518 Kuelewa Ukweli Si Jambo Rahisi

1 Mara tu watu kwa kweli wanaelewa ukweli, wanaweza kutambua hali zao wenyewe za kuwa, kuona hadi kina cha masuala magumu na kujua njia inayofaa kutenda. Iwapo huelewi ukweli, hutaweza kutambua hali zako za kuwepo. Utataka kuasi dhidi yako mwenyewe lakini hutakuwa na wazo la kukifanya ama unachoasi dhidi yake. Utataka kujiacha mapenzi yako lakini ukifikiria kuwa mapenzi yako yanapatana na ukweli, basi utaweza vipi kuiacha? Hivyo, wakati watu hawana ukweli, wana uwezekano wa kufikiri kwamba chochote kinachotokana na mapenzi yao ya kibinafsi, uchafu wao wa kibinadamu na nia njema, upendo wa uliokanganyika wa binadamu na mazoea ya kibinadamu ni sahihi, na kwamba yanalingana na ukweli. Unawezaje, basi, kuasi dhidi ya vitu hivi?

2 Kama huelewi ukweli, au kujua ni maana ya kuuweka ukweli katika matendo, na kama macho yako yamefungwa na hujui pa kugeukia njia gani na hivyo basi unaweza tu kufanya mambo tu kulingana na kile unachofikiri ni sawa, basi utatenda mambo mengine ambayo yatapotoka na yenye makossa. Baadhi ya haya matendo yatakuwa ni kwa kutelekeza kulingana na, masharti, mengine yatatokea kwa shauku na mengine yatakuwa yametokea kutoka kwa Shetani na kuwa yatasababisha usumbufu. Watu wasio na umiliki wa ukweli wanatenda mambo kwa njia hii: kidogo kushoto, kisha kidogo kwa kulia, sahihi dakika moja na kisha kupotoka inayofuata, bila usahihi wowote. Wale wasiomiliki n ukweli wanachukua mtazamo mbaya wa vitu, hivyo basi watawezaje kushughulikia masuala vizuri? Wataweza kutatua vipi shida zozote?

3 Kuuelewa ukweli sio kitu rahisi kufanya. Kuweza kuelewa maneno ya Mungu inategemea, kuelewa ukweli na ukweli ambao watu wanaweza kuelewa pia una viwango vyake. Kuelewa kwao kwa maneno ya Mungu kutazuiliwa hata iwapo wamwamini Yeye kwa maisha yao yote. Hata wale ambao wamepata uzoefu kiasi wanaweza kufikia wakati ambapo wanakoma kuepuka kufanya yale mambo ambayo yanamkataa Mungu, kukoma kufanya yale mambo ambayo kwa dhahiri ni maovu. Haiwezekani kwao kutimia hali ambayo haina mchanganyiko wa mapenzi yao wenyewe ndani yake. Hata hivyo cha msingi ni kutambua sehemu ya mapenzi ya kibinafsi ambayo yanaenda kinyume na maneno ya Mungu, kinyume na ukweli na kinyume na mwangaza kutoka kwa Roho Mtakatifu. Kwa hivyo lazima utie juhudi kujua manenoya Mungu na ni kwa kuuelewa ukweli tu ndio unaweza kuwa na utambuzi.

Umetoholewa kutoka katika “Ni Kwa Kufuatilia Ukweli Tu Ndiyo Unaweza Kupata Mabadiliko Katika Tabia Yako” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 517 Tafuta Ukweli katika Vitu Vyote ili Kuendelea Mbele

Inayofuata: 519 Kupata Ukweli Kuna Maana Gani?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp