30 Mafumbo Yote Yamefunuliwa

1 Mwenyezi Mungu mwenye haki—mwenye Uweza! Ndani Yako hakuna chochote kabisa kilichofichwa. Kila fumbo tangu zamani hadi milele, ambalo halijawahi kufumbuliwa na binadamu, ndani Yako linadhihirika na kwa jumla kuwa wazi. Hatuhitaji tena kutafuta na kupapasa, kwa maana leo nafsi Yako inadhihirika wazi kwetu, Wewe ndiye fumbo ambalo limefichuliwa, Wewe ni Mungu wa vitendo Mwenyewe; kwa kuwa leo Umekuja uso kwa uso na sisi, na tuionapo nafsi Yako, tunaona kila fumbo la ulimwengu wa kiroho.

2 Kweli hiki ni kitu ambacho hakuna mtu angeweza kuwaza! Wewe uko miongoni mwetu leo, hata ndani yetu, karibu sana nasi; haliwezi kuelezeka! Fumbo lililo ndani ya hili ni lisilo na kifani! Mwenyezi Mungu amekamilisha mpango Wake wa usimamizi. Yeye ndiye Mfalme mshindi wa ulimwengu. Vitu vyote na mambo yote yanadhibitiwa mikononi Mwake. Watu wote wanapiga magoti katika ibada, wakiliita jina la Mungu wa kweli—Mwenyezi. Kwa maneno kutoka katika kinywa Chake, mambo yote yanafanyika.

Umetoholewa kutoka katika “Sura ya 47” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 29 Neno la Mwenyezi Mungu Latimiza Kila Kitu

Inayofuata: 31 Hukumu ya Mungu kwa Mataifa na Watu Wote

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp