Mateso na Majaribio Ni Baraka za Mungu

10/06/2019

Na Wang Gang, China

Mimi ni mkulima na kwa sababu familia yangu ni maskini, daima ilinibidi nisafiri kwenda kote kutafuta kazi za muda ili kupata pesa; nilidhani kuwa ningeweza kujipatia maisha mazuri kupitia kazi yangu ya kimwili. Hata hivyo, kwa uhalisi, niliona kuwa hapakuwa na hakikisho la haki za kisheria za wafanyakazi wahamiaji kama mimi; mshahara wangu mara nyingi ulizuiliwa bila sababu yoyote. Mara kwa mara nilidanganywa na kutumiwa na wengine kwa faida yao. Baada ya kazi ngumu ya mwaka mmoja, sikupokea kile nilichopaswa kupokea. Nilihisi kwamba ulimwengu huu kwa kweli ulikuwa wa giza! Watu hutendeana kama wanyama ambapo wenye nguvu huwawinda walio dhaifu; wao hushindana wenyewe kwa wenyewe, kupigana kwa kukaribiana sana, na sikuwa na mahali pa usalama kwendelea kuishi jinsi hii. Katika maumivu mno na mfadhaiko wa roho yangu, na wakati nilipokuwa nimepoteza imani katika maisha, rafiki yangu alishirikiana wokovu wa Mwenyezi Mungu nami. Tangu wakati huo, nilikutana mara kwa mara, kusali na kuimba pamoja na ndugu wa kiume na wa kike; tuliwasiliana ukweli, na tulitumia uwezo wetu ili kufidia udhaifu wa mwingine. Nilijihisi mwenye furaha sana na aliyekombolewa. Katika Kanisa la Mwenyezi Mungu, niliona kwamba ndugu wa kiume na wa kike hawakujaribu kushindana kwa akili au kufanya utofautishaji wa kijamii; wote walikuwa wazi kabisa na walipatana wenyewe kwa wenyewe. Kila mtu alikuwa hapo kutafuta ukweli kwa bidii ili kuziacha tabia zao potovu, na kuishi kama wanadamu na kupata wokovu. Hili liliniwezesha kupitia furaha katika maisha na kuelewa umuhimu na thamani ya maisha. Kwa hiyo, niliamua kuwa ni lazima nieneze injili na kuwaruhusu watu zaidi wanaoishi gizani kuja kwa Mungu ili kupokea wokovu Wake na kuona mwanga tena. Kwa hiyo, nilijiunga na wale wa kutangaza injili na kumshuhudia Mungu. Lakini bila kutarajia, nilikamatwa na serikali ya CCP kwa kuhubiri injili na kupitia unyama mno wa mateso, utendewaji wa kikatili na kifungo cha jela.

Ilikuwa wakati wa alasiri katika majira ya baridi ya mwaka wa 2008, wakati dada wawili na mimi tulipokuwa tukiishuhudia kazi ya Mungu katika siku za mwisho kwa mlengwa wa injili, tuliripotiwa na watu waovu. Maafisa sita wa polisi walitumia udhuru wa haja ya kuangalia vibali vya makazi yetu ili kuingia kwa nguvu katika nyumba ya mlengwa wa injili. Walipokuwa wakiingia mlangoni, walisema kwa sauti kubwa: “Msisonge!” Wawili wa wale polisi waovu walionekana kuwa wazimu kabisa waliponirukia; mmoja wao alikamata kwa nguvu nguo juu ya kifua changu na mwingine akamata mikono yangu kwa nguvu na kutumia nguvu zake zote ili kuikaza nyuma yangu, kisha akaniuliza kwa ukali: “Unafanya nini? Unatoka wapi? Jina lako ni nani?” Nikauliza kwa kujibu: “Unafanya nini? Unanikamatia nini?” Waliposikia nikisema hivi, walikasirika kweli na wakasema kwa ukali: “Haijalishi sababu ni nini, wewe ndiwe tunayetafuta na unakuja nasi!” Baadaye, wale polisi waovu wakanichukua pamoja na wale dada wawili, wakatusukuma ndani ya gari la polisi.

Baada ya kufika kwa kituo cha polisi, wale polisi waovu walinichukua na kunifungia ndani ya chumba kidogo; waliniamuru nichutame sakafuni na kunipangia watu wanne wanichunge. Kwa sababu nilikuwa nimechuchumaa kwa muda mrefu, nikawa nimechoka sana kiasi kwamba sikuweza kustahimili. Papo hapo nilijaribu kusimama, wale polisi waovu walinijia mbio mbio na kugandamiza kichwa changu chini ili kunizuia kusimama. Ilikuwa tu hadi wakati wa usiku walipokuja kunipekua na kuniruhusu kusimama; walipokosa kupata chochote katika utafutaji wao, wote waliondoka. Muda mfupi baadaye, nikasikia mayowe yenye kutia hofu ya mtu aliyekuwa akiteswa katika chumba cha pili, na wakati huo, niliogopa sana: Sijui ni mateso gani na matendo katili watakayotumia kwangu baadaye! Nilianza kumwomba Mungu kwa moyo wangu kwa dharura: ukapungua.

Jioni hiyo baadaya saa moja usiku, walinifunga pigu mikononi mwangu nyuma, wakanipeleka kwenye chumba cha kuhojiwa ghorofani na kunisukuma chini. Kulikuwa kumeandaliwa na aina zote za vyombo vya mateso kama vile kamba, vijiti vya mbao, virungu, mijeledi, Polisi mmoja alishika kirungu cha umeme, ambacho kilitoa sauti za dhoruba za “kushambulia na kuzibua” na akafanya madai ya kuitishia habari: “Ni watu wangapi walio katika kanisa lenu? Eneo la mkutano wenu liko wapi? Ni nani anayesimamia? Ni watu wangapi walio katika sehemu hiyo wakihubiri Injili? Ongea! Vinginevyo, utapata kinachokuja!” Nikaangalia hatari iliyotisha ya kirungu cha umeme na nikaangalia tena kwa chumba kilichojaa vyombo vya mateso; sikuweza kujizuia kuhisi fadhaa na kuogopa. Sikujua kama ningeweza kuyashinda mateso haya. Hivyo nikaendelea kumwomba Mungu. Alipoona sikusema kitu, yeye alivurugika na kunidukua kwa nguvu kwa upande wa kushoto wa kifua changu na kirungu hicho cha umeme. Alinishtua kwa karibu dakika moja. Mara moja nilisikia kama damu katika mwili wangu ilikuwa imechemshwa; nilikuwa na maumivu yasiyovumilika kutoka kwa kichwa hadi kwa mguu na nikabiringika nikipiga mayowe sakafuni. Bado hakutaka kuniacha na ghafla akaanza kunivuta na akatumia kirungu kuniinua kwa kidevu changu, akiguta: “Sema! Hutakiri chochote?” Nilipokuwa napitia haya mateso, niliofia kuwa nitamsaliti Mungu kwa sababu ya kutoweza kuyahimili mateso yao. Wakati huu, nilifikiri juu ya maneno ya Mungu, “Kutoka kwa nje, wale walio na mamlaka wanaweza kuonekana kuwa waovu, lakini msiogope, kwa kuwa hii ni kwa sababu mna imani kidogo. Almuradi imani yenu ikue, hakuna kitu kitakachokuwa kigumu mno(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 75). Maneno ya Mungu yalinipa imani na nguvu tena, na niligundua kuwa ingawa hawa polisi waovu mbele yangu walikuwa na kichaa na bila nidhamu, walipangwa na mkono wa Mungu. Bila idhini ya Mungu, hawawezi niua mimi. Alimradi niliegemea imani na kumtegemea Mungu na sikukubali kushindwa nao, bila kuzuilika wangeshindwa kwa aibu. Katika kufikiri juu ya hili, nilikusanya nguvu zangu zote za mwili wangu na nikajibu kwa sauti kuu: “Kwa nini mmenileta hapa? Kwa nini mnanishtua kwa umeme kwa kirungu cha umeme? Ni kosa gani nimelifanya?” Yule polisi muovu kwa ghafla akawa mtu aliyeshtuka kiasi cha kutowaza na kukandamizwa sana na dhamiri ya hatia. Alianza kugugumiza Kisha wakaondoka kwa aibu. Katika kuona hali ya aibu ya mtanziko wa Shetani, niliguswa hadi nikalia. Katika mashaka haya, kwa kweli nilipitia nguvu na mamlaka ya maneno ya Mwenyezi Mungu. Mradi ninayaweka maneno ya Mungu katika vitendo, basi nitayashuhudia matendo ya Mungu. Maafisa wawili walikuja kwa dakika tano au sita baadaye, lakini wakati huu walijaribu njia nyingine. Afisa mwembamba aliniambia kwa uchangamfu, “Cheza vizuri tu kidogo. Jibu maswali yetu, vinginevyo hatutakuacha uende.” Sikuesema neno, kwa hivyo alileta karatasi ilinitie muhuri. Nilipoona maneno “mafunzo kupitia kazi ngumu” yaliandikwa nilikataa. Afisa mwingine alinipiga vibaya kwenye sikio langu la kushoto, kwa mshindo hadi sakafuni. Sikio langu lilikuwa likilia kwa muda na ilinichukua muda kupata uwazi. Walinifunga pingu tena na kunifungia kwenye kile chumba kidogo.

Baada ya kurudi kwa kile chumba kidogo, nilichubuliwa na kugongwagongwa sana, maumivu yalikuwa yasiyovumilika. Moyo wangu haukuweza kujizuia kuzalisha hisia ya huzuni na udhaifu: Kwa nini waumini wanapaswa kuteseka jinsi hii? Nilihubiri Injili na nia njema za kuwaruhusu watu kuutafuta ukweli na kuokolewa, na bila kutarajia nimepitia mateso haya. Katika kufikiri juu ya hili, nilihisi zaidi kuwa nilikuwa nimekosewa. Nilimwita Mungu kwa maombi katika mateso yangu, nikisema, "Ee Mungu, kimo changu ni kidogo sana na mimi ni dhaifu sana. Mungu, nataka kukutegemea na kusimama kwa ajili yako. Tafadhali niongoze.” Baadaye, nilifikiria wimbo wa maneno ya Mungu: “Usivunjike moyo, usiwe dhaifu, Nitakufichulia. Njia ya kwenda kwa ufalme sio laini hivyo, hakuna kitu kilicho rahisi hivyo! Unataka baraka zije kwa urahisi rahisi, sivyo? Leo kila mtu atakuwa na majaribio machungu ya kukumbana nayo, vinginevyo moyo wa upendo ulio nao Kwangu hautakuwa wenye nguvu zaidi na hutakuwa na upendo wa kweli Kwangu. Hata kama majaribu haya yanajumuisha hali ndogo tu, kila mtu lazima ayapitie; ni kwamba tu ugumu wa majaribu utakuwa tofauti kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine. Majaribu ni Baraka kutoka Kwangu, na ni wangapi kati yenu ambao huja mbele Yangu na kupiga magoti mkiomba baraka Zangu? Wewe daima huhisi kwamba maneno machache ya bahati huhesabika kama baraka Yangu, lakini huhisi kuwa uchungu ni moja ya baraka Zangu(“Maumivu ya Majaribio ni Baraka Kutoka Mungu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Ni kweli. Kukabiliwa na mateso na shida hii ili Mungu akamilishe imani na upendo wangu. Mazingira hayo yalikuwa ni baraka ya Mungu. Ninawezaje kulalamika na kumlaumu Mungu? Nilikamatwa na kuteswa, lakini katika kipindi chote cha majaribu Mungu alikuwa akiniongoza kwa maneno yake huu ulikuwa upendo wa Mungu. Niliimba wimbo huo moyoni mwangu, na kadri nilivyoiimba ndivyo nilivyohisi nguvu zaidi. Pia ilirejesha imani yangu na nikaapa kwa Mungu: “Mungu, bila kujali jinsi polisi wananitesa, ningependa kusimama shahidi na kamwe sikusaliti. Nimeamua kukufuata mpaka mwisho”

Katika kituo cha kizuizi, hao afisa polisi waliendelea kutumia njia zote za mateso kwangu na mara nyingi waliwahimiza wafungwa kunipiga. Katika baridi kali ya majira ya baridi, waliwaagiza wafungwa kunimwagilia ndoo za maji baridi na kunilazimisha kuoga na maji baridi. Nilikuwa nikitetemeka kwa baridi kutoka utosini hadi kidoleni. Kupatwa na uchungu na kutokwa na jasho, moyo wangu uliumia hadi uhakika kwamba mgongo wangu ulikuwa na uchungu pia. Hapa, wafungwa walikuwa mashine ya kutengeneza pesa kwa serikali na hawakuwa na haki yoyote ya kisheria. Hawakuwa na chaguo jingine ila kuvumilia kuminywa na kutumiwa na wengine kwa faida yao kama watumwa. Gereza lilinilazimisha kuchapisha pesa za karatasi zilizotumika kama sadaka za kuteketezwa kwa wafu wakati wa mchana. Mara ya kwanza, waliweka sheria kwamba nilipaswa kuchapisha vipande 1,000 vya karatasi kwa siku, kisha wakaongeza viwe vipande 1, 800 kwa siku, na hatimaye hadi vipande 3,000. Kiasi hiki kilikuwa hakiwezekani kwa mtu mwenye ujuzi kukamilisha sembuse mtu asiye na ujuzi kama mimi kukamilisha. Kwa kweli, walipanga hivyo kwa makusudi ili nisiweze kukamilisha yote ili waweze kuwa na udhuru wa kunitesa na kunidhuru. Alimradi sikuweza kufikia kiasi hicho, hao polisi waovu wangeniwekea pingu za miguu kwa miguu yangu ambazo zilikuwa na uzito wa zaidi ya kilo 5, na kuifunga mikono na miguu pamoja kwa pingu. Yote niliyoweza kufanya ni kuketi pale, kuinamisha kichwa changu na kugeuza kiuno changu, vinginevyo sikuweza kusonga. Aidha, hawa polisi wakatili na wasio na hisia hawakuuliza au kujali kuhusu mahitaji yangu ya msingi. Ingawa choo kilikuwa ndani ya seli ya gereza, sikuweza kabisa kutembea na kukitumia; niliweza tu kuwaomba wenzangu katika seli kuniinua na kuniwekelea kwa choo. Kama walikuwa wafungwa bora zaidi kidogo, basi wangeweza kuniinua; kama hakuna mtu aliyenisaidia, basi singekuwa na chaguo jingine ila kujizuia. Wakati wa maumivu mno ulikuwa wakati wa chakula, kwa sababu mikono na miguu yangu ilikuwa imefungwa pamoja. Niliweza tu kuteremsha kichwa changu kwa nguvu zangu zote na kuinua mikono na miguu yangu. Ni kwa njia hii tu nilivyoweza kuiweka skonsi kinywani mwangu. Nilitumia nguvu nyingi sana kwa kila umo. Pingu zilisugua mikono na miguu yangu na zikisababisha maumivu makubwa. Baada ya muda mrefu, vifundo vya mikono yangu na vya miguu vilikuwa vimekuza sagamba nyeusi na ngumu zilizong’aa. Mara nyingi sikuweza kula wakati nilipokuwa nimefungiwa, na mara chache, wafungwa wangenipa skonsi mbili ndogo. Mara nyingi wangekula sehemu yangu na yote niliyopata ilikuwa tumbo tupu. Nilipokea hata kinywaji kidogo zaidi; awali, kila mmoja alipewa tu bakuli mbili za maji kwa siku, lakini nilikuwa nimefungiwa na sikuweza kusogea, hivyo ni kwa nadra sana niliweza kunywa maji yoyote. Mateso hayo ya kinyama yalikuwa yasiyosemeka. Nilinyanyaswa kwa aina hiyo isiyo ya kibinadamu mara nne, ikidumu jumla ya siku kumi. Hata katika hali hizo, maafisa walinifanya nifanye kazi zamu ya usiku. Ningeenda kwa muda mrefu bila hata kuwa na uwezo wa kula kushiba; mara nyingi njaa iliniacha na kupooza, kichefuchefu, na kubana katika kifua changu. Ningebadilika pia kuwa begi la mifupa. Njaa ilipofika mahali kwamba sikuweza kuistahimili, nilifikiria maneno ambayo Bwana Yesu alisema kwa Shetani katikati ya jaribu: “Mwanadamu hatadumu kwa mkate pekee, lakini kwa kila neno linalotoka kinywani mwa Mungu(Mathayo 4:4). Hiyo ilinipa raha, na nilihisi tayari kupata uzoefu wa maneno hayo kutoka kwa Mungu katika mateso ya Shetani kwangu. Nilijinyamazisha mbele za Mungu ili kuomba na kutafakari maneno Yake, na kabla sijajua hayo, maumivu na njaa yangu ilikuwa imepungua. Wakati mmoja mfungwa aliniambia: “Kulikuwa na kijana ambaye alikuwa amefungwa pingu na kufa na njaa kama hii hapo awali. Nimeona kuwa hujala sana kwa siku kadhaa na bado ungali na furaha kubwa.” Kwa kusikia maneno yake, nikamshukuru Mungu kimya kimya. Nilihisi sana kuwa hii ilikuwa nguvu ya maisha katika maneno ya Mungu yakiniunga mkono. Hili kwa hakika lilinifanya nisihisi kuwa neno la Mungu ni ukweli, njia, na uzima na bila shaka ni msingi ambao napaswa kutegemea ili kuishi. Kwa hiyo, imani yangu kwa Mungu iliongezeka bila kujua. Katika mazingira haya ya mateso niliweza kwa kweli kupitia uhalisi wa ukweli kwamba “Mwanadamu hatadumu kwa mkate pekee, lakini kwa kila neno linalotoka kinywani mwa Mungu.” Huu kwa kweli ni utajiri wa thamani zaidi wa maisha ambao Mungu ameniridhia, na pia ni zawadi yangu ya pekee. Aidha, singeweza kamwe kuupata katika mazingira ambayo sikuhitaji kuwa na wasiwasi juu ya chakula au nguo. Sasa, mateso yangu yalikuwa na maana nyingi sana na thamani!

Uzoefu huo wa mateso na mateso ulizidisha chuki niliyokuwa nayo moyoni mwangu kwa Chama cha Kikomunisti. Nilikamatwa na kuteswa kwa kila aina ya kitu chochote kwa sababu ya kumwamini Mungu. Ilikuwa unyanyasaji usio wa kibinadamu; ulikuwa mbaya kabisa! Nilifikiria kifungu cha maneno ya Mungu niliyosoma hapo awali: “Kina chake ni vurugu na giza, ilhali mtu wa kawaida, anayeteseka na mateso kama hayo, analalamika bila kupumzika. Ni lini mwanadamu ataweza kunyanyua kichwa chake juu? Mwanadamu amekuwa kimbaumbau na amekonda, anawezaje kuridhika na ibilisi huyu katili na dikteta? Kwa nini asiyatoe maisha yake kwa Mungu mapema awezavyo? Kwa nini bado anayumbayumba? Anaweza kumaliza kazi ya Mungu lini? Hivyo anaonewa na kunyanyaswa bila sababu yoyote, maisha yake yote hatimaye yatakuwa bure; kwa nini ana haraka hivyo ya kufika, na haraka hiyo ya kuondoka? Kwa nini hahifadhi kitu kizuri cha kumpa Mungu? Je, amesahau milenia ya chuki?(“Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Limeonekana Katika Mwili). Uzoefu huu ulinionyesha kiini cha kweli cha Chama cha Kikomunisti kama adui wa Mungu, adui wa ukweli. Iliimarisha azimio langu la kutoa ushuhuda kwa Mungu.

Mwezi mmoja baadaye, polisi wa CCP walinifungulia mashtaka ya uongo ya “kushukiwa kuvuruga utaratibu wa jamii na kuharibu utekelezaji wa sheria”; nilihukumiwa mwaka mmoja wa mageuzi kupitia kazi. Nilipoingia kambi ya kazi, maafisa wa polisi walinilazimisha kufanya kazi kila siku. Nilipokuwa katika karakana nikihesabu mifuko, ningehesabu mifuko 100 na kisha kuifunga pamoja. Wafungwa wangekuja daima na kutoa mfuko moja au kadhaa kutoka kwa ile niliyokuwa nimehesabu, kisha wangesema kwamba sikuhesabu vizuri na kuchukua hiyo kama fursa ya kunipiga ngumi na mateke. Wakati msimamizi huyo aliponiona nikipigwa, angekuja na kuniuliza kwa unafiki kilichokuwa kikiendelea na wafungwa wangewasilisha ushahidi wa uongo kwamba sikuwa nimehesabu mifuko ya kutosha. Kisha ningelazimika kustahimili mfululizo wa ukosoaji mkali kutoka kwa msimamizi. “Hivyo, katika siku hizi za mwisho lazima muwe na ushuhuda kwa Mungu. Haijalishi mateso yenu ni makubwa vipi, mnapaswa kuendelea hadi mwisho kabisa, na hata wakati wa pumzi yenu ya mwisho, bado lazima muwe waaminifu kwa Mungu, na kudhibitiwa na Mungu; huku pekee ndiko kumpenda Mungu kweli, na huu pekee ndio ushuhuda thabiti na mkubwa sana(“Tafuta Kumpenda Mungu Bila Kujali Mateso Yako Ni Makubwa Vipi” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Wakati niliimba na kuimba, nilianza kuhisi kusukumwa na kuhamasishwa, na sikuweza kuyazuia machozi kutiririka mashavuni mwangu. Niliweka azimio langu kwamba bila kujali ni mateso gani, nitasimama kwa ajili ya Mungu. Kulikuwa na ndugu mwingine karibu na umri wangu yule ambaye alitokea kufungwa na mimi wakati huo. Hatukuruhusiwa kuongea wakati tunafanya kazi wakati wa mchana, lakini usiku tungeandika kwa siri vifungu vya maneno ya Mungu na nyimbo ambazo tungekariri na kuzibadilishana. Baada ya muda tulipewa kufanya kazi pamoja, kwa hivyo tulishiriki kimya kimya ushirika, tukisaidiana na kutiana moyo. Ilisaidia sana kupunguza mateso.

Aidha, wangeniamuru nikariri “amri za maadili mema” kila asubuhi, na kama sikuzikariri, ningepigwa; pia wangenilazimisha kuimba nyimbo zilizokisifu chama cha Kikomunisti. Kama waliona kwamba sikuwa nikiimba au kwamba midomo yangu haikuwa ikisonga, basi usiku bila shaka ningepigwa. Pia waliniadhibu kwa kunifanya nipanguse sakafu, na kama sikupangusa kwa matarajio yao, basi ningepigwa kwa nguvu nyingi. Wakati mmoja, kwa ghafla wafungwa fulani walianza kunigonga na kunipiga mateke. Baada ya kunipiga, waliniuliza: “Kijana, unajua kwa nini unapigwa? Ni kwa sababu hukusimama na kumsalimu msimamizi wakati alipokuja!” Baada ya kila wakati nilipopigwa, nilikuwa na hasira lakini sikuthubutu kusema chochote; niliweza kulia tu na kumwomba Mungu kimyakimya, nikimwambia Yeye juu ya chuki na malalamiko moyoni mwangu kwa sababu ya mahali hapa palipo na utovu wa sheria, na kukosa mantiki. Hapakuwa na busara hapa, palikuwa na vurugu tu. Kulikuwa hakuna watu hapa, kulikuwa na pepo wenye wazimu na nge tu! Nilihisi maumivu mengi sana na shinikizo nikiishi katika shida hii; sikuwa tayari kukaa hata dakika moja zaidi. Kila wakati nilipotumbukia katika hali ya udhaifu na maumivu, ningefikiri juu ya maneno ya Mwenyezi Mungu: “Mmewahi kuzikubali baraka mlizopewa? Mmewahi kuzitafuta ahadi mlizofanyiwa? Hakika, chini ya mwongozo wa mwangaza Wangu, mtapenya katika utawala wa nguvu za giza. Hakika, katikati ya giza, hamtaupoteza mwangaza unaowaongoza. Hakika mtakuwa bwana wa viumbe vyote. Hakika mtakuwa washindi mbele ya Shetani. Hakika, wakati wa maangamizi ya ufalme wa joka kubwa jekundu, mtasimama miongoni mwa umati mkubwa kushuhudia ushindi Wangu. Hakika mtasimama imara na thabiti katika nchi ya Sinimu. Kupitia katika mateso mnayoyavumilia, mtarithi baraka zinazotoka Kwangu, hakika mtaonyesha utukufu Wangu katika ulimwengu mzima(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 19). Maneno ya Mungu yalinitia moyo. Bila kujali kama kile Mungu alichokuwa akinifanyia kilikuwa neema na baraka au majaribu na usafishwaji, yote ilikuwa ili kunikimu na kuniokoa; ilikuwa ni kuweka ukweli ndani yangu na kufanya ukweli kuwa maisha yangu. Leo, Mungu aliruhusu mateso haya na taabu zinijie. Ingawa jambo hili lilisababishia mateso mengi, liliniruhusu kuona wazi asili mbaya mbaya ya joka nyekundu ya kumpinga na kumchukia Mungu, kuchukia na kuiacha, kuepuka kabisa ushawishi wa Shetani, na kumgeukia Mungu kabisa na kufanywa mshindi na Mungu. Pia iliniruhusu kuweza kwa kweli kuwa na uzoefu kwamba Mungu yu pamoja nami; lilinifanya kwa kweli nifurahie maneno ya Mungu kuwa mkate wa maisha yangu na taa ya miguu yangu na mwanga kwa njia yangu, likiniongoza hatua kwa hatua kupitia mahali hapa padhalimu na pasipovumilika. Huu ndio upendo na ulinzi wa Mungu ambao nilifurahia na kupata wakati wa mchakato wa mateso yangu. Wakati huu, niliweza kuona kwamba nilikuwa kipofu sana na wa ubinafsi na nilikuwa mwenye uroho mno. Katika kumwamini Mungu, nilijua tu jinsi ya kufurahia neema na baraka za Mungu na sikutafuta ukweli na uhai kwa kiwango hata kidogo. Mara mwili wangu uliopitia shida kidogo, ningenung’unika bila kukoma; sikuelewa kabisa mapenzi ya Mungu na sikutafuta kuielewa kazi ya Mungu. Daima ningemfanya Mungu ahisi huzuni na maumivu juu yangu. Kwa kweli nilikuwa bila dhamiri! Kwa majuto na kujilaumu, niliomba kimya kimya kwa Mungu: “Ewe Mwenyezi Mungu, naweza kuona kwamba kila kitu unachokifanya ni kuniokoa na kunipata. Ninachukia tu kwamba mimi ni mkaidi sana na asiyeona, ni kipofu na sina ubinadamu. Daima nimekuelewa visivyo na sijakuwa wa kufikiria mapenzi Yako. Ee Mungu, leo neno Lako limeuamsha moyo wangu wenye ganzi na roho yangu na limenisababisha kuyaelewa mapenzi Yako. Siko tayari tena kuwa na tamaa na mahitaji yangu mwenyewe; nitatii tu mipango Yako. Hata ikiwa ni mateso gani ambayo nitayapitia, nitatoa ushuhuda kwako kupitia unyanyasaji wa shetani.” Baada ya kuomba, nilielewa nia njema za Mungu, na nilijua kwamba kila mazingira ambayo Mungu aliniruhusu kupitia yalikuwa ni upendo na wokovu mkubwa wa Mungu kwangu. Kwa hiyo, singefikiria tena kujikunyata au kumwelewa Mungu visivyo. Ingawa hali ilikuwa bado ni ile ile, moyo wangu kwa kweli ulijaa furaha na ridhaa; nilihisi kuwa ni heshima na fahari kuweza kupitia shida na mateso kwa sababu ya imani yangu kwa Mwenyezi Mungu, na ilikuwa ni zawadi ya pekee kwangu, mtu mpotovu; ilikuwa baraka maalumu na neema za Mungu kwangu.

Baada ya kuwa na uzoefu wa mwaka mmoja wa shida katika jela, naona kwamba mimi ni mdogo sana wa kimo na kwamba nakosa ukweli mwingi sana. Mwenyezi Mungu kwa kweli amefidia upungufu wangu kupitia mazingira haya ya kipekee na ameniruhusu kukua. Katika dhiki yangu, Amenifanya kupata utajiri wa thamani mno katika maisha na kuelewa ukweli mwingi ambao sikuufahamu katika siku za nyuma na kuona kwa dhahiri sura mbaya kwa Shetani, pepo, na kiini cha kupinga maendeleo cha upinzani wake kwa Mungu. Nilitambua uhalifu wake muovu wa kumtesa Mwenyezi Mungu na kuwaua Wakristo. Nilipitia kwa dhati wokovu na huruma kubwa Mwenyezi Mungu aliyokuwa nayo kwangu, mtu mpotovu, na nimehisi kwamba nguvu na maisha katika maneno ya Mwenyezi Mungu yanaweza kunipa mwanga na kuwa maisha yangu na kunielekeza kumshinda Shetani na kwa ushupavu kutoka nje ya bonde la uvuli wa mauti. Asante Mungu.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ujana Usio na Majuto Yoyote

Xiaowen Jijini Chongqing“‘Upendo,’ kama unavyoitwa, unaashiria hisia safi isiyo na dosari, ambapo unatumia moyo wako kupenda, kuhisi,...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp