Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

10/03/2018

Dong Mei, Mkoa wa Henan

Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

Mimi ni mtu wa kawaida. Niliishi maisha ya kawaida. Kama wengi wanaotamani sana mwanga, nilijaribu njia nyingi kutafuta maana ya kweli ya uwepo wa wanadamu, nikijaribu kuyapa maisha yangu umuhimu zaidi. Mwishowe, juhudi zangu zote zilikuwa bure. Lakini baada ya kuwa na bahati ya kutosha kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, mabadiliko ya muujiza yalitokea katika maisha yangu. Yalileta rangi zaidi katika maisha yangu, na nilikuja kuelewa kwamba ni Mungu pekee ni Mtoa wa kweli wa roho na maisha ya wanadamu. Nilikuwa na furaha kwamba hatimaye nilikuwa nimepata njia sahihi ya maisha. Hata hivyo, huku nikitekeleza wajibu wangu wakati mmoja nilikamatwa kiharamu na kuteswa kikatili na serikali ya CCP. Kutoka kwa hili, safari ya maisha yangu ilipata uzoefu ambao kamwe sitasahau …

Siku moja mnamo Desemba 2011 takribani saa moja asubuhi, mimi na kiongozi mwingine wa kanisa ulikuwa tukitekeleza hesabu ya mali ya kanisa wakati zaidi ya maafisa kumi wa polisi ghafla waliingia. Mmoja wa hawa polisi waovu alitukurupia na kusema kwa kelele: “Msisonge!” Baada ya kuona kilichokuwa kikitokea, kichwa changu kilishtuka. Kisha, polisi waovu walituchunguza kama magaidi waliokuwa wakitekeleza wizi. Pia walipekua kila chumba, walivigeuza shelabela kwa haraka sana. Mwishowe, walipata mali fulani ya kanisa, kadi tatu za benki, risiti za kuweka pesa, kompyuta, simu za rununu, na kadhalika. Waliyachukua yote ngawira, na kisha walituchukua sisi wanne kwa kituo cha polisi.

Alasiri, polisi waovu waliwaleta ndani dada wengine watatu ambao walikuwa wamewakamata. Walitufungia sisi saba katika chumba na hawakuacha tuzungumze, wala hawakuturuhusu tulale usiku ulipofika. Baada ya kuona dada wakifungiwa ndani na mimi, na kufikiri kuhusu ni kiasi gani cha pesa ambacho kanisa lilipoteza, nilikuwa nimezuzuliwa na wasiwasi. Yote ambayo ningefanya ni kuomba kwa dharura kwa Mungu: Ee Mungu! Huku nikikabiliwa na hali ya aina hii, sijui la kufanya. Tafadhali linda moyo wangu na kuufanya mtulivu. Baada ya kuomba, nilifikiri maneno ya Mungu: “Usiogope, mambo kama haya yanapotendeka kanisani, yote yanaruhusiwa na Mimi. Simama na kuzungumza kwa niaba Yangu. Kuwa na imani kwamba mambo na masuala yote yanaruhusiwa na kiti Changu cha enzi na yote yana nia Zangu ndani yayo(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 41). “Unapaswa kujua kwamba vitu vyote vilivyo katika mazingira yanayo wazunguka vipo hapo kwa ruhusa Yangu, Mimi napanga yote. Oneni wazi na muridhishe moyo Wangu katika mazingira Niliyokupa(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 26). Maneno ya Mungu yalizima hofu kubwa moyoni mwangu. Nilitambua kwamba, leo, hii hali imenipata kwa ruhusa ya Mungu, na kwamba wakati ulikuwa umewadia ambapo Mungu alitaka nimshuhudie. Baada ya kuelewa mapenzi ya Mungu, nilimwomba Mungu na kusema: “Ee Mungu! Nataka kutii utaratibu na mipango Yako na kusimama imara katika ushuhuda Kwako—lakini mimi ni wa kimo kidogo, na naomba kwamba Unipe imani na nguvu, na kunilinda katika kusimama imara.”

Asubuhi iliyofuata, walitutenga na kutuhoji. “Najua wewe ni kiongozi wa kanisa. Tumekuwa tukiwafuatia ninyi watu kwa miezi mitano,” alisema mmoja wa polisi waovu kwa maringo. Nilipomsikia akieleza kwa utondoti kila kitu ambacho walikuwa wamefanya kunifuatia, nilitetemeka kwaa woga. Katika akili yangu, nilifikiri, serikali ya CCP kweli inaweka matayarisho mengi katika kutukamata. Kwa kuwa tayari wanajua mimi ni kiongozi wa kanisa, hakuna jinsi wataniacha niende. Mara moja niliweka azimio langu mbele ya Mungu: Afadhali nife badala ya kumsaliti Mungu na kuwa Yuda. Baada ya kuona kuwa kuhoji kwao hakukuwa kunazaa matunda yoyote, walimpa mtu kazi ya kunitazama na kutoniacha nilale.

Katika siku ya tatu ya mahojiano, mkuu wa polisi waovu aliwasha kompyuta na kunifanya nisome taarifa zilizomsingizia Mungu. Kwa kuona kwamba sikuguswa, baada ya hapo alinihoji kwa makini kuhusu fedha za kanisa. Niligeuza kichwa changu kwa upande mmoja na kumpuuza. Hili lilimfanya kukasirika sana na alianza kutukana. “Haijalishi usiposema lolote—tunaweza kukuzuia bila mwisho, na kukutesa wakati wowote ule tunaotaka,” alinitisha kwa ukali. Katikati ya usiku huo, polisi walianza mateso yao. Walivuta mkono wangu mmoja nyuma ya bega langu na mwingine juu kutoka kwa mgongo wangu. Walifinya mgongo wangu na miguu yao, kwa nguvu walitia pingu vifundo pamoja. Ilikuwa uchungu sana kiasi kwamba nilipiga yowe kwa maumivu—mifupa na nyama katika mabega yangu zilihizi kana kwamba zingepasuka. Ningeweza tu kupiga magoti bila kusonga na kichwa changu kikiwa sakafuni. Nilifikiri mayowe yangu yangewafanya watulize makali kwangu, lakini badala yake waliweka kikombe cha chai kati ya pingu na mgongo wangu, jambo ambalo lilizidisha tena maumivu. Mifupa katika mwili wangu wa juu ilihisi kana kwamba ilikuwa imevunjwa nusu. Nilihisi uchungu sana hivi kwamba sikuthubutu kupumua nje na jasho baridi ilitiririka usoni pangu. Punde tu nilipohisi kwamba singevumilia uchungu tena, mmoja wa polisi waovu alichukua fursa hii kuniambia: “Tupe tu jina na tutakuachilia uende mara moja.” Wakati huo, nilimwita Mungu aulinde moyo wangu. Mara moja nilifikiria wimbo: “Mungu katika mwili, Anateseka, napaswa kuteseka kiasi gani zaidi? Ikiwa ningekubali giza, ningemwonaje Mungu? Ningewezaje kukuacha kutafuta unaodaiwa kuwa uhuru? Afadhali niteseke ili kufidia moyo Wako unaohuzunika” (“Kusubiri Habari Njema za Mungu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). “Ndiyo,” Nilifikiria. “Kristo ndiye Mungu mtakatifu na mwenye haki. Alipata mwili na kuja duniani kuleta wokovu kwa wanadamu waliopotoka kwa kina. Kwa muda fulani sasa, Amekiwa akiteswa na kuwindwa na serikali ya CCP na amepingwa na kushutumiwa na wanadamu. Haikumpasa Mungu kuteseka kwa njia hii, lakini Anavumilia haya yote ili kutuokoa.” Kwa hivyo, baada ya kutafakari, niliona kwamba nilikuwa nikiteseka sasa ili kupata wokovu—napaswa kupitia mateso haya. Iwapo ningekubali kushindwa na Shetani kwa sababu singeweza kuvumilia uchungu, ningewezaje kukabiliana na Mungu wakati wowote tena? Kufikiri hili kulinipa nguvu, na nikakua mgumu mara nyingine tena. Polisi waovu walinitesa kwa takriban saa moja. Walipoondoa pingu, mwili wangu mzima ulianguka bila nguvu sakafuni. “Usipoongea tutafanya hilo tena!” walinipigia kelele. Niliwatazama na kutosema chochote. Moyo wangu ulijawa na chuki kwa polisi hawa waovu. Mmoja wa polisi waovu alisonga mbele kutia pingu tena. Huku nikifikiri uchungu mkali sana ambao nilikuwa nimeupita karibuni, niliendelea kumwomba Mungu moyoni mwangu. Kwa mshangao wangu, alipojaribu kuvuta mikono yangu nyuma ya mgongo wangu hangeweza kuisogeza. Haikuwa uchungu sana, pia. Alikuwa akijaribu kwa nguvu sana hivi kwamba kichwa chake chote kilikuwa kimejaa jasho—lakini bado hangeweza kutia pingu. “Una nguvu mwingi!” alitweta kwa hasira. Nilijua kwamba huyu alikuwa Mungu akinijali, kwamba Mungu alikuwa akinipa nguvu. Shukrani iwe kwa Mungu!

Kufika alfajiri kulikuwa vigumu. Bado nilikuwa na kiwewe nilipofikiri nyuma jinsi polisi waovu walikuwa wamenitesa. Pia walinitisha, wakiniambia kwamba iwapo singesema chochote, wangelazimika kunipeleka ndani sana ya milimani na kuniua. Baadaye, walipokamata waumini wengine, wangesema nililisaliti kanisa—wangechafua jina langu, na kuwafanya ndugu wengine wa kanisa wanichukie na kunikana. Kufikiri hilo, moyo wangu ulizidiwa na mawimbi ya majonzi na kutojiweza. Nilijipata nikihisi mwoga na mnyonge. Akilini mwangu nilifikiri: Afadhali nife. Kwa njia hiyo sitakuwa Yuda na kumsaliti Mungu, wala sitakanwa na ndugu zangu. Pia nitaepuka uchungu wa mateso ya mwili. Kwa hivyo nilingoja hadi wakati ambapo polisi waovu waliokuwa wakinilinda hawakuwa wakitia makini na kuupiga kichwa changu kwa nguvu sana dhidi ya ukuta—lakini yote yaliyotokea ilikuwa kwamba kichwa changu kiliona kizunguzungu, sikufa. Wakati huo, maneno ya Mungu yalinipa nuru kutoka ndani: “Wengine wanapokuelewa vibaya, unaweza kumwomba Mungu na kusema: ‘Ee Mungu! Siombi kwamba wengine wanivumilie au kunitendea vyema, wala kwamba wanielewe au kunikubali. Naomba tu kwamba niweze kukupenda moyoni mwangu, kwamba niwe na utulivu moyoni mwangu, na kwamba dhamiri yangu ni safi. Siombi kwamba wengine wanisifu, au kuniheshimu, ninatafuta tu kukuridhisha kutoka moyoni mwangu’(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni kwa Kupitia Usafishaji tu Ndiyo Mwanadamu Anaweza Kuwa na Upendo wa Kweli). Maneno ya Mungu yaliondoa huzuni kutoka kwa moyo wangu. Ndiyo. Mungu huona mioyo ya ndani kabisa ya watu. Iwapo polisi wakinisingizia, hata kama ndugu wengine kwa kweli wanielewe visivyo na kunikataa kwa sababu hawajui kile kilichotendeka kwa kweli, naamini kwamba nia za Mungu ni nzuri; Mungu anajaribu imani na upendo wangu Kwake, na napaswa kufuatilia kumfanya Mungu kuridhika. Baada ya kubaini njama janja za Shetani, ghafla nilihisi mwenye fedheha na aibu. Niliona kwamba imani yangu kwa Mungu ilikuwa ndogo sana. Sikuwa nimeweza kusimama imara baada ya kupitia uchungu kidogo, na nilikuwa nimefikiri kutoroka na kuepuke mipango ya Mungu kupitia kifo. Lengo la polisi waovu katika kuzungumza maneno haya ya tishio lilikuwa kunifanya nimkane Mungu. Na isingekuwa ulinzi wa Mungu, ningedanganywa na njama zao janja. Nilipokuwa nikitafakari maneno ya Mungu, moyo wangu ulijawa na mwanga. Sikutaka tena kufa, ila kuishi maisha mazuri, na kutumia kile ambacho kweli niliishi kwa kudhihirisha kumshuhudia Mungu na kumletea Shetani aibu.

Polisi hao wawili waovu waliopewa kazi ya kunilinda waliuliza mbona nilikuwa nimegongesha kichwa changu dhidi ya ukuta. Nilisema kwa sababu polisi hao wengine walikuwa wamenipiga. “Kimsingi tunafanya kazi kupitia elimu. Usijali—sitawaacha wakupige tena,” mmoja wao alisema kwa tabasamu. Baada ya kusikia maneno yake ya faraja, nilifikiri: Hawa watu wawili si wabaya; tangu nikamatwe wamekuwa wazuri kabisa kwangu. Kwa hilo, nililegeza tahadhari yangu. Lakini wakati huo, maneno ya Mungu yalikuja ghafla moyoni mwangu: “Nyakati zote, watu Wangu wanapaswa kujihadhari dhidi ya hila danganyifu za Shetani, walinde lango la nyumba Yangu kwa ajili Yangu, … kitu ambacho kitawazuia kuingia katika mtego wa Shetani, wakati mtakapokuwa na majuto ya kuchelewa sana(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 3). Maneno ya Mungu yalinipa kumbusho la wakati wa kufaa, yakinionyesha kwamba njama janja za ibilisi ni nyingi, na napaswa kuwa hadhari dhidi ya ibilisi hawa wakati wote. Sikutarajia hata kidogo kwamba punde wangefichua tabia zao halisi. Mmoja wa polisi waovu alianza kumkashifu Mungu, huku mwingine aliketi chini kando yangu alinipapasa mguu wangu, akinitazama kwa jicho la husuda na kuuliza kuhusu fedha za kanisa. Jioni, alipoona kwamba nilikuwa nikisinzia, alianza kupapasa kifua changu. Baada ya kuona kwamba walikuwa wamefichua tabia yao halisi, nilijawa na hasira. Ni sasa tu nilipoona waliodhaniwa polisi wa watu walikuwa tu wahuni na wadhalimu. Haya yalikuwa mambo mabaya yenye kustahili dharau, ambayo wangeweza kufanya. Kama matokeo, niliweza tu kumwomba Mungu kwa dharura ili anilinde kutokana na madhara yao.

Katika siku kadhaa zilizofuata, polisi waovu hawakunihoji tu kwa makini kuhusu kanisa, lakini pia walichukua zamu kunitazama ili kwamba nisilale. Baadaye, walipoona jinsi sikuwa nimewapa chochote, polisi hao wawili waovu waliokuwa wakinihoji walizidi kwa ghadhabu. Mmoja wao alinishambulia vikali, akinizaba kofi usoni, akinipiga kwa vishindo mara kadhaa. Uso wangu uliwasha, ulianza kuvimba, na mwishowe ukawa wenye ganzi sana kiasi kwamba singehisi chochote. Kwa sababu maswali yao hayakuwa yamezaa matunda yoyote kutoka kwangu, jioni moja mkuu wa polisi waovu alinipigia unyende na kusema, “Unahitaji kuanza kufungua mdomo wako. Unajaribu subira yangu—siamini kwamba hakuna chochote tunaweza kufanya na wewe. Nimekutana na watu wengi wagumu zaidi kukuliko. Tusipokuwa wakali kwako, hutatii katu!!” Alitoa amri na polisi waovu kadhaa walianza kunitesa. Jioni, chumba cha mahojiano kilikuwa cha huzuni na cha kuogofya—nilihisi kana kwamba nilikuwa jahanamu. Walinifanya nichutame sakafuni na kufunga mikono yangu katikati ya magoti na miguu yangu. Kisha, waliingiza kifimbo cha mbao katikati ya mapindi ya mikono yangu na nyuma ya magoti yangu, wakilazimisha mwili wangu wote kupinda juu. Kisha walikiinua kifimbo na kukiweka katikati ya meza mbili, wakiuacha mwili wangu wote ukining’inia hewani na kichwa changu kikiwa juu chini. Punde waliponiinua juu, kichwa changu kilipata kizunguzungu na niliona vigumu kupumua. Ilihisi kana kwamba nilikuwa nikisongwa. Kwa sababu nilikuwa nilining’inishwa hewani juu chini uzito wangu wote ulikuwa ukiangukia vifundo vyangu. Mwanzoni, ili kukomesha pingu kuukata mwili wangu, nilifumbata mikono yangu pamoja kwa kukaza, nikaupinda mwili wangu, na kujaribu kwa nguvu kadiri nilivyoweza kubaki katika hali hiyo. Lakini nguvu yangu ilipungua polepole. Mikono yangu iliteleza kutoka kwa vifundo vya miguu hadi kwa magoti yangu, na pingu ilikata kwa kina katika mwili wangu, ikiniacha na uchungu mkubwa sana. Baada ya kuning’inia hivi kwa takribani nusu saa, ilihisi kana kwamba damu yote katika mwili wangu ilikuwa imejikusanya kichwani mwangu. Uvimbe mchungu katika kichwa changu na macho ulifanya yahisi kana kwamba yalikuwa karibu kulipuka. Makato ya kina yalikuwa yamechimbwa katika vifundo vyangu, na mikono yangu ilikuwa imevimba sana kiasi kwamba ilionekana kama mikate miwili. Nilihisi nilikuwa ukingoni mwa kifo. “Siwezi kuvumilia tena, niweke chini!” nilipaza sauti kwa kukata tamaa. “Hakuna anayeweza kukuokoa ila wewe mwenyewe. Tuambie tu jina na tutakuacha uteremke chini,” alisema mmoja wa polisi waovu kwa ukali. Mwishowe, waliona kwa kweli nilikuwa katika taabu na waliniweka chini. Walinilisha glukosi kiasi na kuanza kunihoji tena. Nililala bila nguvu kama matope ardhini, macho yangu yakifumbwa kwa kukaza, nikiwa siwatilii makini. Bila kutarajia, polisi waovu waliniinua hewani tena. Bila nguvu ya kushikilia kwa mikono yangu, sikuwa na lingine ila kuacha pingu ijitie ndani katika vifundo vyangu, makali yaliyochongoka yakikata mwili wangu. Wakati huo, ilikuwa uchungu sana nilitoa yowe la kuhuzunisha sana. Sikuwa na nguvu ya kuendelea kupigana na kupumua kwangu kulikuwa kumekua kwa kina kifupi sana. Ilionekana kana kwamba wakati ulikuwa umesimama. Nilihisi kwamba nilikuwa nikiyumbayumba ukingoni mwa kifo. Nilipofikiri kwamba wakati huu kweli ningekufa, nilitaka kumwambia Mungu maneno yaliyokuwa moyoni mwangu kabla ya maisha yangu kuisha: “Ee Mungu! Wakati huu, ambapo kweli niko ukingoni mwa kifo, nahisi woga— lakini hata kama kweli nikifa leo, bado nitasifu haki Yako. Ee Mungu! Katika safari yangu fupi ya maisha, nakushukuru kwa kunichagua nirudi nyumbani kutoka kwa dunia hii ya dhambi, kunizuia kuzurura, nikiwa nimepotea, na kuniruhusu kuishi milele katika kumbatio Lako kunjufu. Ee Mungu, nimefurahia upendo Wako sana—na ilhali sasa tu, wakati maisha yangu yako karibu kuisha, ndipo nagundua kwamba sijatunza upendo Wako. Nyakati nyingi nimekufanya kuwa na huzuni na masikitiko; mimi ni kama mtoto mjinga anayejua tu kufurahia upendo wa mama yake, ilhali hajawahi kufikiria kuulipiza. Sasa tu ambapo niko karibu kupoteza maisha yangu ndipo naelewa kwamba ni lazima nitunze upendo Wako, na ni sasa tu ndipo najuta kukosa nyakati nyingi nzuri. Sasa, ninachojuta zaidi ni kwamba sijaweza kukufanyia lolote na unanidai mengi sana, na kama bado naweza kuishi, kwa hakika nitafanya kila niwezalo kutekeleza wajibu wangu, kufidia kile Unachonidai. Wakati huu, naomba tu kwamba Unipe nguvu, kuniruhusu kutowahi tena kuogopa kifo, na kuwa mwenye nguvu katika kile ninachokabili….” Tone baada ya tone la machozi lilianguka kutoka kwa paji la uso wangu. Usiku ulikuwa kimya kiasi cha kuogofya. Sauti ya pekee ilikuwa saa kubwa ikipiga ta-ta, kana kwamba kuhesabu sekunde ambazo zilisalia za maisha yangu. Hapo ndipo kitu cha muujiza kilifanyika: Nilihisi kana kwamba mwanga wa jua wa vuguvugu ulikuwa ukiniangazia, na polepole niliacha kuhisi uchungu mwilini mwangu. Maneno ya Mungu nguruma akilini mwangu: “Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Kwa kuchukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu Wake, unaanza safari yako katika maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeunda, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake mwenyewe, kwa maana yule Anayetawala kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu). Ndiyo—Mungu ndiye chanzo cha maisha yangu, Mungu hutawala kudura yangu, na lazima nijiachilie mikononi mwa Mungu na kujiweka katika matumizi Yake. Kutafakari maneno ya Mungu kulinipa hisia ya kufurahisha, tulivu moyoni mwangu, kana kwamba nilikuwa nikijinyoosha katika kumbatio kunjufu la Mungu. Nilijipata nikilala. Wakiwa na woga kwamba ningekufa, polisi waovu waliniweka chini na kwa haraka walinipa glukosi kiasi na maji. Katika kukaribia kwangu kifo, nilikuwa nimetazama matendo ya muujiza ya Mungu.

Siku iliyofuata, polisi waovu walishinda jioni nzima wakiniinua juu tena na tena. Walinihoji kuhusu mahali ambapo pesa za risiti ambazo walikuwa wamechukua ngariwa zilikuwa. Wakati huo wote, sikusema chochote—ilhali bado hawakukata tamaa. Ili kupata pesa za kanisa, walitumia kila njia yenye kustahili dharau kunitesa. Wakati huo, maneno ya Mungu yalirudia rudia moyoni mwangu: “Maelfu ya miaka ya chuki ikiwa imejaa kifuani, milenia ya dhambi imeandikwa katika moyo—inawezekanaje hii isichochee chuki? Kumlipiza Mungu, kuuondoa kabisa uadui wake, usimwache kutangatanga tena, na usimruhusu kufanya fujo zaidi kama anavyotaka! Sasa ndio wakati: Mwanadamu ana muda mrefu tangu akusanye nguvu zake zote, amejitolea nguvu zake zote, amelipa kila gharama, kwa hili, kuchana uso uliojificha wa pepo hili na kuwafanya watu, ambao wamepofushwa na kuvumilia kila aina ya mateso na taabu, kuinuka kutoka katika maumivu na kurudi kwa ibilisi huyu wa zamani(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi na Kuingia (8)). Maneno ya Mungu yalinipa nguvu na imani kubwa. Ningepigana hadi kufa na Shetani, na hata kama ningekufa, ningesimama imara katika ushuhuda wangu kwa Mungu. Nikitiwa msukumo na maneno ya Mungu, bila kujua nilisahau uchungu. Kwa njia hii, kila wakati waliniinua juu, maneno ya Mungu yalinitia msukumo na kunipa motisha, na hivyo kadiri walivyonibeba juu mara nyingi, ndivyo nilivyoweza kubaini asili yao zaidi—ambayo ilikuwa ya ibilisi waovu—na ndivyo azimio langu kusimama imara katika ushuhuda wangu na kumridhisha Mungu lilivyokuwa kubwa zaidi. Mwishowe, wote walichoshwa na mimi. “Watu wengi sana hawawezi kuvumilia kutundikwa hivi kwa nusu saa, lakini amevumilia wakati huu wote—kwa kweli yeye ni sugu!” Niliwasikia wakitoa mawazo. Kwa kusikia maneno haya, nilijawa na msisimko. Akilini mwangu, nilifikiri: Mungu msaada wangu, huwezi kunivunja moyo. Mbali na mateso ya mwili, wakati wa siku na usiku zangu tisa katika kituo cha polisi polisi waovu pia walininyima usingizi. Kila wakati nilipofunga macho yangu na kuanza kusinzia, wangepiga vifimbo vyao dhidi ya meza, au sivyo wangenifanya nisimame na kukimbia huku na kule, au sivyo kunipigia kelele tu, wakijaribu kunihuzunisha na kuvunja akili yangu. Baada ya siku tisa, wakiona kwamba hawakuwa wamefikia lengo lao, polisi bado hawakukata tamaa. Walinipeleka katika hoteli, ambapo walitia pingu mikono yangu mbele ya miguu yangu, kisha wakaingiza kifimbo cha mbao katikati ya mapindi ya mikono na miguu yangu, nikilazimika kuketi mwili wangu ukiwa umepinda juu sakafuni. Walinifanya nibaki katika hali hii nikiketi sakafuni kwa siku kadhaa zilizofuata, ambayo ilisababisha pingu kuukata mwili wangu. Mikono na vifundo vyangu vilivimba na kubadilika rangi kuwa zambarau, na kikalio changu kilihisi uchungu sana sikuthubutu kukisugua ama kukishika; ilihisi kama nilikuwa nikikalia sindano. Siku moja, mmoja wa viongozi wa polisi waovu, akiona kwamba mahojiano yangu hayakuwa yamezaa matunda, alitembea kunifikia akiwa amekasirika sana na kunizaba kofi kwa nguvu usoni—kwa nguvu kiasi cha kutosha kulegeza meno yangu mbili.

Mwishowe, wakuu wawili kutoka kwa Idara ya Usalama wa Umma ya Mkoa walikuja. Punde walipowasili, waliondoa pingu, wakanisaidia kwenda kwa kochi, na kunipa kikombe cha maji. “Umekuwa na wakati mgumu kwa siku chache zilizopita—lakini usilitilie moyoni, walikuwa wakifuata tu amri,” walisema kwa unafiki. Unafiki wao ulinifanya niwachukie sana kiasi kwamba nilisaga meno yangu. Pia kuwasha kompyuta na kunionyesha ushahidi usio kweli. Walisema maneno mengi ambayo yalishutumu na kufukuru dhidi ya Mungu. Moyoni mwangu, nilihisi kukasirishwa. Nilitaka kubishana nao, lakini nilijua kwamba kufanya hivyo kungewafanya tu kukufuru dhidi ya Mungu kwa wayowayo hata zaidi. Wakati huu, nilihisi kweli jinsi taabu aliyopitia Mungu mwenye mwili ilivyokuwa kubwa, na jinsi Mungu alivyovumilia fedheha nyingi kwa ajili ya kumwokoa mwanadamu. Kilicho zaidi, niliona uhafifu na kustahili dharau kwa ibilisi hawa waovu. Moyoni mwangu, kwa siri niliapa kwamba ningejiondoa kabisa kwa Shetani na milele kuwa mwaminifu kwa Mungu. Baadaye, bila kujali jinsi walivyojaribu kunidanganya, niliendelea kufunga mdomo wangu na sikusema chochote. Baada ya kuona kuwa maneno yao hayakuwa na athari yoyote, wakuu hao wawili waliondoka tu kwa hasira.

Katika kipindi cha siku na usiku kumi katika hoteli, waliendelea kunitia pingu, wakinifanya kuchuchumaa sakafuni nikishika miguu yangu. Nikikumbuka tangu nilipokamatwa, nilikuwa nimeishi siku na usiku kumi na tisa katika kituo cha polisi na hoteli. Ulinzi wa upendo wa Mungu ulikuwa umeniruhusu nilale kidogo, lakini polisi waovu hawakuwa wameniruhusu kulala wakati huo wote; ningefunga macho tu kwa muda na wangefanya chochote kilichohitajika kuniweka macho—kupiga meza, kunipiga teke kwa nguvu, kunipigia kelele, kuniamuru nikimbie huku na kule, na kadhalika. Kila wakati ningeshtuliwa, moyo wangu ungetwanga kifuani mwangu, na ningehisi woga sana. Hilo, likiongezwa kwa mateso ya mara kwa mara ya polisi waovu, na nguvu yangu iliishia kupunguka kabisa, mwili wangu wote ulikuwa umevimba na usiotulia, na niliona kila kitu vikiwa mbili mbili. Ningejua kulikuwa na watu mbele yangu wakiongea, lakini sauti ya milio yao ingeonekana kana kwamba ilikuwa ikitoka mbali sana. Zaidi ya hayo, mijibizo yangu ilianza kuwa ya polepole sana. Kwa mimi kustahimili hili kwa kiasi fulani kulikuwa yote kwa sababu ya nguvu kuu ya Mungu! Kama alivyosema Mungu: “Husababisha binadamu kuzaliwa upya, na kumwezesha kwa ushupavu kuishi kwa kila jukumu lake. Kwa sababu ya uwezo Wake, na nguvu ya maisha Yake yasiyopungua, binadamu ameishi kwa kizazi baada ya kizazi, ambapo nguvu ya uhai wa Mungu umekuwa uti wa mgongo wa kuwepo kwa binadamu, na ambayo Mungu amelipia gharama ambayo hakuna mtu wa kawaida amewahi kulipa. Nguvu za Mungu za maisha zinaweza kutawala juu ya nguvu zozote; zaidi ya hayo, inazidi mamlaka yoyote. Maisha Yake ni ya milele, nguvu zake za ajabu, na nguvu Zake za maisha haziwezi kuzidiwa na kiumbe yeyote au nguvu za adui(“Ni Kristo Wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele” katika Neno Laonekana katika Mwili). Moyoni mwangu, nilitoa shukrani na sifa ya uaminifu kwa Mungu: Ee Mungu! Unatawala vitu vyote, matendo Yako ni yasiyokadirika, Wewe pekee ni mwenyezi, Wewe ni nguvu ya maisha isiyozimika, Wewe ni chemichemi ya maji hai kwa maisha yangu. Katika hali hii maalum, nimetazama nguvu Yako maalum na mamlaka. Mwishowe, polisi waovu hawakupata majibu kwa maswali yao kutoka kwangu, na walinituma hadi katika kituo cha kuzuia.

Njiani kuelekea katika kituo cha kuzuia, polisi wawili waliniambia: “Umefanya vizuri sana. Ninyi watu huenda mkawa katika kituo cha kuzuia, lakini ninyi ni watu wazuri. Kuna aina nyingi hapo: wauza madawa, wauaji, malaya—utaona utakapowasili.” “Kwa kuwa unajua sisi ni watu wazuri, mbona mnatukamata? Je, serikali haiongei kuhusu uhuru wa dini?” niliuliza. “Hiyo ni Chama cha Kikomunisti inawadanganya. Chama hicho hutupa riziki yetu, kwa hivyo lazima tufanye kinachosema. Hatuna chuki kwako ama kuwa na kitu chochote dhidi yako. Tulikukamata tu kwa sababu unamwamini Mungu,” mmoja wa polisi alisema. Baada ya kusikia hili, nilikumbuka kila kitu nilichokuwa nimepitia. Singeweza kuzuia kukumbuka maneno ya Mungu: “Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi!(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi na Kuingia (8)). Maneno ya Mungu yaliulenga kiini cha suala, yakiniruhusu kuona kwa kweli sura ya kweli ya serikali ya CCP na jinsi inavyojaribu kupata heshima ambayo haistahili; kwa juu juu, inapeperusha bendera ya uhuru wa dini, lakini kwa siri inakamata, kukandamiza, na kushambulia wale wanaomwamini Mungu pande zote za nchi, katika tumaini bure la kupiga marufuku kazi ya Mungu, na pia inapora pesa za kanisa bila aibu,yote ambayo huweka wazi asili yake ya kishetani inayomchukia Mungu na kuchukia ukweli.

Nikiwa katika kituo cha kuzuia, kulikuwa na nyakati ambapo nilikuwa dhaifu na katika maumivu. Lakini maneno ya Mungu yaliendelea kunipa moyo, kunipa nguvu na imani, kuniruhusu kuelewa kwamba ingawa Shetani alikuwa ameniondolea uhuru wa mwili, mateso yalikuwa yameniongeza, yakinifundisha kumtegemea Mungu wakati wa mateso ya hao ibilisi waovu, kuniruhusu kuelewa maana ya kweli ya ukweli mwingi, kuona thamani ya ukweli, na kuongeza azimio langu na motisha ya kufuatilia ukweli. Nilikuwa tayari kuendelea kumtii Mungu, na kupitia yote ambayo Mungu alikuwa amenipangia. Kama matokeo, nilipokuwa nikifanya kazi katika kituo cha kuzuia, niliimba nyimbo na kwa kimya nilifikiri kuhusu upendo wa Mungu. Nilihisi kwamba moyo wangu ulikuwa umekuja karibu na Mungu, na sikuona tena siku zikiwa chungu ama za kudhikisha sana.

Wakati wa kipindi hiki, polisi waovu walinihoji mara mingi zaidi. Nilimshukuru Mungu kwa kuniongoza katika kushinda mateso yao mara kwa mara tena. Baadaye polisi waovu waliondoa pesa zote kutoka kwa kadi zangu tatu za benki. Kutazama bila kujiweza peza za kanisa zikichukuliwa na polisi waovu kuliuvunja moyo wangu. Moyo wangu ulijawa na chuki kwa hili kundi lafi, ovu la ibilisi, na nilitamani sana ufalme wa Kristo kuwasili punde. Mwishowe, licha ya kutokuwa na ushahidi wowote, walinihukumu mwaka mmoja na miezi mitatu ya kuelimishwa tena kupitia kazi kwa ajili ya “kuvuruga utulivu wa umma.”

Baada ya kuteswa kikatili na serikali ya CCP, kwa kweli nilikuwa nimeonja upendo na wokovu wa Mungu kwangu, na nilikuja kufahamu ukuu na uweza wa Mungu na matendo Yake ya muujiza, nilikuwa nimeona mamlaka na nguvu ya maneno ya Mungu. Aidha kwa kweli nilikuwa nimemdharau Shetani. Katika kipindi hicho cha mateso, maneno ya Mungu yalikuwa yameandamana na mimi kupitia mchana na usiku za kudhikisha, maneno ya Mungu yalikuwa yameniruhusu kubaini njama janja za Shetani na kutoa ulinzi wa wakati wa kufaa. Maneno ya Mungu yalikuwa yamenifanya kuwa mwenye nguvu na ujasiri, yakiniruhusu kushinda mateso yao katili mara kwa mara tena. Maneno ya Mungu yalikuwa yamenipa nguvu na imani, yalikuwa yamenipa ujasiri wa kupigana na Shetani hadi mwisho kabisa…. Shukrani ziwe kwa Mungu! Mwenyezi Mungu ndiye ukweli, njia na uzima! Daima nitamfuata Mwenyezi Mungu hadi mwisho kabisa!

Iliyotangulia: Ujana Usio na Majuto Yoyote

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ujana Usio na Majuto Yoyote

Xiaowen Jijini Chongqing“‘Upendo,’ kama unavyoitwa, unaashiria hisia safi isiyo na dosari, ambapo unatumia moyo wako kupenda, kuhisi,...

Utajiri wa Maisha

Wang Jun Mkoa wa Shandong Kwa miaka mingi tangu kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, mke wangu na mimi tumepitia hili...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp