Kumjua Mungu (I)

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 1)

Kila mmoja anapaswa kuchunguza upya jinsi ambavyo anamwamini Mungu katika maisha yake yote, ili muweze kuona kama katika mchakato wa kumfuata Mungu, unaweza kuelewa kwa kweli, umefahamu kwa kweli, na umefikia kumjua Mungu kweli, na kama unajua kwa kweli ni mtazamo gani ambao Mungu anao kwa aina tofauti za wanadamu, na kama unaelewa kwa kweli kazi ambayo Mungu Anaifanya juu yako na jinsi Mungu Anavyofafanua kila tendo lako. Huyu Mungu, Ambaye yuko kando yako, Akiongoza mwelekeo wa maendeleo yako, Akishikilia ukuu juu ya hatima yako, na kukupa mahitaji yako—je, ni kwa kiasi gani, katika uchanganuzi wa mwisho, unaelewa na je, ni kwa kiasi gani unajua kwa uhakika kumhusu Yeye? Je, unajua Anachofanyia kazi kwako kila siku? Je, unajua kanuni na makusudi ambayo kwayo Yeye anazingatia katika kila tendo Lake? Je, unajua jinsi Anavyokuongoza? Unajua mbinu Anazotumia kukupa mahitaji yako? Unajua mbinu ambazo Anatumia kukuongoza? Je, unajua kile Anachotaka kupata kutoka kwako na kile Anachotaka kutimiza kwako? Je, unajua mtazamo Anaochukua katika namna nyingi ambazo unatenda? Je, unajua kama wewe ni mtu Anayependwa na Yeye? Je, unajua chanzo cha furaha, hasira, huzuni na uchangamfu Wake, na fikira na mawazo yanayohusiana na hayo, na kiini Chake? Je, unajua, hatimaye, huyu Mungu ni Mungu wa aina gani ambaye unamwamini? Je, maswali haya na mengine ya aina hii, ni kitu ambacho hujawahi kuelewa ama kuwaza kuyahusu? Katika kufuatilia imani yako kwa Mungu, je, umewahi, kuondoa hali za kutomwelewa Yeye, kupitia ufahamu wako wa kweli na katika uzoefu halisi wa maneno ya Mungu? Je, baada ya kupokea kuadibu na maonyo ya Mungu, umefikia utiifu wa kweli na kujali kwa kweli? Je, wakati wa kuadibu kwa Mungu na hukumu, umepata kutambua uasi na asili ya kishetani ya mwanadamu na kupata ufahamu kidogo kuhusu utakatifu wa Mungu? Je, chini ya uongozi na nuru ya maneno ya Mungu, umeanza kuwa na mtazamo mpya wa maisha? Katika majaribu yaliyotumwa na Mungu, je, umepata kuhisi kutovumilia Kwake makosa ya mwanadamu na pia kile Anachohitaji kutoka kwako na vile Anavyokuokoa? Iwapo hujui kutomwelewa Mungu ni nini, au jinsi ya kumaliza kutoelewa huku, basi mtu anaweza kusema hujawahi kuingia katika ushirika wa kweli na Mungu na hujawahi kumwelewa Mungu, ama angalau mtu anaweza kusema kuwa hujawahi kuwa na nia ya kumwelewa Yeye. Ikiwa hujui nidhamu ya Mungu na kuadibu ni nini, basi kwa hakika hujui kujitiisha na kujali ni nini, ama angalau hujawahi kujinyenyekeza kwa Mungu kwa kweli au kumjali. Ikiwa hujawahi kupitia kuadibu na hukumu ya Mungu, basi kwa hakika hutaweza kujua utakatifu Wake ni nini, na unaweza hata kuwa na ufahamu kidogo kuhusu uasi wa mwanadamu ni nini. Ikiwa hujawahi kuwa na mtazamo sahihi wa maisha, au lengo sahihi katika maisha, lakini bado uko katika hali ya kuchanganyikiwa na kutokuwa na uamuzi juu ya njia yako ya maisha ya baadaye, hata kufikia hatua ya kusita kusonga mbele, basi ni dhahiri kuwa hujawahi kupokea nuru na uongozi wa Mungu, na mtu anaweza tu kusema kuwa hujawahi kweli kuruzukiwa au kujazwa zaidi na maneno ya Mungu. Ikiwa bado hujapitia majaribio ya Mungu, basi ni hakika kuwa bila shaka hutajua kutovumilia kwa Mungu makosa ya mwanadamu ni nini, wala hutaelewa kile ambacho Mungu Anahitaji hatimaye kutoka kwako, ama kweli kuruzukiwa au kujazwa zaidi na maneno ya Mungu. Ikiwa bado hujapitia majaribio Ikiwa bado hujapitia majaribio. Haijalishi ni kwa miaka mingapi mwanadamu ameamini katika Mungu, iwapo hajawahi kupitia ama kutambua chochote katika maneno ya Mungu, basi kwa hakika hatembei katika njia ya wokovu, imani yake katika Mungu kwa hakika haina chochote, maarifa yake kumhusu Mungu pia kwa hakika ni sufuri, na ni hakika kuwa hana ufahamu wowote kuhusu kumcha Mungu ni nini.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 2)

Kile Mungu alicho nacho na uwepo wa Mungu, kiini cha Mungu, tabia ya Mungu—yote yamewekwa wazi katika maneno Yake kwa binadamu. Anapopitia maneno ya Mungu, katika mchakato wa kuyaweka katika vitendo mwanadamu atapata kuelewa kusudi la maneno Anayonena Mungu, na kuelewa chanzo na usuli wa maneno ya Mungu, na kuelewa na kufahamu maneno ya Mungu. Kwa binadamu, haya ni mambo yote ambayo mwanadamu lazima ayapitie, ayatambue, na kuyafikia ili kuufikia ukweli na uzima, kutambua nia za Mungu, kubadilishwa katika tabia yake, na kuweza kutii ukuu na mipango ya Mungu. Katika wakati huo ambao mwanadamu anapitia, anafahamu, na kuvifikia vitu hivi, atakuwa kupata kumwelewa Mungu polepole, na kwa wakati huu pia atakuwa amepata viwango tofauti vya maarifa kumhusu Yeye. Ufahamu huu na maarifa haya hayatoki katika kitu ambacho mwanadamu amefikiria au kutunga, ila kutoka kwa kile ambacho anafahamu, anapitia, anahisi, na anashuhudia ndani yake mwenyewe. Ni baada tu ya kufahamu, kupitia, kuhisi, na kushuhudia vitu hivi ndipo ufahamu wa mwanadamu kumhusu Mungu utapata ujazo, ni maarifa haya tu anayoyapata kwa wakati huu ndio yaliyo halisi, ya kweli na sahihi, na mchakato huu—wa kupata kuelewa kwa kweli na ufahamu wa Mungu kwa kuelewa, kupitia, kuhisi, na kushuhudia maneno Yake—sio kingine ila ushirika wa kweli kati ya mwanadamu na Mungu. Katikati ya aina hii ya ushirika, mwanadamu anakuja kuelewa kwa kweli na kufahamu nia za Mungu, anakuja kuelewa kwa kweli na kujua kile Mungu alicho na uwepo wa Mungu, anakuja kuelewa kujua kwa kweli kiini cha Mungu, anakuja kuelewa na kujua tabia ya Mungu polepole, anafikia uhalisi wa kweli, na ufafanuzi sahihi, kuhusu ukweli wa utawala wa Mungu juu ya vitu vyote vilivyoumbwa, na kupata mambo ya muhimu na ufahamu wa utambulisho wa Mungu na nafasi Yake. Katika ushirika kama huo, mwanadamu anabadilika, hatua kwa hatua, mawazo yake kuhusu Mungu hayamfikirii Yeye kwa mawazo yaliyoundwa, ama kutawaliwa na wasiwasi wake mwenyewe kumhusu Yeye, ama kutomwelewa, ama kumshutumu, ama kutoa hukumu Kwake, ama kuwa na mashaka Naye. Kwa sababu hii, mwanadamu atakuwa na kiwango kidogo cha kutomwelewa Mungu, atakuwa na vipingamizi vichache kwa Mungu, na kutakuwa na matukio machache ambayo mwanadamu atamwasi Mungu. Kwa upande mwingine, kujali na utiifu wa mwanadamu kwa Mungu, utaongezeka kwa kiasi kikubwa, na uchaji wake kwa Mungu utakuwa wa kweli zaidi na pia wa kina zaidi. Katikati ya ushirika kama huo, sio tu kwamba mwanadamu atapata kuruzukiwa ukweli na ubatizo wa maisha, bali pia kwa wakati huo huo atapata maarifa ya kweli ya Mungu. Katika aina hii ya ushirika, sio tu kwamba mwanadamu atapata kubadilishwa tabia yake na kupata wokovu, bali pia kwa wakati huo atafikia uchaji na ibada ya kweli ya kiumbe aliyeumbwa kwa Mungu. Baada ya kuwa na aina hii ya ushirika, imani ya mwanadamu katika Mungu haitakuwa tena ukurasa tupu wa karatasi, ama ahadi ya maneno matupu, ama aina ya kufuata kwa upofu na kuabudu sanamu; ni; katika aina hii ya ushirika pekee ndio maisha ya mwanadamu yatakua kuelekea ukomavu siku baada ya siku, na ni wakati huu ndio tabia yake itabadilika polepole, na imani yake kwa Mungu, hatua kwa hatua, itatoka kwenye imani isiyo dhahiri na imani isiyo na uhakika mpaka kufikia utiifu wa kweli na kujali, na kuwa na uchaji wa kweli, na mwanadamu pia, katika mchakato wa kumfuata Mungu, ataendelea polepole kutoka kwenye mtazamo baridi mpaka kufikia mtazamo wa kiutendaji, kutoka kuwa yule aliye hasi mpaka kuwa chanya; ni kwa aina hii ya ushirika pekee ndipo mwanadamu atafikia kuelewa kwa kweli na ufahamu wa Mungu, kufikia maarifa ya kweli ya Mungu. Kwa sababu watu wengi hawajawahi kuingia katika ushirika wa kweli na Mungu, ufahamu wao kuhusu Mungu unakomea kiwango cha nadharia, katika kiwango cha barua na mafundisho. Hivyo ni kusema, watu wengi, haijalishi ni miaka mingapi wamemwamini Mungu, inapokuja katika suala la kumjua Mungu bado wako mahali pale pale walipoanzia, wamekwama katika msingi wa aina za ibada za kitamaduni, na mitego yao ya hadithi za kutumia rangi na ushirikina wa kikabaila. Ikiwa maarifa ya mwanadamu kumhusu Mungu yanasalia katika hatua ya awali, hii ina maana kwamba hayapo kabisa. Mbali na uthibitisho wa mwanadamu kuhusu nafasi na utambulisho wa Mungu, imani ya mwanadamu kwa Mungu bado iko katika hali ya kutoeleweka na kutokuwa na uhakika. Hii ikiwa hivyo, je, ni kiwango gani ambacho mwanadamu anaweza kuwa nacho kuhusu uchaji wa kweli kwa Mungu?

Haijalishi jinsi unavyoamini kwa uthabiti kuwepo kwa Mungu, hii haiwezi kuchukua nafasi ya ujuzi wako kuhusu Mungu, wala uchaji wako kwa Mungu. Haijalishi kiwango ambacho umefurahia baraka Zake na neema Yake, hii haiwezi kuchukua nafasi ya ufahamu wako wa Mungu. Haijalishi ni kiwango gani unataka kuweka wakfu kila kitu chako na kugharimika kwa ajili Yake, hii haiwezi kuchukua nafasi ya maarifa yako kuhusu Mungu. Ama labda umeyazoea sana maneno ambayo Amenena mpaka unayajua kimoyomoyo na unaweza kuyasema kwa haraka; hata hivyo, hii haiwezi kuchukua nafasi ya maarifa yako kuhusu Mungu. Haijalishi jinsi ambavyo mwanadamu amedhamiria kumfuata Mungu, ikiwa hajawahi kuwa na ushirika wa kweli na Mungu, ama kuwa na uzoefu wa kweli wa maneno ya Mungu, basi ufahamu wake wa Mungu utakuwa mtupu tu au ndoto isiyo na mwisho; kwa kuwa yale yote ambayo unaweza kuwa “umekumbana” nayo katika Mungu kwa kupita, au kukutana Naye uso kwa uso, bado ufahamu wako kuhusu Mungu utakuwa sifuri, na uchaji wako kwa Mungu utakuwa ni maneno matupu tu au mawazo ya kufikirika.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 3)

Watu wengi wanashikilia kusoma maneno ya Mungu siku baada ya siku, kiasi kwamba wanaweka akilini kwa umakini vifungu vyote vinavyotambuliwa sana humo kama vitu vyao vyenye thamani zaidi, na hata zaidi wanayahubiri maneno ya Mungu kila mahali, wakiwatolea na kuwasaidia wengine kwa njia ya maneno Yake. Wanafikiri kuwa kufanya hivi ni kuwa na ushuhuda kwa Mungu, kuwa na ushuhuda kwa maneno Yake, kwamba kufanya hivi ni kufuata njia ya Mungu; wanafikiri kuwa kufanya hivi ni kuishi kulingana na maneno ya Mungu, kwamba kufanya hivi ni kuleta maneno Yake katika maisha yao halisi, kuwa kufanya hivi kutawawezesha kupokea pongezi ya Mungu, na kuokolewa na kukamilishwa. Lakini, hata wanapohubiri maneno ya Mungu, hawazingatii maneno ya Mungu katika matendo, ama kujaribu kujilinganisha na yale yanayofichuliwa katika maneno ya Mungu. Badala yake, wanayatumia maneno ya Mungu ili kupata kuheshimiwa na kuaminiwa na wengine kwa hila, kuingia katika usimamizi wao wenyewe, na kubadhiri na kuiba utukufu wa Mungu. Wanatarajia, kwa ubatili, kutumia nafasi waliyopata kwa kueneza maneno ya Mungu ili kupewa kazi ya Mungu na pongezi Yake. Ni miaka mingapi imepita, lakini sio tu kwamba watu hao hawajaweza kupata kusifiwa na Mungu katika hatua ya kuyahubiri maneno ya Mungu, na sio tu kwamba hawajaweza kugundua njia ambayo wanapaswa kuifuata katika hatua ya kushuhudia maneno ya Mungu, na sio tu kwamba hawajaweza kujisaidia ama kujipatia wao wenyewe katika hatua ya kuwapa na kuwasaidia wengine kwa njia ya maneno ya Mungu, na pia sio tu kwamba hawajaweza kumjua Mungu, ama kuamsha ndani yao uchaji wa kweli wa Mungu, katika mchakato wa kufanya haya yote; bali pia, kwa upande mwingine, kutoelewa kwao kuhusu Mungu kunaongezeka kwa kina zaidi, kutoamini kwao kuhusu Mungu kunazidi kuongezeka zaidi, na mawazo yao kumhusu Yeye yanazidi kutokuwa sahihi. Wakijazwa na kuongozwa na nadharia za kuhusu maneno ya Mungu, wanaonekana kana kwamba zimekuwa sehemu yao kabisa, kana kwamba wanapitia ujuzi wao kwa urahisi bila juhudi, kana kwamba wamepata kusudi lao katika maisha, wito wao, na kana kwamba wamepata maisha mapya na kuokolewa, kana kwamba, maneno ya Mungu yakiwatoka kwa haraka kwenye ulimi kwa kukariri, wameupata ukweli, wamefahamu nia za Mungu, na kugundua njia ya kumjua Mungu, ni kana kwamba, katika mchakato wa kuhubiri maneno ya Mungu, wanakuja kila wakati uso kwa uso na Mungu. Pia, mara nyingi “wanasukumwa” na vipindi vya kulia, na kila wakati wanaongozwa na “Mungu” katika maneno ya Mungu, wanaonekana kuwa wanashikilia bila kukoma kujali Kwake kwa dhati na nia njema, na wakati huo huo wanashikilia wokovu wa Mungu kwa mwanadamu na usimamizi Wake, kuja kujua kiini Chake, na kuelewa tabia Yake ya haki. Kulingana na msingi huu, wanaonekana kuamini hata kwa uthabiti zaidi katika kuwepo kwa Mungu, kuwa na ufahamu zaidi wa hali Yake ya kuinuliwa, na kuhisi hata kwa undani zaidi ukuu Wake na uweza Wake mkuu. Wakiwa wamejawa na ufahamu wao wa kijuujuu wa maneno ya Mungu, itaonekana kuwa imani yao imekua, kuamua kwao kupitia mateso kumetiwa nguvu, na maarifa yao kwa Mungu yamekuwa na kina. Ila hawajui kwamba, ni mpaka watakapopitia maneno ya Mungu kwa kweli, maarifa yao yote kuhusu Mungu na mawazo yao kumhusu Yeye yanatoka kwa mawazo yao wenyewe na dhana zao wenyewe. Imani yao haingeweza kustahimili jaribio la aina yoyote kutoka kwa Mungu, kile wanachoita maisha yao ya kiroho na kimo havingeweza kustahimili majaribu au ukaguzi wa Mungu, azimio lao ni kama ngome iliyojengwa juu ya mchanga, na yale yanayoitwa maarifa yao ya Mungu pia sio zaidi ya ubunifu wa mawazo yao. Kwa hakika, watu hawa, ambao, ni kana kwamba, wameweka juhudi kubwa katika maneno ya Mungu, hawajawahi kutambua imani ya kweli ni nini, utiifu wa kweli ni nini, kujali kwa kweli ni nini, ama maarifa ya kweli ya Mungu ni nini. Wanachukua nadharia, mawazo, maarifa, karama, utamaduni, ushirikina na hata tabia nzuri za binadamu, na kuyafanya kuwa “mtaji na silaha” za kumwamini Mungu na kumfuata Yeye, na hata kuzifanya kuwa misingi ya imani yao kwa Mungu na katika kumfuata Yeye. Wakati uo huo, pia wanachukua mtaji huu na silaha hizi na kuzifanya kuwa hirizi za kichawi ambazo kupitia kwazo wanamjua Mungu, wanazitumia kukabiliana na kushughulika na ukaguzi, majaribio, kuadibu, na hukumu ya Mungu. Mwishowe, wanachopata bado hakijumuishi chochote zaidi ya hitimisho kumhusu Mungu dhana za kidini, ushirikina wa kikabaila, na mambo yote ambayo yanavutia, yanayostaajabisha, na yenye ugumu kuelewa. Mbinu zao za kumjua na kumfafanua Mungu zimetiwa muhuri katika muundo sawa na ule wa watu wanaoamini tu katika Mbingu iliyo Juu, ama Mtu Mzee aliye Angani, wakati uhalisi wa Mungu, kiini Chake, tabia Yake, kile Alichonacho na uwepo Wake, na kadhalika—yote ambayo yanahusiana na Mungu Mwenyewe wa kweli—ni mambo ambayo maarifa yao yameshindwa kuyafahamu, ambayo hayana hata uhusiano kabisa na yako mbali navyo kabisa. Kwa njia hii, ingawa watu hawa wanaishi chini ya utolewaji na ustawishaji wa maneno ya Mungu, hawawezi hata hivyo kutembea kwa kweli katika njia ya kumcha Mungu na kuepuka maovu. Sababu ya kweli ya hili ni kwamba hawajawahi kupata kumfahamu Mungu, wala hawajawahi kuwa na mawasiliano ya kweli ama ushirika Naye, kwa hivyo haiwezekani kwao kufikia maelewano ya pamoja na Mungu, ama kuamsha ndani mwao imani ya kweli katika kumfuata, au kumwabudu Mungu. Kwamba wanapaswa kuzingatia maneno ya Mungu, kwamba wanapaswa kumtazama Mungu—mwelekeo na mtazamo huu umewahukumu kurudi mikono mitupu kutoka kwa jitihada zao, umewahukumu kwa milele yote wasiweze kamwe kutembea katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Lengo ambalo wanalenga, na mwelekeo wanaoelekea, inamaanisha kuwa wao ni maadui wa Mungu milele, na kwamba hata milele hawatawahi kuweza kupokea wokovu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 4)

Iwapo, katika tukio la mwanadamu ambaye amemfuata Mungu kwa miaka mingi na kufurahia ruzuku ya maneno Yake kwa miaka mingi, kama ufafanuzi wake kuhusu Mungu kimsingi utakuwa sawa na ule wa mtu anayesujudu kwa heshima mbele ya sanamu, basi hii ingeashiria kwamba mtu huyu hajapata uhalisi wa maneno ya Mungu. Hii ni kwa sababu hajaingia katika uhalisi wa maneno ya Mungu, na kwa sababu hii uhalisi, ukweli, nia, na matakwa juu ya wanadamu, yote ambayo yamo katika maneno ya Mungu, hayana uhusiano wowote na mtu huyo. Hivyo ni kusema, haijalishi jinsi mtu kama huyo anavyoweza kufanya kazi kwa bidii katika maana ya juu juu ya maneno ya Mungu, yote ni bure: kwani yale anayofuata ni maneno tu, kwa hivyo yale atakayopata yatakuwa pia ni maneno tu. Haijalishi kama maneno yanayonenwa na Mungu ni ya juu juu au ya kina katika mwonekano wa nje, yote ni ukweli ambao ni wa lazima kwa mwanadamu anapoingia katika uzima; ni chemichemi ya maji ya uzima yanayomwezesha kuishi katika roho na mwili. Yanatosheleza kile ambacho mwanadamu anahitaji ili awe hai; ni kanuni na mfumo wa imani wa kuendesha maisha yake ya kila siku; ni njia, lengo, na mwelekeo ambao ni lazima aupitie ili kupokea wokovu; ni kila ukweli ambao anapaswa awe nao kama kiumbe aliyeumbwa mbele za Mungu; na kila ukweli kuhusu jinsi mwanadamu anavyomtii na kumwabudu Mungu. Ni dhamana ambayo inahakikisha kudumu kwa uwepo wa mwanadamu, ni mkate wa kila siku wa mwanadamu, na pia ni nguzo ya msaada inayowezesha mwanadamu kuwa na nguvu na kusimama. Zimejawa na uhalisi wa ukweli ambao kupitia kwazo mwanadamu aliyeumbwa anaishi ubinadamu wa kawaida, zimejawa na ukweli ambao mwanadamu anatumia kutoka kwenye upotovu na kuepuka mitego ya Shetani, zimejaa mafunzo maonyo, uhamasishaji na faraja isiyokwisha ambayo Muumba anampa binadamu aliyeumbwa. Ni ishara ambayo inawaongoza na kuwaelimisha wanadamu kuelewa yale yote yaliyo chanya, ni dhamana inayohakikisha kuwa wanadamu wataishi kwa kudhihirisha na kumiliki yale yote yaliyo ya haki na mema, kigezo ambacho watu, matukio, na vitu vyote vinapimwa, na pia alama ya usafiri inayowaongoza wanadamu kuuelekea wokovu na njia ya mwanga. Na katika uzoefu wa kivitendo wa maneno ya Mungu pekee ndipo mwanadamu anaweza kupewa ukweli na uzima; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kupata kuelewa ubinadamu wa kawaida ni nini, maisha yenye umuhimu ni nini, kiumbe halisi ni nini, utiifu wa kweli kwa Mungu ni nini; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kuelewa anavyofaa kumjali Mungu, jinsi ya kutimiza wajibu ya kiumbe aliyeumbwa, na jinsi ya kumiliki mfano wa mwanadamu halisi; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kuelewa maana ya imani ya kweli na ibada ya kweli; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuelewa nani ndiye Mtawala wa mbingu na nchi na vitu vyote; ni hapa tu ndipo mwanadamu anapoweza kuja kuelewa njia ambayo kwayo Yule ambaye ni Mtawala wa vitu vyote Anatawala, Anaongoza, na kuutosheleza uumbaji; na ni katika hili tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kuelewa na kufahamu njia ambayo kwayo Yule ambaye ni Mtawala wa vitu vyote Anakuwepo, Anadhihirika na kufanya kazi. Akitenganishwa na uzoefu wa kweli wa maneno ya Mungu, mwanadamu hana maarifa ya kweli ama ufahamu katika maneno ya Mungu na ukweli. Mwanadamu wa aina hii ni maiti inayoishi tu, ganda lililoisha, na ufahamu wote unaohusiana na Muumba hauna uhusiano wowote na yeye. Machoni pa Mungu, mwanadamu kama huyo hajawahi kumwamini, ama kuwahi kumfuata, na hivyo Mungu hamtambui yeye kama mwumini Wake wala mfuasi Wake, ama hata kama kiumbe halisi aliyeumbwa.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 5)

Ili kuwa kiumbe halisi aliyeumbwa, sharti ujue Muumba ni nani, uumbaji wa mwanadamu una umuhimu gani, jinsi ya kutekeleza majukumu ya kiumbe, na jinsi ya kumwabudu Bwana wa uumbaji wote, lazima aelewe, ashike, ajue, na kujali kuhusu nia za Muumba, mapenzi Yake, na mahitaji Yake, na lazima atende kulingana na njia ya Muumba—kumcha Mungu na kuepuka maovu.

Kumcha Mungu kuna maana gani? Na mtu anawezaje kuepuka maovu?

“Kumcha Mungu” hakumaanishi woga na hofu isiyoelezeka, wala kukwepa, wala kuweka umbali, wala si ibada ya sanamu ama ushirikina. Bali, ni kuheshimu, kuthamini, kuamini, kuelewa, kujali, kutii, kujiweka wakfu, kupenda, pamoja na ibada isiyo na masharti na isiyo na malalamiko, kulipa na kunyenyekea. Bila ya ufahamu halisi wa Mungu, binadamu hawatakuwa na heshima ya kweli, imani ya kweli, ufahamu wa kweli, kujali au utiifu wa kweli, bali tu hofu na wasiwasi, mashaka pekee, kutokuelewa, kukwepa, na kuepuka; bila maarifa halisi ya Mungu, binadamu hawatakuwa na utakatifu na malipo halisi; bila ujuzi wa kweli wa Mungu, binadamu hawatakuwa na ibada ya kweli na kujisalimisha, wataabudu tu sanamu kwa upofu na ushirikina; bila maarifa halisi juu ya Mungu, binadamu hawawezi kutenda kulingana na njia ya Mungu, ama kumcha Mungu, ama kuepuka maovu. Badala yake, kila tendo na tabia ambayo mwanadamu atajihusisha uasi na ukaidi, na shutuma za kukashfu na hukumu za uwongo kumhusu Yeye, na mienendo miovu inayoenda kinyume na ukweli na maana halisi ya maneno ya Mungu.

Mara tu wanadamu wanapokuwa na imani ya kweli kwa Mungu, watakuwa wa kweli katika kumfuata Yeye na kumtegemea; ni kwa kumwamini na kumtegemea Mungu pekee ndipo binadamu anaweza kuwa na uelewa na ufahamu wa kweli; kukiwa na ufahamu wa kweli wa Mungu kutatokea kumjali Yeye kwa kweli; ni kwa kumjali Mungu kwa kweli pekee ndipo binadamu watakuwa na utiifu wa kweli kwa Mungu; na ni kwa utiifu wa kweli kwa Mungu pekee ndipo binadamu wataweza kujiweka wakfu kwa kweli; na ni kwa kujiweka wakfu kwa kweli kwa Mungu pekee ndipo binadamu wataweza kuwa na malipo yasiyo na masharti na yasiyo na malalamiko; ni kwa kuamini tu na kutegemea kwa kweli, kuelewa na kujali kwa kweli, kutii kwa kweli, kujiweka wakfu kwa kweli na kulipa, ndipo binadamu watakuja kujua kwa kweli tabia na kiini cha Mungu, na kujua utambulisho wa Muumba; ni pale tu watakapopata kumjua Muumba ndipo binadamu wataamsha ndani yao ibada ya kweli na kujisalimisha; watakapokuwa na ibada ya kweli na kujisalimisha kwa Muumba tu ndipo binadamu wataweza kwa kweli kuweka kando njia zao ovu, hivyo ni kusema, watajiepusha na maovu.

Hii inajumuisha mchakato mzima wa “kumcha Mungu na kujiepusha na maovu,” na pia ni maudhui ya jumla katika kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hii ndiyo njia ambayo ni lazima ipitiwe ili kufikia kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

“Kumcha Mungu na kujiepusha na maovu” na kumjua Mungu ni uhusiano usiogawanyishwa na uliounganishwa kwa nyuzi zisizohesabika, na uhusiano kati yao ni dhahiri. Iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kujiepusha na maovu, lazima kwanza amche Mungu kwa kweli; iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kumcha Mungu kwa kweli, lazima awe na maarifa ya kweli kuhusu Mungu; Iwapo mtu anataka kupata maarifa ya Mungu, lazima kwanza apate uzoefu wa maneno ya Mungu, aingie katika uhalisi wa maneno ya Mungu, apitie kuadibu na nidhamu ya Mungu, kuadibu na hukumu Yake; ikiwa mtu anataka kupata uzoefu maneno ya Mungu, lazima aje ana kwa ana na maneno ya Mungu, aje ana kwa ana na Mungu, na kumwomba Mungu Ampe fursa ya kupitia maneno ya Mungu katika kila aina ya mazingira yanayowahusisha watu, matukio na vitu; iwapo mtu anataka kuja ana kwa ana na Mungu na maneno ya Mungu, lazima kwanza awe na moyo wa kweli na wenye uaminifu, awe tayari kuukubali ukweli, kukubali kupitia mateso, awe na azimio na ujasiri wa kujiepusha uovu, na azimio la kuwa kiumbe halisi…. Kwa njia hii, ukiendelea mbele hatua kwa hatua, utamkaribia Mungu zaidi, moyo wako utakuwa safi zaidi, na maisha yako na thamani ya kuwa hai, pamoja na maarifa yako kumhusu Mungu, yatakuwa ya maana zaidi na yatakuwa hata yenye kung’aa zaidi. Mpaka siku moja, utahisi kuwa Muumba sio fumbo tena, kwamba Muumba hajawahi kufichwa kutoka kwako, kwamba Muumba hajawahi kuificha sura Yake kutoka kwako, kwamba Muumba hayuko mbali na wewe hata kidogo, kwamba Muumba siye Yule tena ambaye unamtamani kila mara katika mawazo yako lakini kwamba huwezi kumfikia kwa hisia zako, kwamba Anasimama kwa kweli kama mlinzi kulia na kushoto kwako, Akiruzuku maisha yako, na kudhibiti majaliwa yako. Hayuko katika upeo wa mbali, wala Hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ndiye kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho. Mungu kama huyo Anakuruhusu umpende kutoka moyoni, umshikilie, umweke karibu, umtamani, uhofu kumpoteza, na kutokuwa tayari kumkana tena, kumwasi tena, ama kumwepuka tena ama kumweka mbali. Kile unachotaka ni kumjali tu, kumtii, kulipia kila kitu Anachokupa, na kujisalimisha katika utawala Wake. Haukatai tena kuongozwa, kuruzukiwa, kutazamwa, na kutunzwa na Yeye, haukatai tena kile Anachoamuru na kupangilia kwa ajili yako. Unachotaka tu ni kumfuata, kutembea kando Yake iwe ni kushoto ama kulia Kwake, kile unachotaka ni kumkubali kama uzima wako wa pekee, kumkubali kama Bwana wako wa pekee, Mungu wako wa pekee.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 6)

Imani za Watu Haziwezi Kubadilishwa na Ukweli

Kuna baadhi ya watu wanaoweza kuvumilia magumu; wanaoweza kulipa gharama; tabia yao ya nje ni nzuri sana; wanaheshimika sana; na wanaheshimiwa na wengine. Mnaonaje: Je, tabia kama hii ya nje inaweza kuchukuliwa kama kuweka ukweli katika vitendo? Je, unaweza kusema kwamba mtu huyu anatosheleza nia za Mungu? Kwa nini mara kwa mara watu wanamwona mtu wa aina hii na kufikiria kwamba wao wanamtosheleza Mungu, wanafikiria kwamba wanatembea katika njia kuweka ukweli katika vitendo, kwamba wanatembea katika njia ya Mungu? Kwa nini baadhi ya watu wanafikiria kwa njia hii? Upo ufafanuzi mmoja tu kwa haya. Na ufafanuzi huo ni upi? Sababu ni kwamba kwa watu wengi, maswali kama vile; kuweka ukweli katika vitendo ni nini, kumridhisha Mungu ni nini, ni nini maana ya kuwa na uhalisi wa ukweli—maswali haya hayako wazi sana. Kwa hivyo, kuna baadhi ya watu ambao mara nyingi wanadanganywa na wale ambao kwa nje wanaonekana kuwa wa kiroho, wanaonekana waungwana, wanaonekana kuwa na taswira za ukuu. Kuhusiana na watu hao ambao wanaweza kuzungumza maneno kwa ufasaha na mafundisho, na ambao maneno na matendo yao yanaonekana yanastahili kusifiwa, wale wanaodanganywa nao hawajawahi kuangalia kiini cha matendo yao, kanuni zilizo nyuma ya matendo yao, au malengo yao ni nini. Na hawajawahi kuangalia kama watu hawa wanamtii Mungu kwa kweli, na kama wao ni watu wanaomcha Mungu kwa kweli na kujiepusha na maovu au la. Hawajawahi kutambua kiini cha ubinadamu wa watu hawa. Badala yake, kutoka kwenye hatua ya kwanza ya kuanza kufahamiana nao, kidogo kidogo, wanaanza kuvutiwa na watu hawa, wanawaheshimu watu hawa, na hatimaye watu hawa wanakuwa sanamu zao. Zaidi ya hayo, katika akili za baadhi ya watu, watu hao wanaowaabudu—na ambao wanaamini wanaweza kuziacha familia zao na kazi zao, na wanaoonekana kuwa na uwezo wa juu juu wa kulipa gharama—ndio wanaomridhisha Mungu kwa kweli, na ambao wanaweza kupata matokeo mazuri na hatima nzuri. Katika akili zao, sanamu hizi ndizo ambazo Mungu anazisifu. Ni nini kinachowafanya watu waamini jambo kama hilo? Ni nini kiini cha suala hili? Je, inaweza kusababisha matokeo gani? Hebu kwanza tujadili suala la kiini chake.

Kimsingi, masuala haya kuhusu mitazamo ya watu, mbinu zao za utendaji, ni kanuni zipi za utendaji wanazochagua kufuata, na kile ambacho kwa kawaida kila mmoja anazingatia, hazina uhusiano na mahitaji ya Mungu kwa mwanadamu hata kidogo. Bila kujali kama watu wanazingatia masuala ya juujuu au yale ya kina, au maneno na mafundisho, au uhalisi, watu hawashikilii yale ambayo wanapaswa kushikamana nayo zaidi, wala hawayajui yale ambayo wanapaswa kuyajua zaidi. Sababu ya hili ni kwamba, watu hawaupendi ukweli hata kidogo; kwa hivyo, hawako tayari kutumia muda na juhudi zao katika kutafuta na kuweka katika vitendo kanuni za utendaji zinazopatikana katika matamshi ya Mungu. Badala yake, wanapendelea kutumia njia za mkato, wakihitimisha kile wanachoelewa na kujua kuwa ni utendaji mzuri na tabia njema; muhtasari huu unakuwa lengo lao wenyewe la kufuata, ambalo wanalichukulia kama ukweli wa kutekelezwa. Athari ya moja kwa moja ya haya yote ni kwamba watu wanatumia tabia nzuri ya kibinadamu kama mbadala wa kuweka ukweli katika matendo yao, ambayo pia inatosheleza matamanio yao ya kutaka kupata kibali cha Mungu. Hii inawapa watu mtaji wa kushindana na ukweli, ambao wao pia wanautumia kutoa sababu na kushindana na Mungu. Wakati huo huo, watu pia wanamweka Mungu kando bila uadilifu, wakiwaweka watu wanaowapenda katika nafasi ya Mungu. Kuna sababu moja tu ya msingi ambayo inawafanya watu wawe na vitendo na mitazamo ya kijinga kama hii, au maoni na utendaji wa upande mmoja—na leo Nitawaambia kuhusu hilo. Sababu ni kwamba ingawa watu wengi wanaweza kumfuata Mungu, kumwomba Yeye kila siku, na kusoma neno la Mungu kila siku, hawaelewi kwa hakika nia za Mungu. Hiki ndicho chanzo cha tatizo. Kama mtu aliuelewa moyo wa Mungu, na alijua kile ambacho Mungu anapenda, kile ambacho Anachukia, kile Anachotaka, kile Anachokataa, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anampenda, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu hampendi, ni kiwango gani ambacho Mungu anatumia katika kutoa mahitaji Yake kwa watu, na ni mbinu gani Anazotumia ili kuwakamilisha watu, je, bado mtu kama huyo angeweza kuwa na maoni yake binafsi? Je, watu kama hao wangeweza tu kwenda na kumwabudu mtu mwingine? Je, mwanadamu wa kawaida angeweza kuwa sanamu yao? Watu wanaoelewa nia za Mungu, wana maoni yenye busara zaidi kuliko hayo. Hawataweza kumwabudu mtu mpotovu kiholela, wala, wanapotembea katika njia ya kuweka ukweli katika vitendo, kuamini kwamba kufuata kwa upofu sheria au kanuni chache rahisi ni sawa na kuweka ukweli katika vitendo.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 7)

Kuna Maoni Mengi Kuhusu Kiwango Ambacho Mungu Hutumia Kuamua Matokeo ya Mwanadamu

Kwa sababu kila mmoja anajali matokeo yake, je, mnajua namna ambavyo Mungu huamua matokeo hayo? Na ni kwa njia gani ambayo Mungu huamua matokeo ya mtu? Na je, ni kiwango gani ambacho Mungu anatumia kuamua matokeo ya mtu? Na kwa wakati ambao matokeo ya mtu bado hayajaamuliwa, ni nini ambacho Mungu anafanya ili kufichua matokeo haya? Je, yupo anayejua haya? Kama Nilivyosema muda mfupi uliopita, kuna baadhi ambao tayari wametumia muda mrefu sana kutafiti maneno ya Mungu katika jitihada za kutafuta vidokezo kuhusu matokeo ya watu, kuhusu vipengele ambavyo matokeo hayo yamegawanywa, na kuhusu matokeo mbalimbali yanayowasubiri aina tofauti za watu. Pia wanataka kujua jinsi neno la Mungu linavyoamua matokeo ya watu, ni kiwango cha aina gani ambacho Mungu anatumia, na jinsi hasa Anavyoamua matokeo ya mtu. Mwishowe, hata hivyo, watu hawa hawajaweza kupata majibu yoyote. Kwa hakika, kuna machache ya muhimu yaliyosemwa kuhusu jambo hilo katika matamshi ya Mungu. Kwa nini ni hivyo? Ilimradi matokeo ya watu bado hayajafichuliwa, Mungu hataki kumwambia yeyote kuhusu kile kitakachotokea mwishowe, wala Hataki kumfahamisha yeyote kuhusu hatima yake kabla ya wakati kufika. Sababu ya kufanya hivi ni kwamba Mungu kufanya hivyo hakutaleta manufaa yoyote kwa binadamu. Sasa hivi, Nataka kuwaambia tu kuhusu jinsi ambavyo Mungu anaamua matokeo ya binadamu, kuhusu kanuni Anazotumia katika kazi Yake ili kuamua matokeo ya binadamu, na kuonyesha matokeo hayo, pamoja na kiwango Anachotumia ili kuamua kama mtu ataweza kuishi au la. Je, hiki sicho kile ambacho mnajali zaidi kuhusu? Hivyo basi, ni vipi ambavyo watu wanaamini kuhusu njia ambayo Mungu anaamua matokeo ya binadamu? Mlizungumzia kidogo kuhusu suala hili muda mfupi uliopita. Baadhi yenu mlisema kwamba inahusiana na kufanya wajibu wa mtu kwa uaminifu, kujitumia kwa ajili ya Mungu; baadhi ya watu walisema kumtii Mungu na kumridhisha Mungu; baadhi ya watu walisema kumwacha Mungu akudhibiti; na baadhi ya watu walisema kua na hadhi ya chini…. Mnapoweka ukweli huu katika vitendo, mnapotenda kanuni za kufikiria kwenu, je, mnajua kile ambacho Mungu anafikiria? Je, mmewahi kufikiria kama kuendelea hivi ni kutosheleza nia za Mungu au la? Kama kunakidhi kiwango cha Mungu? Kama kunakidhi mahitaji ya Mungu? Ninaamini kwamba watu wengi hawafikirii sana maswali haya. Wao wanatumia tu sehemu ya neno la Mungu, au sehemu ya mahubiri, au viwango vya watu fulani wa kiroho ambao wanawaabudu, na kujilazimisha kufanya hivi na vile. Wanasadiki kwamba hii ndiyo njia sahihi, kwa hiyo wanaendelea kushikamana nayo na kuifanya, bila kujali kile kitakachowatokea mwishoni. Baadhi ya watu wanafikiri, “Nimeamini kwa miaka mingi sana; nimekuwa nikitenda kwa njia hii siku zote; ninahisi kama nimemridhisha Mungu kabisa; ninahisi pia kuwa nimejifunza mengi kutoka kwa haya. Kwani nimekwishaelewa ukweli mwingi katika kipindi hiki, na nimeelewa mambo mengi ambayo sikuyaelewa awali—hasa, mawazo na mitazamo yangu mingi imebadilika, maadili ya maisha yangu yamebadilika sana, na sasa nina ufahamu mzuri wa ulimwengu huu.” Watu kama hao wanaamini kwamba haya ni mavuno, na kwamba ni matokeo ya mwisho ya kazi ya Mungu kwa binadamu. Kwa maoni yenu, kwa viwango hivi na vitendo vyenu vyote vikiwekwa pamoja—je, mnatosheleza nia za Mungu? Baadhi ya watu watasema kwa uhakika wote, “Bila shaka! Tunatenda kulingana na neno la Mungu; tunatenda kulingana na kile ambacho Aliye juu Alihubiri na kuwasilisha. Sisi siku zote tunafanya wajibu wetu na tunamfuata Mungu bila kukoma, hatujawahi kumwacha Mungu. Hivyo basi tunaweza kusema kwa uhakika kabisa kwamba tunamtosheleza Mungu. Haijalishi ni kiasi gani tunaelewa nia za Mungu, na haijalishi ni kiasi gani tunaelewa neno Lake, daima tumekuwa kwenye njia ya kutafuta kupatana na Mungu. Mradi tu tunachukua hatua sahihi, na kutenda kwa usahihi, basi matokeo yatakuwa sahihi.” Je, mnafikiria nini kuhusu mtazamo huu? Je, ni sahihi? Pengine wapo wale wanaosema: “Sijawahi kufikiria kuhusu mambo haya hapo awali. Mimi nafikiria, mradi tu nikiendelea kufanya wajibu wangu na kutenda kulingana na matakwa ya maneno ya Mungu, basi nitanusurika. Sijawahi kufikiria swali la kama ninaweza kutosheleza moyo wa Mungu, na sijawahi kufikiria kama ninatimiza kiwango kinachohitajika na Yeye. Kwa sababu Mungu hajawahi kuniambia, wala kunipatia maagizo yoyote kwa uwazi, ninaamini kwamba mradi tu nikiendelea kufanya kazi na nisiache, Mungu atatosheka na Yeye hapaswi kuwa na mahitaji yoyote ya ziada kwangu.” Je, kuamini hivi ni sahihi? Kwa maoni Yangu, njia hii ya kutenda, njia hii ya kufikiri, na mitazamo hii—yote yanajumuisha dhana, pamoja na upofu kidogo. Ninaposema hivi, pengine wapo baadhi yenu wanaohisi kuvunjika moyo: “Ni upofu? Kama huu ni ‘upofu,’ basi tumaini letu la wokovu, tumaini letu la kubaki ni dogo sana, na halina uhakika, je, si hivyo? Je, Unaposema hivyo, si sawa na kutumwagia maji ya baridi?” Haijalishi kile mnachoamini, mambo Ninayoyasema na kuyafanya hayanuii kuwafanya ninyi mhisi kama mnamwagiwa maji baridi. Badala yake, yananuia kuboresha uelewa wenu wa nia za Mungu, na kuboresha ufahamu wenu kuhusu kile ambacho Mungu anafikiria, kile ambacho Mungu anataka kutimiza, ni ni watu wa aina gani ambao Anawapenda, kile ambacho Anachukia, kile ambacho Anadharau, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anataka kumpata, na ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anamkataa. Yananuia kupatia akili zako uwazi, na kukupa kufahamu kwa uwazi kuhusu jinsi matendo na mawazo ya kila mmoja wenu yamepotoka kutoka kwenye kiwango kinachohitajika na Mungu. Je, ni muhimu sana kujadili mada hizi? Kwa sababu Ninajua mmeamini kwa muda mrefu, na mmesikiliza mahubiri mengi, lakini kwa hakika haya ndiyo mambo mnayokosa zaidi. Ingawa mmeandika kila ukweli katika daftari zenu, na mmekariri na kuandika katika mioyo yenu baadhi ya mambo ambayo ninyi wenyewe mnaamini kuwa ni ya muhimu, na hata ingawa mmepanga kutumia mambo haya ili kumridhisha Mungu wakati wa kutenda kwenu, kuyatumia wakati mnaona kuwa mnahitaji msaada, kuyatumia ili kupitia nyakati ngumu zilizo mbele yenu, au kuruhusu tu mambo haya yaambatane nanyi mnapoishi maisha yenu. Lakini kulingana na maoni Yangu, haijalishi jinsi mnavyotenda, jinsi mnavyotenda hasa si muhimu sana. Ni nini, basi, kilicho muhimu zaidi? Ni kwamba wakati unatenda, ni lazima ujue moyoni mwako, kwa uhakika kabisa, kama kila kitu unachofanya, kila kitendo, ndicho kile ambacho Mungu anataka au la; na kama matendo yako yote, mawazo yako yote, na matokeo na lengo unalotaka kufikia vinakidhi nia za Mungu na kukidhi matakwa Yake ama la, na vilevile kama Anayakubali ama la. Haya ndiyo mambo ya muhimu zaidi.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 8)

Tembea katika Njia ya Mungu: Mche Mungu na Kujiepusha na Maovu

Kuna msemo ambao mnapaswa kuzingatia. Ninaamini msemo huu ni muhimu sana, kwa sababu Kwangu, unanijia akilini mara nyingi kila siku. Kwa ni nini hivyo? Kwa sababu kila wakati Ninapokumbana na mtu, kila wakati Ninaposikia hadithi ya mtu fulani, na kila wakati Ninaposikia uzoefu wa mtu au ushuhuda wa kumwamini Mungu, kila wakati Ninatumia msemo huu ili kubainisha moyoni Mwangu kama mtu huyu ni aina ya mtu ambaye Mungu anamtaka au la, na kama ni aina ya mtu ambaye Mungu anampenda. Kwa hivyo msemo huu ni upi, basi? Sasa nyinyi nyote mnasubiri kwa hamu. Nitakapoufichua msemo huu, pengine mtakasirika kwa sababu wapo baadhi yenu ambao mmekuwa mkijifanya kuwa mnakubaliana nao kwa miaka mingi. Lakini Kwangu Mimi, Sijawahi kujifanya kuwa nakubaliana nao tu. Msemo huu upo moyoni Mwangu. Hivyo basi msemo huu ni upi? Msemo huuni “tembea katika njia ya Mungu: mche Mungu na kujiepusha na maovu.” Je, hili si neon rahisi sana? Hata ingawa msemo huu unaweza kuwa rahisi, mtu ambaye ana uelewa wa ndani na wa kweli wa msemo huu atahisi kwamba ni wenye uzito mkubwa; kwamba usemi huu ni wa thamani sana kwa utendaji wa mtu; kwamba ni usemi katika lugha ya maisha yenye uhalisi wa ukweli; kwamba inawakilisha lengo la maisha yote kwa wale wanaotafuta kumridhisha Mungu, na kwamba ni njia ya maisha yote ambayo mtu yeyote anayefikiria nia za Mungu anapaswa kufuata. Kwa hivyo mnafikiria nini: Je, msemo huu sio ukweli? Je, una umuhimu kama huo ama la? Vile vile, pengine baadhi yenu wanafikiria kuhusu msemo huu, wakijaribu kuuelewa, na wapo baadhi ambao bado wanautilia shaka. Je, msemo huu ni muhimu sana? Je, ni muhimu zaidi? Je, ni muhimu na unastahili kusisitizwa sana? Pengine wapo baadhi ya watu ambao hawaupendi sana msemo huu kwa sababu wanafikiria kwamba kuchukua njia ya Mungu na kuiweka katika msemo huu mmoja ni kurahisisha kupita kiasi. Kuyachukua yale yote ambayo Mungu aliyasema na kuyafanya yawe msemo mmoja—je, hivi si kumfanya Mungu kuwa yule asiyekuwa na umuhimu sana? Je, hivi ndivyo ilivyo? Huenda ikawa kwamba wengi wenu hamwelewi kikamilifu umuhimu wa kina wa maneno haya. Ingawa ninyi nyote mmeuandika mahali, hamna nia ya kuuhifadhi msemo huu katika mioyo yenu; umeuandika tu kwa urahisi katika daftari lako ili kurejelea na kutafakari katika muda wako wa ziada. Kuna watu wengine ambao hawatajisumbua hata kukariri msemo huu, sembuse hata kujaribu kuutumia vizuri. Lakini kwa nini Nikauzungumzia msemo huu? Licha ya mtazamo wenu, au kile mtakachofikiria, ni lazima Nizungumzie msemo huu, kwa kuwa una uhusiano mkubwa wa jinsi Mungu anavyoamua matokeo ya watu. Haijalishi kama ufahamu wako wa sasa wa msemo huu ni nini, au jinsi mnavyouchukulia, bado Nitawaeleza: kama watu wanaweza kuyaweka maneno ya msemo huu katika vitendo na kuyapitia, na kutimiza kiwango cha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, basi atahakikishiwa kuishi, kisha atahakikishiwa kuwa mtu mwenye matokeo mazuri. Kama huwezi kutimiza kiwango kilichowekwa wazi katika msemo huu, basi inaweza kusemwa kwamba matokeo yako hayajulikani. Hivyo, Ninazungumza kwenu kuhusu msemo huu kwa ajili ya matayarisho yenu ya kiakili, na ili muweze kujua ni kiwango cha aina gani ambacho Mungu anatumia kukupima.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 9)

Mungu Anatumia Majaribio Tofauti ili Kupima Kama Watu Wanamcha Mungu na Kujiepusha na Maovu

Katika kila enzi ya kazi ya Mungu, Yeye huwapa watu baadhi ya maneno Anapofanya kazi ulimwenguni, na kuwaambia kuhusu ukweli fulani. Kweli hizi zinatumika kama njia ambayo watu wanapaswa kuifuata, njia ambayo wanapaswa kuitembea, njia inayowawezesha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, na njia ambayo watu wanapaswa kuiweka katika vitendo na kuitii katika maisha yao na kwenye mkondo wa safari zao za maisha. Ni kwa sababu hizi ambapo Mungu anampa binadamu maneno haya. Binadamu anapaswa kuyatii maneno haya yanayotoka kwa Mungu, na kuyatii ni kupokea uzima. Kama mtu hataweza kuyatii, na hayaweki kwenye matendo, na haishi kwa kudhihirisha maneno ya Mungu katika maisha yake, basi mtu huyo hauweki ukweli katika matendo. Na kama hawaweki ukweli katika matendo, basi hawamchi Mungu na hawaepuki maovu, wala hawawezi kumtosheleza Mungu. Kama mtu hawezi kumtosheleza Mungu, basi hawezi kupokea sifa ya Mungu; mtu wa aina hii hana matokeo. Kwa hivyo, ni kwa jinsi gani, basi, katika mkondo wa kazi Yake, Mungu anaamua matokeo ya mtu? Je, Mungu anatumia njia gani ili kuamua matokeo ya mtu? Pengine bado hamlielewi suala hili kwa sasa, lakini Nitakapowaambia kuhusu mchakato huo, itakuwa wazi kabisa. Hii ni kwa sababu watu wengi tayari wamepitia suala hili wao wenyewe.

Katika mkondo wa kazi ya Mungu, kuanzia mwanzo hadi sasa, Mungu Amepanga majaribio kwa kila mtu—au mnaweza kusema, kila mtu anayemfuata Yeye—na majaribio haya yanakuja kwa ukubwa tofauti. Wapo wale ambao wamepitia jaribio la kukataliwa na familia zao; wapo wale ambao wamepitia jaribio la mazingira mabaya; wapo wale ambao wamepitia majaribio ya kukamatwa na kuteswa; wapo wale ambao wamepitia majaribio ya kukabiliwa na uchaguzi; na wapo wale ambao wamekumbwa na majaribio ya pesa na hadhi. Nikizungumza kwa ujumla, kila moja wenu amekabiliwa na aina zote za majaribio. Kwa nini Mungu anafanya kazi hivyo? Kwa nini Mungu Anamtendea hivi kila mtu? Je, ni matokeo ya aina gani Anayotaka kuyaona? Hii ndiyo hoja muhimu kuhusu kile Ninachotaka kuwaambia: Mungu anataka kuona kama mtu huyu ni yule anayemcha Mungu na kujiepusha na maovu. Maana ya haya ni kwamba wakati Mungu anakupa jaribio, na kukufanya ukabiliwe na baadhi ya hali, Anataka kukupima na kujua kama wewe ndiye yule mtu anayemcha Mungu, mtu anayejiepusha na maovu au la. Kama mtu amekumbwa na wajibu wa kutunza sadaka, na anakutana na sadaka ya Mungu, basi unadhani kwamba hiki ni kitu ambacho Mungu amepanga? Bila shaka! Kila kitu unachokumbana nacho ni kitu ambacho Mungu amepanga. Unapokumbwa na suala hili, Mungu atakuangalia kwa siri, namna unavyochagua, namna unavyotenda, na kile unachofikiria. Matokeo ya mwisho ndiyo ambayo Mungu anayajali zaidi, sababu ni matokeo ambayo yatamruhusu Yeye kupima kama umetimiza kiwango cha Mungu katika jaribio hilo au la. Hata hivyo, wakati watu wanakabiliwa na baadhi ya masuala haya, mara nyingi hawafikirii ni kwa nini wanakumbwa na mambo hayo, au kile kiwango ambacho kinahitajika na Mungu. Hawafikirii kuhusu kile Mungu anachotaka kutoka kwao, kile Anachotaka kupata kutoka kwao. Wanapokumbwa na suala hili, mtu wa aina hii anafikiria tu: “Hili ni jambo ambalo nimekumbwa nalo; lazima niwe makini, nisiwe mzembe! Hata iweje, hii ni sadaka ya Mungu na siwezi kuigusa.” Mtu huyo anaamini kwamba anaweza kutimiza jukumu lake kwa mawazo rahisi kama haya. Je, Mungu ataweza kutosheka na matokeo ya jaribio hili? Au Hatatosheka? Mnaweza kuzungumzia suala hili. (Kama mtu anamcha Mungu katika moyo wake, anapokumbwa na wajibu unaomruhusu kukutana na sadaka ya Mungu, anaweza kufikiria jinsi ilivyo rahisi kuikosea tabia ya Mungu, na hilo litamfanya awe na uhakika wa kuendelea kwa tahadhari.) Jibu lako lipo katika njia sahihi, lakini bado haujafika. Kutembea katika njia ya Mungu hakuhusu kuangalia sharia kwa juujuu. Badala yake, kunamaanisha kwamba unapokabiliwa na suala, kwanza kabisa, unaliangalia kama ni hali ambayo imepangwa na Mungu, wajibu uliopewa wewe na Yeye, au kitu ambacho Amekuaminia wewe, na kwamba unapokabiliana na suala hili, unapaswa kuliona kama jaribio kutoka kwa Mungu. Wakati unapokabiliwa na suala hili, lazima uwe na kiwango, lazima ufikirie kwamba suala hilo limetoka kwa Mungu. Lazima ufikirie ni vipi ambavyo utashughulikia suala hili kiasi cha kwamba utaweza kutimiza wajibu wako, na kuwa mwaminifu kwa Mungu; namna ya kuifanya bila kumkasirisha Mungu; au kuikosea tabia Yake. Tumetoka tu kuzungumzia kuhusu kutunza sadaka. Swala hili linahusu sadaka, na linahusisha pia wajibu wako, jukumu lako. Unahitajika kuwajibikia jukumu hili. Hata hivyo, unapokabiliwa na suala hili, je, kuna jaribio lolote? Lipo! Jaribio hilo linatoka wapi? Jaribio hilo linatoka kwa Shetani, na pia linatokana na tabia ovu na potovu za mwandamu. Kwa sababu kuna jaribio, hili linahusisha kuwa shahidi; kuwa shahidi ni jukumu na wajibu wako pia. Baadhi ya watu husema: “Hili ni suala dogo sana; je, kuna umuhimu wa kufanya suala hili dogo kuwa kubwa hivyo?” Ndiyo pana haja! Kwa sababu ili kutembea katika njia ya Mungu, hatuwezi kuachilia chochote kinachotuhusu sisi wenyewe, au kinachofanyika karibu nasi, hata yale mambo madogo madogo. Haijalishi kama tunadhani tunapaswa kuyazingatia au la, maadamu jambo lolote linatukabili, tusiliache litupite. Mambo yote yanayotutokea yanapaswa kuonwa kama majaribio ya Mungu kwetu. Je, una maoni gani kuhusu mtazamo huu? Kama una mtazamo wa aina hii, basi inathibitisha ukweli mmoja kwamba: Moyo wako unamcha Mungu, na moyo wako upo tayari kujiepusha na maovu. Kama una shauku kama hii ya kumridhisha Mungu, basi kile ambacho unaweka katika vitendo hakiko mbali na kiwango cha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Mara nyingi wale wanaoamini kwamba masuala ambayo hayatiliwi maanani na watu, masuala ambayo kwa kawaida hayatajwi—haya ni mambo madogo tu, na hayana chochote kuhusiana na kuweka ukweli katika matendo. Wakati watu hawa wanakabiliwa na suala kama hilo, hawalifikirii sana na wanaliachilia tu. Lakini ukweli wa mambo ni kwamba, suala hili ni somo ambalo unapaswa kujifunza, somo kuhusu namna ya kumcha Mungu, na namna ya kujiepusha na maovu. Zaidi ya hayo, kile unachopaswa kuzingatia zaidi ni kujua kile ambacho Mungu anafanya wakati suala hili linapokukabili. Mungu yuko kando yako, Anatazama kila neno na tendo lako, na Anatazama kila kitu unachofanya, na ni mabadiliko gani yanayotokea katika mawazo yako—hii ni kazi ya Mungu. Baadhi ya watu wanasema: “Ikiwa hiyo ni kweli, basi ni kwa nini siihisi?” Huihisi kwa sababu jinsi ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu haijawa ndiyo njia ya muhimu zaidi kwako kuishikilia. Kwa hivyo, huwezi kuihisi kazi ya Mungu isiyoeleweka kwa binadamu, ambayo inajidhihirisha kulingana na fikira tofauti na vitendo tofauti vya watu. Wewe upo makini! Suala kubwa ni lipi? Swala dogo ni lipi? Masuala yanayohusu kutembea katika njia ya Mungu hayagawanywi katika masuala makubwa au madogo, yote ni yenye umuhimu—je, mnaweza kulikubali hilo? (Tunaweza kulikubali). Kuhusiana na masuala ya kila siku, kuna yale ambayo watu wanayaona kuwa makubwa sana na muhimu, na mengine yanaonekana kuwa mambo madogo madogo tu. Mara nyingi watu wanayaona masuala haya makubwa kuwa ndiyo ya muhimu zaidi, na wanayachukulia kwamba yametumwa na Mungu. Hata hivyo, kwenye mkondo wa masuala haya makubwa yanayojitokeza, kutokana na kimo kidogo cha watu, na kutokana na kiwango duni cha watu, mara nyingi binadamu haendani sawa na nia za Mungu, hawezi kupata ufunuo wowote, na hawezi kufaidi maarifa yoyote halisi yenye thamani. Kuhusu masuala madogo, haya yanapuuzwa tu na watu, na kuachwa yaondoke moja kwa moja. Kwa hivyo, watu wamepoteza fursa nyingi sana za kuchunguzwa na kujaribiwa mbele za Mungu. Je, inamaanisha nini ikiwa kila mara unapuuza watu, matukio, masuala, na hali ambazo Mungu amekuandalia? Inamaanisha kwamba kila siku, hata kila wakati, unakana ukamilishaji wa Mungu kwako, na uongozi wa Mungu. Kila Mungu anapopanga hali hizi kwako, Yeye anakuangalia kwa siri, Anauchunguza moyo wako, Anaziangalia fikira na hali zako, Anaangalia namna unavyofikiria, Anaangalia namna unavyochukua hatua. Kama wewe ni mtu asiyejali—mtu ambaye hajawahi kujali kuhusu njia ya Mungu, neno la Mungu, au ukweli—basi hutajali, hutatilia maanani kile ambacho Mungu anataka kukamilisha, na yale ambayo Mungu anakuhitaji wewe uyafanye wakati Anapopanga hali hizi kwako. Wala hutajua jinsi watu, matukio na vitu ambavyo unakumbana navyo vinavyohusiana na ukweli au mapenzi ya Mungu. Baada ya kukabiliana na hali nyingi kama hizi na majaribio mengi kama haya, ikiwa Mungu haoni matokeo yoyote ndani yako, je, Atafanyaje? Baada ya kukabiliwa na majaribio mara kwa mara, hujamheshimu Mungu kama Aliye mkuu moyoni mwako, wala hujachukulia zile hali ambazo Mungu amekuandalia kwa uzito—na hujazichukulia kama majaribio au mitihani kutoka kwa Mungu. Badala yake unakataa fursa ambazo Mungu amekupa wewe moja baada ya nyingine, na unaziacha zitokomee mara kwa mara. Je, huku si kutokutii kwa hali ya juu ambako watu wanaonyesha? (Ndiyo, ni kutokutii.) Je, Mungu atahuzunika kwa mambo haya? (Ndiyo, Atahuzunika). Sivyo, Mungu hatahuzunika! Mnaposikia Nikiongea hivi mnashtuka kwa mara nyingine tena. Huenda ukawa unafikiria: “Je, haikusemwa hapo awali kwamba Mungu anahuzunika siku zote? Je, Mungu hatahuzunika? Ni lini basi Mungu atahuzunika? Kwa ufupi, Mungu hatahuzunika kuhusu jambo hili. Kwa hivyo, mtazamo wa Mungu ni upi katika aina hii ya tabia iliyoelezwa hapo juu? Wakati watu wanakataa majaribio na mitihani ambayo Mungu anawapa, wakati wanapoikwepa, kuna mtazamo mmoja tu ambao Mungu anao kwa watu kama hao. Je, mtazamo huo ni upi? Mungu anawadharau watu wa aina hio kutoka kwenye kina cha moyo Wake. Kuna safu mbili za maana ya neno “kudharau.” Je, Ninaelezeaje hilo kutoka kwa mtazamo Wangu? Neno “dharau” linabeba maana ya kukataa na kuchukia. Na je, safu ya pili ya maana ni ipi? Hiyo ndiyo sehemu inayomaanisha kukata tamaa juu ya kitu fulani. Ninyi nyote mnajua maana ya “kukata tamaa,” sivyo? Kwa ufupi, “kudharau” ni neno ambalo linawakilisha mwitikio na mtazamo wa mwisho wa Mungu kwa wale watu ambao wana tabia kama hiyo; ni chuki na karaha ya hali ya juu kwao, na hivyo inapelekea uamuzi wa kukata tamaa juu yao. Huu ndio uamuzi wa mwisho wa Mungu kwa mtu ambaye hajawahi kutembea katika njia ya Mungu, ambaye hajawahi kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Je, nyote mnaweza kuona sasa umuhimu wa msemo huu Niliouzungumzia?

Je, sasa mnaelewa njia ambayo Mungu anatumia katika kuamua matokeo ya watu? (Anapanga hali tofauti kila siku.) Anapanga hali tofauti—hili ni jambo ambalo watu wanaweza kuhisi na kugusa. Kwa hivyo, nia ya Mungu katika kufanya hivi ni nini? Dhumuni ni kwamba Mungu anataka kumpa kila mmoja wetu majaribio katika njia tofauti, katika nyakati tofauti, na katika sehemu tofauti. Ni vipengele vipi vya watu vinavyopimwa katika jaribio? Jaribio huamua kama wewe ni aina ya mtu ambaye anamcha Mungu na kujiepusha na maovu ama la, katika kila suala unalokabiliana nalo, unalosikia kuhusu, unaloliona, na unalolipitia wewe mwenyewe. Kila mtu atakabiliwa na aina hii ya majaribio, kwa sababu Mungu ni mwenye haki kwa watu wote. Baadhi ya watu husema: “Nimemwamini Mungu kwa miaka mingi; inakuaje kwamba sijawahi kukabiliwa na majaribu yoyote?” Unahisi kwamba hujawahi kukabiliwa na jaribio lolote kwa sababu, kila wakati Mungu alipopanga hali kwa ajili yako, hukuzichukulia hali hizo kwa uzito, na hukutaka kufuata njia ya Mungu. Kwa hivyo, huna hisia yoyote ya majaribio ya Mungu. Baadhi ya watu husema: “Nimekabiliwa na majaribio machache, lakini sijui njia bora ya kutenda. Hata ingawa nilitenda, bado sijajua kama nilisimama imara wakati huo wa majaribio.” Watu walioko katika hali ya aina hii bila shaka hawamo katika kundi la wale wachache. Kwa hivyo je, ni kiwango gani ambacho Mungu anawapima watu? Ni kama tu Nilivyosema muda mfupi uliopita: Ni ikiwa unamcha Mungu na kujiepusha na maovu au la, katika kila jambo unalofanya, unalofikiri na kueleza. Hivi ndivyo jinsi inavyoamuliwa kama wewe ni mtu anayemcha Mungu na kujiepusha na maovu. Je, kipengele hiki ni rahisi, au la? Ni rahisi mno kwa kusema, lakini je, ni rahisi kutekeleza? (Si rahisi mno.) Kwa nini si rahisi mno? (Kwa sababu watu hawamjui Mungu, hawajui namna ambavyo Mungu anamfanya binadamu kuwa mkamilifu, na hivyo basi wanapokabiliwa na masuala hawajui namna ya kutafuta ukweli ili kutatua tatizo lao; watu lazima wapitie majaribio mbalimbali, usafishaji, kuadibu, na hukumu kabla ya kuwa na uhalisi wa kumcha Mungu.) Mnasema hivyo, lakini kulingana na vile mnavyojua, kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kunaonekana kuwa rahisi kufanywa kwa sasa. Kwa nini Nasema hivi? Kwa sababu mmesikiliza mahubiri mengi, na mmepokea kiwango kikubwa cha kunyunyiziwa kwa uhalisi wa ukweli. Hii imewaruhusu kuelewa namna ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kwa mujibu wa nadharia na kufikiria. Kuhusiana na jinsi ya kuweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu katika vitendo, maarifa haya yote yamekuwa yenye manufaa na yamewafanya mhisi kwamba kitu kama hicho kinaweza kufanyika kwa urahisi. Basi ni kwa nini katika uhalisia wa mambo watu hawajawahi kukitimiza? Hii ni kwa sababu kiini cha asili ya binadamu hakimchi Mungu na kinapenda maovu. Hiyo ndiyo sababu halisi.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 10)

Kutomcha Mungu na Kutojiepusha na Maovu ni Kumpinga Mungu

Hebu tuanze kwa kuangazia ni wapi ambapo msemo huu “kumcha Mungu na kujiepusha na maovu” ulitokea. (Kitabu cha Ayubu.) Sasa kwa vile mmemtaja Ayubu, hebu tumzungumzie. Katika nyakati za Ayubu, je, Mungu alikuwa akifanya kazi kwa ajili ya wokovu na ushindi wa wanadamu? Hakufanya hivyo, sivyo? Na kuhusiana na Ayubu, ni maarifa ya kiwango gani aliyokuwa nayo kumhusu Mungu kwa wakati huo? (Si mengi.) Je, Ayubu alikuwa na maarifa mengi au kidogo kuhusu Mungu kuliko mliyo nayo ninyi sasa hivi? Kwa nini hamwezi kuthubutu kujibu? Hili ni swali rahisi sana kujibu. Ni kidogo! Hilo halina shaka! Sasa hivi mpo uso kwa uso na Mungu, uso kwa uso na neno la Mungu. Maarifa yenu ya Mungu ni mengi zaidi kuliko yale ya Ayubu. Kwa nini Naleta suala hili? Kwa nini Ninaongea hivi? Ningependa kuwaeleza ukweli mmoja, lakini kabla Sijafanya hivyo, Ningependa kuwauliza swali: Ayubu alijua machache sana kumhusu Mungu, lakini bado aliweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kwa hivyo, ni kwa nini watu siku hizi wanashindwa kufanya hivyo? (Wamepotoka sana.) “Wamepotoka sana”—hili ni jambo la kijuujuu linalosababisha tatizo hili, lakini siwezi kulitazama kwa namna hiyo kamwe. Mara nyingi mnachukua mafundisho na maneno yanayotumiwa mara kwa mara, kama vile “upotovu mkubwa,” “kuasi dhidi ya Mungu,” “kutokuwa mwaminifu kwa Mungu,” “kukosa utiifu,” “kutopenda ukweli,” na kadhalika, mmetumia maneno kama haya katika kuelezea kiini cha kila swali. Hii ni njia isiyofaa ya kufanya mazoezi. Kutumia jibu moja katika kuelezea maswali yaliyo na asili tofauti, bila shaka, inaibua mashaka ya kuukufuru ukweli na Mungu. Sipendi kusikia jibu la aina hii. Hebu fikiria! Hakuna yeyote kati yenu ambaye amefikiria kuhusu suala hili, lakini kila siku Mimi Ninaliona, na kila siku Mimi Ninalihisi. Kwa hivyo, mnapolifanya, Mimi Ninatazama. Wakati mnapolifanya, hamwezi kuhisi kiini halisi cha suala hili. Lakini wakati Ninapoliona, Ninaweza kuona kiini chake, na Ninaweza kuhisi kiini chake. Kwa hivyo, kiini hiki ni kipi basi? Kwa nini watu siku hizi hawawezi kumcha Mungu na kujiepusha na maovu? Majibu yenu yako mbali na kuweza kuelezea kiini cha swali hili, wala hayawezi kulitatua. Hiyo ni kwa sababu ina chanzo ambacho ninyi hamkijui. Je, chanzo hicho ni nini? Ninajua mnataka kusikia kuhusu hilo, kwa hivyo Nitawaambia kuhusu chanzo cha swali hili.

Tangu Mungu Alipoanza kufanya kazi, je, Amewachukuliaje wanadamu? Mungu amewaokoa; Amewaona wanadamu kama washiriki wa familia Yake, kama walengwa wa kazi Yake, kama wale Aliotaka kuwashinda na kuwaokoa, na kama wale Aliotaka kuwakamilisha. Huu ndio ulikuwa mtazamo wa Mungu kwa binadamu mwanzoni mwa kazi Yake. Hata hivyo, je, mtazamo wa wanadamu kwa Mungu ulikuwa ni upi kwa wakati huo? Mungu alikuwa hafahamiki kwa wanadamu, na watu walimwona Mungu kama mgeni. Inaweza kusemwa kwamba, mtazamo wao kwa Mungu haukuleta matokeo sahihi, na kwamba hawakuwa na ufahamu wa wazi kuhusu jinsi wanavyopaswa kumtendea Mungu. Kwa hivyo, walimtendea Yeye jinsi wapendavyo, na wakafanya chochote walichopenda. Je, walikuwa na maoni yoyote kumhusu Mungu? Hapo mwanzo, binadamu hawakuwa na maoni yoyote kumhusu Mungu. Maoni ya binadamu kama yalivyojulikana, yalikuwa tu na baadhi ya dhana na fikira kumhusu Mungu. Kile ambacho kiliendana na dhana za watu kilikubalika; na kile ambacho hakikuendana na dhana zao, walitii kijuujuu, lakini ndani kabisa walihisi kuwa na mgongano mkubwa na waliipinga. Huu ndio ulikuwa uhusiano kati ya mwanadamu na Mungu hapo mwanzo: Mungu alimwona mwandamu kama mshiriki wa familia, lakini binadamu alimchukulia Mungu kama mgeni. Lakini baada ya kipindi cha kazi ya Mungu, binadamu alielewa hatimaye kile ambacho Mungu alikuwa akijaribu kutimiza. Wanadamu walikuja kuelewa kwamba Mungu ndiye aliyekuwa Mungu wa kweli, na hatimaye wakajua kile ambacho binadamu angeweza kupata kutoka kwa Mungu. Je, binadamu alimchukuliaje Mungu kwa wakati huu? Alimchukulia Mungu kama tegemeo kuu, akitumai kupokea neema, kupokea baraka, na kupokea ahadi Zake. Je, kwa wakati huu, Mungu alimchukuliaje binadamu? Mungu alimchukulia binadamu kuwa mlengwa wa ushindi Wake. Mungu alitaka kuyatumia maneno ili kumhukumu binadamu, kumpima binadamu, kumpa majaribio binadamu. Lakini kwa wanadamu wakati huu hasa, Mungu alikuwa kifaa ambacho wangeweza kutumia ili kutimiza malengo yao wenyewe. Watu waliona kwamba ukweli uliotolewa na Mungu ungeweza kuwashinda na kuwaokoa, kwamba walikuwa na fursa ya kupata vitu walivyotaka kutoka Kwake, na pia kufikia malengo waliyotaka. Kwa sababu ya hili, uaminifu mdogo ulijitokeza katika mioyo yao, na wakawa tayari kumfuata Mungu huyu. Muda ulipita, na kwa sababu watu walipata maarifa ya juujuu na ya kimafundisho kuhusu Mungu, inaweza hata kusemwa kwamba wanadamu walikuwa wameanza “kumfahamu” Mungu na maneno Aliyoyasema, mahubiri Yake, kweli Alizotoa, na kazi Yake. Kwa hivyo, watu walifikiria kimakosa kwamba Mungu hakuwa mgeni tena, na kwamba walikuwa tayari wakitembea katika njia ya kupatana na Mungu. Mpaka sasa, watu wamesikiliza mahubiri mengi ya ukweli, na wamepitia kazi nyingi ya Mungu. Hata hivyo, kwa sababu ya maingiliano na vizuizi vinavyosababishwa na mambo na hali nyingi tofauti, watu wengi hawawezi kufanikisha kuweka ukweli katika vitendo, wala hawawezi kumridhisha Mungu. Watu wanazidi kua walegevu na wanazidi kukosa ujasiri. Wanazidi kua na hisia kwamba matokeo yao wenyewe hayajulikani. Hawathubutu kuja na mawazo yoyote ya kupita kiasi, na hawatafuti kufanya maendeleo; wanafuata tu kwa kusita, kwenda mbele, hatua kwa hatua. Kuhusiana na hali ya sasa ya wanadamu, je, Mungu ana mtazamo gani kwao? Anatamani tu kuwapa kweli hizi, na kuwaweka hatua kwa hatua katika njia Yake, na kisha kupanga hali mbalimbali ili kuwajaribu kwa njia tofauti. Lengo Lake ni kuchukua maneno haya, ukweli huu, na kazi Yake, na kuleta matokeo, ambapo wanadamu wataweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Watu wengi ambao Nimewaona wanachukua maneno ya Mungu na kuyachukulia tu kama mafundisho, kama barua tu, wanayachukulia kama kanuni zinazopaswa kufuatwa. Katika matendo na usemi wao, au wanapokabiliwa na majaribu, hawachukulii njia ya Mungu kama njia ambayo wanapaswa kuifuata. Hii ni kweli hasa wakati watu wanapokabiliwa na majaribu makubwa; Sijaona mtu yeyote ambaye amekuwa akitenda katika mwelekeo wa kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kwa sababu ya hili, mtazamo wa Mungu kwa wanadamu umejaa chuki na chuki kubwa! Ijapokuwa Mungu amewapa watu majaribio kadhaa, hata mara mia moja, bado hawana mtazamo wowote wa wazi wa kuonyesha azimio lao kwamba: “Nataka kumcha Mungu na kujiepusha na maovu!” Kwa kuwa watu hawana azimio hili na hawaonyeshi ishara kama hii, mtazamo wa sasa wa Mungu kwao, sio sawa na ulivyokuwa hapo zamani, Alipowapa rehema, uvumilivu, ustahimilivu, na subira Yake. Badala yake, Amekatishwa tamaa sana na binadamu. Je, ni nani aliyesababisha kukata tamaa huku? Je, mtazamo ambao Mungu anao kwa binadamu, unamtegemea nani? Unamtegemea kila mtu anayemfuata Mungu. Kwenye mkondo wa miaka Yake mingi ya kazi, Mungu ametoa mahitaji mengi kwa binadamu, na kupangilia hali nyingi kwa binadamu. Lakini haijalishi jinsi ambavyo binadamu ametenda, na haijalishi ni mtazamo upi ambao binadamu anao kwa Mungu, binadamu hawezi kutenda kwa njia sawa kulingana na malengo ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kwa hivyo, Nitajumuisha yote haya kwa msemo mmoja, na kuweza kutumia msemo huu kuelezea kila kitu ambacho tumeweza kuzungumzia kuhusiana na ni kwa nini watu hawawezi kutembea katika njia ya Mungu—ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Msemo huu ni upi? Msemo huu ni: Mungu huwachukulia wanadamu kama walengwa wa wokovu Wake, na walengwa wa kazi Yake; wanadamu wanamchukulia Mungu kama adui yao, na kama Aliye kinyume nao. Je, unalielewa suala hili sasa? Kile ambacho ni mtazamo wa binadamu; kile ambacho ni mtazamo wa Mungu; kile ambacho ni uhusiano wa binadamu na Mungu—hivi vyote viko wazi sana kwa sasa. Haijalishi ni mahubiri mengi kiasi gani umesikiliza, yale mambo ambayo umefikia hitimisho lako mwenyewe, kama vile kuwa mwaminifu kwa Mungu, kumtii Mungu, kutafuta njia ya kupatana na Mungu, kutaka kutumia maisha yote kwa ajili ya Mungu, na kutaka kuishi kwa ajili ya Mungu—Kwangu, mambo hayo si mifano ya kufuata njia ya Mungu kwa uangalifu, ambayo ni kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Badala yake, ni njia mbalimbali ambazo mnaweza kufikia malengo fulani. Ili kufikia malengo hayo, unafuata kanuni fulani bila kupenda. Na ni kanuni hizi hasa ambazo huwapeleka watu mbali zaidi kutoka katika njia ile ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, na kumweka Mungu katika upinzani na binadamu kwa mara nyingine tena.

Mada ya leo ni nzito kidogo, lakini haijalishi ni nini, bado Ninatumai kwamba wakati unapitia uzoefu ujao, na nyakati zijazo, utaweza kufanya kile ambacho Nimekuambia hivi punde. Usimchukulie Mungu kama hewa tupu-kana kwamba Anakuwepo tu wakati Yeye ni wa manufaa kwako, lakini wakatiambao humhitaji unahisi kwamba Yeye hayupo. Mara tu unapokuwa na wazo kama hilo katika ufahamu wako bila kujua, tayari umemkasirisha Mungu. Pengine kuna watu wanaosema, “Simchukulii Mungu kama hewa tupu. Mimi namwomba Yeye kila mara na ninajaribu kumridhisha Yeye, na kila kitu ninachofanya kipo ndani ya upeo, kiwango, na kanuni ambazo Mungu anahitaji. Bila shaka sifanyi kulingana na mawazo yangu mwenyewe.” Ndio, njia hii ambayo unafanya mazoezi ni sahihi. Hata hivyo, je, unafikiria nini unapokutana ana kwa ana na tatizo? Je, unatenda vipi unapokabiliwa na suala? Baadhi ya watu huhisi kwamba Mungu yupo wakati wanapomwomba Yeye, na kumsihi awasikilizea. Lakini wakati wanapokabiliwa na suala wanakuja na mawazo yao wenyewe na wanataka kuyatii. Hapa Mungu anachukuliwa kama hewa tupu. Hali ya aina hii inamfanya Mungu kutokuwepo katika akili zao. Watu wanafikiri kwamba Mungu anafaa kuwepo wakati wanapomhitaji Yeye, na wakati hawamhitaji Mungu hafai kuwepo. Watu wanafikiri kwamba kutenda kulingana na mawazo yao wenyewe inatosha. Wanaamini kuwa wanaweza kufanya chochote wanachopenda; hawaamini kwamba wanahitaji kutafuta njia ya Mungu. Watu ambao kwa sasa wamo katika hali ya aina hii, na wamekwama katika hali ya aina hii—je, hawaoni kwamba karibu wataingia hatarini? Baadhi ya watu husema: “Haijalishi kama karibu nitaingia hatarini au la, nimeamini kwa miaka mingi sana, na ninaamini kwamba Mungu hataniacha, kwa sababu Asingeweza kustahimili kuniacha mimi.” Watu wengine husema: “Nimemwamini Bwana tangu nilipokuwa tumboni mwa mama yangu. Imekuwa takriban miaka arobaini au hamsini, kwa hiyo katika suala la muda, ninastahili zaidi kuokolewa na Mungu, na ninastahili zaidi kuishi. Katika kipindi cha miongo hii minne au mitano, niliiacha familia yangu na kazi yangu. Nilijitolea kila kitu nilichokuwa nacho kwa Mungu, vitu kama vile pesa, hadhi, starehe, na wakati wa kuwa na familia yangu. Sijala vyakula vingi vitamu, sijafurahia burudani nyingi; sijatembelea sehemu nyingi za kuvutia; nimeweza hata kupitia mateso ambayo hata watu wa kawaida wasingevumilia. Kama Mungu hawezi kuniokoa mimi kwa sababu ya haya yote, basi mimi natendewa kwa njia isiyo ya haki, na siwezi kuamini katika Mungu wa aina hii.” Je, kuna watu wengi walio na mtazamo wa aina hii? (Wapo wengi sana.) Basi leo Nitawasaidia kuelewa ukweli mmoja: Kila mmoja wa hao anayeshikilia mtazamo wa aina hii, anachukua hatua zitakazomdhuru yeye mwenyewe. Hii ni kwa sababu wanatumia maoni yao binafsi katika kuyafunika macho yao. Ni fikira hizi hasa, pamoja na hitimisho zao binafsi, zinazochukua nafasi ya kiwango cha kile ambacho Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu, ndizo zinazowazuia kukubali nia za kweli za Mungu, na kuwafanya wasiweze kuhisi uwepo wa kweli wa Mungu, na kuwafanya pia wapoteze fursa yao ya kukamilishwa na Mungu, na kutokuwa na sehemu au ushiriki katika ahadi ya Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 11)

Jinsi Mungu Anavyoamua Matokeo Ya Mwanadamu na Viwango Ambavyo Anatumia Kuamua Matokeo ya Mwanadamu

Kabla ya kuwa na mitazamo au hitimisho zako binafsi, unapaswa kwanza kuelewa mtazamo wa Mungu kwako ni upi, na kile Anachofikiria, kisha unaweza kuamua kama mawazo yako mwenyewe ni sahihi au la. Mungu hajawahi kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya mtu, na Hajawahi kutumia kiwango cha mateso yaliyovumiliwa na mtu katika kuamua matokeo yake. Kwa hivyo, basi, Mungu anatumia kiwango gani katika kuamua matokeo ya mtu? Kutumia kipimo cha wakati katika kuamua matokeo ya mtu—hii ndiyo inalingana zaidi na dhana za watu. Na pia kuna wale watu ambao mara nyingi mnawaona, wale ambao kwa wakati fulani walijitolea sana, wakatumia muda mwingi sana, wakagharamika sana, wakateseka sana. Hawa ndio, kwa maoni yenu, wanaweza kuokolewa na Mungu. Kile tu ambacho watu hawa wanaonyesha, yote wanayoishi kwa kudhihirisha, ndiyo hasa dhana ya wanadamu kuhusu kiwango ambacho Mungu anatumia kuamua matokeo ya binadamu. Haijalishi kile unachoamini, Sitaorodhesha mifano hii moja baada ya nyingine. Ili kuiweka kwa ufupi, chochote kile ambacho si kiwango kilicho ndani ya mawazo ya Mungu mwenyewe kinatokana na mawazo ya mwanadamu, na mambo hayo yote ni mawazo ya kibinadamu. Ikiwa unasisitiza kwa upofu dhana na matamanio yako mwenyewe, je, matokeo yatakuwa ni yapi? Ni dhahiri kabisa kwamba matokeo ya hili yanaweza tu kuwa Mungu atakukataa. Hii ni kwa sababu kila mara unajivunia sifa zako mbele za Mungu, unashindana na Yeye, na kubishana Naye, na hujaribu kuelewa kwa kweli mawazo Yake, wala hujaribu kuelewa nia Zake au mtazamo Wake kwa wanadamu. Unapoendelea kwa namna hii, unajiheshimu wewe mwenyewe kama mkuu; inakua humheshimu Mungu kama mkuu. Unajiamini wewe mwenyewe; humwamini Mungu. Mungu hamtaki mtu wa aina hii, na Mungu hatamwokoa mtu wa aina hii. Kama utaweza kuachilia mtazamo wa aina hii, na zaidi ya hayo, urekebishe maoni hayo yasiyo sahihi uliyokuwa nayo hapo awali, ikiwa utaweza kuendelea kulingana na matakwa ya Mungu; ikiwa utaweza kutenda kwa njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kuanzia sasa na kuendelea; ikiwa utaweza kumheshimu Mungu na kumwona kama mkuu katika mambo yote; na usitumie matamanio yako binafsi, mitazamo, au imani ili kujifafanua nwenyewe na kumfafanua Mungu. Na kama, badala yake, unatafuta nia za Mungu katika hali zote, kama utafikia utambuzi na uelewa wa mtazamo wa Mungu kwa wanadamu, na kama utamridhisha Yeye kwa kufikia viwango Vyake—kufanya hivyo kutapendeza! Hii itamaanisha kwamba upo karibu kuingia katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kwa kuwa Mungu hatumii fikira, mawazo, na mitazamo mbalimbali ya watu, kama viwango vya kuamua matokeo yao, basi ni kiwango cha aina gani ambacho Anatumia katika kuamua matokeo ya watu? Mungu anatumia majaribio kuamua matokeo ya watu. Kuna viwango viwili vya kutumia majaribio ili kuamua matokeo ya watu: Kiwango cha kwanza ni idadi ya majaribio ambayo watu wanapitia, na kiwango cha pili ni matokeo ya watu katika majaribio hayo. Ni viashiria hivi viwili vinavyoamua matokeo ya mtu. Sasa, hebu tufafanue viwango hivi viwili.

Kwanza kabisa, unapokabiliwa na jaribio kutoka kwa Mungu (Inawezekana kwamba katika macho yako jaribio hili ni dogo sana na halifai kutajwa), Mungu atakufanya uwe na ufahamu kabisa kwamba huu ni mkono wa Mungu juu yako, na kwamba ni Mungu ambaye amepangilia hali hizi zote kwako. Wakati kimo chako hakijakomaa, Mungu atapanga majaribio ili kuweza kukupima. Majaribio haya yatalingana na kimo chako, yale ambayo unaweza kuelewa, na yale ambayo unaweza kustahimili. Ni sehemu gani kwako inayojaribiwa? Ni mtazamo wako kwa Mungu. Je, mtazamo huu ni muhimu sana? Bila shaka ni muhimu! Ina umuhimu maalumu! Kwa sababu mtazamo huu wa binadamu ndiyo matokeo ambayo Mungu anayataka, ndicho kitu cha muhimu zaidi kuliko vyote kwa Mungu. Vinginevyo, Mungu asingetumia juhudi Zake kwa watu kwa kushiriki katika kazi ya aina hiyo. Mungu anataka kuona mtazamo wako Kwake, kupitia kwa majaribio haya; Anataka kujua kama uko kwenye njia sahihi na Anataka kujua kama unamcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hivyo basi, bila kujali kama unaelewa ukweli mwingi au kidogo kwa wakati huo, bado utakabiliwa na majaribio ya Mungu, na kufuatia ongezeko lolote katika kiwango chochote cha ukweli unaouelewa, Mungu ataendelea kupangilia majaribio sawa na hayo kwako. Wakati unapokabiliwa kwa mara nyingine tena na jaribio, Mungu anataka kuona iwapo maoni yako, mawazo yako, na mtazamo wako Kwake umepata ukuaji wowote katika kipindi cha muda. Baadhi ya watu husema: “Kwa nini siku zote Mungu anataka kuona mitazamo ya watu? Kwani Mungu hajaona namna wanavyouweka ukweli katika matendo? Kwa nini Atake tena kuona mitazamo ya watu?” Huku ni kupayuka kipuuzi! Ikizingatiwa kwamba Mungu anafanya kazi kwa namna hii, nia Yake lazima iwe humo. Siku zote Mungu anawaangalia watu Akiwa kando yao, Akiangalia kila neno na tendo lao, kila tendo na kusonga kwao, na hata kila fikira na wazo lao. Kila kitu kinachotokea kwa watu: matendo yao mema, makosa yao, dhambi zao, na hata kuasi na kusaliti kwao, Mungu atazirekodi hizizote kama ushahidi wa kuamua matokeo yao. Kadiri kazi ya Mungu inavyoendelea kuimarika hatua kwa hatua, unasikia ukweli zaidi na zaidi, unakubali mambo mazuri zaidi na zaidi, taarifa nzuri, na uhalisia wa kweli. Kwenye mkondo wa mchakato huu, mahitaji ya Mungu kwako yataongezeka pia. Wakati huo huo, Mungu atapanga majaribio makubwa zaidi kwako. Lengo Lake ni kuchunguza kama mtazamo wako kwa Mungu umekomaa mpaka sasa. Bila shaka, kwenye kipindi hiki, mtazamo ambao Mungu anahitaji kwako unaingiliana na uelewa wako wa uhalisi wa ukweli.

Kadiri kimo chako kinavyoongezeka polepole, kile kiwango ambacho Mungu atahitaji kutoka kwako kitaendelea kuongezeka taratibu pia. Ikiwa bado hujakomaa, Mungu atakupa kiwango kidogo sana; wakati kimo chako kitakapokuwa kikubwa kidogo, Mungu atakupa kiwango cha juu zaidi kidogo. Lakini Mungu atafanya nini baada ya kuwa umeelewa ukweli wote? Mungu atahakikisha kuwa unakabiliana na hata majaribio makubwa zaidi. Katikati ya majaribio haya, kile Mungu anachotaka kupata, kile Mungu anachotaka kuona, ni maarifa yako ya kina zaidi ya Mungu na uchaji wa kweli Kwake. Kwa wakati huu, mahitaji ya Mungu kwako yatakuwa ya juu zaidi “makali zaidi” kuliko wakati ambapo kimo chako kilikuwa kidogo zaidi (watu wanaona kwamba hali hii ni kali, lakini kwa hakika Mungu Anaiona kama inayostahimilika). Wakati Mungu anawapa watu majaribio, ni uhalisia wa aina gani ambao Mungu anataka kuunda? Mungu anauliza kila mara kwamba watu wampe Yeye mioyo yao. Baadhi ya watu watasema: “Mtu anawezaje kufanya hivyo? Natekeleza wajibu wangu, niliacha nyumba yangu na riziki yangu, niligharamika kwa sababu ya Mungu. Hii yote si mifano ya kuutoa moyo wangu kwa Mungu? Ni kwa namna gani tena ningeweza kuutoa moyo wangu kwa Mungu? Yaweza kuwa kwamba, hii si mifano ya kuutoa moyo wangu kwa Mungu? Mahitaji mahususi ya Mungu ni yapi?” Mahitaji haya ni mepesi mno. Kwa hakika, kuna baadhi ya watu ambao tayari wameitoa mioyo yao kwa Mungu katika viwango tofauti na awamu mbalimbali za majaribio yao. Lakini idadi kubwa ya watu hawaikabidhi mioyo yao kwa Mungu. Wakati Mungu anakupa jaribio, Mungu anataka kujua kama moyo wako uko pamoja na Yeye, pamoja na mwili au pamoja na Shetani. Mungu anapokupa jaribio, Mungu anataka kujua kama unasimama kinyume na Yeye au kama unasimama katika hali ambayo inalingana na Yeye, na kutaka kuona pia kama moyo wako uko upande Wake. Wakati haujakomaa na unakabiliwa na majaribio, kiwango cha imani yako kiko chini, na huwezi kujua hasa ni nini ambacho unahitaji kufanya ili kutosheleza nia za Mungu kwa sababu una uelewa mdogo wa ukweli. Licha ya haya yote, bado unaweza kumwomba Mungu kwa dhati na kwa unyofu, kuwa radhi kuutoa moyo wako kwa Mungu, na kumwacha Yeye akutawale, na kuwa radhi kumpa Mungu yale mambo unayosadiki kuwa yenye thamani zaidi. Hii ndiyo maana ya wewe kuwa tayari umempa Mungu moyo wako. Unaposikiliza mahubiri mengi zaidi na zaidi, na kuelewa ukweli zaidi na zaidi kimo chako kitaanza kukomaa kwa utaratibu. Kiwango ambacho Mungu anahitaji kutoka kwako si sawa na kile ambacho ulikuwemo wakati ulikuwa hujakomaa; Anahitaji kiwango cha juu zaidi kuliko hicho. Watu wanapotoa mioyo yao polepole kwa Mungu, mioyo yao inaanza kuwa karibu zaidi na zaidi kwa Mungu; kadri watu wanavyoweza kumkaribia Mungu kwa kweli, ndivyo wanavyozidi kuwa na mioyo inayomcha Mungu. Mungu anahitaji moyo wa aina hiyo.

Wakati Mungu anataka kuumiliki moyo wa mtu, Atawapa majaribio mengi. Kwenye majaribio haya, kama Mungu hatauchukua moyo wa mtu huyu, wala Haoni kama mtu huyu ana mwelekeo wowote—hiyo ni kusema Haoni kwamba mtu huyu anafanya mambo au anatenda kwa njia ya kumcha Mungu, na haoni mtazamo na azimio ambalo huepuka uovu kutoka kwa mtu huyu. Kama hivi ndivyo ilivyo, basi baada ya majaribio mengi, subira ya Mungu kwa mtu huyu binafsi itaondolewa, na Hatamvumilia mtu huyu tena. Hataweza kuwapa watu kama hawa majaribio, na Hataweza tena kuwashughulikia. Basi hiyo inamaanisha nini kwa matokeo ya mtu huyu? Inamaanisha kwamba hawatakuwa na matokeo. Yawezekana kwamba mtu huyu hajafanya maovu yoyote. Yawezekana pia kwamba watu hawa hawajafanya chochote cha kuvuruga au kutatiza. Yawezekana kuwa watu hawa hawajampinga Mungu waziwazi. Hata hivyo, moyo wa mtu huyu umefichwa kutoka kwa Mungu. Hawajawahi kuwa na mwelekeo na mtazamo wa wazi kwa Mungu, na Mungu hawezi kuona waziwazi kwamba moyo wake umekabidhiwa Kwake, na Yeye Hawezi kuona waziwazi kwamba mtu huyu anatafuta kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Mungu hana subira tena kwa watu hawa, Hatawagharamikia tena, Hatatoa tena rehema Yake kwao, na Hatafanya kazi kwao tena. Maisha ya imani ya mtu huyu katika Mungu tayari hayapo tena. Hii ni kwa sababu katika majaribio yote mengi ambayo Mungu amempa mtu huyu, Mungu hajapata matokeo Anayotaka. Kwa hivyo, kuna idadi ya watu ambao Sijawahi kuona mwangaza na nuru ya Roho Mtakatifu. Je, inawezekanaje kuona hili? Mtu wa aina hii anaweza kuwa amemwamini Mungu kwa miaka mingi, na kwa juu juu amekuwa na bidii sana. Wamesoma vitabu vingi, wameshughulikia mambo mengi, wamejaza zaidi ya madaftari 10 na maelezo, na wamefahamu barua na mafundisho mengi. Hata hivyo, hakuna ukuaji wowote unaoonekana, na kamwe hakuna mtazamo wowote unaoonekana kwa Mungu kutoka kwa mtu huyu, wala hakuna mwelekeo wowote wa wazi. Hiyo ni kusema kwamba huwezi kuona moyo wa mtu huyu. Mioyo yao daima imefungwa, mioyo yao imetiwa muhuri—imefungwa kwa Mungu, kwa hivyo Mungu hajauona moyo wa kweli wa mtu huyu, Hajaona hofu ya kweli ya mtu huyu kwa Mungu, na hata zaidi, Hajaona jinsi mtu huyu anatembea katika njia ya Mungu. Kama mpaka sasa Mungu hajampata mtu wa aina hii, je,Anaweza kuwapata katika siku za usoni? Hawezi! Je, Mungu ataendelea kusukumiza mbele mambo ambayo hayawezi kupatikana? Hatafanya hivyo! Mwelekeo wa Mungu kwa watu kama hawa, hivyo basi ni nini? (Anawasukumia mbali, Hawasikilizi.) Yeye hawasikilizi! Mungu hasikilizi mtu wa aina hii; Anawasukumia mbali. Mmetia kwenye kumbukumbu maneno haya kwa haraka sana, kwa usahihi sana. Inaonekana mmeelewa kile mlichosikia!

Kuna baadhi ya watu ambao, punde wanapoanza kumfuata Mungu, hawajakomaa na hawajui chochote; hawaelewi nia za Mungu; pia hawajui maana ya kuamini katika Mungu, huchukua njia iliyobuniwa na mwanadamu na potofu ya kuamini katika Mungu, kumfuata Mungu. Wakati mtu wa aina hii anapokabiliwa na majaribio hana habari na hajali kuhusu mwongozo na nuru ya Mungu. Hajui maana ya kuutoa moyo wake kwa Mungu na maana ya kusimama imara wakati wa jaribio. Mungu atampa mtu huyu kiasi cha muda, na katika wakati huu, Atawaruhusu kuelewa jaribu la Mungu ni nini, nia za Mungu ni nini. Baadaye, mtu huyu anahitaji kuonyesha maoni yake. Kuhusiana na watu wale walio katika awamu hii, Mungu angali anasubiri. Kuhusu wale watu ambao wana maoni fulani lakini bado wanayumba-yumba, wanaotaka kutoa mioyo yao kwa Mungu lakini hawajapatanishwa na kufanya hivyo, ambao, ingawa wameweka ukweli fulani wa kimsingi katika vitendo, wanapokabiliwa na jaribu kuu, wanalikwepa na kutaka kukata tamaa—ni nini mtazamo wa Mungu kuelekea watu hawa? Mungu angali bado ana matarajio kidogo kwa watu kama hawa. Matokeo hutegemea mitazamo na maonyesho yao. Je, Mungu huitikiaje ikiwa watu hawana bidii ili kufanya maendeleo? Anakata tamaa. Hii ni kwa sababu kabla Mungu hajakata tamaa juu yako, tayari wewe umekata tamaa juu yako. Kwa hivyo, huwezi kumlaumu Mungu kwa kufanya hivyo. Ni makosa kwako kuwa na malalamiko dhidi ya Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 12)

Wakati wakimfuata Mungu, ni nadra sana kwa watu kutilia maanani makusudi ya Mungu, na ni nadra wao kutilia maanani mawazo ya Mungu na mtazamo Wake kwa wanadamu. Watu hawaelewi fikira za Mungu, kwa hivyo mnapoulizwa maswali yanayohusisha nia za Mungu, yanayohusisha tabia ya Mungu, mnaingia katika hali ya kutokuwa na uhakika; mnakuwa kwa kweli hamna uhakika, na mnakisia au kubahatisha. Mtazamo huu ni upi? Inathibitisha ukweli huu: kwamba watu wengi wanaomwamini Mungu wanamwona kama kundi la hewa tupu na kama kitu kinachoonekana kuwapo dakika moja na sio ijayo. Kwa nini Nasema hivyo? Kwa sababu kila wakati mnapokumbwa na suala, hamzijui nia za Mungu. Kwa nini hamzijui? Si kwamba hamzijui tu kwa sasa. Badala yake kuanzia mwanzo hadi mwisho hamjui mtazamo wa Mungu katika suala hili. Katika nyakati zile ambazo huwezi kuona na hujui mtazamo wa Mungu, je, umewahi kuifikiria sana? Je, umetafuta kuijua? Je, umeshiriki kuhusu hilo? La! Hii inathibitisha ukwei: Mungu wa imani yako na Mungu wa kweli hawana uhusiano. Wewe, unayeamini katika Mungu, unafikiria tu mapenzi yako mwenyewe, unafikiria tu mapenzi ya viongozi wako, na unafikiria tu maana ya juu juu na ya kimafundisho ya neno la Mungu, lakini hufanyi kwa dhati kujaribu kujua na kutafuta mapenzi ya Mungu hata kidogo. Sivyo ndivyo hali ilivyo? Kiini cha suala hili hakipendezi! Kwa miaka mingi Nimeona watu wanaomsadiki Mungu. Kusadiki huku kunachukua mfumo gani? Baadhi ya watu wanamwamini Mungu kana kwamba Yeye ni hewa tupu. Watu hawa hawana jibu kwa maswali ya kuwepo kwa Mungu kwa sababu hawawezi kuhisi au kufahamu uwepo au kutokuwepo kwa Mungu, sembuse kuona au kuelewa kwa uwazi. Kwa nadharia yao, watu hawa wanafikiria kwamba Mungu hayupo. Baadhi wanasadiki katika Mungu ni kana kwamba Yeye ni binadamu. Watu hawa wanasadiki kwamba Mungu hawezi kufanya mambo yale ambayo wao hawawezi kufanya, na kwamba Mungu anafaa kufikiria namna wanavyofikiria. Ufafanuzi wa mtu huyu kuhusu Mungu ni “mtu asiyeonekana na asiyegusika.” Kunalo pia kundi la watu wanaosadiki katika Mungu kana kwamba Yeye ni kikaragosi; watu hawa wanasadiki kwamba Mungu hana hisia. Wanafikiria kwamba Mungu ni sanamu ya matope, na kwamba wanapokabiliwa na jambo, Mungu hana mwelekeo, hana mtazamo, hana mawazo; Anatawaliwa na binadamu. Watu wanasadiki tu wanavyotaka kusadiki. Wakimfanya kuwa mkubwa, Yeye ni mkubwa; wakimfanya kuwa mdogo, Yeye ni mdogo. Wakati wanapotenda dhambi na wanahitaji rehema za Mungu, wanapohitaji uvumilivu wa Mungu, wanapohitaji upendo wa Mungu, basi Mungu anafaa kutoa rehema Zake. Watu hawa wanamuunda “Mungu” katika akili zao wenyewe, na kisha wanamfanya “Mungu” huyu atimize mahitaji yao na kutosheleza matamanio yao yote. Haijalishi ni lini na ni wapi, na haijalishi watu kama hao wanafanya nini, watachukua dhana hii katika kumtendea Mungu, na katika imani yao kwa Mungu. Kuna hata wale wanaosadiki katika Mungu kuweza kuwaokoa baada kuikera tabia ya Mungu. Hii ni kwa sababu wanasadiki kuwa upendo wa Mungu hauna mipaka, tabia ya Mungu ni ya haki, na kwamba bila kujali ni vipi ambavyo watu wanamkosea Mungu, Hatakumbuka chochote. Wanafikiri kwamba kwa sababu makosa ya binadamu, dhambi za binadamu na kutotii kwa binadamu ni maonyesho ya mara moja ya tabia ya mtu huyo, Mungu atawapatia watu fursa, kuvumilia na kuwa na subira nao. Mungu angali atawapenda kama awali. Kwa hivyo tumaini la wokovu wao lingali kubwa. Kwa hakika, haijalishi jinsi mtu anavyomwamini Mungu, mradi tu hafuatilii ukweli, basi Mungu ana mtazamo hasi kwake. Hii ni sababu wakati unamsadiki Mungu, labda unakithamini kitabu cha neno la Mungu unakichambua kila siku, unakisoma kila siku, lakini unamweka Mungu halisi pembeni, unamchukulia kama hewa tupu, unamchukulia Yeye kama mtu, na baadhi yenu mnamchukulia kuwa kikaragosi. Kwa nini Nasema hivi? Kwa sababu kutokana na jinsi Ninavyoiona, bila kujali kama unakabiliwa na jambo au hali fulani, mambo yale ambayo yapo katika ufahamu wako mdogo, mambo yale ambayo yamekuzwa ndani—hakuna hata moja kati ya hayo yenye uhusiano wowote na neno la Mungu au kufuatilia ukweli. Unajua tu kile ambacho wewe mwenyewe unafikiria, maoni yako mwenyewe ni nini, na kisha unalazimishia mawazo yako na maoni yako mwenyewe kwa Mungu. Katika akili yako yanakuwa maoni ya Mungu, nawe unaweka viwango hivi vya maoni ambavyo unashikilia bila kuyumbayumba. Baada ya muda, kuendelea hivi kunakupeleka mbali zaidi na Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 13)

Elewa Mtazamo wa Mungu na Utupilie Mbali Dhana zote Potovu Kumhusu Mungu

Mungu huyu ambaye kwa sasa mnamwamini, je, mmewahi kufikiria Yeye ni Mungu wa aina gani? Anapomwona mtu mwovu akifanya mambo maovu, je Anayachukia? (Anayachukia.) Anapoona makosa ya watu wajinga, mtazamo Wake ni upi? (Huzuni.) Anapowaona watu wakiiba matoleo Yake, je, mtazamo Wake ni upi? (Anawachukia.) Haya yote yako wazi sana, sivyo? Anapoona mtu akiwa mzembe katika imani yake kwa Mungu, na kwa njia yoyote asifuatilie ukweli, ni nini mtazamo wa Mungu? Hamko wazi kabisa juu ya hili, sivyo? Uzembe ni tabia ambayo si dhambi, na si kumkosea Mungu. Watu wanaamini kuwa haupaswi kuzingatiwa kama kosa. Basi mnafikiria mtazamo wa Mungu ni nini? (Hayuko tayari kuitikia.) Kutotaka kuitikia—huu ni mtazamo gani? Ni kwamba Mungu anawadharau watu hawa, anawachukia watu hawa! Mungu hushughulika na watu hawa kwa kutowathamini. Mtazamo Wake ni kuwaweka kando, bila kujihusisha katika kazi yoyote juu yao, ikiwemo kuwapa nuru, mwangaza, kuwarudi, au kuwaadibu. Mtu wa aina hii hahesabiwi katika kazi ya Mungu. Je, mtazamo wa Mungu kwa watu wanaoikera sana tabia Yake, na kuzikosea amri Zake za kiutawala ni upi? Chuki kupindukia! Kwa kweli Mungu anakasirishwa sana na watu ambao hawatubu kwa kuikera sana tabia Yake! “Hasira Kali” ni hisia tu, hali ya moyo; haiwezi kuwakilisha mtazamo kamili. Lakini hisia hii, hali hii ya moyo, itasababisha matokeo kwa mtu huyu: Itamjaza Mungu chuki kali! Je, ni nini matokeo ya chuki hii iliyokithiri? Ni kwamba Mungu atamweka pembeni mtu huyu, na kutomwitikia kwa sasa. Kisha atasubiri kuwashughulikia “baada ya msimu wa kupukutika kwa majani.” Je, hii inaashiria nini? Je, mtu huyu bado ana matokeo? Mungu hakuwahi kunuia kumpa mtu wa aina hii matokeo! Hivyo basi si jambo la kawaida endapo Mungu kwa sasa hamwitikii mtu wa aina hii? (Ndiyo.) Je, mtu wa aina hii anapaswa kujiandaa kufanya nini? Anapaswa kujitayarisha kukabiliana na zile athari mbaya zilizosababishwa na tabia zao na maovu waliofanya. Huu ndio mwitikio wa Mungu kwa mtu wa aina hii. Hivyo basi Nasema waziwazi kwa mtu wa aina hii: Usishikilie imani za uwongo tena, na usijihusishe katika kufikiria makuu tena. Mungu hatawavumilia watu siku zote bila kikomo; Hatastahimili dhambi zao au kutotii kwao bila kukoma. Baadhi ya watu watasema: “Pia nimeona watu wachache kama hawa. Wanapoomba wanaguswa hasa na Mungu, na wanalia kwa uchungu. Kwa kawaida wao pia wana furaha sana; wanaonekana kuwa na uwepo wa Mungu, na mwongozo wa Mungu.” Usiseme huo upuzi! Kulia kwa uchungu si lazima iwe kwamba mtu ameguswa na Mungu au kuwa na uwepo wa Mungu, achilia mbali mwongozo wa Mungu. Kama watu watamghadhabisha Mungu, je, bado Mungu atawaongoza? Nikiongea kwa ujumla, wakati Mungu ameamua kumwondoa mtu, kuwaacha watu hao, tayari mtu huyo hana matokeo. Haijalishi ni vipi wanavyohisi kutosheka kujihusu wao wenyewe wakati wanapoomba, na imani kiwango kipi walichonacho katika Mungu mioyoni mwao; tayari hii si muhimu. Kitu cha muhimu ni kwamba Mungu hahitaji aina hii ya Imani, kwamba Mungu tayari amemsukumia mbali mtu huyu. Jinsi ya kukabiliana nao baadaye pia sio muhimu. Kilicho muhimu ni kwamba wakati mtu huyu anamghadhabisha Mungu, matokeo yake tayari yameamuliwa. Ikiwa Mungu ameamua kutomwokoa mtu wa aina hii, basi ataachwa nyuma ili kuadhibiwa. Huu ni mtazamo wa Mungu.

Ingawa sehemu ya kiini cha Mungu ni upendo, na Anaitoa rehema yake kwa kila mtu, watu hupuuza na kusahau ukweli kwamba kiini Chake halisi ni heshima vilevile. Kwamba Ana upendo haimaanishi kwamba watu wanaweza kumkosea Yeye wapendavyo na Hana hisia zozote, au miitikio yoyote. Kwamba Ana rehema haimaanishi kwamba Hana kanuni zozote katika jinsi Anavyowatendea watu. Mungu yu hai; kwa kweli Yupo. Yeye si kikaragosi kilichofikiriwa au kitu kingine tu. Kwa kuwa Yeye yuko, tunapaswa kusikiliza kwa makini sauti ya moyo Wake wakati wote, kuzingatia makini mtazamo Wake, na kuzielewa hisia Zake. Hatupaswi kutumia mawazo ya watu kumfafanua Mungu, na hatupaswi kulazimisha mawazo na matamanio ya watu kwa Mungu, na kumfanya Mungu atumie mtindo na kufikiri kwa mwanadamu katika jinsi Anavyowatendea wanadamu. Ukifanya hivyo, basi unamghadhabisha Mungu, unaijaribu hasira ya Mungu, na unapinga heshima ya Mungu! Hivyo basi, baada ya kuelewa ukali na uzito wa suala hili, Ninasihi kila mmoja wenu aliye hapa kuwa makini na wenye busara katika vitendo vyenu. Kuwa makini na wenye busara katika kuongea kwenu. Na kuhusu jinsi mnavyomtendea Mungu, kadiri mnavyokuwa waangalifu na wenye busara zaidi, ndivyo ilivyo bora! Wakati huelewi mtazamo wa Mungu ni nini, usizungumze kwa uzembe, usiwe mzembe katika vitendo vyako, na usipachike majina ovyo ovyo. Na hata zaidi, usikimbilie kufanya hitimisho kiholela. Badala yake, unafaa kusubiri na kutafuta; hili pia ndilo dhihirisho la kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Ikiwa wewe unaweza kufikia kiwango hiki zaidi ya yote, na kuwa na mtazamo huu zaidi ya yote, basi Mungu hatakulaumu kwa upumbavu wako, ujinga wako, na ukosefu wa kuelewa sababu za mambo. Badala yake, kwa sababu ya hofu yako ya kumkosea Mungu, heshima yako kwa mapenzi ya Mungu, na mtazamo wako wa kutaka kumtii, Mungu atakukumbuka, atakuongoza na kukupa mwanga, au kuvumilia uchanga na ujinga wako. Kinyume chake, endapo mtazamo wako Kwake utakuwa usio na heshima—kumhukumu Mungu kiholela, kukisia kiholela, na kufafanua mawazo ya Mungu—Mungu atakupa hukumu, nidhamu, au hata adhabu; au Atakupa kauli. Pengine kauli hii inahusisha matokeo yako. Hivyo basi, Ningali bado nataka kutilia mkazo jambo hili kwa mara nyingine tena: Unapaswa uwe makini na mwenye busara katika kila kitu kinachotoka kwa Mungu. Usiongee kwa uzembe, na usiwe mzembe katika matendo yako. Kabla ya kusema chochote, unafaa kufikiria: Je, kufanya hivi kutamghadhabisha Mungu? Je, kufanya hivi ni kumcha Mungu? Hata katika masuala mepesi, bado unafaa kujaribu kuelewa hakika maswali haya, yafikirie kwa kweli. Ikiwa unaweza kwa kweli kutenda kulingana na kanuni hizi katika nyanja zote, katika mambo yote, kila wakati, na kukubali mtazamo kama huu hasa wakati huelewi kitu, basi Mungu atakuongoza daima na kukupatia njia ya kufuata. Bila kujali ni nini ambacho watu wanaonyesha, Mungu anaona yote waziwazi, dhahiri, na Atakupa utathmini sahihi na unaofaa kwa maonyesho haya. Baada ya kupitia jaribio la mwisho, Mungu atachukua tabia yako yote na kuijumlisha ili kuamua matokeo yako. Matokeo haya yatamshawishi kila mmoja bila shaka lolote. Kile ambacho Ningependa kuwaambia ni kwamba kila kitendo chenu, kila hatua yenu, na kila fikira yenu vyote vitaamua majaliwa yenu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 14)

Ni Nani Hupanga Matokeo ya Binadamu

Kuna jambo lingine muhimu zaidi, na hilo ni mtazamo wenu kwa Mungu. Mtazamo huu ni muhimu sana! Unaamua kama hatimaye mtatembea katika maangamizo, au kwenye hatima nzuri na ya kupendeza ambayo Mungu amewatayarishia. Katika Enzi ya Ufalme, Mungu tayari amefanya kazi kwa zaidi ya miaka 20 na kwenye kipindi cha miaka hii 20 pengine mioyo yenu imekuwa na tashwishi kuhusu utendakazi wenu. Hata hivyo, katika moyo wa Mungu, Ameweka rekodi halisi na ya kweli kwa kila mmoja wenu. Kuanzia wakati kila mtu anapoanza kumfuata na kusikiliza mahubiri Yake, kuelewa zaidi na zaidi ukweli, hadi wakati wanatekeleza wajibu wao—Mungu ana rekodi ya kila moja ya maonyesho haya. Wakati mtu anapofanya wajibu wake, wakati anapokabiliwa na kila aina ya hali, kila aina ya majaribio, mtazamo wa mtu huyo ni upi? Wanatenda kazi vipi? Je, wanajisikiaje kumwelekea Mungu mioyoni mwao? … Mungu anayo maelezo ya haya yote, rekodi yake yote. Pengine kutokana na mtazamo wenu, masuala haya yanakanganya. Hata hivyo, kutoka pale ambapo Mungu yupo, yote yako wazi kabisa, na hakuna hata dalili yoyote ya kutokuwa wazi. Hili ni suala linahusisha matokeo ya kila mmoja, na hatima zao na matarajio ya siku zijazo pia. Hata zaidi, hapa ndipo ambapo Mungu anatumia jitihada Zake zote alizomakinikia. Hivyo basi Mungu hathubutu kuipuuza hata kidogo, na Hatavumilia kutomakinika kokote. Mungu anarekodi haya yote kuhusu mwanadamu, akirekodi historia ya mwenendo mzima wa mwanadamu kumfuata Mungu, kutoka mwanzo hadi mwisho. Mtazamo wako kwa Mungu wakati huu utaamua hatima yako. Je, haya si kweli? Sasa, mnaamini kwamba Mungu ni mwenye haki? Je, matendo ya Mungu yanafaa? Je, bado mna picha nyingine yoyote ya Mungu vichwani mwenu? (La.) Kisha mnasema kwamba matokeo ya mwanadamu ni kwa ajili ya Mungu kuweza kupanga au kwa mwanadamu mwenyewe kupanga? (Ni kwa Mungu kupanga.) Je, ni nani basi anayeyapanga? (Mungu.) Hamna hakika, sivyo? Ndugu kutoka makanisa ya Hong Kong, ongeeni—ni nani anayeyapanga? (Binadamu anayapanga mwenyewe.) Mwanadamu anayapanga? Hivyo basi haimaanishi kwamba haina chochote kuhusu Mungu? Ndugu kutoka Korea Kusini, ongeeni. (Mungu anaamua matokeo ya binadamu kutokana na hatua na vitendo vyake vyote na kutokana pia na njia wanayoitembea.) Hili ni jibu halisi sana. Kuna ukweli hapa ambao ni lazima Niwafahamishe nyinyi: Kwenye mkondo wa kazi ya wokovu wa Mungu, Yeye huweka kiwango kwa binadamu. Kiwango hiki ni kwamba binadamu anaweza kutii neno la Mungu, na kutembea katika njia ya Mungu. Ndicho kiwango kinachotumika kupima matokeo ya binadamu. Kama utatenda kwa mujibu wa kiwango hiki cha Mungu, basi unaweza kupata matokeo mazuri; kama hutafanya hivyo, basi huwezi kupokea matokeo mazuri. Basi ni nani unayesema kwamba anayapanga matokeo haya? Si Mungu pekee anayeyapanga, lakini badala yake Mungu na binadamu pamoja. Hiyo ni sahihi? (Ndiyo.) Kwa nini ipo hivyo? Kwa sababu ni Mungu ambaye anataka kujishughulisha na kujihusisha katika kazi ya wokovu wa wanadamu, na kutayarisha hatima nzuri kwa ajili ya binadamu; binadamu ndiye mlengwa wa kazi ya Mungu, na matokeo haya, hatima hii, ndiyo ambayo Mungu humtayarishia binadamu. Kama kusingekuwa na mlengwa wa kazi Yake, basi Mungu asingehitaji kazi hii; kama Mungu asingefanya kazi hii, basi binadamu asingekuwa na fursa ya wokovu. Binadamu ndiye mlengwa wa wokovu, na ingawa binadamu yumo kwenye upande wa kimya katika mchakato huu, ni mwelekeo wa upande huu ambao unaamua kama Mungu atafanikiwa katika kazi Yake ya kuwaokoa wanadamu au la. Kama si mwongozo ambao Mungu anakupa wewe, basi usingejua kiwango Chake, na usingekuwa na lengo lolote. Kama unacho kiwango hiki, lengo hili, ilhali hushirikiani, huliweki katika vitendo, hulipii gharama, basi bado hutapokea matokeo haya. Kwa sababu hii, Ninasema kwamba matokeo haya hayawezi kutenganishwa na Mungu, na pia hayawezi kutenganishwa na binadamu. Na sasa unaweza kujua ni nani anayepanga matokeo ya binadamu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 15)

Watu Huishia Kumfafanua Mungu Kutokana na Uzoefu Wao

Wakati wa kuwasilisha mada ya kumjua Mungu, je, mmegundua kitu? Je, mmegundua kwamba mtazamo wa sasa wa Mungu umepitia mabadiliko? Je, mtazamo wa Mungu kwa wanadamu hauwezi kubadilika? Je, siku zote Mungu atavumilia hivi, huku Akitoa upendo Wake wote na rehema kwa binadamu bila kikomo? Suala hili pia linahusu kiini halisi cha Mungu. … Punde tu watu wanapojua kwamba Mungu anawapenda wanadamu, wanamfafanua Mungu kama ishara ya upendo: Haijalishi kile wanachofanya watu, haijalishi namna wanavyotenda mambo, haijalishi jinsi wanavyomtendea Mungu na haijalishi ni vipi wasivyotii, hakuna chochote kinachojalisha kwa sababu Mungu ni upendo na upendo wa Mungu hauna mipaka na haupimiki. Mungu ana upendo, hivyo Anaweza kuwa mvumilivu kwa watu; Mungu ana upendo, hivyo anaweza kuwa na huruma kwa watu, Mwenye rehema kwa kutokomaa kwao, Mwenye rehema kwa ujinga wao, na Mwenye rehema kwa kutotii kwao. Je, hivi ndivyo ilivyo kweli? Kwa watu wengine, wanapokuwa wamepitia subira ya Mungu mara moja, au mara chache, watashughulikia suala hili kama mtaji katika uelewa wao wenyewe wa Mungu, wakiamini kwamba Mungu atakuwa mvumilivu kwao milele, kuwa na huruma kwao, na katika maisha yao yote watachukua subira ya Mungu na kuiona kama kiwango cha jinsi Mungu anavyowatendea. Pia kuna wale watu ambao, wakati wamepitia uvumilivu wa Mungu mara moja, watamfafanua Mungu milele kama mvumilivu, na uvumilivu huu hauna kikomo, hauna masharti, na hata hauna kanuni kabisa. Je, imani hizi ni sahihi? Kila wakati mambo kuhusu kiini cha Mungu au tabia ya Mungu yanapozungumziwa, mwaonekana mmechanganyikiwa mno. Kuwaona mkiwa hivi kunanifanya Mimi kuwa na wasiwasi. Mmesikia mambo mengi ya ukweli kuhusiana na kiini cha Mungu; mmeweza pia kusikiliza mada nyingi kuhusiana na tabia ya Mungu. Hata hivyo, katika akili zenu masuala haya, na ukweli wa vipengele hivi, ni kumbukumbu tu kulingana na nadharia na maneno yaliyoandikwa. Hakuna kati yenu anayeweza kupitia kile ambacho tabia ya Mungu inamaanisha katika maisha yenu halisi, wala hamwezi kuona tu tabia ya Mungu ni nini. Kwa hivyo, ninyi nyote mmechanganyikiwa katika imani zenu, nyote mnaamini kwa upofu, hadi kwamba mna mtazamo usio na heshima kwa Mungu, na kwamba mnamweka kando. Mtazamo kama huu kwa Mungu unawaongoza wapi? Mnaongozwa katika hali ya kutoa hitimisho siku zote kuhusu Mungu. Mara tu unapopata maarifa kidogo, unahisi kutosheka sana, unahisi kama umempata Mungu katika ukamilifu Wake. Baadaye unahitimisha kwamba hivi ndivyo Mungu Alivyo, na humruhusu kuendelea mbele na shughuli Zake kwa furaha zaidi. Na kila Mungu anapofanya jambo jipya, hukubali kwamba Yeye ni Mungu. Siku moja, wakati Mungu atakaposema: “Simpendi binadamu tena; Sitoi rehema kwa binadamu tena; Sina uvumilivu au subira yoyote kwa binadamu tena; Nimejaa chuki na uhasama kupindukia kwa binadamu,” watu watakinzana na aina hii ya taarifa kutoka ndani ya mioyo yao. Baadhi yao wataweza hata kusema: “Wewe si Mungu wangu tena; Wewe si Mungu ninayetaka kumfuata tena. Kama hivi ndivyo Unavyosema, basi Hustahili tena kuwa Mungu wangu, na sihitaji kuendelea kukufuata Wewe. Kama Hunipi rehema, hunipi upendo, hunipi uvumilivu, basi nami sitakufuata Wewe tena. Kama Utakuwa mvumilivu tu kwangu bila kikomo, utakuwa mwenye subira kwangu, na kuniruhusu mimi kuona kwamba Wewe ni upendo, kwamba Wewe ni subira, kwamba Wewe ni uvumilivu, hapo tu ndipo nitakapoweza kukufuata Wewe, na hapo tu ndipo nitakapoweza kuwa na ujasiri wa kukufuata mpaka mwisho. Kwa sababu ninapata subira na rehema Zako, kutotii kwangu na dhambi zangu zinaweza kusamehewa bila kikomo, kuondolewa bila kikomo, na ninaweza kutenda dhambi wakati wowote na mahali popote, kutubu na kusamehewa wakati wowote na mahali popote, na kukughadhabisha wakati wowote na mahali popote. Hufai kuwa na fikira au hitimisho Zako binafsi kuhusiana na mimi.” Ingawa unaweza usifikirie juu ya swali la aina hii kwa namna hiyo ya ubinafsi na ufahamu, wakati wowote unapomchukulia Mungu kama chombo cha kupata kusamehe dhambi zako na kitu cha kutumika kupata hatima nzuri, tayari umemweka Mungu aliye hai katika hali ya kukupinga wewe, kuwa adui yako. Hivi ndivyo Ninavyoona. Unaweza kuendelea kusema, “Ninaamini katika Mungu”; “Ninafuatilia ukweli”; “Ninataka kubadilisha tabia yangu”; “Nataka kujitenga na ushawishi wa giza”; “Nataka kumridhisha Mungu”; “Nataka kumtii Mungu”; “Nataka kuwa mwaminifu kwa Mungu, na kufanya wajibu wangu vyema”; na kadhalika. Hata hivyo; haijalishi chochote unachosema kinasikika jinsi gani, haijalishi ni nadharia kiasi gani unajua, haijalishi nadharia hiyo ni ya nguvu kiasi gani, ni ya heshima kiasi gani, ukweli wa mambo ni kwamba sasa kuna wengi wenu ambao tayari mmejifunza jinsi ya kutumia kanuni, mafundisho, nadharia ambayo mmeifahamu ili kuhitimisha mambo kuhusu Mungu, na kujiweka katika upinzani kamili kwa njia ya asili kabisa. Ingawa umejifunza barua na kujifunza falsafa, bado hujaingia kwa hakika katika uhalisia wa ukweli, kwa hivyo, ni vigumu sana kwako kuwa karibu na Mungu, kumjua Mungu, na kumwelewa Mungu. Hali hii inasikitisha!

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 16)

Mtazamo wa Mungu kwa Wale Wanaotoroka Wakati Kazi Yake Inaendelea

Kuna watu kama hawa kila mahali: Baada ya kuwa na uhakika kuhusu njia ya Mungu, kwa sababu mbalimbali, wanaondoka kimyakimya bila kuaga, kwenda na kufanya chochote kile ambacho mioyo yao inatamani. Kwa wakati huu, hatutaangalia kwa nini mtu huyu anaondoka. Kwanza tutaangalia mtazamo wa Mungu ni upi kwa mtu wa aina hii. Iko wazi sana! Kuanzia wakati ambao mtu huyu anaondoka, machoni pa Mungu, muda wa imani yao umekwisha. Sio mtu huyu aliyemaliza, lakini ni Mungu. Kwamba mtu huyu alimwacha Mungu inamaanisha kwamba tayari amemkataa Mungu, kwamba tayari hamtaki Mungu. Inamaanisha kwamba tayari hakubali wokovu wa Mungu. Kwa sababu mtu huyu hamtaki Mungu, Mungu naye anaweza bado kumtaka? Zaidi ya hayo, wakati mtu huyu ana mwelekeo huu, mtazamo huu, na kuazimia kumwacha Mungu, tayari ameikera tabia ya Mungu. Hata ingawa hawakupandwa na hasira na wakamlaani Mungu, hata ingawa hawakujihusisha na tabia yoyote mbaya au ya kupita kiasi, na hata ingawa mtu huyu anafikiria: Kama kutawahi kuwepo na siku nitakapokuwa nimeshiba anasa zangu kwa nje, au nitakapokuwa bado nahitaji kitu kutoka kwa Mungu, nitarudi. Au kama Mungu ataniita, nitarudi. Au wanasema: Kama nitajeruhiwa kwa nje, nikiuona ulimwengu wa nje una giza sana na una maovu sana na sitaki tena kujishirikisha nao, nitarudi kwa Mungu. Hata ingawa mtu huyu amepiga hesabu katika akili zake ni wakati gani anarudi, hata ingawa wanauacha mlango ukiwa wazi wa kurudi kwao, hawatambui kwamba bila kujali ni namna gani wanavyofikiria na ni jinsi gani wanavyopanga, hii ni ndoto tu. Kosa lao kubwa zaidi ni kutokuwa wazi kuhusu namna ambavyo Mungu anahisi wakati wanapotaka kuondoka. Kuanzia muda huo ambao mtu huyu anaamua kumwacha Mungu, Mungu amemwacha kabisa; tayari Mungu ameamua matokeo yao katika moyo Wake. Matokeo hayo ni yapi? Ni kwamba mtu huyu atakuwa mmoja wa panya, na ataangamia pamoja nao. Hivyo basi, watu mara nyingi huona aina hii ya hali: Mtu anamwacha Mungu, lakini hapokei adhabu yoyote. Mungu hufanya kazi kulingana na kanuni Zake binafsi. Watu wanaweza kuona baadhi ya mambo, na baadhi ya mambo yanahitimishwa tu katika moyo wa Mungu, kwa hivyo watu hawawezi kuyaona matokeo. Kile ambacho watu wanaona si lazima kiwe ndio upande wa ukweli wa mambo; lakini upande ule mwingine, ule upande usiouona—haya ndiyo mawazo ya kweli na hitimisho la moyo wa Mungu.

Watu Wanaotoroka Wakati wa Kazi ya Mungu ni Wale Wanaoiacha Njia ya Kweli

Kwa nini Mungu anawapa watu wanaomkimbia wakati wa kazi Yake adhabu kali namna hii? Kwa nini Mungu anakuwa na hasira kali kwao? Kwanza kabisa tunajua kwamba tabia ya Mungu ni ukuu, ni ghadhabu. Yeye si kondoowa kuchinjwa na yeyote; na hata zaidi Yeye si kikaragosiwa kudhibitiwa na watu watakavyo. Yeye pia si hewa tupu ya kuamrishwa huku na kule na watu. Kama kweli unasadiki kwamba Mungu yupo, unapaswa kuwa na moyo unaomcha Mungu, na unapaswa kujua kwamba kiini cha Mungu hakipaswi kughadhabishwa. Ghadhabu hii inaweza kusababishwa na neno; pengine fikira; pengine aina fulani ya tabia mbaya; pengine tabia ya upole, tabia inayoweza kuruhusiwa machoni pake na maadili ya mwanadamu; au pengine inasababishwa na mafundisho, aunadharia. Hata hivyo, punde unapomghadhabisha Mungu, fursa yako inapotea na siku zako za mwisho zinakuwa zimewasili. Hili ni jambo baya sana! Kama huelewi kwamba Mungu hawezi kukosewa, basi pengine humchi Mungu, na pengine unamkosea Yeye kila wakati. Kama hujui jinsi ya kumcha Mungu, basi huwezi kumcha Mungu, na hutaweza kujua namna ya kujiweka kwenye njia ya kutembea katika njia ya Mungu—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Punde unapofahamu, unaweza kuwa na ufahamu kwamba Mungu hawezi kukosewa, kisha utajua ni nini maana ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kutembea katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu si lazima iwe kuhusu ukweli mwingi unaoujua, ni majaribu mangapi ambayo umepitia, au ni kiasi gani umeadhibiwa. Badala yake, kunategemea aina ya mtazamo ulio nao kwa Mungu moyoni mwako, na kiini unachokionyesha. Kiini halisi cha watu na mitazamo yao wenyewe—mambo haya ni muhimu sana, ni muhimu kabisa. Kuhusiana na wale watu ambao wamemkana na kumwacha Mungu, mtazamo wao wa dharau kwa Mungu na mioyo yao inayodharau ukweli ilikera tabia ya Mungu, hivyo basi kulingana na Mungu hawatawahi kusamehewa. Wamejua kuhusu uwepo wa Mungu, wamekuwa na taarifa kwamba Mungu tayari amewasili, wameweza hata kupitia kazi mpya ya Mungu. Kuondoka kwao si kutokana na kudanganywa, wala si suala kwamba wao wamechanganyikiwa kulihusu. Hata zaidi ni suala la wao kulazimishwa kuondoka. Lakini kwa nadhari yao, na kwa akili iliyo wazi, wamechagua kumwacha Mungu. Kuondoka kwao si kupotea njia; si hata kutupwa kwao nje. Kwa hiyo, machoni pa Mungu, wao si mwana-kondoo aliyepotea kutoka katika kundi, sembuse mwana mpotevu aliyepotea njia. Waliondoka bila hofu ya kuadhibiwa, na hali kama hiyo, mfano kama huo unaikera tabia ya Mungu na ni kutokana na kero hii ambapo Yeye anawapa matokeo yasiyo na matumaini. Je, aina hii ya matokeo si ya kutisha? Kwa hivyo, kama watu hawamjui Mungu, wanaweza kumkosea Mungu. Hilo si suala dogo! Kama mtu hatachukulia mtazamo wa Mungu kwa umakinifu, na bado anasadiki kwamba Mungu angali anatarajia kurudi kwake—kwa sababu wao ni mojawapo wa kondoo wa Mungu waliopotea na kwamba Mungu angali anawasubiria kubadilisha mioyo yao—basi hawako mbali na siku zao za adhabu. Mungu hatakataa tu kumkubali—ikizingatiwa kwamba hii ni mara yake ya pili ya kuikera tabia ya Mungu; hivyo basi suala hili ni baya zaidi! Mtazamo wa mtu huyu usioheshimu vitu vitakatifu tayari umekosea agizo la kiutawala la Mungu. Je, bado Mungu atawakaribisha? Katika moyo Wake, kanuni za Mungu kuhusiana na suala hili ni kwamba mtu fulani amepata uhakika kuhusu ni ipi ndiyo njia ya kweli, lakini bado ameweza kwa kufahamu na kwa akili ya wazi kumkataa Mungu, na kuondoka kutoka kwa Mungu, basi Mungu atazuia kabisa barabara iendayo katika wokovu wake, na hata lango la kuingia kwenye ufalme watafungiwa. Wakati mtu huyu atakapokuja kubisha kwa mara nyingine, Mungu hatamfungulia lango. Mtu huyu atafungiwa milele. Labda baadhi yenu mmeisoma hadithi ya Musa katika Biblia. Baada ya Musa kupakwa mafuta na Mungu, viongozi 250 walionyesha kutomtii Musa kwa sababu ya matendo yake na kwa sababu nyinginezo mbalimbali. Walikataa kumtii nani? Haikuwa Musa. Walikataa kutii mipango ya Mungu; walikataa kutii kazi ya Mungu katika suala hili. Walisema yafuatayo: “Ninyi mnachukua mengi kwenu, kwa sababu mkusanyiko wote ni mtakatifu, kila mmoja wao, naye Yehova yuko miongoni mwao….” Katika macho yenu, maneno haya ni mazito? Si mazito! Angalau maana ya juu juu ya maneno haya sio mbaya. Katika mkondo wa kisheria, hawavunji sheria zozote, kwa juujuu kabisa si lugha katili, au msamiati, isitoshe, hayana maana yoyote ya kukufuru. Sentensi ya kawaida ndiyo iliyoko hapo, hamna cha ziada. Ilhali inakuwaje kwamba maneno haya yanaweza kuanzisha hasira kali kama hiyo kutoka kwa Mungu? Ni kwa sababu hayasemwi kwa watu, bali kwa Mungu. Mtazamo na tabia inayoonyeshwa na wao ndicho hasa kinachoikera tabia ya Mungu, na wao wanaikosea tabia ya Mungu ambayo haipaswi kukosewa. Sote tunajua matokeo yao hatimaye yalikuwa ni yapi. Kuhusiana na wale waliomwacha Mungu, mtazamo wao ni upi? Mwelekeo wao ni upi? Na ni kwa nini mtazamo na mwelekeo wao unasababisha Mungu kuwashughulikia kwa njia hiyo? Sababu ni kwamba wanajua waziwazi Yeye ni Mungu ilhali bado wanachagua kumsaliti Yeye. Na ndiyo maana wanaondolewa kabisa fursa yao ya wokovu. Kama vile Biblia inavyosema: “Kwa sababu tukitenda dhambi makusudi baada ya sisi kupokea maarifa ya ukweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi” (Waebrania 10:26). Je, mmelielewa suala hili sasa?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 17)

Hatima ya Mwanadamu Huamuliwa na Mtazamo Wake Kwa Mungu

Mungu ni Mungu aliye hai, na kama vile watu hutenda tofauti katika hali tofauti, mtazamo wa Mungu kuelekea maonyesho haya hutofautiana kwa sababu Yeye si kikaragosi, wala Yeye si hewa tupu. Kupata kuujua mtazamo wa Mungu ni jambo lenye thamani kwa wanadamu. Watu wanapaswa kujifunza jinsi, kwa kuujua mtazamo wa Mungu, wanaweza kujua tabia ya Mungu na kuuelewa moyo Wake kidogo kidogo. Wakati unapokuja kuuelewa moyo wa Mungu kidogo kidogo, hutahisi kwamba kumcha Mungu na kuepuka maovu ni jambo gumu kutimiza. Kilicho zaidi ni kwamba, unapomwelewa Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kufanya hitimisho kuhusu Yeye. Unapoacha kufanya hitimisho kuhusu Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kumkosea Yeye, na bila kujua Mungu atakuongoza kuwa na maarifa Yake, na hivyo basi utamcha Mungu katika moyo wako. Utaacha kumfafanua Mungu kwa kutumia mafundisho, zile barua, na nadharia ambazo umejifunza. Badala yake, kwa kutafuta nia za Mungu katika mambo yote na siku zote utaweza bila kufahamu kuwa mtu anayefuata moyo wa Mungu.

Kazi ya Mungu haionekani na haiwezi kuguswa na wanadamu, lakini kwa jinsi Mungu anavyohusika, matendo ya kila mtu, pamoja na mtazamo wao Kwake—haya hayatambuliki tu na Mungu, lakini yanaonekana pia. Hili ni jambo ambalo kila mmoja anafaa kutambua na kuwa wazi kulihusu. Unaweza kuwa ukijiuliza siku zote: “Je, Mungu anajua kile ninachofanya hapa? Je, Mungu anajua kile ninachofikiria sasa hivi? Pengine Anajua, pengine Hajui.” Kama utakuwa na mtazamo wa aina hii, kumfuata na kumwamini Mungu ilhali unatilia shaka kazi Yake na uwepo Wake, basi hivi karibuni au baadaye siku itawadia ambapo utamghadhabisha, kwa sababu tayari unaelea kwenye ukingo wa mteremko wa hatari. Nimeona watu ambao wamemwamini Mungu kwa miaka mingi, lakini bado hawajapata uhalisi wa ukweli, wala hata hawaelewi mapenzi ya Mungu. Maisha yao na kimo chao havipigi hatua yoyote, wakishikilia tu mafundisho duni kabisa. Hii ni kwa sababu watu hawa hawajawahi kuchukulia neno la Mungu kama maisha yao binafsi, na hawajawahi kukabiliana na kukubali uwepo Wake. Je, unafikiri kwamba Mungu anapowaona watu kama hao, Anajawa na furaha? Je, wanamfariji Yeye? Katika hali hiyo, ni njia ya imani ya watu kwa Mungu ambayo huamua hatima yao. Kuhusu jinsi watu wanavyomwamini Mungu ndivyo inavyoamua hatima yao. Kuhusu jinsi watu wanavyotafuta na jinsi watu wanavyomkaribia Mungu, mitazamo ya watu ni ya muhimu sana. Usimpuuze Mungu kama vile Yeye ni rundo la hewa tupu linalozunguka nyuma ya kichwa chako. Daima mfikirie Mungu wa imani yako kama Mungu aliye hai, Mungu halisi. Yeye hayupo kule juu kwenye mbingu ya tatu bila chochote cha kufanya. Badala yake, Yeye hutazama kila mara ndani ya moyo wa kila mtu, Akiangalia kile unachotaka kufanya, katika kila neno dogo na kila tendo dogo, Akiangalia jinsi unavyotenda na mtazamo wako kwa Mungu ni upi. Iwe uko radhi kujitolea kwa Mungu au la, tabia yako yote na fikira zako na mawazo yako ya ndani zaidi yako mbele za Mungu, na yanaangaliwa na Yeye. Ni kulingana na tabia yako, kulingana na vitendo vyako, na kulingana na mwelekeo wako kwa Mungu, ambapo maoni Yake kwako, na mwenendo Wake kwako, vinaendelea kubadilika. Mimi Ningependa kutoa ushauri fulani kwa baadhi ya watu. Msijiweke kwenye mikono ya Mungu kama watoto wachanga, kana kwamba Yeye Anapaswa kukupenda sana, kana kwamba Hawezi kamwe kukuacha, na kana kwamba mwelekeo Wake kwako ni imara na usingeweza kubadilika, na Ninawashauri muache kuota ndoto! Mungu ni mwenye haki katika kumtendea kila mtu, na Yeye ni mwaminifu katika mtazamo Wake kwa kazi ya kuwashinda na kuwaokoa watu. Huu ndio usimamizi Wake. Anamtendea kila mmoja kwa umakinifu, na wala si kama kiumbe cha kufugwa cha kucheza nacho. Upendo wa Mungu kwa binadamu si ule wa kudekeza au kupotosha; rehema na uvumilivu Wake kwa wanadamu si wa kuendekeza au kutojali. Kinyume cha mambo, upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wa kutunza, kuhurumia, na kuheshimu maisha; rehema na uvumilivu Wake vyote vinaonyesha matarajio Yake kwa binadamu; rehema na uvumilivu Wake ndivyo ambavyo binadamu anahitaji ili kuishi. Mungu yuko hai, na kwa hakika Mungu yupo; Mtazamo Wake kwa wanadamu ni wa kanuni, sio sheria ya kiitikadi hata kidogo, na unaweza kubadilika. Mapenzi Yake kwa ubinadamu yanabadilika polepole na kurekebishwa kulingana na wakati, na hali, na mtazamo wa kila mtu. Kwa hiyo, unapaswa kujua ndani ya moyo wako kwa uwazi kabisa kwamba kiini cha Mungu hakibadiliki, na kwamba tabia Yake itajidhihirisha kwa nyakati tofauti na katika mazingira tofauti. Huenda usifikirie kwamba hili si suala zito, na unatumia mawazo yako binafsi kufikiria jinsi Mungu anapaswa kufanya mambo. Lakini kuna nyakati ambapo kinyume kabisa cha mtazamo wako ni kweli, na kwamba kwa kutumia mawazo yako binafsi katika kumjaribu na kumpima Mungu, tayari umemghadhabisha. Hii ni kwa sababu Mungu hafanyi kazi kama unavyofikiria wewe, Naye Mungu hatalishughulikia suala hili kama vile unavyosema Atalishughulikia. Kwa hivyo, Ninakukumbusha uwe makini na mwenye hekima katika mtazamo wako kwa kila kitu, na ujifunze namna ya kufuata kanuni ya kutembea kwenye njia ya Mungu katika mambo yote—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Lazima uimarishe uelewa thabiti katika masuala ya mapenzi ya Mungu na mtazamo wa Mungu; lazima utafute watu walio na nuru ili wakujulishe mambo haya, na ni lazima utafute kwa bidii. Usimwone Mungu wa imani yako kama kikaragosi—ukimhukumu upendavyo, ukifanya hitimisho kiholela kuhusu Yeye, na kumtendea kwa mtazamo usio na heshima. Katika mchakato wa wokovu wa Mungu, Anapoamua matokeo yako, bila kujali kama Yeye atakupa rehema, au uvumilivu, au hukumu na kuadibu, kwa vyovyote vile, mtazamo Wake kwako unabadilika. Inategemea mtazamo wako kwa Mungu, na uelewa wako kuhusu Mungu. Usiruhusu kipengele kimoja cha kupita cha maarifa yako au uelewa wako katika Mungu kumfafanua Yeye milele. Usiamini katika Mungu aliyekufa; amini katika Aliye hai. Kumbuka hili! Ingawa Nimezungumza ukweli fulani hapa, ukweli mliohitaji kusikia, kwa kuzingatia hali yenu ya sasa na kimo chenu cha sasa, Sitatoa madai yoyote makubwa zaidi ili Nisipunguze shauku yenu. Kufanya hivyo kunaweza kuijaza mioyo yenu na huzuni na simanzi, na kuwafanya mhisi kuvunjika moyo sana kumwelekea Mungu. Badala yake Natumai kwamba mnaweza kutumia upendo wa Mungu katika mioyo yenu, na kutumia mtazamo ambao ni wa heshima kwa Mungu wakati mnapotembea katika njia iliyo mbele. Usichukulie imani katika Mungu kwa njia iliyochanganyikiwa, lakini ichukulie kama jambo muhimu zaidi, iweke moyoni, iweke katika vitendo na iunganishe na maisha halisi, na usizungumze tu maneno matupu. Kwani hili ni suala la uzima na mauti, na ndilo ambalo litaamua hatima yako. Usilichukulie kama mzaha, kama mchezo wa mtoto! Baada ya kuwaambia maneno haya leo, Najiuliza ni uelewa wa kiwango gani ambao akili yako imeweza kupata. Je, kuna maswali yoyote ambayo ungependa kuuliza kuhusu kile Nilichokisema leo?

Ingawa mada hizi ni mpya kidogo, na zimeondolewa kidogo kutoka kwenye mitazamo yenu na kile ambacho kwa kawaida mnafuatilia na kutilia maanani, Nafikiria kwamba baada ya mada hizi kuwasilishwa kwa kipindi cha muda, mtaimarisha uelewa mzuri wa kila kitu Nilichosema hapa. Kwa sababu hizi ni mada mpya, mada ambazo hujawahi kuzifikiria hapo awali, Ninatumai kwamba hazitaongezea mzigo kwako. Ninaongea maneno haya leo si kwa sababu ya kuwatishia nyinyi, wala Sijaribu kukushughulikia wewe; badala yake, nia Yangu ni kukusaidia kuelewa ukweli halisi kuhusu ukweli. Kwa vyovyote vile, kunao umbali kati ya wanadamu na Mungu. Ingawa binadamu anaamini katika Mungu, hajawahi kumwelewa Mungu; hajawahi kujua mitazamo ya Mungu.Mwanadamu pia hajawahi kuwa na shauku katika kujali kwake mtazamo wa Mungu. Badala yake, ameamini kwa upofu, ameendelea kwa upofu, na amekuwa mzembe katika maarifa na uelewa wake wa Mungu. Kwa hivyo Ninahisi kulazimishwa kuwafafanulia masuala haya, na kuwasaidia kuelewa ni Mungu wa aina gani huyu mnayemwamini; kile Anachofikiri; mtazamo Wake ulivyo katika kuwatendea watu wa aina mbalimbali; uko mbali kiasi gani na kutimiza matakwa Yake; na tofauti kati ya matendo yako na kiwango Anachohitaji Yeye. Lengo la kuwajulisha juu ya mambo haya, ni ili kuwapa kigezo cha kujipimia kwenye mioyo yenu, na ili ujue ni aina gani ya mavuno ambayo njia unayoitembea inasababisha, kile ambacho hamjapata kwenye njia hii, na ni katika maeneo gani bado hamjajihusisha. Mnaposhiriki ninyi wenyewe, kwa kawaida mnazungumza juu ya mada chache zinazojadiliwa mara kwa mara, ambazo zina upeo finyu, na maudhui ni ya juujuu sana. Kuna umbali, pengo, kati ya kile ambacho mnazungumzia na nia za Mungu, katikati ya mazungumzo yenu na upana na kiwango cha mahitaji ya Mungu. Kuendelea hivi baada ya muda kutawafanya kupotoka zaidi na zaidi kutoka kwenye njia ya Mungu. Mnayachukua tu maneno yaliyopo kutoka kwa Mungu na kuyageuza kuwa vitu vya kuabudu, kuwa kaida za dini na kanuni. Hayo tu ndiyo maana yake! Kwa hakika, Mungu hana nafasi kamwe katika mioyo yenu, na Mungu hajawahi kuipata mioyo yenu. Baadhi ya watu hufikiria kwamba kumjua Mungu ni vigumu sana—huu ndio ukweli. Ni vigumu! Kama watu wataambiwa kutekeleza wajibu wao na kuhakikisha kwamba mambo yanatendeka kwa nje, kama wataulizwa kutia bidii, basi watu watafikiria kwamba kumwamini Mungu ni jambo rahisi sana, kwa sababu haya yote yanapatikana katika ule upana wa uwezo wa binadamu. Ilhali punde tu mada hizo zinaposonga kuelekea kwenye maeneo ya nia za Mungu na mtazamo wa Mungu kwa binadamu, basi mambo yanapata kuwa magumu zaidi kwa watu wote. Hiyo ni kwa sababu yote haya yanahusisha uelewa wa ukweli na kuingia kwao katika uhalisia; bila shaka kuna kiwango cha ugumu. Lakini baada ya wewe kuingia kupitia mlango wa kwanza, baada ya wewe kuanza kuingia ndani yake, mambo yataanza kuwa mepesi polepole.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 18)

Mahali pa Kuanzia Kumcha Mungu ni Kumchukulia Yeye kama Mungu

Mtu fulani ameuliza swali muda mfupi uliopita: Inakuwaje kwamba, ingawa tunamjua Mungu zaidi ya Ayubu, lakini bado hatuwezi kumcha Mungu? Tuliligusia kidogo suala hili hapo awali, sivyo? Kwa hakika, kiini halisi cha swali hili kimeweza pia kuzungumziwa awali kwamba ingawa Ayubu hakumjua Mungu kwa wakati huo, alimchukulia Yeye kama Mungu, na kumchukulia kama Bwana wa vitu vyote mbinguni na duniani. Ayubu hakumchukulia Mungu kuwa adui. Badala yake, alimwabudu Yeye kama Muumba wa vitu vyote. Watu siku hizi wanampinga Mungu sana kwa nini? Kwa nini hawawezi kumcha Mungu? Sababu moja ni kwamba wamepotoshwa sana na Shetani. Wakiwa na asili hiyo ya kishetani iliyokita mizizi ndani, watu wanageuka na kuwa adui wa Mungu. Hivyo basi, hata ingawa wanasadiki katika Mungu na kumtambua Mungu, bado wanaweza kumpinga Mungu na kujiweka katika nafasi ya upinzani na Yeye. Hili linaamuliwa na asili ya binadamu. Sababu nyingine ni kwamba ingawa watu wanamwamini Mungu, hawamchukulii Yeye kama Mungu. Badala yake, wanamchukulia Mungu kuwa ndiye anayempinga binadamu, wakimwona Yeye kuwa adui wa binadamu, na hawawezi kupatanishwa na Mungu. Ni rahisi hivyo. Je, jambo hili halikuzungumziwa kwenye kikao cha awali? Hebu fikiria: Je, hiyo ndio sababu? Ingawa unaweza kuwa na maarifa kidogo ya Mungu, lakini maarifa haya yanahusisha nini? Je, hayo siyo yale ambayo kila mtu anazungumzia juu yake? Je, hayo si yale ambayo Mungu alikuambia? Unajua tu vipengele vya kinadharia na mafundisho; je umewahi kupitia kipengele halisi cha Mungu? Je, unayo maarifa ya kibinafsi? Je, unayo maarifa na uzoefu wa vitendo? Kama Mungu asingekuambia, ungelijua hili? Maarifa yako ya nadharia hayawakilishi maarifa halisi. Kwa ufupi, bila kujali ni kiwango kipi unachojua na ni vipi ulivyokijua hatimaye, kabla ya wewe kufikia uelewa halisi wa Mungu, Mungu ni adui yako, na mpaka utakapoanza kumchukulia Mungu kama Mungu, Amewekwa kuwa mpinzani wako, kwani wewe ni mfano halisi wa Shetani.

Unapokuwa pamoja na Kristo, labda unaweza kumhudumia milo mitatu kwa siku, labda kumhudumia Yeye chai, kuhudumia mahitaji Yake ya maisha, ni kana kwamba unamchukulia Kristo kama Mungu. Kila wakati jambo linapofanyika, mitazamo ya watu siku zote inakuwa kinyume cha mtazamo wa Mungu. Siku zote wanashindwa kuelewa mtazamo wa Mungu, na wanashindwa kuukubali. Ingawa watu wanaweza kupatana na Mungu kwa juujuu, hii haimaanishi kwamba wanalingana na Yeye. Mara tu jambo linapotokea, ukweli wa kutotii kwa mwanadamu hujitokeza, kuthibitisha uhasama uliopo kati ya mwanadamu na Mungu. Uhasama huu sio Mungu anayempinga mwanadamu; sio Mungu kutaka kuwa na uadui kwa mwanadamu, na sio Mungu kumweka mwanadamu katika upinzani na kumtendea mwanadamu hivyo. Badala yake, ni suala la kiini hiki cha upinzani dhidi ya Mungu kinachonyemelea katika utashi wa mwanadamu, na katika akili ya kutofahamu ya mwanadamu. Kwa sababu binadamu anachukulia kila kitu kinachotoka kwa Mungu kama kitu cha utafiti wake, mwitikio wake kwa hiki ambacho kinatoka kwa Mungu na kile ambacho kinamhusisha Mungu ni, zaidi ya yote, kukisia, na kushuku, na kisha kuchukua kwa haraka sana mtazamo ambao unakinzana na Mungu, na unapingana na Mungu. Baada ya hapo, binadamu atachukua hali hizi za moyo za kimyakimya na kuzua mjadala na Mungu au kushindana na Mungu hadi kufikia kiwango ambacho atatia shaka kama Mungu wa aina hii anastahili kufuatwa. Licha ya ukweli kwamba urazini wa binadamu unamwambia asiendelee hivi, bado atachagua kufanya hivyo licha ya kutotaka kufanya hivyo, kiasi kwamba ataendelea bila kusita hadi mwisho. Kwa mfano, ni nini mwitikio wa kwanza kwa baadhi ya watu wanaposikia uvumi fulani au kashfa fulani kumhusu Mungu? Mwitikio wa kwanza ni: Sijui kama uvumi huu ni kweli au la, kama upo ama haupo, hivyo basi nitasubiri na kuona. Kisha wanaanza kutafakari: Hakuna njia ya kuthibitisha haya; je, hilo lilifanyika kweli? Je, uvumi huu ni wa kweli au la? Ingawa mtu huyu haonyeshi kwa juujuu, mioyo yao tayari imeanza kuwa na shaka, tayari imeanza kumkana Mungu. Ni nini kiini cha aina hii ya mwelekeo, aina hii ya mtazamo? Je, si usaliti? Kabla ya wao kukumbwa na suala, huwezi kuona mtazamo wa mtu huyu ni nini—inaonekana ni kana kwamba wao hawakinzani na Mungu, ni kama hawamchukulii Mungu kuwa adui. Hata hivyo, punde wanapokumbwa na suala hilo, wanasimama mara moja na Shetani na kumpinga Mungu. Hali hii inapendekeza nini? Inapendekeza kwamba binadamu na Mungu wanapingana! Si kwamba Mungu anamchukulia binadamu kama adui, lakini kwamba kile kiini chenyewe cha binadamu kina uadui kwa Mungu. Haijalishi ni kwa muda mrefu kiasi gani ambapo mtu amemfuata Mungu, au ni kiwango kipi anacholipa; bila kujali jinsi mtu anavyomsifu Mungu, jinsi wanavyojizuia kumpinga Mungu, hata kujihimiza kumpenda Mungu, hawawezi kamwe kumchukulia Mungu kama Mungu. Je, hii si inaamuliwa na kiini halisi cha mwanadamu? Ikiwa unamchukulia Yeye kama Mungu, na kuamini kwa kweli kwamba Yeye ni Mungu, je, bado unaweza kuwa na mashaka yoyote Kwake? Je, bado kunaweza kuwa na alama zozote za maswali kuhusu Yeye katika moyo wako? Hakuwezi. Mitindo ya ulimwengu huu ni miovu kweli, na wanadamu wa kizazi hiki pia, hivyo, inawezekanaje kwamba huna fikira zozote kuzihusu? Wewe mwenyewe umejaa uovu, hivyo inakuwaje kwamba huna fikira zozote kuhusu hayo? Na bado, uvumi kidogo tu, kashfa fulani zinaweza kusababisha dhana kubwa mno kumhusu Mungu, zinaweza kuleta mawazo mengi mno, hali inayoonyesha vile ambavyo kimo chako kilivyo bado kichanga! “Mnong’ono” tu wa mbu wachache, nzi wachache wabaya, hilo tu ndilo linalokupotosha? Huyu ni mtu wa aina gani? Je, unajua anachofikiria Mungu kuhusu mtu wa aina hii? Mtazamo wa Mungu kwa hakika uko wazi sana kuhusiana na jinsi Anavyowatendea watu kama hawa. Ni kwamba tu Mungu anavyowatendea watu hawa ni kuwapuuza—mtazamo Wake ni kutowatilia maanani, na kutomakinikia watu hawa wajinga. Kwa nini ni hivyo? Ni kwa sababu katika moyo Wake Hakuwahi kupangilia kuhusu kupata watu kama hao ambao wameahidi kuwa na uadui Kwake hadi mwisho kabisa, na ambao hawajawahi kamwe kupanga kutafuta njia ya kupatana na Yeye. Pengine maneno haya Niliyoyaongea yamewaumiza watu wachache. Kwa kweli, mko radhi kuniruhusu Mimi niwaumize siku zote namna hii? Bila kujali kama mko radhi au la, kila kitu Ninachosema ni ukweli! Kama siku zote Ninawaumiza namna hii, siku zote Nafichua makovu yenu, je, itaathirisura ya juu ya Mungu mioyoni mwenu? (Haitaathiri.) Ninakubali kwamba haitaathiri kwani kwa ufupi hakuna Mungu katika mioyo yenu. Yule Mungu wa juu anayepatikana ndani ya mioyo yenu, yule mnayemtetea kwa dhati na kumlinda, kwa ufupi si Mungu. Badala yake ni mfano wa mawazo ya mwanadamu; kwa ufupi hayupo. Kwa hivyo, ni bora zaidi kama Nitafichua jibu la kitendawili hiki. Je, huu si ukweli wote? Mungu halisi hatokani na mawazo ya mwanadamu Natumai kwamba nyote mnaweza kukabiliana na uhalisia huu, na utawasaidia katika maarifa yenu ya Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 19)

Wale Watu Wasiotambuliwa na Mungu

Kuna baadhi ya watu ambao imani yao haijawahi kutambuliwa katika moyo wa Mungu. Kwa maneno mengine, Mungu hatambui kwamba watu hawa ni wafuasi Wake, kwa sababu Mungu haisifu imani yao. Kwa watu hawa, haijalishi wamemfuata Mungu kwa miaka mingapi, mawazo na mitazamo yao haijawahi kubadilika. Wao ni kama wasioamini, wanatii kanuni na njia ambayo wasioamini wanafanya mambo yao, kutii sheria zao za kunusurika na imani. Hawajawahi kukubali neno la Mungu kama maisha yao, hawajawahi kuamini kwamba neno la Mungu ni ukweli, hawajawahi kunuia kukubali wokovu wa Mungu, na hawajawahi kumtambua Mungu kama Mungu wao. Wanachukulia kuamini katika Mungu kama aina fulani ya burudani ya kielimu, wakimchukulia Mungu kama riziki ya kiroho tu, kwa hivyo hawafikirii kuwa ipo thamani ya kujaribu na kuelewa tabia ya Mungu, au kiini cha Mungu. Unaweza kusema kwamba kila kitu kinacholingana na Mungu wa kweli hakihusiani kwa vyovyote vile na watu hawa. Hawana hamu yoyote, na hawawezi kusumbuliwa kutilia maanani. Hii ni kwa sababu ndani kabisa ya mioyo yao ipo sauti ya nguvu ambayo siku zote inawaambia: Mungu haonekani na hagusiki, na Mungu hayupo. Wanasadiki kwamba kujaribu kumwelewa Mungu wa aina hii hakutastahili jitihada zao; itakuwa sawa na wao kujidanganya. Wao wanaamini tu kwa kumtambua Mungu kwa maneno tu bila kuchukua msimamo wowote halisi au kujiweka ndani yao kupitia vitendo halisi, wao wanakuwa werevu sana. Je, Mungu anawachukuliaje watu hawa? Anawachukulia kuwa wasioamini. Baadhi ya watu huuliza: “Je, wasioamini wanaweza kulisoma neno la Mungu? Je, wanaweza kutekeleza wajibu wao? Je, wanaweza kuyasema maneno haya: ‘Nitaishi kwa ajili ya Mungu’?” Kile ambacho binadamu wanaona mara nyingi ni maonyesho ya juujuu tu ya watu, na wala si kiini chao halisi. Ilhali Mungu haangalii maonyesho haya ya juujuu; Yeye anaona tu kiini chao halisi cha ndani. Kwa hivyo, hii ndiyo aina ya mtazamo na ufafanuzi ambao Mungu anao, kwa watu kama hawa. Kuhusiana na kile ambacho watu hawa husema: “Kwa nini Mungu hufanya hivi? Kwa nini Mungu hufanya vile? Siwezi kuelewa haya; siwezi kuelewa yale; haya hayaingiliani na mawazo ya mwanadamu; Lazima unielezee haya; …” Katika kujibu hili, Nauliza: Je, ni muhimu kweli kukuelezea mambo haya? Je, mambo haya yana uhusiano wowote na wewe? Je, unafikiri wewe ni nani? Ulitokea wapi? Je, umehitimu kumwelekeza Mungu? Je, unamwamini Yeye? Je, Anatambua imani yako? Kwa sababu imani yako haina chochote kuhusiana na Mungu, matendo Yake yana uhusiano gani na wewe? Hujui pale ulipo katika moyo wa Mungu, kwa hivyo, je, umehitimu kuzungumza na Mungu?

Maneno ya Maonyo

Je, hamhisi vibaya baada ya kusikia matamshi haya? Ingawa huenda msiwe radhi kusikiliza maneno haya, au msiwe radhi kuyakubali, yote ni ukweli. Kwa sababu awamu hii ya kazi ni ya Mungu kutenda, kama hujali nia za Mungu, hujali mtazamo wa Mungu na huelewi kiini halisi na tabia ya Mungu, basi hatimaye wewe ndiwe utakayekosa kufaidi. Msiyalaumu maneno Yangu kwa kuwa magumu kuyasikiliza, na msiyalaumu kwa kufifisha shauku yenu. Mimi naongea ukweli; na wala Sinuii kuwavunja moyo. Haijalishi ni nini Ninachowaomba, na haijalishi jinsi mnavyotakiwa kukifanya, Ninatumai kwamba mtatembea katika njia sahihi, na Ninatumai kwamba mtafuata njia ya Mungu na hamtakengeuka kutoka kwa njia hii. Ikiwa hutaendelea kwa mujibu wa neno la Mungu, na hufuati njia Yake, basi hapawezi kuwa na shaka kwamba unamuasi Mungu na umepotoka kutoka kwenye njia sahihi. Hivyo Ninahisi kuna baadhi ya mambo ambayo ni lazima Niwafafanulie, na kuwafanya muamini bila shaka, kwa uwazi, bila hata chembe ya kutokuwa na uhakika, na kuwasaidia kujua kwa uwazi mtazamo wa Mungu, nia za Mungu, jinsi Mungu humkamilisha mwanadamu, na ni kwa njia gani Anapanga matokeo ya mwanadamu. Endapo kutakuwa na siku ambayo hutaweza kuanza katika njia hii, basi Sitahitajika kuwajibika kwa vyovyote vile kwa sababu maneno haya tayari yamezungumzwa kwako waziwazi. Kuhusu matokeo ya aina mbalimbali za watu Mungu ana mitazamo tofauti. Ana njia Zake mwenyewe za kuwapima, pamoja na kiwango Chake mwenyewe cha mahitaji kwao. Kiwango Chake cha kupima matokeo ya watu ni kile ambacho ni chenye haki kwa kila mmoja—hakuna shaka kuhusu hilo. Hivyo basi, woga wa watu fulani hauhitajiki. Je, umepata tulizo la moyo sasa?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 20)

Kwa hakika, tabia ya Mungu iko wazi kwa kila mmoja na haijafichwa, kwa sababu Mungu hajawahi kumwepuka kimakusudi mtu yeyote na Hajawahi kudhamiria kujaribu kujificha Mwenyewe ili watu wasiweze kumjua Yeye au kumwelewa Yeye. Tabia ya Mungu siku zote imekuwa wazi na siku zote imekuwa ikikabiliana na kila mtu kwa uwazi. Katika usimamizi wa Mungu, Mungu hufanya kazi Yake, akimtazama kila mmoja; na kazi Yake inafanywa kwa kila mtu. Anapoifanya kazi hii, Anazidi kuifichua tabia Yake na kuendelea kutumia kiini Chake, na kile ambacho Anacho na Alicho, ili kumuongoza na kumkimu kila mmoja. Katika kila enzi na kwa kila hatua, haijalishi kama hali ni nzuri au ni mbaya, tabia ya Mungu siku zote iko wazi kwa kila mmoja, na vyote Anavyomiliki na uwepo Wake siku zote viko wazi kwa kila mtu, kama vile tu uhai Wake unavyomtosheleza na kumsaidia mwanadamu kila wakati na bila kukoma. Licha ya haya yote, tabia ya Mungu imebakia kufichwa kwa baadhi ya watu. Kwa nini iko hivyo? Ni kwa sababu ingawa watu hawa wanaishi ndani ya kazi ya Mungu na wanamfuata Mungu, hawajawahi kutafuta kumwelewa Mungu au kutaka kumjua Mungu, sembuse hata kumkaribia Mungu. Kwa watu hawa, kuelewa tabia ya Mungu kunamaanisha mwisho wao umekaribia; inamaanisha wako karibu kuhukumiwa na kushtakiwa na tabia ya Mungu. Hivyo basi, watu hawa hawajawahi kutamani kumwelewa Mungu au tabia Yake, na hawatamani uelewa au maarifa ya kina ya mapenzi ya Mungu. Hawanuii kufahamu mapenzi ya Mungu kwa ushirikiano wa hiari—wanafurahia tu milele na hawachoki kufanya mambo wanayotaka kuyafanya; kumwamini Mungu wanayetaka kumwamini; kumwamini Mungu aliyepo tu katika fikira zao, Mungu aliyepo tu katika dhana zao; na kumwamini Mungu asiyeweza kutenganishwa na wao katika maisha yao ya kila siku. Inapokuja kwa suala la Mungu Mwenyewe wa kweli, wanapuuza kabisa, hawataki kusikia mambo ya Mungu na hawana tamanio la kumwelewa Yeye, kumtilia maanani Yeye, sembuse kuwa na tamanio la kuwa karibu zaidi na Yeye. Wanayatumia tu maneno ambayo Mungu anayaonyesha ili kuweza kujipamba, kujiweka kwa namna fulani wao wenyewe. Kwao, hilo tayari linawafanya kuwa waumini wenye mafanikio na watu walio na imani kwa Mungu ndani ya mioyo yao. Katika mioyo yao, wanaongozwa na mawazo yao, dhana zao, na hata ufafanuzi wao binafsi wa Mungu. Mungu Mwenyewe wa kweli, kwa upande mwingine, Hana uhusiano wowote na wao. Kwa sababu pindi wanapomwelewa Mungu Mwenyewe wa kweli, kuelewa tabia ya Mungu ya kweli, na kuelewa kile Mungu anacho na alicho, hii inamaanisha kwamba matendo ya, imani yao, na yale yote wanayoyafuatilia yatashutumiwa. Na ndiyo maana wanachukia kuelewa kiini cha Mungu, ndiyo maana wanasitasita na hawako tayari kutafuta kwa bidii au kuomba ili wamwelewe Mungu zaidi, wapate kujua zaidi kuhusu mapenzi ya Mungu, na kuielewa vizuri zaidi tabia ya Mungu. Ni Afadhali kwao Mungu awe kitu kilichotungwa, kitu kisicho wazi na kisichoeleweka. Afadhali kwao Mungu awe ni mtu ambaye anafanana kabisa na vile ambavyo wamemfikiria Yeye, mtu ambaye Anaweza kutii matakwa yao, Asiyepunguka kutoa na Anayepatikana kila wakati. Wakati wanapotaka kuifurahia neema ya Mungu, wanamwomba Mungu awe neema hiyo. Wanapohitaji baraka za Mungu, wanamwomba Mungu awe baraka hiyo. Wanapokabiliwa na magumu, wanamwomba Mungu awatie moyo, ili Awe ngao yao. Maarifa ya watu hawa juu ya Mungu yamebakia ndani ya upeo wa neema na baraka. Uelewa wao wa kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe umezuiliwa pia kwa mawazo yao na vilevile barua na mafundisho ya kidini tu. Lakini wapo baadhi ya watu walio na shauku ya kuielewa tabia ya Mungu, wanaotaka kumwona Mungu Mwenyewe kwa kweli, na kuielewa tabia ya Mungu kwa kweli na kile Anacho na alicho. Watu hawa wanautafuta uhalisia wa ukweli na wokovu wa Mungu na wanatafuta kupokea ushindi, wokovu, na ukamilishaji wa Mungu. Watu hawa wanaitumia mioyo yao kusoma neno la Mungu, wanaitumia mioyo yao kuthamini kila hali na kila mtu, tukio, au kitu ambacho Mungu amewapangia, na kuomba na kutafuta kwa uaminifu. Kile wanachotaka zaidi ni kuyajua mapenzi ya Mungu na kuielewa tabia ya kweli na kiini cha Mungu. Hivi ndivyo ilivyo ili wasiweze tena kumkosea Mungu, na kupitia kwa mambo waliyoyapitia, waweze kuona zaidi uzuri wa Mungu na upande Wake wa kweli. Ni ili pia kwamba Mungu halisi na wa kweli aweze kuwepo ndani ya mioyo yao, na ili Mungu awe na nafasi katika mioyo yao, kiasi cha kwamba hawatakuwa wakiishi tena katikati ya fikira, dhana, au hali ya kutokuwa dhahiri. Kwa watu hawa, sababu inayowafanya kuwa na shauku kubwa ya kuielewa tabia ya Mungu na kiini Chake ni kwa sababu tabia ya Mungu na kiini Chake ni mambo ambayo mwanadamu anaweza kuyahitaji wakati wowote katika uzoefu wao, ni tabia Yake na kiini Chake ambavyo hutoa uhai katika maisha yao yote walioishi. Pindi wanapoielewa tabia ya Mungu, wataweza kumcha Mungu kwa njia bora zaidi, kushirikiana kwa njia bora zaidi na kazi ya Mungu, na kujali zaidi mapenzi ya Mungu na kutekeleza wajibu wao kwa njia bora zaidi wakitumia uwezo wao. Hawa ndio watu wa aina mbili inapokuja katika mitazamo yao kwa tabia ya Mungu. Watu wa aina ya kwanza hawataki kuielewa tabia ya Mungu. Ingawa wanasema wanataka kuielewa tabia ya Mungu, waweze kumjua Mungu Mwenyewe, kuona kile Mungu anacho na alicho, na kufahamu kwa kweli mapenzi ya Mungu, ndani yao kabisa wanaona afadhali Mungu asikuwepo. Ni kwa sababu watu wa aina hii wanakosa kumtii Mungu kila wakati na wanampinga; wanashindana na Mungu kwa ajili ya nafasi ndani ya mioyo yao na mara nyingi wanashuku na hata kukataa uwepo wa Mungu. Hawataki kuiruhusu tabia ya Mungu au kumuacha Mungu mwenyewe wa kweli aimiliki mioyo yao. Wanataka tu kutosheleza matamanio, mawazo, na maono yao binafsi. Kwa hivyo, watu hawa wanaweza kumwamini Mungu, kumfuata Mungu, na wanaweza pia kuacha familia zao na kazi kwa ajili Yake, lakini hawaachi njia zao mbaya. Wengine hata wanaiba au kutapanya sadaka, au kumlaani Mungu kisirisiri, ilhali wengine wanaweza kutumia nyadhifa zao mara kwa mara ili kujishuhudia, kujitukuza, na kushindana na Mungu kwa ajili ya watu na hadhi. Wanatumia mbinu na njia mbalimbali kuwafanya watu wawaabudu, wakijaribu daimaa kuwa na ufuasi mkubwa wa watu na kutaka kuwadhibiti watu hao. Baadhi hata wanawapotosha watu kwa kudhamiria na wanawafanya wafikirie kwamba wao ni Mungu ili waweze kutendewa kama Mungu. Hawawezi katu kuwaambia watu kwamba wamepotoshwa, kwamba wao pia ni wapotovu na wenye kiburi, na hivyo wasiwaabudu, na kwamba haijalishi wanafanya vizuri kiasi gani, yote ni kwa sababu ya kuinuliwa na Mungu na kwamba, hata hivyo, wanafanya yale wanayopaswa kufanya. Je, ni kwa nini hawasemi mambo haya? Ni kwa sababu wanaogopa sana kupoteza nafasi zao katika mioyo ya watu. Hii ndiyo maana watu kama hao hawamtukuzi Mungu katu na katu hawamshuhudii Mungu, kwani hawajawahi kujaribu kumwelewa Mungu. Je, wanaweza kumjua Mungu kama hawamwelewi? Haiwezekani! Hivyo, ingawa maneno katika mada “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe” yanaweza kuwa rahisi, yana maana tofauti kwa kila mtu. Kwa mtu ambaye mara nyingi anamwasi Mungu, anampinga Mungu, na ana chuki dhidi ya Mungu, maneno hayo yanaashiria shutuma; ilhali mtu anayefuatilia uhalisi wa kweli na mara nyingi anakuja mbele za Mungu kutafuta mapenzi ya Mungu atayachukulia maneno hayo kama kawaida yake. Kwa hivyo kuna wale miongoni mwenu ambao, wanaposikia mazungumzo kuhusu tabia ya Mungu na kazi ya Mungu, wanaanza kuumwa na kichwa, mioyo yao inajaa upinzani, na wanakuwa katika hali isiyo na utulivu kabisa. Lakini kuna wengine miongoni mwenu wanaofikiria: Mada hii ndiyo hasa ninayohitaji, kwa sababu mada hii ni yenye manufaa sana kwangu. Ni sehemu ambayo haiwezi kukosekana katika uzoefu wangu wa maisha; ni kiini cha msingi, msingi wa imani kwa Mungu, na jambo ambalo mwanadamu hawezi kufikiria kuliacha. Kwenu nyote, mada hii inaweza kuonekana kuwa ya karibu na ya mbali, isiyojulikana ilhali inayozoeleka. Lakini haijalishi ni nini, hii ni mada ambayo kila mmoja lazima aisikilize, aijue, na lazima aielewe. Haijalishi ni vipi utakavyoishughulikia, haijalishi haijalishi jinsi unavyoitazama, au jinsi unavyoielewa, lakini umuhimu wa mada hii hauwezi kupuuzwa.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 21)

Mungu amekuwa akifanya kazi Yake tangu Alipowaumba wanadamu. Hapo mwanzo, ilikuwa kazi rahisi sana, lakini licha ya urahisi wake, ingali ilikuwa na maonyesho ya kiini na tabia ya Mungu. Ingawa kazi ya Mungu kwa sasa imepandishwa viwango, na kazi hii kwa kila mtu anayemfuata Yeye imekuwa kubwa mno na thabiti, yenye maonyesho makubwa ya neno Lake, nafsi ya Mungu imekuwa ikifichwa kutoka kwa wanadamu. Ingawa Amefanyika mwili mara mbili, kuanzia wakati wa simulizi za biblia hadi kwa siku za kisasa, ni nani amewahi kuona nafsi halisi ya Mungu? Kutokana na uelewa wenu, je, kuna mtu yeyote aliyewahi kuona nafsi halisi ya Mungu? La. Hakuna aliyewahi kuona nafsi halisi ya Mungu, kumaanisha kwamba hakuna aliyewahi kuona nafsi ya kweli ya Mungu. Hili ni jambo ambalo kila mmoja anakubaliana nalo. Hivi ni kusema, nafsi halisi ya Mungu, au Roho wa Mungu, amefichwa kutoka kwa wanadamu wote, wakiwemo Adamu na hawa, ambao Aliwaumba, na akiwemo Ayubu mwenye haki, ambaye alikuwa Amemkubali. Hata wao hawakuona nafsi halisi ya Mungu. Lakini ni kwa nini Mungu amedhamiria kuificha nafsi Yake halisi? Baadhi ya watu husema: “Mungu anaogopa kuwatisha watu.” Wengine husema: “Mungu huficha nafsi Yake halisi kwa sababu binadamu ni mdogo sana na Mungu ni mkuu sana; wanadamu hawaruhusiwi kumwona Yeye, la sivyo watakufa.” Wapo pia wale wanaosema: “Mungu amekua akishughulika sana na usimamizi wa kazi Yake kila siku, huenda Asiwe na muda wa kuonekana na kuwaruhusu watu kumwona Yeye.” Haijalishi ni nini mnachoamini, Nina hitimisho hapa. Hitimisho hilo ni nini? Ni kwamba tu Mungu hataki watu waione nafsi Yake halisi. Akiwa amefichwa kutoka kwa binadamu ni kitu ambacho Mungu anafanya kimakusudi. Kwa maneno mengine, ni nia ya Mungu kwa watu kutoona nafsi Yake halisi. Hii inapaswa kuwa wazi kwa wote sasa. Kama Mungu hajawahi kuonyesha nafsi Yake kwa yeyote, je, mnafikiria nafsi ya Mungu ipo? (Ipo.) Bila shaka ipo. Uwepo wa nafsi ya Mungu haupingiki. Lakini kuhusu nafsi ya Mungu ni kubwa vipi au inafanana vipi, je, ni maswali ambayo mwanadamu anafaa kuchunguza? La. Jibu ni hapana. Kama nafsi ya Mungu si mada ambayo tunafaa kuchunguza, basi ni swali lipi ambalo tunafaa kuchunguza? (Tabia ya Mungu.) (Kazi ya Mungu.) Kabla hatujaanza kushiriki kuhusu mada hii rasmi, hata hivyo, hebu turudi katika kile tulichokuwa tukikizungumzia muda mfupi uliopita: Kwa nini Mungu hajawahi kuonyesha nafsi Yake kwa wanadamu? Kwa nini Mungu anaficha kimakusudi nafsi Yake kutoka kwa wanadamu? Kuna sababu moja tu, nayo ni hii: Ingawa mwanadamu ambaye Mungu alimuumba, amepitia maelfuya miaka ya kazi ya Mungu, hakuna hata mtu mmoja anayejua kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na kiini cha Mungu. Watu kama hao, machoni pa Mungu, wako kinyume na Mungu, na Mungu asingejionyesha mwenyewe kwa watu walio na uadui na Yeye. Hii ndiyo sababu ya pekee kwa nini Mungu hajawahi kuwaonyesha wanadamu nafsi Yake na ndiyo sababu Anaificha kwa makusudi nafsi Yake dhidi yao. Je, sasa mnaelewa kuhusu umuhimu wa kuijua tabia ya Mungu?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 22)

Tangu kuwepo kwa usimamizi wa Mungu, siku zote Amejitolea kikamilifu katika kutekeleza kazi Yake. Licha ya kuficha nafsi Yake kutoka kwao, siku zote Amekuwa upande wa mwanadamu, Akifanya kazi kwa mwanadamu, Akionyesha tabia Yake, Akiwaongoza wanadamu wote kwa kiini Chake, na kufanya kazi Yake kwa kila mmoja kupitia nguvu Zake, hekima Yake, na mamlaka Yake, hivyo akiileta Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na sasa Enzi ya Ufalme. Ingawa Mungu huificha nafsi Yake kutoka kwa binadamu, tabia Yake, uwepo Wake na miliki Yake, na mapenzi Yake kwa binadamu yanafichuliwa kikamilifu kwa mwanadamu, ili mwanadamu aweze kuona na kupitia. Kwa maneno mengine, ingawa binadamu hawawezi kumwona au kumgusa Mungu, tabia na kiini cha Mungu ambacho binadamu wamekuwa wakikutana nacho ni maonyesho kabisa ya Mungu Mwenyewe. Je, hayo si kweli? Bila kujali ni mbinu gani au ni mtazamo gani ambao Mungu anachagua kwa ajili ya kazi Yake, Yeye huwatendea watu siku zote kupitia utambulisho Wake wa kweli, Akifanya kazi Anayopaswa kufanya, na kunena maneno ambayo Anapaswa kunena. Haijalishi ni nafasi gani ambayo Mungu anazungumza kutoka—Anaweza kuwa amesimama kwenye mbingu ya tatu, au Amesimama akiwa katika mwili, au hata kama mtu wa kawaida—siku zote Anaongea kwa binadamu kwa moyo Wake wote na kwa akili Zake zote, bila udanganyifu wowote au kuficha chochote Anapotekeleza kazi Yake, Mungu huonyesha neno Lake na tabia Yake, na huonyesha kile Anacho na Alicho, bila kuficha chochote. Anawaongoza wanadamu kwa uhai Wake na nafsi Yake na miliki yake. Hivi ndivyo binadamu alivyoishi katika Enzi ya Sheria—enzi asilia ya binadamu—akiongozwa na Mungu asiyeonekana na asiyegusika.

Mungu alifanyika mwili kwa mara ya kwanza baada ya Enzi ya Sheria, kupata mwili ambako kulidumu kwa miaka thelathini na tatu na nusu. Kwa mwanadamu, je, miaka thelathini na mitatu na nusu ni muda mrefu? (Si muda mrefu.) Kwa sababu urefu wa maisha ya mwanadamu kwa kawaida ni mirefu zaidi kuliko miaka thelathini na kitu, huu si muda mrefu kwa mwanadamu. Lakini kwa Mungu mwenye mwili, miaka hii thelathini na mitatu na nusu ilikuwa mirefu mno. Aligeuka na kuwa mtu—mtu wa kawaida aliyetekeleza kazi na agizo la Mungu. Hii ilimaanisha kwamba Alipaswa kufanya kazi ambayo mtu wa kawaida asingeweza kuifanya, huku Akivumilia mateso ambayo binadamu wa kawaida hawezi kuvumilia. Kiwango cha mateso aliyovumilia Bwana Yesu katika Enzi ya Neema, kuanzia mwanzo wa kazi Yake hadi wakati Aliposulubishwa msalabani, huenda isiwe ni kitu ambacho watu wa leo wanaweza kushuhudia wao binafsi, lakini je, mnaweza kutambua angalau kwa kiasi kidogo kupitia hadithi zilizo kwenye Biblia? Haijalishi ni maelezo mangapi yaliyopo kwenye ukweli huu uliorekodiwa, kwa ujumla, kazi ya Mungu katika kipindi hiki ilijaa ugumu na mateso. Kwa mwanadamu aliyepotoka muda wa miaka thelathini na mitatu na nusu si mrefu; mateso kidogo si jambo la kutisha. Lakini kwa Mungu mtakatifu asiye na doa, ambaye lazima Avumilie dhambi zote za binadamu, na kula, kulala na kuishi na watenda dhambi, maumivu haya ni makubwa mno. Yeye ndiye Muumba, Bwana wa viumbe vyote na Mtawala wa vitu vyote, lakini Alipokuja duniani alilazimika kuvumilia unyanyasaji na ukatili wa wanadamu waliopotoka. Ili kuikamilisha kazi Yake na kuwaokoa binadamu kutoka kwa taabu, Alilazimika kushutumiwa na binadamu, na kuvumilia dhambi za wanadamu wote. Kiwango cha mateso Aliyoyapitia hakiwezi kwa kweli kueleweka au kutambulika na watu wa kawaida. Je, mateso haya yanawakilisha nini? Yanawakilisha kujitoa kwa Mungu kwa ajili ya wanadamu. Yanawakilisha fedheha Aliyoipata na gharama Aliyolipa kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu, kukomboa dhambi zao, na kukamilisha hatua hii ya kazi Yake. Pia yanamaanisha kwamba mwanadamu angekombolewa kutoka msalabani na Mungu. Hii ndiyo gharama iliyolipwa kwa damu, kwa maisha, gharama ambayo viumbe walioumbwa hawawezi kumudu. Ni kwa sababu Anacho kiini cha Mungu na Ana kile Mungu anacho na alicho, ndiyo maana Anaweza kuvumilia aina hii ya mateso na aina hii ya kazi. Hili ni jambo ambalo hakuna kiumbe aliyeumbwa ambaye angeweza kufanya badala Yake. Hii ni kazi ya Mungu katika Enzi ya Neema na ufunuo wa tabia Yake. Je, hii inafichua chochote kuhusu kile Mungu anacho na alicho? Je, wanadamu wanastahili kuijua? Katika enzi hiyo, japokuwa mwanadamu hakuiona nafsi ya Mungu, alipokea sadaka ya Mungu dhidi ya dhambi zake na akakombolewa kutoka msalabani na Mungu. Huenda wanadamu wasiijue kazi ambayo Mungu alifanya wakati wa Enzi ya Neema, lakini je, kuna yeyote anayefahamu tabia na nia zilizoonyeshwa na Mungu katika kipindi hiki? Binadamu anajua tu kuhusu maudhui ya kazi ya Mungu katika enzi tofauti na kupitia njia mbalimbali, au anajua hadithi zinazohusiana na Mungu ambazo zilifanyika kwa wakati huo huo ambao Mungu alikuwa akitekeleza kazi Yake. Maelezo haya na hadithi hizi kwa kiasi kikubwa ni taarifa fulani tu au hekaya kuhusu Mungu na hazina uhusiano wowote na tabia na kiini cha Mungu. Hivyo haijalishi ni hadithi ngapi watu wanazojua kuhusu Mungu, haimaanishi kwamba wanao uelewa wa kina na maarifa kuhusu tabia ya Mungu au kiini Chake. Kama vile katika Enzi ya Sheria, ingawaje watu kutoka Enzi ya Neema walikuwa wameweza kupitia kukutana kwa karibu na kwa karibu zaidi na Mungu katika mwili, maarifa yao kuhusu tabia ya Mungu na kiini cha Mungu kwa hakika hayakuwepo.

Katika Enzi ya Ufalme, Mungu akafanyika mwili tena, kwa njia sawa na ile Aliyotumia mara ya kwanza. Katika kipindi hiki cha kazi, bado Mungu anaonyesha neno Lake kikamilifu, Anafanya kazi Anayopaswa kufanya, na kueleza kile Anacho na Alicho. Kwa wakati huohuo, Anaendelea kuvumilia na kustahimili kutotii na kutojua kwa binadamu. Je, Mungu hafichui kila wakati tabia Yake na kuonyesha mapenzi yake katika kipindi hiki cha kazi pia? Hivyo basi, tangu kuumbwa kwa mwanadamu hadi sasa, tabia ya Mungu, nafsi Yake na miliki Zake, na mapenzi Yake, siku zote yamekuwa wazi kwa kila mmoja. Mungu hajawahi kuficha kimakusudi kiini Chake, tabia Yake au mapenzi Yake. Ni vile tu mwanadamu hajali kuhusu kile ambacho Mungu anafanya, mapenzi Yake ni yapi—ndio maana uelewa wa binadamu kumhusu Mungu ni finyu mno. Kwa maneno mengine, wakati Mungu anaficha nafsi Yake, Yeye pia Anasimama kando ya mwanadamu kila wakati, akionyesha waziwazi mapenzi Yake, tabia Yake na kiini chake halisi siku zote. Kimsingi, nafsi ya Mungu pia iko wazi kwa watu lakini kutokana na upofu na kutotii kwa binadamu, siku zote hawawezi kuona kuonekana kwa Mungu. Kwa hivyo ikiwa hivyo ndivyo, si inawezekana kuielewa tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe isiwe ni jambo rahisi kwa kila mmoja? Hili ni swali gumu sana kujibu, sivyo? Mnaweza kusema ni rahisi, lakini wakati watu wengine wanatafuta kumjua Mungu, hatimaye hawamjui Yeye au kupata uelewa wa wazi kumhusu Yeye—siku zote ni jambo lililojaa ukungu na lisiloeleweka. Lakini mkisema si rahisi, hilo si sahihi vilevile. Baada ya kuwa mlengwa wa kazi ya Mungu kwa muda mrefu, kila mmoja anapaswa, kupitia uzoefu wake, kuwa amepitia kwa kweli mambo mbalimbali na Mungu. Angalau wanapaswa kumhisi Mungu kwa kiwango fulani katika mioyo yao au wawe na mguso wa kiroho na Mungu, na angalau wanapaswa kuwa na uwezo fulani wa kutambua kuhusu tabia ya Mungu au kupata uelewa fulani kumhusu Yeye. Kuanzia wakati ambao mwanadamu alianza kumfuata Mungu hadi sasa, mwanadamu amepokea mengi mno, lakini kutokana na kila aina ya sababu—uwezo duni wa mwanadamu, ujinga, uasi, na nia mbalimbali—wanadamu pia wamepoteza mengi sana. Je, Mungu bado hajawapatia wanadamu vya kutosha? Ingawa Mungu huficha nafsi Yake kutoka kwa wanadamu, Anawatosheleza mahitaji yao kwa kile Anacho na alicho, na hata uzima Wake; maarifa ya wanadamu kumhusu Mungu hayafai kuwa vile yalivyo tu sasa. Ndiyo maana Nafikiri inahitajika kuwa na ushirika zaidi na nyinyi kuhusu mada ya kazi ya Mungu, kuhusu tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe. Dhumuni ni ili kwamba maelfu ya miaka ya utunzaji na fikira ambayo Mungu ameweka kwa mwanadamu isiishie kuwa bure, na ili wanadamu waweze kuelewa na kutambua kwa kweli mapenzi ya Mungu kwao. Ni ili watu waweze kusonga mbele kwenye hatua mpya ya maarifa yao kumhusu Mungu. Itaweza pia kumrudisha Mungu katika nafasi Yake iliyo sahihi katika mioyo ya watu; yaani, kumtendea Yeye haki.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 23)

Amri ya Mungu kwa Adamu

Mwa 2:15-17 Naye Yehova Mungu akamchukua mtu huyo, na kumweka ndani ya bustani ya Edeni ili ailime na kuihifadhi. Yehova Mungu akamwamrisha mtu huyo, akisema, Unaweza kula kwa uhuru matunda kutoka miti yote ya bustani: Lakini kutoka mti wa maarifa ya mema na maovu, usiyale: kwa kuwa katika siku ambapo utakula matunda kutoka mti huo bila shaka utakufa.

Je, mlielewa chochote kutoka kwenye mistari hii? Je, sehemu hii ya maandiko inakufanya ujihisi vipi? Ni kwa nini Nimeamua kuzungumzia kuhusu “Amri ya Mungu kwa Adamu”? Je, kila mmoja wenu sasa anayo picha ya Mungu na Adamu katika akili yake? Unaweza kujaribu kufikiria: Kama ungekuwa ni wewe katika tukio hilo, je, Mungu katika moyo wako angekuwa vipi? Je, ni hisia gani ambazo picha hii inakupatia? Hii ni picha ya kusisimua na ya kutia moyo. Ingawa kuna Mungu tu na mwanadamu ndani yake, ule ukaribu kati yao unajaza hisia za kupendeza: Upendo wa Mungu ulio tele umetolewa bure kwa mwanadamu, unamzunguka mwanadamu; mwanadamu ni mnyofu na asiye na hatia, aliye huru kabisa na asiye na wasiwasi wowote, anaishi kwa furaha chini ya uangalizi wa jicho la Mungu; Mungu anaonyesha hali ya kumjali mwanadamu, huku naye mwanadamu anaishi katika ulinzi na baraka za Mungu; kila kitu mwanadamu anachofanya na kusema kinaunganishwa kwa karibu na Mungu na hakiwezi kutenganishwa na Mungu.

Mnaweza kusema kwamba hii ndiyo amri ya kwanza ya Mungu aliyoitoa kwa mwanadamu baada ya kumuumba. Je, amri hii inabeba nini? Amri hii ina mapenzi ya Mungu, lakini pia ina wasiwasi Wake kwa wanadamu. Hii ndiyo amri ya kwanza ya Mungu na pia ndio mara ya kwanza Mungu anakuwa na wasiwasi kuhusu binadamu. Hivi ni kusema, Mungu analo jukumu kwa mwanadamu tangu wakati ule Alipomuumba. Jukumu Lake ni lipi? Anapaswa kumlinda mwanadamu, kumwangalia mwanadamu. Anatumaini kwamba mwanadamu ataweza kuamini na kutii maneno Yake. Hili pia ndilo tarajio la kwanza la Mungu kwa binadamu. Na ni kwa tarajio hili kwamba Mungu anasema yafuatayo: “Unaweza kula kwa uhuru matunda kutoka miti yote ya bustani: Lakini kutoka mti wa maarifa ya mema na maovu, usiyale: kwa kuwa katika siku ambapo utakula matunda kutoka mti huo bila shaka utakufa.” Maneno haya rahisi yanawakilisha mapenzi ya Mungu. Yanafichua pia kwamba moyo wa Mungu tayari umeanza kuonyesha hali ya kumjali mwanadamu. Kati ya vitu vyote, ni Adamu pekee aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu; Adamu alikuwa kiumbe hai pekee mwenye pumzi ya uhai wa Mungu; angeweza kutembea na Mungu, kuzungumza na Mungu. Na ndiyo maana Mungu alimpa amri kama hiyo. Mungu aliweka wazi katika amri hii kile binadamu anachoweza kufanya, na vilevile Akaweka wazi kile asichoweza kufanya.

Katika maneno haya machache rahisi, tunauona moyo wa Mungu. Lakini ni moyo wa aina gani tunaouona? Je, kuna upendo katika moyo wa Mungu? Je, upendo huo unao hali yoyote ya kujali ndani yake? Katika mistari hii, upendo na kujali kwa Mungu sio tu kwamba vinaweza kufahamika, bali pia kuhisiwa kwa karibu. Je, hayo ni kweli? Sasa kwa kuwa Nimesema mambo haya, je, bado unafikiri haya ni maneno machache tu yaliyo rahisi? Si rahisi sana, sivyo? Je, mgeweza kuona hili hapo kabla? Kama Mungu mwenyewe angekuambia maneno hayo machache, ungehisi vipi ndani? Kama wewe si mtu mwenye utu, kama moyo wako ni baridi kama barafu, basi usingehisi chochote, usingethamini upendo wa Mungu, na usingejaribu kuuelewa moyo wa Mungu. Lakini kama wewe ni mtu mwenye dhamiri, mwenye ubinadamu, basi utahisi tofauti. Utahisi joto, utahisi kuwa umetunzwa na umependwa, na utahisi furaha. Je, hayo ni kweli? Unapohisi mambo haya, utatenda vipi kwa Mungu? Je, ungehisi kuunganishwa na Mungu? Je, ungempenda na kumheshimu Mungu kutoka ndani kabisa ya moyo wako? Je, moyo wako ungekua karibu zaidi na Mungu? Unaweza kuona kutoka kwa haya jinsi ambavyo upendo wa Mungu ulivyo muhimu kwa binadamu. Lakini kile kilicho muhimu zaidi ni kuthamini na kufahamu kwa binadamu upendo huu wa Mungu. Kwa hakika, je, Mungu hasemi mambo mengi yanayofanana kwenye awamu hii ya kazi Yake? Lakini je, watu wa leo wanauthamini moyo wa Mungu? Je, mnaweza kung’amua mapenzi ya Mungu Niliyoyazungumzia muda mfupi uliopita? Hamwezi hata kutambua mapenzi ya Mungu wakati yanaonekana waziwazi, yanaweza kuonekana na ni halisi. Na ndiyo maana Nasema hamna maarifa na uelewa halisi wa Mungu. Je, haya si kweli?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 24)

Mungu Amuumba Hawa

Mwa 2:18-20 Yehova Mungu akasema, Si vizuri kuwa mtu huyo akuwe peke yake; nitamuumbia msaidizi anayefanana na yeye. Na kutoka kwa ardhi Yehova Mungu akaumba wanyama wote wa msituni, na ndege wote wa angani; na akawaletea kwa Adamu ndiyo aone majina ambayo angewapa: na chochote ambacho Adamu alikiita kiumbe hai, hilo ndilo likawa jina lake kuanzia hapo. Naye Adamu akawapa wanyama wote wa kufugwa majina, na ndege wa hewani, na wanyama wote wa mwituni; lakini kwa Adamu hakupatikana msaidizi ambaye alifanana na yeye.

Mwa 2:22-23 Nao ubavu, ambao Yehova Mungu aliuchukua kutoka kwa Adamu, Yeye akaufanya uwe mwanamke, na akampeleka kwa Adamu. Naye Adamu akasema, Huyu sasa ni mfupa wa mifupa yangu, na nyama ya nyama zangu: ataitwa Mwanamke, kwa kuwa amechukuliwa kutoka kwa Mwanamume.

Kuna msitari mmoja muhimu katika sehemu hii ya Maandiko: “chochote ambacho Adamu alikiita kiumbe hai, hilo ndilo likawa jina lake kuanzia hapo.” Kwa hivyo, ni nani aliyewapatia viumbe hai wote majina yao? Ilikuwa Adamu, si Mungu. Msitari huu unamwambia mwanadamu ukweli: Mungu alimpa binadamu werevu Alipomuumba. Hivi ni kusema kwamba, werevu wa binadamu ulitoka kwa Mungu. Hili ni kweli. Lakini kwa nini? Baada ya Mungu kumuumba Adamu, je, Adamu alienda shuleni? Je, alijua namna ya kusoma? Baada ya Mungu kuwaumba viumbe hai mbalimbali, je, Adamu aliwatambua viumbe hawa wote? Je, Mungu alimwambia majina ya viumbe hao? Bila shaka, Mungu pia hakumfunza namna ya kutunga majina ya viumbe hawa. Huo ndio ukweli! Basi alijua vipi namna ya kuwapa viumbe hao hai majina yao na aina gani ya majina ya kuwapatia? Haya yote yanahusiana na swali kuhusu ni nini ambacho Mungu aliongezea kwa Adamu Alipomuumba. Ukweli unathibitisha kwamba wakati Mungu alipomuumba mwanadamu, Alimwongezea akili. Huu ni ukweli muhimu sana. Je, nyinyi nyote mmesikiliza kwa makini? Kuna ukweli mwingine wa muhimu ambao unapaswa kuwa wazi kwenu? Baada ya Adamu kuwapatia viumbe hai majina yao, majina haya yalipangwa kwenye msamiati wa Mungu. Kwa nini Ninasema hivyo? Hii pia inahusisha tabia ya Mungu, na lazima Niielezee.

Mungu alimuumba mwanadamu, Alimpulizia uhai ndani yake, na pia akampa sehemu ya akili Zake, uwezo Wake, na kile Anacho na Alicho. Baada ya Mungu kumpa mwanadamu vitu hivi vyote, mwanadamu aliweza kufanya baadhi ya mambo kwa kujitegemea na kwa kufikiria peke yake. Ikiwa kile ambacho mwanadamu anaunda na kufanya ni kizuri machoni mwa Mungu, basi Mungu anakikubali na haingilii kati. Kama kile mwanadamu anachofanya ni sahihi, basi Mungu atakiacha tu kiwe hivyo milele. Kwa hivyo kauli hii “chochote ambacho Adamu alikiita kiumbe hai, hilo ndilo likawa jina lake kuanzia hapo” inaonyesha nini? Hiyo inaonyesha kwamba Mungu hakufanya marekebisho yoyote kwa majina ya wale viumbe hiyo mbalimbali. Jina lolote lile ambalo Adamu aliliita kwa kiumbe, Mungu alisema “Ndiyo” na akasajili jina hilo kama ilivyo. Je, Mungu alitoa maoni yoyote? La, hilo ni hakika. Kwa hivyo, mnaona nini hapa? Mungu Alimpa mwanadamu akili na mwanadamu akatumia akili zake alizopewa na Mungu kufanya mambo. Ikiwa kile mwanadamu anachofanya ni chanya machoni pa Mungu, basi kinathibitishwa, kutambulika, na kukubalika na Mungu bila ya utathmini au ukosoaji wowote. Hili ni jambo ambalo hakuna mtu au roho mwovu, au Shetani, anaeweza kulifanya. Je, mnauona ufunuo wa tabia ya Mungu hapa? Je, mwanadamu, mtu aliyepotoshwa, au Shetani anaweza kuwaruhusu watu wengine katika kuwawakilisha kufanya mambo huku wakitazama? Bila shaka sivyo! Je, wanaweza kupigania cheo na yule mtu mwingine au nguvu nyingine ambayo ni tofauti na wao? Bila shaka wangefanya hivyo! Na kwa muda huo, kama angekuwa ni mtu aliyepotoshwa au Shetani aliyekuwa na Adamu, bila shaka wangekataa kile ambacho Adamu alikuwa akifanya. Ili kuthibitisha kwamba wanao uwezo wa kufikiria kwa kujitegemea na wana ujuzi wao binafsi wa kipekee, wangekataa kabisa kila kitu alichofanya Adamu: “Unataka kukiita hivyo? Kwa kweli, sitakiita hivyo, nitakiita hivi; ulikiita Tom lakini mimi nitakiita Harry. Lazima nionyeshe jinsi nilivyo mwerevu.” Hii ni asili ya aina gani? Je, hiki si kiburi kilichopitiliza? Lakini je, Mungu ana tabia kama hiyo? Je, Mungu alikuwa na upinzani wowote usiokuwa wa kawaida kwa mambo haya ambayo Adamu alifanya? Bila shaka, jibu ni hapana! Kuhusu tabia ambayo Mungu anaifichua, hakuna kidokezo chochote cha mabishano, kiburi, au kujigamba. Hilo liko wazi kabisa hapa. Hili linaweza kuonekana kuwa jambo dogo tu, lakini kama huelewi kiini cha Mungu, kama moyo wako hautajaribu kujua namna ambavyo Mungu anatenda na mtazamo wa Mungu ni upi, basi hutaijua tabia ya Mungu au kuona udhihirisho na ufunuo wa tabia ya Mungu. Je, hayo si kweli? Je, unakubali kile Nimetoka tu kukuelezea? Kwa mujibu wa matendo ya Adamu, Mungu hakutangaza kwa sauti kwamba, “Umefanya vyema. Umefanya sahihi Ninakubali.” Katika Moyo Wake, hata hivyo, Mungu aliidhinisha, Akathamini, na Akashangilia kile ambacho Adamu alikuwa amefanya. Hili ndilo jambo la kwanza tangu uumbaji ambalo binadamu alikuwa amemfanyia Mungu akifuata maagizo Yake. Ni jambo ambalo binadamu alilifanya badala ya Mungu na kwa niaba ya Mungu. Machoni pa Mungu, hili lilitokana na werevu Aliokuwa amempa mwanadamu. Mungu aliliona kama jambo jema, jambo chanya. Kile ambacho Adamu alikifanya kwa wakati huo kilikuwa ni udhihirisho wa kwanza wa werevu wa Mungu kwa binadamu. Huu ulikuwa ni udhihirisho mzuri kutoka kwa maoni ya Mungu. Kile Ninachotaka kuwaambia ninyi hapa ni kwamba nia za Mungu katika kuongezea sehemu ya kile Anacho na Alicho na werevu wake kwa mwanadamu ilikuwa ni ili mwanadamu aweze kuwa kiumbe hai anayemdhihirisha Yeye. Kwa kiumbe hai kama huyo kufanya mambo hayo kwa niaba Yake, ilikuwa ndicho hasa kile ambacho Mungu alikuwa akitamani kuona.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 25)

Mungu Awatengenezea Adamu na Hawa Nguo za Ngozi

Mwa 3:20-21 Adamu akampa mke wake jina la Hawa; kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa mama ya wote wenye uhai. Pia Yehova Mungu akawatengenezea Adamu na mke wake nguo za ngozi; na akawavisha.

“Pia Yehova Mungu akawatengenezea Adamu na mke wake nguo za ngozi; na akawavisha.” Katika tukio hili, ni nafasi ya aina gani ambayo tunamwona Mungu akiichukua Anapokuwa na Adamu na Hawa? Na je, ni kwa njia gani Mungu anajidhihirisha Mwenyewe katika ulimwengu huu, akiwa na wanadamu wawili tu? Je, Anasimama Mwenyewe katika nafasi ya Mungu? Kaka na dada kutoka Hong Kong, tafadhali jibuni. (Anasimama kama mzazi.) Kaka na dada kutoka Korea Kusini, je, ni nafasi ya aina gani ambayo mnafikiria kwamba Mungu anaichukua hapa? (Kiongozi wa familia.) Kaka na dada kutoka Taiwan, je, mnafikiria nini? (Anasimama nafasi ya mtu aliyepo katika familia ya Adamu na Hawa, nafasi ya mwanafamilia.) Baadhi yenu mnafikiria kuwa Mungu anasimama kama mwanafamilia wa Adamu na Hawa, huku wengine wanasema kwamba Mungu anasimama kama kiongozi wa familia na wengine wanasema kwamba Anasimama kama mzazi. Haya yote yanafaa sana. Lakini ni nini hasa Ninachotilia mkazo hapa? Mungu aliwaumba watu hawa wawili na Aliwachukulia kama wandani Wake. Akiwa kama mwanafamilia wao wa pekee, Mungu aliyaangalia maisha yao, na pia Alikidhi mahitaji yao ya msingi. Hapa, Mungu anasimama kama mzazi wa Adamu na Hawa. Wakati Mungu akifanya haya, binadamu haoni jinsi ambavyo Mungu ni mkuu; haoni mamlaka ya juu zaidi ya Mungu, uajabu Wake, na hata zaidi haoni hasira au uadhama Wake. Kile anachoona tu ni unyenyekevu wa Mungu, upendo Wake, Anavyowajali wanadamu, na jukumu Lake na utunzaji Wake kwake. Mtazamo na njia ambayo Mungu aliwatendea Adamu na Hawa ni sawa na jinsi ambavyo wazazi wanawajali watoto wao. Ni kama pia jinsi wazazi wanavyowapenda, kuwaangalia, na kuwatunza watoto wao wenyewe wa kiume na wa kike—kiuhalisia, kwa namna ya kuonekana, na kushikika. Badala ya kujiweka katika nafasi Yake ya juu na ya ukuu, Mungu mwenyewe alitumia ngozi kutengeneza vazi la binadamu. Haijalishi kama koti hili la manyoya lilitumika kufunika utupu wao au wao kujikinga dhidi ya baridi. Kilicho muhimu ni kwamba, vazi hili lililotumika kuufunika mwili wa binadamu lilitengenezwa na Mungu binafsi kwa mikono Yake mwenyewe. Badala ya kuitengeneza tu kupitia fikira au kwa mbinu za kimiujiza kama watu wanavyofikiria, Mungu kwa halali alikuwa Amefanya jambo ambalo mwanadamu anafikiria kwamba Mungu hawezi na hapaswi kufanya. Hili linaweza kuwa jambo rahisi—ambalo hata baadhi ya watu wanaweza wasifikirie kwamba linastahili kutajwa—lakini linamruhusu mfuasi yeyote wa Mungu ambaye alikuwa amejawa na mawazo yasiyoeleweka kumhusu Yeye, kuweza kupata utambuzi wa uhalisi na uzuri Wake, na kuona uaminifu na unyenyekevu Wake. Inawafanya watu wenye kiburi kupindukia wanaofikiri kuwa wako juu na wana nguvu, kuinamisha vichwa vyao vya majivuno kwa aibu mbele ya ukweli na unyenyekevu wa Mungu. Hapa, ukweli na unyenyekevu wa Mungu unawawezesha zaidi watu kuona jinsi ambavyo Anapendeza. Kinyume chake, yule Mungu “mkuu sana,” Mungu “anayependwa” na Mungu “mwenye nguvu zote” ambaye watu wanamshikilia katika mioyo yao, amekuwa mdogo sana, asiyevutia, na mdhaifu. Unapoona sentensi hii na kusikia hadithi hii, je, unamdharau Mungu kwa sababu Alifanya jambo kama hilo? Baadhi ya watu wanaweza kufanya hivyo, lakini wengine watakuwa na mwitikio tofauti. Watafikiri kwamba Mungu ni wa kweli na wa kupendwa, na hasa ni ule ukweli na uzuri wa Mungu ndio unaowasukuma. Kadiri wanavyoona upande halisi wa Mungu, ndivyo wanavyoweza kuthamini zaidi uwepo wa kweli wa upendo wa Mungu, umuhimu wa Mungu mioyoni mwao, na jinsi ambavyo Anasimama kando yao kila wakati.

Kwa sasa, wacha tuhusishe mazungumzo yetu na ya wakati huu. Kama Mungu aliweza kufanya mambo haya madogo tofauti kwa binadamu Aliowaumba hapo mwanzo kabisa, hata vitu vingine ambavyo watu hawangethubutu kamwe kuvifikiria ama kuvitarajia, basi je, Mungu anaweza kuwafanyia watu wa leo mambo kama hayo? Baadhi ya watu wanasema, “Ndiyo!” Kwa nini ni hivyo? Kwa sababu kiini cha Mungu si bandia, uzuri Wake si bandia. Kwa sababu kiini cha Mungu kwa kweli kipo, na si kitu kilichoongezwa tu na wengine, na bila shaka si kitu ambacho kinabadilika kulingana na wakati, mahali, na enzi. Ukweli na uzuri wa Mungu unaweza kwa kweli kuonyeshwa kupitia kufanya jambo ambalo watu wanafikiria si la kipekee na ni dogo, jambo ambalo ni dogo sana kiasi cha kwamba watu hawawezi hata kufikiria kama Angeweza kulifanya. Mungu si mnafiki. Hakuna kutia chumvi, kufunika ukweli, majivuno au kiburi katika tabia na kiini Chake. Siku zote Hajigambi, lakini badala yake Anawapenda, Anaonyesha hali ya kuwajali, Anawaangalia, na kuwaongoza wanadamu Aliowaumba kwa uaminifu na kwa dhati. Haijalishi ni kiwango kipi ambacho watu wanaweza kuthamini, kuhisi, au kuona, Mungu kwa hakika anafanya mambo haya. Je, kujua kwamba Mungu anacho kiini kama hicho kutaweza kuathiri upendo wa watu Kwake? Je, kutaweza kushawishi namna wanavyomcha Mungu? Ninatumai utakapoelewa upande halisi wa Mungu utaweza kuwa hata karibu zaidi na Yeye na kuweza kuthamini hata zaidi na kwa kweli upendo Wake na utunzaji Wake kwa wanadamu, huku wakati huohuo pia ukimpa moyo wako na kutowahi tena kuwa na shaka au wasiwasi wowote Kwake. Mungu anafanya kimyakimya kila kitu kwa ajili ya binadamu, akifanya kimyakimya kupitia ukweli, uaminifu, na upendo Wake. Lakini siku zote Hana hofu au majuto yoyote kwa yale yote Anayofanya, wala hahitaji mtu yeyote amlipe Yeye kwa njia yoyote au kuwa na nia za kuwahi kupokea kitu kutoka kwa wanadamu. Dhumuni tu la kila kitu Alichowahi kufanya ni ili Aweze kupokea imani na upendo wa kweli kutoka kwa wanadamu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 26)

Mungu Anuia Kuuangamiza Ulimwengu kwa Gharika na Amwagiza Nuhu Kuijenga Safina

Mwa 6:9-14 Hivi ni vizazi vyake Nuhu: Nuhu alikuwa mtu mwenye haki na mtimilifu katika vizazi vyake, naye Nuhu alitembea na Mungu. Naye Nuhu akapata watoto watatu wa kiume, Shemu, Hamu, na Yafethi. Dunia pia ilikuwa potovu mbele za Mungu, nayo dunia ilijaa vurugu. Naye Mungu akaiangalia dunia, na, tazama, ilikuwa imepotoka; kwa sababu kila aliye na mwili alikuwa amejipotoshea njia yake duniani. Naye Mungu akasema kwake Nuhu, Mwisho wa wote walio na mwili umefika mbele Zangu; kwa kuwa dunia imejawa na vurugu kupitia kwao; na, tazama, nitawaangamiza pamoja na dunia. Ujitengenezee safina ya mbao wa mvinje; utatengeneza vyumba ndani ya safina, na uipake lami ndani na nje.

Mwa 6:18-22 Lakini na wewe nitaliimarisha agano Langu; na utaingia ndani ya safina, wewe, na wana wako, na mke wako, na wake zao wana wako pamoja na wewe. Na kwa kila kilicho na uhai chenye mwili, utawaleta wawili wa kila aina katika safina, kuwaweka hai pamoja nawe; watakuwa wa kiume na wa kike. Kila ndege arukaye kwa aina yake, na mifugo kwa aina yake, kila kinachotambaa duniani kwa aina yake, wawili wa aina yote watakuja kwa wewe, ili uwaweke hai. Na ujichukulie chakula cha kila aina kinacholika, nawe ukikusanye kwako; na kitakuwa kwa ajili ya chakula cha ninyi, na cha wao. Nuhu alifanya hivyo; kulingana na vyote ambavyo Mungu alimwamrisha, alifanya hivyo.

Je, sasa mna uelewa wa jumla kuhusu Nuhu ni nani baada ya kusoma vifungu hivi viwili? Je, Nuhu ni mtu wa aina gani? Maandiko asili yanasema: “Nuhu alikuwa mtu mwenye haki na mtimilifu katika vizazi vyake.” Kulingana na uelewa wa watu wa sasa, ni mtu wa aina gani aliyekuwa “mtu mwenye haki” kwa siku hizo? Mtu mwenye haki anapaswa kuwa mtu mkamilifu. Je, mnajua kama mtu huyu mkamilifu alikuwa ni mkamilifu machoni pa mwanadamu au ni mkamilifu machoni pa Mungu? Bila shaka, mtu huyu mkamilifu alikuwa mtu mkamilifu machoni pa Mungu na wala si machoni pa mwanadamu. Haya yote ni kweli! Hii ni kwa sababu binadamu ni kipofu na hawezi kuona, ni Mungu tu ndiye Anayeitazama dunia yote na kila mmoja, na ni Mungu tu ndiye Aliyejua Nuhu alikuwa ni mtu mkamilifu. Kwa hivyo, mpango wa Mungu wa kuuangamiza ulimwengu kwa gharika ulianza pindi tu Alipomuita Nuhu.

…………

Kwamba Nuhu aliitwa ni ukweli rahisi, lakini jambo kuu la kile tunachozungumzia—tabia ya Mungu, mapenzi Yake, na kiini Chake katika rekodi hii—si rahisi sana. Ili kuelewa vipengele hivi kadhaa vya Mungu, ni lazima kwanza tuelewe ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anatamani kumwita, na kupitia hili, tutaweza kuelewa tabia Yake, mapenzi Yake na kiini Chake. Hili ni muhimu. Kwa hivyo, machoni pa Mungu, huyu mtu ambaye Anamwita ni mtu wa aina gani? Huyu ni lazima awe mtu ambaye anaweza kusikiliza maneno Yake na ambaye anaweza kufuata maagizo Yake. Wakati huo huo, ni lazima pia mtu huyu awe na hisia ya uwajibikaji, mtu ambaye atatekeleza neno la Mungu kwa kulichukulia kama jukumu na wajibu ambao anahitajika kutimiza. Basi je, mtu huyu anahitajika kuwa mtu anayemjua Mungu? Hapana. Kwa wakati huo, Nuhu hakuwa amesikia mafundisho mengi ya Mungu au kupitia kazi yoyote ile ya Mungu. Kwa hivyo, maarifa ya Nuhu kumhusu Mungu yalikuwa kidogo sana. Ingawa imerekodiwa hapa kwamba Nuhu alitembea na Mungu, je, aliwahi kuiona nafsi ya Mungu? Jibu ni bila shaka hapana! Kwa sababu katika siku hizo, ni wajumbe wa Mungu tu ndio waliokuja kati ya watu. Ingawa waliweza kumwakilisha Mungu katika kunena na kufanya mambo, walikuwa tu wakiwasilisha mapenzi Yake na nia Zake. Nafsi ya Mungu haikufichuliwa kwa binadamu uso kwa uso. Katika sehemu hii ya maandiko, yote tunayoona kimsingi ni kile ambacho Nuhu alipaswa kufanya na maagizo ya Mungu kwake yalikuwa ni yapi. Kwa hivyo ni kiini kipi kilichoonyeshwa na Mungu hapa? Kila kitu anachofanya Mungu kimepangiliwa kwa uhakika. Anapoona jambo au hali inapotokea, kutakuwa na kiwango cha kulipima jambo hilo katika macho Yake, na kiwango hiki kitaamua kama Ataanza mpango wa kulishughulikia au namna ya kuchukulia jambo na hali hiyo. Yeye si asiyejali au Asiye na hisia kwa kila kitu. Kwa hakika ni kinyume kabisa. Kuna mstari hapa ambao Mungu alimwambia Nuhu: “Mwisho wa wote walio na mwili umefika mbele Zangu; kwa kuwa dunia imejawa na vurugu kupitia kwao; na, tazama, nitawaangamiza pamoja na dunia.” Mungu aliposema hivi, je, Alimaanisha kuwa angewaangamiza wanadamu pekee? La! Mungu Alisema kwamba Angeangamiza viumbe vyote vilivyo hai vyenye mwili. Ni kwa nini Mungu alitaka kuviangamiza? Kuna ufunuo mwingine wa tabia ya Mungu hapa: Machoni pa Mungu, kuna kikomo cha uvumilivu Wake kwa upotovu wa mwanadamu, kwa uchafu, dhuluma, na uasi wa kila mwenye mwili. Je, ukomo Wake ni upi? Ni kama vile Mungu alivyosema: “Mungu akaiangalia dunia, na, tazama, ilikuwa imepotoka; kwa sababu kila aliye na mwili alikuwa amejipotoshea njia yake duniani.” Je, kauli hii “kwa sababu kila aliye na mwili alikuwa amejipotoshea njia yake duniani” inamaanisha nini? Inamaanisha kwamba viumbe vyote vilivyo hai, ikiwa ni pamoja na wale waliomfuata Mungu, wale walioliita jina la Mungu, wale waliowahi kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Mungu, wale waliomtambua Mungu kwa vinywa vyao na hata kumsifu Mungu—mara tu tabia zao zilipojaa upotovu na kufikia macho ya Mungu, basi Angelazimika kuwaangamiza. Huo ulikuwa ukomo wa Mungu. Kwa hivyo, ni hadi kiwango gani ambapo Mungu alibaki kuwa mvumilivu kwa mwanadamu na kwa upotovu wa wenye mwili wote? Hadi kufikia kiwango ambacho watu wote, wawe wafuasi wa Mungu au wasioamini, walikuwa hawatembei katika njia sahihi. Hadi kiwango ambacho binadamu alikuwa hajapotoshwa tu katika maadili na kujawa na maovu, lakini hadi pale ambapo hapakuwa na mtu yeyote ambaye aliamini kuwa Mungu yupo, achilia mbali mtu yeyote ambaye aliamini kuwa ulimwengu unatawaliwa na Mungu na kwamba Mungu anaweza kuwaletea watu nuru na njia sahihi. Hadi kiwango ambacho binadamu aliudharau uwepo wa Mungu, na hakumruhusu Mungu kuwepo. Mara tu upotovu wa mwanadamu ulipofikia kiwango hiki, Mungu asingeweza tena kuvumilia. Je, ni nini ambacho kingechukua nafasi ya hilo? Kuja kwa ghadhabu ya Mungu na adhabu ya Mungu. Je, huo haukuwa ufunuo kiasi wa tabia ya Mungu? Katika enzi hii ya sasa, je, bado yupo binadamu mwenye haki machoni pa Mungu? Je, bado yupo binadamu mkamilifu machoni pa Mungu? Je, enzi hii ndiyo ile ambayo tabia ya wenye mwili wote duniani imepotoka machoni pa Mungu? Katika siku na enzi hii, mbali na wale ambao Mungu anataka kuwakamilisha, wale wanaoweza kumfuata Mungu na kuukubali wokovu Wake, je, hawapimi kikomo cha uvumilivu wa Mungu? Je, kila kitu kinachotokea kando yenu, kila mnachokiona kwa macho yenu, na kusikia kwa masikio yenu, na kupitia ninyi wenyewe kila siku katika ulimwengu huu—si kimejaa vurugu? Machoni pa Mungu, je, ulimwengu kama huu, enzi kama hii, haipaswi kukomeshwa? Ingawa usuli wa enzi ya sasa ni tofauti kabisa na usuli wa enzi ya Nuhu, hisia na ghadhabu Aliyo nayo Mungu kwa kupotoka kwa binadamu inabakia vilevile sawa na ilivyokuwa kwa wakati huo. Mungu anaweza kuwa mvumilivu kwa sababu ya kazi Yake, lakini kulingana na mambo na hali, ulimwengu huu ulipaswa kuangamizwa zamani sana machoni pa Mungu. Hali imepitiliza zaidi ya vile ilivyokuwa wakati ulimwengu ulipoangamizwa kwa gharika. Lakini tofauti ni ipi? Hili ndilo jambo jingine linalohuzunisha moyo wa Mungu zaidi, na pengine kitu ambacho hakuna yeyote kati yenu anayeweza kutambua.

Wakati alipokuwa Akiuangamiza ulimwengu kwa gharika, Mungu aliweza kumwita Nuhu ili aijenge safina na kufanya baadhi ya kazi za matayarisho. Mungu aliweza kumwita mtu mmoja—Nuhu—ili afanye mfululizo wa mambo kwa ajili Yake. Lakini katika enzi hii ya sasa, Mungu hana mtu yeyote wa kumuita. Kwa nini ipo hivyo? Kila mmoja aliyeketi hapa pengine anaweza kuelewa na kujua sababu vizuri sana. Je, mngependa Niweze kuiweka wazi? Kuitaja kwa sauti huenda ikawafanya mhisi aibu na kumfanya kila mmoja akasirike. Baadhi ya watu wanaweza kusema: “Ingawa sisi si watu wenye haki na wala sisi si watu wakamilifu machoni pa Mungu, kama Mungu atatuelekeza sisi kufanya kitu, bado tutaweza kukifanya. Hapo awali, Aliposema maafa makubwa yanakuja, tulianza kuandaa chakula na vitu ambavyo vingehitajika wakati wa maafa. Je, haya yote hayakufanywa kulingana na matakwa ya Mungu? Je, kwa kweli hatukuwa tukishirikiana na kazi ya Mungu? Je, mambo haya tuliyofanya hayawezi kulinganishwa na yale aliyofanya Nuhu? Je, kufanya kile tulichofanya si utiifu wa kweli? Je, hatukuwa tunafuata maagizo ya Mungu? Je, hatukufanya kile ambacho Mungu alisema kwa sababu tuna imani katika maneno ya Mungu? Basi ni kwa nini Mungu bado ana huzuni? Kwa nini Mungu anasema Hana mtu wa kumwita?” Je, kuna tofauti yoyote kati ya vitendo vyenu na vile vya Nuhu? Tofauti ni nini? (Kutayarisha chakula leo kwa ajili ya janga kulikuwa nia yetu wenyewe.) (Matendo yetu hayawezi kufikia yale ya “haki,” ilhali Nuhu alikuwa ni mtu mwenye haki machoni pa Mungu.) Kile mlichosema hakiko mbali sana na ukweli. Kile alichofanya Nuhu ni tofauti sana kulingana na kile ambacho watu wanafanya sasa. Wakati Nuhu alipofanya kama vile Mungu alivyomwagiza hakujua nia za Mungu zilikuwa ni nini. Hakujua ni nini ambacho Mungu Alitaka kukamilisha. Mungu alikuwa amempa tu amri, Akamwagiza afanye kitu, na bila ya maelezo mengi, Nuhu aliendelea mbele na kukifanya. Hakujaribu kuelewa kwa siri nia za Mungu zilikuwa ni nini, wala hakumpinga Mungu au kukosa uaminifu. Alienda tu na kuifanya ipasavyo kwa moyo safi na rahisi. Chochote ambacho Mungu alimruhusu afanye alifanya, na kutii na kusikiliza neno la Mungu vyote vilikuwa ni imani yake ya kufanya mambo. Hivyo ndivyo alivyoshughulika moja kwa moja na kwa urahisi na kile ambacho Mungu alimwaminia kufanya. Kiini chake—kiini cha vitendo vyake kilikuwa ni utiifu, si kubahatisha, si kupinga, na zaidi ya hayo, si kufikiria kuhusu maslahi yake binafsi na faida zake na hasara zake. Zaidi ya hayo, wakati Mungu aliposema Angeuangamiza ulimwengu kwa gharika, Nuhu hakuuliza ni lini au kuuliza jinsi mambo yatakavyokuwa, na bila shaka hakumwuliza Mungu jinsi ambavyo Angeuangamiza ulimwengu. Alifanya tu kama Mungu alivyomwagiza. Njia yoyote ile ambayo Mungu alitaka safina hiyo iweze kujengwa na hasa ijengwe na nini, alifanya vile ambavyo Mungu alimwambia, na pia alianza kazi mara moja. Alifanya kulingana na maagizo ya Mungu kwa mtazamo wa kutaka kumridhisha Mungu. Je, alikuwa akifanya hivyo ili kujisaidia yeye mwenyewe kuepuka janga? La. Je, alimwuliza Mungu itachukua muda gani zaidi kabla ya ulimwengu kuangamizwa? Hakuuliza. Je, alimwuliza Mungu au alijua ingechukua muda gani kuijenga safina? Hakujua hilo pia. Alitii tu, akasikiliza, na kufanya hivyo inavyohitajika. Watu wa sasa si sawa: Mara tu taarifa fulani inapojitokeza kupitia kwa neno la Mungu, mara tu watu wanapohisi ishara ya kutatizwa au matatizo, wote watachukua hatua mara moja, haijalishi ni nini, au bila kujali gharama, ili kutayarisha kile ambacho watakula, kunywa, na kutumia baada ya janga kupita, hata kupanga njia za wao kutoroka wakati janga litakapotokea. La kuvutia hata zaidi ni kwamba, wakati huu muhimu, akili za binadamu ni nzuri sana katika “kukamilisha kazi.” Katika hali ambazo Mungu hajatoa maagizo yoyote, binadamu anaweza kupanga kila kitu kwa njia inayofaa. Mnaweza kutumia neno “sahihi” ili kuielezea. Na kuhusiana na kile ambacho Mungu anasema, nia za Mungu ni nini, au kile ambacho Mungu anataka ni nini, hakuna anayejali na hakuna anayejaribu kuzitambua. Je, hii siyo tofauti kubwa zaidi kati ya watu wa leo na Nuhu?

Katika rekodi hii ya hadithi ya Nuhu, je, mnaona sehemu ya tabia ya Mungu? Kuna ukomo kwa subira ya Mungu kwa upotovu, uchafu, na dhuluma ya mwanadamu. Anapofikia kikomo hicho, Hatawahi tena kuwa na subira na badala yake Ataanza usimamizi Wake mpya na mpango mpya, kuanza kufanya kile ambacho lazima Afanye, kufichua matendo Yake na upande ule mwingine wa tabia Yake. Hiki kitendo Chake si cha kuonyesha kwamba lazima Asiwahi kamwe kukosewa na binadamu au kwamba Amejawa na mamlaka na ghadhabu, na wala si kuonyesha kwamba Anaweza kuwaangamiza binadamu. Ni kwamba tabia Yake na kiini Chake kitakatifu hakiwezi tena kuruhusu zaidi, hakiwezi tena kuwavumilia zaidi binadamu wa aina hii waishi mbele Zake, kuishi chini ya utawala Wake. Hivyo ni kusema, wakati wanadamu wote wako dhidi Yake, wakati hakuna mtu yeyote Anayeweza kumwokoa katika ulimwengu mzima, Hatakuwa tena na subira kwa binadamu kama hawa, na Ataweza, bila mashaka yoyote, kutekeleza mpango Wake—kuangamiza binadamu wa aina hii. Kitendo kama hicho cha Mungu kinaamuliwa na tabia Yake. Haya ni matokeo ya lazima, na matokeo ambayo kila kiumbe aliyeumbwa chini ya utawala wa Mungu lazima ayachukue. Je, haya hayaonyeshi kwamba katika enzi ya sasa, Mungu hawezi kusubiri kuukamilisha mpango Wake na kuwaokoa watu Anaotaka kuwaokoa? Katika hali hizi, je, Mungu anajali kuhusu nini zaidi? Sio jinsi wale wasiomfuata Yeye kabisa au wale wanaompinga Yeye, wanavyomtendea au kumpinga Yeye, au jinsi ambavyo mwanadamu anamkashfu Yeye. Anajali tu kuhusu kama wale wanaomfuata Yeye, walengwa wa wokovu Wake katika mpango Wake wa usimamizi, wamekamilishwa na Yeye, na kama wamestahili kuridhika Kwake. Na kuhusiana na wale watu wengine mbali na wale wanaomfuata Yeye, Anawatolea tu adhabu kidogo mara kwa mara ili kuonyesha ghadhabu Yake. Kwa mfano; tsunami, matetemeko ya ardhi, milipuko ya volkano, na kadhalika. Wakati huo huo, pia Anawalinda na kuwaangalia kwa dhati wale wanaomfuata Yeye na ambao wako karibu kuokolewa na Yeye. Tabia ya Mungu ni hii: Kwa upande mmoja, Anaweza kuwa na subira na uvumilivu mwingi kwa watu Anaokusudia kuwakamilisha, na Anaweza kuwasubiria kwa muda mrefu Anavyoweza; kwa upande mwingine, Mungu anawachukia na kuchukizwa kwa dhati na watu wa aina ya Shetani ambao hawamfuati na wanampinga Yeye. Ingawa Hajali kama hawa watu wa aina ya Shetani wanamfuata au wanamwabudu Yeye, bado Anawachukia huku Akiwa na subira kwao katika moyo Wake, na huku Akiamua mwisho wa watu hawa wa aina ya Shetani, Yeye pia anasubiria kufika kwa hatua za mpango Wake wa usimamizi.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 27)

Baraka za Mungu kwa Nuhu Baada ya Gharika

Mwa 9:1-6 Naye Mungu akawabariki Nuhu na wana wake, na akasema kwao, Ninyi Zaeni, na muongezeke, na muijaze tena dunia. Na wanyama wote wa dunia watawaogopa na kuwa na hofu nanyi, na ndege wote wa angani, na vyote vitembeavyo duniani, na kila samaki wa baharini; wamewekwa katika mikono yenu. Kila kisongacho kilicho na uhai kitakuwa chakula chenu, jinsi ambavyo nimewapa mboga ndivyo ninavyowapa vitu vyote. Lakini nyama iliyo na uhai, ambayo ni damu yake, ninyi msiile. Na bila shaka nitahitaji damu yenu ya uhai wenu, nitaihitaji kwa mkono wa kila mnyama, na kwa mkono wa mwanadamu, nitahitaji uhai wa mwanadamu kwa mkono wa ndugu wa kila mwanadamu. Yeyote ambaye atamwaga damu ya mwanadamu, damu yake itamwagika na mwanadamu: kwa kuwa Mungu alimfanya mwanadamu kwa mfano Wake.

Baada ya Nuhu kukubali maagizo ya Mungu na kujenga safina na kuishi katika siku zile ambazo Mungu alitumia gharika ili kuangamiza ulimwengu, familia yake yote ya watu wanane ilinusurika. Mbali na familia ya Nuhu ya watu wanane, wanadamu wote waliangamizwa, na viumbe vyote vilivyokuwa hai duniani viliangamizwa. Kwa Nuhu, Mungu alimpa baraka, na Akasema baadhi ya mambo kwake na kwa watoto wake. Mambo haya yalikuwa yale ambayo Mungu alikuwa amempa na pia ni baraka Zake kwake. Hizi ndizo baraka na ahadi ambazo Mungu anampa yule ambaye anaweza kumsikiliza Yeye na kuyakubali maagizo Yake, na pia namna Anavyowathawabisha watu. Hivi ni kusema, haijalishi kama Nuhu alikuwa binadamu mkamilifu au alikuwa binadamu mwenye haki machoni pa Mungu, na haijalishi ni kiwango kipi alichomjua Mungu, kwa ufupi, Nuhu na watoto wake wa kiume watatu wote waliyasikiliza maneno ya Mungu, walishirikiana na kazi ya Mungu, na kufanya kile ambacho walipaswa kufanya kulingana na maagizo ya Mungu. Kutokana na hayo, walimsaidia Mungu kuweza kubakiza binadamu na aina mbalimbali za viumbe walio na uhai baada ya kuangamizwa kwa ulimwengu na gharika, na hivyo wakawa wamefanya mchango mkubwa kwa hatua iliyofuata ya mpango wa usimamizi wa Mungu. Kwa sababu ya kila kitu alichokuwa amefanya, Mungu alimbariki. Pengine kwa watu wa leo, kile alichofanya Nuhu hakikuwa sana na thamani ya kutajwa. Wengine wanaweza hata kufikiria: “Nuhu hakufanya chochote; Mungu alikuwa ameamua akilini Mwake kumwacha, kwa hivyo bila shaka angeokolewa. Kubaki kwake si kwa sababu ya mambo aliyokamilisha mwenyewe. Hili ndilo jambo ambalo Mungu alitaka lifanyike, kwa sababu mwanadamu hafanyi chochote.” Lakini hicho sicho ambacho Mungu alikuwa anafikiria. Kwa Mungu, haijalishi kama mtu ni mkubwa au asiye wa maana, mradi tu aweze kumsikiliza Yeye, kutii maagizo Yake na kile anachomwaminia na aweze kushirikiana na kazi Yake, mapenzi Yake, na mpango Wake, ili mapenzi Yake na Mpango Wake viweze kukamilika vizuri, basi mwenendo wake unastahili kukumbukwa na Yeye na kustahili kupokea baraka Zake. Mungu huwathamini watu kama hao; Anathamini matendo yao, na Anathamini uaminifu huu na moyo huu wanaouonyesha Kwake. Huu ndio mtazamo wa Mungu. Hivyo kwa nini Mungu alimbariki Nuhu? Kwa sababu hivi ndivyo Mungu anavyoshughulikia vitendo kama hivyo na utiifu wa mwanadamu.

Kuhusiana na baraka za Mungu kwa Nuhu, baadhi ya watu watasema: “Kama binadamu atamsikiliza Mungu na kumtosheleza Mungu, basi Mungu anapaswa kumbariki mwanadamu.” Je, tunaweza kusema hivyo? Watu wengine wanasema: “Hapana.” Kwa nini hatuwezi kusema hivyo? Baadhi ya watu watasema: “Binadamu hastahili kufurahia baraka za Mungu.” Hilo si sahihi kabisa. Kwa sababu wakati mtu anapokubali kile ambacho Mungu amemwaminia, Mungu anacho kiwango cha kuhukumu kama vitendo vya mtu huyu ni vizuri au vibaya na kama mtu huyu amemtii, na kama mtu huyu ametosheleza mapenzi ya Mungu na kama kile anachofanya kinastahili. Kile anachojali Mungu ni kuhusu moyo wa mtu huyu, si vitendo vyake vya juujuu. Siyo kwamba Mungu anapaswa kumbariki mtu ilimradi tu anafanya jambo fulani, bila kujali jinsi wanavyolifanya. Huku ni kutoelewa kwa watu kumhusu Mungu. Mungu haangalii tu mwisho wa matokeo ya mambo, lakini Anazingatia zaidi kuhusu jinsi moyo wa mtu ulivyo na jinsi mtazamo wa mtu ulivyo wakati wa maendeleo ya mambo, na Anaangalia kama kuna utiifu, uzingatiaji, na tamanio la kumtosheleza Mungu katika mioyo yao. Je, ni kiwango gani ambacho Nuhu alijua kuhusu Mungu kwa wakati huo? Je, kiwango hicho kilikuwa ni kikubwa kama mafundisho ya dini mnayojua sasa? Kuhusu vipengele vya ukweli kama vile dhana na maarifa ya Mungu, je, alipokea unyunyiziaji na uchungaji kama ninyi? La, hakupokea! Lakini kuna ukweli mmoja ambao haupingiki: Katika fahamu, akili, na hata kina cha mioyo ya watu wa leo, dhana zao na mtazamo wao kwa Mungu ni usioeleweka na usio na uhakika. Mnaweza hata kusema kwamba sehemu fulani ya watu inashikilia mtazamo hasi kwa uwepo wa Mungu. Lakini katika moyo wa Nuhu na ufahamu wake, uwepo wa Mungu ulikuwa ni halisi na usio na shaka hata kidogo, na hivyo utiifu wake kwa Mungu ulikuwa haujatiwa doa na ungeweza kustahimili majaribio. Moyo wake ulikuwa safi na wazi kwa Mungu. Hakuhitaji maarifa mengi ya mafundisho ili ajishawishi kufuata kila neno la Mungu, wala hakuhitaji ukweli mwingi kuthibitisha uwepo wa Mungu, ili akubali kile ambacho Mungu alimwaminia na kuweza kufanya chochote kile ambacho Mungu angemruhusu kufanya. Hii ni tofauti muhimu kati ya Nuhu na watu wa leo, na pia ndio ufafanuzi wa kweli wa jinsi mtu mkamilifu alivyo machoni pa Mungu. Kile anachotaka Mungu ni watu kama Nuhu. Yeye ni aina ya mtu anayesifiwa na Mungu, na pia hasa mtu wa aina ile ambaye Mungu anambariki. Je, umepata nuru yoyote kutoka kwa hili? Watu wanawatazama watu kutoka kwa nje, ilhali kile ambacho Mungu anatazama ni mioyo ya watu na kiini chao. Mungu hamruhusu mtu yeyote kuwa na moyo usio na ari au wenye mashaka Kwake, wala Hawaruhusu watu wamshuku au kumjaribu kwa njia yoyote ile. Kwa hivyo, ijapokuwa watu wa leo wako uso kwa uso na neno la Mungu—unaweza hata kusema kwamba wako uso kwa uso na Mungu—kutokana na kitu fulani kilicho ndani ya mioyo yao, kuwepo kwa kiini chao potovu, na mtazamo wao wenye uadui Kwake, watu wamezuiwa kuwa na imani ya kweli kwa Mungu na kuzuiwa kutoka kwa utiifu wao Kwake. Kwa sababu hii, ni vigumu sana kwao kupata baraka ile ile ambayo Mungu alimpa Nuhu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 28)

Mungu Aufanya Upinde wa Mvua Kama Ishara ya Agano Lake na Mwanadamu

Mwa 9:11-13 Na nitaweka agano Langu na ninyi, wala miili yote haitaondolewa tena na maji ya gharika; wala hakutakuwa na gharika tena kuiharibu dunia. Naye Mungu akasema, Hii ni alama ya agano ambayo naifanya kati ya Mimi na ninyi na viumbe vyote vyenye uhai vilivyo nanyi, kwa vizazi vya kudumu: naweka upinde Wangu mawinguni, na utakuwa alama ya agano kati ya Mimi na dunia.

Watu wengi zaidi wanajua upinde wa mvua ni nini na wamesikia baadhi ya hadithi zinazohusiana na upinde wa mvua. Kuhusiana na hadithi ile ya upinde wa mvua kwenye biblia, baadhi wa watu wanaisadiki, baadhi wanaichukulia tu kama hadithi ya kale, huku wengine hawaisadiki kabisa. Haijalishi ni nini, kila kitu kilichofanyika kuhusiana na upinde wa mvua ndicho kila kitu ambacho Mungu Alifanya hapo awali, na mambo yaliyofanyika katika mchakato wa usimamizi wa Mungu wa binadamu. Mambo haya yamerekodiwa vivyo hivyo katika Biblia. Rekodi hizi hazituelezi kama Mungu alikuwa katika hali gani kwa wakati huo au nia zilizokuwepo katika maneno haya ambayo Mungu aliyasema. Zaidi ya hayo, hakuna anayeweza kutambua kile ambacho Mungu alikuwa akihisi Aliposema maneno hayo. Hata hivyo, hali ya akili ya Mungu kuhusiana na tukio hili lote imefunuliwa katikati ya mistari ya maandiko. Ni kana kwamba fikira Zake kwa wakati huo zimeandikwa katika kurasa kupitia kila neno na sentensi ya neno la Mungu.

Mawazo ya Mungu ndiyo ambayo watu wanapaswa kuyajali na ndiyo ambayo wanapaswa kuwa wakijaribu kujua zaidi. Hii ni kwa sababu mawazo ya Mungu yana uhusiano wa karibu na uelewa wa mwanadamu kuhusu Mungu, na uelewa wa mwanadamu kuhusu Mungu ni kiungo kisichoweza kukosekana katika kuingia kwa mwanadamu katika maisha. Sasa, Mungu alikuwa akifikiria nini wakati mambo haya yalitokea?

Hapo mwanzo, Mungu aliumba binadamu ambao katika macho Yake walikuwa wazuri sana na karibu na Yeye, lakini waliangamizwa kwa gharika baada ya kuasi dhidi Yake. Je, ilimwumiza Mungu kwamba binadamu kama hao walitoweka tu papo hapo hivyo? Bila shaka Aliumizwa! Kwa hivyo, maonyesho Yake kwa maumivu haya yalikuwa nini? Ilirekodiwaje kwenye Biblia? Ilirekodiwa kwenye Biblia hivi: “Na nitaweka agano langu na ninyi, wala miili yote haitaondolewa tena na maji ya gharika; wala hakutakuwa na gharika tena kuiharibu dunia.” Sentensi hii rahisi inafichuamawazo ya Mungu. Kuangamizwa huku kwa ulimwengu kulimpa Yeye maumivu sana. Kwa maneno ya binadamu, Alikuwa na huzuni sana. Tunaweza kufikiria: Dunia ambayo ilikuwa imejaa maisha ilionekana vipi baada ya kuangamizwa na gharika? Dunia ambayo ilikuwa imejaa wanadamu ilionekana vipi sasa? Hakuna makazi ya kibinadamu, hakuna viumbe hai, maji kila mahali na machafuko kabisa juu ya uso wa maji. Hilo ndilo lililokuwa onyesho la kusudio la asili la Mungu wakati alipoumba ulimwengu? Bila shaka la! Kusudi la awali la Mungu lilikuwa ni kuyaona maisha katika maeneo yote, kuwaona wanadamu Aliowaumba wakimwabudu Yeye, si tu kwa Nuhu kuwa mtu pekee anayemwabudu, au kuwa wa pekee ambaye angeweza kujibu wito Wake wa kukamilisha kile alichoaminiwa kufanya. Ubinadamu ulipotoweka, Mungu hakuona kile Alichokuwa amekusudia awali bali kinyume kabisa cha mambo. Ni vipi ambavyo moyo Wake usingekuwa katika maumivu? Hivyo Alipokuwa akifichua tabia Yake na kuelezea hisia Zake, Mungu alifanya uamuzi. Ni aina gani ya uamuzi Aliofanya? Kuunda upinde mawinguni (upinde wa mvua tunaouona) kama agano na binadamu, ahadi kwamba Mungu hangemwangamiza mwanadamu kwa gharika tena. Wakati huohuo, ilikuwa pia ni kuwaambia watu kwamba Mungu aliwahi kuangamiza ulimwengu kwa gharika, kumfanya mwanadamu akumbuke milele ni kwa nini Mungu alifanya kitu kama hicho.

Je, kuangamizwa kwa ulimwengu wakati huu kulikuwa ni jambo alilotaka Mungu? Bila shaka halikuwa ni jambo ambalo Mungu alitaka. Huenda tukaweza kufikiria sehemu ndogo ya picha ile ya kusikitisha ya ulimwengu baada ya kuangamizwa kwa ulimwengu, lakini hatuwezi kukaribia kufikiria namna hali ilivyokuwa wakati huo machoni pa Mungu. Tunaweza kusema kwamba, haijalishi kama ni watu wa sasa au wa wakati huo, hakuna yeyote anayeweza kufikiria au kutambua ni vipi Mungu alikuwa akihisi Aliposhuhudia tukio hilo, picha hiyo ya ulimwengu baada ya kuangamizwa kwake kwa gharika. Mungu alilazimishwa kufanya haya kutokana na kutotii kwa binadamu, lakini maumivu ambayo moyo wa Mungu ulipitia kutokana na maangamizo haya ya ulimwengu kwa gharika ni uhalisia ambao hakuna anayeweza kuufikiria au kuutambua. Ndiyo maana Mungu aliweka agano na mwanadamu, ambalo kupitia hilo Alilenga kuwaambia watu wakumbuke kwamba Mungu aliwahi kufanya kitu kama hiki, na kuapa kwamba Mungu asingewahi kuangamiza ulimwengu kwa njia hii tena. Katika agano hili, tunauona moyo wa Mungu—tunaona kwamba moyo wa Mungu ulikuwa katika maumivu Alipoangamiza binadamu hawa. Katika lugha ya binadamu, wakati Mungu alipomwangamiza mwanadamu na Akaona mwanadamu akitoweka, moyo Wake ulikuwa ukiomboleza na kuvuja damu. Je, hivyo sivyo tunavyoweza kuifafanua kwa njia bora zaidi? Maneno haya yanatumika na binadamu kuonyesha hisia za kibinadamu, lakini kwa sababu lugha ya binadamu ina upungufu mwingi, kuitumia kufafanua hisia za Mungu haionekani kuwa mbaya sana Kwangu. Sasa mtafikiria nini mtakapouona upinde wa mvua tena? Angalau mtakumbuka namna ambavyo Mungu aliwahi kuwa katika huzuni kwa sababu ya kuuangamiza ulimwengu kwa gharika. Mtakumbuka namna, hata kama Mungu aliuchukia ulimwengu huu na kuudharau ubinadamu huu, Alipowaangamiza wanadamu Aliowaumba kwa mikono Yake mwenyewe, moyo Wake ulikuwa ukisononeka, ukipambana kuachilia, Akihisi kwamba Hakuwa na chaguo lingine, na kupata ugumu kustahimili. Faraja Yake pekee ilikuwa katika familia ya Nuhu ya watu wanane. Ulikuwa ni ushirikiano wa Nuhu uliofanya jitihada Zake za kipekee za kuumba viumbe wote wawe wa thamani. Wakati ambapo Mungu alikuwa akiteseka, hili ndilo jambo pekee ambalo lingeweza kufidia uchungu Wake. Kuanzia hapo, Mungu aliweka matarajio Yake yote ya binadamu kwa familia ya Nuhu, Wakati ambapo Mungu alikuwa akiteseka, hili ndilo jambo pekee ambalo lingeweza kufidia uchungu Wake kwamba wasingeangamizwa.

Ni sehemu gani ya tabia ya Mungu tunayopaswa kujifunza kutokana na hili? Mungu alikuwa amemdharau binadamu kwa sababu binadamu alikuwa na uadui na Yeye, lakini ndani ya moyo Wake, utunzaji Wake, kujali Kwake, na huruma Yake kwa binadamu vilibakia vilevile. Hata wakati alipowaangamiza wanadamu, moyo Wake haukubadilika. Wakati binadamu walikuwa wamejaa upotovu na kutomtii Mungu hadi katika kiwango cha kuhuzunisha, Mungu alilazimika, kwa sababu ya tabia Yake na kiini Chake, na kulingana na kanuni Zake, kuwaangamiza binadamu hao. Lakini kwa sababu ya kiini cha Mungu, bado Aliwahurumia binadamu, hata Akataka kutumia njia mbalimbali za kuwakomboa wanadamu ili waweze kuendelea kuishi. Badala yake, binadamu alimpinga Mungu, akaendelea kumwasi Mungu, na akataa kukubali wokovu wa Mungu, yaani, alikataa kukubali nia Zake nzuri. Haijalishi jinsi ambavyo Mungu aliwaita, kuwakumbusha, kukidhi haja zao, kuwasaidia, au Alivyowavumilia, binadamu hakutambua haya, wala hakutilia maanani. Katika maumivu Yake, Mungu bado hakusahau kumpa binadamu uvumilivu Wake wa kiwango cha juu zaidi, Akimsubiria binadamu ageuke na kubadilika. Baada ya Yeye kufikia kikomo Chake, Alifanya kile Alicholazimika kufanya bila ya kusita. Kwa maneno mengine, kulikuwa na kipindi cha muda mahususi na mchakato kutoka pale ambapo Mungu alipanga kuwaangamiza wanadamu hadi katika mwanzo rasmi wa kazi Yake ya kuwaangamiza wanadamu. Mchakato huu ulikuwepo kwa madhumuni ya kumwezesha mwanadamu kugeuka, na ilikuwa nafasi ya mwisho ambayo Mungu alimpa mwanadamu. Hivyo ni nini ambacho Mungu alifanya kwenye kipindi hiki kabla ya kuwaangamiza wanadamu? Mungu alifanya kiwango kikubwa cha kazi ya kukumbusha na kazi ya kusihi. Haijalishi ni maumivu na huzuni ya kiwango gani yaliyokuwa ndani ya moyo wa Mungu, Aliendelea kutumia utunzaji Wake, kujali, na rehema nyingi kwa wanadamu. Tunaona nini kutoka kwa haya? Bila shaka, tunaona kwamba upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wa kweli na si tu jambo ambalo Analizungumzia bila matendo. Ni jambo halisi, linaloweza kushikika na kutambulika, si bandia, hauna dosari, haudanganyi wala haujifanyi. Mungu kamwe hatumii uongo au kuunda taswira za bandia ili Awafanye watu waone kwamba Yeye anapendeka. Kamwe hatumii ushuhuda wa uongo ili kuwafanya watu wauone uzuri Wake, au kuringia uzuri wake na utakatifu Wake. Je, vipengele hivi vya tabia ya Mungu havistahili kupendwa na mwanadamu? Kwani navyo havistahili kuabudiwa? Kwani navyo havistahili kupendwa sana? Kwa sasa, Ningependa kuwauliza: Baada ya kuyasikia maneno haya, mnafikiri kwamba ukuu wa Mungu ni maneno matupu tu kwenye kipande cha karatasi? Je, uzuri wa Mungu ni maneno matupu tu? La! Bila shaka sivyo! Mamlaka ya juu, ukuu, utakatifu, uvumilivu, upendo wa Mungu na kadhalika—kila undani wa kila mojawapo ya vipengele mbalimbali vya tabia na kiini cha Mungu hupata maonyesho ya kivitendo kila wakati Anapofanya kazi Yake, ikijumuishwa katika mapenzi Yake kwa mwanadamu, na pia kutimizwa na kuakisiwa kwa kila mtu. Licha ya kama umewahi kuihisi hapo awali, Mungu anamtunza kila mtu katika kila njia inayowezekana, kwa kutumia moyo Wake wa dhati, hekima, na mbinu mbalimbali ili kuuchangamsha moyo wa kila mtu, na kuamsha roho ya kila mtu. Huu ni ukweli usiopingika.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 29)

Mungu Aufanya Upinde wa Mvua Kama Ishara ya Agano Lake na Mwanadamu

Mwa 9:11-13 Na nitaweka agano Langu na ninyi, wala miili yote haitaondolewa tena na maji ya gharika; wala hakutakuwa na gharika tena kuiharibu dunia. Naye Mungu akasema, Hii ni alama ya agano ambayo naifanya kati ya Mimi na ninyi na viumbe vyote vyenye uhai vilivyo nanyi, kwa vizazi vya kudumu: naweka upinde Wangu mawinguni, na utakuwa alama ya agano kati ya Mimi na dunia.

Mungu alimuumba mwanadamu; bila kujali kama wamepotoshwa au kama wanamfuata Yeye, Mungu huwachukulia wanadamu kama wapendwa Wake zaidi—au kama vile wanadamu wangesema, watu wanaopendwa sana Naye—na si kama vikaragosi Wake. Ingawa Mungu anasema Yeye ndiye muumba na kwamba binadamu ni uumbaji Wake, hali ambayo inaweza kuonekana ni kana kwamba kuna tofauti kiasi katika mpangilio wa cheo, uhalisia ni kwamba kila kitu ambacho Mungu amefanya kwa mwanadamu kinazidi kabisa uhusiano wa asili hii. Mungu anampenda mwanadamu, Anamtunza mwanadamu, na anaonyesha kwamba anamjali mwanadamu, pamoja na kumkimu mwanadamu bila kuacha na bila ya kusita. Wala Hahisi katika moyo Wake kwamba hii ni kazi ya ziada au ni kitu kinachostahili sifa nyingi. Wala Hahisi kwamba kuwaokoa wanadamu, kuwatosheleza, na kuwapatia kila kitu, ni kutoa mchango mkubwa kwa binadamu. Anamkimu tu mwanadamu kimyakimya na kwa utulivu, kwa njia Yake mwenyewe na kupitia kwa kiini Chake na kileAnacho na alicho. Haijalishi ni kiasi gani cha utoaji na msaada kiasi gani mwanadamu anapokea kutoka Kwake, Mungu kamwe hafikirii wala hajaribu kujipatia sifa. Hii inaamuliwa na kiini cha Mungu, na pia hasa ni maonyesho ya kweli ya tabia ya Mungu. Hii ndiyo sababu, bila kujali ikiwa ni katika Biblia au vitabu vingine vyovyote, hatupati kamwe Mungu akieleza mawazo Yake, na hatupati kamwe Mungu akieleza au kutangaza kwa wanadamu kwa nini Anafanya mambo haya, au kwa nini Anawajali sana wanadamu, ili kuwafanya wanadamu wawe na shukrani Kwake au kumsifu. Hata Anapoumizwa, wakati moyo Wake ukiwa katika maumivu makali, Hasahau kamwe wajibu Wake kwa wanadamu au kujali Kwake kwa wanadamu, wakati wote Anabeba uchungu na maumivu haya peke yake kwa ukimya. Kinyume cha mambo ni kwamba, Mungu anaendelea kumkimu mwanadamu kama Anavyofanya siku zote. Ingawa mwanadamu mara nyingi humsifia Mungu au huwa na ushuhuda Kwake, hakuna kati ya tabia hii ambayo imedaiwa na Mungu. Hii ni kwa sababu Mungu hajawahi kunuia kwa kitu chochote kizuri Anachofanya kwa wanadamu kibadilishwe kwa shukrani au kiweze kulipwa. Kwa upande mwingine, wale wanaomcha Mungu na kujiepusha na maovu, wale wanaomfuata Mungu kwa kweli, wanaomsikiliza Yeye, na walio waaminifu Kwake, na wale wanaomtii Yeye—hawa ndio watu ambao mara nyingi watapokea baraka za Mungu, na Mungu atawakabidhi baraka hizo bila kusita. Zaidi ya hayo, baraka ambazo watu hupokea kutoka kwa Mungu mara nyingi huwa zaidi ya mawazo yao, na pia zaidi ya chochote ambacho wanadamu wanaweza kubadilishana kwa kile ambacho wamefanya au gharama ambayo wamelipa. Wakati wanadamu wanafurahia baraka za Mungu, je, kuna yeyote anayejali kuhusu kile ambacho Mungu anafanya? Je, yupo yeyote anayeonyesha wasiwasi wowote kuhusu vile ambavyo Mungu anahisi? Je, yupo yeyote anayejaribu kutambua maumivu ya Mungu? Jibu la uhakika la maswali haya ni: Hapana! Je, mwanadamu yeyote, akiwemo Nuhu, anaweza kutambua yale maumivu ambayo Mungu alikuwa akihisi wakati huo? Je, kuna yeyote anayeweza kufahamu ni kwa nini Mungu alianzisha agano kama hilo? Hakuna anayeweza! Mwanadamu hafahamu maumivu ya Mungu si kwa sababu hawezi kuelewa maumivu ya Mungu, na si kwa sababu ya umbali uliopo kati ya Mungu na mwanadamu au tofauti kati ya hadhi zao; badala yake, ni kwa sababu mwanadamu hata hajali kuhusu hisia zozote za Mungu. Mwanadamu anafikiria Mungu yuko huru—Mungu hahitaji watu wa kujali kuhusu Yeye, kumwelewa au kumwonyesha namna anavyomfikiria. Mungu ni Mungu, hivyo Hana maumivu, Hana hisia; Hatakasirika, Hahisi huzuni, hata Halii. Mungu ni Mungu, hivyo Hahitaji maonyesho yoyote ya kihisia na Hahitaji faraja yoyote ya kihisia. Ikiwa, chini ya hali fulani, Atahitaji vitu hivi, basi Atatatua mwenyewe na Hatahitaji usaidizi wowote kutoka kwa mwanadamu. Lakini kinyume chake ni kwamba, ni wale binadamu wanyonge, ambao hawajakomaa ndio wanaohitaji faraja ya Mungu, utoaji, himizo, na hata kwa Yeye kuweza kufariji hisia zao wakati wowote na mahali popote. Fikira kama hiyo inajificha ndani kabisa ya mioyo ya wanadamu: Binadamu ndiye mnyonge; wanamhitaji Mungu ili awatunze kwa kila njia, wanastahili utunzaji wote wanaopokea kutoka kwa Mungu, na wanapaswa kudai kutoka kwa Mungu chochote kile wanachohisi kinafaa kuwa chao. Mungu ndiye mwenye Nguvu; Ana kila kitu, na Anahitaji kuwa mlezi wa mwanadamu na Anayetoa baraka. Kwa sababu Yeye tayari ni Mungu, Yeye ni Muweza wa yote na Hahitaji kamwe chochote kutoka kwa mwanadamu.

Kwa vile binadamu hatilii maanani ufunuo wowote wa Mungu, hajawahi kuhisi huzuni, maumivu au furaha ya Mungu. Lakini kinyume chake ni kwamba, Mungu anajua maonyesho yote ya binadamu kama vile anavyojua sehemu ya kiganja cha mkono Wake. Mungu hutosheleza mahitaji ya kila mtu wakati wote na mahali popote, Akitazama mawazo yanayobadilika ya kila mtu na hivyo Anawafariji na kuwahimiza, na kuwaongoza na kuwaangazia. Kuhusu mambo yote ambayo Mungu amemfanyia mwanadamu, na gharama zote Alizolipa kwa sababu yao, je, watu wanaweza kupata kifungu kutoka kwenye Biblia au kutoka kwa chochote ambacho Mungu amesema mpaka sasa kinachoelezea waziwazi kwamba Mungu atadai kitu kutoka kwa binadamu? La! Kinyume cha mambo, haijalishi jinsi watu wanavyopuuza fikira za Mungu, bado Anawaongoza wanadamu mara kwa mara, Anawakimu na kuwasaidia mara kwa mara, Akiwaruhusu wafuate njia ya Mungu ili waweze kupokea hatima nzuri ambayo Amewatayarishia. Inapokuja kwa Mungu, kile Anacho na alicho, neema Yake, rehema Yake, na thawabu Zake zote, zitatotelewa bila ya kusalia kwa wale wanaompenda na kumfuata Yeye. Lakini hajawahi kufichua kwa mtu yeyote maumivu aliyopitia Yeye au hali ya akili Yake, na katu halalamiki kuhusu yeyote ambaye hamtilii Yeye maanani au hajui mapenzi Yake. Anavumilia tu haya yote kimyakimya, Akisubiria siku ambayo mwanadamu ataweza kuelewa.

Kwa nini Nasema mambo haya hapa? Ni nini mnachoona kutoka kwa mambo haya Niliyosema? Kuna kitu katika kiini na tabia ya Mungu ambacho ni rahisi kupuuza, kitu ambacho kinamilikiwa na Mungu pekee na si mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na wale wengine wanaofikiri kuwa watu wakuu, watu wema, au Mungu wa mawazo yao. Kitu gani hiki? Ni kutokuwa na ubinafsi kwa Mungu. Tunapozungumza juu ya kutokuwa na ubinafsi, unaweza kufikiria wewe pia ni mtu asiye na ubinafsi, kwa sababu inapokuja kwa watoto wako, hautawahi kujadiliana nao na wewe ni mkarimu kwao, au unafikiri wewe pia hujitolea sana inapokuja kwa wazazi wako. Haijalishi unafikiria nini, angalau una dhana ya neno “kutokuwa na ubinafsi” na unalifikiria kama neno chanya, na kwamba kuwa mtu asiye na ubinafsi ni jambo la heshima sana. Wakati huna ubinafsi, unajiona wewe ni mkuu. Lakini hakuna anayeweza kuona kutojitolea kwa Mungu kati ya vitu vyote, miongoni mwa watu, matukio, na vitu, na kupitia kazi ya Mungu. Kwa nini ni hivyo? Kwa sababu mwanadamu ni mbinafsi sana! Kwa nini Ninasema hivyo? Mwanadamu anaishi katika ulimwengu yakinifu. Unaweza kumfuata Mungu, lakini huoni wala hufahamu jinsi ambavyo Mungu anakukimu, Anavyokupenda na Anavyoonyesha kwamba Anakujali. Kwa hivyo unaona nini? Unawaona watu wa ukoo wako wanaokupenda au kukujali sana. Unayaona mambo ambayo ni ya manufaa kwa mwili wako, unajali kuhusu watu na vitu unavyopenda. Huku ndiko kutokuwa na ubinafsi kwa binadamu kunakodaiwa. Watu kama hao “wasiokuwa na ubinafsi” hata hivyo, huwa hawajali kamwe kuhusu Mungu anayewapa uzima. Tofauti na ile ya Mungu, kutokuwa na ubinafsi kwa binadamu kunakuwa ubinafsi na kudharauliwa. Kutokuwa na ubinafsi ambako binadamu anaamini ndani yake, ni ule ulio mtupu na usio halisi, ulio na dosari, usiolingana na Mungu, na usiohusika na Mungu. Kutokuwa na ubinafsi kwa binadamu ni kwa ajili yake, huku kutokuwa na ubinafsi kwa Mungu ni ufunuo wa kweli wa kiini Chake. Ni kutokana na kutokuwa na ubinafsi kwa Mungu kwamba mwanadamu anapata mkondo thabiti wa msaada kutoka Kwake. Huenda usiathiriwe sana na mada hii Ninayozungumzia leo na unaweza kuwa tu unatikisa kichwa chako kwa kukubaliana na Mimi, lakini wakati unapojaribu kuuelewa moyo wa Mungu katika moyo wako, bila kujua utaweza kugundua hili: Miongoni mwa watu wote, masuala, na vitu utaweza kuhisi katika ulimwengu huu ni kutokuwa na ubinafsi tu kwa Mungu ambako ni kweli na thabiti, kwa sababu ni upendo wa Mungu tu kwako ndio ambao hauna masharti na hauna dosari. Mbali na Mungu, kutokuwa na kile kinachodaiwa kutokuwa na ubinafsi wa mtu mwingine yeyote ni kwa kujifanya, kwa juu juu, kuna hila; kuna madhumuni, nia fulani, kunabeba mabadilishano, na hakuwezi kusimama ili kupimwa. Unaweza hata kusema kwamba ni wenye uchafu na wa kudharauliwa. Je, unakubaliana na maneno haya?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 30)

Mungu Aufanya Upinde wa Mvua Kama Ishara ya Agano Lake na Mwanadamu

Mwa 9:11-13 Na nitaweka agano Langu na ninyi, wala miili yote haitaondolewa tena na maji ya gharika; wala hakutakuwa na gharika tena kuiharibu dunia. Naye Mungu akasema, Hii ni alama ya agano ambayo naifanya kati ya Mimi na ninyi na viumbe vyote vyenye uhai vilivyo nanyi, kwa vizazi vya kudumu: naweka upinde Wangu mawinguni, na utakuwa alama ya agano kati ya Mimi na dunia.

Mwishoni mwa hadithi ya Nuhu, tunaona kwamba Mungu alitumia mbinu isiyo ya kawaida kuelezea hisia Zake wakati huo. Mbinu hii ni maalumu sana, na ni kuweka agano na mwanadamu ambalo lilitangaza mwisho wa uharibifu wa Mungu wa ulimwengu kwa gharika. Kwa juu juu, kuweka agano kunaonekana kuwa jambo lililo la kawaida sana. Si jambo lolote zaidi ya kutumia maneno kufunga wahusika ili wasitende vitendo vitakavyokiuka agano, ili kusaidia kutimiza kusudio la kulinda maslahi ya pande zote mbili. Kwa nje, ni jambo la kawaida sana, lakini kutokana na motisha zilizopo na dhamira ya Mungu kufanya kitu hiki, ni ufunuo wa kweli wa tabia ya Mungu na hali Yake ya akili. Endapo utayaweka maneno haya kando na kuyapuuza, kama Sitawahi kukuambia ukweli wa mambo, basi binadamu hawatawahi kwa hakika kujua mawazo ya Mungu. Pengine katika kufikiria kwako Mungu alikuwa akitabasamu wakati Alipofanya agano hili, au pengine maonyesho Yake yalikuwa mazito, lakini haijalishi ni maonyesho gani ya kawaida kabisa ambayo watu wanafikiria Mungu alikuwa nayo, hakuna ambaye angeweza kuuona moyo wa Mungu au maumivu Yake, na hata upweke Wake. Hakuna mtu anayeweza kumfanya Mungu amwamini au anayestahili kuaminiwa na Mungu, au kuwa mtu Anayeweza kumweleza mawazo Yake au kuwa mwandani Wake wa kumwambia maumivu Yake. Ndiyo maana Mungu hakuwa na chaguo ila kufanya kitu kama hicho. Kwa juujuu, Mungu alifanya jambo rahisi la kuwaaga binadamu wale wa awali, kuhitimisha hali ya kale ilivyokuwa na kuleta mwisho kamili wa uharibifu Wake wa ulimwengu kwa gharika. Hata hivyo, Mungu alikuwa ameyazika maumivu kuanzia wakati huu ndani kabisa ya moyo Wake. Kwa wakati ambao Mungu hakuwa na yeyote wa kumwita mwandani, Alifanya agano na wanadamu, Akiwaambia kwamba Asingeuangamiza ulimwengu kwa gharika tena. Wakati upinde wa mvua unapojitokeza ni ili kuwakumbusha watu kwamba, kitu kama hicho kiliwahi kufanyika, ni ili kuwapa watu onyo dhidi ya kufanya maovu. Hata katika hali hiyo ya maumivu, Mungu hakusahau kuhusu wanadamu na bado Alionyesha kujali kwingi sana juu yao. Je, huu si upendo na kutokuwa na ubinafsi kwa Mungu? Lakini watu wanafikiria nini wakati wanapoteseka? Je, huu si wakati ambao wanamhitaji Mungu zaidi? Katika nyakati kama hizi, siku zote watu wanamkokota Mungu katika mambo yao ili Mungu aweze kuwapa faraja. Haijalishi ni lini, Mungu hatawahi kuwavunja moyo watu, na siku zote Atawaruhusu watu kutoka katika changamoto zao na kuishi katika mwangaza. Ingawa Mungu anawakimu wanadamu, ndani ya moyo wa mwanadamu, Mungu si chochote ila kidonge cha kutuliza, dawa ya tulizo. Wakati Mungu anateseka, wakati moyo Wake una majeraha, kuwa na kiumbe aliyeumba au mtu yeyote wa kuwa pamoja Naye au wa kumfariji Yeye, bila shaka kungekuwa ni tamanio la kupita kiasi kwa Mungu. Siku zote binadamu hatilii maanani hisia za Mungu, hivyo Mungu siku zote Haulizii wala Hatarajii kuwa kuna mtu anayeweza kumfariji Yeye. Anatumia mbinu Zake mwenyewe kueleza hali Yake. Watu hawafikirii kwamba ni jambo kubwa kwa Mungu kupitia mateso fulani, lakini unapojaribu tu kumwelewa Mungu kwa kweli, unapoweza kufahamu kwa dhati, nia nzuri za Mungu katika kila kitu Anachofanya, ndipo utakapoweza kuuhisi ukuu wa Mungu na kutokuwa na ubinafsi Kwake. Ingawa Mungu alifanya agano na wanadamu kwa kutumia upinde wa mvua, Hakuwahi kumwambia yeyote ni kwa nini Alifanya hivyo, ni kwa nini Alianzisha agano hili, kumaanisha kwamba Hakuwahi kumwambia mtu yeyote fikira Zake halisi. Hii ni kwa sababu hakuna mtu anayeweza kufahamu kina cha upendo ambao Mungu anao kwa wanadamu Aliowaumba kwa mikono Yake mwenyewe, na hakuna pia mtu anayeweza kutambua ni kiwango kipi cha maumivu ambayo moyo Wake uliteseka wakati Alipowaangamiza binadamu. Hivyo basi, hata kama Angewaambia watu jinsi Anavyohisi, wasingeweza kumwamini. Licha ya kuwa katika maumivu, bado Anaendelea na hatua inayofuata ya kazi Yake. Siku zote Mungu Anatoa upande Wake ulio bora zaidi na vitu bora zaidi kwa wanadamu wakati Yeye mwenyewe Akistahimili kimyakimya mateso yote. Mungu kamwe hafichui mateso haya. Badala yake, Anayavumilia na kusubiri kwa ukimya. Ustahimilivu wa Mungu si wa ukimya tu, usio na hisia, au usio na suluhu, wala si ishara ya unyonge. Ni kwamba upendo na kiini cha Mungu siku zote umekuwa usio na ubinafsi. Huu ni ufunuo wa kiasili wa kiini na tabia Yake na maonyesho halisi ya utambulisho wa Mungu kama Muumba wa kweli.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Iliyotangulia: Hatima na Matokeo

Inayofuata: Kumjua Mungu (II)

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp