Tofauti Muhimu Kati ya Mungu Mwenye Mwili na Watu Wanaotumiwa na Mungu

Kwa miaka mingi Roho wa Mungu amekuwa akitafuta bila kikomo Akifanya kazi duniani. Kwa enzi nyingi Mungu Ametumia wanadamu wengi kufanya kazi Yake. Hata hivyo Roho wa Mungu bado hana mahali pazuri pa kupumzika. Kwa hivyo Mungu hufanya kazi Yake, akisonga bila kikomo katika watu tofauti, na kwa ujumla Yeye hutumia watu ili kufanya hili. Yaani, katika miaka hii yote mingi, kazi ya Mungu haijawahi kusimama, lakini inaendelezwa mbele katika mwanadamu, mpaka siku ya leo. Ingawa Mungu Amesema na Ametenda mengi, mwanadamu bado hamjui Mungu, hii ni kwa sababu Mungu hajawahi kuonekana kwa mwanadamu na pia kwa sababu Hana umbo lililo wazi. Na hivyo Mungu lazima Akamilishe kazi hii—kuwasababisha wanadamu wote wajue umuhimu wa Mungu wa matendo. Kufikia lengo hili, Mungu lazima afichulie wanadamu Roho Wake kwa uwazi na kufanya kazi miongoni mwao. Yaani, ni wakati tu ambapo Roho wa Mungu anaingia katika hali ya kimwili, anavaa nyama na mifupa na kutembea akionekana kati ya wanadamu, akiandamana nao katika maisha yao, wakati mwingine akionekana na wakati mwingine kujificha, ndipo wanadamu wataweza kumuelewa kwa undani zaidi. Kama Mungu daima Angebaki katika mwili, Hangeweza kumaliza kwa ukamilifu kazi Yake. Baada ya kufanya kazi katika mwili kwa kipindi cha muda, kumaliza huduma ambayo inastahili kufanyika Akiwa katika mwili, Mungu ataondoka kwenye mwili na Afanye kazi katika ulimwengu wa kiroho kwa mfano wa mwili kama vile Yesu Alivyofanya baada ya kufanya kazi kwa kipindi cha muda katika ubinadamu wa kawaida na kukamilisha kazi yote ambayo Yeye Alihitajika kukamilisha. Mnaweza kukumbuka fungu hili kutoka kwa “Njia…(5)”: “Nakumbuka Baba yangu Akiniambia, ‘Duniani, tafuta tu kufanya mapenzi ya Baba Yako na ukamilishe agizo Lake. Hakuna jambo lingine linalokuhusu Wewe.’” Je, unaona nini katika kifungu hiki? Wakati Mungu Anakuja duniani, Yeye Anafanya tu kazi Yake ndani ya uungu. Hili ndilo Roho wa mbinguni amemwaminia Mungu mwenye mwili. Anapokuja, anakwenda tu kuzungumza kila mahali, kutamka matamshi Yake kwa njia tofauti na kutoka kwa mitazamo tofauti. Yeye kimsingi Anachukulia kumruzuku mwanadamu na kumfundisha mwanadamu kama malengo Yake na kanuni Zake za kazi na hajihusishi na vitu kama uhusiano kati ya wanadamu au maelezo ya maisha ya wanadamu. Huduma Yake kuu ni kuzungumza kwa niaba ya Roho. Wakati Roho wa Mungu Anaonekana katika mwili kwa hali iliyo wazi, Yeye hukimu uzima wa mwanadamu na kuuweka wazi ukweli tu. Yeye hajihusishi katika kazi ya mwanadamu, yaani, Yeye hashiriki katika kazi ya binadamu. Binadamu hawezi kufanya kazi ya uungu, na Mungu hashiriki katika kazi za binadamu. Katika miaka yote tangu Mungu aje duniani kufanya kazi Yake, Yeye daima Ametumia wanadamu kuifanya. Lakini wanadamu hawa hawawezi kuchukuliwa kama Mungu mwenye mwili; wao wanaweza tu kuchukuliwa kama wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Lakini Mungu wa leo Anaweza kuzungumza moja kwa moja kutoka katika mtazamo wa uungu, Akitoa nje sauti ya Roho, na kufanya kazi kwa niaba ya Roho. Wanadamu wote ambao Mungu Ametumia katika enzi zote vivyo hivyo ni mifano ya Roho wa Mungu Akifanya kazi ndani ya mwili wa nyama, hivyo basi kwa nini hawawezi kuitwa Mungu? Lakini Mungu wa leo pia ni Roho wa Mungu Anayefanya kazi moja kwa moja katika mwili, na Yesu pia Alikuwa Roho wa Mungu Aliyefanya kazi katika mwili; Wote hawa wawili wanaitwa Mungu. Basi tofauti ni gani? Katika enzi zote, wanadamu ambao Mungu Ametumia wote wana uwezo wa mawazo na mantiki ya kawaida. Wao wote wanajua kanuni za mienendo ya binadamu. Wamekuwa na mawazo ya kawaida ya binadamu, na wamemilikiwa na vitu vyote ambavyo watu wa kawaida wanapaswa kumiliki. Wengi wao wamekuwa na vipaji vya pekee na werevu wa kiasili. Katika kuwafinyanga watu hawa, Roho wa Mungu Anatumia vipaji vyao, ambavyo ni zawadi zao Alizowapa Mungu. Roho wa Mungu Anayeleta vipaji vyao katika kazi, Akitumia uwezo wao kumhudumia Mungu. Hata hivyo, kiini cha Mungu hakina itikadi na hakina fikira. Hakiungani na mawazo ya binadamu na hata kinakosa vitu ambavyo binadamu wa kawaida huwa navyo. Yaani, Mungu hata hafahamu vizuri kanuni za maadili ya binadamu. Hivi ndivyo ilivyo Mungu wa leo Anapokuja duniani. Kazi Yake na maneno Yake hayajachafuliwa na nia au fikira za binadamu, bali ni dhihirisho la moja kwa moja la nia za Roho, na Anafanya kazi moja kwa moja kwa niaba ya Mungu. Hii ina maana kuwa Roho hunena moja kwa moja, yaani, uungu hufanya kazi moja kwa moja, bila kuchanganya ndani hata nia kidogo za mwanadamu. Yaani, Mungu katika mwili Anajumuisha uungu moja kwa moja, Hana mawazo ya binadamu au itikadi, na Haelewi kanuni za maadili ya binadamu. Kama kungekuwa na kazi ya uungu tu (kumaanisha iwapo ingekuwa Mungu mwenyewe pekee ndiye Anayefanya kazi hiyo), kazi ya Mungu haingeweza kufanyika duniani. Kwa hivyo Mungu Anapokuja duniani, lazima Awe na wanadamu wachache Anaowatumia kufanya kazi katika ubinadamu pamoja na kazi ambayo Mungu hufanya katika uungu. Kwa maneno mengine, Yeye Anatumia kazi ya mwanadamu ili kusaidia kazi Yake takatifu. La sivyo, mwanadamu hangeweza kuja katika mawasiliano ya moja kwa moja na kazi ya uungu. Hivi ndivyo ilivyokuwa baina ya Yesu na wanafunzi wake. Wakati wa maisha Yake duniani Yesu alipiga marufuku sheria za zamani na kuanzisha amri mpya. Pia alizungumza maneno mengi. Yote haya yalifanyika katika uungu. Wale wengine, kama vile Petro, Paulo, na Yohana, wote waliweka kazi yao ya baadaye juu ya msingi wa maneno ya Yesu. Yaani, Mungu alikuwa akizindua kazi Yake katika enzi hiyo, Akikaribisha mwanzo wa Enzi ya Neema; yaani, Alileta enzi mpya, Akaiondoa ile ya zamani, na pia kutimiza maneno “Mungu ni Mwanzo na Mwisho”. Kwa maneno mengine, mwanadamu lazima afanye kazi ya mwanadamu juu ya msingi wa kazi ya Mungu. Yesu alipomaliza kusema yote Aliyohitajika kusema na kumaliza kazi Yake hapa duniani, alitoka katika mwanadamu. Baada ya haya, watu wote, wakifanya kazi, walifanya hivyo kwa mujibu wa kanuni zilizoonyeshwa katika maneno Yake na kutenda kwa mujibu wa ukweli Alioongea. Hawa wote walikuwa watu waliomfanyia Yesu kazi. Kama ingekuwa ni Yesu pekee Yake akifanya kazi, haijalishi kiasi gani Yeye Angezungumza, bado wanadamu hawangeweza kuwa na uhusiano na neno Lake, kwa sababu Yeye Alifanya kazi katika uungu na angeweza tu kuzungumza maneno ya uungu, na Hangeweza kueleza mambo hadi kiwango ambacho watu wa kawaida wangeweza kuelewa maneno Yake. Hivyo basi ilimpasa kuwa na mitume na manabii waliokuja kabla Yake kuongezea kazi Yake. Hii ni kanuni ya jinsi Mungu mwenye mwili Hufanya kazi—kwa kutumia mwili wa nyama kusema na kutenda ili kukamilisha kazi ya uungu, na kisha kwa kutumia wanadamu wachache au zaidi wanaopendeza moyo wa Mungu ili kuongezea kazi Yake. Yaani, Mungu Anatumia wanadamu wanaopendeza moyo Wake kuongoza na kunyunyiza binadamu ili watu wateule wa Mungu waweze kuingia katika uhalisi wa ukweli.

Kama, katika kupata mwili, Mungu anafanya kazi ya uungu tu bila kuwa na wanadamu wachache wa ziada wanaopendeza moyo Wake kushirikiana na Yeye, basi mwanadamu hangekuwa na uwezo kabisa wa kuelewa mapenzi ya Mungu au kuwasiliana na Mungu. Mungu lazima atumie wanadamu wa kawaida wanaopendeza moyo Wake ili kukamilisha kazi hii, kutunza na kuchunga makanisa, ili kufikia kiwango ambapo mchakato wa ufahamu wa mwanadamu, ubongo wake unaweza kubuni. Kwa maneno mengine, Mungu anatumia wanadamu wachache wanaopendeza moyo wake “kutafsiri” kazi anayofanya katika uungu Wake, ili iweze kufunuliwa, yaani, kubadilisha lugha ya Mungu kuwa lugha ya binadamu, hivyo kwamba wanadamu wote waweze kuielewa, wote waifahamu. Kama Mungu hangefanya hivyo, hakuna mwanadamu angeweza kuelewa lugha takatifu ya Mungu, kwa sababu idadi ya wanadamu wanaoupendeza moyo wa Mungu, ni chache mno, na uwezo wa mwanadamu kufahamu ni dhaifu. Hiyo ndiyo maana Mungu hutumia njia hii wakati wa kufanya kazi katika mwili wa nyama. Kama kungekuwa na kazi ya uungu peke yake, mwanadamu hangeweza kabisa kujua au kuwasiliana na Mungu, kwa sababu mwanadamu haelewi lugha ya Mungu. Mwanadamu anaweza kuelewa lugha hii tu kupitia tu kwa nguvu ya wanadamu wanaopendeza moyo wa Mungu kufafanua maneno Yake. Hata hivyo, kama kungekuwa na wanadamu kama hao pekee wakifanya kazi katika ubinadamu, hilo lingeweza tu kudumisha maisha ya kawaida ya mwanadamu; lisingeweza kubadilisha tabia ya mwanadamu. Kazi ya Mungu basi haingekuwa na mwanzo mpya; kungekuwa tu na nyimbo zile zile za zamani, maelezo yale yale ya kawaida ya zamani. Ni kupitia kwa nguvu ya Mungu mwenye mwili pekee, Anayesema yote yanayohitajika kusemwa na kufanya yote ambayo yanafaa kufanywa katika kipindi cha Yeye kupata mwili, ambapo baadaye watu hufanya kazi na kupata uzoefu kulingana na maneno Yake, ndipo tabia ya maisha yao itaweza kubadilika na waweze kusonga na nyakati. Yeye ambaye Anafanya kazi katika uungu Anawakilisha Mungu, ilhali wale wanaofanya kazi katika ubinadamu ni wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Yaani, Mungu mwenye mwili ana tofauti kubwa na wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Mungu mwenye mwili Anaweza kufanya kazi ya uungu, lakini wanadamu wanaotumiwa na Mungu hawawezi. Mwanzoni mwa kila enzi, Roho wa Mungu huongea binafsi kuzindua enzi mpya na kuleta mwanadamu kwenye mwanzo mpya. Wakati Yeye Amemaliza kuongea, hili linaashiria kwamba kazi ya Mungu katika uungu Wake imekamilika. Baada ya hapo, wanadamu wote hufuata mwongozo wa wale ambao wametumiwa na Mungu kuingia katika uzoefu wa maisha. Vile vile, hii pia ni enzi ambapo Mungu huleta mwanadamu katika enzi mpya na Anampa kila mwanadamu mwanzo mpya. Kwa hilo, kazi ya Mungu katika mwili inahitimishwa.

Mungu haji duniani kufanya ubinadamu Wake wa kawaida uwe mkamilifu. Yeye haji kufanya kazi ya ubinadamu wa kawaida, ila kufanya kazi ya uungu katika ubinadamu wa kawaida. Kile ambacho Mungu huongea kama ubinadamu wa kawaida si kile ambacho mwanadamu anakifikiria kuwa. Mwanadamu hufafanua “ubinadamu wa kawaida” kama kuwa na mke, au mume, na watoto. Huu ni ushahidi kwamba mtu ni mwanadamu wa kawaida. Lakini Mungu haoni hivi. Anaona ubinadamu wa kawaida kama kuwa na mawazo ya kawaida ya binadamu, maisha ya kawaida ya binadamu, na kuzaliwa kwa watu wa kawaida. Lakini kuwa Kwake kawaida hakuhusishi kuwa na mke, au mume na watoto vile ambavyo mwanadamu anavyozungumzia hali ya kawaida. Yaani, kwa mwanadamu, ubinadamu wa kawaida ambao Mungu Anazungumzia ni kile mwanadamu angeona kama kukosekana wa ubinadamu, karibu ukose kuwa na hisia na kuonekana hauna mahitaji ya kimwili, kama vile Yesu, Ambaye kwa nje tu alikuwa mwanadamu wa kawaida na alichukua sura ya mwanadamu wa kawaida, lakini katika kiini hakuwa kabisa na vitu alivyo navyo mwanadamu wa kawaida. Kutokana na hili inaweza kuonekana kwamba dutu ya Mungu mwenye mwili haihusishi ubinadamu wote wa kawaida, lakini sehemu tu ya mambo ambayo wanadamu wanapaswa kuwa nayo, ili kuendeleza utaratibu wa maisha ya kawaida ya binadamu na kuruzuku uwezo wa kawaida wa binadamu wa akili. Lakini hivi vitu havihusiani na kile ambacho mwanadamu anaona kama ubinadamu wa kawaida. Ni vitu ambavyo Mungu mwenye mwili Anapaswa kuwa navyo. Hata hivyo, kuna baadhi ya wanadamu wanaoshikilia kwamba Mungu mwenye mwili Anaweza tu kuwa na ubinadamu wa kawaida iwapo Yeye ana mke, watoto na familia. Bila mambo haya, wanasema, Yeye si mwanadamu wa kawaida. Nakuuliza hivi basi, je, Mungu Ana mke? Je, inawezekana kwa Mungu kuwa na mume? Je, Mungu Anaweza kuwa na watoto? Je, hizi sio dhana zenye kosa tu? Hata hivyo, Mungu mwenye mwili hawezi kuchomoka kutoka katika nyufa kwenye miamba au kuanguka chini kutoka mbinguni. Anaweza tu kuzaliwa kwa familia ya kawaida ya binadamu. Hiyo ndiyo maana Anao wazazi na madada. Haya ndiyo mambo ambayo ubinadamu wa kawaida wa Mungu mwenye mwili lazima Awe nayo. Hivi ndivyo Yesu alivyokuwa. Yesu Alikuwa na baba na mama, na ndugu. Haya yote yalikuwa ya kawaida. Lakini kama Angekuwa na mke na watoto, basi Wake haungekuwa ubinadamu wa kawaida ambao Mungu alitaka Mungu mwenye mwili awe nao. Kama hali ingekuwa hivyo, Yeye Hangekuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa niaba ya uungu. Ilikuwa hasa kwa sababu Hakuwa na mke au watoto lakini Alizaliwa na wanadamu wa kawaida katika familia ya kawaida ndipo yeye alikuwa na uwezo wa kufanya kazi ya uungu. Ili kufafanua hili zaidi, kile ambacho Mungu anaona kama mwanadamu wa kawaida ni mwanadamu aliyezaliwa katika familia ya kawaida. Mwanadamu kama huyo tu ndiye anayestahili kufanya kazi ya Mungu. Kama, kwa upande mwingine, mtu huyo angekuwa na mke, watoto, au mume, mwanadamu huyo basi hangekuwa na uwezo wa kufanya kazi ya uungu kwa sababu angekuwa tu na ubinadamu wa kawaida ambao binadamu wanataka lakini si ubinadamu wa kawaida ambao Mungu anataka. Kile ambacho Mungu huona kuwa na kile ambacho Mungu huelewa ni tofauti sana mara nyingi, havifanani kabisa. Katika hatua hii ya kazi ya Mungu kuna mengi ambayo yanapingana na kutofautiana sana na fikra za wanadamu. Unaweza kusema kwamba hatua hii ya kazi ya Mungu hujumuisha uungu ukifanya kazi moja kwa moja, huku ukisaidiwa na ubinadamu. Kwa sababu Mungu anakuja duniani kufanya kazi Yake Mwenyewe badala ya kumruhusu mwanadamu aifanye, hiyo ndiyo maana Anajipa mwili wa nyama (katika mwanadamu wa kawaida asiye mkamilifu) ili kufanya kazi Yake. Anatumia mwili huu kuwapa wanadamu enzi mpya, kuwaambia wanadamu hatua inayofuata katika kazi Yake, na kuwataka watende kwa mujibu wa njia iliyoelezwa katika maneno Yake. Na hapo Mungu Anakamilisha kazi Yake katika mwili, na yuko karibu kuondoka kwa wanadamu, asiishi tena katika mwili wa ubinadamu wa kawaida, na badala yake kusonga mbali na mwanadamu ili kuendelea na sehemu nyingine ya kazi Yake. Kisha, kwa kutumia wanadamu wanaoupendeza moyo Wake, Anaendeleza kazi Yake hapa duniani miongoni mwa kundi hili la wanadamu, lakini katika ubinadamu.

Mungu mwenye mwili hawezi kukaa na mwanadamu milele kwa sababu Mungu Ana kazi zingine nyingi za kufanya. Yeye hawezi kufungwa katika mwili; lazima aondoe mwili ili kufanya kazi ambayo Anahitaji kufanya, ingawa Yeye hufanya kazi hiyo kwa mfano wa mwili. Wakati Mungu Anakuja duniani, Yeye hasubiri hadi Afikie umbo ambalo mwanadamu wa kawaida anapaswa kufika kabla ya kufa na kuwaacha wanadamu. Haijalishi mwili Wake ni mzee vipi, wakati kazi Yake imemalizika, Anaondoka na kumwacha mwanadamu. Hakuna kitu kama umri Kwake, Yeye hahesabu siku zake kulingana na maisha ya mwanadamu; badala yake Yeye hukamilisha maisha Yake katika mwili kulingana na hatua katika kazi Yake. Baadhi ya watu wanaweza kuhisi kwamba Mungu, kwa kuingia katika mwili, lazima akue mpaka afikie hatua fulani, Awe mwanadamu mzima, kufikia umri wa uzee, na kuondoka tu wakati mwili umeshindwa. Haya ni mawazo ya mwanadamu; Mungu hafanyi kazi kwa namna hiyo. Yeye Anakuja katika mwili kufanya kazi Anayostahili kufanya tu, bali si kuishi maisha ya kawaida ya mwanadamu ya kawaida ya kuzaliwa kwa wazazi, kuwa mtu mzima, kutengeneza familia na kuanza kazi, na kulea watoto, au kupitia panda shuka za maisha—shughuli zote za mtu wa kawaida. Mungu anapokuja duniani, huyu ni Roho wa Mungu akivaa mwili, akiingia katika mwili, lakini Mungu Haishi maisha ya mtu wa kawaida. Yeye huja tu kukamilisha sehemu moja katika mpango Wake wa usimamizi. Baada ya hapo Atawaacha wanadamu. Anapoingia katika mwili, Roho wa Mungu hakamilishi ubinadamu wa kawaida wa mwili. Badala Yake, kwa wakati ulioamuliwa kabla na Mungu, uungu unafanya kazi moja kwa moja. Kisha, baada ya kufanya yote ambayo Yeye anahitajika kufanya na kukamilisha huduma Yake kikamilifu, kazi ya Roho wa Mungu katika hatua hii imekamilika, na wakati huo maisha ya Mungu mwenye mwili yanaisha pia, bila kujali kama mwili Wake wa nyama umekamilisha maisha yake au la. Yaani, haijalishi mwili wa nyama unafika hatua gani ya maisha, muda ambao unaishi duniani, yote hutegemea kazi ya Roho. Haihusiani na kile mwanadamu anachoona kuwa ubinadamu wa kawaida. Chukua Yesu kama mfano. Yeye Aliishi katika mwili kwa miaka thelathini na mitatu na nusu. Kuhusiana na urefu wa maisha ya mwili wa binadamu, Yeye Hakupaswa kufariki Akiwa na umri huo na Hakupaswa kuondoka. Lakini Roho wa Mungu hakujali kuhusu hayo hata kidogo. Baada ya kazi Yake kumalizika, hapo mwili ulichukuliwa, ukitoweka pamoja na Roho. Hii ni kanuni ambayo Mungu hutumia kufanya kazi katika mwili. Na hivyo, kusema kwa uzito kabisa, ubinadamu wa Mungu mwenye mwili si lenye umuhimu wa kimsingi. Kusema tena, Yeye haji duniani kuishi maisha ya mtu wa kawaida. Yeye kwanza haasisi maisha ya kawaida ya binadamu na kisha Aanze kufanya kazi. Badala Yake, alimradi tu Amezaliwa katika familia ya kawaida ya binadamu, Yeye ana uwezo wa kufanya kazi ya Mungu, ambayo haijatiwa doa na nia zap mwanadamu, ambayo si ya mwili ambayo hakika haitumii njia za jamii au kuhusisha mawazo au fikra za mwanadamu, na aidha, isiyohusiana na falsafa za binadamu za kuishi. Hii ni kazi ambayo Mungu mwenye mwili ananuia kufanya, na pia ni umuhimu wa vitendo wa kupata mwili Kwake. Mungu anakuja katika mwili kimsingi kufanya hatua ya kazi inayohitaji kufanyika katika mwili, bila kupitia michakato mingine isiyo na maana, na, hana uzoefu wa mwanadamu wa kawaida. Kazi ambayo Mungu mwenye mwili anahitaji kufanya haihusishi uzoefu wa kawaida wa binadamu. Hivyo, Mungu Anakuja katika mwili ili kumaliza kazi Anayohitaji kukamilisha katika mwili. Yaliyobaki Hayamhusu. Hapitii michakato mingi isiyo ya maana hivyo. Mara kazi Yake inapokamilika, umuhimu wa kupata mwili Kwake pia unaisha. Kumaliza hatua hii kuna maana kwamba kazi ambayo Yeye Anahitajika kufanya katika mwili imekamilika, na huduma ya mwili Wake imekamilika. Lakini Yeye hawezi kuendelea kufanya kazi katika mwili kwa muda usio na mwisho. Yeye lazima aende mahali pengine kufanya kazi, mahali ambapo ni nje ya mwili. Ni kwa njia hii tu ndio kazi Yake inaweza kuwa kamili zaidi, na kupanuka vizuri zaidi. Mungu hufanya kazi kulingana na mpango Wake wa awali. Yeye Anajua vyema kazi Anayohitaji kufanya na kazi Aliyomaliza kama kiganja cha mkono Wake. Mungu humwongoza kila mwanadamu kutembelea njia ambayo Yeye tayari Ameamua. Hakuna anayeweza kuepuka hili. Ni wale tu ambao hufuata uongozi wa Roho wa Mungu ndio watakaokuwa na uwezo wa kuingia katika pumziko. Huenda ikawa kwamba, katika kazi ya baadaye, sio Mungu Atakayezungumza katika mwili ili kumwongoza mwanadamu, ila Roho anayegusika akiongoza maisha ya mwanadamu. Hapo tu ndipo mwanadamu atakuwa na uwezo thabiti wa kumgusa Mungu, kumwona Mungu, na kwa kikamilifu zaidi kuingia katika uhalisi ambao Mungu anataka, ili aweze kukamilishwa na Mungu wa vitendo. Hii ndiyo kazi ambayo Mungu ananuia kukamilisha, ambayo amepanga tangu zamani. Kutokana na hili, nyote mnapaswa kuona njia ambayo mnafaa kuchukua!

Iliyotangulia: Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni

Inayofuata: Katika Imani, Mtu Lazima Alenge Ukweli—Kujihusisha na Kaida za Dini Sio Imani

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp