75 Upendo wa Mungu Unaenea Duniani Kote

Mwenyezi Mungu, mtakatifu, mwenye haki.

Upendo Wako safi ni kama matone ya theluji inayopeperuka.

Safi, meupe na mazuri,

na harufu ya mbali, huelea na kuyeyuka juu yangu.

Sauti Yako huamsha,

neno Lako linagonga

kwenye moyo wangu.

Uso Wako mzuri

huufanya moyo wangu uhisi

karibu na Wewe zaidi!

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Maneno ya Mungu yana nguvu duniani!

Ufalme wa Kristo unakuja!

Upendo wa Mungu uko kila mahali,

kote ulimwenguni,

ukiipa joto mioyo ya mamilioni!

Ulimwengu umejaa sauti zinazomsifu Mungu.

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Tuna njaa na kiu ya kufurahia maneno Yako.

Tunaishi ndani ya maneno Yako,

ana kwa ana na Wewe, Mungu wetu.

Ukweli watuletea amani na mwanga!

Mwenyezi Mungu,

Wewe ndiwe ukweli, njia,

na uzima.

Maneno Yako

yenye thamani sana kwetu,

na mioyo yetu inayapenda!

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Maneno ya Mungu yana nguvu duniani!

Ufalme wa Kristo unakuja!

Upendo wa Mungu uko kila mahali,

kote ulimwenguni,

ukiipa joto mioyo ya mamilioni!

Ulimwengu umejaa sauti zinazomsifu Mungu.

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Hukumu na kuadibu husafisha upotovu wetu.

Tukijua ukweli tunayajali mapenzi Yako.

Majaribu, usafishaji, huufanya upendo wetu

Kwako uwe safi zaidi.

Tunaijua tabia Yako

na kuona jinsi unavyopendeka

Wewe.

Kila ninapokutii

Wewe na kukusifu,

furaha kamili huujaza moyo wangu.

Siwezi kuacha kukupenda,

na kamwe siwezi kukupenda vya kutosha.

Nitakuwa na Wewe usiku na mchana, kamwe kutokuwa mbali.

Katika majaribu na dhiki,

tunapitia upendo Wako kwa undani zaidi.

Maneno Yako yako pamoja nasi daima, si mbali kamwe.

Tunapitia saa ya giza zaidi kabla ya alfajiri

na kukaribisha ujio wa Jua la haki.

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Maneno ya Mungu yana nguvu duniani!

Ufalme wa Kristo unakuja!

Upendo wa Mungu uko kila mahali,

kote ulimwenguni,

ukiipa joto mioyo ya mamilioni!

Ulimwengu umejaa sauti zinazomsifu Mungu.

Watu wapya, nyimbo mpya, ngoma mpya, maisha mapya.

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Maisha yetu ni yenye furaha kamili na matamu!

Iliyotangulia: 74 Ee Mpendwa Wangu, Nakutafuta Wewe

Inayofuata: 76 Uhusiano na Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp