Kwa Kuelewea Hizi Hoja Nne, Uhusiano Wetu na Mungu Utakuwa Wa Karibu Daima

23/07/2020

Na Xiaomo, China

Biblia inasema, “Kujeni karibu na Mungu, naye atakuja karibu nanyi” (Yakobo 4:8). Kama Wakristo, ni kwa kumkaribia Mungu tu na kuwa na ushirikiano halisi na Mungu ndiyo tunaweza kudumisha uhusiano wa kawaida na Mungu na kupata kazi ya Roho Mtakatifu. Ni kama tu watu wawili wanaoshirikiana, ambao wanaweza tu kuendeleza uhusiano wao wa karibu kwa muda mrefu kwa kuwa wazi zaidi kwa kila mmoja, kuwasiliana zaidi wanapokumbana na masuala, na kwa kuelewawana na kuheshimiana. Hata hivyo, katika enzi hii ya maisha yenye kasi, kazi zenye shughuli nyingi, mahusiano yenye utata na mienendo mibaya ya kijamii hutuvutia na kututawala zaidi na zaidi. Mioyo yetu inasumbuliwa kwa urahisi na watu, matukio na mambo ya ulimwengu wa nje, na hutuzuia kuendeleza uhusiano wa kawaida na Mungu. Hii hutusababisha kuwa mbali zaidi na Mungu na, tunapokumbana na masuala, inakuwa vigumu sana kwetu kujinyenyekeza mbele ya Mungu, kumkaribia Mungu na kutafuta nuru na mwongozo wa Roho Mtakatifu. Tunapofanya mambo, mara nyingi tunayafanya bila mwongozo wowote au sababu, na roho zetu daima ziko katika hali ya utupu na mkorogo. Hivyo tunawezaje kudumisha uhusiano wa karibu na Mungu? Tunahitaji tu kuelewa hoja nne zilizo hapa chini, na uhusiano wetu na Mungu bila shaka utakuwa wa karibu.

Kwa Kuelewea Hizi Hoja Nne, Uhusiano Wetu na Mungu Utakuwa Wa Karibu Daima

1. Mwombe Mungu kwa Moyo Mwamininifu na Uguswe na Roho Mtakatifu

Maombi ni njia ambayo kwayo tunawasiliana na Mungu. Kupitia kwa maombi, mioyo yetu inaweza kunyenyekea mbele ya Mungu vyema zaidi, kutafakari neno la Mungu, kutafuta mapenzi ya Mungu na kuanzisha uhusiano wa kawaida na Mungu. Lakini maishani, kwa sababu sisi tunajishughulisha na kazi au kazi za nyumbani, tunaweza tu kufanya maombi kama jambo la kupita tu, na tunamtendea Mungu kwa uzembe tu kwa kusema maneno machache ya usahaulifu. Tunapokuwa na shughuli nyingi jambo la kwanza asubuhi, kwa mfano, tunapoenda kazini au kujishughulisha na kitu kingine, tunaomba kwa haraka: “Ee Mungu! Naikabidhi kazi ya leo mikononi Mwako, na nakukabidhi watoto wangu na wazazi wangu. Nakabidhi kila kitu mikononi Mwako, na nakuomba Unibariki na unilinde. Amina!” Tunamtendea Mungu kwa uzembe kwa kusema maneno machache yasiyo na mpangilio. Mioyo yetu si mitulivu, sembuse sisi kuwa uhusiano wowote wa kweli na Mungu. Wakati mwingine, tunasema maneno matamu, na baadhi maneno matupu, ya kujisifu kwa Mungu katika maombi, na hatumwambii Mungu kile kilicho mioyoni mwetu. Au wakati mwingine, tunapoomba, tunakariri maneno fulani kwa moyo, na tunasema maneno hayo hayo ya zamani, yaliyoisha ladha kila wakati, na hili linakuwa kabisa ombi la ibada ya kidini. Maombi mengi kama haya yanasemwa maishani mwetu—maombi ambayo hushikilia sheria, na maombi ambayo kwayo hatufungui mioyo yetu kwa Mungu wala kutafuta mapenzi ya Mungu. Mungu huchukia tunaposema maombi bila kumaanisha neno lolote, kwa sababu maombi ya aina hii yanahusu tu kuonekana kwa nje na ibada ya kidini, na hakuna ushirikiano halisi na Mungu katika roho yetu. Watu wanaoomba namna hii wanamtendea Mungu kwa uzembe na wanamdanganya Mungu. Kwa hiyo, maombi kama haya hayasikiki na Mungu na inakuwa vigumu kwa watu wanaoomba kwa njia hii kuguswa na Roho Mtakatifu. Wanapoomba namna hii, hawawezi kuhisi uwepo wa Mungu, roho zao ni za giza na dhaifu, na uhusiano wao na Mungu unakuwa wa mbali zaidi.

Bwana Yesu alisema: “Mungu ni Roho: na wale ambao wanamwabudu ni lazima wamwabudu kwa roho na kwa ukweli(Yohana 4:24). Mungu ni Muumba anayejaza mbingu na dunia nzima. Yeye yuko karibu nasi wakati wote, akiangalia kila neno na tendo letu, kila wazo na wazo letu. Mungu ni mkuu, anayeheshimika kabisa, na tunapomwomba Mungu, tunamwabudu Mungu, na ni lazima tuje mbele za Mungu kwa moyo mwaminifu. Kwa hiyo, tunapomwomba Mungu, tunapaswa kuwa na moyo unaomcha Mungu, tunene kwa uamininfu na kweli kwa Mungu, tulete hali zetu halisi, matatizo yetu na taabu zetu mbele za Mungu na kumwambia kuzihusu, na lazima tutafute mapenzi ya Mungu na kutafuta njia ya kutenda, kwani ni kwa njia hii tu ndiyo maombi yetu yatalingana na mapenzi ya Mungu. Kwa mfano, tunakumbana na ugumu fulani katika maisha, au tunajiona tunaishi katika hali ambayo sisi daima tunatenda dhambi na kukiri, na tunahisi kuteswa. Na hivyo, tunafungua mioyo yetu kwa Mungu, tunamwambia Mungu kuhusu matatizo haya na kutafuta mapenzi ya Mungu, na Mungu ataona uaminifu wetu na Atatugusa. Atatupa imani, au Atatupa nuru ili tuelewe mapenzi Yake. Kwa njia hii, tunapata kuelewa ukweli na kuwa na njia ya kuendelea. Kwa mfano, tunapotambua kwa kweli kwamba maombi yetu yanafuata tu sharia na yanasemwa tu kama utaratibu, au tunazungumza kwa kujivuna au kwa utupu, na hatuna uhusiano wowote na Mungu, tunaweza kisha kuomba kwa njia hii: “Ee Mungu! Nilipoomba hapo awali, nilikuwa tu nikikutendea kwa uzembe. Kila kitu nilichosema kilisemwa ili kukudanganya na sikuwa nanena kwa uaminifu kabisa; nahisi mwenye deni sana Kwako. Kuanzia siku hii kuendelea, ningependa kuomba kwa moyo wangu. Nitakwambia chochote ninachofikiria moyoni mwangu, na nitakuabudu kwa moyo mwaminifu, na kuomba mwongozo Wako.” Tunapojiweka wazi kwa Mungu namna hii kutoka kwa vina vya mioyo yetu, mioyo yetu basi inaguswa. Kisha tunaona tumeasi kiasi gani dhidi ya Mungu, na tunatamani hata zaidi kutubu kwa kweli kwa Mungu na kuzungumza na Yeye kwa uaminifu. Kwa wakati huu, tutahisi kuwa uhusiano wetu na Mungu ni wa karibu sana, kana kwamba tuko uso kwa uso na Yeye. Haya ndiyo matokeo ya kufungua mioyo yetu kwa Mungu.

Kufungua mioyo yetu kwa Mungu hakuna uhusiano na kiasi gani tunachomwambia, au kama tunatumia maneno ya kifahari au lugha ya kupendeza. Almradi tunafungua mioyo yetu kwa Mungu na kumwambia kuhusu hali yetu ya kweli, kutafuta uongozi Wake na nuru Yake, basi Mungu atasikiliza hata kama tunasema maneno machache rahisi tu. Tunapomkaribia Mungu mara kwa mara kwa njia hii, iwe ni katika mikusanyiko au wakati wa ibada za kiroho, au tunapokuwa tunatembea katika mtaa au tunakaa kwenye basi au kazini, mioyo yetu daima itakuwa inafunguka kimya kimya kwa Mungu katika maombi. Bila kufahamu hilo, mioyo yetu basi inaweza kuwa mitulivu mbele ya Mungu hata zaidi, tutaelewa mapenzi ya Mungu zaidi na, tunapokumbana na masuala, tutajua jinsi ya kutenda ukweli ili kumridhisha Mungu. Kwa njia hii, uhusiano wetu na Mungu utakuwa wa kawaida zaidi.

2. Unaposoma Maneno ya Mungu, Yafikirie kwa Moyo Wako na Utaelewa Maana Yake ya Kweli

Wakristo hutenda ibada za kiroho na kusoma maneno ya Mungu kila siku. Tunawezaje kusoma maneno ya Mungu kwa namna ambayo inafanikisha matokeo mazuri na ambayo inaweza kuwezesha uhusiano wetu na Mungu kuwa wa karibu zaidi? Neno la Mungu linasema: “Watu wanaamini katika Mungu, wanampenda Mungu, na kumkidhi Mungu kwa kugusa Roho wa Mungu kwa moyo wao, hivyo kupata ridhaa ya Mungu; na wakati wanajihusisha na maneno ya Mungu kwa moyo wao, kwa hivyo wanasisimuliwa na Roho wa Mungu(“Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kawaida na Mungu”). Maneno ya Mungu yanatuambia kwamba, tunaposoma maneno Yake, tunapaswa kuyatafakari na kwenda kutafuta kwa mioyo yetu, tunapaswa kupata nuru na mwanga wa Roho Mtakatifu, na tunapaswa kuelewa mapenzi ya Mungu na kile Anachohitaji kutoka kwetu. Ni kwa kusoma tu maneno ya Mungu kwa njia hii ndiyo juhudi zetu zitazaa matunda na tutamkaribia Mungu zaidi. Tunaposoma maneno ya Mungu, tukiyapitia tu bila kuwa makini, ikiwa tu tunazingatia kuelewa baadhi ya maneno na mafundisho ili tujionyeshe na hatujali kuelewa maana halisi ya maneno ya Mungu, basi haijalishi tunasoma maneno Yake kiasi gani, hatutaweza kulingana na mapenzi Yake, sembuse kuwa na uwezo wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na Mungu.

Kwa hiyo, tunaposoma maneno ya Mungu, tunapaswa kuinyenyekeza mioyo yetu na kutumia mioyo yetu kutafakari kwa nini Mungu anasema mambo kama hayo, mapenzi ya Mungu ni nini na Mungu anataka kufanikisha matokeo gani kwetu kwa kusema mambo kama hayo. Ni kwa kutafakari tu maneno Yake kwa kina kwa njia hii ndiyo tunaweza kuelewa mapenzi ya Mungu na kuupendeza moyo Wake zaidi, na uhusiano wetu na Mungu utazidi kuwa wa kawaida. Kwa mfano, tunaona kwamba Bwana Yesu anasema: “Kweli nawaambia, Ila msipobadilishwa, na kugeuka kama wana wadogo, hamtaingia ndani ya ufalme wa mbinguni(Mathayo 18:3). Tunaweza kuelewa maana ya juu ya neno hili, kwamba Mungu anatutaka tuwe watu waaminifu. Lakini masuala kama umuhimu wa kuwa mtu mwaminifu, kwa nini Mungu anapenda watu waaminifu na jinsi hasa ya kuwa mtu mwaminifu, ni masuala ambayo tunapaswa kutafakari kwa kina zaidi. Kupitia kuomba kwa kusoma na kutafakari maneno ya Mungu, kisha tunaelewa kwamba asili ya Mungu ni aminifu, na kwamba hakuna uongo au udanganyifu katika chochote ambacho Mungu anasema au kufanya, na kwa hivyo Mungu huwapenda watu waaminifu na kuwachukia watu wa wadanganyifu. Mungu anahitaji kwamba lazima tuwe watu waaminifu, kwa sababu ni kwa kuwa tu watu waaminifu kulingana na mahitaji ya Mungu ndiyo tunaweza kuongozwa na Mungu kwenda katika ufalme Wake. Hivyo tunakuwaje hasa watu waaminifu? Kwanza, hatupaswi kusema uongo, lakini tunapaswa kuwa safi na wazi na kusema kile kilicho mioyoni mwetu; pili, hatupaswi kutenda kwa udanganyifu, tunapaswa kuwa na uwezo wa kuacha maslahi yetu wenyewe, na kutomdanganya Mungu wala mwanadamu; tatu, hakupaswi kuwa na udanganyifu mioyoni mwetu, hakupaswi kuwa na nia au lengo la kibinafsi katika matendo yetu, lakini badala yake tunapaswa tu kutenda ukweli na kumridhisha Mungu. Baada ya mwangaza huu kufanikishwa kwa kutafakari, tunafikiria kuhusu matendo yetu na tabia yetu na kisha tunaona kwamba bado tunayo maonyesho mengi ya udanganyifu: Tunapokuwa tunashughulika na watu wengine, mara nyingi hatuwezi kujizuia kusema uongo au kudanganya ili kulinda maslahi sifa na hadhi yetu wenyewe. Tunapojitumia kwa ajili ya Mungu, tunaweza kusema katika maombi kwamba tunatamani kumpenda Mungu na kumridhisha Mungu, lakini majaribio yanapotukumba, kama vile mtoto wetu awe mgonjwa au labda sisi wenyewe au mmoja wa familia apoteze kazi yake, mara moja tunaanza kumlalamikia Mungu, kiasi kikubwa kwamba tunataka kuacha kazi yetu kanisani; katika hili, tunaweza kuona kwamba tunajitumia kwa ajili ya Mungu kwa njia ambayo ni chafu, na kwa namna fulani ambayo tunafanya mikataba na Mungu. Tunajitumia kwa ajili ya Mungu ili tufaidike kutoka kwa Mungu, na sio ili tu kumridhisha Mungu. Hii ni mifano tu ya maonyesho yetu ya udanganyifu. Kutoka kwa maonyesho haya, tunaweza kuona kwamba sisi sio watu waaminifu kweli. Mara tunapoona makosa yetu na upungufu wetu wazi, uamuzi unatokea ndani yetu kuwa na kiu ya ukweli na tunatafuta kutenda maneno ya Mungu zaidi maishani mwetu. Haya ndiyo matokeo yanayopatikana kwa kutafakari maneno ya Mungu.

Bila shaka, matokeo haya hayawezi kupatikana kwa kutafakari maneno ya Mungu mara moja, lakini badala yake kwa kutafakari maneno Yake mara nyingi. Pia, tunapaswa kutenda kwa kujua maneno ya Mungu wakati wowote tunapokumbana na maswala. Kwa ufupi, almradi tunatafakari bila kukoma maneno ya Mungu kwa mioyo yetu kwa njia hii, tutaweza basi kupata nuru na mwanga wa Roho Mtakatifu. Siku moja, tutapata mwanga mpya, na siku inayofuatia tutapata mwanga mpya zaidi na, baada ya muda, tutaweza kuelewa zaidi kuhusu ukweli katika maneno ya Mungu, njia ya kutenda itakuwa wazi zaidi, maisha yetu yatapiga hatua taratibu, na uhusiano wetu na Mungu utakuwa wa karibu zaidi na zaidi. Kama tu inavyosema katika Biblia: “Nawapenda wanaonipenda, na wanaonitafuta kwa bidii watanipata” (Methali 8:17).

3. Tafuta Ukweli na Utende Neno la Mungu Katika Mambo Yote

Mambo muhimu zaidi kwa Wakristo kudumisha uhusiano wa kawaida na Mungu ni kutafuta ukweli wanapokumbana na masuala na kutenda kulingana na neno Lake. Lakini maishani, tunakabiliwa na masuala, mara nyingi sisi hutegemea uzoefu wetu wenyewe au tunatumia njia za kibinadamu kuyashughulikia, au tunayashughulikia kulingana na mapendeleo yetu wenyewe. Sisi mara chache sana hujituliza mbele ya Mungu na kutafuta ukweli, au kushughulikia suala hilo kulingana na mapenzi ya Mungu. Hili linatufanya tupoteze fursa nyingi za kutenda ukweli, na tunasonga mbali na Mungu zaidi na zaidi. Neno la Mungu linasema, “Bila kujali unachokifanya, jambo ni kubwa au dogo kiasi gani, na kama unalifanya ili kutimiza wajibu wako katika familia ya Mungu au kwa ajili ya sababu zako za faragha, lazima ufikirie kama kile unachofanya kinalingana na mapenzi ya Mungu, na vile vile kama ni kitu ambacho mtu ambaye ana ubinadamu anapaswa kufanya. Ukitafuta ukweli kwa namna hiyo katika kila kitu unachofanya, basi wewe ni mtu anayemwamini Mungu kwa kweli(“Kutafuta Mapenzi ya Mungu ni Kwa Ajili ya Kutenda Ukweli”). “Mkidumu katika neno langu, basi ninyi ni wanafunzi wangu kweli(Yohana 8:31). Maneno ya Mungu yanatuonyesha njia wazi. Ikiwa tunafanya kazi kanisani au tunashughulikia masuala ambayo tumekumbana nayo maishani mwetu, lazima daima tutafute ukweli na kuelewa mapenzi ya Mungu, tutazame jinsi ya kushughulikia jambo hilo kwa njia inayoridhisha mahitaji ya Mungu, tutumie ukweli ili kutatua matatizo yote tunayoweza kukumbana nayo na kudumisha uhusiano wetu wa kawaida na Mungu.

Chukua jinsi tunapaswa kutafuta ukweli tunapochagua mchumba, kwa mfano. Tunapotafuta mwenzi, sisi hufuata mapendeleo yetu wenyewe na kuzingatia kuonekana kwa nje kwa mtu na tabia, na tunatafuta mwanamme mrefu, tajiri, mwenye kupendeza, au mwanamke mweupe mwenye ngozi laini, tajiri, mwenye kupendeza, tukiamini kwamba tutakuwa na ndoa ya furaha tu tukimwoa mtu kama huyo, na kwamba tutaishi maisha ya urahisi, faraja na furaha, na wengine watatuonea wivu. Hata hivyo, je, sisi hujiuliza kamwe kama kupata mwenzi kama ule kuna manufaa kwa imani yetu katika Mungu na ukuaji wa maisha yetu? Ikiwa mwenzi wetu hamwamini Mungu na ajaribu kutuzuia kumwamini Mungu, matokeo yatakuwa nini? Biblia inasema, “Ninyi msifungiwe nira pamoja na wale wasiomwamini Mungu kwa njia isiyolingana” (2 Wakorintho 6:14). Kutoka kwa hili, tunaweza kuona kwamba matamanio ya waumini na wasioamini hayaambatani na hayafaani. Katika mitazamo yao kwa imani na mienendo ya kijamii, kila mmoja atakuwa na maoni yake mwenyewe na atatekeleza mambo tofauti: Mkristo atataka kufuata njia ya kumcha Mungu na kuepuka uovu, ilhali asiyeamini atataka kufuata mienendo mibaya wa ulimwengu. Tunapoungana na asiyeamini, tutashawishiwa nao kwa lazima, na ukuaji wa maisha yetu utacheleweshwa. Kwa hiyo, wakati wa kuchagua mwenzi, ni lazima tuzingatie ubinadamu na tabia ya mtu huyo na kuzingatia ikiwa kushirikiana naye kutafaidi imani yetu kwa Mungu au la, ikiwa tuko na mawazo sawa au la, na kama matamanio yetu yanalingana au la. Tusipozingatia mambo haya, lakini tulenge tu kuonekana kwa nje kwa mtu huyo na hali ya familia yake, basi, baada ya kuoana, uchungu utakuja kwa sababu hatuko katika uwiano. Ikiwa mwenzi wetu pia anajaribu kutushurutisha na kutuzuia kumwamini Mungu, basi hili litaharibu maisha yetu ya kiroho hata zaidi. Kwa hiyo inaweza kuonekana kwamba, bila kujali suala gani tunaloweza kukumbana nalo maishani mwetu, ni kwa kutafuta tu ukweli, kufahamu mapenzi ya Mungu na kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu ndiyo tunaweza kuishi chini ya utunzaji na ulinzi wa Mungu, na ni kwa njia hiyo tu ndiyo tunaweza kudumisha uhusiano wetu wa kawaida na Mungu.

4. Njoo Mbele ya Mungu na Utafakari Kujihusu Kila Siku, na Udumishe Uhusiano Wako wa Karibu na Mungu

Yehova Mungu alisema: “Zingatieni njia zenu(Hagai 1:7). Kutoka kwa maneno ya Mungu, tunaweza kuona kwamba kutafakari kujihusu ni muhimu sana kwa kuingia kwetu katika maisha yetu! Kupitia kutafakari, tunaweza kuona kwamba tuna dosari nyingi na kwamba sisi tumepungukiwa katika sana vigezo anavyohitaji Mungu. Kichocheo cha kufuatilia ukweli kwa hiyo kinaibuka ndani yetu, tunaamua kuutelekeza mwili wetu na tunafanya kila tuwezalo kutenda kulingana na neno la Mungu. Kwa njia hii, tunatilia maanani kutenda kulingana na mahitaji ya Mungu katika uzoefu wetu wa vitendo, tunatenda neno la Mungu, na uhusiano wetu na Mungu unazidi kuwa wa kawaida. Kwa mfano, wale kati yetu ambao huhudumu kama viongozi kanisani tunaona kwamba inasema katika Biblia: “Lilisheni kundi la Mungu ambalo liko miongoni mwenu, mkilisimamia, si kwa kushurutisha, lakini kwa kutaka; si kwa ajili ya hela tu, lakini kwa dhati. Wala msiwe mabwana juu ya waliowekwa chini ya utunzaji wenu, ila muwe vielelezo kwa kundi hilo” (1 Petro 5:2–3). Kwa hiyo, tunapaswa kujishughulisha na kutafakari kujihusu tunapowachunga ndugu zetu, na kujiuliza hivi: Je, tunajitahidi kushuhudia maneno ya Bwana na mapenzi Yake, na kuwaongoza ndugu zetu mbele za Mungu, au tunazungumza mambo ya kifahari, yasiyo na maana tunapotoa mahubiri ili tujionyeshe, na kuhubiri maneno na mafundisho ili kuwafanya ndugu zetu watuabudu na kutuheshimu? Wakati ndugu wanatupa mapendekezo ya maana, je, sisi hutafakari kuhusu matatizo yetu au tunakataa kukubali mapendekezo yao, mpaka kwa kiwango ambapo tunatoa vijisababu na kujaribu kujithibitisha? Kupitia kutafakari kujihusu, tunaweza kuona kwamba bado kuna maeneo mengi katika huduma yetu kwa Mungu ambayo sisi ni waasi, na kwamba bado tunamiliki tabia nyingi potovu ambazo zinatuhitaji kuendelea kutafuta ukweli ili ziweze kutatuliwa. Kwa njia hii, tunaweza kutenda kwa unyenyekevu, tunaweza kutafuta mapenzi ya Mungu zaidi katika kazi yetu, na tunaweza kuwaongoza ndugu zetu kulingana na mahitaji ya Mungu. Ikiwa hatuwezi kuja mara nyingi mbele za Mungu na kutafakari juu yetu wenyewe, basi tutashindwa kutambua upotovu wetu na dosari zetu na bado tutaamini kuwa sisi ni watu wanaofuatilia ukweli. Kwa hiyo tutaridhika na kusimama imara na tutakataa kufanya maendeleo zaidi, na tutakuwa wenye kiburi zaidi na zaidi na wenye kujidai, tukijiamini kuwa wanaoupendeza moyo wa Mungu. Kwa kweli, hata hivyo, vitendo na tabia zetu hazitakubalika kwa Mungu, na Mungu atatuchukia. Kwa hiyo inaweza kuonekana kwamba kujishughulisha mara kwa mara na kutafakari kujihusu ni muhimu sana na kwamba kutenda kwa ukweli kwa mtu kunajengwa kwa msingi wa kujitambua. Ni kwa kuwa na ufahamu wa kweli juu ya upotovu wa mtu na dosari zake ndipo majuto yanaweza kuinuka, na mtu kisha atakuwa na ridhaa ya kufuatilia ukweli na kutenda maneno ya Mungu. Kutafakari kujihusu ni kwa manufaa sana kwa maendeleo yetu ya maisha, na ni jambo la muhimu tusiloweza kuliepuka la sisi kumkaribia Mungu.

Kuna njia nyingi za kutafakari juu ya sisi wenyewe: Tunaweza kutafakari juu yetu wenyewe kwa mwongozo wa maneno ya Mungu; tunaweza kutafakari juu yetu wenyewe katika makosa tunayofanya katika maisha yetu ya kila siku; wengine kuonyesha dosari zetu na upotovu hata zaidi ni fursa nzuri ya kutafakari juu yetu wenyewe; zaidi ya hayo, tunapoona makosa yaliyofanywa na wale walio karibu na sisi, tunaweza pia kutafakari juu yetu wenyewe, kuchukua makosa yao kama onyo, tujifunze masomo na kufaidika nao, na kadhalika. Kutafakari kujihusu hakuna mipaka kwa mchana au usiku. Wakati wowote na mahali popote, tunaweza kumwomba Mungu mioyoni mwetu, kutafakari kuhusu na kutambua upotovu wetu wenyewe, na tunaweza kutafuta mapenzi na mahitaji ya Mungu ndani ya maneno Yake, na kutubu kwa wakati. Hata hivyo, kabla ya kulala kila usiku, tunapaswa kutafakari na kufanya muhtasari wa kila kitu tulichofanya siku hiyo, na kisha tutaweza kuwa na ufahamu wazi zaidi juu ya hali zetu na kujua vitu ambavyo hatujafanya sahihi. Mara tunapoanza kufanya jambo hili, kufuatilia kwetu kutakuwa na mwelekeo zaidi na kutakuwa na manufaa zaidi katika kuanzisha uhusiano wa kawaida na Mungu.

Ndugu, hoja nne zilizo hapo juu ndizo njia ya kutenda kwa sisi kumkaribia Mungu. Almradi tunaweka hoja hizi katika vitendo, basi uhusiano wetu na Mungu utakuwa wa karibu, tutakuwa na njia ya kutenda kwa masuala tunayokumbana nayo, na Mungu atatupa amani na furaha na atatuwezesha kuishi katika baraka Zake. Kwa hiyo, kwa nini tusianze sasa hivi?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ishara 6 za kurudi kwa Bwana Yesu Zimeonekana

Miaka elfu mbili iliyopita, Bwana Yesu alituahidi: “Tazama, Naja upesi” (Ufunuo 22:12). Sasa, kila aina ya ishara za kurudi Kwake zimeonekana, na ndugu wengi wamekuwa na maono kwamba siku ya Bwana iko karibu. Je, Bwana tayari Amerudi? Je, tunaweza kufanya nini ili kumkaribisha Bwana? Hebu tujadili hili sasa kwa kuchunguza unabii ulio katika Biblia.

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp