173 Azimio Langu Huimarishwa Kupitia Mateso

1

Shetani hushikilia mamlaka na kuipinga Mbingu, ni mpotovu, mhalifu na mwovu.

Anamchukia Kristo na kushutumu ukweli, huwakandamiza watu kiibilisi na mawingu meusi yanafunika ardhi yote.

Kumfuata Kristo na kufuatilia maisha ni barabara iliyo na mashimomashimo ukifuata, na ina hatari na dhiki nyingi.

Tutaweza kukusanyika kwa usalama ili kushiriki kuhusu maneno ya Mungu, na kutoishi tena mafichoni lini?

Tutaweza kutekeleza wajibu wetu lini bila kutahadhari dhidi ya wapelelezi na polisi wenye nguo za raia?

Tutaweza kuhubiri injili na kushuhudia kwa Mungu bila kukabiliwa na kukamatwa na kufungwa lini?

Ni lini ambapo ndugu wanaosakwa hawatalazimika tena kuishi kama wakimbizi?

Nimehisi uchungu mno mara nyingi, kiasi kwamba sina budi ila kulia:

Kwa nini lazima atunyime uhuru wetu wa kuamini na kuwaangamiza Wakristo wote?

Kwa nini yeye huficha ukweli ili kuwadanganya na kuwahadaa watu wa ulimwengu?

Kwa uchungu, ninamsihi Mungu na kumtegemea, nikimwomba imani na nguvu.

Bila kujali mateso na shida ni kubwa kiasi gani, kamwe sitajisalimisha kwa Shetani.

2

Kupitia kifungo, mateso na maumivu, maneno ya Mungu yananiongoza, na moyo wangu hauogopi tena.

Ninaelewa ukweli na ninabaini uso mbaya wa shetani, na ninachukia joka kubwa jekundu hata zaidi.

Ingawa ninapata maumivu, imani yangu imeimarishwa. Ninajua nipende nini na nichukie nini, na hata zaidi nahisi jinsi Mungu anavyopendeza.

Wakati ambapo siwezi tena kuvumilia mateso na maumivu, maneno ya Mungu yanaitegemeza imani yangu.

Maisha yangu yanapokuwa hatarini, Mungu hunilinda kwa siri kutokana na madhara.

Ninapozingirwa na majaribu ya Shetani, maneno ya Mungu hunipa ujasiri na hekima.

Nikiwa na Mungu kando yangu, sihisi tena mpweke kupitia usiku usiokuwa na mwisho.

Ee Mungu, maneno Yako yameniongoza na kunilinda hadi sasa.

Nimepitia maneno Yako ambayo yana mamlaka makubwa na nguvu ya kupita uwezo wa binadamu.

Katika shida, nahisi uwepo Wako. Ingawa mwili wangu unateseka, moyo wangu unahisi utamu mno.

Kunapendeza sana kuteseka ubavuni pa Mungu, ninaahidi maisha yangu kupigana vita vya kuamua mshindi na mshinde dhidi ya Shetani hadi mwisho.

Ninaimarisha azimio langu na kutoa ushuhuda mkuu sana, ili kumtukuza Mungu na kushuhudia kwa Mungu.

Iliyotangulia: 172 Tunakamilisha Misheni Yetu

Inayofuata: 174 Mfuate Mungu kwa Karibu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp