E. Juu ya Jinsi ya Kuwa Mtu Mwaminifu
384. Mnapaswa kujua kwamba Mungu anampenda binadamu mwaminifu. Mungu ana kiini cha uaminifu, na kwa hivyo neno Lake siku zote linaweza kuaminika. Aidha, matendo Yake hayana dosari wala hayatiliwi. Hii ndiyo maana Mungu anawapenda wale walio waaminifu kabisa Kwake. Uaminifu unamaanisha kumpa Mungu moyo wako; kutomdanganya kamwe katika kitu chochote; kuwa wazi Kwake katika mambo yote, kutowahi kuficha ukweli; kutowahi kufanya kile kinachowadanganya wale walio juu na kuwafumba macho wale walio chini; na kutowahi kufanya kile ambacho unajipendekeza tu mwenyewe kwa Mungu. Kwa ufupi, kuwa waaminifu ni kujizuia dhidi ya uchafu katika matendo na maneno yenu, na kutomdanganya Mungu wala binadamu. Kile Ninachoongea ni rahisi sana lakini ni kigumu maradufu kwenu. Watu wengi wanaona ni afadhali wahukumiwe kwenda kuzimu kuliko kunena na kutenda kwa uaminifu. Si ajabu kwamba Nina utendaji mwingine kwa wale ambao si waaminifu. Bila shaka, Ninaelewa ugumu mkubwa mnaokumbana nao kwa kuwa binadamu waaminifu. Ninyi nyote ni werevu sana na wastadi katika kuwapima watu kwa kipimo chenu kidogo; hii inafanya kazi Yangu iwe rahisi zaidi. Na kwa sababu nyinyi mnaficha siri katika mioyo yenu, basi, Nitawapeleka, mmoja baada ya mwingine, katika janga ili “mfundishwe” kwa moto, ili kwamba baada ya hapo mjitoe kikamilifu katika kuamini maneno Yangu. Hatimaye, Nitaondoa vinywani mwenu maneno “Mungu ni Mungu mwaminifu,” kisha ndipo mtakapojipiga vifua na kuomboleza, “Moyo wa mwanadamu ni mdanganyifu!” Je, hali za akili zenu zitakuwa vipi kwa wakati huu? Ninafikiri hamtakuwa na majivuno kama mlivyo sasa. Na hata hamtakuwa “wa kina sana kiasi cha kushindwa kueleweka” kama mlivyo sasa. Baadhi ya watu hutenda kwa ustaarabu na wanaonekana hasa “wana tabia nzuri” mbele za Mungu, lakini bado wanakuwa waasi na wasiojizuia mbele ya Roho Mtakatifu. Je, mnaweza kumhesabu binadamu kama huyu miongoni mwa wale walio waaminifu? Kama wewe ni mnafiki, mtu ambaye ni stadi katika “mahusiano baina ya watu,” basi Nasema kwamba bila shaka wewe ni mtu ambaye unajaribu kumchezea Mungu. Kama maneno yako yamejaa visingizio na uthibitisho usio na maana, basi Nasema kwamba wewe ni mtu ambaye unachukia kabisa kuuweka ukweli katika vitendo. Kama wewe una siri nyingi usizotaka kuzitoa, na kama hauko tayari kabisa kuziweka wazi siri zako—yaani, magumu yako—kwa wengine ili uweze kutafuta njia yenye mwanga, basi Ninasema kwamba wewe ni mtu ambaye hutapokea wokovu kwa urahisi na ambaye hutaweza kuibuka kutoka gizani kwa urahisi. Kama kutafuta njia ya kweli kunakupendeza sana, basi wewe ni mtu ambaye unakaa daima katika nuru. Kama wewe unafurahia kuwa mtenda-huduma katika nyumba ya Mungu, ukifanya kazi kwa bidii na kwa uangalifu bila kuonekana, daima ukitoa na kamwe usipokee, basi Nasema kwamba wewe ni mtakatifu mwaminifu, kwani hutafuti tuzo na unakuwa tu binadamu mwaminifu. Kama uko radhi kuwa wazi, kama uko radhi kutoa kila kitu ulichonacho, kama una uwezo wa kujitolea maisha yako kwa ajili ya Mungu na kuwa shahidi, kama wewe ni mwaminifu hadi kwa kiwango ambacho unajua tu kumridhisha Mungu na si kujifikiria au kuchukua chochote kwa ajili yako, basi Nasema kwamba watu kama hao ndio wanaostawishwa na mwangaza na wataishi milele katika ufalme.
Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maonyo Matatu
385. Nawathamini sana wale wasio na shaka kuhusu wengine na pia nawapenda sana wale wanaokubali ukweli kwa urahisi; kwa aina hizi mbili za wanadamu Ninaonyesha utunzaji mkubwa, kwani machoni Pangu wao ni waaminifu. Kama una udanganyifu mwingi, basi utakuwa na moyo wenye hadhari na mawazo ya shaka juu ya mambo yote na wanadamu wote. Kwa sababu hii, imani yako Kwangu inajengwa juu ya msingi wa mashaka. Imani kama hii ni moja ambayo kamwe Sitaitambua. Bila imani ya kweli, basi utakuwa mbali hata zaidi na upendo wa kweli. Na ikiwa unaweza kumshuku Mungu na kumkisia utakavyo, basi wewe bila shaka ni mdanganyifu zaidi kati ya wanadamu wengine. Mnakisia iwapo Mungu anaweza kuwa kama mwanadamu: mwenye dhambi isiyosameheka, mwenye tabia ndogondogo, anayependelea na asiye na mantiki, aliyekosa hisia ya haki, mwenye mbinu ovu, mdanganyifu na mjanja, na pia anayefurahishwa na uovu na giza, na kadhalika. Si sababu ambayo mwanadamu ana mawazo kama haya kwamba hana hata ufahamu mdogo wa Mungu? Imani kama hii ni sawa na dhambi! Zaidi ya hayo, kuna hata wale wanaoamini kwamba Sifurahishwi na yeyote isipokuwa wale wanaojirairai na kujipendekeza, na kwamba wale wasio na ujuzi huu hawatakaribishwa na watapoteza nafasi yao katika nyumba ya Mungu. Je, haya ndiyo maarifa ambayo mmepata kwa miaka hii yote mingi? Ni haya ndiyo mliyoyapata? Na ufahamu wenu kunihusu hauko kwa kutoelewa kama huku tu; mbaya hata zaidi ni kufuru yenu dhidi ya Roho wa Mungu na kuitukana Mbingu. Hii ndiyo maana Ninasema kwamba imani kama yenu itawasababisha tu kupotea mbali na Mimi na kuwa na upinzani mkubwa dhidi Yangu.
Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jinsi ya Kumjua Mungu Duniani
386. Leo, watu wengi wanaogopa sana kuyaleta matendo yao mbele za Mungu, na ingawa unaweza kuudanganya mwili wa Mungu, huwezi kumdanganya Roho wa Mungu. Yale yote ambayo hayawezi kustahimili uchunguzi wa Mungu hayakubaliani na ukweli nayo lazima yawekwe kando, ama unatenda dhambi dhidi ya Mungu. Kwa hivyo, haijalishi kama ni wakati unaomba, unaponena na kushiriki na ndugu na dada zako, ama unapofanya wajibu wako na kufanya biashara yako, lazima uuweke moyo wako mbele za Mungu. Unapoitimiza kazi yako, Mungu yuko nawe, na bora nia yako iwe sawa, nayo iwe kwa ajili ya kazi ya nyumba ya Mungu, Atakubali kila kitu ufanyacho, kwa hivyo ni lazima uweke bidii kwa dhati kujishughulisha na kuitimiza kazi yako. Unapoomba, kama una upendo kwa Mungu katika moyo wako, na kama unatafuta utunzaji wa Mungu, ulinzi, na uchunguzi, kama haya ndio nia yako, maombi yako yatafaulu. Kwa mfano, unapoomba kwenye mikutano, ikiwa utafungua moyo wako na kumwomba Mungu na kumwambia yaliyomo moyoni mwako bila kusema uwongo, basi maombi yako hakika yatakuwa na matokeo. …
Kuwa muumini katika Mungu kunamaanisha kuwa kila kitu ufanyacho lazima kiletwe mbele za Mungu na kupitia uchunguzi wa Mungu. Kama kile ufanyacho kinaweza kuletwa mbele za Roho wa Mungu lakini sio mbele ya mwili wa Mungu, hii inadhibitisha kuwa hujajitiisha katika uchunguzi wa Roho wa Mungu. Roho wa Mungu ni nani? Mtu huyu aliyeshuhudiwa na Mungu ni nani? Je, Wote si sawa? Wengi Huwaona kama nafsi mbili tofauti, wakiamini kwamba Roho wa Mungu ni Roho wa Mungu, naye mtu anayeshuhudiwa na Mungu ni binadamu tu. Lakini, je, hujakosea? Je, mtu huyu anafanya kazi kwa niaba ya nani? Wale ambao hawaujui mwili wa Mungu hawana uelewa wa kiroho. Roho wa Mungu na mwili Wake ni mmoja, kwa sababu Roho wa Mungu anatokea kwa mwili. Kama mtu huyu si mwema kwako, Roho wa Mungu Atakuwa mwema? Ni nini kimekuchanganya? Leo, hakuna asiyekubali uchunguzi wa Mungu anaweza kupokea idhini ya Mungu, na yeyote asiyemjua Mungu mwenye mwili hawezi kukamilishwa. Jiangalie nawe ujiulize kama kila kitu unachofanya kinaweza kuletwa mbele za Mungu. Iwapo huwezi kuleta kila kitu unachofanya mbele za Mungu, hii inaonyesha kuwa wewe ni mtenda maovu. Je, watenda maovu wanaweza kufanywa wakamilifu? Kila kitu unachofanya, kila tendo, kila nia, na kila jibu lazima kiletwe mbele za Mungu. Hata maisha yako ya kawaida ya kiroho—maombi yako, ukaribu wako kwa Mungu, jinsi unavyokula na kunywa maneno ya Mungu, ushirika wako na kina ndugu zako na maisha yako ndani ya kanisa—na huduma yako katika ushirikiano wako vinaweza kuletwa mbele za Mungu ili Yeye avichunguze. Ni matendo kama hayo ndiyo yatakayokusaidia kustawi katika maisha. Mchakato wa kukubali uchunguzi wa Mungu ni mchakato wa kutakaswa. Kadri unavyoukubali uchunguzi wa Mungu, ndivyo unavyotakaswa zaidi na kadri unavyokubaliana na matakwa ya Mungu, ili kwamba hutajipata katika ufisadi, na moyo wako utaishi katika uwepo wa Mungu; kadri unavyokubali uchunguzi wa Mungu, ndivyo unavyomuaibisha Shetani na kuutelekeza mwili. Kwa hivyo, kukubali uchunguzi wa Mungu ni njia ambayo watu wanafaa kutenda. Haijalishi kile unachokifanya, hata katika ushirika na ndugu na dada zako, ukiyaleta matendo yako mbele za Mungu na kutafuta uchunguzi wa Mungu, na kama nia yako ni kumtii Mungu Mwenyewe, unachotenda ni sahihi zaidi. Kama tu wewe ni mtu anayeleta kila kitu unachofanya mbele za Mungu na kukubali uchunguzi wa Mungu ndipo utakapokuwa mtu anayeishi kwa hakika katika uwepo wa Mungu.
Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Anawakamilisha Wale Wanaoupendeza Moyo Wake
387. Kuwa mwaminifu, lazima kwanza uuweke wazi moyo wako ili kila mtu aweze kuuona moyo wako, kuona vyote unavyofikiri, na kuuona uso wako wa kweli; hupaswi kujifanya ama kujaribu kujificha. Hapo tu ndipo watu watakuamini na kukuchukua kuwa mwaminifu. Hili ndilo tendo la msingi kabisa, na sharti, la kuwa mwaminifu. Unaonyesha taswira ya uongo kwa watu, ili waamini kwamba wewe ni mwadilifu, mkuu, anayejitolea, asiyependelea na asiye na ubinafsi. Huu ni udanganyifu. Usijifanye na usijionyeshe usivyo; badala yake, jiweke wazi na uweke wazi moyo wako ili wengine waone. Iwapo unaweza kuweka wazi moyo wako ili wengine waone, na kuweka wazi yote unayofikiri na kupanga kufanya ndani ya moyo wako—bila kujali iwapo ni nzuri ama mbaya—basi wewe huwi mwaminifu? Iwapo unaweza kujiweka wazi kwa wengine waone, Mungu pia atakuona, na kusema: “Umejiweka wazi kwa wengine wakuone, na hivyo mbele Yangu bila shaka wewe ni mwaminifu pia.” Iwapo unajiweka wazi kwa Mungu wakati wengine hawaoni pekee, na daima unajifanya kuwa mkuu na mwadilifu ama mwenye haki na asiye na ubinafsi mbele yao, basi Mungu atafikiri nini na Mungu atasema nini? Mungu atasema: “Kwa kweli wewe ni mdanganyifu, wewe ni nafiki kabisa na anayejishughulisha na mambo madogo madogo, na wewe si mwaminifu.” Mungu atakuhukumu hivi. Iwapo unataka kuwa mwaminifu, basi bila kujali kile unachofanya mbele ya Mungu ama watu, unapaswa kuweza kuufungua moyo wako na kujiweka wazi.
Neno, Vol. 3. Mihadhara ya Kristo wa Siku za Mwisho. Vitendo vya Msingi Kabisa vya Kuwa Mtu Mwaminifu
388. Hatima zenu na majaliwa yenu ni muhimu sana kwenu—zina umuhimu mkubwa sana. Mnaamini kuwa msipofanya mambo kwa uangalifu sana, itakuwa sawa na kutokuwa na hatima, na uharibifu wa majaliwa yenu. Lakini mmewahi kufikiri kwamba kama juhudi ambazo mtu anatumia, ni kwa ajili tu ya hatima zao wenyewe, hizo zitakuwa tu ni kazi zisizo na matunda? Juhudi kama hizo si za kweli—ni bandia na danganyifu. Kama ni hivyo, wale ambao wanafanya kazi kwa ajili ya hatima zao watapokea maangamizo yao ya mwisho, kwa sababu kushindwa kwa imani za watu katika Mungu kumesababishwa na udanganyifu. Hapo awali Nilisema kwamba Sipendi kubembelezwa au kusifiwa kinafiki, au kutendewa kwa shauku kubwa. Ninapenda watu waaminifu ili wakabiliane na ukweli na matarajio Yangu. Hata zaidi, Ninapenda wakati watu wanapoweza kuonyesha uangalifu mkubwa na kuujali moyo Wangu, na wakati wanapoweza hata kuacha kila kitu kwa ajili Yangu. Ni kwa njia hii tu ndipo Moyo wangu utaweza kufarijiwa.
Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Juu ya Hatima
389. Watu wakitafuta kuwa waaminifu tu ndiyo wanaweza kujua jinsi walivyopotoka kwa kina na kujua iwapo wana mfano wowote wa binadamu au la; ni wakati tu wanapokuwa wakitenda uaminifu ndipo wanaweza kugundua ni kiasi gani cha uwongo ndicho wao husema na jinsi udanganyifu na uongo wao ulivyojificha sana. Ni wakati tu wanapopitia kitendo cha kuwa waaminifu ndipo watu wanaweza kuja kujua ukweli wa upotovu wao wenyewe na kutambua kiini asili chao, na ni wakati huo tu ndipo tabia zao potovu zinaweza kutakaswa kila wakati. Tabia zao potovu zikitakaswa mara kwa mara tu ndipo watu wataweza kupata ukweli. Chukua muda wako kupitia maneno haya. Mungu hawakamilishi wale walio wadanganyifu. Ikiwa moyo wako si mwaminifu, ikiwa wewe si mtu mwaminifu, basi Mungu hatakupata kamwe. Wewe, pia, hutapata ukweli kamwe, na hutakuwa na uwezo wa kumpata Mungu. Kama huwezi kumpata Mungu, na huelewi ukweli, basi inamaanisha kwamba wewe ni wa uhasama kwa Mungu, hulingani na Mungu, na Yeye si Mungu wako. Na kama Mungu sio Mungu wako, huwezi kupata wokovu. Kama huwezi kupata wokovu, wewe utakuwa adui mkubwa wa Mungu milele, na matokeo yako yameamuliwa. Kwa hivyo, ikiwa watu wanataka kuokolewa, basi lazima waanze kwa kuwa waaminifu. Kuna ishara inayowaonyesha wale ambao mwishowe watapatwa na Mungu. Je, unajua ishara hiyo ni nini? Imeandikwa katika Ufunuo, katika Biblia: “Na katika vinywa vyao haukuonekana uongo wowote; hawana mawaa.” “Hawa” wanaotajwa ni akina nani? Ni wale ambao wanaokamilishwa na kupatwa na Mungu, na kuokolewa. Je, Mungu anawaelezaje watu hawa? Je, sifa na maonyesho ya matendo yao zipi? (Wao hawana mawaa. Hawasemi uwongo). Nyote mnapaswa kuelewa na kufahamu maana ya kutosema uongo: Inamaanisha kuwa mwaminifu. Maana ya kuwa bila mawaa ni nini? Je, Mungu anamfafanuaje mtu asiye na mawaa? Wale wasio na mawaa wanaweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu; wao ndio wanaweza kukaa katika njia ya Mungu. Watu kama hao ni wakamilifu machoni pa Mungu; hawana mawaa.
Neno, Vol. 3. Mihadhara ya Kristo wa Siku za Mwisho. Ishara Sita za Ukuaji katika Maisha
390. Unapaswa kujua kama una imani ya kweli na uaminifu wa kweli ndani yako, kama una rekodi ya kuteseka kwa ajili ya Mungu, na kama umemtii Mungu kikamilifu. Kama unakosa hivi Nilivyotaja, basi ndani yako kunasalia uasi, udanganyifu, ulafi, na malalamiko. Kwa vile moyo wako uko mbali na uaminifu, hujawahi kupokea idhinisho kutoka kwa Mungu na hujawahi kuishi katika nuru. Jinsi ambavyo hatima ya mtu itakuwa mwishoni inategemea kama wana moyo wenye uaminifu na wa kweli, na ikiwa wana nafsi safi. Kama wewe ni mtu ambaye si mwaminifu kabisa, ni mtu mwenye moyo muovu, mwenye nafsi isiyo safi, basi una uhakika wa kuishia mahali ambapo mwanadamu anaadhibiwa, kama ilivyoandikwa katika rekodi ya majaliwa yako. Kama unadai kwamba wewe ni mwaminifu sana, na bado kamwe hutendi kulingana na ukweli au kuongea neno la kweli, hivyo je, bado unatarajia Mungu akupe thawabu? Je, bado unatumaini kwamba Mungu atakuchukulia kama mboni ya jicho Lake? Je, mawazo kama hayo si ya kipumbavu? Unamdanganya Mungu katika mambo yote, hivyo nyumba ya Mungu inawezaje kumpa nafasi mtu kama wewe, ambaye mikono yake si safi?
Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maonyo Matatu