214 Ni Bahati Yetu Nzuri Kumhudumia Mungu

1

Tunasikia sauti ya Mungu

na kuthibitisha kuonekana na kazi ya Mungu.

Tunahisi msisimko sana kumwona Mungu wa vitendo uso kwa uso.

Tuna bahati sana kukaribisha kurudi kwa Bwana.

Ee! Kwa kuhudhuria sikukuu pamoja na Mungu,

tunainuliwa hadi katika ufalme wa mbinguni!

Kuanzia sasa kuendelea tutakula, kunywa na kufurahia maneno ya Mungu,

tunafurahia sana kuwa na Mungu.

Ee! Tuko tayari kufanya kazi kama wanyama wa mzigo kwa ajili ya Mungu

na kutii mipango na taratibu Zake.

Kwa mioyo yetu yote, tutamhudumia Mungu maisha yetu yote,

na tutasifu tabia ya Mungu yenye haki milele.

2

Tukitaka sana na kutamani kubarikiwa, tunakutana

na ufunuo na hukumu ya maneno ya Mungu.

Mioyo yetu inachomwa na upanga Wake

na tunahisi maumivu na uchungu mwingi.

Sisi ni wapotovu hatustahili kuuona uso wa Mungu.

Kwa kumwamini Mungu

ili kubarikiwa

na kuingia katika ufalme wa mbinguni pekee

Miaka mingi sana ya kutamani imepotea yote,

tunadhoofika katika maumivu na mioyo yetu imevunjika.

Maneno ya Mungu yanashinda mioyo yetu, tumeridhika kabisa,

na tunaanguka chini mbele Yake.

3

Ni kupitia hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu

pekee ndiyo tunaona jinsi ambavyo tumepotoshwa sana.

Tukiwa tumejawa nia na tamaa ya kubarikiwa,

tabia zetu potovu hazijatakaswa.

Si tu kwamba hatustahili kuingia katika ufalme wa mbinguni pekee,

kwa neema ya Mungu ndio tunahudumu.

Tuko tayari na ni bahati yetu nzuri.

Huu ndio upendo na baraka kubwa zaidi ya Mungu.

Ee! Tuko tayari kufanya kazi kama wanyama wa mzigo kwa ajili ya Mungu

na kutii mipango na taratibu Zake.

Kwa mioyo yetu yote, tutamhudumia Mungu maisha yetu yote,

na tutasifu tabia ya Mungu yenye haki milele.

Leo, tunaweza kumhudumia Mungu, na tunahisi kuwa hatustahili kabisa.

Hatujali ikiwa tutabarikiwa au tutakutana na maafa, wala hatujali hatima yetu itakuwa nini.

Mungu anamshinda Shetani kwa maneno Yake

na kutuokoa kutoka gizani.

Iliyotangulia: 213 Kufanya Upya Kiapo Changu cha Kumpenda Mungu

Inayofuata: 215 Sifa kwa Mungu Kutoka kwa Kizazi cha Moabu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp