Kujijua kwa Hakika kwa Kuuelewa Ukweli Tu

15/01/2018

Wenwen Mji wa Changchun, Mkoa wa Jilin

Kwa maoni yangu, daima nililidhani kwamba mradi matendo ya nje yalionekana ya kufaa ambapo watu hawangeweza kuona upotovu wowote, basi lilichukuliwa kuwa mabadiliko. Kwa hiyo, nilizingatia kwa namna ya kipekee matendo ya nje katika kila kitu nilichokifanya. Nilijali tu kuhusu kama matendo yangu yalikuwa sahihi au la, na mradi tabia zangu za nje na matendo yalikuwa ya maana, nilikuwa sawa. Nilipokabiliwa na upogolewaji, nilijali tu kama kulikuwa na kitu kibaya na matendo yangu. Ningeridhishwa tu kama ningekanushwa katika matendo yangu. Singekubali mawasiliano zaidi kuhusu kutambua asili yangu potovu. Baadaye, ndugu wa kike na wa kiume waliniambia kwamba mtu anaweza tu kubadilisha tabia yake kwa kujua asili yake, na kuwa sikuwa nimejua asili yangu. Baada ya kusikiliza maneno ya ndugu wa kike na wa kiume, nilianza kujifunza kutambua asili yangu. Mtu fulani aliposema, “maonyesho haya ya kuringa yanatawaliwa na asili ya kiburi chako,” kisha nikasema, “Aa, mimi si mwenye kiburi, asili yangu ni yenye kiburi!” Mtu mwingine akasema, “tabia hii isiyo ya kawaida na isiyozuiwa inatawaliwa na asili yako mbovu ya kibinadamu.” Kisha nikaendelea, “Aa, asili yangu mbovu.” Sikufikiri ilikuwa vigumu kujua asili yangu mradi nilirudia aina zipi za asili zinatawala tabia hizi mtawalia. Kama mtu aliniuliza, “Hii tabia inatawaliwa na asili gani?” Kisha nikasema, “Ni majisifu, uovu, ubaya, ujanja….” Aina hii ya kuuliza na kujibu ilikuwa kama kujaza nafasi zilizoachwa wazi, ambayo ilionekana rahisi sana. Ilibainika kuwa hawa ndugu wa kike na wa kiume waliniambia kuwa nilijua asili yangu kwa kiwango cha juu juu. Kwa hiyo, katika kuzungumza baadaye kuhusu kujitambua, nilisema, “Mimi ni mwenye kiburi mno, na bila mipaka. Mimi ni mwovu mno, na pia mwenye makosa mno.” Nilifikiri kwamba kuongeza “mno” kwa utambuzi wangu wa awali kungeongeza ufahamu wangu. Sikuelewa juu ya maana ya mahitaji ya Mungu kwa watu kutambua asili zao, kwa hiyo, nilipofichua upotovu au wakati nilipoona maneno ya Mungu yaliyofichuliwa kuhusu asili ya binadamu, nililielewa tu kutoka kwa mtazamo wa kufuata kanuni; nilikuwa sana kama kasuku, kurudia maneno kuhusu kujitambua badala ya kweli kuelewa na kujua kutoka kwa moyo wangu. Sikujichukia, wala kuhisi jinsi ilivyokuwa hatari. Hata kwa kusikia maneno makali kutoka kwa Mungu, sikuhisi kushtuka. Badala yake, halikunisumbua, hali ambayo ilisababisha mabadiliko kidogo katika tabia yangu. Ingawa mimi ni mpumbavu, mwenye ganzi, na duni katika ubora, Mungu hanitengi, lakini badala yake, Yeye huniongoza na kuninurisha daima, akiniongoza kujua asili na kiini changu na kupata njia ya kubadili tabia yangu.

Siku chache zilizopita, mimi na ndugu mmoja tulihamia kwa familia mwenyeji mpya. Tulipowasiliana baada ya kuhamia huko, dada mzee katika familia mwenyeji akataja jinsi ndugu wa kiume na wa kike aliokuwa amezoea kuwakaribisha walivyofichua upotovu; pia alizungumzia maoni yake juu yao. Baada ya kusikiliza, sikujibu au kuathiriwa na jambo hilo, na sikuwasiliana ukweli kwa dada huyu mzee. Hivi ndivyo muda ulivyopita. Baada ya siku kadhaa, ndugu wengine wawili wa kiume ambao walifanya kazi na sisi walikuja kwetu kwa malazi kwa muda wa siku kadhaa. Baada ya wao kuondoka, dada huyu mzee aliongea nasi juu ya maoni yake ya ndugu hawa wawili, na kwa wakati huo, mawazo yangu yalionyesha hisia: Mengi ya yale uliyoyasema hayaambatani na ukweli; hii yote ni shaka yako. Mungu huhitaji kwamba ndugu wa kiume na wa kike wapendane na wasaidiane. Ni lazima nitende ukweli na kupitisha ukweli wa kuwa mwaminifu na wewe. Siku mbili baada ya mawasiliano yetu, dada mzee alikuja na kuniambia sentensi gani zangu ambazo zilikuwa zimemzuia, na ni mambo gani niliyoyafanya yaliyomzuia. Alizungumzia mawazo yake yote na kulia. Kuona hili, nilifikiri: Wewe ni mwenye shaka kabisa kumhusu kila mtu. Wakati huu una shaka na mimi. Hili si sawa. Nahitaji kuwasiliana na wewe kwa dhahiri ili usiwe na dhuluma dhidi yangu. Kwa hiyo, nilikuwa na majadiliano ya wazi naye, na kulenga asili aliyoonyesha pamoja na tabia zake za tuhuma na hukumu. Yule dada mzee alionekana kulikubali, lakini yeye hakuridhishwa kwa ndani. Katika siku zilizofuata, yeye alidai kuwa na aina hii na aina ile ya ugonjwa. Kuona hili, nilifikiri: Wewe hujaridhika ndani, bali unajifanya kulikubali; si huku ni kujifanya na udanganyifu? Kuna mafundisho ya kujifunza wakati mtu ni mgonjwa. Lazima ujichungue kiasi, kwa kuwa umekuwa katika magonjwa yasiosita. Katika kuwaza hili, nilipokea “mzigo” mwingine, jambo lililonielekeza kuwasiliana na huyo dada mzee tena. Nilimwambia ajichungue kiasi na kujijua mwenyewe. Hata hivyo, katika mawasiliano haya, huyu dada mzee hakuonekana mzima. Hata hakujifanya kukubali hilo. Nilipigwa na bumbuazi, na kufikiri: nimekuwa mwangalizi sana katika kukusaidia na nimewasiliana nawe tena na tena, lakini hulikubali na hata umekuwa mwenye shaka nami. Wewe ni mtu asiye mwaminifu! Kama hukubali ukweli, ni nani mwingine angeweza kukusaidia? Lisahau hilo, siwezi kufanya lolote, ni juu yako. Nilisukuma lawama zote na wajibu kwa dada mzee nikifikiri kwamba alikuwa mjanja mno; niliamini kuwa nilikuwa ndugu mzuri ambaye alitenda ukweli, ambaye alikuwa na nia ya kuwasaidia ndugu zangu wa kiume na wa kike na ambaye aliyajali mapenzi ya Mungu. Kwa njia hii, nilikuwa nimejawa na dhana za dada mzee, na yeye hangenisikiliza tena.

Katika kukakabili mtanziko huu, ilibidi kujichungua binafsi kiasi: Je, nina makosa? Sikuwa na makosa kwa kumsaidia dada mzee kwa huruma nilipoona dosari zake. Je, ni kwa sababu sikumtegemea Mungu? Sivyo, niliomba kila wakati kabla ya kuwasiliana na dada mzee. Sijafanya kitu kibaya katika matendo yangu, na sijakuwa katika hali nzito kama hii nikiwasaidia wengine wakati wa nyuma. Tatizo lazima liwe kwa dada mzee na ni kwa sababu yeye si maasumu. Hata hivyo, wakati nikifikiria kwa njia hii, nilijihisi kuvurugika. Nilijihisi mwenye hatia hasa wakati nikimwona dada mzee akiugua kutokana na ugonjwa wake. Nilitaka kumsaidia kwa dhati, hata hivyo, sikujua jinsi ya kushirikiana naye. Bila kuwa na uchaguzi, nilikuja kwa Mungu na kutaka msaada Wake. Nilisoma maneno ya Mungu, “Midomo yako ni mikarimu zaidi kuliko njiwa, lakini moyo wako ni mwovu zaidi kuliko yule nyoka wa zamani. Midomo yako ni ya kupendeza hata kama wanawake wa Lebanoni, lakini moyo wako si mwema zaidi kuliko yao, na hakika hauwezi kulinganishwa na uzuri wa Wakanaani. Moyo wako ni mdanganyifu mno!(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ninyi Nyote Ni Waovu Sana Katika Tabia!). Maneno hayo kutoka kwa Mungu mara moja yakagusa moyo wangu. Singekuwa na budi kuchungua kile nilichokuwa nimefanya siku hizo na mawazo yaliyokuwa msingi wake. Nilipokuwa nikisikia dada mzee akiongea juu ya hukumu yake kwa ndugu wengine wa kiume na wa kike, sikujibu kwa sababu nilifikiri lilikuwa halinihusu ndewe wala sikio na halingenizuia; wakati nikisikia dada mzee akizungumzia chuki yake bila sababu ya ndugu wawili wa kiume niliowajua, singesubiri kuwasiliana naye iwapo aliwaelewa visivyo; niliposikia kwamba dada mzee alikuwa na maoni juu ya kile nilichokuwa nimesema na kufanya, nilizingatia zaidi kuwasiliana naye iwapo alikuwa na maoni yoyote kunihusu. Nilidai kwamba nilikuwa nikiwasaidia ndugu zangu wa kike na wa kiume kwa ajili ya huruma kwao. Ukweli ni kwamba nilitaka kumshawishi na kuwashinda wengine na ukweli, kuifunga midomo yao, na kuzuia wengine kunihukumu na kuingilia maslahi yangu. Nikifikiria kuhusu tabia yangu, niligundua kwamba haikuwa ya kujali. Kungekuwaje na kiini chochote cha upendo? Kuangalia nyuma, sikuonyesha huruma yoyote kwa dada mzee kuanzia mwanzo, wala kuonyesha fikira zozote. Kwa kweli asili yangu ilikuwa ovu! Dada mzee alianza kuwa mwenyeji alipofika kwa familia ya Mungu. Hakuwa ametamka hata neno la malalamiko. Kwa sababu kwa kawaida alikosa kuhudhuria mikutano na kufanya ushirika, hakuwa ameongeza uketo wa uzoefu wake katika maisha. Hata hivyo, alikuwa tayari kufuatilia na kusoma maneno ya Mungu mradi alikuwa huru. Kwa vile hakuwa wazi kabisa kuhusu ukweli, alichukulia kuwahukumu ndugu wa kiume na kike bila wao kufahamu na kuzungumzia dosari zao kama mizigo kwao; alifahamu tu visivyo tuhuma zake kwa ndugu wa kiume na wa kike kama kuzungumza bila kuficha. Yeye hakuwa na habari ni ipi kati yazo iliyokuwa tuhuma na ni ipi iliyokuwa kupiga chuku, na sikumjali. Bila kujali kimo chake, mimi bila kuchagua kwa mpango nilijitetea mradi zilihusisha maslahi yangu, na nikamlazimisha ajijue mwenyewe. Mimi ni mwenye kukosa mantiki vipi! Ni kwa sababu gani sipaswi kuwaruhusu wengine kunihukumu? Hata kama wengine hawatoi mawazo bila woga, si namna ambavyo niliishi sawa na ya Shetani? Kila kitu nilichokuwa nimekifanya kilikuwa chote ni kwa sababu yangu mwenyewe, na kilikuwa kujilinda mwenyewe. Mradi maslahi yangu hayakuwa yakiingiliwa, sikujali kuhusu watu wengine. Sikuonyesha fikira yangu kwa udhaifu wa wengine, wala kufikiria kama wengine wangeweza kuhimili mawasiliano yangu au kama mawasiliano yangu yalileta madhara yoyote hasi. Jinsi nilivyoishi ilishawishiwa na tabia ya upotovu ya Shetani. Nilichokuwa nimekileta kwa watu kilikuwa ni madhara na shambulio. Wengine wangewezaje kuuunga hili mkono? Nilichokisema na kufanya kilimfanya Mungu achukizwe, na kumfanya Roho Mtakatifu asifanye kazi kwangu. Mawasiliano yangu yangekuwaje na ufanisi?

Mungu alisema, “Mtu yeyote anaweza kutumia maneno na vitendo vyake wenyewe kuwakilisha tabia yake halisi. Sura hii ya kweli bila shaka ni asili yake. Kama wewe ni mtu anayeongea bila kuwa dhahiri, basi una asili mbovu. Kama asili yako ni yenye hila sana, basi namna ambayo unafanya mambo ni janja na laghai sana, nawe unafanya iwe rahisi sana kwa watu kulaghaiwa nawe. Kama asili yako ni mbovu sana, huenda maneno yako ni mazuri kusikiliza, lakini vitendo vyako haviwezi kuficha njia zako mbovu. Kama asili yako ni vivu sana, basi kila kitu unachosema vyote vinalenga kukwepa lawama na wajibu wa uzembe na uvivu wako, na vitendo vyako vitakuwa vya polepole sana na vizembe, na vizuri sana katika kuuficha ukweli. Kama asili yako ni yenye uwezo wa kuhisi maono ya wengine sana, basi maneno yako yatakuwa yenye busara na hatua zako pia zitalingana sana na ukweli. Kama asili yako ni aminifu sana, basi maneno yako lazima yawe ya dhati na namna ambayo unafanya mambo lazima iwe yenye kuhusika na mambo halisi, bila mengi ya kufanya bwana wako asikuamini. Kama asili yako ni yenye tamaa sana au ni yenye tamaa ya fedha, basi moyo wako mara nyingi utajazwa na mambo haya na utafanya baadhi ya mambo yaliyopotoka bila kukusudia, mambo maovu ambayo hufanya iwe vigumu kwa watu kusahau na zaidi ya hayo yatawaudhi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Tatizo Zito Sana: Usaliti (1)). Kwa maneno ya Mungu, nilitambua kwamba jinsi watu wanavyojifichua na kuishi maisha yao vinatawaliwa na asili zao. Aina ya asili ndani itatarajiwa kuamua ni tabia ipi itakayofichuliwa nje. Kama kuna jambo bovu ndani, basi tabia itatawaliwa na asili mbaya, na haitaonyesha ukarimu kamwe. Wakati motisha yangu ya kuwasiliana na dada mzee ilikuwa yenye kosa, kilichonitawala ndani hakikuwa Mungu, ukweli au mambo mazuri, bali alikuwa ni Shetani. Jinsi ambavyo niliishi ilikuwa ni picha ya Shetani. Kwa hiyo, mawasiliano yangu hayangeweza kuwafaidi wengine. Kama nilikutana na kitu cha aina hii katika siku za nyuma, ningekuwa nimelenga matendo ya nje; ningefikiri kuwa sikuwa nimeongoza kanisa, kwamba sikuwa mzuri kwa kuwasiliana na watu wengine, na ningetafuta sababu nyingi za kujitoa katika lawama. Ni leo tu nilipotambua kwamba matendo ya nje hayafanyizi dhima yenye uamuzi, bali ni kama moyo ni sahihi au la. Ni muhimu kuona kiini kilicho ndani. Kwa mfano, kama mtu kweli anampenda mtu mwingine, atachunguza na kuzingatia kile anachokipenda kwa moyo wake, na hatimaye ataonyesha upendo wake kwake na kumfanya auhisi. Kama niliwapenda ndugu zangu wa kike na wa kiume kwa ndani, ningekuwa nimezingatia zaidi na kuonyesha huruma zaidi kwa matatizo yao na kuzijali hisia zao, na kisha ningechukua hatua sahihi na kutumia lugha na toni sahihi kuwasiliana nao. Hata kama sikutatua matatizo ya wengine, singekuwa nimeleta madhara kwao. Kwa sababu hakuna upendo ndani yangu, kile ninachofichua ni uovu, hata kama matendo yangu ya nje ni mazuri na sahihi. Kwa sababu Mungu anawapenda wanadamu, bila kujali kile Yeye hufanya, ni ufunuo na dhihirisho la upendo. Mungu alisema, “Kusudi la Mungu kusema mambo haya ni kuwabadilisha na kuwaokoa watu. Ni kwa kuzungumza tu kwa namna hii ndiyo Anaweza kupata matokeo mazuri kabisa. Unapaswa kuona kwamba nia njema za Mungu ni kwa ajili ya kuwaokoa watu na zote ni mfano halisi waupendo wa Mungu. Bila kujali kama unauangalia kwa mtazamo wa hekima katika kazi ya Mungu, kwa mtazamo wa hatua na mbinu katika kazi ya Mungu, au kwa mtazamo wa wakaa wa kazi au mipangilio na mipango Yake sahihi, chote kina upendo Wake. Kwa mfano, watu wote wana upendo kwa wana na mabinti zao; ili watoto wao waweze kutembea katika njia sahihi, wote wameweka jitihada kubwa. Wanapogundua udhaifu wa watoto wao, wazazi wanahofia kwamba ikiwa watazungumza kwa sauti laini, watoto wao hawatasikia na hawataweza kubadilika, na wanahofia kwamba ikiwa watazungumza kwa ukali sana, wataumiza staha ya watoto wao, na watoto wao hawataweza kuvumilia. Hii yote inafanyika kutokana na upendo, na wanaiwekea kiwango kikubwa cha jitihada. Nyinyi kama wana na mabinti, huenda mmepitia upendo wa wazazi wenu. Upendo hauhusu tu upole na kujali; hata zaidi, unahusu kuadibu vikali. Zaidi ya haya, kila kitu Mungu afanyacho kwa wanadamu kinafanywa kutokana na upendoYeye hutenda chini ya sharti la mwanzo la upendo, ndiyo sababu Yeye kufanya kadri ya uwezo Wake kuleta wokovu kwa wanadamu waliopotoka. Hawashughulikii watu kwa kutimiza wajibu tu; Yeye hufanya mipango sahihi na kuiendeleza hatua kwa hatua. Kwa kuzingatia wakati, eneo, toni ya sauti, mbinu ya kuzungumza, na kiwango cha jitihada Anachoweka..., inaweza kusemwa kwamba yote hii inafichua upendo Wake, na yote inaelezea vizuri kabisa kwamba upendo Wake kwa binadamu hauna mipaka na haupimiki. Watu wengi husema mambo ya uasi wanapokuwa katikati ya majaribu; wanatoa malalamiko. Lakini Mungu hagombanigombani juu ya mambo haya, na hakika hawaadhibu watu kwa hili. Kwa sababu Anawapenda watu, Anasamehe kila kitu. Ikiwa Angekuwa na chuki tu badala ya upendo, basi Angeweza kuwahukumu watu mapema kabisa. Kwa kuwa Mungu ana upendo, Hagombanigombani, bali Anavumilia, na Anaweza kuona shida za watu. Hii kabisa ni kufanya kila kitu chini ya ushawishi wa upendo(“Je, Unauelewa Upendo wa Mungu kwa Binadamu?” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Kiini cha Mungu ni upendo, hivyo dhihirisho la Mungu pia ni upendo. Upendo wa Mungu kwa binadamu hauakisiwi kwa mdomo, lakini unajumuishwa kivitendo katika kazi Yake, katika kila hatua ya kazi Yake, na kwa njia za kazi Yake. Jinsi na wakati Mungu hufanya kazi katika kila mtu, watu gani, vitu au matukio Yeye hupanga kwa ajili yake na kwa muda gani Yeye atamsafisha, yote huakisi mipango sahihi na jitihada angalifu za Mungu. Kazi yote ya vitendo ya Mungu husambaza upendo Wake safi kwa binadamu bila ubaguzi. Mungu anawapenda wanadamu kiasi kwamba Anatumia jitihada Zake zote kutuokoa, anavumilia kutomwelewa na kumpinga kwetu na kuvumilia na kusamehe upumbavu na ujinga wetu. Haya yote hunifanya nione ukuu na uadilifu wa Mungu. Kwa kulinganisha, kile ambacho nimeishi kwa kudhihirisha ni tabia ya kishetani ambayo ni mbaya na ya kudharauliwa. Katika kutambua yote haya, kwa kweli nilishirikiana mambo haya mapotofu katika moyo wangu na dada mzee. Farakano kati yetu liliondolewa pasipo sisi kujua. Namshukuru Mungu kwa moyo wangu wote. Utukufu uwe kwa Mungu.

Hapo awali, ufahamu wangu kujihusu ulikuwa maneno tu. Ulikuwa ufahamu niliokuwa nimejifunza kwa ghibu, na sikujua asili yangu mwenyewe kulingana na ufunuo wa maneno ya Mungu. Naielewa leo kutokana na uzoefu wangu. Mara mtu anapopotoshwa na Shetani, asili yake hugeuka kuwa asili ya Shetani. Bila kujali hotuba, kitendo, au mawazo, zote hutawaliwa na asili ya binadamu. Mtu anaweza kushughulika na tabia yake potovu na hatua kwa hatua kuibadilisha, ikiwa tu anaitambua asili yake. Kama hana maarifa ya asili yake, anaweza tu kupitia utawala wa asili ya Shetani na kumwasi na kumpinga Mungu pasipo kujua—bila kutaja kwamba hawezi kubadilisha tabia yake. Kuanzia sasa kuendelea, nitabadilisha mbinu mbaya nilizotumia awali za kuzingatia sana matendo ya nje. Mimi nitajaribu kutolalamika kuhusu desturi zao za nje, na sitaegemeza kujua hali yangu katika ufuataji wa sheria. Kwa kweli na kwa dhati nitachukua hukumu na kuadibu kwa Mungu, nitajua asili yangu, na kwa hakika kutambua asili yangu kwa njia ya ufunuo wa maneno ya Mungu ili kubadilisha tabia yangu mapema iwezekanavyo, na kuokolewa na Mungu.

Iliyotangulia: Nilifurahia Karamu Kubwa

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Utajiri wa Maisha

Wang Jun Mkoa wa Shandong Kwa miaka mingi tangu kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, mke wangu na mimi tumepitia hili...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp