226 Kile Ambacho Waumini Katika Mungu Wanapaswa Kutafuta

1 Nilimwamini Bwana kwa miaka mingi, nilieneza injili mara nyingi, lakini bado sikuweza kutoa ushuhuda kwa Mungu. Niliweza tu kuzungumza juu ya ushuhuda wa kufurahia neema Yake, lakini sikuweza kunena juu ya ufahamu wa kweli juu Yake. Lakini bado nilitamani kunyakuliwa hadi katika ufalme wa mbinguni Bwana atakaporudi. Ilikuwa mzaha kabisa! Kupitia hukumu mbele ya kiti cha Kristo kumenifanya nijute kabisa na kuhisi aibu. Imetukia kuwa sikujua cha kupata kutokana na kumwamini Mungu. Nilifanya tu kazi kwa raghba lakini sikuudhukuru moyo wa Mungu. Nilikuwa kama Paulo, kwa moyo mkunjufu ili kupata thawabu na taji. Baada ya kumwamini Mungu kwa miaka mingi bila kubadilisha tabia yangu, nahisi aibu kubwa. Kwani wokovu wote wa Mungu kwa wanadamu ni ili tupate uzima.

2 Hukumu ya Mungu imenifanya nione upendo na baraka za Mungu. Maneno ya Mungu yamefunua tabia yangu ya kishetani, na imeshughulikia asili yangu ya kiburi. Mwishowe nimeona kuwa nimepotoka sana na nina mfano mdogo wa kibinadamu. Ninapotekeleza wajibu wangu namaliza kwa kubahatisha, bila upendo halisi kwa Mungu. Nataka kushuhudia kwa Mungu na kulipa upendo Wake lakini sina nguvu. Nisipotia bidii bado katika kufuatilia ukweli, kufuata ukweli, maisha yangu yatamfedhehesha Mungu. Nimefanya uamuzi, ninaapa kutopumzika hadi nipate ukweli. Ili kupata ukweli, bila kujali nitateseka kiasi gani, kamwe sitakufa moyo, kamwe sitakufa moyo.

Iliyotangulia: 225 Nampa Mungu Upendo Wangu

Inayofuata: 227 Kupata Ukweli Kupitia Imani kwa Mungu Kuna Thamani Sana

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp