206 Sitawahi Tena Kujitenga na Mungu

1

Baada ya mimi kuwa muumini katika Mungu, kulikuwa na wakati ambapo nilianza kufuatilia pesa na utajiri, nilipomtelekeza Mungu na kurudi katika ulimwengu wa nje.

Nilitumia siku zangu kukurupuka huku na kule kwa ajili ya mwili, nikichosha akili na mwili.

Siku hizo bila Mungu zilikuwa siku za uchungu.

Nilikuwa nimetumbukia gizani, na moyo wangu ulijawa na woga.

Ni baada tu ya kurudi na kufundishwa nidhamu kali kwa Mungu ndipo nilianza kutafakari kujihusu.

Sikuwa nimemfuata Mungu kamwe kwa dhati, na sikuwa nimethamini maneno ya Mungu kamwe.

Iliuvunja moyo wa Mungu nilipokana imani yangu na kuacha haki. Nilijiuliza: Dhamiri yangu iko wapi?

Sikumwogopa Mungu, nilikuwa nimekiuka tabia Yake, lakini bado nilisalia kutotambua.

2

Ni wakati tu ambapo hukumu na kuadibu kwa Mungu viliniokoa ndipo nilijua asili yangu—asili ambayo humsaliti Mungu.

Niliinama mbele za Mungu, nikijawa na majuto, na hatia na lawama moyoni mwangu.

Ukatili na uasi wangu vilikuwa vimeuvunja moyo wa Mungu; ningefutaje vitu vya aibu nilivyokuwa nimefanya?

Ni huruma na wema wa Mungu vilivyonipa nafasi ya kutubu,

vikiniruhusu nirudi katika nyumba ya Mungu na kutekeleza wajibu wangu mara nyingine tena.

Nilihisi upendo wa kweli wa Mungu, na moyoni mwangu kulikuwa na ufahamu mkubwa zaidi kuhusu jinsi nilivyo na deni Lake kubwa.

Nilihisi kwamba kuna haki na uadhama katika tabia Yake, na vile vile huruma na wema.

Nilijipa lengo jipya: kuanza upya, kulipa upendo wa Mungu na kumshuhudia.

Iliyotangulia: 205 Pingu

Inayofuata: 207 Sitaacha Majuto Moyoni Mwangu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp