143 Ee Mungu, Moyo Wangu Utakupenda Daima

1 Umeonyesha ukweli ili kumwokoa binadamu, huu ni upendo Wako mkubwa. Maneno Yako yote ni ukweli na yameushinda moyo wangu. Nimepotoshwa sana na Shetani ilhali Wewe hujitahidi kuniokoa na huniachi. Ingawa wakati mwingine nakosea na kuanguka na wakati mwingine mimi ni dhaifu na hasi, lakini Wewe daima huninyunyizia na kunikimu, kunipa nguvu ya kusimama imara. Maneno Yako yananiongoza kwenye njia ya nuru ya maisha. Kwa kukufuata, moyo wangu umejaa amani na furaha. Mwenyezi Mungu! Moyo wangu utakuwa Wako milele!

2. Ulinitoa kutoka mavumbini, ukaniinua nitimize wajibu, lakini sikuthamini fursa hiyo, nilikuwa mzembe sana katika wajibu wangu. Ulihukumu na kunifunua kwa maneno hivyo nilitafakari na kujijua mwenyewe. Maneno Yako yalinichoma kwa ukali lakini nimeshawishika kabisa. Niliona nia Zako njema na nimejaa majuto. Ninainama mbele Yako na niko tayari kukubali hukumu na utakaso Wako. Nimepitia hukumu Yako na kuonja upendo Wako. Mwenyezi Mungu! Moyo wangu utakuwa Wako milele!

3. Umepitia shida zote ili kumwokoa binadamu, Umevumilia dhoruba na sisi. Nilipokamatwa na kuteswa, maneno Yako yaliniongoza. Uko pamoja nami katika shida, maneno Yako yanafariji maumivu yaliyo moyoni mwangu. Naona mamlaka na nguvu katika maneno Yako na ninakusifu. Unateseka pamoja nasi, ambalo ni onyesho kubwa zaidi la upendo Wako! Kupitia shida na mateso upendo Wangu Kwako unakua thabiti. Naapa kukushuhudia Wewe na kumwaibisha Shetani. Mwenyezi Mungu! Moyo wangu utakuwa Wako milele!

4 Maneno Yako yalinipa maisha mapya, yaliniacha niishi upya. Hukumu Yako ilinitakasa, tabia yangu potovu imebadilika. Upendo Wako na maneno Yako yamekita mizizi sana moyoni mwangu. Haijalishi jinsi barabara mbele ilivyo na mabonde, najua Wewe ni ukweli na maisha, nimeamua kukufuatia mpaka mwisho. Haijalishi ni lini au wapi, nitashuhudia matendo Yako. Kukupenda na kukutolea ushuhuda ni heshima kubwa zaidi kwangu. Mwenyezi Mungu! Moyo wangu utakuwa Wako milele!

Iliyotangulia: 142 Nitauweka Upendo wa Mungu Mawazoni Mwangu Siku Zote

Inayofuata: 144 Kumpenda Mungu ni Tamanio la Moyo Wangu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp