70 Msifu Mungu Kwa Moyo Mmoja

Tunakusanyika kula, kunywa, kufurahia maneno ya Mungu,

na tunapokea kazi ya Roho Mtakatifu.

1

Tunamfikiria Mungu, tunaomba na kusoma, tunafanya ushirika,

na tunatafakari, kufikiria, na kumtafuta Mungu.

Kuishi katika maneno ya Mungu, tunaona Anapendeza.

Ukweli unatuokoa; tunaonja upendo wa kweli wa Mungu.

Maisha ya kanisa ni mazuri mno; sifa ni ya aina nyingi.

Hatuna budi ila kuimba na kucheza kwa sifa ya Mungu.

Hakuna sheria au vizuizi katika sifa zetu.

Sifa za kweli hutufanya tufurahie kila wakati.

Maisha mbele ya Mungu huleta furaha ya kweli,

tutampenda na kumtii Mungu milele.

Kuona ukuu wa wokovu wa Mungu,

tunamsifu Mungu kwa moyo mmoja.

Tunashiriki ukweli, tunapata kazi ya Roho Mtakatifu,

tunashiriki uzoefu, maisha yetu yanakua.

2

Sote ni watu wa ufalme wa Mungu,

na sote tuna mioyo ya kweli inayompenda.

Tunatekeleza wajibu wetu kwa nia, moyo mmoja,

na tunaona baraka na uongozi wa Mungu.

Hukumu inatutakasa, tunaona Mungu ni mwenye haki.

Tunatupilia mbali upotovu wetu, tunafanywa upya.

Tunaishi kwa kuudhihirisha mfano wa wanadamu waaminifu.

Ni maisha ya ufalme kumwabudu Mungu kwa roho na ukweli.

Maisha mbele ya Mungu huleta furaha ya kweli,

tutampenda na kumtii Mungu milele.

Kuona ukuu wa wokovu wa Mungu,

tunamsifu Mungu kwa moyo mmoja.

Ndugu, wakusanyika pamoja,

tumepitia panda shuka nyingi.

3

Ukandamizaji wa serikali ni mbaya sana,

mateso na ugumu tumevumilia.

Hakuna kitu ambacho kimetikisa azimio letu daima.

Hii ni kwa sababu ya mwongozo wa maneno ya Mungu.

Gharama kuu ambayo Mungu amelipa

kwa ajili ya wokovu wetu haiwezi kupimika.

Mungu anaishi kati yetu, Akituongoza kila wakati.

Wakati huu mzuri, maisha, ni vya thamani sana.

Maisha mbele ya Mungu huleta furaha ya kweli,

tutampenda na kumtii Mungu milele.

Kuona ukuu wa wokovu wa Mungu,

tunamsifu Mungu kwa moyo mmoja.

Maisha mbele ya Mungu huleta furaha ya kweli,

tutampenda na kumtii Mungu milele.

Kuona ukuu wa wokovu wa Mungu,

tunamsifu Mungu kwa moyo mmoja,

tunamsifu Mungu kwa moyo mmoja,

tunamsifu Mungu kwa moyo mmoja.

Iliyotangulia: 68 Furaha Katika Nchi ya Kanaani

Inayofuata: 71 Furaha Kubwa Zaidi ni Kumpenda Mungu Kweli

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp