647 Tunaokolewa Kwa Sababu Mungu Alituchagua

1 Tunazaliwa katika nchi ya uchafu, lakini kwa sababu ya ulinzi wa Mungu, kwa sababu ya uongozi Wake, na kwa sababu Ametushinda, tumejiondoa katika ushawishi wa Shetani. Kwamba tunaweza kutii leo pia ni matokeo ya kushindwa na Mungu, na sio kwa sababu sisi ni wema, au kwa sababu tunampenda Mungu kwa asili. Ni kwa sababu Mungu alituchagua, na kutujaalia, ndio tumeshindwa leo, tunaweza kuwa na ushuhuda Kwake, na tunaweza kumhudumia.

2 Ni kwa sababu Alituchagua, na kutulinda, ndio tumechaguliwa na kutolewa katika miliki ya Shetani, na tunaweza kuachana na uchafu na kutakaswa katika nchi ya joka kuu jekundu. Ni kweli kwamba sisi ni wapotovu kuliko watu wote—hili lilitamkwa na Mungu, huu ni ukweli, na haupingwi na mtu yeyote. Lakini leo tumeukwepa ushawishi huo. Tunawachukia sana mababu zetu, tupo radhi kuwageuzia migongo mababu zetu, kuwatelekeza kabisa na kutii mipango yote ya Mungu, kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu, na kutimiza matakwa Yake kwetu, na kufikia ridhaa ya mapenzi ya Mungu.

Umetoholewa kutoka katika “Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Ushindi (2)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 644 Kutumika kama Foili ni Baraka ya Milele

Inayofuata: 649 Huwezi Kusikitisha Mapenzi ya Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp