61 Kutiwa Moyo na Upendo wa Mungu

Kwa kufanya wajibu wangu katika familia ya Mungu,

nimepitia upendo mkubwa wa Mungu.

Utunzaji wa ndugu hapa

unazidi upendo wote wa wazazi wangu.

Kukutana na kushiriki juu ya upendo wa Mungu,

sote tunatoa machozi ya hisia za kweli.

Tunaruzukiwa kwa kushiriki ukweli,

kusaidiana na kuungana mkono.

Kwa kusoma maneno ya Mungu, kuishi mbele Yake,

moyo wangu uko mtulivu na umejaa nuru.

Natafuta kumpenda Mungu, kufanya wajibu wangu

na hivyo kuishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana.

Yote ninayofurahia leo

ni kwa neema na baraka za Mungu.

Upendo Wake wanitia moyo

kumpenda na kumridhisha.

Nitamtii Mungu daima

na nirejeshe upendo Wake kwangu.

Kwa asili potovu, mwanadamu anampinga Mungu.

Akipitia hukumu ya maneno ya Mungu,

Naona ukweli wa upotovu wangu:

Nina majivuno, ujanja, sina mfanano wa binadamu.

Kwa kuunyima mwili, kutenda ukweli,

upotovu wangu unatakaswa.

Maneno ya Mungu yatunyunyizia, yatulisha kila siku.

Kwa kuishi maneno Yake, nafurahia upendoWake.

Kutenda ukweli, kumfuata Mungu,

njia ni angavu zaidi, nisongavyo zaidi.

Natafuta kumpenda Mungu, kufanya wajibu wangu

na kwa hivyo kuishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana.

Yote ninayofurahia leo

ni kwa neema na baraka za Mungu.

Upendo Wake wanitia moyo

kumpenda na kumridhisha.

Nitamtii Mungu daima

na nirejeshe upendo Wake kwangu.

Katika mateso ya serikali,

dhamira yangu kumfuata Mungu imeimarishwa.

Licha ya kukandamizwa na ugumu,

upendo wa Mwenyezi Mungu umenichochea niendelee.

Mara nikiwa salama kutoka na uwindwaji, naona uweza wa Mungu.

Namwacha Shetani, nampenda Mungu daima.

Nimehisi upendo wa Mungu, ni wa kweli sana, halisi.

Mungu ni mwenye haki, mtakatifu, Anayestahili sifa.

Yote ninayofurahia leo

ni kwa neema na baraka za Mungu.

Upendo Wake wanitia moyo

kumpenda na kumridhisha.

Nitamtii Mungu daima

na nirejeshe upendo Wake kwangu.

Iliyotangulia: 59 Kukubali Ukweli ni Kuwa Mwanamwali Mwenye Busara

Inayofuata: 62 Kujituliza Mbele za Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp