477 Yachukulie Maneno ya Mungu kama Msingi wa Matendo Yako

1 Natumai tu kwamba hamtapoteza juhudi Zangu zenye kujitahidi na zaidi ya hayo, kwamba mnaweza kuelewa utunzaji wote na fikira ambazo Nimetumia, mkiyachukulia maneno Yangu kama msingi wa jinsi mnavyotenda kama binadamu. Iwe ni maneno ambayo mko tayari kuyasikiliza au la, iwe ni maneno ambayo mnafurahia kuyakubali au mnayakubali bila raha, lazima muyachukulie kwa uzito. Vinginevyo, tabia na mielekeo yenu isiyokuwa ya kujali itanifadhaisha Mimi kweli na hata zaidi, kuniudhi.

2 Natumai sana kwamba nyote mnaweza kuyasoma maneno Yangu tena na tena—mara elfu kadhaa—na hata kuyakariri. Ni kwa namna hiyo tu ndiyo hamtayaacha matarajio Yangu kwa ajili yenu. Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishi hivi sasa. Hata, nyote mmezama katika maisha fisadi ya kula na kunywa hadi kushiba, na hakuna yeyote kati yenu anayeyatumia maneno Yangu kuusitawisha moyo na nafsi yake. Kwa sababu hii ndiyo Nimehitimisha kuhusu uso wa kweli wa mwanadamu: Mwandamu anayeweza kunisaliti wakati wowote, na hakuna yeyote anayeweza kuwa mwaminifu kabisa kwa maneno Yangu.

Umetoholewa kutoka katika “Tatizo Zito Sana: Usaliti (1)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 476 Kile Vijana Hawana Budi Kufuatilia

Inayofuata: 478 Jinsi ya Kuyachukulia Maneno ya Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp