9 Ufalme Wenye Haki wa Kristo Umetimia

Watu wa Mungu wamwimbia sifa,

kwa maana ufalme Wake umetimia.

Umeme umeangaza kutoka Mashariki hadi Magharibi,

na Mwana wa Adamu ameshuka duniani.

Kristo wa siku za mwisho ameonyesha ukweli,

na hili ndilo Neno kuonekana katika mwili.

Hukumu ya siku za mwisho

tayari imeanza na nyumba ya Mungu,

na ukweli utafunua watu wote duniani.

Mwenyezi Mungu anatawala na kuujaza ulimwengu wote

kwa haki na uadilifu.

Ufalme wenye haki wa Kristo

umetimia kikamilifu duniani.

Watu wote wa Mungu wanaimba

katika kumsifu mpaka milele.

Hakuna anayeweza kuepuka hukumu ya Mungu yenye haki.

Wabaya wote na wale wasioamini,

watasafishwa kupitia ugumu, majaribu na uchungu.

Lakini watu wa Mungu wanakubali hukumu na kuadibu.

Upotovu wao unatakaswa, na kupitia ugumu wote

ni waaminifu kwa Mungu hata hadi hatua ya kufa.

wanamfuata Kristo kwa uthabiti.

Mwenyezi Mungu anatawala na kuujaza ulimwengu wote

kwa haki na uadilifu.

Ufalme wenye haki wa Kristo

umetimia kikamilifu duniani.

Watu wote wa Mungu wanaimba

katika kumsifu mpaka milele.

Mungu amemshinda Shetani

na kuunda kundi la washindi.

Wote wampendao Mungu kweli

hakika watatembea katika nuru Yake.

Vigelegele vinasikika kwa ajili ya ufalme wa Kristo,

na ngurumo saba zinatikisa mbingu na dunia.

Nguvu ya kazi ya Mungu ni kuu na pana.

Hakuna chochote wala yeyote anayeweza kuidhibiti.

Maafa makubwa yatawaangamiza binadamu wote waovu,

na yatafichua jinsi Mungu alivyo mwenye haki, na jinsi Alivyo mtakatifu.

Mwenyezi Mungu anatawala na kuujaza ulimwengu wote

kwa haki na uadilifu.

Ufalme wenye haki wa Kristo

umetimia kikamilifu duniani.

Watu wote wa Mungu wanaimba

katika kumsifu mpaka milele.

Mapenzi ya Mungu yanafanyika duniani,

joka kubwa jekundu linaangamizwa.

Maneno ya Mungu yanaenea kote ulimwenguni,

yakiyatikisa mataifa na nchi zote.

Yote yanabadilishwa kupitia maneno ya Mungu mwenyewe,

dunia na mbingu zimeibuka.

Usimamizi wa Mungu ulifanikiwa,

mwishowe Amepata utukufu wote.

Ufalme wa Kristo umetimia.

Iliyotangulia: 8 Ufalme wa Kristo Umeshuka Duniani

Inayofuata: 10 Ufalme Wa Kristo Unapatikana Miongoni mwa Wanadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp