahiri sana na kufahamu kwa kina sana kwamba Mungu ni mwenye haki? Kwa hiyo, kweli, mwenendo wako uko vipi na una moyo wako wa aina gani? Je, umeacha kiasi gani kwa ajili Yangu? Unaniabudu Mimi kwa kina gani? Wewe mwenyewe unajua kwa dhahiri sana ulivyo Kwangu—je, hiyo si kweli? Unapaswa kujua vizuri zaidi kuliko mtu yeyote jinsi utakavyokuwa hatimaye!

2 Kweli Nakwambia, Niliwaumba tu wanadamu, na Nilikuumba wewe, lakini Sikuwakabidhi kwa Shetani; wala kuwafanya kwa makusudi muasi dhidi Yangu au kunipinga Mimi na kwa hivyo kuadhibiwa na Mimi. Hamjapata majanga haya kwa sababu mioyo yenu imekuwa migumu mno na mienendo yenu yenye kustahili dharau mno? Kwa hiyo si kweli kwamba mnaweza kuamua hatima yenu wenyewe? Je, si kweli kwamba mnajua ndani ya mioyo yenu, bora zaidi kuliko yeyote, vile mtaishia? Sababu ya Mimi kuwashinda watu ni kuwafichua, na pia kuhakikisha bora zaidi wokovu wako. Sio kukusababisha ufanye uovu au kwa makusudi kukusababisha uingie katika jahanamu ya uharibifu. Wakati utakapofika, mateso yako yote makuu, kulia kwako na kusaga meno—je, hayo yote hayatakuwa kwa ajili ya dhambi zako? Kwa hiyo, uzuri wako mwenyewe au uovu wako mwenyewe sio hukumu bora zaidi kukuhusu? Je, sio thibitisho bora zaidi ya kile ambacho mwisho wako utakuwa?

Umetoholewa kutoka katika “Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Ushindi (1)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 381 Mtu wa Aigan Gani Hawezi Kuokolewa?

Inayofuata: 383 Nani Awezaye Kuepuka Kuja kwa Nuru ya Mungu?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp