223 Maisha ni ya Thamani

1

Mbingu zisizo na mipaka, kubwa na za kupendeza, za ajabu isiyo na mwisho.

Eh, watu waishio katika dunia hii, ni nani mnastahili kutii na kuabudu?

Mungu kuumba na kutawala vitu vyote kumejaa mafumbo.

Tunaweza kuona kila mahali ajabu ya matendo ya Mungu.

Kusonga kwa vitu hivi vyote ulimwenguni kumo mikononi mwa Mungu kabisa.

Baraka na bahati mbaya ya kudura ya mwanadamu haviwezi kuepuka udhibiti wa Mungu.

Maisha yanapita kwa haraka, lazima tuhakikishe roho zetu hazina majuto.

Mtu akiweza tu kumjua na kumpenda Mungu ndiyo maisha yetu yatakuwa na maana.

2

Baada ya kumwamini Mungu miaka mingi, naelewa ukweli, na hatimaye najua mapenzi Yake.

Amani ya roho huja tu kwa kuishi kwa neno la Mungu.

Tukipendana sisi kwa sisi, maisha yetu yanakuwa bora zaidi na zaidi.

Kumwabudu Mungu kwa moyo na ukweli kunaleta raha na uzima.

Kupitia hukumu, naelewa ukweli na kutambua upendo wa Mungu.

Nimeona sasa jinsi upotovu wangu ulivyo wa kina, kwamba sistahili hata kuitwa binadamu.

Ukweli ulioonyeshwa na Mungu unanionyesha njia ya uzima.

Kwa kumpenda Mungu kweli hatimaye naishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana.

3

Mungu kuonekana katika mwili na kufanya kazi ni nafasi ya kipekee.

Kupitia magumu na mateso ili kukamilishwa ni heshima kubwa zaidi.

Napitia hukumu Yake ili nitakaswe na kuishi kwa kudhihirisha mfano wa binadamu.

Kwa kuweka maneno ya Mungu katika vitendo na kuingia katika uhalisi, napata ukweli na uzima.

Kama viumbe walioumbwa, ni wajibu wa binadamu kumtii na kumwabudu Mungu.

Napata baraka za Mungu kwa kujitumia kwa ajili ya Mungu na kufuatilia ukweli.

Natimiza wajibu wangu, nakamilisha misheni yangu, nahubiri na kumshuhudia Mungu.

Kama naweza kupata kibali cha Mungu na kupatwa na Yeye, sitakuwa na majuto maishani tena.

Iliyotangulia: 222 Nimeona Uzuri wa Mungu

Inayofuata: 224 Nimekusudia Kumridhisha Mungu kwa Uaminifu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp