713 Sifa za Mabadiliko ya Tabia

1 Mabadiliko katika tabia yana sifa bainifu. Yaani, kuweza kukubali kile ambacho ni sahihi na kinacholingana na ukweli. Haijalishi ni nani anayekupa mapendekezo—awe ni kijana au mzee, iwe mnashirikiana vizuri, na iwe uhusiano kati yenu ni mzuri ama mbaya—alimradi anasema kitu kilicho sahihi na kinacholingana na ukweli, na chenye manufaa kwa kazi ya familia ya Mungu, basi unaweza kukisikiza, ukichukue na kukikubali, na usiathiriwe na mambo mengine yoyote. Hiki ndicho kipengele cha kwanza cha sifa hiyo bainifu. Kingine ni kuweza kutafuta ukweli wakati wowote unapokumbana na shida. Ukikumbana na shida mpya ambayo hakuna mtu anaweza kuielewa, unaweza kutafuta ukweli, uone ni nini unachopaswa kutenda ama kufanya ili kufanya jambo hilo lilingane na kanuni za ukweli, na kinatosheleza mahitaji ya Mungu.

2 Kipengele kingine ni kupata uwezo wa kufikiria mapenzi ya Mungu. Hili linategemea ni wajibu upi unatimiza na ni mahitaji yapi ambayo Mungu anayo kwako katika wajibu wako. Lazima uelewe kanuni hii. Tekeleza wajibu wako kulingana na kile ambacho Mungu anahitaji, na kitekeleze ili kumridhisha Mungu, na lazima uweze kutenda kwa uwajibikaji na uaminifu. Yote haya ni njia ya kufikiria mapenzi ya Mungu. Kama hujui jinsi ya kufikiria mapenzi ya Mungu katika jambo unalotenda, lazima ufanye utafutaji fulani ili kukamilisha hilo, na kumridhisha Yeye. Ikiwa mnaweza kuweka kanuni hizi tatu katika vitendo, mpime njia ambayo kwa kweli mnaishi kulingana nazo, na kupata njia ya kutenda, basi mtakuwa mnayashughulikia mambo kwa njia yenye maadili. Bila kujali unalokabiliana nalo na bila kujali ni shida gani unazoshughulikia, lazima utafute ni kanuni gani unazopaswa kutenda kulingana nazo. Mara utakapokuwa na ufahamu dhahiri wa vitu hivi, utaweza kutenda ukweli kwa urahisi.

Umetoholewa kutoka katika “Ni kwa Kuweka Ukweli Katika Vitendo Tu Ndipo Unaweza Kutupa Minyororo ya Tabia Potovu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 712 Maonyesho ya Wale Ambao Tabia Yao Imebadilika

Inayofuata: 714 Wale Walio na Mabadiliko ya Tabia Wanaweza Kuishi Kama Binadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp