616 Kanuni Mbili Ambazo Viongozi na Wafanyakazi Lazima Waelewe

1 Katika kazi yao, viongozi wa kanisa na wafanyakazi wanapaswa kuzingatia mambo mawili: Moja ni kufanya kazi yao kabisa kulingana na kanuni zilizowekwa masharti na mipangilio ya kazi, bila kamwe kukiuka kanuni hizi na kutotegemeza kazi yao juu ya chochote watakachofikiri au juu ya nia zao wenyewe. Katika kila kitu wafanyacho; wanapaswa kujali kazi ya familia ya Mungu, na siku zote kuweka maslahi yake kwanza. Kuna kitu kingine ambacho ni muhimu, nacho ni kwamba katika kila kitu wakifanyacho, lazima wazingatie kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu, na kufanya kila kitu kwa usahihi kulingana na neno la Mungu.

2 Ikiwa bado una uwezo wa kuenda kinyume na mwongozo wa Roho Mtakatifu, au ikiwa kwa ukaidi unafuata mawazo yako mwenyewe na kufanya mambo kulingana na fikira zako mwenyewe, basi matendo yako yatakuwa na upinzani mkali sana dhidi ya Mungu. Mara kwa mara kuasi nuru na mwongozo wa Roho Mtakatifu kutakuongoza tu kwa mwisho kabisa. Ukipoteza kazi ya Roho Mtakatifu, basi hutaweza kufanya kazi, na hata ukiweza kufanya kazi, hutatimiza chochote. Hizi ndizo kanuni mbili kuu za kuzingatia wakati unafanya kazi: Moja ni kufanya kazi kulingana na mipangilio kutoka hapo juu kabisa na pia kutenda kulingana na kanuni zilizowekwa na hayo ya hapo juu. Jambo jingine ni kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu ndani. Mara tu mambo haya mawili yanapofahamika, hutafanya makosa kwa urahisi.

Umetoholewa kutoka katika “Kanuni Kuu za Kazi kwa Viongozi na Wafanyakazi” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 615 Jinsi ya Kustahili Kutumiwa na Mungu

Inayofuata: 617 Kumbusho la Mungu kwa Mwanadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp