47 Ni Mwenyezi Mungu Pekee Aliye Uzima Uliofufuka wa Milele

1 Milima na mito huenda ikibadilika, vijito hutiririka kwenye mikondo yao, na maisha ya mwanadamu ni yenye uvumilivu mdogo kuliko ardhi na anga. Mwenyezi Mungu pekee ndiye maisha ya milele yaliyofufuka milele, katika vizazi hai milele! Vitu vyote na matukio viko katika mikono Yake, Shetani yuko chini ya miguu Yake. Leo hii ni kwa sababu ya uteuzi wa Mungu ulioamuliwa kabla kwamba Ametuokoa kutoka kukamatwa na Shetani. Yeye kweli ni Mkombozi wetu. Maisha ya kufufuliwa ya Kristo milele yametugusa ndani yetu, hivi sisi tumejaliwa kuhusiana na maisha ya Mungu, tunaweza kuwa naye ana kwa ana, kumla Yeye, kumnywa Yeye, na kumfurahia Yeye. Huku ni kujitolea kwa Mungu kwa bidi na kusio na ubinafsi.

2 Majira yanakuja na ku kuenda, yakipitia upepo na jalidi, yakikumbana na taabu, mateso na majonzi mengi sana ya maisha, kukataliwa na kukashifiwa duniani, serikali kusingizia mashtaka, hakuna upungufu wa imani ya Mungu wala kusudi. Kwa ukamilifu kwa ajili ya mapenzi ya Mungu, ili usimamizi wa Mungu na mpango utimizwe, Yeye huweka maisha Yake Mwenyewe kando. Kwa ajili ya watu Wake wote, huwa Hapuri juhudi yoyote, kwa uangalifu Akilisha na kunyunyizia. Haidhuru kiasi cha ujinga, tu wagumu kiasi kipi, tunahitaji tu kutii mbele Yake, na maisha ya kufufuka kwa Kristo yatabadilisha asili yetu ya zamani…. Kwa wana hawa wazaliwa wa kwanza, Yeye hufanya kazi bila kuchoka, huachilia chakula na usingizi. Ni mchana na usiku ngapi, ni kupitia joto ngapi kali, na baridi ya kuganda, Yeye hutazama kwa moyo mmoja katika Sayuni.

3 Ulimwengu, nyumba, kazi vimeachiliwa kabisa, bila kusita, bila raha za kidunia kumgusa…. Maneno kutoka kinywa Chake yanatupiga kwa ndani, yakifunua mambo yaliofichwa kwenye kina cha mioyo yetu. Ni vipi haturidhishwi? Kila sentensi inayotoka katika kinywa Chake inatendeka wakati wowote kwetu. Kila kitendo chetu, hadharani na faraghani, hakuna ambacho Yeye hakijui, hakuna Asichokijua. Kwa kweli vyote vitafichuliwa mbele Yake, licha ya mipango yetu wenyewe na matayarisho.

4 Tukiwa tumeketi mbele Yake, roho zetu hufurahia, kustareheshwa na tulivu, daima kuhisi tupu ndani, kwa kweli kuwiwa kwa Mungu. Hili ni jambo la ajabu lisilofikirika na lisiloweza kufanikishwa. Roho Mtakatifu anathibitisha vya kutosha kwamba Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja wa kweli! Asiyepingika! Sisi, kundi hili la watu, kwa kweli tumebarikiwa! Kama si kwa neema ya Mungu na rehema, lazima tuangamie milele na kumfuata Shetani. Ni Mungu Mwenyezi pekee Anayeweza kutuokoa! Ah! Mwenyezi Mungu, Mungu wa vitendo! Ni Wewe ambaye Umefungua macho yetu ya kiroho, kwamba tumeweza kuona siri za dunia ya kiroho. Taswira za ufalme hazina na mwisho. Kuweni waangalifu na wenye kusubiri. Siku haiwezi kuwa mbali sana.

5 Mioto ya vita huzunguka, moshi wa bunduki huelekea, hali ya hewa huwa vuguvugu, tabia ya nchi hubadilika, tauni litaenea, na watu lazima wafariki, na tumaini ndogo la kuishi. Ah! Mwenyezi Mungu, Mungu wa vitendo! Wewe ni mnara wetu imara. Wewe ni kimbilio letu. Sisi tunakusanyika chini ya mabawa Yako, na janga haliwezi kutufikia. Huu ni utunzaji Wako mtakatifu. Sisi sote tunainua sauti zetu, kuimba sifa, sifa ambazo zinavuma kote Sayuni! Mwenyezi Mungu, Mungu wa vitendo ameandaa hatima hio tukufu kwa ajili yetu. Kuwa mwangalifu—mwangalifu! Wakati hauwezi kuwa mbali sana.

Umetoholewa kutoka katika “Sura ya 5” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 46 Ni Mwenyezi Mungu Pekee Awezaye Kumwokoa Mwanadamu

Inayofuata: 48 Ulimwengu Mzima ni Mpya Kabisa

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp