2 Wimbo Wa Ufalme
(II) Mungu Amekuja, Mungu Ni Mfalme

1

Katika wakati huu mzuri, katika wakati huu wa kusisimua,

sifa zinasikika kila mahali, juu mbinguni na chini duniani. Nani asingesisimka kwa ajili ya hili?

Ni moyo wa nani usingechamka? Ni nani asingelia kwa sababu ya tukio hili?

Anga si anga ya zamani, sasa ni anga ya ufalme.

Dunia si dunia ya awali, sasa ni nchi takatifu.

Baada ya mvua kubwa kupita, ulimwengu mchafu wa kale unafanywa upya kabisa.

2

Milima inabadilika … maji yanabadilika …

watu pia wanabadilika … vitu vyote vinabadilika….

Aa, milima iliyo mitulivu! Inukeni na mnichezee!

Aa, maji yaliyotuama! Endeleni kutiririka kwa wingi!

Ninyi wanadamu mnaoota ndoto! Jiinueni na mfuate!

Nimekuja … Mimi ni mfalme….

Wanadamu wote watauona uso Wangu kwa macho yao wenyewe, wataisikia sauti Yangu kwa masikio yao wenyewe,

watafurahia wenyewe maisha katika ufalme….

Matamu sana… mazuri sana….

Yasiyosahaulika … yasiyoweza kusahaulika….

3

Katika mwako wa hasira Yangu, joka kubwa jekundu linapambana;

katika hukumu Yangu adhimu, pepo wanaonyesha sura zao za kweli;

kwa maneno Yangu makali, watu wote wanaona aibu sana, na hawana popote pa kujificha.

Wanakumbuka zamani, jinsi walivyonidhihaki na kunikejeli.

Hakukuwahi kuwa na wakati ambapo hawakujiringa, hakukuwa kamwe na wakati ambapo hawakuniasi.

Leo, nani halii? Nani hahisi majuto?

Ulimwengu dunia wote umejawa machozi …

umejaa sauti za kushangilia … umejaa sauti za vicheko….

Furaha isiyoweza kufananishwa … furaha isiyo na kifani….

4

Mvua nyepesi inatarakanya … theluji nzito inaanguka….

Ndani ya watu, huzuni na furaha zinachanganyika … baadhi wakicheka …

baadhi wakilia … na baadhi wakishangilia….

Kana kwamba watu wote wamesahau … ikiwa haya ni majira ya kuchipua yaliyojaa mvua na mawingu,

majira ya joto yenye maua yanayochanua, majira ya kupukutika kwa majani yenye mavuno mengi,

au majira ya baridi yaliyo baridi kama barafu na jalidi, hakuna anayejua….

Angani mawingu yanaenda pepe, duniani bahari zinavurugwa.

Wana wanapunga mikono yao … watu wanasogeza miguu yao wakicheza….

Malaika wanafanya kazi … malaika wanachunga….

Watu wote duniani wanashughulika, na vitu vyote duniani vinazidishwa.

Umetoholewa kutoka katika “Wimbo wa Ufalme” ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 1 Wimbo wa Ufalme
(I) Ufalme Unashuka Duniani

Inayofuata: 3 Wimbo wa Ufalme
(III) Watu Wote, Pigeni Kelele za Furaha

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp