53. Kulegeza Uhusiano Unaowafunga Watu Pamoja

Na Cuibai, Italia

Mwenyezi Mungu anasema, “Kwa minajili ya majaliwa yenu, mnastahili kutafuta kuidhinishwa na Mungu. Hii ni kusema kwamba, kwa sababu mnatambua kwamba nyinyi mmehesabiwa miongoni mwa wale walio katika nyumba ya Mungu, basi mnastahili kumletea Mungu utulivu wa akili katika mambo yote na kumtosheleza katika kila jambo. Kwa maneno mengine, lazima muwe wenye maadili katika matendo yenu na kutii ukweli katika mambo kama hayo. Kama hali hii inazidi uwezo wako, basi utachukiwa na kukataliwa na Mungu na vilevile kukataliwa kwa dharau na kila mwanadamu. Punde utakapokuwa katika hali mbaya kama hii, basi hauwezi kuhesabiwa miongoni mwa wale walio kwenye nyumba ya Mungu. Hii ndiyo maana ya kutoidhinishwa na Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maonyo Matatu). Kutoka katika maneno ya Mungu tunaona kile Anachohitaji kutoka kwetu: tuwe wenye maadili katika matendo yetu na tufuate ukweli ili tuweze kupata kibali Chake na kumridhisha katika mambo yote. Nilishindwa kufanya hivi awali, kwa kiasi kikubwa kwa sababu nilitawaliwa na hisia zangu, kila wakati nikiishi na kutenda kulingana na hisia zangu. Ingawa haikuonekana kama kwamba nilikuwa nikifanya uovu wowote, matendo yangu yalikwenda kinyume na kanuni za ukweli na hili liliizuia kazi ya kanisa. Lakini baada ya Mungu kunihukumu na kuniadibu kwa maneno Yake, nilianza kuelewa asili na athari za kutenda kwa namna hii. Ningeweza kisha kuyakabili mambo kwa nia sahihi badala ya kutegemea hisia, na ningeweza kutia maneno ya Mungu katika vitendo.

Mnamo Novemba iliyopita wakati wajibu wangu ulikuwa kiongozi wa kanisa, kulikuwa na kura juu ya jinsi kiongozi wa kikundi wa kila mahali pa mkutano alivyokuwa akifanya kazi. Kutoka katika majibu, niliona kwamba kiongozi wa kikundi Dada Li daima alikuwa mzembe katika wajibu wake na kwamba ikiwa kosa lake lolote lingetajwa, mbali na kukataa kukubali ukweli, pia alibishana. Wakati wengine walipatwa na shida, hangewasaidia kwa kufanya ushirika juu ya ukweli, lakini badala yake angewakaripia kwa njia ya kuwashushia hadhi na kuwazuilia. Baada ya kusoma haya yote, nilijua kwamba kwa kuzingatia kanuni za uteuzi katika nyumba ya Mungu, ilibidi abadilishwe. Lakini tulitoka katika mji mmoja wa nyumbani na tulikuwa tumefanya kazi pamoja katika wajibu wetu hapo awali. Siku zote tulikuwa karibu na alikuwa amenitunza sana. Kama ningemwachisha kazi, je, angefikiria mimi ni mkatili? Miaka michache kabla alikuwa ameondolewa kutoka katika wadhifa wake kama kiongozi wa kanisa, na alikuwa ameweza kujiondoa kutoka katika uhasi kidogo tu. Ikiwa wadhifa mwingine ungechukuliwa kutoka kwake, hilo halingekuwa pigo kubwa hata zaidi? Je, angeweza kustahimili hilo? Niliona kwamba nilihitaji kushiriki na yeye mara moja ili aweze kuona jinsi hali yake ilivyokuwa ya hatari. Niliwaza kwamba kama angeweza kugeuza mambo kwa wakati basi angeweza kuhifadhi wadhifa wake. Kwa hivyo, niliwasiliana na Dada Li katika ushirika kuhusu maswala yake lakini nikagundua kwamba hakuwa na kujitambua kwa kweli hata kidogo. Nilifanya kila niwezalo katika ushirika huo na yeye, na baadaye alikuwa radhi kubadilika, kutafakari, na mwishowe nikashusha pumzi ya afueni. Nilidhani kwamba ikiwa ningeweza kusema maneno machache mazuri juu yake kwa wafanyakazi wenza, labda angeendelea kufanya wajibu huo.

Baadaye wakati wa kujadili kazi, wafanyakazi wenza wachache walisema Dada Li hakukubali ukweli kamwe na wote walikubali kumwondoa kutoka katika wadhifa huo. Kusikia hili kulinisababishia msukosuko. Niliwaza, “Dada Li ana matatizo kadhaa, lakini yuko tayari kubadilika, kwa hivyo hamwezi kumpa nafasi nyingine? “Wakati huo tu Dada Zhou alisema, “Dada Li amekuwa katika hali hii kwa muda sasa. Yeye hufanya ushirika vizuri, lakini hatendi kile anachosema. Hakuna mabadiliko kabisa. Hastahili kabisa kufanya kazi hii.” Niliingilia kwa kuunga mkono, “Dada Li ana wakati mgumu kukubali ukweli, lakini yeye ni mwenye vitendo kweli na anayewajibika katika wajibu wake. Hivi majuzi tu ndugu wengine walikuwa baridi katika wajibu wao na aliwatia motisha.” Dada Bai alijibu mara moja, “Dada Li anaonekana kama kwamba kila wakati yeye hukimbia huku na kule, akiwa mwenye vitendo, lakini kwa kweli anafanya yote kwa sababu ya kujionyesha, na hawezi kutatua matatizo ya kweli.” Kila walichosema kilikuwa kweli, na sikuweza kusema chochote ili kujibu. Kisha kiongozi mwingine wa kanisa, Dada Zhang, akasema, “Ni kweli kuwa Dada Li hafai kabisa kuwa kiongozi wa kikundi, lakini hatuna mgombea anayefaa kuchukua nafasi yake sasa. Tumwache asalie katika nafasi hiyo hadi tuweze kupata mtu anayefaa kuchukua nafasi hiyo.” Hili ndilo nililotaka hasa, kwa hivyo niliharakisha kuongezea, “Nakubali. Acha tumbadilishe mtu mwingine atakapopatikana.” Nilishangaa, baada ya chini ya wiki moja baadaye, Dada Zhou aliibua suala hilo tena baada ya sisi kumaliza kujadili kazi ya kanisa. Alisema kwamba Ndugu Chen alikuwa chaguo zuri, na wafanyakazi wenza wengine wachache walikubali. Moyo wangu ulishtuka. Kama Ndugu Chen angechaguliwa kama kiongozi wa kikundi, Dada Li angefukuzwa kazi. Kwa hivyo nilisema mambo fulani kuhusu upotovu na upungufu wa Ndugu Chen, na nikasema kwamba hakufaa kwa kazi hiyo. Kisha kila mtu alianza kusita na nilihisi wasiwasi kidogo, lakini bado sikutafuta ukweli.

Kiongozi wangu baadaye aliniuliza nimpe muhtasari kuhusu viongozi wa kikundi, na nilipomfikia Dada Li, sikuonyesha kwa usahihi tathmini ya akina ndugu kumhusu. Nilihisi kusumbuka kidogo baada ya yeye kuondoka. Nilijiuliza kwa nini nilikuwa nikizungumza kwa niaba ya Dada Li, nikihangaika kila wakati juu yake. Je, sikuwa nikimwonyesha upendeleo? Ni nia ya aina gani iliyokuwa ikinidhibiti? Kisha nilisoma maneno haya ya Mungu: “Kimsingi, hali ya mhemuko ni nini? Ni tabia potovu. Tukitumia maneno machache kuelezea vipengele halisi vya hali ya mhemuko, ni upendeleo na ubaguzi wa kuwalinda watu fulani, kudumisha uhusiano wa kimwili, na kutokuwa wenye haki; hii ndiyo hali ya mhemuko. Kwa hivyo, kutupilia mbali mhemuko wa mtu hakumaanishi tu kutofikiria tena kuhusu mtu fulani. Kwa kawaida, huenda usifikirie kumhusu hata kidogo, lakini punde tu mtu anapowakosoa watu wa familia yako, makazi yako ya kudumu, au mtu yeyote ambaye una uhusiano naye, unakasirika na unakuwa tayari kwenda kupigana kwa niaba yao. Unahisi uliyelazimika kabisa kubadilisha yale yaliyosemwa kuwahusu; huwezi kuruhusu wakumbwe na kosa ambalo halijarekebishwa. Unahisi haja ya kufanya kila uwezalo ili kutetea sifa zao, kufanya kila kitu kibaya kionekane kuwa sawa, na kutowaruhusu wengine waseme ukweli kuwahusu au kuwafunua. Hii siyo haki, na inaitwa kuwa wa mhemuko(“Uhalisi wa Ukweli ni Nini?” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). “Watu wakikosa uchaji kwa Mungu, na kama Mungu hana nafasi mioyoni mwao, basi hawawezi kamwe kutenda kulingana na kanuni bila kujali ni wajibu upi wanaotimiza au ni shida gani wanazozishughulikia. Watu wanaoishi ndani ya dhamira zao na matamanio ya ubinafsi hawawezi kuingia katika uhalisi wa ukweli. Kwa sababu hii, wakati wowote wanapokumbana na shida, hawachunguzi dhamira zao na hawawezi kutambua ni wapi ambapo dhamira zao zina makosa. Badala yake, wao hutumia uhalalishaji wa kila aina kujibunia uongo na visingizio. Wao hufanya kazi nzuri sana ya kulinda masilahi, sifa, na uhusiano wao baina ya watu, lakini kwa kweli, hawajaanzisha uhusiano wowote na Mungu(Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Hii inaonyesha jinsi katika shida, hatuwezi kutenda kwa haki kulingana na kanuni za ukweli. Lakini hatutofautishi kati ya mema na mabaya, kupendelea na kulinda wale ambao tunahusiana nao, au wanaotufaidi. Huku ni kutenda kulindana na hisia na ni aina ya tabia potovu. Tunapotawaliwa na hisia, iwe ni katika wajibu wetu au kushughulikia shida, tunafikiria tu hisia zetu za kimwili na masilahi ya kibinafsi bila kutenda ukweli au kufanya wajibu wetu vizuri hata kidogo. Hiyo ndiyo hali niliyokuwa ndani. Sikutaka kumfukuza Dada Li kwa sababu nilikuwa nikitenda kulingana na hisia zangu. Nilikuwa nalinda uhusiano wetu na niliogopa kwamba angenikasirikia. Kwa hivyo wafanyakazi wenza walipotaka kufuata kanuni na kumbadilisha, nilifanya kila nilichoweza kumlinda ili aweze kushikilia wadhifa wake. Nilipompa kiongozi tathmini yangu kumhusu nilificha uzito wa tathmini hiyo, nikamficha kwa sababu ya upendeleo, na nikamfunika kutumia kisingizio. Ninapokumbuka nyuma, naona kwamba nia na motisha zangu zote zilitawaliwa na hisia. Nilikuwa naishi katika tabia potovu ya ujanja na udanganyifu, nikiwa tayari kuachana na masilahi ya nyumba ya Mungu ili kulinda uhusiano, tayari kumkosea Mungu kabla ya kumkosea mtu. Nilikosa uchaji kwa Mungu kabisa, nilikuwa mbinafsi na mwenye kustahili dharau kabisa! Nilihisi mwenye hatia kuhusu yote haya, kwa hivyo nilimwendea kiongozi kumwambia ukweli. Baada ya hapo, niliomba na kumwita Mungu: “Je, kwa nini mimi huongozwa na hisia kila wakati, nisiweze kutenda ukweli? Kiini cha tatizo hili ni nini?”

Siku moja katika ibada zangu, nilisoma maneno haya kutoka kwa Mungu: “Kwa sababu ya kuzaliwa katika nchi ya uchafu vile, mwanadamu ameangamizwa kabisa na jamii, amekuwa akishawishiwa na maadili ya kikabaila, na amefundisha katika ‘taasisi za elimu ya juu.’ Fikra zilizo nyuma kimaendeleo, maadili potovu, mtazamo mbaya juu ya maisha, falsafa za kudharauliwa za kuishi, uwepo usio na thamani, na hali potovu za maisha na desturi—mambo yote haya yameuingilia moyo wa mwanadamu, na kudhoofisha na kushambuliwa dhamiri yake pakubwa. Matokeo yake, mwanadamu kamwe yuko mbali kutoka kwa Mungu, na kila mara anampinga. Tabia ya mwanadamu inakuwa matata zaidi kila siku, na hakuna hata mmoja ambaye kwa hiari yake atatoa chochote kwa ajili ya Mungu, hakuna hata mmoja ambaye kwa hiari atamtii Mungu, wala, zaidi ya hayo, mwanadamu mmoja ambaye kwa hiari yake atatafuta uso wa Mungu. Badala yake, chini ya umiliki wa shetani, mwanadamu hafanyi kitu ila kukimbiza anasa, kujitoa mwenyewe kwa upotovu wa mwili katika nchi ya matope. Hata wanaposikia ukweli, wale wanaoishi gizani hawafikiri kuuweka katika vitendo, na wala kuelekea kumtafuta Mungu hata kama wameuona mwonekano Wake. Jinsi gani wanadamu wapotovu kiasi hiki wawe na nafasi yoyote ya wokovu? Jinsi gani wanadamu waovu kiasi hiki kuishi katika mwanga?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu). Kisha nikagundua kwamba kutenda kulingana na hisia hutokana na kudanganywa na kupotoshwa na Shetani. Kupitia elimu ya shule na ushawishi wa kijamii, ibilisi Shetani huwalowesha watu katika kila aina ya falsafa za ulimwengu na sheria za kuishi kama “Mbingu huwaangamiza wale wasio wabinafsi,” “Damu ni nzito kuliko maji,” na “Mwanadamu si asiye na uhai, anawezaje kukosa hisia?” Nimeishi kwa kufuata falsafa hizi, kuona kuwalinda wale walio karibu nami kama jambo zuri, kuona utu wema na huruma kama kuwa mwenye upendo. Na kuhusu Dada Li kubadilishwa, niliendelea kufikiria tunatoka katika sehemu moja na kwamba alinitunza kila wakati, kwa hivyo alipokuwa anakabiliwa na kufukuzwa kazini niliona nilipaswa kumsaidia na kumtetea. Nilifikiria hilo ndilo lilikuwa jambo la haki kufanya. Nilijua kwamba hakuwajibikia wajibu wake kama kiongozi wa kikundi lakini mara nyingi aliwakaripia wengine na kuwadhibiti. Kutombadilisha kungewaumiza vibaya akina ndugu na kuiathiri kazi ya kanisa. Lakini nilienda kinyume na kanuni za ukweli na nikayapuuza masilahi ya nyumba ya Mungu, nikifanya yote niliyoweza kumlinda na kumhifadhi katika wadhifa wake. Nilitumia wajibu wangu kuulinda uhusiano wetu na nikatumia kazi ya kanisa kulipa fadhila zake kwangu. Nilikuwa nikitumia mamlaka na wajibu wangu kwa manufaa yangu mwenyewe. Kama kiongozi, nilipaswa kuwa nikiifikiria kazi ya kanisa na maisha ya akina ndugu, na kutenda kwa kufuata kanuni za ukweli katika wajibu wangu. Lakini nilikuwa nikiweka hisia kuwa muhimu zaidi vyote, nikiwa najua ukweli vizuri kabisa, lakini sikuutenda. Je, huko hakukuwa kuusaliti ukweli na kanuni, na kuichukulia kazi ya kanisa kimzaha? Huko kulikuwa kuuma mkono unaonilisha! Kisha niliona kwamba hizo falsafa za ulimwengu ni uwongo ambao Shetani hutumia kuwapotosha na kuwadanganya watu. Kuongea na kutenda namna hiyo ni kukosa usawa na haki kabisa, na kwa kweli hakuna kanuni za ukweli ndani yake. Hiyo hasa ndiyo falsafa ya maisha ya maafisa wa Chama cha Kikomunisti: “Mtu apatapo Tao, hata wanyama wake wapenzi hupaa kwenda mbinguni” Mtu anapokuwa ofisa, jamaa zake wengi hunufaika pia, na wanaweza kufanya chochote bila hofu ya kuadhibiwa. Jamii inayodhibitiwa na CCP ni yenye giza sana, ovu sana, isiyo na usawa au haki kabisa. Kama kiongozi wa kanisa, kutotenda kulingana na kanuni lakini kuishi kwa kufuata hizi falsafa za kishetani, nilikuwaje tofauti na ofisa wa CCP? Kutotaka kumfukuza Dada Li hakukuwa kwa sababu ya upendo wa kweli au kusaidia, niliogopa tu kwamba angesema nilikuwa mkatili na asiye na hisia na hagenitazama tena kwa njia ile ile. Sikuwa nikizingatia maisha yake hata kidogo. Kumbadilisha mtu katika nyumba ya Mungu hufanywa ili kuhimiza kujitafakari, ili aweze kutubu na kubadilika kwa wakati unaofaa. Ni njia mojawapo ambayo Mungu huwaokoa na kuwalinda watu. Nimewahi kufukuzwa kutoka katika wajibu wangu, pia, na baada ya kupata funzo kutoka kwa kushindwa kwangu, kanisa lilinipangia wajibu mwingine unaonifaa. Ni kujikwaa na kuanguka tu ndivyo vilivyonifanya nitafakari na kuniruhusu nipate kujitambua kwa kweli. Pia nilielewa zaidi juu ya mapenzi ya Mungu kumwokoa mwanadamu na nikaona kwamba upendo Wake una rehema na haki. Kuna kanuni kwa upendo wa Mungu; Yeye hatuendekezi au kutubembeleza. Lakini “upendo” wangu kwa wengine ulikuwa umejaa falsafa za ulimwengu za kishetani na ulitegemezwa katika masilahi ya kibinafsi. Ulikuwa finyu na wa ubinafsi, wa kukirihi na chukizo kwa Mungu. Kwa hivyo niligundua kwamba ni jambo la kuwadhuru wengine na kwa sisi wenyewe tunapotegemea hisia zetu, na hicho ndicho kilikuwa kizuizi kikubwa zaidi kwangu katika kutenda ukweli na kufanya wajibu wangu vizuri. Bila kukubali hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu, bila toba ya kweli, ningeikosea tabia ya Mungu na kukataliwa, kuchukiwa na kuondolewa na Mungu.

Baadaye nilisoma kifungu kingine cha maneno ya Mungu: “Ikiwa unataka kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu, basi lazima moyo wako umgeukie Mungu. Hili likiwa msingi, pia utakuwa na uhusiano wa kawaida na watu wengine. Iwapo huna uhusiano wa kawaida na Mungu, basi haijalishi unachofanya kudumisha uhusiano wako na watu wengine, haijalishi jinsi gani unafanya kazi kwa bidii au ni nguvu kiasi gani unaweka ndani yake, bado ni ya falsafa ya mwanadamu ya maisha. Unadumisha nafasi yako miongoni mwa watu kupitia mtazamo wa mwanadamu na falsafa ya mwanadamu ili kwamba watu wakupe wewe sifa, lakini hufuati neno la Mungu ili kuanzisha uhusiano wa kawaida na watu. Iwapo huzingatii uhusiano wako na watu lakini unadumisha uhusiano wa kawaida na Mungu, ikiwa uko tayari kumpa Mungu moyo wako na ujifunze kumtii, basi kwa kawaida sana, uhusiano wako na watu wote utakuwa wa kawaida. Kwa njia hii, uhusiano huu haujengwi kwa mwili, bali juu ya msingi wa upendo wa Mungu. Kwa kiasi kikubwa hakuna ushirikiano uliojengwa juu ya mwili, lakini katika roho kuna ushirikiano na vilevile upendo, starehe, na kutoleana kwa wenza. Haya yote yanafanywa kwa msingi wa moyo unaomridhisha Mungu. Uhusiano huu haudumishwi kwa kutegemea falsafa ya mwanadamu ya maisha, bali unaundwa kwa kawaida kupitia mzigo wa Mungu. Hauhitaji jitihada zilizofanywa na binadamu. Unahitaji tu kutenda kulingana na maadili ya neno la Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kawaida na Mungu).

Baada ya kusoma maneno ya Mungu nilielewa kwamba uhusiano na kina ndugu mara nyingi hutegemezwa kwa upendo wa Mungu. Haushikiliwi na falsafa za kilimwengu za Shetani. Kutenda ukweli ndilo jambo muhimu. Hasa linapokuja suala la kazi ya nyumba ya Mungu, tunapomwona mtu akifanya wajibu wake dhidi ya kanuni za ukweli, lazima tushiriki juu ya ukweli ili kumsaidia na kumhimili. Ikiwa bado hatubu baada ya ushirika kadhaa, basi anahitaji kupogolewa na kushughulikiwa inapohitajika. Hata kwa familia na marafiki, hatuwezi kutegemea hisia zetu au kufuata falsafa za ulimwengu. Lazima tufanye mambo kwa kufuata kanuni za maneno ya Mungu: Fanya ushirika inapohitajika na tuwabadilishe ikiwa ushirika hausaidii. Kazi ya kanisa na masilahi ya nyumba ya Mungu lazima yatetewe kila wakati. Hili tu ndilo linaloambatana na mapenzi ya Mungu. Baadaye nilijadili haya na wafanyakazi wenza na nikamfukuza Dada Li nikizingatia kanuni za ukweli. Pia nilifanya ushirika kuchambua utendaji wake kwa kuzingatia maneno ya Mungu na nikampandisha cheo Ndugu Chen kuwa kiongozi wa kikundi. Ni hapo tu ndipo nilihisi utulivu moyoni mwangu. Baada ya muda nilimsomea Dada Li maneno fulani ya Mungu na nikamuuliza alivyokuwa anaendelea? Alisema, “Shukrani ziwe kwa Mungu! Kila Anachofanya ni kizuri. Mwanzoni nilihisi uhasi na nilikuwa nikiteseka, lakini kupitia kusoma maneno ya Mungu na kuomba, nilielewa kwamba Mungu alikuwa Akifanya kazi kwa njia hii ili Anibadilishe, na nisingefukuzwa kazi na shida zangu zionyeshwe, nisingejijua mwenyewe, wala nisingebadilika na kutubu kama nilivyofanya sasa.” Kusikia hili, nilihisi jinsi ilivyo tamu kuukana mwili na kutenda ukweli. Nilifahamu pia kwamba kutenda ukweli tu na kufuata kanuni ndiko kunakopatana na mapenzi ya Mungu. Hiyo ndiyo njia pekee yenye heshima.

Iliyotangulia: 52. Buriani, Mtu Mwenye Kujipendekeza

Inayofuata: 54. Vita vya Kiroho

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

54. Vita vya Kiroho

Na Yang Zhi, MarekaniMwenyezi Mungu anasema, “Tangu watu waanze kumwamini Mungu, wamekuwa na nia ambazo si sahihi. Wakati ambapo huweki...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp