Kutoka kwa Mateso Kunatoka Harufu Nzuri ya Upendo

10/03/2018

Xiaokai, Mkoa wa Jiangxi

Mimi ni mwanamke wa kawaida wa mashambani, na, kwa sababu ya dhana ya kikabaila ya kuthamini tu watoto wa kiume, sikuweza kuinua kichwa changu mbele ya wengine kwa ajili ya aibu ya kutozaa mtoto wa kiume. Wakati tu nilikuwa nikiteseka zaidi kabisa, nilichaguliwa na Bwana Yesu na, miaka miwili baadaye, nilikubali wokovu wa Mwenyezi Mungu. Aidha, nilielewa ukweli mwingi kutoka kwa ndani ya maneno ya Mwenyezi Mungu na moyo wangu ulipata ufunguliaji wa kweli. Hata hivyo, nilipokuwa nikitekeleza wajibu wangu wa kulipiza upendo wa Mungu, nilikamatwa mara mbili na serikali ya CCP na nilipitia mateso katili na maumivu mikononi mwa vibaraka wa CCP. Wakati tu nilikuwa ukingoni mwa kifo, maneno ya Mwenyezi Mungu yaliniongoza na kunitia moyo na kunisababisha kuwa na ushuhuda katikati ya madhara katili ya Shetani, hivyo kuimarisha azimio langu la kumfuata Mungu na kumpenda Mungu maisha yangu yote.

Takribani saa kumi na moja jioni moja, mnamo Mei 2003, nilikuwa njiani kutekeleza wajibu wangu wakati ghafla katibu wa kamati ya kijiji alikuja akiwa juu ya pikipiki na kuzuia njia yangu. Aliniamuru kwa ukali, akisema: “Simama! Unafanya nini? Kuja nami!” Nilifumaniwa, na nikatambua kwamba nilikuwa nimefuatwa. Mara moja nilifikiri kuhusu peja, risiti za pesa za kanisa na vitu vingine nilivyokuwa navyo mfukoni mwangu na kwamba, punde vitu hivi vingekuwa mikononi mwake, ingeleta hasara kubwa kwa kazi ya kanisa. Kwa hivyo nilikimbia kwa kasi kadri nilivyoweza, nikitumaini kupata fursa ya kurusha vitu vilivyokuwa mfukoni mwangu, lakini sikuenda mbali sana kabla ya yeye kunikamata. Muda mfupi baadaye, gari jeusi lilikuja na ghafla wakatokea polisi watano ama sita walioonekana wakatili ambao walinizingira mara moja. Walicheka kwa uovu na kusema: “Wakati huu, kweli tumekupata, kiongozi. Bado unafikiri unaweza kutoroka? Endelea kuota!” Kisha kwa nguvu walipinda mikono yangu nyuma ya mgongo wangu, wakaniweka katika gari la polisi na kunipeleka katika kituo cha polisi cha mtaa.

Nilipofika katika kituo cha polisi, polisi waovu walinirusha katika chumba ndogo, chenye giza, kilichonuka vibaya, na walianza kunitamkia kwa kelele na ukali: “Sema ukweli! Jina lako ni nani? Umetoka wapi? Unafanya nini hapa? Zungumza kwa sauti!” Moyo wangu ulikuwa ukigonga, nikiona tabia yao ya kutisha, na niliogopa kwamba vitu katika mfuko wangu vingeanguka mikononi mwao, na pia nilikuwa na woga kwamba wangenitesa kikatili. Wakati haya yote yalikuwa yakijiri, nililia kwa Mungu kwa shauku: “Ee Mungu, leo nimeanguka mikononi mwa ibilisi na hili limetendeka kwa ruhusa Yako. Bila kujali kile watakachonifanyia, natamani tu kusimama kando Yako. Naomba hekima Yako na imani ya kuwa na ushuhuda.” Wakati huo tu, nilifikiria maneno ya Mungu: “Haupaswi kuwa na hofu ya hili na lile. Haidhuru wingi wa matatizo na hatari unazokabili, utabaki thabiti mbele Yangu…. Usiwe na hofu; kwa msaada Wangu, ni nani angeweza daima kuzuia barabara?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 10). Kweli kabisa, Mungu ni wa pekee. Yeye husimamia vitu vyote na kutawala mambo yote, kwa hivyo si hawa polisi waovu wachache hata zaidi ni sehemu ya mipango ya Mungu? Mungu akinisaidia na kuwa na mimi, kulikuwa na nini zaidi ya kuogopa? Maneno ya Mungu yalinisababisha kuwa na imani na mwili wangu mzima ukawa umejaa nguvu, nisimwogope tena Shetani. Lakini wakati huo, bado nilikuwa na wasiwasi kuhusu vitu mfukoni mwangu, na moyo wangu daima ulimwilia Mungu kwa ajili ya ulinzi. Nilimshukuru Mungu kwa kusikia maombi yangu, na kundi hili la polisi waovu lilinihoji tu na halikuchunguza mfuko wangu. Wakati ulipofika wa wao kubadili zamu, wote waliondoka chumbani, na kwa haraka nilichukua risiti za akaunti na vifaa vya imani vilivyokuwa mfukoni mwangu na kuvirusha nje ya dirisha, na nilivunja peja sakafuni na kuirusha katika pipa la takataka, na hapo tu ndipo moyo wangu ungepata tulizo. Nilikuwa nimemaliza kufanya hili tu wakati ambapo polisi waovu wa zamu mpya ya polisi waovu waliingia chumbani. Walinipa mtazamo mkali, kisha kwa haraka walichunguza mfuko wangu, lakini hawakupata chochote. Niliona kwa macho yangu mwenyewe ukuu na uweza wa Mungu, na imani yangu iliongezeka pakubwa. Kwa sababu walikuwa wameambulia patupu, polisi waovu walinihoji kwa hasira, wakiniuliza nani hasa nilikuwa nimewasiliana naye, viongozi wa ngazi za juu walikuwa nani, na kadhalika. Niliogopa kwamba ningesema kitu na kuanguka katika mtego wao, kwa hivyo sikusema chochote kabisa. Kwa kuona hili, polisi watano ama wasita waovu walinijia mara moja kwa vichapo na mateke, wakinitukana wakifanya hivyo, wakisema: “Usipotuambia, tutakuchapa hadi ufe!” Nilichapwa vibaya sana nilipinda kuwa mpira, nikibingirika nyuma na mbele sakafuni. Kisha polisi mmoja mwovu kwa nguvu sana alivuta nywele zangu na kunitisha vikali: “Bado wewe ni mkaidi sana. Hutaongea? Tuna njia zetu, hivyo utaona jinsi tutakushughulikia leo usiku!” Nilijua Mungu alikuwa nami, na kwa hivyo nilikabili mateso yaliyokuwa yakija na moyo mtulivu.

Ilikuwa baada ya saa mbili usiku huo wakati ambapo polisi waovu wawili walinitia pingu na kufuatana nami hadi katika Shirika la Usalama wa Umma wa manispaa. Baada ya kuingia katika chumba cha mahojiano, polisi mmoja mwovu aliyekuwa katika miaka yake ya arobaini alianza kujifanya polisi mzuri, akijaribu kunilaghai na kunishawishi: “Wewe ni mdogo, na una sura nzuri. Haya yote kuhusu kumwamini Mungu ni nini? Shirikiana na kazi yetu. Mradi utuambie viongozi wa ngazi ya juu ni nani, nitamfanya mtu akupeleke nyumbani mara moja. Naweza kukusaidia na shida yoyote ambayo unaweza kuwa nayo. Mbona uteseke hapa? …” Kwa sababu ya ulinzi wa Mungu, nilijua kwamba hii ilikuwa hila janja ya Shetani, na sikumtilia maanani bila kujali kile alichosema. Polisi mwovu aliona kuwa hila yake haikuwa imefaulu, kwa hivyo mara moja alionyesha tabia yake halisi. Alinikamata kwa nywele na kunifinya dhidi ya sakafu, kwa ukatili akiupiga teke kichwa changu hadi nikahisi kizunguzungu na kuhisi mahali pote pakizunguka. Na hilo, alikanyaga kichwa changu na kusema kwa ukatili sana: “Huzungumzi? Nitafanya kila juhudi kukutesa leo, na utatamani heri hungezaliwa kamwe. Je, utatwambia tunachotaka kujua?” Kwa kuona kwamba bado sikusema chochote, aliwaita ndani polisi kadhaa zaidi waovu ambao walinivuta nisimame na kuanza kuzaba kofi uso wangu wote tena na tena, mpaka uso wangu uliumia sana ulihisi kama ulikuwa ukiungua moto. Lakini bila kujali jinsi walivyonipiga, nilimwomba Mungu kwa mfululizo na kimya, na nilikereza meno yangu na sikusema neno hata moja. Wakiona kwamba bado sikuwa nikisalimu amri, walinivuta hadi katika chumba kingine, wakibubujika hasira. Polisi mwovu alichukua kifimbo cha umeme na kunicheka kwa ubaya sana, akisema: “Haijalishi kwamba wewe ni sugu. Tuna njia zetu! Acha tuone ni ipi itadumu kwa muda mrefu zaidi—wewe ama kifimbo chetu cha umeme!” Kisha alinipiga kwa nguvu nacho kwa ukatili. Mara moja, mwili wangu mzima ulipenywa na mkondo mkubwa sana wa umeme na nilisukasuka pasipo kutaka. Ilikuwa ni kana kwamba wadudu wengi sana walikuwa wakiuuma mwili wangu, na singeweza kujizuia kutoa ukelele wa ghafula. Bila kusubiri nishike pumzi, polisi mwingine mwovu alichukua kikita cha magazeti nene na kuanza kuyaponda juu ya kichwa changu kwa nguvu zake zote, na kisha, alinivuta kwa ghafla kwa nywele na kwa ukatili alibamiza kichwa changu dhidi ya ukuta. Kila kitu kiligeuka cheusi na nikaanguka sakafuni. Polisi waovu walinitamkia kwa hasira, “Unajifanya mfu!” Kisha walinivuta juu kutoka sakafuni na kuniamuru nipige magoti, lakini nilikuwa dhaifu sana kiasi kwamba ningeweza tu kupiga magoti kwa muda mfupi kabla ya kuanguka sakafuni tena. Wakati huo, nilihisi kweli kwamba singeweza kuvumilia tena, singeweza kujizuia kuhisi dhaifu, na nilifikiri: “Hawa ibilisi kweli ni wakatili sana, na kweli nitakufa leo mikononi mwao….” Katika uchungu na kutojiweza, nilimwomba Mungu kwa ari kamili, nikimwomba Mungu aniongoze, na kwa ajili ya nguvu ya kumshinda Shetani. Wakati huo tu, maneno ya Mungu yalikuja ghafla akilini mwangu: “Mwenyezi Mungu, Mkuu wa vitu vyote, hushika madaraka Yake ya kifalme kutoka kwa kiti Chake cha enzi. Yeye hutawala ulimwengu na vitu vyote na Yeye yuko katika harakati ya kutuongoza katika dunia yote. Kila wakati tutakuwa karibu na Yeye…. Kama unayo pumzi moja tu, Mungu hatakuacha ufariki(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 6). Maneno ya Mungu yalinifanya nielewe kwamba maisha yangu yalikuwa yakishikwa mikononi mwa Mungu na kwamba, ilimradi Mungu hakutoa ruhusa Yake, basi ibilisi hawa hawangethubutu kuchukua maisha yangu. Nilifikiri jinsi nilikuwa nimemfuata Mungu mpaka hapo, jinsi Mungu alikuwa amenilinda njia hiyo yote, jinsi nilikuwa nimefurahia upendo wa Mungu sana na pakubwa sana, na nilifikiri kuhusu jinsi hali hii iliyokuwa ikifanyika sasa ilikuwa wakati wa Mungu kujaribu uaminifu na upendo wangu, na kwamba pia ilikuwa wakati wa mimi kulipiza upendo wa Mungu. Ibilisi walikuwa wakinitesa hivyo kwa lengo lenye kustahili kudharauliwa la kunitaka nimsaliti Mungu; lakini ningekuwa mtu mgumu. Mtu aliye na azimio na, hata kama wangenitesa hadi nife, bado singesalimu amri kwa Shetani. Katu singekuwa Yuda ili tu kwamba ningeendeleza kwa muda mrefu uwepo wa aibu—singeacha njama ya Shetani ifaulu, ningemshuhudia Mungu kabisa na kuacha moyo wa Mungu ufarijiwe! Maneno ya Mungu yalinipa nguvu isiyoisha, nilisahau uchungu ulioupiga mwili wangu wote, na kisha nilikuwa na imani na ujasiri wa kuendelea kupigana na ibilisi hawa.

Kisha, ili kutoa kukiri kutoka kwangu, polisi waovu walianza kuchukua zamu ili kunilinda na kunizuia kulala, wakinishinikiza na maswali tena na tena: “Viongozi wa ngazi ya juu katika kanisa lako ni nani? Wanaishi wapi? Nani pia ni mshiriki? … “Wakiniona nikibaki kimya, mara kwa mara wangenyakua nywele zangu na kunipiga teke. Ningefunga tu macho yangu na wangenichapa na kunipiga mateke na kutumia fataki za vidole vya mguu kwa viatu vyao vya ngozi kukanyaga na kusaga makonzi yangu kwa nguvu zao zote. Uchungu mkali ulinipa mateso yasiyosemeka, na niliendelea tu kupiga mayowe. Walinipiga mateke huku na kule kana kwamba nilikuwa mpira wa kandanda… Alfajiri ilipokuwa ikifika, nilikuwa nimeteswa sana kiasi kwamba mwili wangu wote ulijazwa na majeraha mengi na nilikuwa katika uchungu usiovumilika. Nilipofikiri jinsi sikuwahi kupitia mateso kama hayo awali, na nikifikiri kuhusu uharibifu na mateso niliyokuwa nikiyapitia sasa mikononi wa polisi waovu wa CCP kwa sababu ya imani yangu kwa Mungu, moyo wangu ungehisi huzuni na udhaifu tu. Wakati huo, yote yalikuwa giza ndani yangu, na hofu yangu ilikua na kua, nisijue ni mateso gani katili waliyokuwa wakinipangia ya kufuata. Nikiwa nimejilaza kwa uchungu, nilimwomba Mungu kwa kimya: “Ee Mwenyezi Mungu, nakuomba Unitie nuru na kuniongoza kuelewa mapenzi Yako katika taabu yangu, ili kwamba nisipoteze ushuhuda wangu.” Nilipokuwa nikiomba, nilifikiri kuhusu wimbo wa maneno ya Mungu: “Lazima uvumilie mateso kwa ajili ya ukweli, lazima ujitoe kwa ajili ya ukweli, lazima uvumilie udhalilishaji kwa ajili ya ukweli, na kupata ukweli zaidi lazima upate mateso zaidi. Hili ndilo unalopaswa kufanya. … Unapaswa kufuata yote ambayo ni ya kupendeza na mema, na unapaswa kufuatilia njia katika maisha ambayo ni ya maana zaidi. … Unapaswa kuziacha starehe zote za mwili kwa ajili ya ukweli mmoja, na hupaswi kutupilia mbali ukweli wote kwa ajili ya starehe ya muda mfupi(“Unapaswa Kuyaacha Yote Kwa Ajili Ya Ukweli” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Maneno ya Mungu yaliuamsha moyo wangu na kunifanya nielewe kwamba uchungu wa mateso niliyokuwa nikiyapitia sasa kwa ajili ya imani yangu kwa Mungu ulikuwa wa thamani kubwa zaidi na umuhimu mkubwa zaidi. Nilielewa kwamba Mungu alikuwa akitumia hali hii ya mateso kunionyesha waziwazi asili ya Shetani ambayo ina uadui na Mungu, ili kwamba ningeweza kumwacha kabisa na hivyo kugeuza moyo wangu kumrudia Mungu na kutimiza upendo wa kweli kwa Mungu. Mungu tayari amevumilia uchungu wote kwa ajili ya kuniokoa, kwa hivyo mwanadamu mpotovu kama mimi hapaswi kuteseka hata zaidi kwa ajili ya kupata ukweli na ili kupata mabadiliko ya kweli katika tabia ya maisha yangu? Mateso haya ni kitu ambacho napaswa kuvumilia katika ufuatiliaji wangu ili kupata wokovu, na nahitaji aina hii ya taabu kunituliza na kunirekebisha maadili: hili ndilo lile maisha yangu yanahitaji na natamani kukubali upendo mkuu wa Mungu. Leo, nateseka kandokando na Kristo na nashiriki katika ufalme wa Kristo na katika taabu Zake—hili kabisa ni kwa kupitia kuinuliwa na Mungu. Ni upendo mkuu zaidi wa Mungu na baraka kwangu, na napaswa kuwa na furaha. Nikifikiri hili, moyo wangu ulihisi kufarijiwa sana, na niliacha kuamini kwamba kukabiliana na hali kama hii ilikuwa kitu cha kuumiza, lakini kinyume chake nilihisi kwamba hii ilikuwa baraka maalum ya Mungu ambayo ilikuwa imenifanyikia. Kwa kimya nilitoa maombi kwa Mungu: “Ee, Mwenyezi Mungu! Natoa shukrani Kwako kwa kunipa nuru ili kwamba nielewe mapenzi Yako. Bila kujali jinsi Shetani ananitesa, sitaridhiana kabisa ama kusalimu amri kwake. Nikiishi au kufa, nataka kutii mipango Yako, kujitoa kabisa Kwako, na kukupenda hadi nife!” Polisi waovu walinitesa kwa usiku mbili na siku moja na hawakupata chochote kutoka kwangu kabisa. Mwishowe, yote ambayo wangesema ilikuwa kwamba tayari nilikuwa “nimefanywa Mungu”, na nilitumwa kwa nyumba ya kuzuia.

Punde tu nilipofika kwa seli katika nyumba ya kuzuia, mkuu wa bloku ya seli, kwa kushawishiwa na polisi waovu, alianza kunitisha: “Haya, kiri! Ama utateseka!” Akiona kwamba singesalimu amri, alishirikiana na wafungwa wengine kuniadhibu kwa kila njia inayowezekana: Hawakunipa chochote cha kula, hawakunipa maji yoyote ya moto, walinilazimu nilale kwenye sakafu baridi sana ya saruji kila usiku, na kunilazimu nifanye kazi ya kuchosha, chafu. Kama sikuimaliza ilinibidi nifanye kazi kwa saa za ziada, na iwapo sikuifanya vizuri vya kutosha nilidhulumiwa kwa maneno na kufanywa kusimama kama adhabu…. Kila siku nililazimika kukabiliana na kufanyiwa mzaha, kufedheheshwa, kubaguliwa, kuchapwa na kudhulumiwa kwa maneno na wafungwa wengine. Hata zaidi, pesa yangu ilikuwa imechukuliwa ngawira na polisi waovu kwa hivyo, bila hata senti moja, singeweza hata kununua vitu muhimu vya kila siku. Sikuwa na habari siku hizi zingeisha lini na ndani nilihisi huzuni sana, mpweke sana, na mwenye maumivu mengi sana, nikitamani daima kutoka mahali hapo pa kishetani haraka kadiri nilivyoweza. Lakini kadri nilivyotaka kutoka katika hali hiyo, ndivyo moyo wangu ulizidi kuwa wa giza na wenye kudhikishwa, na bila kutambua machozi yalitiririka kutoka machoni mwangu. Nikiwa sijiwezi sana, niliweza tu kumwambia Mungu tena na tena kuhusu uchungu wangu, nikimtumainia Mungu kwa ari aniongoze mara nyingine tena na kunifanya niweze kutii utaratibu na mipango Yake. Mungu ndiye msaada wangu na tegemeo langu wakati wote, na kwa mara nyingine tena Aliniongoza kufikiria kifungu hiki cha maneno Yake: “Haijalishi jinsi Mungu anavyofanya kazi, na haijalishi mazingira uliyomo, unaweza kufuatilia maisha na kutafuta ukweli, na kutafuta maarifa ya kazi ya Mungu, na kuwa na ufahamu wa matendo Yake, na unaweza kutenda kulingana na ukweli. Kufanya hivi ndiko kuwa na imani ya kweli, na kufanya hivyo kunaonyesha kwamba hujapoteza imani katika Mungu. Unaweza tu kuwa na imani ya kweli katika Mungu ikiwa bado unaweza kuendelea kufuatilia ukweli kupitia ukiwa katika usafishaji, ikiwa unaweza kumpenda Mungu kwa kweli na huna na mashaka kumhusu Yeye, ikiwa bila kujali Anachokifanya bado unatenda ukweli kumridhisha Yeye, na ikiwa unaweza kutafuta kwa dhati mapenzi Yake na ujali mapenzi Yake. Zamani, wakati Mungu alisema kwamba ungetawala kama mfalme, ulimpenda, na wakati Alijionyesha hadharani kwako, ulimfuata. Lakini sasa Mungu amejificha, huwezi kumwona, na shida zimekujia—je, hapo unapoteza matumaini kwa Mungu? Hivyo, lazima ufuatilie uzima wakati wote na kutafuta kuyaridhisha mapenzi ya Mungu. Hii inaitwa imani ya kweli, na huu ndio aina ya upendo ulio wa kweli na mzuri zaidi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Wanaopaswa Kukamilishwa Lazima Wapitie Usafishaji). Maneno ya Mungu yalikuwa kama mama mwenye upendo akimtuliza mtoto aliyedhikishwa, na yalinipa faraja na kunitia moyo sana. Nilihisi kwamba Mungu alikuwa kando yangu kabisa akinichunga na kunitarajia niweze kudumisha imani yangu ya kweli katika Mungu mbele ya Shetani, kuvumilia uchungu kwa kimya ili kuweza bado kumpenda na kumridhisha Mungu katikati ya hali ya kuumiza na nilipozongwa na nguvu za giza, na kumshuhudia Mungu—huu ni ushuhuda wa nguvu kabisa unaomwaibisha Shetani. Ingawa nilikuwa nimekamatwa katika pango la Shetani, upendo wa Mungu daima ulikuwa na mimi. Nilipopitia mateso katili na maumivu makali na kuhisi dhaifu, na wakati ambapo nilivumilia mashambulizi ya Shetani na kuhisi mwenye kuumizwa na kudhikishwa, daima niliweza kuona utoaji wa Mungu kwa ajili ya maisha yangu, ningeweza kuhisi faraja ya upendo wa Mungu, na ningeweza kuona mkono wa Mungu ukifungulia njia ya kutoka. Mungu daima yuko kando yangu, nilifikiri, akinilinda na kuwa nami. Upendo wa Mungu kwangu ni mkubwa sana, ningewezaje kutoridhisha mapenzi Yake kamwe? Napaswa kutotilia maanani mwili wangu na sembuse kujaribu kutoroka hali ambazo Mungu hunipangia. Napaswa kukumbuka imani niliyokuwa nayo awali, kutoa upendo wangu wa kweli kwa Mungu na kumshuhudia Mungu mbele ya Shetani. Nikifikiri vitu hivi, uchungu moyoni mwangu ulitoweka, na niliamua kumpenda na kumridhisha Mungu hata kama nililazimika kupitia maumivu yote makubwa. Sikuweza kujizuia kuimba wimbo wa kanisa: “Mimi ni mtu mwenye moyo na roho, hivyo kwa nini nisiweze kumpenda Mungu? Mungu ni msaada wangu, kuna nini cha kuhofu? Ninaahidi maisha yangu kupigana na Shetani mpaka mwisho. Mungu anatuinua, tunapaswa kuacha kila kitu nyuma na kupigana kuwa na ushuhuda kwa Kristo. Mungu atatekeleza mapenzi Yake duniani. Nitaandaa upendo wangu na uaminifu na kuvitoa kwa Mungu. Nitakaribisha kurudi kwa Mungu kwa shangwe atakaposhuka katika utukufu, na kukutana na Yeye tena ufalme wa Kristo utakapofanyika” (“Ufalme” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Nilipoimarisha imani yangu na tamaa ya kumridhisha Mungu, kwa mara nyingine tena nilipitia upendo mwema wa Mungu kwangu. Mungu alipanga ofisa wa gereza kunipa vitu vingi kwa matumizi yangu ya kila siku. Moyo wangu uliguswa sana na nilimshukuru Mungu kwa dhati. Baada ya siku 40, polisi waovu waliona hakukuwa na njia ya kupata chochote kutoka kwangu, kwa hivyo walinilazimishia mashtaka ya kuwa “mshirika wa dhehebu,” na kuuliza familia yangu kulipa yuan elfu kadhaa kabla ya kuniachilia.

Nilidhani ningepata uhuru wangu punde niliporudi nyumbani, lakini polisi wa CCP hawakuwahi kuacha kunifuatia na bado walizuia uhuru wangu binafsi. Walinikanya kutoka kwa nyumba yangu, wakaniamuru daima niwe wa kupatikana nao, na kumtuma mtu kunichunga. Pia walitishia familia yangu karibu kila baada ya siku chache, wakiwaonya waniangalie kwa makini. Kutoka kwa nje, ilionekana kana kwamba nilikuwa nimeachiliwa, lakini nilikuwa nimezuiliwa nyumbani kwa kweli na polisi waovu. Kwa hivyo sikuthubutu kuwasiliana na ndugu zangu katika kanisa, wala singeweza kutekeleza wajibu wangu, na moyo wangu ulihisi kukandamizwa na kuumizwa sana. Kitu ambacho kilinifanya hata mwenye uchungu zaidi kilikuwa kwamba polisi waovu walikuwa wakiwalaghai watu katika kijiji kwa uongo wao muovu, wakiwaambia kwamba imani yangu katika Mungu ilikuwa imenifanya kushikwa na wazimu, kwamba sikuwa sawa akilini na kwamba nilikuwa na uwezo wa kufanya lolote…. Huku nikikabiliwa na tabia yenye kustahili dharau kama kutoa uvumi kwao na kashfa, singeweza kuzuia kuiacha ichochee hasira yangu. Singeweza kudhibitiwa na ibilisi kwa njia hii, na napaswa kung’ang’ana kujiweka huru kutoka kwa mishiko yao miovu ya ibilisi na kulipiza upendo wa Mungu. Na kwa hivyo, ili kuepuka kufuatiwa na polisi waovu, sikuwa na lingine ila kuondoka nyumbani na kuenda kutekeleza wajibu wangu.

Miaka mitatu ilipita kufumba kufumbua. Nilidhani polisi wa CCP hawangekuwa wakinifuatia tena, kwa hivyo nilirudi nyumbani kutekeleza wajibu wangu. Hata hivyo, ilikuwa ghafla wakati, asubuhi moja mapema mnamo Agosti 2006, kabla ya mimi hata kuwa nyumbani kwa zaidi ya siku chache, polisi waovu walinitembelea. Asubuhi hiyo, sauti iliyokuwa ikipiga makelele iliniamsha kwa ghafla kutoka usingizini: “Harakisha na ufungue mlango, la sivyo tutauvunja!” Mume wangu alikuwa amefungua tu mlango wakati ambapo polisi saba ama wanane waovu waliingia upesi kama magaidi na, bila maelezo yoyote, walinishika na kunibeba kwa gari lao. Kwa sababu Mungu alikuwa akinilinda, sikuhisi hofu. Niliomba tu na kuomba: “Ee Mwenyezi Mungu! Leo tena nimeanguka katika mikono ya hawa ibilisi. Naomba Uulinde moyo wangu, Nipe nguvu, na hebu mara nyingine nikushuhudie Wewe.” Punde tulipofika kituo cha polisi, polisi waovu walinipiga picha kwa nguvu na kuchukua alama za vidole vyangu. Kisha walichukua orodha ya majina na kuanza kunishinikiza na maswali: “Je, unawajua watu hawa? Wenza wako ni nani?” Baada ya kuona majina niliyojua ya dada wengine kwenye orodha hiyo, nilijibu kwa utulivu: “Siwajui, na sina wenza!” Mara nilipomaliza kuzungumza mmoja wao aliniambia kwa sauti kubwa, “Ulitoweka kwa miaka kadhaa, kwa hivyo ulikuwa wapi? Hakika una wenza. Bado unamwamini Mwenyezi Mungu? Sema ukweli.” Maneno ya polisi mwovu yalinifanya mara moja mwenye huzuni na pia chuki, na nilikuwa na hasira sana: Kile ambacho naamini leo ni Mungu mmoja wa kweli ambaye aliumba mbingu na dunia na vitu vyote, kile ambacho natafuta ni ukweli, njia ambayo natembelea ni njia sahihi maishani, na vitu hivi vyote ni ng’avu na vya haki. Na ilhali ibilisi hawa, wasio na dhamiri kabisa, wanazidi kunifuata, wakizuia uhuru wangu binafsi, kunilazimisha niondoke nyumbani mwangu, kunitenga na familia yangu na kujaribu kunilazimisha nimsaliti Mungu. Kosa ni lipi la kumwamini Mungu na kutafuta kuwa mtu mzuri? Mbona wasiniruhusu nimfuate Mwenyezi Mungu na kutembelea njia sahihi maishani? Genge la ibilisi linalounda serikali ya CCP kweli ni kaidi na kafiri; wao ni adui wasioweza kupatanishwa kwa Mungu na hata zaidi ni adui ambao siwezi kuishi pamoja nao. Katika huzuni na chuki yangu, singeweza kuzuia kuleta maneno ya Mwenyezi Mungu akilini: “Vikaragosi hawa! Wanalipa upole kwa chuki, wanamtweza Mungu kwa muda mrefu, wanamtukana Mungu, ni washenzi kupita kiasi, hawamjali Mungu hata kidogo, wanapora na kuteka nyara, wamepoteza dhamiri yote, wanaenda kinyume na dhamiri yote … Udukuzi wao umeacha wote walio chini ya mbingu katika hali ya giza na machafuko! Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi! … Maelfu ya miaka ya chuki ikiwa imejaa kifuani, milenia ya dhambi imeandikwa katika moyo—inawezekanaje hii isichochee chuki? Kumlipiza Mungu, kuuondoa kabisa uadui wake, usimwache kutangatanga tena, na usimruhusu kufanya fujo zaidi kama anavyotaka! Sasa ndio wakati: Mwanadamu ana muda mrefu tangu akusanye nguvu zake zote, amejitolea nguvu zake zote, amelipa kila gharama, kwa hili, kuchana uso uliojificha wa pepo hili na kuwafanya watu, ambao wamepofushwa na kuvumilia kila aina ya mateso na taabu, kuinuka kutoka katika maumivu na kurudi kwa ibilisi huyu wa zamani(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi na Kuingia (8)). Kutoka kwa maneno haya ya Mungu nilielewa mapenzi Yake, na kuliibuka kwangu chuki kali kwa hawa ibilisi. Mungu aliumba mbinguni na dunia na vitu vyote na Yeye huwainua wanadamu; wanadamu hufurahia ukarimu mwingi wa Mungu, na kumwamini Mungu na kumwabudu Mungu daima imekuwa sheria ya mbinguni na kanuni ya dunia. Na ilhali serikali ya CCP inafanya kila iwezalo kuzuia wale wanaomwamini Mwenyezi Mungu kwa ukatili; inawawinda kinyama, inawatia gerezani kiharamu, kuwatesa na kuwatia maumivu kwa ukatili, huwazuia katika kambi za kazi na kuwatukana na kuwadhihaki, ikijaribu bila mafanikio kuangamiza wale wote wanaomwamini Mungu na kukomesha kazi ya Mungu ya kumwokoa mwanadamu katika siku za mwisho—kwa kweli ni ovu na ya kustahili dharau mno! Katika miaka hii, isingekuwa Mwenyezi Mungu kunilinda na kunitunza, ningeuwawa kikatili muda mrefu uliopita na Shetani ibilisi. Huku nikikabiliwa na mapigano haya ya roho ya uhai na kifo, nilikuwa na azimio: Ni lazima nitetee ukweli na lazima bado nimpende Mungu hata ingawa napitia uchungu mwingi, na naapa maisha yangu kumshuhudia Mungu!

Huku wakiniona nikiwakazia macho bila kusema neno, polisi waovu waliniongelesha kwa kero: Hutaongea, siyo? Ngoja hadi mabosi wetu waje kukuhoji wao wenyewe, na tutaona iwapo mdogo wako utabaki umefungwa!” Baada ya kusikia kwamba wakuu wa polisi waovu wangenihoji wao wenyewe, singejizuia kuhisi mwenye wasiwasi kidogo. Lakini nilifikiri kuhusu jinsi kwa kweli nilikuwa nimepitia ndani ya taabu ukuu wa Mungu juu ya yote na kusimamia Kwake vitu vyote, na kuhusu jinsi maneno ya Mungu yana mamlaka ya pekee na uhai wa nguvu, na mara moja kuliibuka ndani yangu imani na ujasiri wa kushinda nguvu za Shetani zenye uovu. Ingawa hawa polisi waovu ni wakatili mno na wasio na huruma, wao ni tishio la bure tu—wanaonekana wenye nguvu kwa nje lakini ndani wao ni dhaifu—na pia wanatawaliwa kwa hila na mikono ya Muumba. Moyoni mwangu, azimio langu kwa Mungu likawa dhabiti: Ee, Mungu, bila kujali jinsi ibilisi wananitesa, naomba tu kwamba Ufanye imani yangu kuwa imara, uimarishe moyo wangu ambao unakupenda, na kuniacha niwe ushuhuda Wako wa ushindi hata kwa kupoteza maisha yangu mwenyewe. Lazima ilikuwa baada ya saa nne usiku walipokuja wanaume wawili waliojiita naibu wakurugenzi wa Shirika la Usalama wa Umma. Waliniangalia bila kusema neno, kisha mmoja wao alinikamata kwa nywele na kunishinikiza kwa maswali: “Bado unamwamini Mwenyezi Mungu?” Kwa kuona kwamba nilibaki kimya, mkuu huyo mwingine mwovu wa polisi aliniambia kwa ukatili: “Usipoongea, tutakupa kionjo cha uchungu leo!” Alipokuwa akisema hili, akifoka kama mnyama mwitu, alinyakua nywele zangu na kunirusha sakafuni, na nilianguka kwa nguvu sana kiasi kwamba sikuweza kuinuka tena. Kisha walinivuta kwa nywele na kunichapa na kunipiga mateke, wakipiga kelele walipokuwa wakinichapa: “Je, utaongea?” Mara moja, uso wangu uliwaka kwa uchungu na ngozi yangu ya kichwa na nywele iliuma kiasi cha kutovumilika kana kwamba ilikuwa umeraruliwa. Hawa wanyama wawili wenye mavazi ya binadamu walionekana kwa nje kama wangwana wa heshima, lakini kwa ndani walikuwa wakatili na wasio na huruma kama wanyama mwitu. Walinifanya nione hata dhahiri zaidi kwamba chama hiki kiovu cha kiasa—CCP—ni mfano halisi wa Shetani, na vibaraka wake ni genge la ibilisi na roho waovu! Watakabiliana mwishowe na laana ya Mungu! Mabosi hawa wawili wa polisi waovu waliona kwamba sikuwa nikisalimu amri kwa nguvu zao za udikteta, kwa hivyo walinyakua nywele zangu na kuanza kunifinya dhidi ya sakafu kana kwamba walikuwa wamepoteza akili zao, wote wakiitumia miguu yao kunipiga mateke kwa utundu na kunikanyaga. Kisha walinivuta nisimame na kwa ukatili kukanyaga upande wa nyuma wa miguu yangu, wakinipiga teke chini kwa nguvu sana hivyo nilianguka nikipiga magoti sakafuni, na walisema kwa ukatili: “Piga magoti na usisonge! Unaweza kusimama utakaposema ukweli. Iwapo hutaongea, basi hata usithubutu!” Iwapo ningesonga hata kidogo, kwa ukali sana wangevuta nywele zangu na kunichapa na kunipiga mateke. Nilipiga magoti kwa saa tatu ama nne, kwa kipindi hicho walinipiga mara nyingi kwa sababu singeweza kubaki juu. Mwishowe, nilianguka sakafuni kwa kuchanganyika, na wakanikaripia kwa kujifanya kufa, na bila huruma na kwa ukali walivuta nywele zangu ili kwamba ngozi yangu ya kichwa na nywele iliumia kana kwamba ilikuwa imeraruliwa. Wakati huo, ilikuwa kama kwamba mwili wangu mzima ulikuwa umeanguka vipande vipande—singeweza kusongesha msuli na nilikuwa katika uchungu usiovumilika. Nilihisi kama moyo wangu ungeacha kugonga wakati wowote. Niliendelea kumwita Mungu kunipa nguvu, na ushawishi wa Mungu na maneno ya kutia moyo yaliingia akilini mwangu: “Petro aliweza kumpenda Mungu hadi kifo. Alipokufa—alipoangikwa msalabani—bado alimpenda Mungu; hakufikiria juu ya matarajio yake mwenyewe au kufuatilia mambo yaliyo makuu au fikra za anasa, na alitafuta tu kumpenda Mungu, na kutii mipango yote ya Mungu. Hicho ndicho kiwango unachopaswa kutimiza kabla hujahesabiwa kuwa na ushuhuda, kabla hujawa mtu ambaye amefanywa mkamilifu baada ya kushindwa(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Ushindi (2)). Maneno ya Mungu yalinipa imani na nguvu: Ndiyo! Petro alitundikwa msalabani juu chini kwa ajili ya Mungu na bado aliweza kumpenda Mungu sana hata wakati mwili wake ulikuwa katika uchungu usiovumilika. Alishinda mwili, alimshinda Shetani, na ni ushuhuda wa aina hii pekee ndio mkubwa sana na unaweza kuufariji moyo wa Mungu. Nataka kumwiga Petro, kwamba Mungu aweze kutukuzwa ndani yangu. Ingawa mwili wangu uko katika uchungu mno, bado ni kiasi cha chini kuliko kile ambacho Petro alipitia tundikwa msalabani kichwa kikiwa chini. Shetani hutaka kunifanya nimsaliti Mungu kwa kuutesa mwili wangu, lakini Mungu hutumia fursa hii kukamilisha upendo wangu wa kweli Kwake. Leo, sitasalimu amri kwa Shetani kabisa na kuruhusu njama yake kufaulu! Nataka kuishi kwa ajili ya upendo kwa Mungu! Mara moja, sikuwa tena katika hofu yoyote ya kufa; nilikuwa na dhamira ya kujitoa kwa Mungu kabisa na niliapa na maisha yangu kwamba ningekuwa mwaminifu kwa Mungu! Kwa hivyo, nilimwomba Mungu: “Ee, Mwenyezi Mungu, mimi ni kiumbe aliyeumbwa anayekuabudu na kukutii ninavyopaswa. Nakupa maisha yangu, na iwapo niishi au nife, nakuamini na nakupenda!” Ghafla nilihisi utulivu mkubwa wa uchungu mwilini mwangu, na mwili wangu mzima na akili zilikuwa na hisia ya wepesi na ufunguliaji. Wakati huo, singeweza kujizuia kuimba moyoni mwangu wimbo wa kanisa: “Leo ninakubali hukumu na utakaso ya Mungu, kesho nitapokea baraka Zake. Niko radhi kutoa ujana wangu na kutoa maisha yangu ili kuona siku ya utukufu wa Mungu. Eh, upendo wa Mungu umeufurahisha moyo wangu. Anafanya kazi na kuonyesha ukweli, akinipa maisha mapya. Niko radhi kunywa kutoka kikombe cha dhiki na kuteseka ili kupata ukweli. Nitastahimili fedheha bila malalamiko, ninatamani kuishi maisha yangu nikilipiza wema wa Mungu” (“Ninatamani Kuona Siku ya Utukufu wa Mungu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Mabosi waovu wa polisi walichoka kabisa kutokana na kunitesa, na walisimama hapo bila kusema chochote kwa muda mrefu. Mwishowe, wasijue cha kufanya, walinikaripia kwa hasira: “Wewe subiri tu!” Kisha waliondoka. Wale polisi wengine waovu walisimama huku na kule wakijadiliana: “Huyu mwanamke ni sugu sana, hakuna anayeweza kufanya chochote na yeye. Yeye ni sugu zaidi kuliko Liu Hulan….” Wakati huo, nilishtuka sana kiasi kwamba singezuia machozi yangu kutiririka. Mungu alikuwa mshindi! Isingekuwa maneno ya Mwenyezi Mungu kuniauni tena na tena, na isingekuwa Mungu kuniruzuku kwa siri, nisingeweza kabisa kusimama imara. Utukufu na sifa zote iwe kwa Mwenyezi Mungu! Mwishowe, polisi waovu walinifungia katika nyumba ya kuzuia.

Katika nyumba ya kuzuia, polisi waovu bado hawakutaka kuiachilia, na walinihoji mara moja kila siku chache. Kila wakati waliponihoji, walinifanya niketi katika chumba cha mahojiano mbele ya dirisha lililokuwa na vizuizi vya chuma toka upande mmoja wake hadi mwingine, na mara walipohisi kutoridhika na jibu langu, wangenyosha mkono na kwa ukali kupiga uso wangu ama kunyakua nywele zangu na kubamiza kichwa changu dhidi ya vizuizi. Kwa kuona kwamba bado hawakufua dafu, walitiwa mhemuko na hasira kali. Mwishowe, walitambua kwamba kunitendea bila huruma kulikuwa bure, kwa hivyo waligeuka kutumia mbinu zisizo kali na kujaribu kunilaghai na kunishawishi, wakisema: “Watoto na mume wako wote wanakungoja nyumbani! Na mume wako alitusihi kwa niaba yako. Ongea nasi na punde utarudi na kuungana tena nao.” Maneno haya ya uongo yalinichukiza na kunifanya niwachukie sana kiasi kwamba niliomba moyoni mwangu kwa Mungu kuwalaani. Nilidharau genge hili la polisi waovu wabaya na wasio na aibu. Bila kujali mbinu waliyotumia, singesonga hata kidogo! Katika maisha haya, hakuna anayeweza kutikisa azimio langu la kumfuata Mwenyezi Mungu! Mwishowe, polisi waovu walikuwa wametumia mbinu zote, na walizuia korokoroni kwa siku 40, kunitoza faini ya yuan 2000 na kisha kuniachilia.

Kupitia uzoefu wangu wote hadi leo, katika njia yote, nimetambua kwa kina kwamba mtu kama mimi—mwanamke wa kawaida wa mashambani, ambaye awali hakuwa na umaizi ama ujasiri—anaweza kushinda katikati ya vipindi kadhaa vya kuteswa ili kukiri na kutiwa maumivu kwa njia katili na kuharibiwa na polisi wa CCP, anaweza kuona kwa dhahiri asili ya kupinga maendeleo ya serikali ya CCP ambayo kwa ukaidi inampinga Mungu na hudhuru wateule wa Mungu bila mpango, anaweza kuona kwa dhahiri utendaji wake wa kuchukiza ambao unadanganya umma kuidhinisha sifa yake na ambao unaficha njia zake ovu, na kwamba hili kabisa ni kupitia matendo ya ajabu na nguvu ya Mungu. Katika uzoefu wangu wa vitendo, kwa kweli nimekuja kufahamu kwamba mamlaka na nguvu ya maneno ya Mungu ni kubwa sana, kwamba uhai ambao Mungu humpa mwanadamu ni usio na mwisho na kwamba unaweza kushinda nguvu zote ovu za Shetani! Katika mateso, nilitambua ulikuwa ni upendo wa Mungu ulionifariji na kunipa moyo, na uliniweka dhidi ya kupotea njia yangu. Bila kujali mahali ambapo naweza kuwa ama ni hali za aina gani ninazojipata kwazo, Mungu daima ananichunga, na upendo Wake daima uko nami. Ni heshima yangu kuweza kumfuata huyu Mungu wa vitendo wa kweli, na kwamba naweza kupitia mateso na taabu ya aina hii na kupata kionjo cha ajabu ya Mungu, hekima Yake na uweza Wake ni hata zaidi bahati yangu nzuri. Kutoka siku hii kuendelea, hebu nifanye kila linalowezekana kutafuta ukweli na kutimiza maarifa ya kweli ya Mungu, kumpenda Mungu hadi mwisho, na kuwa imara katika uaminifu wangu!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ujana Usio na Majuto Yoyote

Xiaowen Jijini Chongqing“‘Upendo,’ kama unavyoitwa, unaashiria hisia safi isiyo na dosari, ambapo unatumia moyo wako kupenda, kuhisi,...

Utajiri wa Maisha

Wang Jun Mkoa wa Shandong Kwa miaka mingi tangu kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, mke wangu na mimi tumepitia hili...

Imani Isiyoweza Kuvujika

Meng Yong, China Mimi kwa asili ni mtu mwaminifu, ikiwa ndiyo maana nimekuwa nikidhulumiwa daima na watu wengine. Kwa sababu hiyo, nimeonja...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp