Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III

Mamlaka ya Mungu (II)

Leo tutaendelea na ushirika wetu kuhusu mada ya “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee.” Tayari tumekuwa na ushirika mara mbili katika mada hii, wa kwanza kuhusiana na mamlaka ya Mungu na wa pili kuhusiana na tabia ya haki ya Mungu. Baada ya kusikiliza ushirika huu mara mbili, je, mmepata ufahamu mpya wa utambulisho wa Mungu, hadhi, na kiini Chake? Je, maono haya yamewasaidia kufikia maarifa mazito zaidi na uhakika wa ukweli kuuhusu uwepo wa Mungu? Leo Ninapanga kufafanua mada hii ya “Mamlaka ya Mungu.”

Kuelewa Mamlaka ya Mungu Kutoka kwa Mitazamo Mikubwa na Midogo

Mamlaka ya Mungu ni ya kipekee. Ndiyo maonyesho ya tabia ya, na dutu maalum ya,, utambulisho wa Mungu Mwenyewe. Hakuna kiumbe ambacho kiliumbwa wala kile ambacho hakikuumbwa kinachomiliki maonyesho ya tabia kama hii, na dutu maalum kama hii; ni Muumba tu ndiye anayemiliki aina hii ya mamlaka. Hivyo ni kusema kwamba, ni Muumba tu—Mungu Yule wa Kipekee—ambaye anaonyeshwa kwa njia hii na ndiye aliye na dutu kama hii. Kwa nini tuzungumzie mamlaka ya Mungu? Mamlaka ya Mungu Mwenyewe yanatofautiana vipi na mamlaka yaliyomo kwenye akili ya binadamu? Ni nini maalum sana kuyahusu? Na kunao umuhimu gani haswa kuyazungumzia hapa? Kila mmoja wenu lazima aweze kutilia maanani kwa umakinifu suala hili. Kwa watu wengi zaidi, “Mamlaka ya Mungu” ni fikira isiyoeleweka, ile ambayo ni ngumu sana kupata kuielewa, na mazungumzo yoyote kuihusu huenda yasizae matunda mazuri. Kwa hivyo lazima kutakuwepo na pengo kati ya maarifa ya mamlaka ya Mungu ambayo binadamu anaweza kuwa nayo, na kiini cha mamlaka ya Mungu. Ili kuliziba pengo hili, ni lazima mtu aweze kuelewa mamlaka ya Mungu hatua kwa hatua kupitia kwa maisha halisi ya watu, matukio, vitu, au mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wa wanadamu, ambayo wanadamu wanaweza kuyaelewa. Ingawaje kauli hii “Mamlaka ya Mungu” inaweza kuonekana kama isiyoeleweka, mamlaka ya Mungu kwa kweli si ya dhahania kamwe. Yeye yupo na binadamu kila dakika ya maisha yake, akimwongoza kila siku. Kwa hivyo, katika maisha ya kila siku ya kila mtu ataweza haswa kuona na kupitia dhana halisi ya mamlaka ya Mungu. Uhalisi huu ni uthibitisho wa kutosha kwamba mamlaka ya Mungu kwa kweli yapo, na inamuruhusu mtu kutambua na kuelewa kimamilifu ukweli huu kwamba Mungu anamiliki mamlaka haya.

Mungu aliumba kila kitu, na baada ya kuviumba, Anao utawala juu ya kila kitu. Pamoja na kuwa na utawala juu ya kila kitu, pia anadhibiti kila kitu. Wazo hili linamaanisha nini “Mungu anadhibiti kila kitu”? Hali hii inaweza kuelezewa vipi? Hali hii inatumika vipi katika maisha halisi? Mnawezaje kuyajua mamlaka ya Mungu kwa kuelewa hoja hii kwamba “Mungu Anadhibiti kila kitu”? Kutoka kwenye kauli ile ile “Mungu anadhibiti kila kitu” tunafaa kuona kwamba kile ambacho Mungu anadhibiti si sehemu ya sayari, sehemu ya uumbaji, wala sehemu ya mwanadamu, lakini kila kitu: kuanzia kwa viumbe vile vikubwa hadi vile vidogovidogo, kuanzia kwa vile vinavyoonekana hadi visivyoonekana, kuanzia kwenye nyota za angani hadi kwenye vitu vilivyo na uhai ulimwenguni, pamoja na viumbe vidogovidogo visivyoweza kuonekana kwa macho ya kawaida au viumbe vilivyo katika maumbo mengine. Huu ndio ufafanuzi hakika wa “kila kitu” ambacho Mungu “anadhibiti,” na ndio upana ambao Mungu anaonyesha mamlaka Yake, kiwango cha ukuu na utawala Wake.

Kabla ya binadamu hawa kuwepo, viumbe vyote—sayari zote, nyota zote kule mbinguni—tayari vilikuwepo. Kwenye kiwango cha vitu vikubwa, vyombo hivi vya mbinguni vimekuwa vikizunguka mara kwa mara chini ya udhibiti wa Mungu, kwa kuwepo kwao kote, hata hivyo miaka mingi imepita. Ni sayari gani inaenda wapi na wakati gani haswa; ni sayari gani inafanya kazi gani, na lini; ni sayari gani inazunguka katika mzingo gani, na ni lini inatoweka au inabadilishwa—vitu hivi vyote vinasonga mbele bila ya kosa lolote dogo. Nafasi za sayari na umbali kati yazo ni masuala yanayofuata mifumo maalum, ni masuala ambayo yanaweza kufafanuliwa kwa data sahihi; njia ambazo zinasafiria, kasi na mifumo ya mizunguko yao, nyakati ambapo zinapatikana kwenye nafasi mbalimbali zinaweza kufafanuliwa kwa usahihi na kufafanuliwa kwa sheria maalum. Kwa miaka na mikaka sayari zimefuata sheria hizi na hazijawahi kukosea hata kidogo. Hakuna nguvu inayoweza kubadilisha au kuharibu njia zao au mifumo ambayo zinafuata. Kwa sababu sheria maalum ambazo zinaongoza mizunguko yao na data maalum inayozifafanua ziliamuliwa kabla na mamlaka ya Muumba, zinatii sheria hizi zenyewe, kulingana na ukuu na udhibiti wa Muumba. Kwenye kiwango cha mambo makubwamakubwa, si vigumu kwa binadamu kujua zaidi kuhusu mifumo fulani, data fulani, pamoja na sheria au matukio fulani yasiyoeleweka au yasiyoelezeka. Ingawaje binadamu hawakubali kwamba Mungu yupo, haukubali hoja kwamba Muumba aliumba na anatawala kila kitu na zaidi ya yote hautambui uwepo wa mamlaka ya Muumba, wanasayansi wa kibinadamu, wanafalaki, nao wanafizikia wanachunguza na kugundua zaidi na zaidi kwamba uwepo wa kila kitu kwenye ulimwengu, na kanuni na mifumo inayoamuru mizunguko yao, vyote vinatawaliwa na kudhibitiwa na nishati nyeusi kubwa na isiyoonekana. Ukweli huu unamlazimisha mwanadamu kukabiliana na kukiri kwamba kuna Mwenye Nguvu katikati ya mifumo hii ya mizunguko, Anayepangilia kila kitu. Nguvu zake si za kawaida, na ingawaje hakuna anayeweza kuona uso Wake wa kweli, Yeye hutawala na kudhibiti kila kitu kila dakika. Hakuna binadamu au nguvu zozote zile zinazoweza kuuzidi ukuu Wake. Huku binadamu akiwa amekabiliwa na hoja hii, lazima atambue kwamba sheria zinazotawala uwepo wa kila kitu haziwezi kudhibitiwa na binadamu, haziwezi kubadilishwa na yeyote; na wakati uo huo binadamu lazima akubali kwamba, binadamu hawezi kuelewa kikamilifu sheria hizi. Na hizi sheria hazitokei kiasili lakini zinaamrishwa na Mtawala. Haya yote ni maonyesho na mamlaka ya Mungu yanayoonyesha kwamba mwanadamu anaweza kuelewa katika kiwango cha mambo makubwa.

Kwenye kiwango cha mambo madogomadogo, milima, mito, maziwa, bahari, na maeneo ya ardhi yote ambayo binadamu anatazama nchini, misimu yote ambayo yeye anapitia, mambo yote yanayopatikana kwenye ulimwengu, kukiwemo mimea, wanyama, vijiumbe na binadamu, vyote viko chini ya ukuu wa Mungu na vinadhibitiwa na Mungu Mwenyewe. Katika ukuu na udhibiti wa Mungu, vitu vyote vinakuwepo au vinatoweka kulingana na fikira Zake, maisha ya vitu hivi yanatawaliwa na sheria fulani, na vinakua na kuzaana kulingana nazo. Hakuna binadamu au kiumbe chochote kilicho juu ya sheria hizi. Kwa nini hali iko hivi? Jibu la pekee tu ni, kwa sababu ya mamlaka ya Mungu. Au, nikijibu kwa njia nyingine, kwa sababu ya fikira za Mungu na matamshi ya Mungu; kwa sababu Mungu Mwenyewe hufanya haya yote. Hivi ni kusema, ni mamlaka ya Mungu na ni akili ya Mungu ambayo iliunda sheria hizi; zitasonga na kubadilika kulingana na fikira Zake, na kusonga huku na mabadiliko haya yote yanafanyika au kutoweka kwa minajili ya mpango Wake. Hebu tuchukulie magonjwa ya mlipuko, kwa mfano. Yanazuka tu bila onyo, hakuna anayejua asili yake, au sababu maalum zinazoelezea ni kwa nini huwa yanatokea, na kila wakati magonjwa ya mlipuko yanapofika mahali fulani, wale walio na bahati mbaya hawawezi kukwepa maafa. Sayansi ya binadamu inafafanua na kutuelewesha kwamba magonjwa ya mlipuko yanasababishwa na kuenea kwa vijidudu hatari au vyenye madhara, na kasi yao, eneo lao, na njia ya maambukizi haiwezi kutabiriwa au kudhibitiwa na sayansi ya wanadamu. Ingawaje watu hupingana na magonjwa ya mlipuko kwa kila njia iwezekanayo, hawawezi kudhibiti ni watu gani au wanyama gani watakaoathirika wakati magonjwa ya mlipuko yanapozuka. Kitu cha pekee ambacho binadamu wanaweza kufanya ni kujaribu kuyazuia, kuyapinga, na kuyafanyia utafiti. Lakini hakuna anayejua sababu za msingi zinazoelezea mwanzo au mwisho wa magonjwa ya mlipuko ya aina yoyote ile,, na hakuna anayeweza kuyadhibiti. Wakiwa wamekabiliwa na ongezeko na kuenea kwa magonjwa ya mlipuko, suala la kwanza ambalo binadamu hufanya ni kuunda chanjo, lakini mara nyingi magonjwa hayo ya mlipuko hayo hutoweka kabisa kabla ya hata chanjo kuwa tayari. Kwa nini magonjwa ya mlipuko hutoweka kabisa? Wengine husema kwamba vijidudu vimeweza kudhibitiwa, wengine husema kwamba vimetoweka kabisa kwa sababu ya mabadiliko katika misimu…. Kuhusiana na ikiwa makisio haya ya kuchanganyikiwa ni kweli au la, sayansi haiwezi kutupa ufafanuzi wowote, na wala haitoi jibu lolote lenye uhakika. Kile ambacho binadamu wanakabiliwa nacho si makisio haya tu lakini pia ukosefu wa mwanadamu katika kuelewa na woga wa magonjwa haya ya mlipuko. Hakuna anayejua, baada ya kila kitu kuchambuliwa, ni kwa nini magonjwa haya ya mlipuko huanza au ni kwa nini huisha. Kwa sababu wanadamu wanayo imani tu katika sayansi, wanaitegemea sayansi kabisa, lakini hawatambui mamlaka ya Muumba au kuukubali ukuu Wake, hawatawahi kupata jibu kamwe.

Katika ukuu wa Mungu, vitu vyote vinazaana, vinakuwepo, na kupotea kwa sababu ya mamlaka Yake na usimamizi Wake. Baadhi ya mambo huja na kwenda polepole, na binadamu hawezi kutambua ni wapi yalitokea au kung’amua sheria ambazo mambo haya hufuata, sisemi hata kuelewa sababu za mambo haya kuja na kwenda. Ingawaje binadamu anaweza kushuhudia, kusikia, au kupitia yote yanayotokea ulimwenguni; ingawa yote yanamhusu mwanadamu, na ingawa mwanadamu bila kujua anapitia hali isiyo ya kawaida, ukawaida, au hata ugeni wa matukio mbalimbali, bado hajui chochote kuhusu nia za Muumba na mawazo Yake yaliko nyuma ya mambo hayo yanayotokea katika ulimwengu. Kunazo hadithi nyingi zinazotokana na haya mambo yote, ukweli mwingi uliofichwa. Kwa sababu binadamu amepotoka na kwenda mbali na Muumba, kwa sababu hakubali hoja hii kwamba Mamlaka ya Muumba ndiyo hutawala mambo yote, hatawahi kujua kila kitu kinachofanyika katika ukuu Wake. Kwa sehemu nyingi zaidi, udhibiti na ukuu wa Mungu huzidi mipaka ya fikra ya binadamu, maarifa ya binadamu, kuelewa kwa binadamu, na kile ambacho sayansi ya binadamu inaweza kufikia; uwezo wa binadamu walioumbwa hauwezi kushindana nayo.. Baadhi ya watu husema “Kwa sababu hujashuhudia ukuu wa Mungu wewe mwenyewe, unawezaje kusadiki kwamba kila kitu kinatokana na mamlaka Yake?” Kuona si kuamini kila mara; kuona si kutambua na kuelewa kila mara. Kwa hivyo imani inatoka wapi? Ninaweza kusema kwa uhakika, “Imani huja kutokana na kiwango na kina cha uelewa wa watu wa, na uzoefu wa, uhalisia na sababu za msingi za mambo.” Kama unasadiki kwamba Mungu yupo, lakini huwezi kutambua, na wala huwezi kuelewa, hoja ya udhibiti wa Mungu na ukuu wa Mungu katika mambo yote, basi katika moyo wako hutawahi kukubali kwamba Mungu anayo mamlaka kama haya na kwamba mamlaka ya Mungu ni ya kipekee. Hutawahi kukubali kwa kweli Muumba kuwa Bwana wako, Mungu wako.

Hatima ya Binadamu na Hatima ya Ulimwengu Haviwezi Kutenganishwa na Ukuu wa Muumba

Nyinyi nyote ni watu wazima. Baadhi yenu ni wa umri wa kati; baadhi mmefikisha umri wa uzee. Kutoka kwa yule asiyeamini hadi kwa yule anayeamini, na kuanzia mwanzo wa kumwamini Mungu hadi kukubali neno la Mungu na kuweza kupitia kazi ya Mungu, je, una kiwango gani cha maarifa kuhusu ukuu wa Mungu? Je, ni uelewa gani mlioupata kuhusu hatima ya mwanadamu? Je, mtu anaweza kutimiza kila kitu anachotamani katika maisha? Je, ni mambo mangapi kwenye miongo michache iliyopita katika kuwepo kwenu mliyoweza kutimiza kama mlivyopenda? Ni mambo mangapi hayafanyiki kama yalivyotarajiwa? Ni mambo mangapi hutupata kwa mshangao mzuri? Ni mambo mangapi ambayo ungali unasubiri yatimie—unasubiri bila kufahamu muda sahihi, unasubiria mapenzi ya Mbinguni? Mambo mangapi yanakufanya uhisi kana kwamba huna wa kukusaidia na umezuiliwa? Watu wote wanayo matumaini kuhusu hatima zao, na hutarajia kwamba kila kitu katika maisha yao kitaenda sawa na wanavyopenda, kwamba hawatakosa chakula wala mavazi, kwamba utajiri wao utaongezeka pakubwa. Hakuna anayetaka maisha ya kimaskini na ya taabu, yaliyojaa ugumu, na kuandamwa na majanga. Lakini watu hawawezi kuona mbele au kudhibiti mambo haya. Pengine kwa baadhi ya watu, yaliyopita ni mchanganyiko tu wa yale mambo waliyoyapitia; hawajifunzi katu ni nini mapenzi ya Mbinguni, wala hawajali mapenzi hayo ni yapi. Wanaishi kwa kudhihirisha maisha yao bila kufikiria, kama wanyama, wakiishi siku baada ya siku, bila kujali kuhusu hatima ya binadamu ni nini, kuhusu ni kwa nini binadamu wako hai au vile wanavyostahili kuishi. Watu hawa hufikia umri wa uzee bila ya kufaidi ufahamu wowote wa hatima ya binadamu, na mpaka wakati ule wanapokufa hawana habari yoyote kuhusu maana ya maisha. Watu kama hao wamekufa; ni viumbe bila roho; wao ni wanyama. Ingawaje katika kuishi miongoni mwa mambo haya yote, watu hupata furaha kutoka kwa njia nyingi ambazo ulimwengu hutosheleza mahitaji yao ya anasa, ingawaje wanauona ulimwengu huu wa anasa ukiwa unapiga hatua bila kusita, hali yao binafsi waliyoipitia—kile ambacho mioyo yao na roho zao zinahisi na kupitia—hakina uhusiano wowote na mambo ya anasa, na hakuna kitu chochote cha anasa ambacho kinaweza kuchukua nafasi yake. Ni utambuzi ulio ndani ya moyo wa mtu, kitu ambacho hakiwezi kuonekana kwa macho. Utambuzi huu upo katika ufahamu wa mtu wa, na hisia za mtu za, maisha ya mwanadamu na hatima ya mwanadamu. Na mara nyingi humwongoza mtu katika kuelewa kwamba Bwana yule asiyeonekana anapanga vitu vyote, Anaunda kila kitu kwa ajili ya binadamu. Katikati ya haya yote, mtu hawezi kuepuka ila kukubali mipangilio na mipango ya hatima ya mambo; wakati uo huo, mtu hawezi kuepuka ila kukubali njia iliyo mbele ambayo Muumba amempangia, ukuu wa Muumba dhidi ya hatima ya mtu. Hii ndiyo hoja isiyopingika. Haijalishi ni maono na mtazamo gani ambao mtu anao kuhusu hatima yake, hakuna anayeweza kubadilisha ukweli huu.

Pale utakapoenda kila siku, kile utakachofanya, yule au kile utakachokumbana nacho, kile utakachosema, kile kitakachokufanyikia—je, kati ya vyote hivi kipo kinachoweza kutabirika? Watu hawawezi kutabiri matukio haya yote, sikutajii kudhibiti namna ambavyo yanaendelea. Katika maisha, matukio haya yasiyotabirika hufanyika kila wakati, na ni tukio la kila siku. Mabadiliko haya ya kila siku na njia ambazo yanajitokeza, au mifumo inayofuata, ni vikumbusho vya kila wakati kwa binadamu kwamba hakuna kinachofanyika bila mpango, kwamba mchakato wa kutokea kwa kila tukio, na kutoepukika kwa mambo haya, haviwezi kubadilishwa na mapenzi ya binadamu. Kila tukio linaonyesha onyo kutoka kwa Muumba kwa mwanadamu, na pia linatuma ujumbe kwamba, binadamu hawawezi kudhibiti hatima zao wenyewe; na wakati uo huo kila tukio ni upingaji wa malengo yasiyo na mwelekeo, yasiyo na maana ya binadamu na tamanio la kuchukua hatima yake na kutaka kuidhibiti yeye mwenyewe kwa mikono yake. Ni sawa na makofi yenye nguvu juu ya masikio ya binadamu moja baada ya jingine, yanayomlazimisha binadamu kufikiria upya ni nani, hatimaye, anatawala na kudhibiti hatima zao. Na kama vile malengo na matamanio yao yanavyokiukwa mara kwa mara na kusambaratika, binadamu kwa kawaida huishia kukubali bila kujua kile ambacho hatima yao imehifadhi, kukubali uhalisia, kukubali mapenzi ya mbinguni, na kukubali ukuu wa Muumba. Kutokana na mabadiliko haya ya kila siku katika hatima za maisha yote ya binadamu, hakuna kitu ambacho hakifichui mipango ya Muumba na ukuu Wake; hakuna kile ambacho hakiutumi ujumbe huu kwamba “yale mamlaka ya Muumba hayawezi kupitwa,” ambacho hakionyeshi ukweli wa milele kwamba “mamlaka ya Muumba ni ya juu zaidi.”

Hatima za binadamu na zile za ulimwengu zimeingiliana kwa undani na ukuu wa Muumba, zimefungamanishwa na haziwezi kutenganishwa na mipango ya Muumba; na hatimaye, haziwezi kutenganishwa na mamlaka ya Muumba. Kupitia kwenye sheria za mambo yote binadamu huja kuelewa mipango ya Muumba na ukuu Wake; kupitia kwenye sheria za namna ya kuishi ambazo anaona katika utawala wa Muumba; kutoka kwenye hatima za mambo yote anapata hitimisho kuhusu njia ambazo Muumba huonyesha ukuu Wake na kuvidhibiti; na katika mizunguko ya maisha ya wanadamu na vitu vyote, mwanadamu kwa kweli huja kupitia ile mipango na mipangilio ya Muumba kwa mambo yote na kwa viumbe vyote vilivyo hai na anashuhudia kwa kweli namna ambavyo mipango na mipangilio hiyo inavyozidi sheria zote za nchi, kanuni, na taasisi, mamlaka na nguvu zingine zote. Kwa mujibu wa haya, binadamu wanashawishiwa kutambua kwamba, ukuu wa Muumba hauwezi kukiukwa na kiumbe chochote kilichoumbwa, kwamba hakuna nguvu zinazoweza kuharibu au kubadilisha matukio na mambo yaliyoamuliwa kabla na Muumba. Ni kupitia kwenye sheria na kanuni hizi takatifu ambapo binadamu na viumbe vyote wanaweza kuishi na kuzaliana, kizazi baada ya kizazi. Je, huu si mfano halisi wa mamlaka ya Muumba? Ingawaje binadamu huona, kwenye sheria zile za malengo, ukuu wa Muumba na utaratibu Wake wa matukio yote na mambo yote, je, ni watu wangapi wanaweza kung’amua kanuni ya ukuu wa Muumba juu ya ulimwengu? Ni watu wangapi wanaweza kujua, kutambua, kukubali kwa kweli na kujinyenyekeza katika ukuu na mpangilio wa Muumba dhidi ya hatima zao wenyewe? Nani, ambaye baada ya kusadiki hoja ya ukuu wa Muumba juu ya viumbe vyote, ataweza kusadiki kwa kweli na kutambua kwamba Muumba pia anaamrisha hatima hii ya maisha ya binadamu? Ni nani anayeweza kuelewa kwa kweli hoja hii kwamba hatima ya binadamu imo kwenye kiganja cha mkono wa Muumba? Ni aina gani ya mtazamo ambao binadamu wanafaa kuchukua katika ukuu wa Muumba, wanapokabiliwa na ukweli kwamba Anatawala na kudhibiti hatima ya binadamu, huu ni uamuzi ambao kila binadamu ambaye kwa sasa anakabiliwa na ukweli huu ni lazima ajiamulie mwenyewe.

Awamu Sita katika Maisha ya Binadamu

Katika mkondo wa maisha ya mtu, kila mtu hufikia kwenye misururu ya awamu muhimu. Hizi ni hatua za kimsingi zaidi, na muhimu zaidi, zinazoamua hatima ya maisha ya mtu. Kile kinachofuata ni ufafanuzi mfupi kuhusu hatua hizi muhimu ambazo kila mtu lazima apitie kwenye mkondo wa maisha yake.

Awamu ya Kwanza: Kuzaliwa

Mahali ambapo mtu amezaliwa, ni familia gani alimozaliwa, jinsia ya mtu, umbo la mtu, na wakati wa kuzaliwa—haya ndiyo maelezo ya awamu ya kwanza ya maisha ya binadamu.

Hakuna yeyote aliye na chaguo kuhusu sehemu hizi za awamu hii; zote ziliamuliwa kabla, mapema kabisa na Muumba. Haziathiriwi na mazingira ya nje kwa vyovyote vile, na hakuna masuala yanayosababishwa na binadamu yanaweza kubadilisha hoja hizi ambazo Muumba aliamua kabla. Kwa mtu kuweza kuzaliwa inamaanisha kwamba Muumba tayari ametimiza hatua ya kwanza ya hatima ambayo Amempangilia mtu huyo. Kwa sababu Aliamua kabla maelezo haya yote tena mapema mno, hakuna aliye na nguvu za kubadilisha maelezo yoyote yale. Licha ya hatima ya baadaye ya mtu, hali za kuzaliwa kwa mtu ziliamuliwa kabla, na zinabakia kama zilivyo; haziathiriwi kwa njia yoyote ile na hatima ya mtu katika maisha, wala haziathiri kwa vyovyote vile ukuu wa Muumba juu yazo.

1) Maisha Mapya Yanazaliwa Kulingana na Mipango ya Muumba

Ni maelezo yapi ya awamu ya kwanza—mahali mtu anapozaliwa, familia ya mtu, jinsia ya mtu, umbo la mwili wa mtu, muda wa kuzaliwa kwa mtu—ambayo mtu anaweza kuchagua? Bila shaka, kuzaliwa kwa mtu ni tukio asiloweza kuchagua: Mtu anazaliwa bila hiari yake, katika mahali fulani, muda fulani, kwenye familia fulani, akiwa na umbo fulani la kimwili; mtu anakuwa mmojawapo wa familia fulani bila hiari, anarithi kizazi fulani cha familia. Mtu hana chaguo kwenye awamu hii ya kwanza ya maisha, lakini anazaliwa kwenye mazingira yanayochaguliwa kulingana na mipango ya Muumba, kwenye familia mahususi, na jinsia na umbo mahususi, kwenye wakati mahususi ambao unaunganishwa kwa undani na mkondo wa maisha ya mtu huyu. Mtu anaweza kufanya nini katika awamu hii muhimu? Yote yakisemwa, kwa kweli mtu hana chaguo kuhusu maelezo yoyote yale yanayohusu kuzaliwa kwake. Kama isingekuwa kuamua kabla kwa Muumba na mwongozo Wake, mtu aliyezaliwa upya kwenye ulimwengu huu asingejua ni wapi atakapoenda au ni wapi atakapoishi, asingekuwa na mahusiano yoyote, asingekuwa na popote na asingekuwa na maskani yoyote halisi. Lakini kwa sababu ya mipangilio makinifu ya Muumba, anaanza safari ya maisha yake akiwa na mahali pa kuishi, wazazi, na mahali anapoita nyumbani na watu wa ukoo. Kotekote kwenye mchakato huu, mwanzo wa maisha haya mapya unaamuliwa na mipango ya Muumba, na kila kitu ambacho mtu huyu atakuja kumiliki ataweza kukabidhiwa na Muumba. Kutoka kwenye kiumbe kinachoelea kisichokuwa na jina lolote hadi kinapoanza kuwa na nyama na damu polepole, kinachoweza kuonekana, na hatimaye kuwa binadamu anayeweza kushikika, mmojawapo wa viumbe vya Mungu, anayefikiria, anayepumua, anayehisi joto na baridi, anayeshiriki katika shughuli za kawaida za kiumbe kilichoumbwa kwenye ulimwengu yakinifu na ambaye atapitia mambo haya yote ambayo kiumbe kilichoumbwa lazima kipitie maishani. Kule Kuamuliwa kabla kwa kuzaliwa kwa mtu na Muumba kunamaanisha kwamba ataweza kumpa mtu huyu mambo yote yanayohitajika kwa kuishi kwake; na kwamba mtu anazaliwa vilevile inamaanisha kwamba yeye atapokea mambo yote yanayohitajika kutoka kwa Muumba, kwamba kuanzia wakati ule kwenda mbele yeye ataishi katika umbo jingine, linalotolewa na Muumba na linalotii ukuu wa Muumba.

2) Kwa Nini Binadamu Tofauti Wanazaliwa Katika Hali Tofauti

Mara nyingi watu wanapenda kufikiria kwamba, kama wangezaliwa tena, wangezaliwa kwenye familia maarufu; kama wangekuwa wanawake, wangefanana na Binti wa Kifalme Anayependeza na wangependwa na kila mtu, na kama wangezaliwa wanaume, wangekuwa Kaka Mwenye Mvuto na Haiba, wasikose mahitaji yoyote, huku ulimwengu mzima ukiwaitikia mara moja kila unapoitwa na wao. Mara nyingi kuna wale walio na picha nyingi kuhusu kuzaliwa kwao na huwa hawajatosheka kabisa na huko kuzaliwa kwao, wanachukia familia zao, umbo lao, jinsia yao, na hata wakati wa kuzaliwa kwao. Ilhali watu hawajawahi kuelewa ni kwa nini wamezaliwa katika familia fulani au kwa nini wanafanana jinsi fulani. Hawajui kwamba, licha ya ni wapi wamezaliwa au ni vipi wanavyoonekana, wanafaa kuendeleza wajibu mbalimbali na kutimiza kazi maalum tofautitofauti katika usimamizi wa Muumba—kusudi hili halitawahi kubadilika. Ingawa katika macho ya Muumba, mahali anapozaliwa mtu, jinsia ya mtu, umbo la mwili wa mtu hivi vyote ni vitu vya muda. Ni misururu ya mambo madogomadogo katika kila awamu ya usimamizi Wake wa mwanadamu kwa ujumla. Na hatima halisi ya mtu na mwisho wake vyote haviamuliwi kutokana na wapi ambapo yeye amezaliwa katika awamu yoyote ile, lakini vinaamuliwa na kazi maalum ambayo yeye atatekeleza katika kila maisha, na kwa hukumu ya Muumba juu yao wakati mpango Wake wa usimamizi utakapokamilika.

Inasemekana kwamba kunayo sababu katika kila athari, na kwamba hakuna athari ambayo haina sababu. Na kwa hivyo kuzaliwa kwa mtu kumefungamanishwa haswa na maisha yake ya sasa na yale ya awali. Kama kifo cha mtu kinasitisha awamu yake ya sasa ya maisha, basi kuzaliwa kwa mtu ndio mwanzo wa mzunguko mpya; kama mzunguko wa kale unawakilisha maisha ya awali ya mtu, basi mzunguko huo mpya kwa kawaida ndio maisha yao ya sasa. Kwa sababu kuzaliwa kwa mtu kunaunganishwa na maisha ya kale ya mtu huyu pamoja na maisha ya sasa ya mtu huyu, basi mambo mbalimbali yanayohusiana na mahali alipozaliwa mtu huyo, familia, jinsia, umbo, na mambo mengine kama hayo ambayo yanahusishwa na kuzaliwa kwake, yote yanahusiana na maisha yake ya zamani na ya sasa. Hii inamaanisha kwamba, mambo mbalimbali yanayohusiana na kuzaliwa kwa mtu hayaathiriwi tu na maisha ya awali ya mtu, lakini yanaamuliwa na hatima ya mtu katika maisha ya sasa. Hii inaelezea mseto wa hali tofauti ambazo watu wanazaliwa: Baadhi wanazaliwa katika familia fukara, wengine katika familia tajiri. Baadhi wanazaliwa katika kundi la watu wa kawaida, wengine wanazaliwa katika ukoo wa kipekee. Baadhi wanazaliwa kusini, wengine wanazaliwa kaskazini. Baadhi wanazaliwa jangwani na wengine wanazaliwa katika ardhi zenye rutuba. Kuzaliwa kwa baadhi ya watu kunaandamana na vifijo, vicheko, na sherehe, wengine wanaleta machozi, janga, na matatizo. Baadhi wanazaliwa ili wathaminiwe, wengine wawekwe pembeni kama magugu. Baadhi wanazaliwa wakiwa na heshima na staha na wengine wanazaliwa wakiwa na mikosi na mikasa. Baadhi wanapendeza kuwatazama, na wengine wanatisha kuwatazama. Baadhi wanazaliwa usiku wa manane, wengine wanazaliwa chini ya jua kali la utosi. … Kuzaliwa kwa watu wa kila aina kunaamuliwa na hatima ambazo Muumba ameweka kwa ajili yao; kuzaliwa kwao kunaamua hatima zao katika maisha ya sasa pamoja na wajibu ambao wataendeleza na kazi maalum watakazotimiza. Yote haya yanategemea ukuu wa Muumba, ulioamuliwa kabla na Yeye; hakuna anayeweza kuepuka hatima hii iliyoamuliwa kabla, hakuna anayeweza kubadilisha kuzaliwa kwao, na hakuna anayeweza kuchagua hatima yake binafsi.

Awamu ya Pili: Kukua

Kulingana na aina ya familia ambayo wamezaliwa ndani, watu hukua katika mazingira tofauti ya nyumbani na wakajifunza mafunzo tofauti kutoka kwa wazazi wao. Sababu hizi zinaamua hali ambazo mtu atakulia na kukua inawakilisha awamu ya pili muhimu ya maisha ya mtu. Inajulikana kwamba, watu hawana chaguo katika awamu hii, vilevile. Hii pia imepangwa, ilipangwa kabla.

1) Hali Ambazo Mtu Hukulia Ndani Zimepangwa na Muumba

Mtu hawezi kuchagua watu, matukio au vitu anavyoadilishwa na kushawishiwa navyo anapokua. Mtu hawezi kuchagua ni maarifa au mbinu gani atapata, ni tabia gani ataishia kuwa nayo. Mtu hana kauli kuhusiana na wazazi na watu wake wa ukoo, aina ya mazingira ambayo atakulia ndani; mahusiano yake na watu, matukio, na mambo yaliyo katika mazingira yake na namna yanavyoathiri maendeleo yake, vyote viko nje ya udhibiti wake. Ni nani anayeamua mambo haya, basi? Ni nani anayeyapangilia? Kwa sababu watu hawana chaguo katika suala hili, kwa vile hawawezi kuamua mambo haya wao wenyewe, na kwa sababu bila shaka hayajipangi yenyewe kwa kawaida, ni wazi kabisa kwamba kuundwa kwa watu, matukio na vitu hivi vyote kunategemea mikono ya Muumba. Bila shaka, kama vile tu Muumba anavyopanga hali fulani za kuzaliwa kwa kila mtu, Yeye hupangilia pia hali mahususi ambazo mtu hukulia. Ikiwa kuzaliwa kwa mtu kutaleta mabadiliko kwa watu, kwa matukio, na mambo yanayomzunguka yeye, basi kukua na maendeleo ya mtu huyo vyote vitaweza kuwaathiri vilevile. Kwa mfano, baadhi ya watu wanazaliwa katika familia fukara, lakini wanalelewa wakiwa wamezungukwa na utajiri; wengine wanazaliwa katika familia tajiri lakini husababisha utajiri wa familia zao kupungua, kiasi cha kwamba wanalelewa katika mazingira ya kimaskini. Hakuna mtu anayezaliwa chini ya sheria maalum, na hakuna anayelelewa katika hali zisizozuilika, na zisizobadilika. Haya si mambo ambayo binadamu anaweza kufikiria au kudhibiti; mambo haya yote ni mazao ya hatima ya mtu, na yanaamuliwa na hatima ya mtu. Bila shaka, kimsingi ni kwamba yote haya yaliamuliwa kabla katika hatima ya mtu na Muumba, yanaamuliwa na ukuu wa Muumba juu ya, na mipango Yake ya, hatima ya mtu huyu.

2) Hali Mbalimbali Ambazo Watu Hukulia Ndani Husababisha Wajibu Tofauti

Hali za kuzaliwa kwa mtu huanzisha katika kiwango cha kimsingi mazingira na hali ambazo atakulia ndani, na hali ambazo mtu hukulia ndani vilevile ni zao la hali za kuzaliwa kwake. Kwenye wakati huu mtu anaanza kujifunza lugha, na akili za mtu zinaanza kukumbana na kuchanganua mambo mengi mapya, na katika mchakato huu mtu anakua bila kusita. Mambo ambayo mtu anasikia kwa masikio yake, anaona kwa macho yake, na anang’amua kwa akili zake huboresha na kuhuisha kwa utaratibu ulimwengu wa ndani wa mtu. Watu, matukio, na mambo ambayo mtu anakumbana nayo, akili ya kawaida, maarifa, na mbinu anazojifunza, na njia za kufikiria ambazo mtu anaathiriwa nazo, anaambiwa au kufunzwa, vyote vitamwongoza na kuathiri hatima ya maisha yake. Lugha anayojifunza mtu anapokua na njia yake ya kufikiria haviwezi kutenganishwa kutoka kwenye mazingira ambayo yeye analelewa katika ujana wake, na hayo mazingira yana wazazi, ndugu zake, na watu wengine, matukio, na mambo yanayomzunguka. Kwa hivyo mkondo wa maendeleo ya mtu unaamuliwa na mazingira ambayo yeye anakulia ndani, na pia unategemea watu, matukio, na mambo ambayo mtu anakumbana nayo kwenye kipindi hiki cha muda. Kwa sababu masharti ambayo mtu hukulia ndani yaliamuliwa kabla na tena mapema mno, mazingira anayoishi kwenye mchakato huu pia, kwa kawaida, yaliamuliwa kabla. Hayaamuliwi na chaguo na mapendeleo ya mtu, lakini yanaamuliwa kulingana na mipango ya Muumba, yanaamuliwa na mipangilio makinifu ya Muumba, na ukuu wa Muumba juu ya hatima ya mtu huyo katika maisha. Kwa hivyo watu ambao mtu yeyote hukumbana nao katika mkondo wa kukua, na mambo ambayo mtu hukutana nayo, vyote vimeunganishwa bila kuzuilika kwa mipango na mipangilio ya Muumba. Watu hawawezi kutabiri aina hizi za mahusiano yaliyo magumu kuelezeka, wala hawawezi kuyadhibiti au kuweza kuyaelewa. Mambo mengi tofauti na watu wengi tofauti wanao mwelekeo wa mazingira ambayo mtu hukulia, na hakuna binadamu anayeweza kupangilia na kupanga mtandao mpana kama huo wa muunganisho. Hakuna mtu au kitu isipokuwa Muumba anayeweza kudhibiti kujitokeza, kuwepo, na kutoweka kwa watu mbalimbali, matukio na mambo, na ni mtandao mpana ajabu wa muunganisho unaounda maendeleo ya mtu kama ilivyoamuliwa kabla na Muumba, na kuunda mazingira tofauti ambayo watu wanakulia ndani, na kuunda wajibu mbalimbali unaohitajika kwa minajili ya kazi ya Muumba ya usimamizi, kuweka misingi thabiti, yenye nguvu ili watu waweze kukamilisha kwa ufanisi kazi yao maalum.

Awamu ya Tatu: Uhuru

Baada ya mtu kupitia utoto na wakati wake wa kubaleghe na kwa utaratibu bila kuzuilika kufikia ukomavu, hatua inayofuata ni kwake yeye kuachana kabisa na ujana wake, kuwaaga wazazi wake, na kukabiliana na barabara iliyo mbele yake akiwa mtu mzima huru. Wakati huo, lazima wakabiliane na watu, matukio na mambo yote ambayo mtu mzima lazima apitie, na kukabiliana na sehemu zote za hatima yake ambazo zitajiwasilisha hivi karibuni. Hii ndiyo awamu ya tatu ambayo lazima mtu apitie.

1) Baada ya Kuwa Huru, Mtu Huanza Kupitia Ukuu wa Muumba

Kama kuzaliwa kwa mtu na kulelewa kwake ni “kipindi cha matayarisho” katika safari ya mtu maishani, kuweka lile jiwe la msingi katika hatima ya mtu, basi uhuru wa mtu ndio ufunguzi wa pekee wa hatima ya maisha ya mtu. Kama kuzaliwa na kukua kwa mtu ni utajiri ambao wameweza kulimbikiza kwa minajili ya hatima yao maishani, basi uhuru wa mtu huyo unaanza wakati ule wanaanza kutumia au kuongeza utajiri huo. Wakati mtu anawaacha wazazi na kuwa huru, masharti ya kijamii ambayo anakabiliana nayo, na aina ya kazi na ajira inayopatikana kwa mtu, vyote vinaamriwa na hatima na havina uhusiano wowote na wazazi wa mtu. Baadhi ya watu huchagua kozi nzuri chuoni na kuishia kupata kazi ya kuridhisha baada ya kuhitimu, na hivyo basi kupiga hatua ya kwanza ya mafanikio katika safari yao ya maisha. Baadhi ya watu hujifunza na kumiliki ujuzi mwingi wa aina tofauti na kamwe hawapati kazi ambayo inawafaa au kupata vyeo vyao, sembuse kuwa na ajira yoyote; wakati wa safari ya maisha yao wanajipata wakiwa wamewekewa vipingamizi katika kila kona, wameandamwa na matatizo, matumaini yao madogo na maisha yao hayana uhakika. Baadhi ya watu wanatia bidii katika masomo yao, ilhali wanakosa kwa karibu sana fursa zao zote za kupokea elimu ya juu zaidi, na wanaonekana kuwa na hatima ya kutoweza kupata mafanikio, matamanio yao ya kwanza kabisa katika safari yao ya maisha yalitowekea tu hewani. Bila kujua kama barabara iliyo mbele ni laini au yenye miamba, wanahisi kwa mara ya kwanza namna ambavyo hatima ya binadamu imejaa vitu vya kubadilikabadilika, na wanachukulia maisha kwa tumaini na hofu. Baadhi ya watu, licha ya kutokuwa na elimu nzuri sana, huandika vitabu na kutimiza kiwango cha umaarufu; baadhi, ingawaje hawajui kusoma na kuandika sana, huunda pesa katika biashara na hivyo basi wanaweza kujikidhi…. Kazi anayochagua mtu, namna mtu anavyopata riziki: je, watu wanao udhibiti wowote kuhusu, kama wanaweza kufanya uchaguzi mzuri au uchaguzi mbaya? Je, yanapatana na matamanio na uamuzi wao? Watu wengi zaidi wanatamani wangeweza kufanya kazi kidogo na kupata mapato mengi zaidi, wasitie bidii sana katika jua na mvua, wavae vizuri, wameremete na kung’aa wakiwa kila pahali, wawe juu sana kuliko wengine kwa uwezo, na kuleta heshima kwa mababu zao. Matamanio ya watu ni kamilifu sana, lakini wakati ambao watu wanachukua hatua zao za kwanza katika safari ya maisha yao, polepole wanakuja kutambua jinsi ambavyo hatima ya mwanadamu si kamilifu, na kwa mara ya kwanza wanafahamu ukweli kwamba, ingawa mtu anaweza kufanya mipango thabiti kwa ajili ya maisha yake yajayo, ingawa mtu anaweza kuhodhi ndoto za kijasiri, hakuna yule aliye na uwezo au nguvu za kutambua ndoto zake mwenyewe, hakuna yule aliye katika hali ya kudhibiti mustakabali wake. Siku zote kutakuwepo na umbali fulani kati ya ndoto za mtu na uhalisia ambao lazima mtu akabiliane nao; mambo siku zote hayawi vile ambavyo mtu angetaka yawe, na watu wanapokumbwa na uhalisi kama huu hawawezi kutimiza hali ya kutosheka au kuridhika. Baadhi ya watu wataenda hadi kiwango chochote cha kufikirika, wataweza kutia bidii za kipekee na kujitolea pakubwa kwa minajili ya riziki na mustakabali wao, katika kujaribu kubadilisha hatima yao wenyewe. Lakini hatimaye, hata kama wataweza kutambua ndoto na matamanio yao kupitia kwa njia ya bidii yao wenyewe, hawawezi kubadilisha hatima zao, na haijalishi watajaribu vipi kwa njia ya ukaidi hawatawahi kuzidi kile ambacho hatima yao imewapangia. Licha ya tofauti katika uwezo, kiwango cha akili, na hiari ya kutenda, watu wote ni sawa mbele ya hatima, jambo ambalo halileti tofauti kati ya wakubwa na wadogo, wale wa kiwango kile cha juu na cha chini, wanaotukuzwa na wakatili. Ile kazi ambayo mtu anafuatilia, kile anachofanya mtu ili kupata riziki, na kiasi gani cha mali anachokusanya maishani hakiamuliwi na wazazi wa mtu, vipaji vya mtu, jitihada za mtu au malengo ya mtu, vyote vinaamuliwa kabla na Muumba.

2) Kuwaacha Wazazi wa Mtu na Kuanza kwa Bidii Kuendeleza Wajibu Wako Kwenye Ukumbi wa Sanaa wa Maisha

Wakati mtu anapofikia ukomavu, mtu anaweza kuacha wazazi wake na kutoka nje kwenda kuanza kujitegemea yeye mwenyewe na ni katika wakati huu ambapo mtu huanza kwa kweli kuonyesha wajibu wake binafsi, kwamba kazi maalum ya mtu maishani inaacha kuwa ya kutoeleweka na polepole kuanza kuwa wazi. Kimsingi mtu huyo bado huonyesha uhusiano wa karibu na wazazi wake, lakini kwa sababu kazi yake maalum na wajibu anaoendeleza katika maisha huwa hauna uhusiano wowote na mama na baba wa mtu huyo, kwa hakika uhusiano huu wa karibu huvunjika polepole kwa kadiri ambavyo mtu anazidi kuendelea kuwa huru. Kutoka katika mtazamo wa kibiolojia, watu bado hawana budi kutegemea wazazi katika njia za kufichika akilini, lakini kwa kusema ukweli, mara tu wanapokuwa watu wazima wanakua na maisha tofauti kabisa na yale ya wazazi wao, na wataweza kutekeleza wajibu watakaoamua kufanya kwa uhuru wao. Mbali na kuwazaa na kuwalea watoto, jukumu la kila mzazi katika maisha ya mtoto ni kuweza kuwapatia tu mazingira rasmi ya kukulia ndani, kwa maana hakuna kingine chochote isipokuwa kule kuamuliwa kabla kwa Muumba ambako kunachukua mwelekeo katika hatima ya mtu huyu husika. Hakuna anayeweza kudhibiti ni mustakabali gani ambao mtu atakuwa nao; huwa umeamuliwa kabla na mapema sana, na hata wazazi wa mtu hawawezi kubadilisha hatima yake. Kulingana na mambo ya hatima, kila mtu yuko huru na kila mtu anayo hatima yake. Kwa hivyo hakuna wazazi wa mtu yeyote wanaoweza kuiondoa hatima ya mtu katika maisha au kusisitizia ushawishi wowote ule mdogo katika wajibu ambao mtu huendeleza maishani. Inaweza kusemekana kwamba, familia ambayo mtu ameamuliwa kuzaliwa ndani, na mazingira ambayo mtu atakulia ndani, ni yale masharti ya awali ya kutimiza kazi maalum ya mtu maishani. Yote haya hayaamui kwa vyovyote vile hatima ya mtu katika maisha au aina ya hatima ambayo mtu huyo atatimiza katika kazi yake maalum. Na kwa hivyo hakuna wazazi wa mtu yeyote yule wanaweza kusaidia katika kutimiza kazi hii maalum katika maisha, hakuna watu wowote wa ukoo wanaoweza kumsaidia mtu kuchukua wajibu huu katika maisha. Vile ambavyo mtu hutimiza kazi yake maalum na katika aina gani ya mazingira ya kuishi ambayo mtu hutekeleza wajibu wake, vyote vinaamuliwa na hatima ya mtu maishani. Kwa maneno mengine, hakuna masharti mengine yoyote yanayoweza kuathiri kazi maalum ya mtu, ambayo imeamuliwa kabla na Muumba. Watu wote hukomaa katika mazingira yao binafsi ya kukulia, na kisha kwa taratibu, hatua kwa hatua, huanza safari katika barabara zao binafsi za maisha, hutimiza hatima walizopangiwa na Muumba, kwa kawaida, bila hiari wao huingia katika bahari kubwa ya binadamu na kuchukua nafasi zao binafsi katika maisha, pale ambapo wao huanza kutimiza majukumu yao kama viumbe vilivyoumbwa kwa minajili ya kuamuliwa kabla kwa Muumba, kwa minajili ya ukuu Wake.

Awamu ya Nne: Ndoa

Kadiri mtu anavyokua na kukomaa, ndivyo anavyozidi kuwa mbali na wazazi wake na mazingira ambayo amezaliwa na kulelewa, na badala yake mtu huanza kutafuta mwelekeo wa maisha yake na kufuatilia shabaha binafsi kwa njia ya maisha iliyo tofauti na ile ya wazazi. Kwenye kipindi hiki cha muda mtu hahitaji tena wazazi wake, bali mwandani ambaye anaweza kuishi naye katika maisha yake: mwenza, ni mtu ambaye hatima ya mtu imefungamanishwa naye kwa karibu. Kwa njia hii, tukio kuu ambalo mtu hukabiliana nalo kufuatia uhuru wake ni ndoa, awamu ya nne ambayo lazima mtu apitie.

1) Mtu Hana Chaguo Kuhusu Ndoa

Ndoa ni tukio muhimu katika maisha ya mtu yeyote; ni wakati ule ambao mtu huanza kwa kweli kuendeleza aina mbalimbali za majukumu, huanza kwa utaratibu kutimiza aina mbalimbali za kazi maalum. Watu huwa na picha nyingi kuhusu ndoa kabla ya kuipitia wao wenyewe, na picha hizi zote ni nzuri. Wanawake hufikiria kwamba waume wao watakuwa Kaka Mwenye Mvuto na Haiba, nao wanaume hufikiria kwamba wataweza kuoa Binti wa Kifalme Anayependeza. Kubuni huku kwa mawazo kunaonyesha kwamba kila mtu anayo mahitaji fulani ya ndoa, orodha fulani ya kile anachohitaji na viwango anavyopenda. Ingawaje katika enzi hii ya maovu watu wanaambiwa kila mara kuhusu ujumbe uliopotoka juu ya ndoa, hali ambayo husababisha hata mahitaji mengi zaidi, pamoja na kupatia watu aina zote za mizigo na mitazamo isiyo ya kawaida, mtu yeyote aliyepitia ndoa anajua kwamba haijalishi ni kiasi kipi ambacho mtu ataielewa, haijalishi pia mtu anao mtazamo gani katika ndoa hiyo, ndoa si suala la chaguo la mtu binafsi.

Mtu hukumbana na watu wengi katika maisha yake, lakini hakuna anayejua ni nani atakayekuwa mwandani wake katika ndoa. Ingawaje kila mtu anazo fikira zake binafsi na mtazamo wake wa kibinafsi kuhusu suala la ndoa, hakuna anayeweza kuona mbele na kujua ni nani atakayekuwa mwandani wake wa kweli hatimaye, na fikira za mtu huwa zinachangia kidogo sana. Baada ya kukutana na mtu unayempenda, unaweza kumfuatilia mtu huyo; kama mtu huyo amevutiwa na wewe au la, kama mtu huyo anaweza kuwa mwandani wako au la, hilo si la kwako kuamua. Kiini cha mahaba yenu si haswa mtu ambaye utaweza kuishi naye katika maisha yako; na huku haya yakiendelea mtu ambaye hukuwahi kumtarajia anaingia katika maisha yako na kuwa mwandani wako, anakuwa msingi muhimu sana katika hatima yako, nusu yako ile nyingine, ambaye hatima yako imefungamanishwa naye ajabu. Na kwa hiyo, ingawaje kunazo ndoa milioni kwa milioni ulimwenguni, kila ndoa ni tofauti: Ni ndoa ngapi ambazo hazitoshelezi, ni ngapi zinayo furaha; ni ngapi zinazopatikana Mashariki na Magharibi, ni ngapi Kaskazini na Kusini; ni ngapi ambazo wanandoa wanafaa na wameendana, na ni ngapi ambazo wanandoa wana mwonekano bora ni ngapi zenye furaha na utulivu, ni ngapi zenye maumivu na huzuni; ni ngapi zinaonewa wivu na wengine, na ni ngapi hazieleweki na hazipendelewi kabisa; ni ngapi zimejaa furaha, na ni ngapi zimejaa machozi na zinakatisha tamaa…. Kwenye ndoa hizi zote, binadamu wanafichua utiifu na kujitolea kwa maisha katika ndoa hizo, au pendo, au mshikamano, na hali ya kutotenganishwa, au kukata tamaa na kutoeleweka, au usaliti, au hata chuki. Haijalishi kama ndoa inaleta furaha au maumivu, kazi maalum ya kila mmoja katika ndoa iliamuliwa kabla na Muumba na haitabadilika; kila mmoja lazima aitimize. Na hatima ya kila mtu iliyopo nyuma ya kila ndoa haibadiliki; iliamuliwa kitambo naye Muumba.

2) Ndoa Inazaliwa Kutokana na Hatima ya Wandani Wote Wawili

Ndoa ni awamu muhimu katika maisha ya mtu. Ni zao la hatima ya mtu, kiungo muhimu katika hatima ya mtu; haiundwi kwa misingi ya uamuzi wa mtu yeyote binafsi au mapendeleo yake, na haiathiriwi na mambo yoyote ya nje, lakini inaamuliwa kabisa na hatima za wandani wawili, kupitia kwa mipangilio ya Muumba na kuamuliwa kabla kwa Muumba kuhusiana na hatima za wanandoa hao. Ukiangalia juujuu, kusudi la ndoa ni kuendeleza kizazi cha binadamu, lakini kwa kweli ndoa si chochote ila ni utaratibu ambao mtu anapitia katika mchakato wa kutimiza kazi yake maalum. Wajibu mbalimbali ambao watu huendeleza katika ndoa si ule tu wa kuleta kizazi kinachofuata; kunao wajibu mbalimbali ambao mtu huwa anao na kazi maalum ambazo mtu lazima atimize kwenye mkondo wa kuendeleza ndoa. Kwa sababu kuzaliwa kwa mtu huathiri mabadiliko ya watu, matukio, na mambo yanayomzunguka, ndoa ya mtu itaweza pia kuathiri bila shaka watu hao, na zaidi itawabadilisha kwa njia tofauti.

Wakati mtu anapokuwa huru, mtu huanza safari yake binafsi ya maisha, inayoongoza mtu hatua kwa hatua kuelekea kwa watu, na kwa matukio, na kwa vitu vinavyohusiana na ndoa ya mtu; na wakati uo huo, yule mtu mwingine atakayeunda ile ndoa anakaribia, hatua kwa hatua, kuelekea watu hao hao, matukio na hata mambo. Kwenye ukuu wa Muumba, watu wawili wasiohusiana walio na hatima inayohusiana wanaingia kwa utaratibu kwenye ndoa na kuwa, kimiujiza, familia, “nzige wawili wanaoshikilia kamba moja.” Kwa hivyo mtu anapoingia kwenye ndoa, safari ya mtu katika maisha itaathiri na kumgusa yule mwenzake, na vilevile safari ya mwandani katika maisha itashawishi na kugusa hatima ya yule mwenzake katika maisha. Kwa maneno mengine, hatima za wanadamu zimeingiliana na hakuna yule anayeweza kutimiza kazi yake maalum maishani au kutekeleza wajibu wake kabisa akiwa huru mbali na wengine. Kuzaliwa kwa mtu kunao mwelekeo kwa msururu mkubwa wa mahusiano; kukua pia kunahusisha msururu mkubwa wa mahusiano; na vilevile, ndoa inakuwepo bila shaka na kuendelezwa katika mtandao mpana na mgumu wa miunganisho ya binadamu, ikihusisha kila mwanachama na kuathiri hatima ya kila mmoja ambaye ni sehemu yake. Ndoa si mazao ya familia za wanachama wale wawili, hali ambazo wao walilelewa, maumbo yao, umri wao, ubora wao, vipaji vyao, au mambo mengine yoyote; badala yake, inatokana na kazi maalum ya pamoja na hatima inayohusiana. Hii ndiyo asili ya ndoa, zao la hatima ya binadamu lililopangwa na lililopangiliwa na Muumba.

Awamu ya Tano: Uzao

Baada ya kuoa, mtu anaanza kulea kizazi kijacho. Mtu hana uwezo wa kujua atakuwa na watoto wangapi na watoto hawa watakuwa wa aina gani; hili pia linaamuliwa na hatima ya mtu, iliyoamuliwa kabla na Muumba. Hii ndiyo awamu ya tano ambayo lazima mtu apitie.

Ikiwa mtu amezaliwa ili kutimiza wajibu wake akiwa mwana wa binadamu, basi kulea kizazi kijacho ni kutimiza wajibu wake akiwa kama mzazi wa mwingine. Mabadiliko haya ya majukumu yanamruhusu mtu apate uzoefu wa awamu tofauti za maisha kutoka kwa mitazamo tofauti. Pia yanampa mtu uzoefu tofauti wa mambo mbalimbali katika maisha, ambapo mtu anakuja kujua ukuu ule wa Muumba, pamoja na ukweli kwamba hakuna mtu anayeweza kuzidi au kubadilisha kile ambacho Muumba aliamua kabla.

1) Mtu Hana Udhibiti wa Hatima ya Uzao Wake

Kuzaliwa, kukua, na kuoa ni awamu ambazo zinaleta aina tofauti na viwango tofauti vya masikitiko. Baadhi ya watu hawatosheki na familia zao au maumbile yao ya kimwili; baadhi hawapendi wazazi wao; baadhi wanachukia au wanalalamikia mazingira ambayo walikulia ndani. Na kwa baadhi ya watu wengi, miongoni mwa masikitiko haya yote, ndoa ndiyo ambayo haitoshelezi zaidi. Licha ya vile ambavyo unayo masikitiko kwa kuzaliwa kwako, au kukua kwako, au ndoa yako, kila mmoja ambaye amepitia awamu hizi amejua kwamba hawezi kuchagua ni wapi au ni lini alizaliwa, ni vipi anavyofanana, wazazi wake ni nani, na mume au mke wake ni nani, lakini wanaweza kukubali tu mapenzi ya Mbinguni. Lakini wakati wa watu kulea kizazi kijacho unapowadia, wataweza kuweka matamanio yao yote ambayo hayajatimizwa katika nusu ya kwanza ya maisha yao kwenye vizazi vyao, wakitumai kwamba, uzao wao utajaliza sehemu ile ambayo wao wamepitia masikitiko, kwenye nusu ile ya kwanza ya maisha yao. Kwa hivyo watu hujihusisha katika kutunga taswira za aina zote kuhusu watoto wao: kwamba binti zao watakua na kuwa warembo ajabu, watoto wao wa kiume watakuwa wanaume wa kipekee; kwamba binti zao watakuwa na maadili na wenye vipaji nao watoto wao wa kiume watakuwa wanafunzi werevu, na wanariadha wa kusifika; na kwamba binti zao watakuwa watulivu na waadilifu, wenye busara, kwamba watoto wao wa kiume watakuwa wenye akili, wenye uwezo na wanaojali. Wanatumai kwamba wawe watoto wa kike au wa kiume wataheshimu wazee wao, watajali wazazi wao, watapendwa na kusifiwa na kila mmoja…. Kufikia hapa matumaini ya maisha yanajitokeza upya, na matamanio mapya yanapata nguvu katika mioyo ya watu. Watu wanajua kwamba hawana nguvu na tumaini katika maisha haya, kwamba hawatakuwa na fursa nyingine, tumaini jingine, la kujitokeza mbele ya watu, na kwamba hawana chaguo lolote ila kukubali hatima zao. Na kwa hivyo wanaelekeza matumaini yao yote, matamanio na maadili yao ambayo hayajatimizwa, hadi kwenye kizazi kijacho, wakitumai uzao wao unaweza kuwasaidia kutimiza ndoto zao na kutambua matamanio yao; na kwamba binti zao na watoto wao wa kiume wataleta utukufu katika jina la familia, kuwa muhimu, kuwa matajiri au maarufu; kwa ufupi, wanataka kuona bahati za watoto wao zikizidi kuongezeka. Mipango na taswira za watu ni timilifu; Je, hawajui kwamba idadi ya watoto walio nao, umbo lao, uwezo wao na kadhalika, si juu yao kuamua, kwamba hatima za watoto wao hazimo kamwe katika viganja vya mikono yao? Binadamu si waendeshaji wa hatima zao binafsi, ilhali wanatumai kubadilisha hatima ya kizazi kichanga zaidi; hawana nguvu za kutoroka hatima zao wenyewe, ilhali, wanajaribu kudhibiti zile za watoto wao wa kiume ni wa kike. Je, hawazidishi ukadiriaji wao? Je, huu si ujinga na hali ya kutojua kwa upande wa binadamu? Watu huenda kwa mapana yoyote kwa minajili ya uzao wao, lakini hatimaye, idadi ya watoto aliyonayo mtu, na vile ambavyo watoto wake walivyo, si jibu la mipango na matamanio yao. Baadhi ya watu hawana hela lakini wanazaa watoto wengi; baadhi ya watu ni matajiri ilhali hawana mtoto. Baadhi wanataka binti lakini wananyimwa tamanio hilo; baadhi wanataka mtoto wa kiume lakini wanashindwa kuzaa mtoto wa kiume. Kwa baadhi, watoto ni baraka; kwa wengine, mtoto ni laana. Baadhi ya wanandoa ni werevu, ilhali wanawazaa watoto wanaoelewa polepole; baadhi ya wazazi ni wenye bidii na waaminifu, ilhali watoto wanaowalea ni wavivu. Baadhi ya wazazi ni wapole na wanyofu lakini wana watoto wanaogeuka na kuwa wajanja na wenye chuki. Baadhi ya wazazi ni wazima kiakili na kimwili lakini wanajifungua watoto walemavu. Baadhi ya wazazi ni wa kawaida na hawajafanikiwa ilhali watoto wao wanafanikiwa pakubwa. Baadhi ya wazazi ni wa hadhi ya chini ilhali watoto wanaowalea ni wenye taadhima. …

2) Baada ya Kulea Kizazi Kijacho, Watu Wanapata Ufahamu Mpya Kuhusu Hatima

Watu wengi wanaooa hufanya hivyo karibu kwenye umri wa miaka thelathini, na kwa wakati huu wa maisha, mtu hana ufahamu wowote wa hatima ya binadamu. Lakini wakati watu wanapoanza kulea watoto, kwa kadri uzao wao unapokua, wanatazama kizazi kipya kikirudia maisha na hali zote walizopitia katika kizazi kilichopita, na wanaona maisha yao ya kale yakijionyesha kwao na wanatambua kwamba barabara inayotumiwa na kizazi kile kichanga zaidi, kama tu yao, haiwezi kupangwa wala kuchaguliwa. Wakiwa wamekabiliwa na hoja hii, hawana chaguo lolote bali kukubali kwamba hatima ya kila mtu iliamuliwa kabla; na bila ya hata kutambua wanaanza kwa utaratibu kuweka pembeni matamanio yao binafsi, na hisia kali katika mioyo yao inapungua na kuwatoka…. Kwenye kipindi hiki cha muda, mtu ameweza kupita sehemu nyingi zaidi na muhimu katika mafanikio ya maisha yake na ametimiza ufahamu mpya wa maisha, na kuchukua mtazamo mpya. Je, mtu wa umri huu anaweza kutarajia kwa siku za usoni kiasi kipi cha mambo na ni matarajio yapi wanayoyatazamia? Ni mwanamke yupi mwenye umri wa miaka hamsini angali anaota kuhusu Kaka Mwenye Mvuto na Haiba? Ni mwanamume yupi wa miaka hamsini angali anatafuta Binti wa Kifalme Anayependeza? Ni mwanamke yupi wa umri wa kati atakuwa anatumai kugeuka kutoka kwa mtoto wa bata mwenye sura mbaya hadi kuwa batamaji? Je, wanaume wazee zaidi wangali wana msukumo sawa wa ajira na wanaume vijana? Kwa ujumla, haijalishi kama mtu ni mwanamume au mwanamke, yeyote anayeishi na kuufikia umri huu anao uwezekano wa kuwa na mtazamo unaofaa kwa kiasi fulani, utakaoweza kutumika kwenye ndoa, familia, na watoto. Mtu kama huyo, kimsingi hana chaguo zozote zilizobakia, hana msukumo wowote wa kukabiliana na hatima yake. Kwa mujibu wa kile ambacho binadamu amepitia, punde tu mtu anapofikia umri huu mtu huanza kwa kawaida kuwa na mtazamo kwamba “lazima mtu akubali hatima yake; watoto wa mtu wana majaliwa yao binafsi binafsi; hatima ya binadamu Imepangwa na Mbingu.” Watu wengi ambao hawaelewi ukweli, baada ya kupitia mabadiliko, mahangaiko, na ugumu wote wa ulimwengu huu, watatoa muhtasari wa utambuzi wao wa maisha ya binadamu kwa maneno matatu: “Hiyo ndiyo hatima!” Ingawaje kauli hii inatoa muhtasari wa hitimisho ya watu wa ulimwengu na utambuzi kuhusu hatima ya binadamu, ingawaje inaelezea kutoweza kusaidika kwa binadamu na inaweza kusemekana kwamba inapenyeza na ni sahihi, ni kilio cha mbali kutoka kwa ufahamu wa ukuu wa Muumba, na haichukui nafasi ya maarifa ya mamlaka ya Muumba.

3) Kusadiki Katika Hatima si Mbadala wa Maarifa ya Ukuu wa Muumba

Baada ya kuwa wafuasi wa Mungu kwa miaka mingi, je, kunayo tofauti kubwa katika maarifa yenu ya hatima na yale ya watu wa ulimwengu? Je, mmeelewa kwa kweli kule kuamuliwa kabla kwa Muumba, na unaweza kujua kwa kweli ukuu wa Muumba? Baadhi ya watu wanao ufahamu wa kina, na hisia za ndani za kauli hii “hii ndiyo hatima,” ilhali hawasadiki hata kidogo katika ukuu wa Mungu, hawasadiki kwamba hatima ya binadamu hupangiliwa na kuratibiwa na Mungu, na hawako radhi kunyenyekea mbele ya ukuu wa Mungu. Watu kama hao ni kana kwamba wanaelea baharini, wanatoswatoswa na mawimbi, huku wakielea na kufuata mkondo wa maji, wasiwe na chaguo ila kusubiri kimyakimya na kuachia maisha yao hatima. Hata hivyo hawatambui kwamba hatima ya binadamu inategemea ukuu wa Mungu; hawawezi kwa hiari yao wenyewe kuutambua ukuu wa Mungu, na hivyo kupata ufahamu wa mamlaka ya Mungu, kunyenyekea katika mipango na mipangilio ya Mungu, kuacha kukinzana na hatima na kuishi katika utunzwaji, ulinzi na mwongozo wa Mungu. Kwa maneno mengine, kukubali hatima si jambo sawa na kunyenyekea kwa ukuu wa Muumba; kusadiki katika hatima haimaanishi kwamba mtu anakubali, anatambua, na anajua ukuu wa Muumba; kusadiki katika hatima ni ule utambulisho wa hoja hii na suala hili la nje, ambalo ni tofauti na kujua namna Muumba Anavyotawala hatima ya binadamu, kuanzia katika kutambua kwamba Muumba ndiye chanzo cha kutawala juu ya hatima za mambo yote na hata zaidi kunyenyekea kwa mipango na mipangilio ya Muumba kwa ajili ya hatima ya binadamu. Tuseme kwamba mtu anaamini tu katika hatima, na hata anahisi kwa undani kuihusu, lakini kwa sababu hiyo hawezi kujua na kukubali mamlaka ya Muumba juu ya hatima za watu, kuyatii na kuyakubali. Katika hali hiyo, maisha yake yatakuwa ya kusikitisha; bila shaka yatakuwa yameishiwa bure, yatakuwa utupu. Bado hataweza kutii utawala wa Muumba, kuwa mwanadamu aliyeumbwa kwa maana halisi ya neno hilo, na kupata utambuzi wa Muumba. Mtu anayejua na kupitia mamlaka ya Muumba kwa kweli anapaswa kuwa katika hali chanya, si katika hali ambayo ni hasi au ya kukata tamaa. Huku akitambua kwamba haya yote yamepangwa, moyoni mwake anamiliki ufafanuzi sahihi wa maisha na hatima, ambao ni kwamba maisha yote ya mwanadamu yako chini ya mamlaka ya Muumba. Anapotazama nyuma kwenye njia aliyoitembea, anapokumbuka kila awamu ya safari yake ya maisha, anaona kwamba katika kila hatua, iwe kwamba safari yake ilikuwa ngumu au laini, Mungu alikuwa akiiongoza njia yake, Akiipanga kwa ajili yake. Anaelewa kwamba ilikuwa ni mipango ya Mungu ya uangalifu, pamoja na mipango Yake makini, iliyowaongoza, bila kujua, hadi kufikia leo. Anatambua kwamba kuweza kukubali mamlaka ya Muumba, kukubali wokovu Wake, ndiyo baraka kubwa zaidi katika maisha ya mtu! Kama mtu ana mtazamo hasi kuelekea hatima, inathibitisha kwamba anapinga kila kitu ambacho Mungu amempangia, kwamba hana mtazamo wa utiifu. Iwapo mtu ana mtazamo chanya kuelekea mamlaka ya Mungu juu ya hatima ya mwanadamu, basi anapotazama nyuma kwenye safari yake, anapopitia mamlaka ya Mungu kweli, atatamani zaidi kutii kila kitu ambacho Mungu amepanga, na atakuwa na azimio na imani zaidi ya kumwacha Mungu aipange hatima yake na kutomwasi Mungu tena. Hii ni kwa sababu anaona kwamba wakati watu hawajui hatima inahusu nini au hawaelewi mamlaka ya Mungu, anajitahidi kimakusudi na kujikwaa katika ukungu, na safari hiyo ni ngumu sana, na husababisha maumivu mengi ya moyo. Kwa hivyo watu wanapotambua kwamba Mungu ndiye mwenye mamlaka juu ya hatima ya mwanadamu, werevu huchagua kujua na kuyakubali mamlaka ya Mungu, na kuaga siku zenye uchungu za “kujaribu kuunda maisha mazuri kwa nguvu zao wenyewe,” badala ya kuendelea kupambana dhidi ya hatima na kufuatilia hayo wanayoita malengo yao ya maisha kwa njia yao wenyewe. Mtu anapokosa kuwa na Mungu, wakati hawezi kumwona, wakati hawezi kujua mamlaka ya Mungu kwa kweli na wazi, kila siku haina maana, haina thamani, na ni yenye uchungu usioelezeka. Haijalishi alipo mtu, na kazi yake ni ipi, njia yake ya kupata riziki na malengo anayofuatilia humletea tu uchungu wa moyo usio na mwisho, na maumivu ambayo ni vigumu kuyashinda, ambayo hawezi kuvumilia kuyakumbuka. Ni kwa kukubali mamlaka ya Muumba tu, kutii mipango na mipangilio Yake, na kufuatilia kufikia maisha ya kweli ya mwanadamu, ndiyo mtu anaweza kujikomboa polepole kutoka katika maumivu yote ya moyo na uchungu, na polepole kujiondolea utupu wote wa maisha ya mwanadamu.

4) Ni Wale tu Wanaonyenyekea kwa Ukuu wa Muumba Ndio Wanaoweza Kupata Uhuru wa Kweli

Kwa sababu watu hawatambui mipango ya Mungu, na ukuu wa Mungu, siku zote wanakabiliana na hatima hiyo kwa dharau, kwa mtazamo wa kuasi, na siku zote wanataka kutupilia mbali mamlaka na ukuu wa Mungu, na mambo yale ambayo hatima imewahifadhia, wakitumai kwamba watabadilisha hali zao za sasa na kubadilisha hatima yao. Lakini hawawezi kufaulu; wanazuiliwa kwa kila sehemu ya mabadiliko katika maisha. Mvutano huu, unaoendelea ndani ya nafsi ya mtu, ni wa maumivu; maumivu haya hayasahauliki; na wakati wote huu mtu anapoteza maisha yake mwenyewe. Sababu ya maumivu haya ni nini? Je, ni kwa sababu ya ukuu wa Mungu au kwa sababu ya mtu kuzaliwa bila bahati? Bila shaka kati ya sababu hizi hakuna iliyo ya kweli. Kimsingi, ni kwa sababu ya njia ambazo watu huchukua, njia ambazo watu huchagua kuishi katika maisha yao. Baadhi ya watu huenda wasitambue mambo haya. Lakini unapojua kwa kweli, unapotambua kwa kweli kwamba Mungu anao ukuu juu ya hatima ya binadamu, unapoelewa kwa kweli kwamba kila kitu ambacho Mungu amekupangilia na kukuamulia ni chenye manufaa makubwa, na ni ulinzi mkubwa, basi utahisi maumivu yako yakipungua polepole, na mwili wako utaanza kutulia, kuwa huru na kukombolewa. Tukitazama kutokana kwenye hali za watu wengi leo, ingawa wao wenyewe hawataki kuendelea kuishi kama walivyokuwa wakiishi awali, ingawa wanataka tulizo katika maumivu yao, kimsingi hawawezi kung’amua kwa kweli thamani na maana halisi ya ukuu wa Muumba juu ya hatima ya binadamu; hawawezi kutambua kwa kweli na kunyenyekea kwa ukuu wa Muumba, sembuse kujua namna ya kutafuta na kukubali mipango na mipangilio ya Muumba. Kwa hivyo kama watu hawawezi kutambua ukweli kwamba Muumba anao ukuu juu ya hatima ya binadamu na juu ya mambo yote ya binadamu, kama hawawezi kunyenyekea kwa kweli chini ya utawala wa Muumba, basi itakuwa vigumu sana kwao kutoendeshwa na kufungwa na, fikira hii kwamba “hatima ya mtu imo kwenye mikono ya mtu,” itakuwa vigumu kwao kutupilia mbali maumivu ya kung’ang’ana kwao kwingi dhidi ya hatima na mamlaka ya Muumba, ni wazi kwamba hali hii pia itakuwa ngumu kwao katika kuweza kukombolewa kwa kweli na kuwa huru, kuwa watu wanaomwabudu Mungu. Njia rahisi zaidi ya kujikomboa kutoka katika hali hii ni kuiaga kwaheri njia yako ya awali ya kuishi, kuaga kwaheri malengo yako ya maisha ya awali; kufanya muhtasari na kuchanganua njia ya kuishi ya awali, mtazamo wa maisha, mambo uliyoyafuatilia, matamanio, na hamu ya kupata vitu; na kisha kuyalinganisha haya yote na nia za na mahitaji ya Mungu kwa wanadamu, na kuona kama kuna yoyote kati ya hayo yanayolingana na nia za Mungu, kujua kama kuna yoyote kati ya hayo yanayolingana na mahitaji ya Mungu, iwapo kuna yoyote kati ya hayo yanayoleta maadili sahihi ya maisha, kumwongoza mtu kuelewa ukweli zaidi na zaidi, na kumruhusu mtu kuishi na ubinadamu na mfano wa mwanadamu. Unapochunguza mara kwa mara na kuchanganua malengo mbalimbali ambayo watu hufuatilia maishani na njia zao mbalimbali za kuishi, utapata kwamba hakuna hata moja kati ya hizo zote ambayo inaambatana na nia ya asili ya Muumba Aliyokuwa nayo alipowaumba binadamu. Zote hizi zinawavuta watu mbali na ukuu na mamlaka ya Muumba; zote ni mitego ambayo huwasababisha watu wawe wapotovu, na ambayo inawaelekeza jehanamu. Baada ya kutambua haya, unachopaswa kufanya ni kuachilia mtazamo wako wa zamani wa maisha, kuwa mbali na mitego mbalimbali, kumwachia Mungu kuchukua usukani wa maisha yako na kuyafanyia mipangilio, utafute tu kutii mipango na mwongozo wa Mungu bila kufanya chaguzi zako mwenyewe, na kuwa mtu anayemwabudu Mungu. Haya yote yanaonekana kuwa rahisi, lakini ni jambo gumu kufanya. Baadhi ya watu wanaweza kuvumilia maumivu yake, wengine hawawezi. Baadhi wako radhi kutii, wengine hawako radhi. Wale wasiokuwa radhi wanakosa tamanio na uamuzi wa kufanya hivyo; wanayo habari kamili kuhusu ukuu wa Mungu, wanajua vyema kabisa kwamba ni Mungu anayepanga na kupangilia hatima ya binadamu, na ilhali wangali wanang’ang’ana tu, bado hawajaridhiana na nafsi zao kuhusiana na kuziacha hatima zao kwenye kiganja cha mkono wa Mungu na kunyenyekea katika ukuu wa Mungu, na zaidi, wanachukia mipango na mipangilio ya Mungu. Kwa hivyo, siku zote kutakuwa na baadhi ya watu wanaotaka kujionea wenyewe kile wanachoweza kufanya; wanataka kubadilisha hatima zao wenyewe kwa mikono yao miwili, au kutimiza furaha kwa kutumia nguvu zao wenyewe, kuona kama wanaweza kukiuka mipaka ya mamlaka ya Mungu na kuinuka juu ya ukuu wa Mungu. Huzuni ya mwanadamu, sio juu ya yeye kutafuta maisha mazuri, si kwamba anatafuta umaarufu na utajiri au sio kwamba anapingana na hatima yake mwenyewe kwenye ukungu, lakini ni kwamba baada ya yeye kuona uwepo wa Muumba, baada ya yeye kujifunza ukweli kwamba Muumba anao ukuu juu ya hatima ya binadamu, bado hawezi kurekebisha njia zake, hawezi kuvuta miguu yake kutoka kwenye mtego, lakini anaufanya moyo wake kuwa mgumu na kudumu katika makosa yake. Afadhali aendelee kutapatapa kwenye matope, akishindana kwa ukaidi dhidi ya ukuu wa Muumba, akiupinga mpaka kufikia mwisho ulio na uchungu, bila hata chembe ya majuto. Ni mpaka pale tu anapolazwa akiwa amevunjika na anavuja damu ndipo anapoamua hatimaye kusalimu amri na kugeuka na kubadilisha mwenendo. Hii ni huzuni ya kweli ya mwanadamu. Kwa hivyo Ninasema, wale wanaochagua kunyenyekea ni wenye busara na wale waliochagua kutoroka ni wapumbavu kweli.

Awamu ya Sita: Kifo

Baada ya mahangaiko mengi na masikitiko mengi, na kuvunjwa moyo kwingi, baada ya furaha nyingi na huzuni nyingi na baada ya misukosuko ya maisha, baada ya miaka mingi sana isiyosahaulika, baada ya kutazama misimu ikipita na kujirudia, mtu hupita kwenye hatua muhimu sana ya maisha bila ya taarifa, na kwa ghafla tu mtu anajipata kwenye miaka yake ya kufifia. Alama za muda zimejichora kotekote kwenye mwili wa mtu: Mtu hawezi tena kusimama wima, kichwa cha nywele nyeusi kinageuka na kuwa cha nywele nyeupe, macho maangavu na mazuri yanabadilika na kuanza kuwa hafifu na kuwa na ukungu mbele yao, nayo ngozi laini, na inayong’aa inageuka na kuwa na makunyanzi na madoadoa. Usikivu wa mtu unaanza kudhoofika, meno yake yanaanza kulegea na kung'ooka, mwitikio wa mtu unaanza kuchelewachelewa, kutembea kunakuwa ni kwa kujikokota…. Wakati huu mtu ameaga kwaheri kabisa miaka yake ya nguvu ya ujana wake na kuingia katika maisha yake ya kwaheri: umri wa uzee. Kisha, mtu atakabiliana na kifo, awamu ya mwisho ya maisha ya binadamu.

1) Muumba Pekee Ndiye Anayeshikilia Nguvu ya Uzima na Mauti Juu ya Mwanadamu

Kama kuzaliwa kwa mtu kulipangiwa kutokana na maisha yake ya awali, basi kifo cha mtu kinaadhimisha mwisho wa hatima hiyo. Kama kuzaliwa kwa mtu ndiyo mwanzo wa kazi maalum ya mtu katika maisha haya, basi kifo cha mtu kinaashiria mwisho wa kazi hiyo maalum. Kwa sababu Muumba ameweka mpangilio maalum wa hali kwa ajili ya kuzaliwa kwa mtu, ni wazi kwamba Yeye pia Amepanga mpangilio maalum wa hali za kifo cha mtu. Kwa maneno mengine, hakuna anayezaliwa kwa bahati na hakuna kifo cha mtu kinachotokea kwa ghafla, na kuzaliwa kwa mtu na kifo chake vyote vina uhusiano na maisha ya mtu ya awali na ya sasa. Hali za kuzaliwa na kifo cha mtu, vyote viliamuliwa kabla na Muumba; hii ni kudura ya mtu, hatima ya mtu. Kwa kuwa kuna maelezo mengi ya kuzaliwa kwa mtu, ni kweli pia kwamba kifo cha kila mtu kitatokea chini ya hali maalum zinazotofautiana. Hii ndiyo sababu ya kutofautiana kwa urefu wa maisha ya watu, njia na nyakati tofauti za vifo vyao. Baadhi ya watu wana nguvu na afya na ilhali wanakufa mapema; wengine ni wanyonge na wanauguaugua ilhali wanaishi hadi umri wa uzee, na wanaaga dunia kwa amani. Baadhi ya watu hupoteza maisha kwenye matukio yasiyotarajiwa, na wengine hufariki kutokana na sababu za kawaida. Baadhi wanakata roho wakiwa mbali na nyumbani, wengine wanayafumba macho yao kwa mara ya mwisho wakiwa na wapendwa wao kando yao. Baadhi ya watu hufia angani, na wengine hufia chini ya ardhi. Wengine huzama chini ya maji, wengine nao kwenye majanga. Baadhi hufa asubuhi, wengine hufa usiku. … Kila mtu anataka kuzaliwa kwa heshima, kuwa na maisha mazuri, na kifo kitukufu, lakini hakuna mtu anayeweza kufika zaidi ya hatima yake mwenyewe, hakuna mtu anayeweza kukwepa ukuu wa Muumba. Hii ni hatima ya binadamu. Mwanadamu anaweza kupanga kila aina ya mipango kwa ajili ya maisha yake ya baadaye, lakini hakuna mtu anayeweza kupanga njia na muda wa kuzaliwa kwake na kuondoka kwake ulimwenguni. Ingawa watu wanajitahidi kadiri wawezavyo kuepuka na kuzuia ujio wa kifo chao, lakini bado, bila wao kujua, kifo huwa kinawakaribia kimyakimya. Hakuna ajuaye ni lini ataaga dunia na kwa njia ipi, sembuse kujua ni wapi ambapo hilo litatokea. Bila shaka, si binadamu wanaoshikilia nguvu za maisha na kifo, wala si kiumbe fulani kwenye ulimwengu wa asili, bali ni Muumba, ambaye mamlaka yake ni ya kipekee. Maisha na kifo cha binadamu si zao la sheria fulani ya ulimwengu wa asili, bali ni matokeo ya ukuu wa mamlaka ya Muumba.

2) Yule Asiyejua Ukuu wa Muumba Atahangaika kwa Woga wa Kifo

Wakati mtu anapoingia kwenye umri wa uzee, changamoto anazokabiliana nazo si kutosheleza mahitaji ya familia au kuanzisha maono makubwa katika maisha yake, bali ni namna ya kuyaaga maisha yake, namna ya kukutana na mwisho wa maisha yake, namna ya kuweka kikomo kwenye mwisho wa uwepo wake binafsi. Ingawa kwa juu juu inaonekana kwamba watu hawazingatii sana kifo, hakuna anayeweza kuepuka kuchunguza suala hili, kwani hakuna anayejua ikiwa kuna ulimwengu mwingine uliopo kwenye upande ule wa mbali wa kifo, ulimwengu ambao binadamu hawawezi kuuona au kuuhisi, ulimwengu wasiojua chochote kuuhusu. Hali hii huwafanya watu kuwa na wasiwasi kukabiliana na kifo moja kwa moja, wanaogopa kukikabili kama inavyostahili, na badala yake wanafanya kadri ya uwezo wao kuepuka mada hii. Na kwa hivyo mada hii humfanya kila mmoja kutishika kuhusu kifo, huongezea uzito kwenye fumbo hili kuhusiana na ukweli huu wa maisha usioepukika, ikiweka kivuli kisichoisha juu ya moyo wa kila mmoja.

Wakati mtu anapohisi mwili wake unaanza kudhoofika, wakati mtu anapohisi kwamba kifo chake kinakaribia, mtu anahisi wasiwasi na, woga usioelezeka. Woga wa kifo humfanya mtu kuhisi kuwa mpweke zaidi na asiyejiweza, na kwa wakati huu mtu hujiuliza: Nilitoka wapi? Ninakwenda wapi? Je, hivi ndivyo nitakavyokufa, huku maisha yangu yakinipita kwa haraka hivi? Je, huu ndio wakati unaodhihirisha mwisho wa maisha yangu? Ni nini, hatimaye, maana ya maisha? Maisha yana thamani gani, kwa kweli? Je, yanahusu umaarufu na utajiri? Je, yanahusu kulea familia? … Haijalishi kama mtu amewahi kufikiria maswali haya mahususi, haijalishi ni vipi mtu ana woga wa kifo, katika kina cha moyo wa kila mmoja siku zote kuna tamanio la kutaka kuchunguza zaidi mafumbo, kuna hisia fulani za sintofahamu kuhusu maisha, pamoja na hayo, kuna hisia za matukio yaliyopita yanayohusiana na ulimwengu huu, na kutotaka kuuacha. Pengine hakuna anayeweza kufafanua zaidi ni nini ambacho binadamu huogopa, ni nini ambacho binadamu hutaka kuchunguza zaidi, na nini kile ambacho ana uhusiano wa karibu nacho na kinachomfanya kutotaka kuondoka au kukiacha nyuma …

Kwa sababu wanaogopa kifo, watu huwa na wasiwasi mno; kwa vile wanaogopa kifo, vipo vitu vingi ambavyo hawawezi kuviachilia. Wakati wanakaribia kufa, baadhi ya watu huhangaika kuhusu hiki au kile; wanakuwa na wasiwasi kuhusu watoto wao, wapendwa wao, utajiri wao, ni kana kwamba kwa kuwa na wasiwasi hivyo wanaweza kuondoa mateso na hofu ambayo kifo huleta, ni kana kwamba kwa kuendeleza aina fulani ya urafiki wa karibu na wale wanaoishi wanaweza kukwepa ile hali ya kutoweza kujisaidia na upweke unaoandamana na kifo. Katika kina cha moyo wa binadamu kunao woga usio dhahiri, woga wa kutenganishwa na wapendwa wake, woga wa kutowahi kutazama tena anga la buluu, woga wa kutowahi kuutazama tena ulimwengu huu yakinifu. Nafsi pweke, iliyozoeana na wapendwa wake, inasita kuachilia maisha yake na kuondoka, ikiwa peke yake, kuelekea kwenye ulimwengu usiojulikana, usiozoeleka.

3) Maisha ya Kuishi Ukitafuta Umaarufu na Utajiri Yatamwacha Mtu Akiwa na Hasara Akikabiliana na Kifo

Kwa sababu ya ukuu na kuamuliwa kabla kwa Muumba, nafsi pweke iliyoanza bila chochote kwa jina lake huweza kupata wazazi na familia, fursa ya kuwa mwanachama wa kizazi cha binadamu, fursa ya kupitia maisha ya binadamu na kuona ulimwengu; na pia inafaidi fursa ya kupitia ukuu wa Muumba, kujua uzuri wa uumbaji wa Muumba, na zaidi kuliko vyote, kujua na kutii mamlaka ya Muumba. Lakini watu wengi zaidi huwa hawatumii vizuri fursa hii nadra na ya kipekee. Mtu hutumia nguvu zake zote maishani akipigana dhidi ya hatima yake, akitumia muda wake wote kushughulika akijaribu kuilisha familia yake na akisafiri huku na kule katika kutafuta utajiri na hadhi kwenye jamii. Mambo ambayo watu huthamini ni familia, pesa, na umaarufu; wanaona mambo haya kuwa mambo yenye thamani zaidi katika maisha. Watu wote wanalalamika kuhusu hatima zao, ilhali bado wanasukuma nyuma ya akili zao maswali ambayo ni ya lazima sana kuyachunguza na kuyaelewa: kwa nini binadamu yuko hai, namna ambavyo binadamu anafaa kuishi, ni nini maana na thamani ya maisha. Katika maisha yao yote, hata hivyo haijalishi ni miaka mingapi, wanaharakisha tu kutafuta umaarufu na utajiri, mpaka pale ujana wao unapowaacha, mpaka wanapokuwa na nywele za kijivu na makunyanzi kwenye nyuso zao; mpaka wanapogundua utajiri na umaarufu ni vitu visivyoweza kumzuia mtu kuelekea katika udhaifu unaotokana na uzee, kwamba pesa haiwezi kujaza utupu wa moyo: mpaka wanapoelewa kwamba hakuna mtu ambaye anaachwa nje kutoka kwenye sheria ya kuzaliwa, kuwa mzee, magonjwa, na kifo, kwamba hakuna mtu anayeweza kutoroka hatima ile inayomsubiri. Ni mpaka tu pale ambapo anapolazimishwa kukabiliana na awamu ya mwisho maishani ndipo anapoelewa kwa kweli kwamba hata kama mtu anamiliki mamilioni ya mali, hata kama mtu anayo heshima na cheo kikubwa, hakuna anayeweza kutoroka kifo, kwamba kila mtu atarudi kwenye sehemu yake asilia: nafsi pweke, bila chochote kwa jina lake. Wakati mtu anapokuwa na wazazi, mtu husadiki kwamba wazazi wa mtu ndio kila kitu; wakati mtu anapokuwa na mali, mtu hufikiri kwamba pesa ndiyo tegemeo la mtu, kwamba hiyo ndiyo njia ambayo kwayo mtu huishi; wakati watu wanapokuwa na hadhi katika jamii, wanaishikilia na hata wanaweza kuhatarisha maisha yao kwa ajili ya hadhi hiyo. Ni pale tu ambapo watu wanakaribia kuondoka ulimwenguni ndipo wanapotambua kwamba mambo yale waliyoishi katika maisha yao wakiyafuatilia si chochote bali mawingu yanayopita, hakuna chochote kati ya vitu hivi ambacho wanaweza kushikilia, hakuna hata chochote wanachoweza kwenda nacho, hakuna hata chochote kinachoweza kuwaondolea kifo, hakuna chochote kile kinachoweza kuwasindikiza au kutoa faraja kwa nafsi yao pweke inayoelekea kufa; na hata, hakuna kati ya hivyo vyote vinavyoweza kumpa mtu wokovu, na kuwaruhusu kushinda kifo. Umaarufu na utajiri ambao mtu hupata kwenye ulimwengu yakinifu humpa mtu hisia ya kuridhika kwa muda, furaha isiyodumu, hisia ya uwongo ya utulivu, na kumfanya mtu kupoteza njia. Na kwa hivyo watu, wanapong’ang’ana kila pahali kwenye bahari kubwa ya binadamu, wakitafuta amani, faraja na utulivu wa moyo, wanafunikwa zaidi na zaidi na mawimbi. Wakati ambapo watu hawajapata maswali ambayo ni muhimu zaidi kuelewa—ni wapi wametoka, ni kwa nini wako hai, ni wapi wanakoenda na kadhalika—wanashawishiwa na umaarufu na utajiri, wanapotoshwa, wanadhibitiwa na vitu hivyo, na wanaishia kupotea bila kujua njia. Muda unayoyoma; kwa kufumba na kufumbua miaka inapita; na kabla ya mtu kutambua, mtu anaaga kwaheri miaka iliyo bora zaidi ya maisha yake. Wakati mtu anakaribia kuondoka ulimwenguni, mtu anafika katika utambuzi wa taratibu kwamba kila kitu ulimwenguni kinamwacha polepole, kwamba mtu hawezi kushikilia tena vitu alivyomiliki; kisha mtu anahisi kwa kweli kwamba hamiliki kitu chochote kile, na ni kama tu mtoto mchanga anayelia ambaye ndio kwanza amezaliwa na kubisha mlango ulimwenguni. Wakati huu, mtu anashawishiwa kutafakari kile ambacho amefanya maishani, thamani ya kuwa hai, ni nini maana yake, kwa nini mtu alikuja ulimwenguni; na wakati huu, mtu anaendelea kutaka kujua kama kwelikuna maisha ya baadaye, kama kweli Mbingu ipo, kama kweli kuna adhabu…. Kadri mtu anavyokaribia kufa, ndivyo mtu anavyotaka kuelewa maisha yanahusu nini hasa; kadri mtu anavyokaribia kufa, ndivyo moyo wake unavyoonekana kuwa mtupu; kadri mtu anavyokaribia kufa, ndivyo anavyozidi kuhisi kuwa hawezi kusaidika; na kwa hivyo hofu ya mtu kuhusu kifo inazidi kuongezeka siku baada ya siku. Kunazo sababu mbili zinazoelezea kwa nini watu huwa hivi wanapokaribia kifo: Kwanza, wapo karibu kupoteza umaarufu na utajiri ambao maisha yao yalitegemea, wapo karibu kuacha nyuma kila kitu kinachoonekana ulimwenguni; na pili, wapo karibu kukabiliana, wakiwa peke yao, na ulimwengu usiojulikana, wenye mafumbo, ulimwengu usiojulikana ambao wana woga wa kukanyaga mguu wao kule, kule wasikokuwa na wapendwa na mbinu zozote za kupata msaada. Kwa hizo sababu mbili, kila mtu anayekabiliana na kifo anahisi wasiwasi, anapitia hali ya hofu kubwa na anahisi hali ya kutoweza kusaidika ambayo hajawahi kuipitia hapo awali. Ni pale tu watu wanapofikia hatua hii ndipo wanapotambua kwamba kitu cha kwanza ambacho mtu lazima aelewe, pale anapokanyaga mguu wake hapa duniani, ni wapi ambapo wanadamu wanatoka, kwa nini watu wako hai, ni nani anayeamuru hatima ya binadamu, ni nani anayekidhi mahitaji ya binadamu, na Aliye na ukuu juu ya uwepo wa binadamu. Maarifa haya ndiyo njia ya kweli ambayo kwayo mtu huishi, msingi muhimu kwa kuwepo kwa binadamu—sio kujifunza namna ya kutosheleza familia ya mtu au namna ya kutimiza umaarufu na utajiri, sio kujifunza namna ya kujitokeza katika umati wala namna ya kuishi maisha mazuri zaidi, sembuse kujifunza namna ya kuwa bora na kushindana kwa mafanikio dhidi ya wengine. Ingawa maarifa mbalimbali ya kuishi ambayo watu hutumia maisha yao kuyamiliki yanaweza kutoa starehe nyingi za kimwili, hazijawahi kuleta amani na tulizo la kweli moyoni, lakini badala yake hufanya watu kila wakati kupoteza mwelekeo wao, kuwa na wakati mgumu kujidhibiti, na kukosa kila fursa ya kujifunza maana ya maisha; mbinu hizi za kuishi huleta wasiwasi uliofichwa ndani ya watu kuhusu jinsi ya kukabiliana na kifo kwa usahihi. Maisha ya watu yanaharibiwa kwa njia hii. Muumba humtendea kila mmoja kwa haki, Akimpatia kila mmoja fursa ya maisha yote ya kupata uzoefu na kuujua ukuu Wake, ilhali ni mpaka tu kifo kinapokaribia, wakati kivuli cha kifo kinaponing’inia karibu na mtu, ndipo mtu huyu anaanza kuona nuru—na ndipo inapokuwa kuchelewa mno.

Watu huishi maisha yao wakitafuta pesa na umaarufu; wanashikilia nyuzi hizi, wakifikiri kwamba ndizo mbinu zao pekee za msaada, ni kana kwamba wakiwa nazo wangeendelea kuishi, wangejitoa kwenye hesabu ya wale watakaokufa. Lakini nipale tu wanapokaribia kufa ndipo wanapotambua namna ambavyo vitu hivi vilivyo mbali na wao, namna walivyo wanyonge mbele ya kifo, namna wanavyosambaratika kwa urahisi, namna walivyo wapweke na wasivyoweza kusaidika, na hawana popote pa kugeukia. Wanatambua kwamba uzima hauwezi kununuliwa kwa pesa au umaarufu, kwamba haijalishi mtu ni tajiri vipi, haijalishi cheo chake kilivyo cha hadhi, watu wote ni maskini kwa njia sawa na wanaofanya mambo bila mpango mbele ya kifo. Wanatambua kwamba pesa haziwezi kununua uzima, kwamba umaarufu hauwezi kufuta kifo, kwamba si pesa wala umaarufu unaoweza kurefusha maisha ya mtu kwa hata dakika moja, hata sekunde moja. Kadiri watu wanavyohisi hivi, ndivyo wanavyotamani zaidi kuendelea kuishi; kadiri watu wanavyohisi hivi, ndivyo wanavyohofia zaidi kuikaribia kifo. Ni kwa wakati huu tu ndipo wanapotambua kwa kweli kwamba maisha waliyo nayo sio ya kwao wenyewe, sio yao kuyadhibiti, na kwamba mtu hana maamuzi juu ya iwapo ataishi au atakufa, kwamba haya mambo yote yanapatikana nje ya udhibiti wa mtu.

4) Jisalimishe Chini ya Utawala wa Muumba na Ukabiliane na Kifo kwa Utulivu

Wakati ule ambao mtu anazaliwa, nafsi ya mtu iliyo pweke inaanza kupitia maisha hapa duniani, inapitia mamlaka ya Muumba ambayo Muumba ameipangilia. Bila shaka, kwa mtu, kwa nafsi, hii ni fursa nzuri kabisa ya kupata maarifa kuhusu ukuu wa Muumba, kujua mamlaka Yake na kuyapitia kibinafsi. Watu wanaishi maisha yao kulingana na sheria za hatima zilizowekwa kwa ajili yao na Muumba, na kwa mtu yeyote mwenye akili timamu aliye na dhamiri, kuelewa ukuu wa Muumba na kutambua mamlaka yake kwenye mkondo wa miongo yao kadhaa hapa duniani si jambo gumu kufanya. Kwa hivyo, inapaswa kuwa rahisi sana kwa kila mtu kutambua, kupitia uzoefu wao wenyewe wa maisha katika miongo kadhaa, kwamba hatima zote za wanadamu zimeamuliwa kabla, na inapaswa kuwa rahisi kufahamu au kutathmini ni nini maana ya kuishi. Kwa wakati huo huo ambao mtu anayapokea mafunzo haya ya maisha, polepole atakuja kuelewa ni wapi maisha yanapotokea, kufahamu kile ambacho moyo unahitaji kwa kweli, ni nini kitamwongoza mtu kwenye njia ya kweli ya maisha, kazi maalum na lengo la maisha ya mwanadamu inapaswa kuwa ni nini; na mtu ataanza kutambua hatua kwa hatua kwamba kama mtu hatamwabudu Muumba, kama mtu hatajisalimisha chini ya utawala Wake, basi wakati utakapofika wa mtu kukabiliana na kifo—wakati nafsi ya mtu inakaribia kumkabili Muumba kwa mara nyingine—basi moyo wa mtu utajawa na hofu na kukosa utulivu kusikoisha. Kama mtu amekuwepo ulimwenguni kwa miongo kadhaa ilhali hajajua ni wapi maisha ya binadamu hutoka, angali hajatambua ni kwenye viganja vya mikono ya nani hatima ya binadamu inategemea, basi si ajabu hataweza kukabiliana na kifo kwa utulivu. Mtu aliyepata maarifa ya ukuu wa Muumba baada ya kupitia miongo kadhaa ya maisha, ni mtu aliye na ufahamu sahihi wa maana na thamani ya maisha; mtu aliye na maarifa ya kina kuhusu kusudi la maisha, aliye na uzoefu halisi na uelewa wa ukuu wa Muumba; na hata zaidi, mtu anayeweza kunyenyekea mbele ya mamlaka ya Muumba. Mtu kama huyo anaelewa maana ya uumbaji wa Mungu wa mwanadamu, anaelewa kwamba binadamu anapaswa kumwabudu Muumba, kwamba kila kitu anachomiliki binadamu kinatoka kwa Muumba na kitarejea Kwake siku fulani isiyo mbali sana kwenye siku za usoni; mtu kama huyo anaelewa kwamba Muumba hupangilia kuzaliwa kwa binadamu na ana ukuu juu ya kifo cha binadamu, na kwamba maisha na kifo vyote vimeamuliwa kabla na mamlaka ya Muumba. Kwa hivyo, wakati mtu anapofahamu mambo haya kwa kweli, kwa kawaida mtu ataweza kukabiliana na kifo kwa utulivu, kuweka kando mali zake zote za kidunia kwa utulivu, kukubali na kunyenyekea kwa furaha kwa yote yatakayofuata, na kukaribisha awamu ya mwisho ya maisha iliyopangiliwa na Muumba badala ya kuhofu na kupambana dhidi ya kifo. Ikiwa mtu anayaona maisha kama fursa ya kupitia ukuu wa Muumba na kuja kujua mamlaka yake, ikiwa mtu anayaona maisha yake kama fursa adimu ya kutekeleza wajibu wake akiwa binadamu aliyeumbwa na kutimiza kazi yake maalum, basi mtu atakuwa ana mtazamo sahihi wa maisha, ataishi maisha yaliyobarikiwa na yanayoongozwa na Muumba, atatembea kwenye nuru ya Muumba, atajua ukuu wa Muumba, atakuwa katika utawala Wake, atakuwa shahidi wa matendo Yake ya ajabu na mamlaka Yake. Bila shaka, mtu kama huyo hakika atapendwa na kukubaliwa na Muumba, na ni mtu kama huyo tu anayeweza kuwa na mtazamo wenye utulivu mbele ya kifo, na anayeweza kukaribisha awamu hii ya mwisho ya maisha kwa furaha. Bila shaka Ayubu alikuwa na mtazamo kama huu kuelekea kifo; alikuwa katika nafasi ya kukubali kwa furaha awamu ya mwisho ya maisha, na baada ya kuhitimisha safari yake ya maisha vizuri, baada ya kukamilisha kazi yake maalum, alirudi kuwa upande wa Muumba.

5) Harakati na Aliyofaidi Ayubu katika Maisha Yamruhusu Kukabiliana na Kifo kwa Utulivu

Katika Maandiko imeandikwa kuhusu Ayubu: “Kwa hivyo Ayubu akafariki, akiwa mzee na aliyejawa na siku” (Ayubu 42:17). Hii inamaanisha kwamba wakati Ayubu alipoaga dunia, hakuwa na majuto na hakuhisi maumivu, lakini aliondoka kwa kawaida kutoka kwa ulimwengu huu. Kama vile kila mmoja anavyojua, Ayubu alikuwa mtu aliyemcha Mungu na kuepuka maovu alipokuwa hai; Mungu alimpongeza kwa matendo yake ya haki, watu waliyakumbuka, na maisha yake, zaidi ya yeyote yule mwingine, yalikuwa na thamani na umuhimu. Ayubu alifurahia baraka za Mungu na aliitwa mwadilifu na Yeye hapa duniani, na aliweza pia kujaribiwa na Mungu na kujaribiwa na Shetani; alisimama kuwa shahidi wa Mungu na alistahili kuitwa mtu mwenye haki. Katika miongo kadhaa baada ya kujaribiwa na Mungu, aliishi maisha ambayo yalikuwa yenye thamani zaidi, yenye maana zaidi, yenye msingi, na yenye amani zaidi kuliko hata awali. Kutokana na matendo yake ya haki, Mungu alimjaribu; na pia kwa sababu ya matendo yake ya haki, Mungu alionekana kwake na kuongea naye moja kwa moja. Kwa hiyo, kwenye miaka yake baada ya kujaribiwa, Ayubu alielewa na kufahamu thamani ya maisha kwa njia thabiti zaidi, aliweza kupata ufahamu wa kina zaidi wa ukuu wa Muumba, na akapata maarifa sahihi na yenye uhakika zaidi kuhusu namna ambavyo Muumba anavyotoa na kuzichukua baraka zake. Kitabu cha Ayubu kinarekodi kwamba Yehova Mungu alimpa hata baraka nyingi zaidi Ayubu kuliko hapo awali, Akimweka Ayubu katika nafasi bora zaidi ya kujua ukuu wa Muumba na kujua kukabiliana na kifo kwa utulivu. Kwa hiyo, Ayubu alipozeeka na kukabiliana na kifo, bila shaka asingekuwa na wasiwasi kuhusu mali yake. Hakuwa na wasiwasi wowote, hakuwa na chochote cha kujutia, na bila shaka hakuogopa kifo; kwani aliishi maisha yake akitembea ile njia ya kumcha Mungu, kuepuka maovu, na hakuwa na sababu yoyote ya kuwa na wasiwasi kuhusu mwisho wake mwenyewe. Ni watu wangapi leo wanaweza kuchukua hatua kwa njia zote hizo ambazo Ayubu alitumia alipokabiliwa na kifo chake mwenyewe? Kwa nini hakuna mtu anayeweza kuendeleza mwelekeo wa mtazamo rahisi kama huu? Kunayo sababu moja tu: Ayubu aliishi maisha yake katika hali ya kufuatilia imani, utambuzi, na unyenyekevu kwa ukuu wa Mungu, na ilikuwa ni kupitia imani, utambuzi, na unyenyekevu huu ambapo aliweza kupitia zile awamu muhimu za maisha, aliishi kwa kudhihirisha miaka yake ya mwisho, na kukaribishaa awamu yake ya mwisho ya maisha. Licha ya kile ambacho Ayubu alipitia, yale aliyoyafuatilia na malengo yake katika maisha yalikuwa ni yenye furaha, na hayakuwa na maumivu. Alikuwa na furaha si tu kwa sababu ya baraka au kibali alichopewa na Muumba, lakini muhimu zaidi kwa sababu ya yale aliyoyafuatilia na malengo yake katika maisha, kwa sababu ya maarifa yaliyoongezeka kwa utaratibu na ufahamu wa kweli wa ukuu wa Muumba ambao alitimiza kupitia kwa kumcha Mungu na kwa kuepuka maovu, na zaidi, kwa sababu ya matendo Yake ya ajabu ambayo Ayubu aliyapitia kibinafsi wakati huu akiwa chini ya ukuu wa Muumba, na hisia zenye kujali na zisizosahaulika na kumbukumbu ya mwanadamu na Mungu kuwepo pamoja, kufahamiana, na kuelewana. Ayubu alikuwa na furaha kwa sababu ya faraja na furaha iliyotokana na kujua nia za Muumba, na kwa sababu ya heshima iliyotokea baada ya kuona kwamba Yeye ni mkuu, wa ajabu, wa kupendeza na mwaminifu. Sababu iliyomfanya Ayubu aweze kukabiliana na kifo bila mateso yoyote ni kwamba alijua, katika kufa, angerudi kuwa upande wa Muumba. Na ilikuwa ni yale aliyoyafuatilia na kuyapata maishani mwake ambayo yalimruhusu kukabiliana na kifo kwa utulivu, yalimruhusu kukabiliana na matarajio ya Muumba kuuchukua uhai wake tena, akiwa na moyo wenye utulivu, na zaidi ya hayo, yalimruhusu kusimama imara bila kutikisika na bila wasiwasi mbele za Muumba. Je, watu wanaweza siku hizi kutimiza aina ya furaha ambayo Ayubu alikuwa nayo? Je, nyinyi wenyewe mko katika hali ya kufanya hivyo? Kwa kuwa watu siku hizi wana hali hizi, kwa nini hawawezi kuishi kwa furaha, kama alivyofanya Ayubu? Kwa nini hawawezi kuepuka mateso yanayotokana na hofu ya kifo? Wakati wanapokabiliwa na kifo, baadhi ya watu hujiendea haja ndogo; wengine wanatetemeka, wanazimia, wanapiga kelele kwa hasira dhidi ya Mbingu na wanadamu vilevile, wengine hata wakalia kwa huzuni na kutokwa machozi. Kwa vyovyote vile, hii siyo miitikio ya ghafla inayotokea wakati kifo kinapokaribia. Watu hutenda kwa njia hizi za aibu hasa kwa sababu, ndani ya mioyo yao, wanaogopa kifo, kwa sababu hawana maarifa yaliyo wazi na utambuzi wa ukuu wa Mungu na mipangilio Yake, sembuse kujinyenyekeza mbele ya vitu hivi; kwa sababu watu hawataki chochote isipokuwa kupanga na kutawala kila kitu wao wenyewe, kudhibiti hatima zao binafsi, maisha yao binafsi na hata kifo. Kwa hivyo, si ajabu kwamba watu hawawezi kamwe kuepuka hofu ya kifo.

6) Ni kwa Kukubali tu Ukuu wa Muumba Ndipo Mtu Anaweza Kurejea Upande Wake

Wakati mtu hana maarifa yaliyo wazi na hajapitia ukuu wa Mungu na mipangilio Yake, maarifa ya mtu kuhusu hatima na yale ya kifo yatakuwa yale yasiyoeleweka. Watu hawawezi kuona waziwazi kwamba haya yote yamo kwenye kiganja cha mkono wa Mungu, hawatambui kwamba kila kitu kiko chini ya udhibiti na ukuu wa Mungu, hawatambui kwamba mwanadamu hawezi kutupilia mbali au kuepuka ukuu kama huo; na kwa hivyo wakati wanapokabiliwa na kifo hakuna mwisho wowote katika maneno yao ya mwisho, wasiwasi wao, na hata majuto. Wamelemewa sana na mizigo mingi, kusitasita kwingi, kuchanganyikiwa kwingi, na haya yote yanawafanya kuogopa kifo. Kwa mtu yeyote aliyezaliwa katika ulimwengu huu, kuzaliwa kwake ni muhimu na kifo chake hakiepukiki; na hakuna mtu anayeweza kuupiga chenga mkondo huu. Kama mtu atataka kuondoka katika ulimwenguni huu bila maumivu, kama mtu atataka kukabiliana na awamu ya mwisho ya maisha bila kusitasita au wasiwasi, njia pekee ni kuondoka bila majuto. Na njia pekee ya kuondoka bila majuto ni kujua ukuu wa Muumba, kujua mamlaka yake, na kunyenyekea mbele ya vitu hivi. Ni kwa njia hii tu ndipo mtu anaweza kuwa mbali na mahangaiko ya binadamu, mbali na maovu, mbali na utumwa wa Shetani; na ni kwa njia hii tu ndipo mtu anaweza kuishi maisha kama ya Ayubu, akiongozwa na akibarikiwa na Muumba, maisha yaliyo huru na yaliyokombolewa, maisha yenye thamani na maana, maisha yenye uaminifu na moyo wazi; ni kupitia kwa njia hii tu ndipo mtu anaweza kunyenyekea, kama Ayubu, katika kujaribiwa na kunyang’anywa na Muumba, katika kujinyenyekeza kwenye mipango na mipangilio ya Muumba; ni kwa njia hii tu ndipo mtu anaweza kumwabudu Muumba maisha yake yote na kuweza kupata sifa Zake, kama Ayubu alivyopata, na kusikia sauti Yake, kumwona Akionekana; ni kwa njia hii tu ndipo mtu anaweza kuishi na kufa kwa furaha, kama Ayubu, bila ya maumivu, bila wasiwasi, bila majuto; ni kwa njia hii tu ndipo mtu anaweza kuishi katika nuru, kama Ayubu, na kupita kila hatua ya maisha katika nuru, kukamilisha kwa urahisi safari ya mtu katika nuru, kutimiza kwa ufanisi kazi yake maalum—kupitia, kujifunza, na kujua ukuu wa Muumba kama kiumbe kilichoumbwa—na kuiaga dunia katika nuru, na kuanzia wakati huo na kuendelea anasimama upande wa Muumba kama mwanadamu aliyeumbwa, anayesifiwa na Yeye.

Usikose Fursa ya Kujua Ukuu wa Muumba

Awamu sita zilizofafanuliwa hapo juu ni awamu muhimu zilizowekwa wazi na Muumba ambazo kila mtu wa kawaida lazima azipitie katika maisha yake. Kila mojawapo ya awamu hizi ni halisi; hakuna hata moja kati yazo ambayo inaweza kuepukwa, na zote zimebeba uhusiano wa kuamuliwa kabla kwa Muumba na ukuu Wake. Hivyo basi kwa binadamu, kila mojawapo ya awamu hizi ni sehemu muhimu ya kujikagua, na namna ya kupitia kila mojawapo vizuri ni suala muhimu sana ambalo nyinyi nyote mnakabiliwa nalo.

Miongo kadhaa ambayo inaunda maisha ya binadamu si mirefu sana wala mifupi sana. Miaka zaidi ya ishirini tangu kuzaliwa hadi kufikia utu uzima kwa muda mfupi kwa kufumba na kufumbua, na ingawa katika hatua hii ya maisha mtu huchukuliwa kuwa mtu mzima, watu katika umri huu wanajua machache sana kuhusu maisha ya binadamu na hatima ya binadamu.Kadri wanavyopata uzoefu zaidi, ndivyo wanavyoingia hatua kwa hatua kufikia umri wa kati. Watu katika miaka yao ya thelathini na arubaini wanaanza kupata uzoefu wa maisha na hatima, lakini mawazo yao kuhusu mambo haya bado hayana uelewa wa wazi. Ni mpaka kufikia tu umri wa miaka arubaini ndipo baadhi ya watu huanza kupata uelewa juu ya binadamu na ulimwengu, ambavyo viliumbwa na Mungu, na kuelewa kwamba maisha ya binadamu yanahusu nini, na hatima ya binadamu ni nini. Baadhi ya watu, ingawa wamekuwa wafuasi wa Mungu kwa muda mrefu na sasa wanao umri wa kati, bado hawamiliki maarifa na ufafanuzi sahihi wa ukuu wa Mungu, sembuse utiifu wa kweli. Baadhi ya watu hawajali chochote isipokuwa namna ya kupokea baraka, na ingawa wameishi kwa miaka mingi, hawajui au hawaelewi hata kidogo ukweli wa ukuu wa Muumba juu ya hatima ya binadamu, na kwa hivyo bado hawajaingia hata kidogo kwenye mafunzo ya kivitendo ya kujitiisha katika mipango na mipangilio ya Mungu. Watu kama hao ni wapumbavu kabisa; watu kama hao wanaishi maisha yao yasiyofaa.

Kama maisha ya binadamu yangegawanywa kulingana na kiwango cha mtu cha kile alichopitia maishani na maarifa yake kuhusu hatima ya binadamu, basi yangegawanywa katika awamu tatu. Awamu ya kwanza ni ujana, ambayo ni miaka kati ya kuzaliwa na umri wa kati, au kutoka kuzaliwa hadi kufikia umri wa miaka thelathini. Awamu ya pili ni ya utu uzima, kuanzia umri wa miaka ya kati hadi umri wa uzee, au kuanzia thelathini hadi kufikia sitini. Na awamu ya tatu ni kile kipindi cha ukomavu wa mtu, unaoanzia umri wa uzee, kuanzia miaka sitini, mpaka pale mtu atakapoondoka duniani. Kwa maneno mengine, kuanzia kuzaliwa hadi umri wa miaka ya kati, maarifa ya watu wengi kuhusu hatima na maisha yanabakia tu katika kuiga mawazo ya wengine, na hayana uhalisia, wa kivitendo. Katika kipindi hiki, mtazamo wa mtu kuhusu maisha, na jinsi ambavyo mtu huingiliana na watu katika ulimwengu vyote ni vya kijuujuu na vya kijinga sana. Hiki ndicho kipindi cha ujana wa mtu. Ni baada tu ya mtu kuonja furaha na huzuni zote za maisha ndipo mtu anapataufahamu halisi wa hatima, ndipo mtu—bila kujua ndani kabisa ya moyo wake—anaanza taratibu kufahamu kuwa hatima haiwezi kubadilishwa, na anaanza kutambua polepole kwamba ukuu wa Muumba juu ya hatima ya binadamu kwa kweli upo. Kwa kweli hiki ndicho kipindi cha utu uzima wa mtu. Baada ya mtu kuacha kupambana dhidi ya hatima, na pale ambapo mtu hayuko radhi tena kuvutwa kwenye mabishano, lakini anajua msimamo wake, anajinyenyekeza kwa mapenzi ya Mbinguni, anafanya muhtasari wa mafanikio na makosa yake katika maisha, na anasubiria hukumu ya Muumba juu ya maisha yake —hiki ni kipindi cha ukomavu. Kwa kuzingatia uzoefu wa aina tofauti na ufahamu ambao watu hupata katika vipindi hivi vitatu, katika hali za kawaida fursa ya mtu ya kujua ukuu wa Muumba si kubwa sana. Kama mtu ataishi kufikisha umri wa miaka sitini, mtu anayo miaka thelathini tu au zaidi ya kuujua ukuu wa Mungu; kama mtu atataka kipindi kirefu zaidi cha muda, hilo linawezekana tu kama maisha ya mtu yatakuwa marefu zaidi, tuseme kama mtu ataweza kuishi karne moja. Kwa hivyo Ninasema, kulingana na sheria za kawaida za uwepo wa binadamu, ingawa ni mchakato mrefu sana kuanzia wakati ule mtu anakumbana na mada ya kujua ukuu wa Muumba hadi pale ambapo mtu anaweza kutambua ukweli wa ukuu wa Muumba, na kutoka hapo mpaka pale ambapo mtu anaweza kujinyenyekeza kwa utawala huo, kama kwa hakika mtu atahesabu miaka hiyo, miaka hiyo haizidi thelathini au arubaini hivi ambapo mtu anayo fursa ya kufaidi haya yote. Na mara nyingi, watu hujisahau kutokana na matamanio yao na malengo yao ya kupokea baraka; hawawezi kutambua ni wapi ambapo kiini halisi cha maisha ya binadamu kipo, hawang’amui umuhimu wa kujua ukuu wa Muumba, na kwa hivyo hawafurahii fursa hii yenye thamani ya kuingia kwenye ulimwengu wa binadamu kuhusiana na maisha ya binadamu na kile alichopitia, kupitia ukuu wa Muumba, na hawatambui namna lilivyo jambo la thamani kwa kiumbe chochote kilichoumbwa kupokea mwongozo wa kibinafsi kutoka kwa Muumba. Kwa hivyo Ninasema, wale watu wanaotaka kazi ya Mungu imalizike kwa haraka, wale wanaotamani kwamba Mungu angepangilia mwisho wa binadamu haraka iwezekanavyo, ili waweze mara moja kutazama nafsi Yake halisi na kubarikiwa haraka iwezekanavyo—ni wenye hatia ya aina mbaya zaidi ya kutotii na wao ni wapumbavu kupindukia. Na kwa wale wanaotamani, katika muda wao mfupi, kushikilia fursa hii ya kipekee ili kuujua ukuu wa Muumba, hao ni watu wenye hekima, walio na akili. Matamanio haya mawili tofauti yanafichua mitazamo miwili tofauti na ufuatiliaji tofauti: Wale wanaotafuta baraka ni wabinafsi na wa kudharauliwa, hawafikirii kamwe mapenzi ya Mungu, hawataki kamwe kujua ukuu wa Mungu, na wala hawataki kutii ukuu wa Mungu, bali wanataka tu kuishi wanavyopenda. Wao ni wapotovu wasiojali; wao ndio wameku kuangamizwa. Wale wanaotafuta kumjua Mungu wanaweza kuweka pembeni matamanio yao, wako radhi kujinyenyekeza kwa ukuu wa Mungu na mipangilio ya Mungu; wanajaribu kuwa aina ya watu ambao wananyenyekea katika mamlaka ya Mungu na kukidhi nia za Mungu. Watu kama hao wanaishi katika nuru, wanaishi katikati ya baraka za Mungu; kwa hakika wataweza kusifiwa na Mungu. Haijalishi ni nini, chaguo la binadamu halina manufaa, binadamu hawana kauli yoyote kuhusiana na muda ambao kazi ya Mungu itachukua. Ni bora zaidi kwa watu kujiweka chini ya udhibiti wa Mungu, kunyenyekea katika ukuu Wake. Usipojiweka chini ya udhibiti Wake, ni nini utakachofanya? Je, Mungu atakuwa na hasara yoyote? Usipojiweka chini ya udhibiti Wake, ukijaribu kuushika usukani, unafanya chaguo la kipumbavu, na wewe tu ndiwe utakayepata hasara hatimaye. Endapo tu watu watashirikiana na Mungu haraka iwezekanavyo, endapo tu watafanya hima kukubali mipango Yake, kujua mamlaka Yake, na kutambua yote ambayo Amewafanyia, ndipo watakapokuwa na tumaini, ndipo maisha yao yatakapokuwa hawajayaishi bure, na, ndipo watakapopata wokovu.

Hakuna Anayeweza Kubadilisha Ukweli Kwamba Mungu Anashikilia Ukuu juu ya Hatima ya Binadamu

Baada ya kusikiliza kila kitu Nilichomaliza kusema, je, fikira zenu juu ya hatima zimebadilika? Je, mnaelewa vipi ukweli ya ukuu wa Mungu juu ya hatima ya binadamu? Ili kuiweka kwa urahisi, chini ya mamlaka ya Mungu kila mtu anakubali waziwazi au kimyakimya ukuu Wake na mipangilio Yake, na haijalishi ni vipi ambavyo mtu anashughulika katika mkondo wa maisha yake, haijalishi ni njia ngapi potovu ambazo mtu ametembelea, mwishowe atarudi tu kwenye njia ya hatima ambayo Muumba amempangia yeye. Hii ndiyo hali ya kutoweza kushindwa kwa mamlaka ya Muumba, namna ambavyo mamlaka Yake yanadhibiti na kutawala ulimwengu. Ni hii hali ya kutoweza kushindwa, aina hii ya udhibiti na utawala, ambao unawajibikia sheria zinazoamuru maisha ya kila kitu, ambayo inawaruhusu wanadamu kuzaliwa upya tena na tena bila kuingiliwa, ambayo inaufanya ulimwengu kuzunguka mara kwa mara na kusonga mbele, siku baada ya siku, mwaka baada ya mwaka. Mmezishuhudia kweli hizi zote na mmezielewa, haijalishi kama ni za juujuu ama ni za kina; kina cha ufahamu wako kinategemea kile unachopitia na maarifa ya ukweli, na maarifa yako kuhusu Mungu. Jinsi unavyojua vyema uhalisia wa ukweli, ni kiwango kipi ambacho umepitia matamshi ya Mungu, jinsi unavyojua vyema kiini cha Mungu na tabia Yake —hii inawakilisha kina cha ufahamu wako wa ukuu na mipangilio ya Mungu. Je, kuwepo kwa ukuu na mipangilio ya Mungu kunategemea ikiwa wanadamu wanaitii? Je, ukweli kwamba Mungu anamiliki mamlaka haya inaamuliwa na iwapo wanadamu wanayanyenyekea? Mamlaka ya Mungu yapo licha ya hali mbalimbali; katika hali zote, Mungu anaamuru na kupangilia hatima ya kila binadamu na mambo yote kulingana na fikira Zake, na mapenzi Yake. Hili halitabadilika kutokana na mabadiliko ya mwanadamu; haitegemei mapenzi ya mwanadamu, haiwezi kubadilishwa na mabadiliko yoyote ya wakati, anga, na jiografia, kwa kuwa mamlaka ya Mungu ni kiini Chake hasa. Iwapo mwanadamu anaweza kujua na kukubali ukuu wa Mungu, na kama mwanadamu anaweza kuunyenyekea—hakuna lolote kati ya haya linalobadilisha hata kidogo ukweli wa ukuu wa Mungu juu ya hatima ya binadamu. Hiyo ni kusema kwamba, haijalishi ni mtazamo gani ambao binadamu atachukua kwa ukuu wa Mungu, haiwezi tu kubadilisha ukweli kwamba Mungu anashikilia ukuu juu ya hatima ya mwanadamu na juu ya vitu vyote. Hata kama hutanyenyekea katika ukuu wa Mungu, bado Anaamuru hatima yako; hata kama huwezi kuujua ukuu Wake, mamlaka Yake yangali yapo. Mamlaka ya Mungu na ukweli wa ukuu wa Mungu dhidi ya hatima ya binadamu viko huru dhidi ya mapenzi ya binadamu, na hayabadiliki kulingana na mapendeleo na machaguo ya binadamu. Mamlaka ya Mungu yapo kila mahali, kila saa, kila mara. Mbingu na nchi zitapita, lakini mamlaka Yake hayatapita kamwe, kwa kuwa Yeye ni Mungu Mwenyewe, Anamiliki mamlaka ya kipekee, na mamlaka Yake hayazuiliwi au kuwekewa mipaka na watu, matukio, au vitu, na anga au na jiografia. Siku zote Mungu hushikilia mamlaka Yake, huonyesha uwezo Wake, huendeleza usimamizi Wake wa kazi kama kawaida; kila wakati Anatawala vitu vyote, Anatosheleza vitu vyote, Anapangilia vitu vyote—kama tu Anavyofanya daima. Hakuna anayeweza kubadilisha hili. Huu ni ukweli; umekuwa ukweli usiobadilika tangu zamani!

Mtazamo na Vitendo Vinavyofaa kwa Mtu Anayetamani Kujinyenyekeza katika Mamlaka ya Mungu

Je, watu wanapaswa kuwa na mtazamo gani sasa katika kuelewa na kuyachukulia mamlaka ya Mungu, na ukweli wa ukuu wa Mungu juu ya hatima ya binadamu? Hili ni tatizo halisi linalomkabili kila mmoja. Wakati wa kukabiliana na matatizo halisi katika maisha, je, unafaa kujua na kuelewa vipi mamlaka ya Mungu na ukuu Wake? Wakati hujui namna ya kuelewa, kushughulikia, na kupitia matatizo haya, je, ni mtazamo gani unaofaa kutumia ili kuonyesha nia yako, tamanio lako, na uhalisia wako wa kujinyenyekeza katika ukuu na mipangilio ya Mungu? Kwanza lazima ujifunze kusubiri; kisha lazima ujifunze kutafuta; kisha lazima ujifunze kujinyenyekeza. “Kusubiri” kunamaanisha kusubiria muda wa Mungu, kusubiria watu, matukio, na mambo ambayo Amekupangilia wewe, kusubiria mapenzi Yake ili yaweze kwa utaratibu kujifichua kwako. “Kutafuta” kunamaanisha kuchunguza na kuelewa nia za Mungu katika fikira Zake kwako wewe kupitia watu, matukio, na mambo ambayo Amekuwekea wazi, kuelewa ukweli kupitia mambo hayo, kuelewa kile ambacho binadamu lazima watimize na njia ambazo lazima wafuate, kuelewa matokeo ambayo Mungu ananuia kufanikisha kwa wanadamu na mafanikio Anayonuia kufikia ndani yao. “Kujinyenyekeza,” bila shaka, kunaashiria kukubali watu, matukio, na mambo ambayo Mungu amepanga, kukubali ukuu Wake na, kupitia kwayo, kupata kujua namna ambavyo Muumba anaamuru hatima ya binadamu, namna Anavyomjaliza binadamu na maisha Yake, na namna Anavyofanya kazi ya ukweli ndani ya mwanadamu. Vitu vyote chini ya mipango na ukuu wa Mungu vinatii sheria za asili, na kama utaamua kumwachia Mungu akupangilie na kuamuru kila kitu kwa ajili yako, unafaa kujifunza kusubiri, unafaa kujifunza kutafuta, unafaa kujifunza kujinyenyekeza. Huu ndio mtazamo ambao kila mtu anayetaka kujinyenyekeza katika mamlaka ya Mungu lazima awe nao, ubora wa kimsingi ambao kila mmoja anayetaka kuukubali ukuu na mipangilio ya Mungu lazima aumiliki. Ili kushikilia mtazamo kama huu, kumiliki ubora kama huu, lazima mfanye kazi kwa bidii zaidi; na hapo ndipo mtakapoweza kuingia kwenye uhalisi wa kweli.

Kumkubali Mungu kama Bwana Wenu wa Kipekee Ndiyo Hatua ya Kwanza katika Kufikia Wokovu

Ukweli kuhusiana na mamlaka ya Mungu ni ukweli ambao kila mmoja lazima atilie maanani kwa umakinifu, lazima apitie na aelewe katika moyo wake; kwani ukweli huu unao uhusiano katika maisha ya kila mmoja, kwenye maisha ya kale, ya sasa, na ya siku za usoni za kila mmoja, kwenye awamu muhimu ambazo kila mtu lazima apitie maishani, katika maarifa ya binadamu kuhusu ukuu wa Mungu na mtazamo ambao anafaa kuwa nao katika mamlaka ya Mungu, na kwa kawaida, kwenye hatima ya mwisho ya kila mmoja. Kwa hivyo inachukua nguvu za maisha yako yote kujua na kuyaelewa. Unapochukulia mamlaka ya Mungu kwa umakinifu, unapoukubali ukuu wa Mungu, kwa utaratibu utaanza kutambua na kuelewa kwamba mamlaka ya Mungu kwa kweli yapo. Lakini kama hutawahi kutambua mamlaka ya Mungu, hutawahi kuukubali ukuu Wake, basi haijalishi ni miaka mingapi utakayoishi, hutapata maarifa hata kidogo ya ukuu wa Mungu. Kama hutajua na kuelewa kwa kweli mamlaka ya Mungu, basi utakapofika mwisho wa barabara, hata kama utakuwa umesadiki katika Mungu kwa miongo kadhaa, hutakuwa na chochote cha kuonyesha katika maisha yako, na kwa kawaida hautakuwa na maarifa hata kidogo ya ukuu wa Mungu juu ya hatima ya mwanadamu. Je, hili si jambo la kusikitisha sana? Kwa hivyo haijalishi umetembea kwa umbali gani maishani, haijalishi unao umri wa miaka mingapi sasa, haijalishi safari yako iliyosalia itakuwa ya umbali gani, kwanza lazima utambue mamlaka ya Mungu na uyachukulie kwa uzito, na ukubali ukweli kwamba Mungu ni Bwana wako wa kipekee. Kutimiza maarifa yaliyo wazi, sahihi na kuelewa ukweli huu kuhusiana na ukuu wa Mungu juu ya hatima ya binadamu ni funzo la lazima kwa kila mmoja, ndio msingi wa kuyajua maisha ya binadamu na kupata ukweli, ndiyo maisha na funzo la msingi la kumjua Mungu ambalo kila mtu anakabiliana nalo kila siku, na ambayo hakuna yeyote anayeweza kuyakwepa. Kama mmoja wenu angependa kuchukua njia za mkato ili kufikia lengo hili, basi Ninakuambia, hilo haliwezekani! Kama mmoja wenu anataka kukwepa ukuu wa Mungu, basi hilo nalo ndilo haliwezekani zaidi! Mungu ndiye Bwana wa pekee wa binadamu, Mungu ndiye Bwana wa pekee wa hatima ya binadamu, na kwa hivyo haiwezekani kwa binadamu kuamuru hatima yake mwenyewe, haiwezekani kwake kuizidi hatima yake. Haijalishi uwezo wa mtu ni mkubwa kiasi gani, mtu hawezi kuathiri, sembuse kuunda, kupangilia, kudhibiti, au kubadilisha hatima za wengine. Ni Mungu Mwenyewe wa kipekee tu ndiye Anayeweza kuamuru mambo yote kwa binadamu, kwani Yeye tu ndiye anayemiliki mamlaka ya kipekee yanayoshikilia ukuu juu ya hatima ya binadamu; na kwa hivyo Muumba pekee ndiye Bwana wa kipekee wa binadamu. Mamlaka ya Mungu yanashikilia ukuu sio tu juu ya binadamu walioumbwa, lakini hata juu ya viumbe ambavyo havikuumbwa visivyoweza kuonekana na binadamu, juu ya nyota, juu ya ulimwengu mzima. Huu ni ukweli usiopingika, ukweli ambao upo kiuhalisia, ambao hakuna mtu au kitu kinachoweza kuubadilisha. Kama mmoja wenu angali hajatosheka na mambo kama yalivyo, akiamini kwamba kwa kiasi fulani ana ujuzi au uwezo maalum, na bado anafikiria kwamba anaweza kubahatika na kubadilisha hali yake ya sasa au hata kuiepuka; kama utajaribu kubadilisha hatima yako mwenyewe kupitia kwa juhudi za kibinadamu, na hivyo basi kujitokeza kati ya wengine na kupata umaarufu na utajiri; basi Ninakwambia, unayafanya mambo kuwa magumu kwako, unajitakia taabu tu, unajichimbia kaburi lako mwenyewe! Siku moja, hivi karibuni au baadaye, utagundua kwamba ulifanya chaguo baya, kwamba jitihada zako ziliambulia patupu. Malengo yako, tamanio lako la kupambana dhidi ya hatima, na mwenendo wako mwenyewe ulio mbaya, utakuongoza kwenye barabara isiyoweza kukurudisha kule ulikotoka, na kwa hili utaweza kujutia baadaye. Ingawa sasa huoni ubaya wa athari hiyo, unapopitia na kuelewa zaidi na zaidi ukweli kwamba Mungu ndiye Mtawala wa hatima ya mwanadamu, utaanza kwa utaratibu kutambua kile Ninachozungumzia leo na athari zake za kweli. Ikiwa kweli una moyo na roho, na ikiwa wewe ni mtu anayependa ukweli, inategemea ni mtazamo wa aina gani ambao utachukua kuhusiana na ukuu wa Mungu na kuhusiana na ukweli. Na kwa kawaida, hili linaamua kama kweli unaweza kujua na kuelewa mamlaka ya Mungu. Kama hujawahi katika maisha yako kuhisi ukuu wa Mungu na mipangilio yake, na isitoshe hujawahi kutambua na kukubali mamlaka ya Mungu, basi utakuwa huna thamani kabisa, na bila shaka utakuwa ni mlengwa wa kuchukiwa na kukataliwa na Mungu, hayo yote ni kutokana na njia uliyochukua na chaguo ulilofanya. Lakini wale ambao, katika kazi ya Mungu, wanaweza kukubali jaribio Lake, kukubali ukuu Wake, kujinyenyekeza katika mamlaka Yake, na kupata kwa utaratibu uzoefu halisi wa matamshi Yake, watakuwa wametimiza maarifa halisi ya mamlaka ya Mungu, ufahamu halisi wa ukuu Wake, na watakuwa kwa kweli wamejisalimisha kwa Muumba. Watu kama hao tu ndio watakaokuwa wameokolewa kwa kweli. Kwa sababu wameujua ukuu wa Mungu, kwa sababu wameukubali, uelewa wao na kujinyenyekeza kwao katika ukweli wa ukuu wa Mungu juu ya hatima ya binadamu ni halisi na sahihi. Wakati wanakabiliwa na kifo wataweza, kama Ayubu, kuwa na akili isiyotishwa na kifo, kujinyenyekeza katika mipango na mipangilio ya Mungu katika mambo yote, bila chaguo lolote la kibinafsi, bila tamanio lolote la kibinafsi. Mtu kama huyo tu ndiye atakayeweza kurudi katika upande wa Muumba kama mwanadamu wa kweli aliyeumbwa.

Desemba 17, 2013

Iliyotangulia: Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II

Inayofuata: Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IV

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp