283 Mwishowe Naweza Kumpenda Mungu

1

Upendo Wako ni wa kweli na safi, Una moyo mwema na mwaminifu, na Ulikuwa mwili wa kuwaokoa wanadamu.

Naona kuwa unyenyekevu na usiri Wako ni wa kupendeza sana, naona jinsi Usivyoweza kupimika.

Nakufuata kwa ukaribu na woga; maneno Yako huniletea raha.

Unasimama nami katika ugumu, maneno Yako yaniongoza, kuniokoa na kunikamilisha.

Mwishowe naweza kukupenda, mchana na usiku mimi nipo na Wewe na naelewa mapenzi Yako.

Kuona uzuri Wako zaidi na zaidi, nakuja kukujua, Mwenyezi Mungu.

Uko pamoja nami, na nimepata mengi sana, nashangaa kwa uzuri kila wakati.

Unanipa upendo Wako wote, na wakati wangu na Wewe ni wa thamani sana.

2

Upendo Wako umeniamsha na kuuchochea moyo wangu, na natamani kukupenda na kuwa mwaminifu Kwako.

Unatumia neno Lako kunihukumu na kunitakasa, na Unaniokoa kutoka kwa ushawishi wa Shetani.

Nimefurahia upendo Wako mwingi sana, nimeelewa ukweli, na najua jinsi ya kuwa mwaminifu Kwako.

Uchungu na usafishaji hunileta karibu na Wewe na naahidi maisha yangu kuwa na ushuhuda mzuri wa kukutukuza Wewe.

Nimekufuata mpaka leo, nimepata riziki Yako ya ukweli, na barabara inakuwa angavu zaidi.

Kupita upendo Wako usio na mipaka, nakuja kukujua Mwenyezi Mungu.

Ni kwa neema Yako kwamba nimetakaswa na kuokolewa leo, sijui jinsi ya kukushukuru.

Kwa mwongozo Wako, naishi katika nuru, na napaswa kujitahidi hata zaidi katika ufuatiliaji wangu wa kukupenda.

Iliyotangulia: 282 Matamko Rasmi Juu ya Imani Katika Mungu

Inayofuata: 284 Kutembea kwenye Njia ya Kumpenda Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp