183 Ninatamani Kuona Siku ya Utukufu wa Mungu

1

Leo ninakubali hukumu na utakaso ya Mungu, kesho nitapokea baraka Zake.

Niko radhi kutoa ujana wangu na kutoa maisha yangu ili kuona siku ya utukufu wa Mungu.

Eh, upendo wa Mungu umeufurahisha moyo wangu.

Anafanya kazi na kuonyesha ukweli, akinipa maisha mapya.

Niko radhi kunywa kutoka kikombe cha dhiki na kuteseka ili kupata ukweli.

Nitastahimili fedheha bila malalamiko, ninatamani kuishi maisha yangu nikilipiza wema wa Mungu.

2

Nitampa Mungu upendo na uaminifu wangu na kukamilisha misheni yangu ya kumtukuza Mungu.

Nimeazimia kusimama imara katika ushuhuda kwa Mungu, na kamwe kutoshindwa na Shetani.

Eh, kichwa changu kinaweza kupasuka na damu kutiririka, lakini ujasiri wa watu wa Mungu hauwezi kupotea.

Ushawishi wa Mungu umo moyoni, ninaamua kumwaibisha Shetani Ibilisi.

Maumivu na shida vimeamuliwa kabla na Mungu, nitastahimili aibu ili kuwa mwaminifu Kwake.

Kamwe sitamsababisha Mungu alie au kusumbuka tena.

3

Maneno ya Mungu hunipa imani na uwezo, nitamfuata Mungu kwa uthabiti hadi mwisho.

Nitatangaza na kushuhudia injili ya Mungu siku zote hadi nife.

Eh, namsifu Mungu kwa furaha, na kumwimbia wimbo na dansi mpya.

Ninazungumza waziwazi kutoka moyoni, ninatoa uaminifu wangu kwa Mungu.

Moyo wangu utakuwa na Mungu daima. Siku ya utukufu wa Mungu itakapokuja,

tutakusanyika kandokando ya kiti cha enzi na kucheza kwa furaha, tutafurahia mapumziko ya milele katika mbingu mpya na nchi mpya.

Iliyotangulia: 182 Watakatifu Ni Washindi

Inayofuata: 184 Ufalme

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp