658 Imani ya Kweli ni Nini?

1 Je, neno hili “imani”, linarejelea nini? Imani ni kusadiki kwa kweli na moyo wa dhati ambao wanadamu wanapaswa kumiliki wakati wao hawawezi kuona au kugusa kitu, wakati kazi ya Mungu haiambatani na za binadamu, wakati inazidi uwezo wa binadamu. Hii ndiyo imani Ninayozungumzia. Watu wanahitaji imani katika nyakati za shida na usafishaji, na imani ni kitu kinachofuatwa na usafishaji; usafishaji na imani haviwezi kutenganishwa. Haijalishi jinsi Mungu anavyofanya kazi, na haijalishi mazingira uliyomo, unaweza kufuatilia maisha na kutafuta ukweli, na kutafuta maarifa ya kazi ya Mungu, na kuwa na ufahamu wa matendo Yake, na unaweza kutenda kulingana na ukweli. Kufanya hivi ndiko kuwa na imani ya kweli, na kufanya hivyo kunaonyesha kwamba hujapoteza imani katika Mungu.

2 Unaweza tu kuwa na imani ya kweli katika Mungu ikiwa bado unaweza kuendelea kufuatilia ukweli kupitia ukiwa katika usafishaji, ikiwa unaweza kumpenda Mungu kwa kweli na huna na mashaka kumhusu Yeye, ikiwa bila kujali Anachokifanya bado unatenda ukweli kumridhisha Yeye, na ikiwa unaweza kutafuta kwa dhati mapenzi Yake na ujali mapenzi Yake. Zamani, wakati Mungu alisema kwamba ungetawala kama mfalme, ulimpenda, na wakati Alijionyesha hadharani kwako, ulimfuata. Lakini sasa Mungu amejificha, huwezi kumwona, na shida zimekujia—je, hapo unapoteza matumaini kwa Mungu? Hivyo, lazima ufuatilie uzima wakati wote na kutafuta kuyaridhisha mapenzi ya Mungu. Hii inaitwa imani ya kweli, na huu ndio aina ya upendo ulio wa kweli na mzuri zaidi.

Umetoholewa kutoka katika “Wale Wanaopaswa Kukamilishwa Lazima Wapitie Usafishaji” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 657 Majaribu Yanahitaji Imani

Inayofuata: 659 Wale Wanaoshuhudia Katika Taabu ni Washindi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp