Kumjua Mungu (I)

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 1)

Kila mmoja anapaswa kuchunguza maisha yake upya ya kumwamini Mungu ili kuona iwapo, katika mchakato wa kumfuata Mungu, ameelewa kwa dhati, amefahamu kwa dhati, na kuja kumjua Mungu kwa dhati, iwapo anajua kweli ni mawazo gani Mungu Anayo kwa aina tofauti za binadamu, na iwapo kweli anaelewa kile ambacho Mungu Anafanya juu yake na jinsi Mungu Anaeleza kila tendo lake. Huyu Mungu, Ambaye yuko kando yako, Akiongoza mwelekeo wa kuendelea kwako, Akiamuru hatima yako, na kukupa mahitaji yako—ni kiasi gani ambacho, katika uchambuzi wako, unaelewa nani kiasi gani ambacho kweli unajua kumhusu Yeye? Je, unajua Anachofanyia kazi kwako kila siku? Je, unajua kanuni na makusudi Anayozingatia katika matendo Yake yote? Unajua jinsi Anavyokuongoza? Unajua mbinu Anazotumia kukupa mahitaji yako? Unajua mbinu ambazo Anatumia kukuongoza? Je, unajua kile Anachotaka kupata kutoka kwako na kile Anachotaka kutimiza kwako? Je, unajua mtazamo Anaochukua katika namna nyingi ambazo unatenda? Unajua iwapo wewe ni mtu Anayependwa na Yeye? Unajua chanzo cha furaha, hasira, huzuni na uchangamfu Wake, fikira na dhana zinazohusiana na hayo, na kiini Chake? Unajua, hatimaye, huyu Mungu ni Mungu wa aina gani ambaye unamwamini? Je, maswali haya na mengine ya aina hii kitu ambacho hujawahi kuelewa ama kuwaza kuyahusu? Katika kufuata imani yako kwa Mungu, umewahi, katika ufahamu halisi na kuyatambua maneno ya Mungu, umeondoa hali za kutomwelewa? Je, baada ya kupokea adhabu na kurudi kwa Mungu, umefikia unyenyekevu halisi na kujali kwa kweli? Je, wakati wa kuadibu kwa Mungu na hukumu, umepata kutambua uasi na asili ya kishetani ya mwanadamu na kupata kiasi kidogo cha kuelewa kuhusu utakatifu wa Mungu? Je, chini ya uongozi na kupata nuru kwa maneno ya Mungu, umeanza kuwa na mtazamo mpya wa maisha? Katika majaribu yaliyotumwa na Mungu, umepata kuhisi kutovumilia Kwake makosa ya mwanadamu na pia kile Anachohitaji kutoka kwako na vile Anavyokuokoa? Iwapo hujui kutomwelewa Mungu ni nini, au jinsi ya kumaliza kutoelewa huku, basi mtu anaweza kusema hujawahi kuingia katika ushirika wa kweli na Mungu na hujawahi kumwelewa Mungu, ama angalau mtu anaweza kusema kuwa hujawahi kuwa na nia ya Kumwelewa. Iwapo hujui nidhamu ya Mungu na kuadibu ni nini, basi kwa hakika hujui kujiwasilisha na kujali ni nini, ama angalau hujawahi kujiwasilisha kwa Mungu kwa kweli au kumjali. Iwapo hujawahi kupitia kuadibu kwa Mungu na hukumu, basi kwa kweli hutajua utakatifu Wake ni nini, na utakuwa hata na ufahamu dhahiri kiasi kidogo kwa mintarafu ya uasi wa mwanadamu ni nini. Iwapo hujawahi kuwa na mtazamo sahihi wa maisha, au lengo sahihi katika maisha, bali bado uko katika hali ya mshangao na kutokuwa na uamuzi kuhusu njia yako ya maisha ya baadaye, hata kwa kiwango cha kusita kuenda mbele, basi ni dhahiri kuwa hujawahi kupokea nuru na uongozi wa Mungu, na mtu anaweza tu kusema kuwa hujawahi kupewa au kujazwa tena na maneno ya Mungu kwa kweli. Iwapo bado hujapitia majaribu ya Mungu, basi ni hakika kuwa bila shaka hutajua kutovumilia kwa Mungu makosa ya mwanadamu ni nini, wala hutaelewa kile ambacho Mungu Anahitaji hatimaye kutoka kwako, ama hata kidogo zaidi, hatimaye, kazi Yake ya kumsimamia na kumwokoa mwanadamu ni nini. Haijalishi ni kwa miaka mingapi mwanadamu ameamini katika Mungu, iwapo hajawahi kupitia ama kutambua chochote katika maneno ya Mungu, basi kwa hakika hatembei katika njia ya kuelekea wokovu, imani yake katika Mungu kwa hakika haina chochote, maarifa yake kumhusu Mungu pia kwa hakika ni sufuri, na ni hakika kuwa hana ufahamu wowote kuhusu ni nini kumcha Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 2)

Miliki na uwepo wa Mungu, kiini cha Mungu, tabia ya Mungu—yote yamewekwa wazi katika maneno Yake kwa binadamu. Anapopitia maneno ya Mungu, katika mchakato wa kuyatekeleza mwanadamu atapata kuelewa kusudi la maneno Anayonena Mungu, na kuelewa chemichemi na usuli wa maneno ya Mungu, na kuelewa na kufahamu matokeo yaliotarajiwa ya maneno ya Mungu. Kwa binadamu, haya ni mambo yote ambayo mwanadamu lazima ayapitie, ayatambue, na kuyafikia ili kuufikia ukweli na uzima, kutambua nia ya Mungu, kubadilishwa katika tabia yake, na kuweza kutii mamlaka ya Mungu na mipango. Katika wakati huo ambao mwanadamu anapitia, anafahamu, na kuvifikia vitu hivi, atakuwa kupata kumwelewa Mungu polepole, na katika wakati huu atakuwa pia amepata viwango tofauti vya ufahamu kumhusu Yeye. Kuelewa huku na maarifa havitoki katika kitu ambacho mwanadamu amefikiria ama kutengeneza, ila kutoka kwa kile ambacho anafahamu, anapitia, anahisi, na anashuhudia ndani yake mwenyewe. Ni baada tu ya kufahamu, kupitia, kuhisi, na kushuhudia vitu hivi ndipo ufahamu wa mwanadamu kumhusu Mungu utapata ujazo, ni maarifa anayopata katika wakati huu pekee ndio ulio halisi, wa kweli na sahihi, na mchakato huu—wa kupata kuelewa kwa kweli na ufahamu wa Mungu kwa kuelewa, uzoefu, kuhisi, na kushuhudia maneno Yake—sio kingine ila ushirika wa kweli kati ya mwanadamu na Mungu. Katikati ya aina hii ya ushirika, mwanadamu anakuja kuelewa kwa dhati na kufahamu nia za Mungu, anakuja kuelewa kwa dhati na kujua miliki na uwepo wa Mungu, anakuja na kuelewa kujua kwa kweli kiini cha Mungu, anakuja kuelewa na kujua tabia ya Mungu polepole, anafikia uhakika wa kweli kuhusu, na ufafanuzi sahihi wa, ukweli wa mamlaka ya Mungu juu ya vitu vyote vilivyoumbwa, na kupata mkondo kamili kwa na ufahamu wa utambulisho wa Mungu na nafasi Yake. Katika aina hii ya ushirika, mwanadamu anabadilika, hatua kwa hatua, mawazo yake kuhusu Mungu, bila kumwaza pasi na msingi, ama kuipa nafasi tashwishi yake kumhusu Yeye, ama kutomwelewa, ama kumshutumu, ama kupitisha hukumu Kwake, ama kuwa na shaka Naye. Kwa sababu hii, mwanadamu atakuwa na mijadala michache na Mungu, atakuwa na uhasama kiasi kidogo na Mungu, na kutakuwa na matukio machache ambapo atamuasi Mungu. Kwa upande mwingine, kujali kwa mwanadamu na utii kwa Mungu kutakua kwa kiasi kikubwa, na uchaji wake Mungu utakuwa wa kweli zaidi na pia mkubwa zaidi. Katika ya aina hii ya ushirika, mwanadamu hatapata kupewa ukweli pekee na ubatizo wa uzima, bali wakati uo huo pia atapata maarifa ya kweli ya Mungu. Katika aina hii ya ushirika, mwanadamu hatapata kubadilishwa kwa tabia yake na kupata wokovu pekee, bali pia kwa wakati huo atafikia uchaji na ibada ya kweli ya kiumbe aliyeumbwa kwa Mungu. Baada ya kuwa na aina hii ya ushirika, imani ya mwanadamu katika Mungu haitakuwa tena ukurasa tupu wa karatasi, ama ahadi ya maneno matupu, ama harakati na tamanio lisilo na lengo na kuabudu kama mungu; katika aina hii ya ushirika pekee ndio maisha ya mwanadamu yatakua kuelekea ukomavu siku baada ya siku, na ni wakati huu ndio tabia yake itabadilika polepole, na imani yake kwa Mungu, hatua kwa hatua, itatoka kwenye imani ya wasiwasi na kutoeleweka na imani isiyo ya hakika mpaka katika utii wa kweli na kujali, na kuwa katika uchaji Mungu wa kweli, na mwanadamu pia, katika mchakato wa kumfuata Mungu, ataendelea polepole kutoka kuwa mtazamaji na kuwa na hali ya utendaji, kutoka yule anayeshughulikwa na kuwa anayechukua nafasi ya kutenda; kwa aina hii ya ushirika pekee ndipo mwanadamu atafikia kuelewa kwa kweli na ufahamu wa Mungu, kwa ufahamu wa kweli wa Mungu. Kwa sababu watu wengi hawajawahi kuiingia katika ushirika wa kweli na Mungu, ufahamu wao wa Mungu unakomea kiwango cha nadharia, katika kiwango cha barua na kanuni. Hivyo ni kusema, watu wengi, haijalishi ni miaka mingapi wamemwamini Mungu, ikija kwa kumjua Mungu bado wako mahali walipoanzia, wamekwama katika msingi wa aina za heshima, na mitego yao ya hadhi na kabaila za kishirikina. Kwamba maarifa ya mwanadamu kumhusu Mungu yanapaswa kukomea yalipoanzia ina maana kwamba hayapo kabisa. Mbali na uthibitisho wa mwanadamu kuhusu nafasi ya Mungu na utambulisho, imani ya mwanadamu kwa Mungu bado iko katika hali ya kutoeleweka na kutokuwa na uhakika. Hii ikiwa hivyo, ni kiasi gani ambacho mwanadamu anaweza kuwa nacho kuhusu uchaji Mungu wa kweli?

Haijalishi kiwango cha imani yako katika uwepo Wake, hili haliwezi kuchukua mahali pa ufahamu wako wa Mungu, wala uchaji wako wa Mungu. Haijalishi kiwango ambacho umefurahia baraka Zake na neema Yake, hii haiwezi kuchukua nafasi ya ufahamu wako wa Mungu. Haijalishi ni kiwango gani unataka kuweka wakfu kila kitu chako na kugharimika kwa ajili Yake, hii haiwezi kuchukua nafasi ya maarifa yako kuhusu Mungu. Ama labda umeyazoea sana maneno ambayo Amenena mpaka unayajua kimoyomoyo na unaweza kuyasema upesi kinyumenyume; hata hivyo, hii haiwezi kuchukua nafasi ya maarifa yako kuhusu Mungu. Haijalishi kiwango cha dhamira ya mwanadamu katika kumfuata Mungu, iwapo hajawahi kuwa na ushirika wa kweli na Mungu, ama kuwa na uzoefu wa kweli wa maneno ya Mungu, basi ufahamu wake wa Mungu utakuwa utupu tu au ndoto isiyo na mwisho; kwa kuwa yote yale unaweza kuwa “umekumbana” na Mungu kwa kupita, au kukutana Naye uso kwa uso, ufahamu wako wa Mungu bado utakuwa sufuri, na uchaji wako wa Mungu utakuwa tu kidahizo ama njozi.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 3)

Watu wengi huyashika maneno ya Mungu kuyasoma siku baada ya siku, kiasi kwamba wanaviweka akilini vifungu vyote maarufu humo kama vitu vyao vyenye thamani zaidi, na zaidi kuyahubiri maneno ya Mungu kila mahali, wakiwatolea na kuwasaidia wengine kwa njia ya maneno Yake. Wanafikiri kuwa kufanya hivi ni kuwa na ushuhuda kwa Mungu, kuwa na ushuhuda kwa maneno Yake, kwamba kufanya hivi ni kufuata njia ya Mungu; wanafikiri kuwa kufanya hivi ni kuishi kulingana na maneno ya Mungu, kwamba kufanya hivi ni kuleta maneno Yake katika maisha yao halisi, kuwa kufanya hivi kutawawezesha kupokea pongezi ya Mungu, na kuokolewa na kukamilika. Lakini, hata wanapohubiri maneno ya Mungu, hawazingatii maneno ya Mungu katika matendo, ama kujaribu kujileta sambamba na yale yanayofichuliwa katika maneno ya Mungu. Badala yake, wanayatumia maneno ya Mungu kupata upendo na imani ya wengine kwa hila, kuingia katika usimamizi wao wenyewe, na kubadhiri na kuiba sifa za Mungu. Wanatarajia, kwa ubatili, kutumia nafasi waliyopata kwa kueneza maneno ya Mungu ili kupewa kazi ya Mungu na pongezi Yake. Miaka mingapi imepita, lakini hao watu hawajaweza tu kupata pongezi ya Mungu katika hatua ya kuyahubiri maneno ya Mungu, na hawajaweza tu kugundua njia ambayo wanafaa kufuata katika hatua ya kushuhudia maneno ya Mungu, na hawajajisaidia tu ama kujipatia wenyewe katika hatua ya kuwapa na kuwasaidia wengine kwa njia ya maneno ya Mungu, na hawajaweza tu kumjua Mungu, ama kuamsha ndani yao uchaji wa kweli wa Mungu, katika hatua ya kufanya haya yote; kwa upande mwingine, kutoelewa kwao kuhusu Mungu kunakuwa hata wenye kina zaidi, kutokuwa na imani kwao kwa Mungu kunazidi kuwa na mashaka, na mawazo yao kumhusu yanatiwa chumvi zaidi. Wakijazwa na kuongozwa na mawazo yao kuhusu maneno ya Mungu, wanaonekana kuwa katika haki yao kamili, kana kwamba wanapitia ujuzi wao bila juhudi, kana kwamba wamepata kusudi lao katika maisha, wito wao, na kana kwamba wameshinda maisha mapya na kuokolewa, kana kwamba, maneno ya Mungu yakibiringika kutoka kwenye ulimi kwa kukariri, wameupata ukweli, kushika nia za Mungu, na kugundua njia ya kumjua Mungu, kana kwamba, katika wakati wa kuhubiri maneno ya Mungu, wanakuja kila wakati uso kwa uso na Mungu, pia, wana “sukumwa” kila wakati mpaka kiwango cha kilio, na kila wakati kuongozwa na “Mungu” katika maneno ya Mungu, wanaonekana kushika bila kukoma wasiwasi Wake wenye ari na nia njema, na wakati uo huo kushika wokovu wa Mungu kwa mwanadamu na usimamizi Wake, kuja kujua kiini Chake, na kuelewa tabia Yake ya haki. Msingi huu ukizingatiwa, wanaoneka kuamini hata zaidi katika uwepo wa Mungu, kujua zaidi hali ya utukufu Wake, na kuhisi hata kwa kina zaidi ukuu Wake na kuvuka mipaka Kwake. Wakiwa wameinuka katika ufahamu wao wa kijuujuu wa maneno ya Mungu, itaonekana kuwa imani yao imekua, kuamua kwao kupitia mateso kumetiwa nguvu, na maarifa yao kwa Mungu yamekuwa na kina. Ila hawajui kwamba, hadi watakapopitia maneno ya Mungu kwa kweli, maarifa yao yote kuhusu Mungu na mawazo yao kumhusu Yeye yanatoka kwa mawazo yao wenyewe ya kufikiri kwa ubunifu na kukisia. Imani yao haiwezi kusimama jaribio lolote kutoka kwa Mungu, wanachoita kiroho na kimo haviwezi kusimama chini ya majaribu ya Mungu na ukaguzi, uamuzi wao ni ngome tu iliyojengwa juu ya changarawe, na wanachoita maarifa juu ya Mungu pia sio zaidi ya ubunifu wa mawazo yao. Kwa hakika, watu hawa, ambao, ilivyokuwa, wameweka juhudi kubwa katika maneno ya Mungu, hawajawahi kutambua imani ya kweli ni nini, kujiwasilisha kwa kweli ni nini, kujali kwa kweli ni nini, ama maarifa ya kweli ya Mungu ni nini. Wanachukua nadharia, mawazo, maarifa, zawadi, utamaduni, ushirikina na hata tabia nzuri za binadamu, na kuyafanya kuwa “mtaji na silaha” za kumwamini Mungu na ufuataji wao wa Mungu, hata kuyafanya kuwa misingi ya imani yao kwa Mungu na katika kumfuata Yeye. Wakati uo huo, pia wanachukua uwekezaji msingi huu na silaha na kuyafanya kuwa hirizi ya uchawi kwa kumjua Mungu, ya kukutana na kubishana na ukaguzi wa Mungu, majaribu, kuadibu, na hukumu. Mwishowe, wanachopata bado hakijumlishi chochote zaidi ya hitimisho kumhusu Mungu zinazoegemea hisia za kidini, katika kabaila za ushirikina, na kwa yote yaliyo ya kimapenzi, ya kustaajabisha, na yenye ugumu kuelewa, na njia yao ya kujua na kumweleza Mungu imepigwa muhuri katika muundo sawa na wa wale watu wanaoamini katika Mbingu iliyo Juu pekee, ama Mtu Mzee aliye Mawinguni, wakati ukweli wa Mungu, kiini Chake, tabia Zake, miliki Zake na asili, na kadhalika, yote yanayomhusu Mungu wa kweli Mwenyewe, ni vitu ambavyo kuvijua kumekosa mshiko, havina uhusiano kabisa na viko mbali kabisa. Katika njia hii, ingawa wanaishi chini ya upaji na ustawishaji wa maneno ya Mungu, hawawezi hata hivyo kutembea kwa kweli katika njia ya kumcha Mungu na kuepuka maovu. Sababu ya hakika ya hii ni kwamba hawajawahi kupata kujuana na Mungu, wala hawajawahi kuwa na mawasiliano ya kweli ama ushirika Naye, kwa hivyo haiwezekani kufikia maelewano ya pamoja na Mungu, ama kuamsha ndani mwao imani halisi katika, kufuata, ama ibada ya Mungu. Kwamba wanafaa kuyahusisha maneno ya Mungu, kwamba wanafaa kumhusisha Mungu—mwelekeo huu na tabia imewahukumu kurudi mkono mtupu kutoka kwa jitihada zao, imewahukumu katika maisha yote wasiweze kutembea katika njia ya kumcha Mungu na kuepuka maovu. Lengo wanalolengea, na mwelekeo wanaoelekea, inamaanisha kuwa ni maadui wa Mungu milele, na kwamba hata milele hawatawahi kuweza kupokea wokovu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 4)

Iwapo, katika tukio la mwanadamu ambaye amemfuata Mungu kwa miaka mingi na kufurahia kupewa maneno Yake kwa miaka mingi, ufafanuzi wake kuhusu Mungu ni, katika kiini chake, sawa na ule wa mtu anayejisujudu kwa heshima mbele ya sanamu, basi hii itamaanisha kuwa huyu mtu hajapata ukweli wa maneno ya Mungu. Kwa kutazama katika chanzo cha hii, mtu anaona kuwa tu hajaingia katika ukweli wa maneno ya Mungu, na kwa sababu hii hali halisi, ukweli, nia, na matarajio juu ya binadamu, yote ambayo yana asili kwa maneno ya Mungu, hayana uhusiano wowote na yeye. Hivyo ni kusema, haijalishi ni kiwango gani mwanadamu wa aina hii anaweza kufanya bidii katika maana ya juu ya maneno ya Mungu, yote ni bure: kwani yale anayofuata ni maneno tu, kwa hivyo yale atakayopata yatakuwa pia ni maneno tu. Haijalishi kama maneno yanayonenwa na Mungu ni makavu au makubwa katika mwonekano wa nje, yote ni ukweli ulio lazima kwa mwanadamu anapoingia katika uzima; ni chemichemi ya maji ya uzima yanayomwezesha kuishi katika roho na mwili. Yanatosheleza kile ambacho mwanadamu anahitaji ili awe hai; kanuni na imani ya kufanya maisha yake ya kila siku; njia, lengo, na mwelekeo ambao lazima apitie ili kupokea wokovu; kila ukweli ambao anapaswa awe nao kama kiumbe aliyeumbwa mbele za Mungu; na kila ukweli jinsi mwanadamu anavyotii na kumwabudu Mungu. Ni uhakika ambao unahakikisha kuishi kwa mwanadamu, ni mkate wa kila siku wa mwanadamu, na pia ni nguzo ya msaada inayowezesha mwanadamu kuwa na nguvu na kusimama. Yamejaa utajiri wa ukweli wa ubinadamu wa kawaida anavyoishi binadamu aliyeumbwa, yamejaa ukweli ambao mwanadamu anatumia kutoka kwa upotovu na kuepuka mitego ya Shetani, yamejaa mafunzo bila kuchoka, kuonya, kuhamasisha na furaha ambayo Muumba anampa binadamu aliyeumbwa. Ni ishara ambayo inawaongoza na kuwaelimisha wanadamu kuelewa yale yote yaliyo mazuri, hakika inayohakikisha kuwa wanadamu wataishi kwa kudhihirisha na kumiliki yale yote yaliyo ya haki na mema, kigezo ambacho watu, matukio, na vitu vyote vinapimwa, na pia alama ya usafiri inayowaongoza wanadamu kuelekea wokovu na njia ya mwanga. Katika uzoefu wa vitendo wa maneno ya Mungu tu ndipo mwanadamu anaweza kupewa ukweli na uzima; humu pekee ndimo anaweza kuja kupata kuelewa ubinadamu wa kawaida ni nini, maisha yenye umuhimu ni nini, kiumbe halisi ni nini, utiifu wa kweli kwa Mungu ni nini; humu pekee ndimo anaweza kuja kuelewa anavyofaa kumjali Mungu, jinsi ya kutimiza wajibu ya kiumbe aliyeumbwa, na jinsi ya kumiliki mfano wa mwanadamu wa kweli; humu tu ndimo anaweza kupata kuelewa maana ya imani halisi na ibada halisi; humu tu ndimo anaweza kuelewa nani ndiye Mtawala wa mbingu na nchi na vitu vyote; humu tu ndimo mwanadamu anaweza kuja kuelewa njia ambayo Yule ambaye ni Bwana wa uumbaji wote Anatawala, anaongoza, na kuutosheleza uumbaji; na hapa pekee ndipo anaweza kuja kuelewa na kushika njia ambayo Yule aliye Bwana wa uumbaji wote Anakuwa, Anadhihirishwa na kufanya kazi. Akitenganishwa na uzoefu wa kweli wa maneno ya Mungu, mwanadamu hana maarifa ya kweli ama ufahamu katika maneno ya Mungu na ukweli. Mwanadamu wa aina hii ni maiti inayoishi tu, ganda lililoisha, na ufahamu wote unaohusiana na Muumba hauna chochote kingine kumhusu. Katika macho ya Mungu, mwanadamu kama huyo hajawahi kumwamini, ama kuwahi kumfuata, na hivyo Mungu hamtambui yeye kama mwumini Wake wala mfuasi Wake, ama hata kama kiumbe halisi aliyeumbwa.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 5)

Ili kuwa kiumbe halisi aliyeumbwa, sharti ujue Muumba ni nani, uumbaji wa mwanadamu ni wa umuhimu gani, jinsi ya kutekeleza majukumu ya kiumbe, na jinsi ya kumwabudu Bwana wa uumbaji wote, lazima aelewe, ashike, ajue, na kujali kuhusu nia za Muumba, mapenzi Yake, na madai Yake, na lazima atende kulingana na njia ya Muumba—kumcha Mungu na kuepuka maovu.

Kumcha Mungu kuna maana gani? Na mtu anawezaje kuepuka maovu?

“Kumcha Mungu” hakumaanishi woga na hofu isiyotajika, wala kukwepa, wala kuweka umbali, wala si kuabudu kama mungu ama ushirikina. Ila, ni kutazama na kupendezwa, sifa, imani, kuelewa, kujali, kutii, kuweka wakfu, upendo, na pia ibada isiyo na vikwazo au malalamishi, malipo na kutii. Bila ya ufahamu halisi wa Mungu, binadamu hawatakuwa na kupendezwa halisi, imani halisi, kuelewa halisi, kujali halisi ama utiifu, ila tu hofu na kukosa utulivu, shaka pekee, kutoelewa, kukwepa, na kuepuka; bila maarifa halisi ya Mungu, binadamu hawatakuwa na utakatifu na malipo halisi; bila ufahamu halisi wa Mungu, binadamu hawatakuwa na ibada halisi na kujisalimisha, uabudu kama mungu upofu tu na ushirikina; bila maarifa halisi juu ya Mungu, binadamu hawawezi kutenda kulingana na njia ya Mungu, ama kumcha Mungu, ama kuepuka maovu. Badala yake, kila tendo na tabia ambayo mwanadamu anashiriki litajaa uasi na kutotii, na kumbukumbu zinazokashifu na hukumu ya usengenyaji kumhusu Yeye, na mienendo miovu inayokwenda kinyume na ukweli na maana ya kweli ya maneno ya Mungu.

Punde wanadamu wanapokuwa na imani ya kweli kwa Mungu, watakuwa wa kweli katika kumfuata Yeye na kumtegemea; kwa imani ya kweli pekee na tegemeo kwa Mungu ndipo binadamu watakuwa na kuelewa kwa kina na ufahamu; pamoja na ufahamu wa kweli wa Mungu inakuja kumjali Kwake kwa kweli; ni kwa kumjali Mungu kwa kweli pekee ndipo binadamu watakuwa na utiifu wa kweli kwa Mungu; na ni kwa utiifu wa Mungu kwa kweli pekee ndipo binadamu watakuwa na uwekaji wakfu wa kweli; na ni kwa uwekaji wakfu wa kweli kwa Mungu pekee ndipo binadamu watakuwa na malipo yasiyo na kiwango na kulalamika; ni kwa imani na msimamo wa kweli, kuelewa na kujali kwa kweli, utiifu wa kweli, utakatifu wa kweli na malipo, ndipo binadamu watakuja kujua kwa kweli tabia na kiini cha Mungu, na kujua utambulisho wa Muumba; Watakapopata kumjua Muumba ndipo binadamu wataamsha ndani yao ibada ya kweli na kujisalimisha; watakapokuwa na ibada ya kweli na kujisalimisha kwa Muumba tu ndipo binadamu wataweza kwa kweli kuweka kando njia zao za uovu, hivyo ni kusema, kuepuka maovu.

Hii inajumlisha hatua yote ya “kumcha Mungu na kuepuka maovu” na pia ni maudhui katika kumcha Mungu na kuepuka maovu kwa ujumla, na pia njia ambayo ni lazima kupitia ili kufikia kumcha Mungu na kuepuka maovu.

“Kumwogopa Mungu na kuepuka maovu” na kumjua Mungu ni uhusiano usiogawanyishwa na uliounganishwa kwa nyuzi zisizohesabika, na uhusiano kati yao ni dhahiri. Iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kuepuka maovu, lazima kwanza amche Mungu kwa kweli; iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kumcha Mungu kwa kweli, lazima awe na maarifa ya kweli kuhusu Mungu; Iwapo mtu anataka kupata maarifa ya Mungu, lazima kwanza ayapitie maneno ya Mungu, aingie katika ukweli wa maneno ya Mungu, apitie kuadibu na nidhamu ya Mungu, kuadibu Kwake na hukumu; iwapo mtu anataka kupitia maneno ya Mungu, lazima aje ana kwa ana na maneno ya Mungu, aje ana kwa ana na Mungu, na kumwomba Mungu Ampe fursa ya kupitia maneno ya Mungu katika hali ya aina yote ya mazingira inayowahusisha watu, matukio na vitu; iwapo mtu anataka kuja ana kwa ana na Mungu na maneno ya Mungu, lazima kwanza amiliki moyo wa kweli na mwaminifu, awe tayari kuukubali ukweli, kukubali kupitia mateso, uamuzi na ujasiri wa kuepuka uovu, na azimio la kuwa kiumbe halisi…Kwa njia hii, kuendelea mbele hatua kwa hatua, utamkaribia Mungu zaidi, moyo wako utakuwa safi zaidi, na maisha yako na thamani ya kuwa hai, pamoja na maarifa yako kumhusu Mungu, yatakuwa ya maana zaidi na yatakuwa hata ya kupevuka zaidi. Mpaka siku moja, utahisi kuwa Muumba sio fumbo tena, kwamba Muumba hajawahi kufichwa kutoka kwako, kwamba Muumba hajawahi kuificha sura Yake kutoka kwako, kwamba Muumba hayuko mbali na wewe hata kidogo, kwamba Muumba siye yule unayemtamania katika mawazo yako lakini kwamba huwezi kumfikia na hisia zako, kwamba Anasimama kwa kweli kama mlinzi kulia na kushoto kwako, Akiruzuku maisha yako, na kudhibiti majaliwa yako. Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho. Mungu kama huyo Anakukubali umpende kutoka moyoni, umshikilie, umweke karibu, umtamani, uhofu kumpoteza, na kutotaka kumkataa tena, kutomtii tena, ama kumwepuka tena ama kumweka mbali. Kile unachotaka ni kumjali tu, kumtii, kulipia kila kitu Anachokupa, na kujisalimisha katika himaya Yake. Hukatai tena kuongozwa, kupewa, kuangaliwa, na kuwekwa na Yeye, hukatai tena Anachoamuru na kukitawaza kwako. Unachotaka tu ni kumfuata, kutembea kando Yake katika kushoto ama kulia Kwake, kile utakacho ni kumkubali kama maisha yako ya pekee, kumkubali kama Bwana wako mmoja na wa pekee, Mungu wako mmoja na wa pekee.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 6)

Imani za Watu Haziwezi Kubadilishwa na Ukweli

Kunao baadhi ya watu wanaoweza kuvumilia ugumu; wanaweza kulipia bei; tabia yao ya nje ni nzuri sana; wanaheshimika sana; na wanatamaniwa na wengine. Mnafikiria nini: Je, tabia kama hii ya nje inaweza kuchukuliwa kama ya kutia ukweli katika matendo? Mnaweza kusema kwamba mtu huyu anatosheleza nia za Mungu? Kwa nini mara kwa mara watu wanamwona mtu wa aina hii na kufikiria kwamba wao wanamtosheleza Mungu, wanafikiria kwamba wanatembelea njia ile ya kutia ukweli katika matendo, kwamba wanatembea katika njia ya Mungu? Kwa nini baadhi ya watu hufikiria kwa njia hii? Upo ufafanuzi mmoja tu kwa haya. Na ufafanuzi huu ni upi? Sababu ni kwamba kwa kiasi kikubwa cha watu, maswali kama kutia ukweli katika matendo ni nini, kutosheleza Mungu ni nini, ni nini kuwa na uhalisia wa ukweli—maswali haya hayako wazi sana. Hivyo basi kunao baadhi ya watu ambao mara nyingi wanadanganywa na wale ambao kwa nje wanaonekana wa kiroho, wanaonekana wa kilodi, wanaonekana kuwa na taswira za ukuu. Kuhusiana na watu hao wanaoweza kuzungumzia barua na falsafa, na ambao hotuba na vitendo vyao vinaonekana kuwa vyenye kustahili uvutiwaji, wale wanaodanganywa nawao hawajawahi kuangalia kiini halisi cha vitendo vyao, kanuni zinazoendesha vitendo vyao, au shabaha zao ni nini. Na hawajawahi kuangalia kama watu hawa wanatii Mungu kwa kweli, na kama wao ni watu wanaomcha Mungu kwa kweli na kujiepusha na uovu au la. Hawajawahi kutambua kile kiini halisi cha ubinadamu cha watu hawa. Badala yake, kutoka kwenye hatua ya kwanza ya kujua na kuzoeana nao, hatua kwa hatua wanaanza kuwapenda watu hawa, kuwatukuza watu hawa, na hatimaye watu hawa wanakuwa sanamu zao. Aidha, katika akili za baadhi ya watu, sanamu hizi wanazoziabudu, wanaosadiki wanaweza kuacha familia na kazi zao, na kulipa ile bei kwa juujuu—sanamu hizi ndizo ambazo kwa kweli zinatosheleza Mungu, ndizo zile zinazoweza kupokea kwa kweli matokeo mazuri na hatima nzuri. Katika akili zao, sanamu hizi ndizo wale watu ambao Mungu husifu. Ni nini husababisha watu kuwa na aina hii ya kusadiki? Ni nini kiini halisi cha suala hili? Ni nini matokeo hali hii inaweza kuleta? Hebu na tuzungumzie kwanza suala la kiini chake halisi.

Masuala haya kuhusiana na mitazamo ya watu, vitendo vya watu, ni kanuni gani ambazo watu wanachagua kutenda, na kile ambacho kwa kawaida kila mtu anatilia mkazo, kimsingi haya yote hayahusu mahitaji ya Mungu kwa mwanadamu hata kidogo. Bila kujali kama watu wanazingatia masuala ya juujuu au yale ya kina, wanazingatia barua na falsafa au uhalisia, watu hawatii yale ambayo wanafaa kutii zaidi, na hawajui kile wanachofaa kujua zaidi. Sababu ya hali hii kuwa hivi ni kwamba watu hawaupendi ukweli kamwe. Hivyo basi, watu hawako radhi kutumia muda na jitihada zao katika kutafuta na kuendeleza kanuni katika neno la Mungu. Badala yake, wanapendelea kutumia njia za mkato, na kujumlisha kile wanachoelewa, kile wanachojua, kuwa vitendo vizuri na tabia nzuri. Muhtasari huu nao huwa shabaha yao ya binafsi ya kufuata, unakuwa ukweli wa kutendwa. Athari ya moja kwa moja ya haya yote ni kwamba watu wanatumia tabia nzuri ya kibinadamu kama kisawazisho cha kutia ukweli katika matendo yao, hali ambayo inatosheleza pia matamanio ya watu ili kupata fadhila na Mungu. Hii inawapa watu mtaji wa kushindania ukweli, ambao pia wao hutumia kutoa sababu na kushindana na Mungu. Wakati uo huo, watu wanamweka Mungu kando kwa njia za ufidhuli, na kuiweka ile sanamu ya mioyo yao katika nafasi ya Mungu. Kunayo sababu moja tu ya chanzo cha haya ambayo huwafanya watu kuwa na vitendo wasivyovijua, mitazamo wasiyoijua, au mitazamo na vitendo vya upande mmoja, na leo Nitawaelezea kuhusu haya. Sababu ni kwamba ingawa watu wengi wanaweza kumfuata Mungu, kumwomba Yeye kila siku, na kusoma neno la Mungu kila siku, hawaelewi kwa hakika nia za Mungu. Hiki ndicho chanzo cha tatizo. Kama mtu huelewa moyo wa Mungu, huelewa kile anachopenda Mungu, kile humchukiza Mungu, kile anachotaka Mungu, kile anachokataa Mungu, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu humpenda, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu hampendi, ni kiwango kipi ambacho Mungu hutumia katika kutoa mahitaji Yake kwa binadamu, ni mtazamo gani ambao Anauchukua katika kumfanya binadamu kuwa mtimilifu, je, mtu huyu anaweza bado kuwa na mawazo yake ya kibinafsi? Wanaweza tu kuenda na kumwabudu mtu mwingine? Mtu wa kawaida anaweza kuwa sanamu yao? Kama mtu anaelewa nia za Mungu, mtazamo wake ni wenye kirazini zaidi kuliko hapo. Hawatamwabudu kama Mungu kiongozi aliyepotoka kiholela, wala hawataweza, huku wakitembea njia ya kutia ukweli katika matendo, kusadiki kwamba kutii kiholela katika sheria au kanuni chache rahisi ni sawa na kutia ukweli katika matendo.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 7)

Kunayo Maoni Mengi Yanayohusu Kiwango Ambacho Mungu Hutumia Kuasisi Matokeo ya Binadamu

Kwa sababu kila mmoja anajali matokeo yake, je, mnajua namna ambavyo Mungu huamua matokeo hayo? Na ni kwa njia gani ambayo Mungu huanzisha matokeo ya mtu? Na ni kiwango gani ambacho Mungu hutumia kuasisi matokeo ya mtu? Na wakati ambapo matokeo ya mtu yangali bado hayajaasisiwa, ni nini anachofanya Mungu ili kufichua matokeo haya? Je, yupo anayejua haya? Kama Nilivyosema tu, kunao baadhi ambao tayari wamefanyia uchunguzi neno la Mungu kitambo sana. Watu hao wanatafuta dalili fulani kuhusu matokeo ya mwanadamu, kuhusu kategoria ambazo matokeo haya yamegawanywa, na kuhusu matokeo tofauti yanayosubiria aina tofauti ya watu. Wanataka pia kujua namna neno la Mungu linavyoanzisha matokeo ya binadamu, aina za kiwango ambacho Mungu hutumia, na njia ambayo Yeye huasisi matokeo ya binadamu. Ilhali mwishowe watu hawa hawafanikiwi kupata chochote. Kwa hakika, yapo mambo machache yenye thamani yanayozungumzwa kuhusu suala hili miongoni mwa neno la Mungu. Kwa nini hali iko hivi? Ili mradi matokeo ya binadamu yangali hayajafichuliwa, Mungu hataki kumwambia yeyote kuhusu kile kitakachofanyika mwishowe, wala Hataki kumfahamisha yeyote kuhusu hatima yao kabla ya wakati kufika. Sababu ya kufanya hivi ni kwamba Mungu kufanya hivyo hakutaleta manufaa yoyote kwa binadamu. Sasa hivi, Nataka kuwaambia tu kuhusu namna Mungu huasisi matokeo ya binadamu, kuhusu kanuni Anazotumia katika kazi Yake ili kuyaasisi matokeo ya binadamu, na kuonyesha matokeo haya, pamoja na kiwango Anachotumia ili kuanzisha kama mtu ataweza kuishi au la. Hiki sicho kile ambacho mnajali zaidi kuhusu? Hivyo basi, ni vipi ambavyo watu hufahamu njia ambayo Mungu anaanzisha matokeo ya binadamu? Mlizungumzia kidogo kuhusu suala hili muda mfupi uliopita. Baadhi yenu mlisema kwamba ni swali la kutenda wajibu wao kwa uaminifu, kugharamika kwa ajili ya Mungu; baadhi ya watu walisema kumtii Mungu na kutosheleza Mungu; baadhi ya watu walisema kudhibitiwa na Mungu; na baadhi ya watu walisema kuishi maisha ya hadhi ya chini…. Wakati mnapotia ukweli huu katika matendo, wakati mnapotenda kanuni za kufikiria kwenu, je mnajua kile Mungu anachofikiria? Mmewahi kufikiria kama kuendelea hivi ni kutosheleza nia za Mungu au la? Kama kunatilia maanani kiwango cha Mungu? Kama kunatilia maanani mahitaji ya Mungu? Ninasadiki kwamba watu wengi zaidi hawalifikirii suala hili kwa undani. Wanatumia tu bila kutilia maanani sehemu ya neno la Mungu, au sehemu ya mahubiri, au viwango vya watu fulani wa kiroho ambao wanawaabudu, na kujilazimisha kufanya hivi na vile. Wanasadiki kwamba hii ndiyo njia sahihi, na hivyo basi wanaendelea kuitii, kuifanya, liwalo liwe hatimaye. Baadhi ya watu hufikiria: “Nimesadiki kwa miaka mingi siku zote nimetenda mambo kwa njia hii; nahisi kuwa nimemtosheleza kabisa Mungu; ninahisi pia kuwa nimejifunza mengi kutoka kwa haya. Kwani nimekwishaelewa ukweli mwingi katika kipindi hiki, na nimeelewa mambo mengi ambayo sikuyaelewa awali—hasa, wingi wa fikira na mitazamo yangu imebadilika, maadili ya maisha yangu yamebadilika sana, na ninao uelewa mzuri sana wa ulimwengu huu.” Watu kama hao wanasadiki kwamba haya ni mavuno, na ndiyo matokeo ya mwisho ya kazi ya Mungu kwa binadamu. Kwa maoni yenu, kwa viwango hivi na vitendo vyenu nyote vimewekwa pamoja—je, mnatosheleza nia za Mungu? Baadhi ya watu watasema kwa uhakika wote: “Bila shaka! Tunatenda kulingana na neno la Mungu; tunatenda kulingana na kile ambacho yule aliye juu alihubiri na kushiriki nasi; siku zote tunafanya wajibu wetu, siku zote tunamfuata Mungu, hatujawahi kumwacha Mungu. Hivyo basi tunaweza kusema kwa imani kamili kwamba tunamtosheleza Mungu. Haijalishi ni kiasi kipi tunachoelewa kuhusu nia za Mungu, haijalishi ni vipi tunavyoelewa neno la Mungu, siku zote tumekuwa kwa njia ya kutafuta kuweza kutangamana na Mungu. Kama tutachukua hatua kwa usahihi, na kutenda kwa usahihi, basi matokeo yatakuwa sahihi.” Je, mnafikiria nini kuhusu mtazamo huu? Je, ni kweli? Pengine wapo wale wanaosema: “Sijawahi kufikiria kuhusu mambo haya awali. Mimi nafikiria tu kwamba nikiendelea kutimiza wajibu wangu na kuendelea kutenda kulingana na mahitaji ya neno la Mungu, basi nitasalia. Sijawahi kufikiria swali la kama ninaweza kutosheleza moyo wa Mungu, na sijawahi kufikiria kama ninatimiza kiwango kinachohitajika na Yeye. Kwa sababu Mungu hajawahi kuniambia, wala kunipatia maagizo yoyote kwa uwazi, ninasadiki kwamba mradi tu niendelee kupiga hatua mbele, Mungu atatosheka na Yeye hafai kuwa na mahitaji yoyote ya ziada kwangu mimi.” Je, kusadiki huku ni sahihi? Kulingana na Ninavyojua, njia hii ya kutenda, njia hii ya kufikiria, na mitazamo hii—yote yanakuja na madoido fulani na kiasi kidogo cha upofu. Ninaposema hivi, pengine wapo baadhi yenu mnaohisi kuvunjika moyo: “Yaani upofu? Kama ni ‘upofu,’ basi tumaini letu la wokovu, tumaini letu la kuishini dogo mno, na halina uhakika, hapo ni kweli? Je, wewe kulitamka hivyo lilivyo si sawa na kutumwagilia maji baridi?” Haijalishi kile mnachosadiki, mambo Ninayoyasema na kufanya hayanuii kukufanya ninyi kuhisi kama mnamwagiliwa maji baridi. Badala yake, yananuia kuboresha uelewa wenu wa nia za Mungu, na kuboresha ung’amuzi wenu kuhusu kile ambacho Mungu anafikiria, kile ambacho Mungu anataka kukamilisha ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anapenda, nini kinachukiza Mungu, nini Mungu anadharau, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anataka kumpata, na ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anatupilia mbali. Yananuia kupatia akili zenu uwazi, kuwasaidia kujua wazi ni kiwango kipi vitendo na fikira za kila mmoja wenu yamepotea kutoka kwa kiwango kinachohitajika na Mungu. Je, inahitajika kuzungumzia mada hii? Kwa sababu Ninajua mmesadiki kwa muda mrefu, na mmesikiliza mahubiri mengi, lakini kwa hakika haya ndiyo mambo yanayokosekana zaidi. Mmerekodi kila ukweli katika daftari zenu, mmerekodi pia kile ambacho nyie wenyewe mnasadiki kibinafsi kuwa muhimu katika akili zenu na ingawa mnapanga kutumia haya kumridhisha Mungu wakati wa kutenda kwenu, kuyatumia mnapojipata mkihitaji msaada, kuyatumia kupitia nyakati ngumu zilizo mbele yenu, au mnaacha ukweli huu uandamane na ninyi mnapoishi maisha yenu tu. Lakini kulingana na Ninavyojua, iwapo mnatenda tu, namna mnavyotenda hasa si muhimu. Nini, basi, ndicho kitu cha muhimu sana? Ni kwamba wakati unatenda, moyo wako hujua kwa uhakika wote kama kila kitu unachofanya, kila kitendo, ndicho kile anachotaka Mungu au la; kama kila kitu unachofanya ni sahihi au la, kila kitu unachofikiria ni sahihi au la, na matokeo na shabaha katika moyo wako yanatosheleza nia za Mungu au la, kama yanatilia maanani mahitaji ya Mungu au la, na kama Mungu anayaidhinisha au la. Haya ni mambo muhimu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 8)

Tembea katika Njia ya Mungu: Mche Mungu na Kuepuka Maovu

Kunao msemo ambao mnafaa kutilia maanani. Ninasadiki msemo huu ni muhimu sana, kwa sababu kwangu Mimi unakuja akilini mara nyingi kila siku. Kwa nini hivyo? Kwa sababu kila wakati Ninapokumbana na mtu, kila wakati Ninaposikia hadithi ya mtu, kila wakati Ninaposikia kile alichopitia mtu au ushuhuda wake wa kusadiki Mungu, siku zote Ninatumia msemo huu kuweza kupima kama mtu huyu binafsi ni mtu wa aina ambayo Mungu anataka au la, mtu wa aina ambayo Mungu anapenda. Hivyo msemo huu ni upi, basi? Sasa nyinyi nyote mnasubiri kwa hamu. Nitakapoufichua msemo huu, pengine mtakasirika kwa sababu wapo baadhi yenu ambao mmekuwa mkijifanya kuwa mnakubaliana nao kwa miaka mingi. Lakini Kwangu Mimi, Sijawahi kujifanya kuwa nakubaliana nao. Msemo huu umo moyoni Mwangu. Hivyo basi msemo huu ni upi? Msemo ni “tembea katika njia ya Mungu: mche Mungu na kuepuka maovu.” Je, huoni kwamba kauli hii ni rahisi kupindukia? Ilhali ingawa msemo huu unaweza kuwa rahisi, mtu ambaye anao uelewa wa ndani na wa kweli wa msemo huu atahisi kwamba ni wenye uzito mkubwa; kwamba unao thamani nyingi ya kutenda; kwamba ni lugha ya uzima iliyo na uhalisia wa ukweli; ambayo ni lengo la maishani katika kulenga wale wanaotafuta kutosheleza Mungu; na hiyo ni njia ya maisha marefu itakayofuatwa na mtu yeyote anayejali nia za Mungu. Hivyo basi mnafikiria nini: Je, msemo huu sio ukweli? Je, unao umuhimu kama huo au la? Pia, pengine baadhi yenu mnafikiria kuhusu msemo huu, wakijaribu kuuelewa, na wapo baadhi ambao bado wanautilia shaka. Je, msemo huu ni muhimu sana? Je, ni muhimu sana? Unahitajika sana na unastahili kutiliwa mkazo? Pengine wapo baadhi ya watu ambao hawapendi sana msemo huu kwa sababu wanafikiria kwamba kuchukua njia ya Mungu na kuitiririsha ndani ya msemo huu mmoja ni urahisishaji wa kupindukia. Kuyachukua yale yote ambayo Mungu alisema na kuyafanya yawe msemo mmoja—je, hivi si kumfanya Mungu kuwa yule asiyekuwa na umuhimu sana? Hivi ndivyo ilivyo? Inaweza kuwa kwamba wengi wenu nyinyi hamwelewi kabisa maana kuu ya maneno haya. Ingawa mmeyanakili na kuyatilia maanani, hamnuii kuuweka msemo huu katika mioyo yenu; mnaunakili tu katika vitabu vyenu, na kuudurusu tu, na kuufikiri katika muda wenu wa ziada. Wapo baadhi ya watu ambao hata hawatashughulika kuutia kwenye kumbukumbu msemo huu, sikuambii hata kujaribu kuutumia vizuri. Lakini kwa nini Nikauzungumzia msemo huu? Licha ya mtazamo wenu, au kile mtakachofikiria, lazima Nizungumzie msemo huu kwa sababu unafaa ajabu namna ambavyo Mungu huasisi matokeo ya binadamu. Bila kujali kama uelewa wenu wa sasa wa msemo huu upo, namna mnavyouchukulia, bado Nitawaeleza: kama watu wanaweza kuyaweka maneno ya msemo huu katika vitendo na kuyapitia, na kutimiza kiwango cha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, basi atahakikishiwa kuishi kisha atahakikishiwa kuwa mtu mwenye matokeo mazuri. Kama huwezi kutimiza kiwango kilichowekwa wazi katika msemo huu, basi inaweza kusemekana kwamba matokeo yako hayajulikani. Hivyo basi Ninaongea kwenu kuhusu msemo huu kwa matayarisho yenu ya kiakili, na ili mjue ni kiwango aina gani ambacho Mungu anatumia kuwapima.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 9)

Mungu Hutumia Majaribio Tofauti ili Kupima Kama Watu Humcha Mungu na Kujiepusha na Maovu

Katika kila enzi, Mungu huwapa binadamu baadhi ya maneno Anapofanya kazi ulimwenguni, huku akimwambia mwanadamu kuhusu baadhi ya ukweli. Ukweli huu unahudumu kama njia ambayo binadamu anafaa kuitii, njia ya kutembelewa na binadamu, njia ambayo humwezesha binadamu kumcha Mungu na kujiepusha na uovu, na njia ambayo watu wanafaa kuweka katika vitendo na kuitii katika maisha yao na kwenye mkondo wa safari zao za maisha. Ni kwa sababu hizi ambapo Mungu anampa binadamu maneno haya. Binadamu anafaa kuyatii maneno haya yanayotoka kwa Mungu, na kuyatii ni kupokea uzima. Kama mtu hataweza kuyatii, na hayatii kwenye matendo, na haishi kwa kudhihirisha maneno ya Mungu katika maisha yake, basi mtu huyo hautilii ukweli katika matendo. Na kama hawatilii ukweli katika matendo, basi hawamchi Mungu na hawaepuki uovu, wala hawawezi kumtosheleza Mungu. Kama mtu hawezi kumtosheleza Mungu, basi hawezi kupokea sifa ya Mungu; mtu wa aina hii hana matokeo. Hivyo basi ni vipi katika mkondo wa kazi ya Mungu ndipo Anapoasisi matokeo ya mtu? Ni mbinu gani anayoitumia Mungu kuasisi matokeo ya binadamu? Pengine nyinyi hamlielewi suala hili sasa hivi, lakini Nitakapowaambia mchakato jambo hili litakuwa wazi kabisa. Hii ni kwa sababu watu wengi tayari wamelipitia suala hili wenyewe.

Katika mkondo wa kazi ya Mungu, kuanzia mwanzo hadi sasa, Mungu Amepanga majaribio kwa kila mtu—au mnaweza kusema, kila mtu anayemfuata Yeye—na majaribio haya yanakuja kwa ukubwa tofauti. Wapo wale ambao wamepitia jaribio la kukataliwa na familia zao; wapo wale ambao wamepitia jaribio la mazingira mabovu; wapo wale ambao wamepitia majaribio ya kukamatwa na kuteswa; wapo wale ambao wamepitia majaribio ya kukumbwa na chaguo; na wapo wale ambao wamekumbwa na majaribio ya pesa na hadhi. Nikizungumza kwa ujumla, kila moja wenu amekabiliwa na aina zote za majaribio. Kwa nini Mungu anafanya kazi hivyo? Kwa nini Mungu Anamtenda hivi kila mtu? Ni matokeo aina gani Anayotaka kuyaona? Hii ndiyo hoja muhimu kuhusu kile Ninachotaka kuwaambia: Mungu anataka kuona kama mtu huyu ni yule anayemcha Mungu na kujiepusha na uovu. Maana ya haya ni kwamba wakati Mungu anakupa jaribio, na kukufanya kukabiliwa na baadhi ya hali, Anataka kukupima na kujua kama wewe ndiye yule mtu anayemcha Mungu, mtu huyo anayejiepusha na uovu au la. Kama mtu amekumbwa na wajibu wa kutunza sadaka, na anakutana na sadaka ya Mungu, basi unadhani kwamba hiki ni kitu ambacho Mungu amepanga? Bila shaka! Kila kitu unachokumbana nacho ni kitu ambacho Mungu amepanga. Unapokumbwa na suala hili, Mungu atakuangalia kwa siri, namna ulivyochagua, namna unavyotenda, na kile unachofikiria. Matokeo yake ya mwisho ndiyo ambayo Mungu anayajali zaidi, sababu ni matokeo ambayo yatamruhusu Yeye kupima kama umetimiza kiwango cha Mungu katika jaribio hilo au la. Hata hivyo, wakati watu wanapokumbwa na baadhi ya masuala haya, mara nyingi hawafikirii kuhusu ni kwa nini wanakumbwa na mambo hayo, au kile kiwango ambacho kinahitajika na Mungu. Hawafikirii kuhusu kile Mungu anachotaka kutoka kwao, kile Anachotaka kupata kutoka kwao. Wakati wanapokumbwa na suala hili, mtu wa aina hii anafikiria tu: “Hili ni jambo ambalo nimekumbwa nalo; lazima niwe makinifu, wala si mzembe! Haijalishi ni nini, hii ni sadaka ya Mungu na siwezi kuigusa.” Mtu huyo anasadiki kwamba anaweza kutimiza jukumu lake kupitia kufikiria huko sahili. Je, Mungu ataweza kutosheka na matokeo ya jaribio hili? Au Hatatosheka? Mnaweza kuzungumzia suala hili. (Kama mtu anamcha Mungu katika moyo wake, kisha anapokumbwa na wajibu unaomruhusu kukutana na sadaka ya Mungu, anaweza kufikiria namna ilivyo rahisi kukosea tabia ya Mungu, ili wawe na hakika ya kuendelea kwa tahadhari.) Mwitikio wako u katika njia sahihi, lakini bado haujafika. Kutembea katika njia ya Mungu hakuhusu kuangalia sheria juujuu. Badala yake, kunamaanisha kwamba unapokabiliwa na suala, kwanza kabisa, unaliangalia kama ni hali ambayo imepangwa na Mungu, wajibu uliopewa wewe na Yeye, au kitu ambacho Amekuaminia wewe, na kwamba unapokabiliana na suala hili, unapaswa kuliona kama jaribio kutoka kwa Mungu. Wakati unapokabiliwa na suala hili, lazima uwe na kiwango, lazima ufikirie kwamba suala hilo limetoka kwa Mungu. Lazima ufikirie ni vipi ambavyo utashughulikia suala hili kiasi cha kwamba unaweza kutimiza wajibu wako, na kuwa mwaminifu kwa Mungu; namna ya kulifanya bila ya kumghadhabisha Mungu; au kukosea tabia Yake. Tumetoka tu kuzungumzia kutunza sadaka. Swala hili linahusu sadaka, na linahusisha pia wajibu wako, jukumu lako. Unahitajika kuwajibikia jukumu hili. Ilhali unapokabiliwa na suala hili, kunalo jaribio lolote? Lipo! Jaribio hilo linatoka wapi? Jaribio hilo linatoka kwa Shetani, na linatoka pia kwa tabia potovu na ya uovu ya binadamu. Kwa sababu kunalo jaribio, hili linahusisha kuwa shahidi; kuwa shahidi ni jukumu na wajibu wako pia. Baadhi ya watu husema: “Hili ni suala dogo; kwa kweli linahitajika kulifanya suala hili dogo kuwa kubwa hivyo?” Ndiyo pana haja! Kwa sababu ili kutembea katika njia ya Mungu, hatuwezi kuwachilia chochote kinachotuhusu sisi wenyewe, au kinachofanyika karibu nasi, hata yale mambo madogo madogo. Haijalishi kama tunafikiria tunafaa kumakinika au la, mradi tu suala lolote linatukabili hatufai kuliacha. Lote linafaa kuonekana kama jaribio la Mungu kwetu. Mwelekeo aina hii uko vipi? Kama unao mwelekeo aina hii, basi unathibitisha hoja moja: Moyo wako unamcha Mungu, na moyo wako uko radhi kujiepusha na maovu. Kama unalo tamanio hili la kumtosheleza Mungu, basi kile unachotia katika matendo hakiko mbali na kiwango cha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kunao mara nyingi wale wanaosadiki kwamba masuala ambayo hayatiliwi maanani na watu, masuala ambayo kwa kawaida hayatajwi—haya ni mambo madogo tu, na hayana chochote kuhusiana na kutia ukweli katika matendo. Wakati watu hawa wanakabiliwa na suala kama hilo, hawalifikirii sana na wanaliachilia tu. Lakini ukweli wa mambo ni kwamba, suala hili ni funzo ambalo unafaa kulidadisi, funzo kuhusu namna ya kumcha Mungu, namna ya kujiepusha na maovu. Zaidi, kile unachofaa kujali hata zaidi ni kujua kile Mungu anachofanya wakati suala hili linapoibuka kukabiliana na wewe. Mungu yuko kando yako, anaangalia kila mojawapo ya maneno na vitendo vyako, anaangalia hatua zako, mabadiliko ya akili zako—hii ni kazi ya Mungu. Baadhi ya watu husema: “Basi kwa nini siihisi?” Huihisi kwa sababu namna ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu haijawa ndiyo njia muhimu zaidi kwako kushughulikiwa. Hivyo basi, huwezi kuhisi kazi ngumu ya Mungu katika binadamu, inayojionyesha kulingana na fikira tofauti na vitendo tofauti vya watu. Wewe u makini! Suala kubwa ni lipi? Swala dogo ni lipi? Masuala yote yanayohusu kutembea katika njia ya Mungu hayagawanywi kwa masuala makubwa au madogo. Mnaweza kulikubali hilo? (Tunaweza kulikubali.) Kuhusiana na masuala ya kila siku, kunayo yale ambayo watu wanayaona kuwa makubwa sana na muhimu, na mengine yanaonekana kuwa mambo madogo madogo tu. Mara nyingi watu huyaona masuala haya makubwa kuwa ndiyo muhimu zaidi, na wanayachukulia kwamba yametumwa na Mungu. Hata hivyo, kwenye mkondo wa masuala haya makubwa kujitokeza, kutokana na kimo finyu cha binadamu, na kutokana na kiwango cha binadamu kisichotosha, mara nyingi binadamu haendani sawa na nia za Mungu, hawezi kupata ufunuo wowote, na hawezi kufaidi maarifa yoyote halisi yenye thamani. Kuhusu masuala madogo, haya yanapuuzwa tu na binadamu, kuachwa kuponyoka kidogokidogo. Hivyo basi, wamepoteza fursa nyingi sana za kuchunguzwa mbele ya Mungu, kujaribiwa na Yeye. Je unafaa kuwapuuza watu, masuala na hali hizi siku zote ambazo Mungu anakupangilia wewe, hii itamaanisha nini? Inamaanisha kwamba kila siku, hata kila wakati, siku zote unakana ukamilifu wa Mungu kwako, na uongozi wa Mungu. Kila Mungu anapopanga hali hizi kwako wewe, Yeye anakuangalia kwa siri, Anauangalia moyo wako, Anaziangalia fikira na hali zako, Anaangalia namna unavyofikiria wewe, Anaangalia namna unavyochukua hatua. Kama wewe ni mtu asiyejali—mtu ambaye hajawahi kujali kuhusu njia ya Mungu, neno la Mungu, au ukweli—basi hutajali, hutatilia maanani kile ambacho Mungu anataka kukamilisha, na yale ambayo Mungu anakuhitaji wewe kufanya wakati Anapopanga hali hizi kwako wewe. Hutajua pia namna ambavyo masuala haya ya kila siku yanavyohusiana na ukweli au nia za Mungu. Baada ya kukabiliana na hali nyingi kama hizi na majaribio mengi kama haya, huku naye Mungu haoni mafanikio yoyote kutokana na wewe, ataweza kuendelea vipi? Baada ya kukabiliwa na majaribio mara kwa mara, humkuzi Mungu katika moyo wako, na hushughulikii zile hali ambazo Mungu anakupangia wewe kama zilivyo—kama majaribio ya Mungu au mitihani ya Mungu. Badala yake unakataa fursa ambazo Mungu amekupa wewe moja baada ya nyingine, na unaziacha kutokomea mara kwa mara. Je huu si kutotii kwa kiwango cha juu na binadamu? (Naam, ni kutotii.) Je, Mungu atahuzunika kwa sababu ya haya? (Naam Atahuzunika.) Mungu hatahuzunika! Mkinisikia Nikiongea hivi mnashtuka kwa mara nyingine tena. Kwani umesahau, ilisemekana hapo awali kwamba Mungu huhuzunika siku zote? Mungu hatahuzunika? Ni lini basi Mungu atahuzunika? Usijali, Mungu hatahuzunika na hali hii. Basi mwelekeo wa Mungu kwa aina hii ya tabia iliyoelezwa kwa muhtasari hapo juu ni upi? Wakati watu wanapokataa majaribio, mitihani, ambayo Mungu anawapa, wakati wanapoikwepa, kunao mwelekeo mmoja tu ambao Mungu anao kwa watu kama hawa. Mwelekeo huu ni upi? Mungu husukumia mbali aina hii ya watu kutoka kina cha moyo Wake. Kunazo safu mbili za maana ya kauli “sukumia mbali”. Ninawezaje kuzielezea? Ndani kabisa ya moyo, kauli hii inao mkazo wa kuchukiza, wa chuki Na je, safu ya pili ya maana? Sasa hiyo ndiyo sehemu inayoashiria kukata tamaa dhidi ya kitu. Nyote mnajua “kukata tamaa” kunamaanisha nini, ni kweli? Kwa ufupi, kusukumia mbali kunamaanisha uamuzi na mwelekeo wa mwisho wa Mungu kwa watu wanaokuwa na mwenendo huu. Ni chuki ya kupindukia dhidi yao, maudhi, na hivyo basi uamuzi wa kuwaacha. Huu ndio uamuzi wa mwisho wa Mungu kwa mtu ambaye hajawahi kutembea katika njia ya Mungu, ambaye hajawahi kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Je, nyote mnaweza kuona sasa umuhimu wa msemo huu Niliouzungumzia?

Sasa mnaelewa mbinu ambayo Mungu hutumia kuasisi matokeo kwa binadamu? (Kupanga hali tofauti kila siku.) Kupangilia hali tofauti—hivi ndivyo watu wanavyoweza kuhisi na kugusa. Basi nia ya Mungu kwa haya yote ni nini? Nia ni kwamba Mungu anataka kumpa kila mmoja wetu majaribio katika njia tofauti, katika nyakati tofauti, na katika sehemu tofauti. Ni dhana zipi za binadamu zinazopimwa katika jaribio? Haijalishi kama wewe ni mtu wa aina ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu katika kila suala unalokabiliwa nalo, unalosikia kuhusu, unaloliona, na unalolipitia wewe binafsi au la. Kila mmoja atakabiliwa na aina ya jaribio, kwa sababu Mungu ni mwenye haki kwa watu wote. Baadhi ya watu husema: “Nimesadiki Mungu kwa miaka mingi; inakuaje kwamba sijawahi kabiliwa na jaribio?” Unahisi hujakabiliwa na jaribio kwa sababu kila wakati Mungu amepanga hali kwako wewe, hujazichukulia hali hizo kwa umakinifu, na hujataka kutembea kwa njia ya Mungu. Hivyo basi huna kamwe hisia zozote za majaribio ya Mungu. Baadhi ya watu husema: “Nimekabiliwa na majaribio machache, lakini sijui njia bora ya kufanya mazoezi. Hata ingawa nilitenda, bado sijajua kama nilisimama imara wakati huo wa majaribio.” Watu walio na aina hii ya hali bila shaka hawamo katika kundi la walio wachache. Hivyo basi ni nini kiwango ambacho Mungu hupimia watu? Ni vile tu Nilivyosema muda mfupi uliopita: Kila kitu unachofanya, kila kitu unachofikiria, na kila kitu unachoelezea—ni kumcha Mungu na kujiepusha na uovu? Hivi ndivyo inavyobainika kama wewe ni mtu unayemcha Mungu na kujiepusha na maovu au la. Hii ni dhana rahisi? Ni rahisi mno kusema, lakini ni rahisi pia kutia katika matendo? (Si rahisi mno.) Kwa nini si rahisi mno? (Kwa sababu watu hawamjui Mungu, hawajui namna ambavyo Mungu humfanya binadamu kuwa mtimilifu, na hivyo basi wanapokabiliwa na masuala hawajui namna ya kutafuta ukweli ili kutatua tatizo lao; watu lazima wapitie majaribio mbalimbali, usafishaji, kuadibu, na hukumu kabla ya kuwa na uhalisia wa kumcha Mungu.) Mnasema hivyo, lakini kulingana na vile mnavyojua, kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kunaonekana rahisi kufanywa kwa sasa. Kwa nini Nasema hivi? Kwa sababu mmesikiliza ibada nyingi, na umepokea kiwango kingi cha kunyunyiziwa kwa uhalisia wa ukweli. Hii imewaruhusu kuelewa namna ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kwa mujibu wa nadharia na kufikiria. Kuhusiana na matendo yenu ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, haya yote yamekuwa yenye manufaa na kuwafanya kuhisi kwamba kitu kama hicho kinaweza kutimizika. Basi ni kwa nini katika uhalisia wa mambo watu hawajawahi kukitimiza? Hii ni kwa sababu kiini halisi cha asili ya binadamu hakimchi Mungu na kinapenda maovu. Hiyo ndiyo sababu halisi.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 10)

Kutomcha Mungu na Kutojiepusha na Maovu ni Kumpinga Mungu

Sasa hivi mnaangaliana uso kwa uso na Mungu, uso kwa macho na neno la Mungu. Maarifa yenu ya Mungu ni mengi zaidi kuliko yale ya Ayubu. Kwa nini Naleta suala hili? Kwa nini Ninaongea hivi? Ningependa kuwaelezea hoja moja, lakini kabla Sijafanya hivyo, Ningependa kuwauliza swali: Ayubu alijua machache sana kumhusu Mungu, ilhali angeweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hivyo basi kwa nini watu siku hizi wanashindwa kufanya hivyo? (Upotoshaji mkubwa.) Upotoshaji mkubwa—hicho ndicho kiini cha swali, lakini Sitawahi kulitazama hivyo. Mara nyingi mnachukua falsafa na barua ambazo mnazungumzia mara kwa mara, kama vile “upotoshaji mkuu,” “kuasi dhidi ya Mungu,” “kutotii Mungu,” “kutotii,” “kutopenda ukweli,” na mnatumia vidahizo kama hivi kuelezea kiini halisi cha kila swali. Hii ni njia isiyofaa ya kufanya mazoezi. Kutumia jibu moja kuelezea maswali yaliyo na asili tofauti mara moja huibua shaka ya kuukufuru ukweli na Mungu. Sipendi kusikia aina hii ya jibu. Hebu fikiria! Hakuna yeyote kati yenu amefikiria kuhusu suala hili, lakini kila siku Mimi Ninaliona, na kila siku Mimi Ninalihisi. Hivyo basi, mnafanya, na Mimi Ninatazama. Wakati mnapolifanya, hamwezi kuhisi kiini halisi cha suala hili. Lakini wakati Ninapoliona, Ninaweza kuona kiini halisi chake, na Ninaweza kuhisi kiini chake halisi vilevile. Hivyo basi kiini hiki ni nini basi? Kwa nini watu siku hizi hawamchi Mungu na hawaambai maovu? Majibu yenu yako mbali na kuweza kueleza kiini halisi cha swali hili, na haziwezi kutatua kiini halisi cha swali hili. Hiyo ni kwa sababu kunacho chanzo hapa ambacho nyinyi hamna habari kukihusu. Chanzo hiki ni kipi? Ninajua mnataka kusikia kukihusu, hivyo basi Nitawaambia kuhusu chanzo cha swali hili.

Hapo mwanzo kabisa wa kazi ya Mungu, Alichukulia vipi binadamu? Mungu alimwokoa binadamu; Alimchukulia binadamu kama mmoja wa familia Yake, kama mlengwa wa kazi Yake, kama kile ambacho Alitaka kukishinda, kuokoa, na kile ambacho Alitaka kufanya kuwa kitimilifu. Huu ndio uliokuwa mwelekeo wa Mungu kwa binadamu mwanzoni mwa kazi Yake. Lakini mwelekeo wa binadamu kwa Mungu wakati huo ulikuwa upi? Mungu alikuwa haeleweki kwa binadamu na binadamu alimchukulia Mungu kuwa mgeni. Inaweza kusemwa kwamba mtazamo wao kwa Mungu haukuleta matokeo sahihi, na kwamba hawakuelewa wazi jinsi wanastahili kumshughulikia Mungu. Hivyo basi Alimshughulikia alivyopenda yeye, na akafanya kile alichopenda yeye. Je, binadamu alikuwa na mtazamo kuhusu Mungu? Hapo mwanzoni, binadamu hakuwa na mtazamo wowote kuhusu Mungu. Mtazamo wa binadamu kama ulivyojulikana, ulikuwa tu baadhi ya dhana na fikira kumhusu Mungu. Kile ambacho kiliingiliana na dhana za watu kilikubalika; kile ambacho hakikuingiliana kiliitikiwa juujuu, lakini katika mioyo yao watu waligongana pakubwa nacho na wakakipinga. Huu ndio uliokuwa uhusiano wa binadamu na Mungu hapo mwanzoni: Mungu alimwona binadamu kama mwanachama wa familia, ilhali binadamu alimchukulia Mungu kama mgeni. Lakini baada ya kipindi cha kazi ya Mungu, binadamu alielewa hatimaye kile ambacho Mungu alikuwa akijaribu kutimiza. Watu hatimaye walijua kwamba Mungu ndiye aliyekuwa Mungu wa kweli, na hatimaye wakajua kile ambacho binadamu angepokea kutoka kwa Mungu. Binadamu alimchukulia Mungu wakati huu kuwa nini? Binadamu alichukulia Mungu kuwa tegemeo kuu, akitumai kupokea neema, kupokea baraka, kupokea ahadi. Naye Mungu alimchukulia binadamu wakati huu kuwa nini? Mungu alimchukulia binadamu kuwa mlengwa wa ushindi Wake. Mungu alitaka kuyatumia maneno ili kumhukumu binadamu, kumjaribu binadamu, kumpa majaribio binadamu. Lakini kwa wanadamu wakati huu hasa, Mungu alikuwa kifaa ambacho angetumia kutimiza shabaha zake binafsi. Watu waliona kwamba ukweli uliotolewa na Mungu ungeweza kushinda na kuwaokoa, na kwamba walikuwa na fursa ya kupokea vitu walivyotaka kutoka kwa Mungu, hatima ambayo walikuwa wakitaka. Kwa sababu ya haya, chembechembe ya uaminifu kajitunga katika mioyo yao, na walikuwa radhi kumfuata Mungu huyu. Muda ukapita na watu wakawa na maarifa fulani ya juujuu na ya kifalsafa kuhusu Mungu. Inaweza kusemekana kwamba walikuwa wameanza “kuzoeana” zaidi na zaidi na Mungu. Neno likitamkwa na Mungu, mahubiri Yake, ukweli Aliokuwa ameutoa awali, na kazi Yake—watu walikuwa “wamezoea” zaidi na zaidi. Hivyo basi, watu walidhania kimakosa kwamba Mungu hakuwa tena mgeni, na kwamba tayari walikuwa wakitembea njia ya uwiano na Mungu. Tangu hapo mpaka sasa, watu wamesikiliza mahubiri mengi ya ukweli, na wamepitia kazi nyingi ya Mungu. Ilhali kwenye uingiliaji kati na uzuiaji wa mambo mengi tofauti na hali, watu wengi hawawezi kufikia hali ya kutia ukweli katika matendo, na hawawezi kufikia hali ya kumtosheleza Mungu. Watu wanazidi kuwa goigoi, wanazidi kuikosa imani. Wanazidi kuhisi ni kana kwamba matokeo yao binafsi hayajulikani. Hawathubutu kuwa na mawazo yoyote ya kupita kiasi, na hawatafuti kupiga hatua yoyote ya maendeleo; wanafuata tu shingo upande, wakienda mbele hatua kwa hatua. Kuhusiana na hali ya sasa ya binadamu, mwelekeo wa Mungu kwa binadamu ni upi? Tamanio tu la Mungu ni kuukabidhi ukweli huu kwa binadamu, na kutia moyoni mwa binadamu njia Yake, na kupangilia hali mbalimbali ili kujaribu binadamu katika njia tofauti. Shabaha yake ni kuweza kuchukua maneno haya, ukweli huu, na kazi Yake, na kusababisha matokeo ambapo binadamu anaweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Watu wengi ambao Nimewaona wanalichukua tu neno la Mungu na kuliona kuwa falsafa, kuliona kuwa barua, kuliona kuwa kanuni za kufuatwa. Wanapoendelea na shughuli zao na kuongea au kukabiliwa na majaribio, hawachukulii njia ya Mungu kama njia ambayo wanafaa kuifuata. Hali hii hasa ni kweli wakati watu wanapokabiliwa na majaribio makuu; Sijamwona yeyote ambaye alikuwa anatia katika matendo kwa mwelekeo wa kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kwa sababu ya hili, mwelekeo wa Mungu kwa binadamu umejaa chuki na chukizo ya kupindukia. Baada ya Mungu kuwapa watu majaribio kadhaa, hata mara mia, bado hawana mwelekeo wazi wa kuonyesha bidii yao—ninataka kumcha Mungu na kujiepusha na maovu! Kwa sababu watu hawana bidii hii, na hawaonyeshi ishara kama hii, mwelekeo wa sasa wa Mungu kwao si kama ule wa hapo nyuma, Alipotoa rehema Yake, akatoa uvumilivu wake, akatoa ustahimilivu na subira yake. Badala yake, Amesikitishwa mno na binadamu. Ni nani aliyesababisha masikitiko haya? Aina hii ya mwelekeo ambao Mungu anao kwa binadamu, unamtegemea nani? Unategemea kila mtu anayemfuata Mungu. Kwenye mkondo wa miaka Yake mingi ya kazi, Mungu ametaja mahitaji mengi kwa binadamu, na kupangilia hali nyingi kwa binadamu. Lakini haijalishi ni vipi binadamu ametenda, na haijalishi ni mwelekeo upi ambao binadamu anao kwa Mungu, binadamu hawezi kutenda kwa njia wazi kulingana na shabaha ya kumcha Mungu na kujiepusha na uovu. Hivyo basi, Nitajumlisha yote haya kwa msemo mmoja, na kuweza kutumia msemo huu kuelezea kila kitu ambacho tumeweza kuzungumzia kuhusiana na ni kwa nini watu hawawezi kutembea kwa njia ya Mungu—mche Mungu na kujiepusha na maovu. Msemo huu ni upi? Msemo huu ni: Mungu humchukulia binadamu kama kifaa cha wokovu Wake, kifaa cha kazi Yake; binadamu humchukulia Mungu kama adui wake, kama tabaini yake. Je, unalielewa suala hili sasa? Kile ambacho ndicho mwelekeo wa binadamu; kile ambacho ndicho mwelekeo wa Mungu; kile ambacho ni uhusiano wa binadamu na Mungu—hivi vyote viko wazi sana sasa. Haijalishi ni kiwango kipi cha mahubiri ambayo mmeyasikiliza, yale mambo ambayo mliyoyatolea muhtasari nyinyi wenyewe—kama vile kuwa mwaminifu kwa Mungu, kumtii Mungu, kutafuta njia ya uwiano na Mungu, kutaka kuishi daima dawamu kwa ajili ya Mungu, kuishi kwa ajili ya Mungu—kwangu Mimi mambo hayo hayajumuishi kutembea kwa njia ya Mungu kwa nadhari, ambako ni kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Badala yake, ni njia mbalimbali kupitia kwazo mnaweza kufikia shabaha fulani. Ili kutimiza shabaha hizi, mnaangalia shingo upande baadhi ya taratibu. Na ni taratibu hizi hasa ambazo huwapeleka watu mbali zaidi kutoka katika njia ile ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, na kumweka Mungu katika upinzani na binadamu kwa mara nyingine.

Swali tunalolizungumzia leo ni zito kidogo, lakini licha ya chochote bado Natumai kwamba mtakapopitia yale yote yajayo, na kwenye nyakati zijazo, mnaweza kufanya kile ambacho Nimewaambia mfanye. Msipuuze Mungu na kumchukulia Yeye kama hewa tupu, kuhisi kwamba Anakuwepo tu nyakati zile Anapokuwa Mwenye manufaa kwako, lakini wakati ule ambao humhitaji unahisi kwamba Yeye hayupo. Unaposhikilia uelewa huu katika bila ufahamu, tayari umemghadhabisha Mungu. Pengine kunao watu wanaosema: “Mimi sichukulii Mungu kama hewa tupu, mimi siku zote humwomba Mungu, siku zote mimi humtosheleza Mungu, na kila kitu ninachokifanya huwa katika ule upana na kiwango na kanuni zinazohitajika na Mungu. Bila shaka siendelei kulingana na mawazo yangu binafsi.” Ndiyo, namna ambayo unafanya mambo ni sahihi. Lakini unafikiria vipi wakati unakumbana macho kwa macho na suala? Unakuwa na matendo gani unapokabiliwa na suala? Baadhi ya watu huhisi kwamba Mungu yupo wakati wanapomwomba Yeye, na Kumsihi kuwasikiliza. Lakini wakati wanapokabiliwa na suala wanakuja na fikira zao binafsi na wanataka kuzitii. Hapa Mungu huchukuliwa kama hewa tupu. Aina hii ya hali humfanya Mungu kutokuwepo. Watu hufikiria kwamba Mungu anafaa kuwepo wakati wanapomhitaji Yeye, na wakati hawamhitaji Mungu Hafai kuwepo. Watu hufikiria kwamba kufanya mambo kulingana na mawazo yao katika matendo ya maisha ni tosha. Wanasadiki wanaweza kufanya mambo vyovyote vile wapendavyo. Wanafikiria tu kwamba hawahitaji kutafuta njia ya Mungu. Watu ambao kwa sasa wamo katika aina hii ya hali, hali hii ya namna—huoni kwamba karibu wataingia hatarini? Baadhi ya watu husema: “Haijalishi kama karibu nitaingia hatarini au la, nimesadiki kwa miaka mingi sana, na ninasadiki kwamba Mungu hataniacha kwa sababu Asingeweza kustahimili kuniacha mimi.” Watu wengine husema: “Hata tangu nilipokuwa kwenye tumbo la mama yangu, nilimsadiki Bwana, tangu hapo mpaka sasa, jumla ya miaka arubaini au hamsini hivi. Kwa mujibu wa muda, mimi ndimi nimefuzu zaidi kuokolewa na Mungu; mimi ndimi nimefuzu zaidi kuwepo. Kwenye kipindi hiki cha muda cha miongo minne au mitano, niliiacha familia yangu na kazi yangu. Nilijitolea kila kitu nilichokuwa nacho kwa Mungu, kama pesa, ardhi, anasa na muda wa familia; sijala vyakula vingi vitamu; sijafurahia vitu vingi vya kusisimua; sijatembelea sehemu nyingi za kuvutia; nimeweza hata kupitia mateso ambayo hata watu wa kawaida wasingevumilia. Kama Mungu hawezi kuniokoa mimi kwa sababu ya haya yote, basi mimi nashughulikiwa kwa njia isiyo ya haki na siwezi kuamini kwa aina hii ya Mungu.” Je, kunao watu wengi walio na aina hii ya mtazamo? (Kunao wengi sana.) Basi leo Nitawasaidia kuelewa hoja moja: Kila mmoja wa hao anayeshikilia aina hii ya maoni anachukua hatua zitakazomdhuru mwenyewe. Hii ni kwa sababu wanatumia maoni yao binafsi katika kuyafunika macho yao. Ni kufikiria kwao hasa, na hitimisho yao binafsi zinazochukua nafasi ya kiwango cha kile Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu, ndizo zinazowashikilia dhidi ya kukubali nia za kweli za Mungu, na kuwafanya kutoweza kuhisi uwepo wa kweli wa Mungu, na kuwafanya pia kupoteza fursa yao kufanywa kuwa watimilifu na Mungu na kutokuwa na sehemu au mgao katika ahadi ya Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 11)

Namna Ambavyo Mungu Huanzisha Matokeo Ya Binadamu na Kiwango Ambacho Hutumia Kuasisi Matokeo ya Binadamu

Kabla ya kuwa na mitazamo au hitimisho zako binafsi, unafaa kwanza kuelewa mwelekeo wa Mungu kwako, kile ambacho Mungu anafikiria, na kuamua kama kufikiria kwako ni sahihi au la. Mungu hajawahi kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya mtu, na Hajawahi kutumia kiwango cha mateso yaliyovumiliwa na mtu katika kuasisi matokeo yake. Basi Mungu hutumia kiwango gani katika kuasisi matokeo ya binadamu? Kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya binadamu—hii ndiyo inaingiliana zaidi na dhana za watu. Na pia kuna hao watu binafsi ambao mara nyingi mnawaona, wale ambao katika wakati fulani walijitolea kabisa, wakatumia muda mwingi kabisa, wakagharamika kabisa, wakateseka kabisa. Hawa ndio, kwa maoni yenu, wanaweza kuokolewa na Mungu. Kile tu ambacho watu hawa wanaonyesha, yote wanayoishi kwa kudhihirisha, ndiyo hasa dhana ya wanadamu kuhusu kiwango ambacho Mungu anaanzisha kuhusiana na matokeo ya binadamu. Bila kujali ni nini unachosadiki, Sitaorodhesha mifano hii mmoja baada ya mwingine. Nikiongea kwa ujumla, mradi tu si kiwango cha kufikiria binafsi kwa Mungu, basi kinakuja kutoka kwenye kufikiria kwa binadamu na ni dhana tu ya binadamu. Ni nini athari za kusisitiza bila mwelekeo dhana na kufikiria kwako binafsi? Bila shaka, athari inaweza kuwa tu Mungu akikusukuma mbali. Hii ni kwa sababu siku zote unaringa kuhusu sifa zako mbele ya Mungu, unashindana na Mungu, na kuleta mzozo dhidi ya Mungu, na hujaribu hata kufahamu kwa kweli kufikiria kwa Mungu, wala hujaribu kuzifahamu nia za Mungu na mwelekeo wa Mungu kwa binadamu. Kuendelea mbele hivi ni kujiheshimu kuliko yote na wala si kumheshimu Mungu. Unajisadiki; husadiki Mungu. Mungu hataki mtu wa aina hii, na Mungu hatamwokoa mtu wa aina hii. Kama huwezi kuachilia aina hii ya mtazamo, na kisha kuirekebisha mitazamo hii ya kale isiyokuwa sahihi; kama ungeweza kuendelea mbele kulingana na maagizo ya Mungu; anza kutenda njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kwa sasa na kusonga mbele; kuweza kuheshimu Mungu na kumwona kuwa mkubwa katika mambo yote; usitumie ndoto zako za kibinafsi, mitazamo au imani katika kujifafanua, kumfafanua Mungu. Na badala yake, unazitafuta nia za Mungu kwa hali zote, unatimiza utambuzi na uelewa wa mwelekeo wa Mungu kwa binadamu, na unatumia kiwango cha Mungu kutosheleza Mungu—kufanya hivi kungependeza! Huku kungemaanisha karibu unaanza katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kwa sababu Mungu hatumii namna ambavyo watu hufikiria kwa njia hii au njia ile mawazo na mitazamo yao, kama kiwango cha kuanzisha matokeo ya binadamu, basi ni aina ipi ya kiwango Anayoitumia? Mungu hutumia majaribio kuanzisha matokeo ya binadamu. Kunavyo viwango viwili vya kutumia katika majaribio yanayoasisi matokeo ya binadamu: Kiwango cha kwanza ni idadi ya majaribio ambayo watu hao wanapitia, na kiwango cha pili ni matokeo ya watu hawa katika majaribu haya. Ni viashirio hivi viwili vinavyoasisi matokeo ya binadamu. Sasa tutaweza kufafanua viwango hivi viwili.

Kwanza kabisa, unapokabiliwa na jaribio kutoka kwa Mungu (kidokezo: Inawezekana kwamba katika macho yako jaribio hili ni dogo sana na halifai kutajwa), Mungu atakufanya kuwa na ufahamu kabisa kwamba huu ni mkono wa Mungu juu yako, na kwamba ni Mungu ambaye amepangilia hali hizi zote kwako. Wakati kimo chako hakijakomaa, Mungu atapanga majaribio ili kuweza kukupima. Majaribio haya yatalingana na kimo chako, yale ambayo unaweza kuelewa, na yale ambayo unaweza kustahimili. Kujaribu sehemu yako gani? Kujaribu mwelekeo wako kwa Mungu. Je, mwelekeo huu ni muhimu sana? Bila shaka ni muhimu! Zaidi ya hayo, ni muhimu hasa! Kwa sababu mwelekeo huu wa binadamu ndiyo matokeo anayotaka Mungu, ndicho kitu muhimu zaidi kulingana na Mungu. Ama sivyo Mungu asingetumia jitihada Zake kwa watu kwa kujihusisha na aina hizi za kazi. Mungu hutaka kuuona mwelekeo wako kwake Yeye, kupitia kwa majaribio haya; Anataka kujua kama uko kwenye njia sahihi na Anataka kujua kama unamcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hivyo basi, bila kujali kama unaelewa ukweli mwingi au kidogo wakati huo, bado utakabiliwa na majaribio ya Mungu, na kufuatia ongezeko lolote katika kiwango chochote cha ukweli unaouelewa, Mungu ataendelea kupangilia majaribio sawa na hayo kwako. Wakati unapokabiliwa kwa mara nyingine tena na jaribio, Mungu anataka kuona iwapo mtazamo wako, mawazo yako, na mwelekeo wako kwa Mungu umekuwa na ukuaji wowote mpaka sasa. Baadhi ya watu husema: “Kwa nini siku zote Mungu anataka kuiona mielekeo ya watu? Kwani Mungu hajaona namna wanavyouweka ukweli katika matendo? Kwa nini Atake tena kuiona mielekeo ya watu?” Huku ni kupayuka kwa upuuzi! Kwa sababu Mungu anaendelea hivi, basi nia za Mungu lazima ziwe mumohumo. Siku zote Mungu huwaangalia watu kutoka pembeni mwao, akiangalia kila neno na tendo lao, kila kitendo na kusonga kwao, na hata kila fikira na wazo lao. Kila kitu kinachowafanyikia watu: vitendo vyao vizuri, makosa yao, dhambi zao, na hata kuasi na kusaliti kwao, Mungu atazirekodi zote kama ithibati katika kuasisi matokeo yao. Kwa kadri kazi ya Mungu inavyoendelea kuimarika hatua kwa hatua, unasikia ukweli zaidi na zaidi, unakubali mambo mazuri zaidi na zaidi, taarifa nzuri, na uhalisia wa kweli. Kwenye mkondo wa mchakato huu, mahitaji ya Mungu kwako wewe yataongezeka pia. Wakati uo huo, Mungu atapanga majaribio makubwa zaidi kwako. Shabaha yake ni kuchunguza kama mwelekeo wako kwa Mungu umekomaa mpaka sasa. Bila shaka, kwenye kipindi hiki, mtazamo ambao Mungu anahitaji kwako unaingiliana na uelewa wako wa uhalisia wako wa ukweli.

Huku kimo chako kinapoendelea kuimarika kwa utaratibu, kile kiwango ambacho Mungu anahitaji kutoka kwako wewe kitaendelea kuimarika kwa utaratibu pia. Kama utakuwa hujakomaa, Mungu atakupa kiwango kidogo sana; wakati kimo chako kitakapokuwa kikubwa kidogo, Mungu atakupa kiwango cha juu zaidi kidogo. Lakini Mungu atakuwa vipi baada ya wewe kuuelewa ukweli wote? Mungu atahakikisha kuwa unakabiliana na hata majaribio makubwa zaidi. Katikati ya majaribio haya, kile Mungu anachotaka kupata, kile Mungu anachotaka kuona, ni maarifa yako ya kina zaidi ya Mungu na kumcha kwako Kwake kwa njia ya kweli. Wakati huu, mahitaji ya Mungu kwako wewe yatakuwa ya juu zaidi “makali zaidi” kuliko wakati ambapo kimo chako kilikuwa kidogo zaidi (kidokezo: Watu huona kwamba hali hii ni kali, lakini Mungu kwa hakika Huiona kuwa ya kustahimilika). Wakati Mungu anawapa watu majaribio, ni uhalisia gani ambao Mungu anataka kuunda? Mungu anauliza kila mara kwamba watu wampe Yeye moyo wao. Baadhi ya watu watasema: “Mtu anawezaje kufanya hivyo? Natekeleza wajibu wangu, niliacha nyumba yangu na riziki yangu, niligharamika kwa sababu ya Mungu. Hii yote si mifano ya kuutoa moyo wangu kwa Mungu? Ni vipi vingine nitakavyoutoa moyo wangu kwa Mungu? Yaweza kuwa kwamba, hii si mifano ya kuutoa moyo wangu kwa Mungu? Mahitaji mahususi ya Mungu ni yapi?” Mahitaji haya ni mepesi mno. Kwa hakika, kunao baadhi ya watu ambao tayari wameitoa mioyo yao kwa Mungu katika viwango tofauti na awamu mbalimbali za majaribio yao. Lakini wengi wa watu huwa hawapi Mungu mioyo yao. Wakati Mungu anapokupa jaribio, Mungu hutaka kujua kama moyo wako uko pamoja Naye, pamoja na mwili au pamoja na Shetani. Wakati Mungu anapokupa jaribio, Mungu anataka kujua kama unasimama katika upinzani na Yeye au kama unasimama katika hali ambayo inalingana na Yeye, na kutaka kuona moyo wako kama uko na Yeye. Wakati hujakomaa na wakati wa kukabiliwa na majaribio, kiwango cha imani yako kiko chini, na huwezi kujua hasa ni nini unachohitaji ili kutosheleza nia za Mungu kwa sababu unao uelewa finyu wa ukweli. Licha ya haya yote, bado unaweza kumwomba Mungu kwa dhati na uaminifu, kuwa radhi kuutoa moyo wako kwa Mungu, kumfanya Mungu kuwa mkuu wako, na kuwa radhi kumpa Mungu yale mambo unayosadiki kuwa yenye thamani zaidi. Hii ndiyo maana ya wewe kuwa tayari umempa Mungu moyo wako. Unaposikiliza mahubiri mengi zaidi na zaidi, na kuelewa ukweli zaidi na zaidi kimo chako kitaanza kukomaa kwa utaratibu. Kiwango ambacho Mungu huhitaji kutoka kwako si sawa na kile ambacho ulikuwemo wakati ulikuwa hujakomaa; Anahitaji kiwango cha juu zaidi kuliko hicho. Wakati moyo wa binadamu unapewa Mungu kwa utaratibu, unaanza kuwa karibu zaidi na karibu zaidi na Mungu; wakati binadamu anaweza kuwa karibu na Mungu kweli, wanaanza kuwa na moyo ambao sanasana unamcha Yeye. Mungu anataka aina hii ya moyo.

Wakati Mungu anataka kuumiliki moyo wa mtu, Atawapa majaribio mengi. Kwenye majaribio haya, kama Mungu hatauchukua moyo wa mtu huyu, wala Haoni kama mtu huyu anao mwelekeo wowote—hivi ni kusema Havioni vitu ambavyo mtu huyu anapitia au anafanya mambo kwa njia ambayo ni ya kumcha Mungu, na Haoni mwelekeo au suluhisho ambalo linajiepusha na maovu kutoka kwa mtu huyu. Kama hivi ndivyo ilivyo, basi baada ya majaribio mengi, subira ya Mungu kwa mtu huyu binafsi itaondolewa, na Hatamvumilia mtu huyu tena. Hataweza kuwapa watu kama hawa majaribio, na Hataweza tena kuwashughulikia. Basi hiyo inamaanisha nini kwa matokeo ya mtu huyu? Inamaanisha kwamba hawatakuwa na matokeo. Yawezekana kwamba mtu huyu hajafanya maovu yoyote. Yawezekana pia kwamba watu hawa hawajafanya chochote cha kukatiza au kutatiza. Yawezekana kuwa watu hawa hawajampinga Mungu waziwazi. Hata hivyo, moyo wa mtu huyu umefichwa kutoka kwa Mungu. Hawajawahi kuwa na mwelekeo na mtazamo wazi kwa Mungu, na Mungu hawezi kuona waziwazi kwamba moyo wake amekabidhiwa Yeye, na Yeye Hawezi kuona waziwazi kwamba mtu huyu anatafuta kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Mungu hana subira tena kwa watu hawa, Hatawagharamia tena, Hatatoa tena rehema Yake kwao, na Hatawafanyia kazi wao tena. Maisha ya imani ya mtu huyu katika Mungu tayari hayapo tena. Hii ni kwa sababu katika majaribio yote mengi ambayo Mungu amempa mtu huyu, Mungu hajapata matokeo Anayotaka. Hivyo basi, kunayo idadi ya watu ambao ndani yao Sijawahi kuuona mwangaza na kupata nuru kwa Roho Mtakatifu. Inawezekanaje kuona haya? Mtu wa aina hii huenda aliamini katika Mungu kwa miaka mingi, na kwenye sehemu ya juujuu wamekuwa amilifu. Wamevisoma vitabu vingi, wameyashughulikia masuala mengi, wameandika nakala nyingi, wamekuwa na ujuzi wa barua na falsafa nyingi. Hata hivyo, hakuna ukuaji wowote unaonekana kamwe, na wala kuwa na mtazamo wowote wa kuonekana kwa Mungu kutoka kwa mtu huyu, wala hakuna mwelekeo wowote wazi. Hivi ni kusema kwamba huwezi kuona moyo wa mtu huyu. Moyo wao siku zote umesetiriwa, moyo wao umefumikwa—Umefunikwa kutoka kwa Mungu, hivyo basi Mungu hajauona moyo wa kweli wa mtu huyu, Hajaona kumcha Mungu kwa mtu huyu, na hata zaidi Hajaona namna ambayo mtu huyu anatembea katika njia za Mungu. Kama mpaka sasa Mungu hajampata mtu wa aina hii, Anaweza kuwapata katika siku za usoni? Hawezi! Je, Mungu ataendelea kusukumiza mbele mambo ambayo hayawezi kupatikana? Hatafanya hivyo! Mwelekeo wa Mungu kwa watu kama hawa, hivyo basi ni nini? (Anawasukumia mbali, Hawasikilizi.) Yeye hawasikilizi! Mungu hasikilizi mtu wa aina hii; Anawasukumia mbali. Mmetia kwenye kumbukumbu maneno haya kwa haraka sana, kwa usahihi sana. Inaonekana mmeelewa kile mlichosikia!

Kunao baadhi ya watu ambao, punde wanapoanza kumfuata Mungu wao hawana ukomavu na hawajui chochote; hawaelewi nia za Mungu; hawajui pia maana ya kusadiki Mungu, kuchukua njia iliyoundwa na binadamu na inayokosewa na wengi ya kusadiki Mungu, kufuata Mungu. Wakati mtu wa aina hii anakabiliwa na majaribio hawana habari na hawajali kuhusu mwongozo na nuru ya Mungu. Hawajui maana ya kuutoa moyo wao kwa Mungu na maana ya kusimama imara wakati wa jaribio. Mungu atampa mtu huyu kiwango finyu cha muda na katika kipindi hiki, Atawaacha kuelewa jaribio la Mungu ni nini, na nia za Mungu ni nini. Baadaye mtu huyu atahitaji kuonyesha mtazamo wao. Kuhusiana na watu wale walio katika awamu hii, Mungu angali anasubiri. Kuhusiana na watu wale ambao mitazamo yao ingali inayumbayumba, wale wanaotaka kumpa Mungu mioyo yao lakini hawajawa na maridhiano ya kufanya hivyo, ambao, ingawa wameweza kutenda ukweli fulani, wakati wanapokumbwa na jaribio kuu, wanaokwepa na wanataka kukata tamaa—mwelekeo wa Mungu kwa watu kama hawa ni upi? Mungu angali bado ana matarajio kidogo kwa watu kama hawa. Matokeo yanategemea na mielekeo na utendakazi wao. Mungu anaitikia vipi kama watu si amilifu katika kuwa na maendeleo? Yeye hukata tamaa. Hii ni kwa sababu kabla Mungu hajakata tamaa kwako, tayari wewe mwenyewe umekata tamaa. Kwa hivyo, huwezi kumlaumu Mungu kwa kufanya hivyo, je, unaweza? Je, hiyo ni haki? (Ni haki.)

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 12)

Wakati wakimfuata Mungu, ni nadra sana kwa watu kutilia maanani makusudi ya Mungu, na ni nadra wao kutilia maanani mawazo ya Mungu na mtazamo Wake kwa wanadamu. Watu hawaelewi fikira za Mungu, kwa hivyo mnapoulizwa maswali yanayohusisha nia za Mungu, yanayohusisha tabia ya Mungu, mnaingia katika hali ya kutokuwa na hakika; mnakuwa kwa kweli hamna uhakika, na mnakisia au kubahatisha. Mwelekeo huu ni upi? Unathibitisha hoja hii: kwamba watu wengi wanaomwamini Mungu wanamchukulia kuwa kifungo cha hewa tupu na kama kitu kinachoonekana kuishi dakika moja na hakipo tena dakika ifuatayo. Kwa nini Nasema hivyo? Kwa sababu kila wakati mnapokumbwa na suala, hamzijui nia za Mungu. Kwa nini hamzijui? Si kwamba hamzijui tu kwa sasa. Badala yake kuanzia mwanzo hadi mwisho hamjui mwelekeo wa Mungu katika suala hili. Kwenye nyakati zile ambazo huwezi kuona na hujui mwelekeo wa Mungu, umewahi kuutafakaria? Umeutafuta? Umewasiliana ili kuupata? La! Hii inathibitisha hoja: Mungu unayemsadiki na Mungu wa kweli hawajaunganika. Wewe, unayemsadiki Mungu, unafikiria Mungu kuhusu mapenzi yako, unafikiria tu kuhusu mapenzi ya kiongozi wako, na unafikiria tu yale mambo ya juujuu na maana ya kifalsafa ya neno la Mungu, lakini hujaribu kwa kweli kujua na kutafuta mapenzi ya Mungu kamwe. Sivyo ndivyo hali ilivyo? Kiini halisi cha suala hili hakipendezi! Kwa miaka na mikaka Nimeona watu wanaomsadiki Mungu. Kusadiki huku kunachukua mfumo gani? Baadhi ya watu wanasadiki katika Mungu ni kana kwamba Yeye ni hewa tupu. Watu hawa hawana majibu ya maswali kuhusu uwepo wa Mungu kwa sababu hawawezi kuhisi au kuwa na ufahamu uwepo au kutokuwepo kwa Mungu, sikuambii hata kuuona waziwazi au kuuelewa. Kwa nadharia yao, watu hawa wanafikiria kwamba Mungu hayupo. Baadhi wanasadiki katika Mungu ni kana kwamba Yeye ni binadamu. Watu hawa wanasadiki kwamba Mungu hawezi kufanya mambo yale ambayo wao hawawezi kufanya, na kwamba Mungu anafaa kufikiria namna wanavyofikiria. Ufafanuzi wa mtu huyu kuhusu Mungu ni “mtu asiyeonekana na asiyegusika.” Kunalo pia kundi la watu wanaosadiki katika Mungu kana kwamba Yeye ni kikaragosi; watu hawa wanasadiki kwamba Mungu hana hisia. Wanafikiria kwamba Mungu ni sanamu ya matope, na kwamba wanapokabiliwa na jambo, Mungu hana mwelekeo, hana mtazamo, hana mawazo; Anatawaliwa na binadamu. Watu wanasadiki tu wanavyotaka kusadiki. Wakimfanya kuwa mkubwa, Yeye ni mkubwa; wakimfanya kuwa mdogo, Yeye ni mdogo. Wakati wanapotenda dhambi na wanahitaji rehema ya Mungu, wanahitaji uvumilivu wa Mungu, wanahitaji upendo wa Mungu, basi Mungu anafaa kutoa rehema Zake. Watu hao wanafikiria kuhusu Mungu kwenye akili zao binafsi na kumfanya Mungu kutimiza mahitaji yao na kutosheleza matamanio yao yote. Haijalishi ni lini na ni wapi, na haijalishi hata mtu huyu anafanya nini, watakubali mvuto huu katika matendo yao kwa Mungu na kusadiki kwao katika Mungu. Kuna hata wale wanaosadiki katika Mungu kuweza kuwaokoa baada kuikera tabia ya Mungu. Hii ni kwa sababu wanasadiki kuwa upendo wa Mungu hauna mipaka, tabia ya Mungu ni haki, na kwamba bila kujali ni vipi ambavyo watu wanakosea Mungu, Hatakumbuka chochote. Kwa sababu makosa ya binadamu, dhambi za binadamu na kutotii kwa binadamu ni maonyesho ya mara moja ya tabia ya mtu huyo, Mungu atawapatia watu fursa, kuvumilia na kuwa na subira nao. Mungu angali atawapenda kama awali. Kwa hivyo tumaini la wokovu wao lingali kubwa. Kwa hakika, haijalishi ni vipi mtu anavyosadiki Mungu, mradi tu hafuatilii ukweli basi Mungu anashikilia mwelekeo mbaya kwake. Hii ni sababu wakati unamsadiki Mungu, labda unakithamini kile kitabu cha neno la Mungu unakichambua kila siku, unakisoma kila siku, lakini unamweka Mungu halisi pembeni, unamchukulia kama hewa tupu, unamchukulia Yeye kama mtu, na baadhi yenu mnamchukulia kuwa kikaragosi. Kwa nini Nasema hivi? Kwa sababu kutokana na vile Ninavyoona, licha ya kama unakabiliwa na suala au kukumbana na hali, yale mambo yanayopatikana katika nadharia yako, yale mambo ambayo yameimarishwa ndani kwa ndani—hakuna kati ya haya ambayo yana uunganisho wa neno la Mungu au yanafuatilia ukweli. Unajua tu kile wewe mwenyewe unatafuta, maoni yako wewe binafsi, na kisha mawazo yako binafsi, mitazamo yako binafsi inalazimishiwa Mungu. Inakuwa mitazamo ya Mungu. Akilini mwako hii inakuja kuwa mitazamo ya Mungu, na unafanya hii mitazamo kuwa viwango ambavyo unavishikilia bila kutetereka. Kwa muda, kuendelea namna hii kunakufanya uwe mbali na mbali kutoka kwa Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 13)

Elewa Mwelekeo wa Mungu na Utupilie Mbali Dhana zote Potovu Kumhusu Mungu

Mungu huyu ambaye kwa sasa mnasadiki, mmewahi kufikiria kuhusu Yeye ni Mungu wa aina gani? Anapomwona mtu mwovu akifanya mambo maovu, je Anayachukia? (Anayachukia.) Anapoona makosa ya mtu asiyejua, mwelekeo Wake ni upi? (Huzuni.) Anapowaona watu wakiiba sadaka Yake, mwelekeo Wake ni upi? (Anawachukia.) Haya yote yako wazi, sivyo? Anapoona mtu akiwa mzembe katika kusadiki kwake Mungu, na mtu huyo akikosa kufuatilia ukweli kwa namna yoyote, mwelekeo wa Mungu ni upi? Bado hamjaelewa jambo hili, sivyo? Uzembe ni mwelekeo ambao si dhambi, na humkosei Mungu. Watu husadiki kwamba haupaswi kuchukuliwa kama kosa. Basi mnafikiria mwelekeo wa Mungu ni nini? (Hayuko radhi kujibu swali hili.) Hayuko radhi kulijibu—mwelekeo huu ni upi? Ni kwamba Mungu huwa anawadharau watu hawa, anawabeza watu hawa! Mungu hushughulikia watu hawa kwa kutowathamini. Mtazamo wake ni kuwaweka pembeni, kutojihusisha na kazi yoyote inayowahusu, ikiwemo kuwapa nuru, mwangaza, kuwarudi au kuwafundisha nidhamu. Mtu wa aina hii kwa kweli si wa thamani kwa kazi ya Mungu. Mwelekeo wa Mungu kwa watu wanaozikera tabia Yake, na kuzikosea amri Zake za kiutawala ni upi? Chuki mno kwa kupindukia! Kwa kweli Mungu hupandwa na hasira kali na watu ambao hawaghairi kuhusu kukera tabia Yake! “Hasira Kali” ni hisia tu, hali ya moyo; haiwezi kuwakilisha mwelekeo kamili. Lakini hisia hii, hali hii ya moyo, itasababisha matokeo kwa mtu huyu: Itamjaza Mungu na chukizo la kupindukia! Ni nini matokeo ya kuchukia huku kwa kupindukia? Ni kwamba Mungu atamweka pembeni mtu huyu, na kutomwitikia kwa sasa. Kisha atasubiri sasa kuwashughulikia “baada ya msimu wa kupukutika kwa majani.” Hali hii inaashiria nini? Mtu huyu angali anayo matokeo? Mungu hakuwahi kunuia kumpa mtu wa aina hii matokeo! Hivyo basi si jambo la kawaida endapo Mungu kwa sasa hamwitikii mtu wa aina hii? (Ndiyo.) Mtu wa aina hii anafaa kujitayarisha vipi sasa? Wanafaa kujitayarisha kukabiliana na zile athari mbaya zilizosababishwa na tabia zao na maovu waliofanya. Huu ndio mwitikio wa Mungu kwa mtu wa aina hii. Hivyo basi Nasema waziwazi kwa mtu wa aina hii: Usishikilie imani za uwongo tena, na usijihusishe katika kufikiria makuu tena. Mungu hatavumilia watu siku zote bila kikomo; Hatastahimili dhambi zao au kutotii kwao bila kukoma. Baadhi ya watu watasema: “Nimeweza pia kuona watu wachache kama hawa. Wanapoomba wanaguswa hasa na Mungu, na wanalia kwa machungu. Kwa kawaida wao pia wanakuwa na furaha sana; wanaonekana kuwa na uwepo wa Mungu, na mwongozo wa Mungu.” Usiseme huo upuzi! Kulia kwa machungu si lazima iwe kwamba umeguswa na Mungu au unao uwepo wa Mungu, acha hata mwongozo wa Mungu. Kama watu watamghadhabisha Mungu, je, bado Mungu atawaongoza? Nikiongea kwa ujumla, wakati Mungu ameamua kumwondoa mtu, kuwaacha watu hao, tayari mtu huyo hana matokeo. Haijalishi ni vipi wanavyohisi kutosheka kujihusu wao wenyewe wakati wanapoomba, na imani kiwango kipi walichonacho katika Mungu mioyoni mwao; tayari hii si muhimu. Kitu cha muhimu ni kwamba Mungu hahitaji aina hii ya imani kwamba Mungu tayari amemsukumia mbali mtu huyu. Namna ya kuwashughulikia baadaye pia si muhimu. Kilicho muhimu ni kwamba katika muda ule ambao mtu huyu atamghadhabisha Mungu, matokeo yao tayari yameanzishwa. Kama Mungu ameamua kutomwokoa mtu wa aina hii, basi ataachwa na kuadhibiwa. Huu ndio mwelekeo wa Mungu.

Ingawa sehemu ya kiini halisi cha Mungu ni upendo, na Anaitoa rehema yake kwa kila mtu, watu hupuuza na kusahau hoja kwamba kiini Chake halisi ni heshima vilevile. Kwamba Anao upendo haimaanishi kwamba watu wanaweza kumkosea Yeye wapendavyo na kwamba Yeye hana hisia zozote, au mijibizo yoyote. Kwamba Anayo rehema haimaanishi kwamba Hana kanuni zozote kuhusiana na namna Anavyoshughulikia watu. Mungu yu hai; kwa kweli Yupo. Yeye si kikaragosi kilichofikiriwa au kitu kingine tu. Kwa sababu Yeye yupo, tunafaa kusikiliza kwa makini sauti ya moyo Wake siku zote, kutilia makini mwelekeo Wake, na kuzielewa hisia Zake. Hatufai kutumia kufikiria kwa watu ili kumfafanua Mungu, na hatufai kulazimisha fikira na matamanio ya watu kwa Mungu, kumfanya Mungu kutumia mtindo na fikira za binadamu katika namna Anavyomshughulikia binadamu. Ukifanya hivyo, basi unamghadhabisha Mungu, unaijaribu hasira ya Mungu, na unapinga heshima ya Mungu! Hivyo basi, baada ya kuelewa ukali na uzito wa suala hili, Ninasihi kila mmoja wenu mlio hapa kuwa makini na wenye busara katika vitendo vyenu. Kuwa makini na wenye busara katika kuongea kwenu. Na kuhusiana na namna mnavyoshughulikia Mungu, mnapokuwa makini zaidi na wenye busara zaidi, ndivyo ilivyo bora zaidi! Wakati huelewi mwelekeo wa Mungu ni nini, usizungumze kwa uzembe, usiwe mzembe katika vitendo vyako, na usipachike majina ovyo ovyo. Na hata zaidi, usikimbilie hitimisho kiholela. Badala yake, unafaa kusubiri na kutafuta; hili pia ndilo dhihirisho la kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kama unaweza kutimiza hoja hii kati ya zote, na kumiliki mwelekeo huu kati ya yote, basi Mungu hatakulaumu wewe kwa upumbavu wako, kutojua kwako, na ukosefu wa kuelewa kwa sababu zinazosababisha vitu. Badala yake, kutokana na hofu yako ya kumkosea Mungu, heshima yako kwa nia za Mungu, na mwelekeo wako wa kuwa radhi kumtii Yeye, Mungu atakukumbuka, atakuongoza na kukuangaza wewe, au kustahimili kutokuwa mkomavu kwako na kutojua kwako. Kinyume chake, endapo mwelekeo wako kwake Yeye utakuwa usioheshimu—kuhukumu Mungu kiholela, kukisia kiholela, na kufafanua maana ya Mungu—Mungu atakupa hukumu, nidhamu, au hata adhabu; au Atakupa taarifa. Pengine kauli hii inahusisha matokeo yako. Hivyo basi, Ningali bado nataka kutilia mkazo jambo hili kwa mara nyingine: Unapaswa uwe makini na mwenye busara katika kila kitu kinachotoka kwa Mungu. Usiongee kwa uzembe, na usiwe mzembe katika matendo yako. Kabla ya kusema chochote, unafaa kufikiria: Je, kufanya hivi kutamghadhabisha Mungu? Kufanya hivi ni kumcha Mungu? Hata katika masuala mepesi, bado unafaa kujaribu kuelewa hakika maswali haya, yafikirie kwa kweli. Kama unaweza kwa kweli kutenda haya kulingana na kanuni hizi kila pahali, katika hali zote, katika vitu vyoye, nyakati zote, na kushikilia mtazamo wa aina hiyo hasa wakati huelewi kitu basi Mungu siku zote atakuongoza wewe, na kukupa na hata njia ya kufuata. Bila kujali ni nini ambacho watu wanaonyesha, Mungu anaona yote waziwazi, dhahiri, na Atakupa utathmini sahihi na unaofaa kwa maonyesho haya. Baada ya kupitia jaribio la mwisho, Mungu atachukua tabia yako yote na kuijumlisha ili kuasisi matokeo yako. Matokeo haya yatashawishi kila mmoja bila shaka lolote. Kile ambacho Ningependa kuwaambia ni kwamba kila kitendo chenu, kila hatua yenu, na kila fikira yenu vyote vitaamua majaliwa yenu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 14)

Ni Nani Hupanga Matokeo ya Binadamu

Kunalo jambo jingine muhimu zaidi, na hilo ni mwelekeo wenu kwa Mungu. Mwelekeo huu ni muhimu sana! Huamua kama hatimaye mtatembea kuelekea katika maangamizo, au kwenye hatima nzuri na ya kupendeza ambayo Mungu amewatayarishia. Katika Enzi ya Ufalme, Mungu tayari amefanya kazi kwa zaidi ya miaka 20 na kwenye kipindi cha miaka hii 20 pengine mioyo yenu imekuwa na tashwishi kuhusu utendakazi wenu. Hata hivyo, katika moyo wa Mungu, Ameweka rekodi halisi na ya kweli kwa kila mmoja wenu. Kuanzia wakati ule ambao kila mtu anaanza kumfuata Yeye na kusikiliza mahubiri Yake, kuelewa zaidi na zaidi kuhusu ukweli, hadi pale ambapo wanatekeleza wajibu wao—Mungu anayo rekodi ya kila mojawapo ya maonyesho haya. Wakati mtu anapofanya wajibu wake, wakati anapokabiliwa na kila aina ya hali, kila aina ya majaribio, mwelekeo wa mtu huyo ni upi? Wanatenda kazi vipi? Wanahisi vipi kwa Mungu katika mioyo yao? … Mungu ameweka rekodi ya yote haya, rekodi yote kwa hakika. Pengine kutokana na mtazamo wenu, masuala haya yanakanganya. Hata hivyo, kutoka pale ambapo Mungu yupo, yote yako wazi kabisa, na hakuna hata dalili yoyote ya kutokuwa wazi. Hili ni suala linalohusisha matokeo ya kila mmoja, na majaliwa yao na matarajio yao ya siku za baadaye vilevile. Hata zaidi, hapa ndipo ambapo Mungu anatumia jitihada Zake zote alizomakinikia. Hivyo basi Mungu hathubutu kuipuuza hata kidogo, na hatavumilia kutomakinika kokote. Mungu anarekodi haya yote kuhusu wanadamu, anarekodi mambo kuhusu mkondo mzima wa binadamu anayefuata Mungu, kuanzia mwanzo hadi mwisho. Mwelekeo wako kwa Mungu wakati huu utaamua hatima yako. Je, haya si kweli? Kutoka hapo mpaka sasa, mnasadiki kwamba Mungu ni mwenye haki? Vitendo vya Mungu vinafaa? Bado mnayo picha yoyote ya Mungu vichwani mwenu? (La.) Basi mnasema kwamba matokeo ya binadamu ni kwa ajili ya Mungu kuweza kupanga au kwa ajili ya binadamu mwenyewe kupanga? (Ni kwa Mungu kupanga.) Ni nani basi anayeyapanga? (Mungu.) Hamna hakika, sivyo? Ndugu kutoka makanisa ya Hong Kong, ongeeni—ni nani anayeyapanga? (Binadamu anayapanga mwenyewe.) Mwanadamu anayapanga? Hivyo basi haimaanishi kwamba haina chochote kuhusu Mungu? Ndugu kutoka Korea Kusini, ongeeni. (Mungu huanzisha matokeo ya binadamu kutokana na hatua na vitendo vyake vyote na kutokana pia na njia wanayotembelea.) Hili ni jibu halisi sana. Kunayo hoja hapa ambayo lazima Niwafahamishe nyinyi: Kwenye mkondo wa kazi ya wokovu wa Mungu, Yeye huweka kiwango kwa binadamu. Kiwango hiki ni kwamba binadamu anaweza kutii neno la Mungu, na kutembea kwa njia ya Mungu. Ndicho kiwango kinachotumika kupima matokeo ya binadamu. Kama utafanya mazoezi kwa mujibu wa kiwango hiki cha Mungu, basi unaweza kupata matokeo mazuri; kama hutafanya hivyo, basi huwezi kupokea matokeo mazuri. Basi ni nani unayesema kwamba anayapanga matokeo haya? Si Mungu pekee anayeyapanga, lakini badala yake Mungu na binadamu pamoja. Hiyo ni sahihi? (Ndiyo.) Kwa nini hivyo? Kwa sababu ni Mungu ambaye anataka kujishughulisha na kujihusisha katika kazi ya wokovu wa wanadamu, na kutayarisha hatima nzuri kwa ajili ya binadamu; binadamu ndiye mlengwa wa kazi ya Mungu, na matokeo haya, hatima hii, ndiyo ambayo Mungu humtayarishia binadamu. Kama kusingekuwa na kilengwa cha kazi Yake, basi Mungu asingehitaji kazi hii; kama Mungu asingefanya kazi hii, basi binadamu asingekuwa na fursa ya wokovu. Binadamu ndiye mlengwa wa wokovu, na ingawa binadamu yumo kwenye upande wa kimya katika mchakato huu, ni mwelekeo wa upande huu ambao unaamua kama Mungu atafanikiwa katika kazi Yake ya kuwaokoa wanadamu au la. Kama si mwongozo ambao Mungu anakupa wewe, basi usingejua kiwango Chake, na usingekuwa na lengo lolote. Kama unacho kiwango hiki, lengo hili, ilhali hushirikiani, hulitilii kwenye matendo, hulipii gharama, basi bado hutapokea matokeo haya. Kwa sababu hii, Ninasema kwamba matokeo haya hayawezi kutenganishwa na Mungu, na pia hayawezi kutenganishwa na binadamu. Na sasa unaweza kujua ni nani anayepanga matokeo ya binadamu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 15)

Watu Huishia Kumfafanua Mungu Kutokana na Uzoefu Wao

Wakati wa kuwasilisha mada ya kumjua Mungu, mmegundua kitu? Mmegundua kwamba mwelekeo wa sasa wa Mungu umepitia mabadiliko? Je, mwelekeo wa Mungu kwa wanadamu hauwezi kubadilika? Je, siku zote Mungu atavumilia hivi, huku akimpa upendo Wake wote na rehema kwa binadamu bila kikomo? Suala hili pia linahusu kiini halisi cha Mungu. Hebu turejelee swali la yule mtoto wa kiume mbadhirifu kama aitwavyo kutoka awali. Baada ya swali hili kuulizwa, majibu yenu hayakuwa wazi sana. Kwa maneno mengine, bado hamwelewi vizuri nia za Mungu. Punde tu watu wanapojua kwamba Mungu anawapenda wanadamu, wanamfafanua Mungu kama ishara ya upendo: Haijalishi kile wanachofanya watu, haijalishi namna wanavyotenda mambo, haijalishi vipi wanavyomshughulikia Mungu na haijalishi ni vipi wasivyotii, hakuna chochote kinachojalisha kwa sababu Mungu ni upendo na upendo wa Mungu hauna mipaka na haupimiki. Mungu anao upendo, hivyo basi Anaweza kuvumilia watu; Mungu anao upendo, hivyo basi Anaweza kuwa mwenye rehema kwa watu, mwenye rehema kwa kutokomaa kwao, mwenye rehema kwa kutojua kwao, na mwenye rehema kwa kutotii kwao. Hivi ndivyo ilivyo kwa kweli? Kwa baadhi ya watu, wakati wamepitia subira ya Mungu mara moja, au mara chache, watashughulikia suala hili kama mtaji katika uelewa wao wa Mungu, wakisadiki kwamba Mungu atakuwa mara moja na milele mwenye subira kwao, atakuwa mwenye rehema kwao, na kwenye mkondo wa maisha yao watachukua subira ya Mungu na kuichukulia kama kiwango cha ni vipi ambavyo Mungu anawashughulikia. Kunao pia watu ambao, wakati wamepitia uvumilivu wa Mungu mara moja, daima watamfafanua Mungu kuwa uvumilivu, na uvumilivu huu hauna mipaka, hauna masharti, na hata usio na kanuni zozote. Je, kusadiki huku ni sahihi? Kila wakati mambo kuhusu kiini cha Mungu au tabia ya Mungu yanapozungumziwa, mwaonekana mmekanganywa mno. Kuwaona mkiwa hivi kunanifanya Mimi kuwa na wasiwasi. Mmeusikia mambo mengi ya ukweli kuhusiana na kiini halisi cha Mungu; mmeweza pia kusikiliza mada mengi kuhusiana na tabia ya Mungu. Hata hivyo, katika akili zenu masuala haya, na ukweli wa dhana hizi, ni kumbukumbu tu kutokana na nadharia na maneno yaliyoandikwa. Hakuna kati yenu anaweza kupitia kile ambacho tabia ya Mungu inamaanisha katika maisha yenu halisi, wala hamwezi kuona tu tabia ya Mungu ni nini. Hivyo basi, nyote mmechanganyikiwa katika kusadiki kwenu, nyote mnasadiki bila kujua, hadi kufikia kiwango ambacho mnao mwelekeo usiofaa kwa Mungu, kwamba mnamweka pembeni. Mwelekeo kama huu kwa Mungu unawaongoza wapi? Mnaongozwa katika hali ya kutoa hitimisho siku zote kuhusu Mungu. Punde unapopata maarifa kidogo, unahisi umetosheka kweli, unahisi ni kana kwamba umempokea Mungu kwa uzima Wake wote. Baadaye unahitimisha kwamba hivi ndivyo Mungu Alivyo, na humruhusu kuendelea mbele na shughuli Zake kwa furaha zaidi. Na kila Mungu anapofanya jambo jipya, hukubali kwamba Yeye ni Mungu. Siku moja, wakati Mungu atakaposema: “Simpendi binadamu tena; Sitoi rehema kwa binadamu tena; Sina uvumilivu au subira yoyote kwa binadamu tena; Nimejaa chuki na uhasama kupindukia kwa binadamu,” watu watakinzana na aina hii ya taarifa kutoka kwenye ndani ya mioyo yao. Baadhi yao wataweza hata kusema: “Wewe si Mungu wangu tena; Wewe si Mungu ninayetaka kufuata tena. Kama hivi ndivyo Unavyosema, basi Hujafuzu tena kuwa Mungu wangu, na sitaki kuendelea kukufuata Wewe. Kama Hunipi rehema, hunipi upendo, hunipi uvumilivu, basi nami sitakufuata Wewe tena. Kama Utakuwa mvumilivu tu kwangu bila kikomo, utakuwa mwenye subira kwangu mimi, na kuniruhusu mimi kuona kwamba Wewe ni upendo, kwamba Wewe ni subira, kwamba Wewe ni uvumilivu, hapo tu ndipo nitakapoweza kukufuata Wewe, na hapo tu ndipo nitakapoweza kuwa na ujasiri kukufuata mpaka mwisho. Kwa sababu ninapata subira na rehema Yako, kutotii kwangu na dhambi zangu zinaweza kusamehewa bila kikomo, kuondolewa bila kikomo, na ninaweza kutenda dhambi wakati wowote na mahali popote, kutubu na kusamehewa wakati wowote na mahali popote, na kukughadhabisha wakati wowote na mahali popote. Hufai kuwa na fikira au hitimisho Zako binafsi kuhusiana na mimi.” Ingawa huenda usifikirie kuhusu aina hii ya swali kwa namna ya kibinafsi na ya kufahamu kama hiyo, kila unapomchukulia Mungu kuwa zana ya dhambi zako kusamehewa na kifaa cha kutumika cha kupata hatima nzuri, tayari unamweka kwa njia isiyoeleweka Mungu aliye hai na katika hali ya kukupinga wewe, kuwa adui yako. Hivi ndivyo Ninavyoona. Unaweza kuendelea kusema, “Ninasadiki Mungu”; “Ninafuatilia ukweli”; “Ninataka kubadilisha tabia yangu”; “Ninataka kuwa huru dhidi ya ushawishi wa giza”; “Ninataka kumtosheleza Mungu”; “Nataka kumtii Mungu”; “Ninataka kuwa mwaminifu kwa Mungu, na kufanya wajibu wangu vizuri”; na kadhalika. Hata hivyo; haijalishi ni vipi utakavyosema kinasikika kuwa kizuri, haijalishi ni nadharia kiasi kipi unayojua, haijalishi ni vipi nadharia hiyo inavyovutia, ni vipi nadharia hiyo ilivyo na heshima, hoja ya mambo ni kwamba kunao wengi wenu ambao tayari wamejifunza namna ya kutumia taratibu, falsafa, nadharia mlizojifunza katika kuhitimisha mambo kuhusu Mungu, na kumweka yeye katika upinzani na nyinyi wenyewe kwa njia ambayo ni ya kimaumbile kabisa. Ingawa umejifunza barua na kujifunza falsafa, bado hujaingia kwa hakika katika uhalisia wa ukweli, hivyo basi ni vigumu sana kwako kuwa karibu na Mungu, kumjua Mungu, na kumwelewa Mungu. Hali hii inasikitisha!

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 16)

Mwelekeo wa Mungu kwa Wale Wanaotoroka Wakati Kazi Yake Inaendelea

Utampata mtu wa aina hii kila pahali: Baada ya kuwa na hakika kuhusu njia ya Mungu, kwa sababu mbalimbali, wanaondoka kimyakimya bila ya neno la kwaheri na kufanya chochote kile ambacho moyo wao unatamani. Huku haya yakiendelea, hatutaingilia kwa nini mtu huyu anaondoka. Kwanza tutaangalia mwelekeo wa Mungu ni upi kwa mtu wa aina hii. Iko wazi sana! Tangu muda ule ambao mtu huyu huondoka, machoni mwa Mungu, kile kipindi cha imani yao kimekwisha. Si mtu huyu aliyekimaliza, bali ni Mungu. Kwamba mtu huyu alimwacha Mungu inamaanisha kwamba tayari amemkataa Mungu, kwamba tayari hamtaki Mungu. Inamaanisha kwamba tayari hakubali wokovu wa Mungu. Kwa sababu mtu huyu hamtaki Mungu, Mungu naye anaweza bado kumtaka? Aidha wakati mtu huyu anao mwelekeo huu, mtazamo huu, na anayo azma ya kumwacha Mungu, tayari ameikera tabia ya Mungu. Hata ingawa hawakujipata wakiwa na hasira na wakalaani Mungu, hata ingawa hawakujihusisha katika uovu wowote au tabia au utovu wa nidhamu, na hata ingawa mtu huyu hafikirii: Kama kutawahi kuwepo na siku nitakapokuwa nimeshiba anasa zangu kwa nje, au nitakapokuwa bado nahitaji kitu kutoka kwa Mungu, nitarudi. Au kama Mungu ataniita, nitarudi. Au wanasema: Kama nitajeruhiwa kwa nje, nikiuona ulimwengu wa nje una giza sana na una maovu sana na sitaki tena kujishirikisha nao, nitarudi kwa Mungu. Hata ingawa mtu huyu amepiga hesabu katika akili zake ni wakati gani anarudi, hata ingawa wanauacha mlango ukiwa wazi wa kurudi kwao, hawatambui kwamba bila kujali ni namna gani wanavyofikiria na namna gani wanavyopanga, hii ni ndoto tu. Kosa lao kubwa zaidi ni kutokuwa wazi kuhusu namna ambavyo Mungu anahisi wakati wanapotaka kuondoka. Kuanzia muda ule ambao mtu huyu anaamua kumwacha Mungu, Mungu amemwacha kabisa; tayari Mungu ameanzisha matokeo katika moyo Wake. Matokeo hayo ni yapi? Kwamba mtu huyu ni mmoja wa buku, na ataangamia pamoja nao. Hivyo basi, watu mara nyingi huona aina hii ya hali: Mtu anamwacha Mungu, lakini hapokei adhabu yoyote. Mungu hufanya kazi kulingana na kanuni Zake binafsi. Watu wanaweza kuona baadhi ya mambo, na baadhi ya mambo yanahitimishwa tu katika moyo wa Mungu, kwa hivyo watu hawawezi kuyaona matokeo. Kile ambacho watu huona si lazima kiwe ndio upande wa ukweli wa mambo; lakini upande ule mwingine, ule upande usiouona—hizi ndizo fikira na hitimisho la kweli kuhusu moyo wa Mungu.

Watu Wanaotoroka Wakati wa Kazi ya Mungu ni Wale Wanaoiacha Njia ya Kweli

Hivyo basi kwa nini Mungu ampe mtu wa aina hii adhabu kali kama hiyo? Kwa nini Mungu anakuwa na hasira kali kwao? Kwanza kabisa tunajua kwamba tabia ya Mungu ni adhama, ni hasira. Yeye si kondoo ili achinjwe na yeyote; na hata zaidi Yeye si kikaragosi ili adhibitiwe na watu vyovyote vile wanavyotaka. Yeye pia si hewa tupu ili kuamrishwa huku na kule na watu. Kama kweli unasadiki kwamba Mungu yupo, unafaa kuwa na moyo unaomcha Mungu, na unafaa kujua kwamba kiini halisi cha Mungu hakifai kughadhabishwa. Ghadhabu hii inaweza kusababishwa na neno; pengine fikira; pengine aina fulani ya tabia bovu; pengine tabia ya upole tabia inayoweza kuruhusiwa kwenye macho na maadili ya binadamu; au pengine inasababishwa na falsafa, nadharia. Hata hivyo, punde unapomghadhabisha Mungu, fursa yako inapotea na siku zako za mwisho zinakuwa zimewasili. Hili ni jambo baya! Kama huelewi kwamba Mungu hawezi kukosewa, basi pengine humchi Mungu, na pengine unamkosea Yeye kila wakati. Kama hujui namna ya kumcha Mungu, basi huwezi kumcha Mungu, na hutaweza kujua namna ya kujiweka kwenye njia ya kutembelea kwa njia ya Mungu—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Punde unapokuwa na habari, unaweza kuwa na ufahamu kwamba Mungu hawezi kukosewa, kisha utajua ni nini maana ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kutembea katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu si lazima kuumaanishe ni kiwango kipi cha ukweli unachojua, ni majaribio mangapi ambayo umepitia, au ni mitihani mingapi ambayo umepitia na kutiwa adabu. Badala yake, kunategemea aina ya mtazamo ulio nao kwa Mungu moyoni mwako, na kiini unachokionyesha. Kiini halisi cha watu na mielekeo yao ya kibinafsi—mambo haya ni muhimu sana, muhimu kabisa. Kuhusiana na wale watu ambao wamemkana na kumwacha Mungu, mwelekeo wao wa dharau kwa Mungu na mioyo yao inayodharau ukweli ulikera tabia ya Mungu, hivyo basi kulingana na Mungu hawatawahi kusamehewa. Wamejua kuhusu uwepo wa Mungu, wamekuwa na taarifa kwamba Mungu tayari amewasili, wameweza hata kupitia kazi mpya ya Mungu. Kuondoka kwao si kutokana na kudanganywa, wala si suala kwamba wao wamechanganyikiwa kulihusu. Hata si suala hata kidogo la wao kulazimishwa kuondoka. Lakini kwa nadhari yao, na kwa akili iliyo wazi, wamechagua kumwacha Mungu. Kuondoka kwao si kupotea kwao; si hata kutupwa kwao nje. Hivyo basi, katika macho ya Mungu, wao si kondoo aliyepotea njia kutoka kwenye kondoo wale wengine, sikuambii hata mtoto wa kiume mbadhirifu aliyepotea njia yake. Waliondoka bila hofu ya kuadhibiwa, na hali kama hiyo, mfano kama huo unaikera tabia ya Mungu na ni kutokana na kero hili ambapo Yeye huwapa matokeo yasiyo na matumaini. Je, huoni kwamba matokeo kama haya yanatisha? Hivyo basi kama watu hawamjui Mungu, wanaweza kumkosea Mungu. Hilo ni suala dogo! Kama mtu hatachukulia mwelekeo wa Mungu kwa umakinifu, na bado anasadiki kwamba Mungu angali anatarajia kurudi kwake—kwa sababu wao ni mojawapo wa kondoo wa Mungu waliopotea na kwamba Mungu angali anawasubiria kubadilisha moyo wao—basi mtu huyu hayupo mbali sana na kuweza kuondolewa kwenye siku yake ya adhabu. Mungu hatakataa tu kumkaribisha. Hii ndiyo mara yake ya pili ya kuikera tabia ya Mungu; hivyo basi suala hili ni baya zaidi! Mwelekeo wa mtu huyu usioheshimu vitu vitakatifu tayari umekosea agizo la kiutawala la Mungu. Bado Mungu atawakaribisha? Kwa moyo Wake, kanuni za Mungu kuhusiana na suala hili ni kwamba mtu amefikia uhakika kuhusu ni ipi ndiyo njia ya kweli, ilhali anaweza bado kwa nadhari yake na kwa akili wazi kumkataa Mungu, na kuondoka kutoka kwa Mungu, basi Mungu atazuia kabisa barabara iendayo katika wokovu wake, na hata lango la kuingia kwenye ufalme watafungiwa. Wakati mtu huyu atakapokuja kubisha kwa mara nyingine, Mungu hatamfungulia lango. Mtu huyu atafungiwa milele. Pengine baadhi yenu mmeisoma hadithi hii ya Musa kwenye Biblia. Baada ya Musa kupakwa mafuta na Mungu, viongozi 250 walionyesha ukosefu wa utiifu kwa Musa kwa sababu ya hatua zake na sababu nyinginezo mbalimbali. Ni nani waliyekataa kumtii? Hakuwa Musa. Walikataa kutii mipango ya Mungu; walikataa kutii kazi ya Mungu katika suala hili. Walisema yafuatayo: “Ninyi mnachukua mengi kwenu, kwa sababu mkusanyiko wote ni mtakatifu, kila mmoja wao, naye Yehova yuko miongoni mwao….” Katika macho yenu, maneno haya ni mazito? Si mazito! Angaa maana ya moja kwa moja ya maneno haya si mazito. Katika mkondo wa kisheria, hawavunji sheria zozote, kwa sababu kwenye sehemu ya juu kabisa si lugha katili, au msamiati, isitoshe, hayana maana yoyote ya kukufuru. Sentensi ya kawaida ndiyo iliyo hapo, hamna cha ziada. Ilhali inakuwaje kwamba maneno haya yanaweza kuanzisha hasira kali kama hiyo kutoka kwa Mungu? Ni kwa sababu hayasemwi kwa watu, mbali kwa Mungu. Mwelekeo na tabia iliyoelezewa na wao ndicho hasa kinachoikera tabia ya Mungu, na wao wanaikosea tabia ya Mungu ambayo haipaswi kukosewa. Sote tunajua matokeo yao hatimaye yalikuwa yapi. Kuhusiana na wale waliomwacha Mungu, mtazamo wao ni upi? Mwelekeo wao ni upi? Na ni kwa nini mtazamo na mwelekeo wao unasababisha Mungu kuwashughulikia kwa njia hiyo? Sababu ni kwamba wanajua waziwazi Yeye ni Mungu ilhali bado wanachagua kumsaliti Yeye. Na ndiyo maana wanaondolewa kabisa fursa yao ya wokovu. Kama vile Biblia inavyosema: “Kwa sababu tukitenda dhambi makusudi baada ya sisi kupokea maarifa ya ukweli, hakuna tena dhabihu ya dhambi.” Je, mmelielewa suala hili sasa?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 17)

Majaliwa ya Binadamu Yanaamuliwa na Mwelekeo Wake Kwa Mungu

Mungu ni Mungu aliye hai, na kama vile tu watu wanavyotenda tofauti katika hali tofauti, ndivyo mwelekeo wa Mungu ulivyo katika utendakazi huu na unavyotofautiana kwa sababu Yeye si kikaragosi, wala Yeye si hewa tupu. Kupata kuujua mwelekeo wa Mungu ni jambo lenye thamani kwa wanadamu. Watu wanafaa kujifunza vipi, kwa kuujua mwelekeo wa Mungu, wanaweza kuijua tabia ya Mungu na kuuelewa moyo Wake kidogo kidogo. Unapouelewa moyo wa Mungu kidogo kidogo hutahisi kwamba kumcha Mungu na kujiepusha na maovu ni jambo gumu la kutimiza. Kilicho zaidi ni kwamba, unapomwelewa Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kufanya hitimisho kuhusu Yeye. Unapoacha kufanya hitimisho kuhusu Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kumkosea Yeye, na bila kujua Mungu atakuongoza kuwa na maarifa Yake, na hivyo basi utamcha Mungu katika moyo wako. Utaacha kumfafanua Mungu kwa kutumia falsafa, zile barua, na nadharia ambazo umejifunza. Badala yake, kwa kutafuta nia za Mungu katika mambo yote na siku zote utaweza bila kufahamu kuwa mtu anayefuata moyo wa Mungu.

Kazi ya Mungu haionekani wala kugusika na wanadamu, lakini kulingana na Mungu, hatua za kila mmoja, pamoja na mwelekeo wake kwake Yeye—haya hayatambuliki tu na Mungu, lakini pia kuonekana vilevile. Hili ni jambo ambalo kila mmoja anafaa kutambua na kuwa wazi kulihusu. Unaweza kuwa ukijiuliza siku zote: “Je, Mungu anajua kile ninachofanya hapa? Je, Mungu anajua kile ninachofikiria sasa hivi? Pengine Anajua, pengine Hajui.” Kama utakuwa na aina hii ya mtazamo, kufuata na kusadiki Mungu ilhali unatia shaka katika kazi Yake na uwepo Wake, basi hivi karibuni au baadaye siku itawadia ambapo utamghadhabisha, kwa sababu tayari unayumbayumba pembezoni pa jabali hatari. Nimewaona watu ambao wamesadiki katika Mungu kwa miaka mingi lakini bado hawajapata uhalisia wa ukweli, wala hawaelewi hata mapenzi ya Mungu. Maisha yao na kimo chao havipigi hatua yoyote, ukitii tu falsafa zile za kiwango cha chini zaidi. Hii ni kwa sababu watu hawa hawajawahi kuchukulia neno la Mungu kama maisha yao binafsi, na hawajawahi kukabiliana na kukubali uwepo Wake. Je, unafikiri kwamba Mungu huwaona watu kama hawa na kujawa na furaha? Je, wanamtuliza Yeye? Katika jinsi hiyo, ni mbinu ya imani ya watu katika Mungu ambayo inaamua majaliwa yao. Kuhusu jinsi watu humtafuta na jinsi wanavyomweleka Mungu, mitazamo ya watu ni ya umuhimu wa kimsingi. Usimwache Mungu kana kwamba yeye ni fungu la hewa kavu tu linaloelea karibu na nyuma ya kichwa chako. Usikose kumjali Mungu ni kana kwamba Yeye ni hewa tupu nyuma ya kichwa chako. Siku zote fikiria kuhusu Mungu wa imani yako kama Mungu hai, Mungu halisi. Yeye hayupo kule juu kwenye mbingu ya tatu bila chochote cha kufanya. Badala yake, siku zote bila kusita Anaangalia kwenye mioyo ya kila mmoja, Akiangalia ni nini unachofanya, akichunguza kila neno dogo na kila tukio dogo, akiangalia mwenendo wako na mwelekeo wako kwa Mungu. Kama uko radhi kujitolea kwa Mungu au la, tabia yako yote na fikira zako na mawazo yako ya ndani zaidi ziko mbele ya Mungu, na yanaangaliwa na Yeye. Ni kulingana na tabia yako, kulingana na vitendo vyako, na kulingana na mwelekeo wako kwa Mungu, ambapo maoni Yake kwako, na mwenendo Wake kwako, vinaendelea vikibadilika. Mimi Ningependa kutoa ushauri fulani kwa baadhi ya watu. Msijiweke kwenye mikono ya Mungu kama watoto wachanga, kana kwamba Yeye Anapaswa kukupenda sana, kana kwamba Asingewahi kukuacha, na kana kwamba mwelekeo Wake kwako ni imara na usingeweza kubadilika, na Ninawashauri muache kuota ndoto! Mungu ni mwenye haki katika kutendea kila mtu. Anakabiliana na kazi ya ushindi wa wanadamu na wokovu kwa bidii. Huo ndio usimamizi Wake. Anashughulikia kila mmoja kwa umakinifu, na wala si kama kiumbe cha kufugwa cha kucheza nacho. Upendo wa Mungu kwa binadamu si ule wa kudekeza au kupotosha; rehema na uvumilivu Wake kwa wanadamu si dokezi au ya kutotilia maanani. Kinyume cha mambo, upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wa kutunza, kusikitikia, na kuheshimu maisha; rehema na uvumilivu Wake vyote vinaonyesha matarajio Yake kwa binadamu; rehema na uvumilivu Wake ndivyo ambavyo binadamu anahitaji ili kuishi. Mungu yuko hai, na kwa hakika Mungu yupo; mwelekeo Wake kwa wanadamu unafuata kanuni, si yenye kutangazwa kama imani ya dini, na unaweza kubadilika. Mapenzi Yake kwa binadamu yanabadilika kwa utaratibu na kurekebishwa kwa muda, hali na mwelekeo wa kila mtu. Kwa hiyo, unafaa kujua rohoni mwako na uwazi wote kwamba kiini halisi cha Mungu hakibadiliki, na kwamba tabia Yake itajitokeza katika nyakati tofauti, na muktadha tofauti. Huenda usifikirie kwamba hili si suala muhimu, na wewe unatumia dhana zako za kibinafsi katika kufikiria namna ambavyo Mungu anafaa kufanya mambo. Lakini zipo nyakati ambapo kinyume kabisa cha mtazamo wako ni kweli, na kwa kutumia dhana zako za kibinafsi katika kujaribu na kumpima Mungu, tayari umemghadhabisha. Hii ni kwa sababu Mungu hafanyi kazi kama unavyofikiria wewe, Naye Mungu hatalishughulikia suala hili kama vile unavyosema Atalishughulikia. Na hivyo basi Nakukumbusha kuwa makini na mwenye hekima katika mtazamo wako katika kila kitu, na ujifunze namna ya kufuata kanuni ya kutembea kwenye njia ya Mungu katika mambo yote—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Lazima uimarishe uelewa dhabiti katika masuala ya mapenzi ya Mungu na mwelekeo wa Mungu; kutafuta watu walio na nuru kuuwasilisha kwako, na kutafuta kwa dhati. Usimwone Mungu wa imani yako kama kikaragosi—kuhukumu kiholela, kufikia hitimisho kiholela, kutomshughulikia Mungu kwa heshima Anayostahili. Katika mchakato wa wokovu wa Mungu Anapofafanua matokeo yako, bila kujali kama Yeye atakupa rehema, au uvumilivu, au hukumu na kuadibu, mwelekeo Wake kwako wewe unabadilika. Inategemea na mwelekeo wako kwa Mungu, na uelewa wako wa Mungu. Usiache dhana moja ya kupita ya maarifa au uelewa wako katika Mungu kumfafanua Yeye daima. Usisadiki katika Mungu aliyekufa; amini kwa yule aliye hai. Kumbuka hili! Ingawa Nimezungumzia ukweli fulani hapa, ukweli mliohitaji kusikia, kwa mujibu wa hali yenu ya sasa na kimo chenu cha sasa, Sitatoa mahitaji yoyote makubwa zaidi ili nisije nikaiondoa shauku yenu. Kufanya hivyo kutajaza mioyo yenu na huzuni na simanzi, na kuwafanya nyinyi kuhisi masikitiko mengi mno kwa Mungu. Badala yake Natumai kwamba mnaweza kutumia upendo wa Mungu katika mioyo yenu, na kutumia mwelekeo ambao ni wa heshima kwa Mungu wakati mnapotembea kwenye njia iliyo hapo mbele. Usimalizie suala la jinsi ya kushughulikia imani ya Mungu kwa kubahatisha. Lishughulikie kama mojawapo ya maswali makubwa zaidi yaliyopo. Liwekeni kwenye mioyo yenu, litieni kwenye matendo, unganeni nalo kupitia kwa maisha halisi—msikubaliane nalo kwa maneno pekee. Kwani hili ni suala la uzima na mauti, na ndilo ambalo litaamua hatima yako. Usilichukulie kama mzaha, kama mchezo wa mtoto! Baada ya kuwaambia maneno haya leo, Najiuliza mavuno ya uelewa yamekuwa nini katika akili zenu? Kunayo maswali yoyote ambayo ungependa kuuliza kuhusu kile Nilichokisema leo?

Ingawa mada hizi ni mpya kidogo, na zimeondolewa kidogo kutoka kwenye mitazamo yenu na kile ambacho kwa kawaida mnafuatilia na kutilia maanani, Nafikiria kwamba baada ya mada hizi kuwasilishwa kwa kipindi cha muda, mtaimarisha uelewa mzuri wa kila kitu Nilichosema hapa. Kwa sababu hizi ni mada mpya, mada ambazo hujawahi kufikiria awali, Ninatumai kwamba hazitaongezea mzigo kwako. Ninaongea maneno haya leo si kwa sababu ya kuwatishia nyinyi, wala Sijaribu kukushughulikia wewe; badala yake, nia Yangu ni kukusaidia kuelewa ukweli wa hoja. Kwa vyovyote vile, kunao umbali kati ya wanadamu na Mungu. Ingawa binadamu anaamini katika Mungu, hajawahi kumwelewa Mungu; hajawahi kujua mitazamo ya Mungu. Binadamu pia hajawahi kuwa na shauku katika kuujali mwelekeo wa Mungu. Badala yake, amesadiki kwa kutojua, ameendelea mbele kwa kutojua na amekosa kumakinika katika maarifa na uelewa wake wa Mungu. Hivyo basi Nahisi mshawasha wa kuyafumbua masuala haya kwa niaba yenu na kuwasaidia kuelewa huyu Mungu unayemsadiki hasa ni Mungu wa aina gani; kile Anachofikiria; mwelekeo Wake ni nini katika kushughulikia Kwake kwa watu wa aina tofauti; uko mbali kiasi gani kukamilisha mahitaji Yake; na tofauti iliopo kati ya hatua zako na kiwango anachohitaji Yeye. Shabaha katika kujua kwako haya ni kuwapa kigezo cha kupimia kwenye mioyo yenu ambacho mtaweza kupimia dhidi ya na kujua barabara mnayotembelea imewaelekeza katika mavuno aina gani, kile ambacho hamjapata kwenye barabara hii, na sehemu zile ambazo hamjajihusisha kwazo. Wakati mnawasiliana miongoni mwa nyinyi wenyewe, kwa kawaida mnazungumzia mada chache zinazungumziwa kwa kawaida; upana huo wa kazi ni mwembamba, na maudhui ni ya juujuu sana. Kunao umbali, nafasi, kati ya kile ambacho mnazungumzia na nia za Mungu, katikati ya mazungumzo yenu na upana na kiwango cha mahitaji ya Mungu. Kuendelea hivi baada ya muda kutawafanya kupotoka zaidi na zaidi kutoka kwenye njia ya Mungu. Mnayachukua tu maneno yaliyopo kutoka kwa Mungu na kuyageuza kuwa vifaa vya kuabudu, kuwa kaida za dini na utaratibu. Hayo tu ndiyo maana yake! Kwa hakika, Mungu hana nafasi kamwe katika mioyo yenu, na Mungu hajawahi kuipata mioyo yenu. Baadhi ya watu hufikiria kwamba kumjua Mungu ni vigumu sana—huu ndio ukweli. Ni vigumu! Kama watu wataambiwa kutekeleza wajibu wao na kuhakikisha kwamba mambo yanatendeka kwa nje, kama wataulizwa kutia bidii, basi watu watafikiria kwamba kusadiki Mungu ni jambo rahisi sana, kwa sababu haya yote yanapatikana katika ule upana wa uwezo wa binadamu. Ilhali punde tu mada hizo zinaposonga kuelekea kwenye maeneo ya nia za Mungu na mwelekeo wa Mungu kwa binadamu, basi mambo yanapata kuwa magumu zaidi kwa watu wote. Hiyo ni kwa sababu yote haya yanahusisha uelewa wa ukweli na kuingia kwao katika uhalisia; bila shaka kuna kiwango cha ugumu. Lakini baada ya wewe kuingia kupitia mlango wa kwanza, baada ya wewe kuanza kuingia ndani yake, mambo yanaanza kuwa rahisi na rahisi kwa utaratibu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 18)

Sehemu ya Mwanzo ya Kumcha Mungu ni Kumtendea Kama Mungu

Mtu fulani amelizua swali hivi punde: Inakuwaje kwamba tunajua zaidi kuhusu Mungu kuliko alivyojua Ayubu, ilhali bado hatuwezi kumcha Mungu? Tuliligusia suala hili hapo awali kidogo, sivyo? Kwa hakika, kiini halisi cha swali hili kimeweza pia kuzungumziwa awali kwamba ingawa Ayubu hakumjua Mungu wakati huo, alimshughulikia Yeye kama Mungu, na kumchukulia Yeye kama Bwana wa mambo yote mbinguni na nchini. Ayubu hakumchukulia Mungu kuwa adui. Badala yake, alimwabudu Yeye kama Muumba wa viumbe vyote. Watu siku hizi wanampinga Mungu sana kwa nini? Kwa nini hawawezi kumcha Mungu? Sababu moja ni kwamba wamepotoshwa pakubwa na Shetani. Wakiwa na asili yao ya kishetani ikiwa imekita mizizi ndani, watu wanageuka na kuwa adui wa Mungu. Hivyo basi, hata ingawa wanasadiki katika Mungu na kumtambua Mungu, bado wanaweza kumpinga Mungu na kujiweka katika nafasi ya upinzani na Yeye. Hili linaamuliwa na asili ya binadamu. Sababu nyingine ni kwamba ingawa watu wanasadiki Mungu, hawamchukulii Yeye tu kama Mungu. Badala yake, wanamchukulia Mungu kuwa ndiye anayempinga binadamu, wakimwona Yeye kuwa adui wa binadamu, na hawawezi kupatanishwa na Mungu. Ni rahisi hivyo. Je, jambo hili halikuzungumziwa kwenye kikao cha awali? Hebu fikiria: Hiyo ndiyo sababu? Ingawa unayo maarifa kidogo ya Mungu, maarifa haya hasa ni nini? Haya siyo yale kila mtu anazungumzia? Haya si yale ambayo Mungu alikuambia? Unajua tu zile dhana za kinadharia na kifalsafa; umewahi kupitia dhana halisi ya Mungu? Je, unayo maarifa ya kibinafsi? Je, unayo maarifa na uzoefu wa kimatendo? Kama Mungu asingekuambia, ungelijua hili? Maarifa yako katika nadharia hayawakilishi maarifa halisi. Kwa ufupi, bila kujali ni kiwango kipi unachojua na ni vipi ulivyokijua hatimaye, kabla ya wewe kufikia uelewa halisi wa Mungu, Mungu ndiye adui wako, na kabla ya wewe kumshughulikia Mungu hivyo, Amewekwa kuwa mpinzani wako, kwani wewe ni mfano halisi wa Shetani.

Unapokuwa pamoja na Kristo, pengine unaweza kumhudumia kwa milo mitatu kwa siku, pengine kumhudumia Yeye kwa chai, kuyashughulikia mahitaji Yake ya maisha, ni kana kwamba unamshughulikia Kristo kama Mungu. Kila wakati jambo linapofanyika, mitazamo ya watu siku zote inakuwa kinyume cha mtazamo wa Mungu. Siku zote wanashindwa kuelewa mtazamo wa Mungu, na wanashindwa kuukubali. Ingawa watu wanaweza kupatana na Mungu juujuu, hii haimaanishi kwamba wanalingana na Yeye. Punde tu jambo linapofanyika, ukweli wa kutotii kwa binadamu unaibuka, na kuthibitisha ukatili uliopo kati ya binadamu na Mungu. Ukatili huu si wa Mungu kumpinga binadamu; si Mungu kutaka kuwa katili kwa binadamu, na si Mungu kumweka binadamu katika upinzani na kumshughulikia binadamu hivyo. Badala yake, ni hali ya upinzani huu wa kiini halisi kwa Mungu ambao unajificha katika mapenzi ya kibinafsi ya binadamu, na katika akili ya kutofahamu ya binadamu. Kwa sababu binadamu anachukulia kila kitu kinachotoka kwa Mungu kama kifaa cha utafiti wake, mwitikio wake kwa hiki ambacho kinatoka kwa Mungu na kile ambacho kinamhusisha Mungu ni, zaidi ya yote, kukisia, na kushuku, na kisha haraka sana kuingia katika mwelekeo ambao unakinzana na Mungu, na unapingana na Mungu. Baada ya hapo, binadamu atachukua hali hizi za moyo za kimyakimya na kuzua mjadala na Mungu au kushindana na Mungu hadi kufikia kiwango ambacho atatia shaka kama Mungu wa aina hii anastahili kufuatwa. Licha ya hoja kwamba urazini wa binadamu unamwambia asiendelee hivi, bado atachagua kufanya hivyo licha ya kutotaka kufanya hivyo, kiasi kwamba ataendelea bila kusita hadi mwisho. Kwa mfano, ni nini mwitikio wa kwanza kwa baadhi ya watu wanaposikia uvumi fulani au matusi fulani kumhusu Mungu? Mwitikio wa kwanza ni: Sijui kama uvumi huu ni kweli au la, kama upo ama haupo, hivyo basi nitasubiri na kuona. Kisha wanaanza kutafakari: Hakuna njia ya kuthibitisha haya; ipo kweli? Uvumi huu ni kweli au la? Ingawa mtu huyu haonyeshi juujuu, moyo wake tayari umeanza kutia shaka, tayari umeanza kumkataa Mungu. Ni nini kiini halisi cha aina hii ya mwelekeo, aina hii ya mtazamo? Je huu si usaliti? Kabla ya wao kukumbwa na suala, huwezi kuona mtazamo wa mtu huyu ni nini—yaonekana ni kana kwamba wao hawakinzani na Mungu, ni kama hawamchukulii Mungu kuwa adui. Hata hivyo, punde wanapokumbwa na suala hilo, wanasimama mara moja na Shetani na kumpinga Mungu. Hali hii inapendekeza nini? Inapendekeza kwamba binadamu na Mungu wanapingana! Si kwamba Mungu anamchukulia binadamu kama adui, lakini kwamba kile kiini halisi chenyewe cha binadamu ni kikatili kwa Mungu. Haijalishi ni kwa muda mrefu vipi ambapo mtu humfuata Mungu, ni kiwango kipi anacholipia; haijalishi vipi ambavyo mtu anamsifu Mungu, anavyojihifadhi dhidi ya kumpinga Mungu, hata akijisihi kumpenda Mungu, hatawahi kufaulu kumshughulikia Mungu kama Mungu. Si hali hii inaamuliwa na kiini halisi cha mwanadamu? Kama Utamshughulikia kama Mungu, unaweza kwa kweli kusadiki kwamba Yeye ni Mungu, unaweza bado kuwa na shaka lolote kwake Yeye? Bado kunaweza kuwa na maswali yoyote yanayomhusu Yeye katika moyo wako? Hakuwezi. Mitindo ya ulimwengu huu ni miovu kweli, na wanadamu wa kizazi hiki pia, hivyo, inawezekanaje kwamba huna fikira zozote kuzihusu? Wewe mwenyewe umejaa uovu, hivyo inakuwaje kwamba huna fikira zozote kuhusu hayo? Ilhali uvumi mchache tu, matusi fulani yanaweza kusababisha dhana kubwa mno kumhusu Mungu, zinaweza kuleta mawazo mengi mno, hali inayoonyesha vile ambavyo kimo chako kilivyo bado kichanga! “Mnong’ono” tu wa mbu wachache, nzi wachache wabaya, hilo tu ndilo linalokupotosha? Huyu ni mtu wa aina gani? Je, unajua anachofikiria Mungu kuhusu mtu wa aina hii? Mwelekeo wa Mungu kwa hakika uko wazi sana kuhusiana na ni vipi Anavyowashughulikia watu hawa. Ni kwa sababu tu kwamba ushughulikiaji wa Mungu kwa watu hawa ni kuwapuuza—mwelekeo Wake ni kutowatilia maanani, na kutomakinikia watu hawa wasiojua. Kwa nini hivyo? Kwa sababu katika moyo Wake Hakuwahi kupangilia kuhusu kupata watu hao ambao wameahidi kuwa wakatili kwake Yeye hadi mwisho, na ambao hawajawahi kupangilia kutafuta njia ya uwiano na Yeye. Pengine maneno haya Niliyoyaongea yamewaumiza watu wachache. Kwa kweli, mko radhi kuniruhusu Mimi kuwadhuru siku zote namna hii? Bila kujali kama mko radhi au la, kila kitu Ninachosema ni ukweli! Kama siku zote Ninawadhuru namna hii, siku zote Nafichua makovu yenu, je, itaathiri taswira za majivuno kuhusu Mungu katika mioyo yenu? (Haitaathiri.) Ninakubali kwamba haitaathiri kwani kwa ufupi hakuna Mungu katika mioyo yenu. Yule Mungu wa majivuno anayepatikana ndani ya mioyo yenu, yule mnayemtetea kwa dhati na kulinda, kwa ufupi si Mungu. Badala yake ni ndoto ya kufikiria kwa binadamu; kwa ufupi haipo. Hivyo basi ni bora zaidi kama Nitafichua jibu la kitendawili hiki. Je, huu si ukweli wote? Mungu halisi hatokani na kufikiria kwa binadamu. Natumai kwamba nyote mnaweza kukabiliana na uhalisia huu, na utawasaidia katika maarifa yenu ya Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 19)

Wale Watu Wasiotambuliwa na Mungu

Kunao baadhi ya watu ambao imani yao haijawahi kutambuliwa katika moyo wa Mungu. Kwa maneno mengine, Mungu hatambui kwamba watu hawa ni wafuasi Wake, kwa sababu Mungu haisifu imani yao. Kwa watu hawa, haijalishi wamemfuata Mungu kwa miaka mingapi, mawazo na mitazamo yao haijawahi kubadilika. Wao ni kama wasioamini, wanatii kanuni na njia ambayo wasioamini wanafanya mambo yao, kutii sheria zao za kusalia na imani. Hawakuwahi kukubali neno la Mungu kama maisha yao, hawakuwahi kusadiki kwamba neno la Mungu ni ukweli, hawakuwahi kunuia kukubali wokovu wa Mungu, na hawakuwahi kutambua Mungu kama Mungu wao. Wanachukulia kusadiki Mungu kuwa uraibu fulani wa wanagenzi, wakishughulikia Mungu kama riziki ya kiroho, hivyo basi hawafikirii kwamba ipo thamani ya kujaribu na kuelewa tabia ya Mungu, au kiini halisi cha Mungu. Unaweza kusema kwamba kila kitu kinacholingana na Mungu wa kweli hakihusiani kwa vyovyote vile na watu hawa. Hawana hamu yoyote, na hawawezi kusumbuliwa kutilia maanani. Hii ni kwa sababu ndani kabisa ya mioyo yao kunayo sauti ya nguvu ambayo siku zote inawaambia: Mungu haonekani na hagusiki, na Mungu hayupo. Wanasadiki kwamba kujaribu kumwelewa Mungu wa aina hii hakutastahili jitihada zao; itakuwa sawa na wao kujidanganya. Wao wanaamini tu kwa kumtambua Mungu kwa maneno tu bila kuchukua msimamo wowote halisi au kujiweka ndani yao kupitia vitendo halisi, wao wanakuwa werevu sana. Mungu anachukulia vipi watu kama hawa? Anawachukulia kuwa wasioamini. Baadhi ya watu huuliza: “Je, wasioamini wanaweza kulisoma neno la Mungu? Je, wanaweza kutekeleza wajibu wao? Je, wanaweza kuyasema maneno haya: ‘Nitaishi kwa ajili ya Mungu’?” Kile ambacho binadamu huona mara nyingi ni maonyesho ya juujuu tu ya watu, na wala si kiini chao halisi. Ilhali Mungu haangalii maonyesho haya ya juujuu; Yeye huona tu kiini chao halisi cha ndani. Hivyo basi, Mungu anao mwelekeo wa aina hii, ufafanuzi wa aina hii, kwa watu kama hawa. Kuhusiana na kile ambacho watu hawa husema: “Kwa nini Mungu hufanya hivi? Kwa nini Mungu hufanya vile? Siwezi kuelewa haya; siwezi kuelewa yale; haya hayaingiliani na fikira za binadamu; Lazima unielezee haya; …” Jibu langu ni: Inahitajika kuelezea suala hili kwako? Je, suala hili lina chochote kuhusiana na wewe? Unafikiria wewe ni nani? Ulitokea wapi? Umefuzu kumwelekeza Mungu? Je, unamwamini Yeye? Je, Anatambua imani yako? Kwa sababu imani yako haina chochote kuhusiana na Mungu, matendo Yake yana uhusiano gani na wewe? Hujui pale ulipo katika moyo wa Mungu, ilhali umefuzu kuzungumza na Mungu?

Maneno ya Maonyo

Hamhisi vibaya baada ya kusikia matamshi haya? Ingawa huenda msiwe radhi kusikiliza maneno haya, au msiwe radhi kuyakubali, yote ni uhakika. Kwa sababu awamu hii ya kazi ni ya Mungu kutenda, kama hujali nia za Mungu, hujali mwelekeo wa Mungu na huelewi kiini halisi na tabia ya Mungu, basi hatimaye wewe ndiwe utakayekosa kufaidi. Msiyalaumu maneno yangu kwa kuwa magumu kusikiliza, na msiyalaumu kwa kupunguza majivuno ya shauku yenu. Mimi naongea ukweli; na wala Sinuii kuwavunja moyo. Haijalishi ni nini Ninachowauliza ninyi, na haijalishi ni vipi mnavyohitajika kukifanya, Ninatumai kwamba mtatembelea njia sahihi, na ninatumai kwamba mtafuata njia ya Mungu na wala msipotoke katika njia hii. Kama hutaendelea kulingana na neno la Mungu, na hufuati njia Yake, basi hakutakuwa na shaka kwamba unaasi dhidi ya Mungu na umepotea kutoka kwa njia sahihi. Hivyo basi Nahisi kwamba yapo masuala fulani ambayo lazima Niwabainishie, na kuwafanya kusadiki dhahiri shairi, waziwazi, bila ya tone la mashaka na kuwasaidia waziwazi kujua mwelekeo wa Mungu, nia za Mungu, namna Mungu anavyomfanya binadamu kuwa mtimilifu, na ni kwa njia gani Yeye Hupanga matokeo ya binadamu. Endapo kutakuwa na siku ambayo hutaweza kuanza katika njia hii, basi Sitahitajika kuwajibika kwa vyovyote vile kwa sababu maneno haya tayari yamezungumzwa kwako waziwazi. Kuhusiana na matokeo ya aina tofauti ya watu Mungu Anayo mitazamo tofauti. Anazo njia Zake binafsi za kuwapima, vile vile kama kiwango Chake binafsi cha mahitaji kwao. Kiwango Chake cha kupima matokeo ya watu ni kile ambacho ni chenye haki kwa kila mmoja—hakuna shaka kuhusu hilo. Hivyo basi, woga wa watu fulani hauhitajiki. Je, umepata tulizo la moyo sasa?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 20)

Kwa hakika, tabia ya Mungu iko wazi kwa kila mmoja na haijafichwa, kwa sababu Mungu hajawahi kuepuka kimakusudi mtu yeyote na Hajawahi kimakusudi kujaribu kujificha Mwenyewe ili watu wasiweze kumjua Yeye au kumwelewa Yeye. Tabia ya Mungu siku zote imekuwa wazi na siku zote imekuwa ikitazama kila mtu kwa njia ya uwazi. Katika usimamizi wa Mungu, Mungu hufanya kazi Yake akitazama kila mmoja; na kazi Yake ndiyo inafanywa kwa kila mtu. Anapofanya kazi hii, Anafichua bila kusita tabia Yake, huku Akitumia bila kusita kiini Chake na kile Anacho na alicho kuongoza na kukimu kila mmoja. Katika kila enzi na kila awamu, licha ya kama hali ni nzuri au mbaya, tabia ya Mungu siku zote iko wazi kwa kila mtu binafsi, na vile vitu Anavyomiliki na uwepo Wake siku zote viko wazi kwa kila mtu binafsi, kwa njia sawa kwamba maisha Yake yanamtoshelezea mwanadamu kila wakati na bila kusita na kumsaidia mwanadamu. Licha ya haya yote, tabia ya Mungu inabakia fiche kwa baadhi ya watu. Kwa nini iko hivyo? Ni kwa sababu ingawaje watu hawa wanaishi ndani ya kazi ya Mungu na wanamfuata Mungu, hawajawahi kutafuta kuelewa Mungu au kutaka kumjua Mungu, sikwambii hata kumkaribia Mungu. Kwa watu hawa, kuelewa tabia ya Mungu kunamaanisha mwisho wao wawadia; kwa maanisha karibu wanahukumiwa na kushtakiwa na tabia ya Mungu. Hivyo basi, watu hawa hawajawahi kutamani kuelewa Mungu au tabia Yake, na hawatamani uelewa au maarifa ya kina ya mapenzi ya Mungu. Hawanuii kufahamu mapenzi ya Mungu kupitia ushirikiano wa kimakusudi—wanafurahia tu milele na hawachoki kufanya mambo wanayotaka kuyafanya; kusadiki kwa Mungu wanayetaka kusadiki Kwake; kusadiki kwa Mungu aliyepo tu katika fikira zao, Mungu aliyepo tu katika dhana zao; na kusadiki kwa Mungu asiyeweza kutenganishwa na wao katika maisha yao ya kila siku. Na kwake Mungu Mwenyewe wa kweli, wanapuuza kabisa, hawataki kusikia mambo ya Mungu na hawana tamanio la kumwelewa Yeye, kumtilia maanani Yeye, sembuse kuwa na tamanio la kuwa karibu zaidi na Yeye. Wanayatumia tu maneno ambayo Mungu anayaonyesha ili kuweza kujirembesha, kujiandaa upya. Kwa wao, hilo tayari linawafanya kuwa waumini wenye mafanikio na watu walio na imani kwa Mungu ndani ya mioyo yao. Ndani ya mioyo yao, wanaongozwa na kufikiria kwao, dhana zao, na hata ufasili wao binafsi wa Mungu. Mungu Mwenyewe wa kweli, kwa mkono mwingine, hana chochote kuhusiana na wao. Kwa sababu pindi wanapomwelewa Mungu Mwenyewe wa kweli, kuelewa tabia ya Mungu ya kweli, na kuelewa kile Mungu anacho na alicho, hii inamaanisha kwamba vitendo vyao, imani yao, na yale yote wanayoyafuatilia yatashutumiwa. Na ndiyo maana hawako radhi kukielewa kiini cha Mungu, na ndiyo maana wanasitasita na hawako radhi kutafuta kwa bidii au kuomba kumwelewa zaidi Mungu, kupata kujua zaidi kuhusu mapenzi Yake Mungu, na kuelewa kwa njia bora zaidi tabia ya Mungu. Afadhali Mungu kwao awe kitu kilichotungwa, kitu kisicho na chochote na kisicho dhahiri. Afadhali kwao Mungu awe mtu ambaye yupo hasa vile ambavyo wamemfikiria Yeye, Anayeweza kunyenyekea mbele zao, Asiyeishiwa na ujazo na Anayepatikana siku zote. Wanapotaka kufurahia neema ya Mungu, wanamuomba Mungu kuwa hiyo neema. Wanapohitaji baraka za Mungu, wanamuomba Mungu kuwa baraka hizo. Wanapokabiliwa na dhiki, wanamwomba Mungu kuwatia wao moyo, na kuwa usalama wao. Maarifa ya watu hawa kumhusu Mungu imebakia palepale pa mipaka ya neema na baraka. Uelewa wao wa kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na Mungu umezuiliwa pia na kufikiria kwao na vilevile barua na mafundisho ya kidini tu. Lakini wapo baadhi ya watu walio na hamu ya kuielewa tabia ya Mungu, wanaotaka kumwona Mungu Mwenyewe kwa kweli, na kuielewa tabia ya Mungu kwa kweli na kile Anacho na alicho. Watu hawa wanautafuta uhalisia wa ukweli na wokovu wa Mungu na wanatafuta kupokea ushindi, wokovu, na utimilifu wa Mungu. Watu hawa wanaitumia mioyo yao kulisoma neno la Mungu, wanaitumia mioyo yao kuthamini hali na kila mtu, tukio, au kitu ambacho Mungu amewapangia, na kuomba na kutafuta kwa uaminifu. Kile wanachotaka zaidi ni kuyajua mapenzi ya Mungu na kuielewa tabia ya kweli na kiini cha Mungu. Hivi ndivyo ilivyo ili wasiweze tena kumkosea Mungu, na kupitia kwa mambo waliyoyapitia, waweze kuona upendo zaidi wa Mungu na upande Wake wa kweli. Iko hivyo pia ili Mungu halisi na wa kweli ataweza kuwepo ndani ya mioyo yao, na ili Mungu atakuwa na nafasi katika mioyo yao, kiasi cha kwamba hawatakuwa wakiishi tena miongoni mwa kufikiria, dhana, au hali ya kuyaepuka mambo. Kwa watu hawa, sababu inayowafanya kuwa na tamanio kuu la kuielewa tabia ya Mungu na kiini Chake ni kwa sababu tabia ya Mungu na kiini Chake ni mambo ambayo mwanadamu anaweza kuyahitaji wakati wowote katika uzoefu wao, mambo yanayojaza uhai katika maisha yao yote walioishi. Pindi wanapoielewa tabia ya Mungu, wataweza kumheshimu sana kwa njia bora zaidi, kushirikiana kwa njia bora zaidi na kazi ya Mungu, na kuyaweka zaidi katika fikira mapenzi ya Mungu na kutekeleza wajibu wao kwa njia bora zaidi wakitumia uwezo wao. Hawa ndio watu wa aina mbili inapokuja katika mielekeo yao kwa tabia ya Mungu. Watu wa aina ya kwanza hawataki kuielewa tabia ya Mungu. Ingawaje wanasema wanataka kuielewa tabia ya Mungu, kupata kumjua Mungu Mwenyewe, kuona kile Mungu anacho na alicho, na kushukuru kwa dhati mapenzi ya Mungu, ndani yao kabisa wanaona afadhali Mungu asikuwepo. Ni kwa sababu watu wa aina hii wanakosa kumtii Mungu kila wakati na wanampinga; wanapigana na Mungu kwa sababu ya vyeo vilivyo ndani ya mioyo yao na mara nyingi wanashuku na hata kukataa uwepo wa Mungu. Hawataki kuruhusu tabia ya Mungu au kuacha Mungu mwenyewe wa kweli kumiliki mioyo yao. Wanataka tu kutosheleza matamanio, kufikiria, na maono yao binafsi. Hivyo basi, watu hawa wanaweza kumsadiki Mungu, kumfuata Mungu, na hata wanaweza kutupilia mbali familia na kazi zao kwa sababu Yake Yeye, lakini hawasitishi njia zao za maovu. Baadhi yao hata huiba au kubadhiri sadaka au kumlaani Mungu kisirisiri, huku wengine wakiweza kutumia vyeo vyao kushuhudia mara kwa mara kuhusu wao wenyewe, kujiongezea zaidi umaarufu wao, na kushindana na Mungu kwa ajili ya watu na hadhi. Wanatumia mbinu na njia mbalimbali kuwafanya watu kuwaabudu, kujaribu mara kwa mara kuwa na ufuasi mkubwa wa watu na kutaka kuwadhibiti watu hao. Baadhi hata hupotosha kimakusudi watu na kuwafanya kufikiria kwamba wao ni Mungu ili waweze kuchukuliwa kama Mungu. Hawawezi katu kuwaambia watu kwamba wamepotoshwa, kwamba pia wao wamepotoka na wana kiburi, na hivyo basi hawafai kuwaabudu, na kwamba haijalishi watafanya vyema kiasi kipi, haya yote ni kutokana na utukuzaji wa Mungu na kile wanachostahili kufanya kwa kweli. Kwa nini hawasemi mambo haya? Kwa sababu wana hofu kuu ya kupoteza nafasi yao ndani ya mioyo ya watu. Hii ndiyo maana watu kama hao hawamtukuzi Mungu katu na katu hawamshuhudii Mungu, kwani hawajawahi kujaribu kumwelewa Mungu. Wanaweza kumjua Mungu kama hawamwelewi? Haiwezekani! Hivyo, ingawa maneno katika mada “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe” yanaweza kuwa rahisi, maana yao ni tofauti kwa kila mmoja. Kwa mtu anayekosa kumtii Mungu mara kwa mara, na anampinga Mungu na ni mkatili kwa Mungu, maneno hayo yanabashiri shutuma; ilhali mtu anayefuatilia uhalisi wa kweli na mara nyingi anakuja mbele ya Mungu kutafuta mapenzi ya Mungu atayachukulia maneno hayo kama kawaida yake. Hivyo kuwa wale walio miongoni mwenu, wanaposikiza mazungumzo ya tabia ya Mungu na kazi ya Mungu, wanaanza kuumwa na kichwa, mioyo yao inajaa upinzani, na wanakuwa katika hali isiyo na utulivu kabisa. Lakini kuna wengine miongoni mwenu wanaofikiria: Mada hii ndiyo hasa Ninayohitaji, kwa sababu mada hii ni yenye manufaa sana kwangu. Ni sehemu ambayo haiwezi kukosekana katika uzoefu wangu wa maisha; ni swali ambalo halijapata jibu bado, msingi wa imani kwa Mungu, na jambo ambalo mwanadamu hawezi kufikiria kuliacha. Kwenu nyote, mada hii inaweza kuonekana kuwa karibu na mbali, isiyojulikana ilhali inayozoeleka. Lakini haijalishi ni nini, hii ni mada ambayo kila mmoja lazima aisikilize, aijue, na lazima aielewe. Haijalishi ni vipi utakavyoishughulikia, haijalishi ni vipi utakavyoiangalia au utakavyoipokea, lakini umuhimu wa mada hii huwezi kupuuzwa.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 21)

Mungu amekuwa akifanya kazi Yake tangu Awaumbe wanadamu. Mwanzoni, ilikuwa kazi rahisi sana, lakini licha ya urahisi wake, ingali ilikuwa na maonyesho ya kiini na tabia ya Mungu. Ingawa kazi ya Mungu sasa imepandishwa daraja, na Yeye akitia kiwango kikubwa mno cha kazi thabiti kwa kila mmoja anayemfuata Yeye, na kuonyesha kiwango kikubwa cha neno Lake, kuanzia mwanzo hadi sasa, nafsi ya Mungu imekuwa ikifichwa kutoka kwa mwanadamu. Ingawaje amekuwa mwili mara mbili, kuanzia wakati wa simulizi za biblia hadi kwa siku za kisasa, nani amewahi kuona nafsi halisi ya Mungu? Kutokana na uelewa wenu, yupo mtu amewahi kuona nafsi halisi ya Mungu? La. Hakuna aliyewahi kuona nafsi halisi ya Mungu, kumaanisha hakuna aliyewahi kuona nafsi ya kweli ya Mungu. Hili ni jambo ambalo kila mmoja anakubaliana nalo. Hivi ni kusema, nafsi halisi ya Mungu, au Roho wa Mungu, amefichwa kutoka kwa binadamu wote, wakiwemo Adamu na hawa, ambao Aliwaumba, na akiwemo Ayubu mwenye haki, ambaye alikuwa Amemkubali. Hata wao hawakuona nafsi halisi ya Mungu. Lakini kwa nini Mungu anaficha kimakusudi nafsi Yake halisi? Baadhi ya watu husema: “Mungu anaogopa kuwaogofya watu.” Wengine husema: “Mungu huficha nafsi Yake halisi kwa sababu binadamu ni mdogo sana na Mungu ni mkubwa sana; wanadamu hawaruhusiwi kumwona Yeye, la sivyo watakufa.” Wapo pia wale wanaosema: “Mungu ameshughulika sana akisimamia kazi Yake kila siku, huenda Asiwe na muda wa kuonekana na kuruhusu watu kumwona Yeye.” Haijalishi ni nini mnachosadiki, Ninayo hitimisho hapa. Hitimisho hilo ni nini? Ni kwamba Mungu hataki hata watu kuona nafsi Yake halisi. Akiwa amefichwa kutoka kwa binadamu ni kitu ambacho Mungu anafanya kimakusudi. Kwa maneno mengine, ni nia ya Mungu kwa watu kutoona nafsi Yake halisi. Hili linafaa kuwa wazi kwa wote sasa. Kama Mungu hajawahi kuonyesha nafsi Yake kwa yeyote, basi mnafikiria nafsi ya Mungu ipo? (Ipo.) Bila shaka ipo. Uwepo wa nafsi ya Mungu haupingiki. Lakini kuhusu nafsi ya Mungu ni kubwa vipi au inafanana vipi, haya ni maswali ambayo mwanadamu anafaa kuchunguza? La. Jibu ni la. Kama nafsi ya Mungu si mada ambayo tunafaa kuchunguza, basi ni swali lipi ambalo tunafaa kuchunguza? (Tabia ya Mungu.) (Kazi ya Mungu.) Kabla hatujaanza kuwasiliana mada hii rasmi, hata hivyo, hebu turudi katika kile tulichokuwa tukikizungumzia muda mfupi uliopita: Kwa nini Mungu hajawahi kuonyesha nafsi Yake kwa mwanadamu? Kwa nini Mungu anaficha kimakusudi nafsi Yake kutoka kwa mwanadamu? Kunayo sababu moja tu, nayo ni: Ingawaje binadamu aliyeumbwa amepitia miaka elfu na elfu ya kazi ya Mungu, hakuna hata mtu mmoja anayejua kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na kiini cha Mungu. Watu kama hao, mbele ya macho ya Mungu, ni upinzani kwake Yeye, na Mungu hatajionyesha kwa watu walio wakatili kwake Yeye. Hii ndiyo sababu ya pekee mbona Mungu hajawahi kumwonyesha binadamu nafsi Yake na ndiyo sababu anaikinga yeye kimakusudi nafsi Yake dhidi yao. Sasa mnaelewa kuhusu umuhimu wa kujua tabia ya Mungu?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 22)

Tangu kuwepo kwa usimamizi wa Mungu, siku zote amejitolea kabisa katika kutekeleza kazi Yake. Licha ya kuficha nafsi Yake kutoka kwao, siku zote Amekuwa katika upande wa binadamu, akiwafanyia kazi, akionyesha tabia Yake, akiongoza binadamu wote na kiini Chake, na kufanya kazi Yake kwa kila mmoja kupitia nguvu Zake, hekima Yake, na mamlaka Yake, hivyo akiileta Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na sasa Enzi ya Ufalme katika uwepo. Ingawaje Mungu huificha nafsi Yake kutoka kwa binadamu, tabia Yake, uwepo Wake na miliki Yake, na mapenzi Yake kwa binadamu yanafichuliwa bila wasiwasi wowote kwa binadamu kwa minajili ya kuona na kupitia hali hiyo. Kwa maneno mengine, ingawaje binadamu hawawezi kumwona au kumgusa Mungu, tabia na kiini cha Mungu ambacho binadamu wamekuwa wakigusana nacho ni maonyesho kabisa ya Mungu Mwenyewe. Je, hayo si kweli? Licha ya ni mbinu gani au ni kutoka katika mtazamo gani Mungu hufanya kazi Yake, siku zote Anawatendeakaribisha watu kulingana na utambulisho Wake wa kweli, akifanya kile ambacho Anafaa kufanya na kusema kile Anachofaa kusema. Haijalishi ni nafasi gani Mungu anazungumzia kutoka—Anaweza kuwa amesimama kwenye mbingu ya tatu, au amesimama akiwa mwili Wake, au hata kama mtu wa kawaida—siku zote Anaongea kwa binadamu kwa moyo Wake wote na kwa akili Zake zote, bila uongo na bila ufichaji wowote. Wakati Anapotekeleza kazi Yake, Mungu huonyesha neno Lake na tabia Yake, na huonyesha kile Anacho na alicho, bila kuficha chochote. Anamwongoza mwanadamu na maisha Yake na uwepo Wake na miliki yake. Hivi ndivyo binadamu alivyoishi katika Enzi ya Sheria—enzi asilia ya binadamu—akiongozwa na Mungu asiyeonekana na asiyegusika.

Mungu alipata mwili kwa mara ya kwanza baada ya Enzi ya Sheria, hali ya kupata mwili iliyodumu kwa miaka thelathini na tatu na nusu. Kwa mwanadamu, miaka thelathini na mitatu na nusu ni muda mrefu? (Si mrefu sana.) Kwa sababu urefu wa maisha ya mwanadamu ni mirefu kuliko miaka thelathini na fulani, huu si muda mrefu kwa mwanadamu. Lakini kwa Mungu mwenye mwili, miaka hii thelathini na mitatu na nusu ilikuwa mirefu mno. Aligeuka na kuwa mtu—mtu wa kawaida aliyetekeleza kazi na agizo la Mungu. Hii ilimaanisha kwamba lazima angefanya kazi ambayo mtu wa kawaida asingeweza kufanya, huku akivumilia mateso ambayo binadamu wa kawaida hawezi kuvumilia. Kiwango cha mateso aliyovumilia Bwana Yesu katika Enzi ya Neema, kuanzia mwanzo wa kazi Yake hadi wakati Aliposulubishwa kwenye msalaba, huenda kisiwe ni kitu watu wa leo wangeweza kushuhudia wao binafsi, lakini mnaweza angaa kutambua kiasi kupitia hadithi zilizo kwenye Biblia? Licha ya ni maelezo mangapi yaliyopo kwenye ukweli huu uliorekodiwa, kwa ujumla, kazi ya Mungu katika kipindi hiki kilijaa ugumu na mateso. Kwa mwanadamu aliyepotoka muda wa miaka thelathini na mitatu na nusu si mrefu; mateso kidogo si jambo la kutisha. Lakini kwa Mungu mtakatifu asiye na doa, ambaye lazima avumilie dhambi zote za binadamu, na kula, kulala na kuishi na watenda dhambi, maumivu haya ni mengi mno. Yeye ndiye Muumba, Bwana wa viumbe vyote na Mtawala wa vitu vyote, lakini Alipokuja duniani alilazimika kuvumilia unyanyasaji na ukatili wa wanadamu waliopotoka. Ili kuikamilisha kazi Yake na kuokoa binadamu kutoka kwa taabu, Alilazimika kushutumiwa na binadamu, na kuvumilia dhambi za wanadamu wote. Kiwango cha mateso aliyopitia hakiwezi kwa kweli kueleweka au kutambulika na watu wa kawaida. Mateso haya yanawakilisha nini? Yanawakilisha Mapenzi ya Mungu kwa wanadamu. Yanasimamia udhalilishaji Alioteseka na gharama Aliyolipia kwa sababu ya wokovu wa binadamu, kukomboa dhambi zake, na kukamilisha awamu hii ya kazi Yake. Yanamaanisha binadamu angekombolewa kutoka katika msalaba na Mungu. Hii ndiyo gharama iliyolipwa kwa damu, kwa maisha, gharama ambayo viumbe walioumbwa hawawezi kumudu. Ni kwa sababu Anacho kiini cha Mungu na Amejihami na kile Mungu anacho na alicho, ndiyo maana Anaweza kuvumilia aina hii ya mateso na aina hii ya kazi. Hili ni jambo ambalo hakuna kiumbe aliyeumbwa anaweza kufanya badala Yake. Hii ni kazi ya Mungu katika Enzi ya Neema na ufunuo wa tabia Yake. Je, hii inafichua chochote kuhusu kile Mungu anacho na alicho? Je, wanadamu wanastahili kuijua?

Katika enzi hiyo, japokuwa mwanadamu hakuiona nafsi ya Mungu, alipokea sadaka ya Mungu dhidi ya dhambi zake na akakombolewa kutoka kwenye msalaba na Mungu. Huenda mwanadamu awe amezoeana na kazi aliyofanya Mungu katika Enzi ya Neema, lakini yupo yeyote aliyezoeana na tabia na mapenzi yalionyeshwa na Mungu katika kipindi hiki? Binadamu anajua tu kuhusu maudhui ya kazi ya Mungu katika enzi tofauti katika vipindi mbalimbali, au anajua hadithi zinazohusiana na Mungu zilizofanyika kwa wakati mmoja na ule Mungu alikuwa akitekeleza kazi Yake. Maelezo haya na hadithi ni kwa ukweli zaidi taarifa fulani tu au hadithi za kumbukumbu kuhusu Mungu na vyote hivi havina chochote kuhusiana na tabia na kiini cha Mungu. Hivyo haijalishi ni hadithi ngapi watu wanajua kuhusu Mungu, haimaanishi kwamba wanao uelewa wa kina na maarifa kuhusu tabia ya Mungu au kiini Chake. Kama vile katika Enzi ya Sheria, ingawaje watu kutoka Enzi ya Neema walikuwa wamepitia mtagusano wa karibu sana na wa kikweli na Mungu wa mwili, maarifa yao kuhusu Mungu na kiini cha Mungu yalikuwa kweli mambo yasiyokuwepo.

Katika Enzi ya Ufalme, Mungu akawa mwili tena, kwa njia sawa na ile Aliyotumia mara ya kwanza. Katika kipindi hiki cha kazi, Mungu angali anaonyesha bila kusita neno Lake, anafanya kazi anayofaa kufanya na kuonyesha kile Anacho na alicho. Wakati huohuo, Anaendelea kuvumilia na kustahili na kutotii na kutojua kwa binadamu. Je, Mungu hafichui kila wakati tabia Yake na kuonyesha mapenzi yake katika kipindi hiki cha kazi pia? Hivyo basi, kuanzia uumbaji wa binadamu hadi sasa, tabia ya Mungu, nafsi Yake na miliki Zake, na mapenzi Yake, siku zote yamekuwa wazi kwa kila mmoja. Mungu hajawahi kuficha kimakusudi kiini Chake, tabia Yake au mapenzi Yake. Ni vile tu mwanadamu hajali kuhusu kile ambacho Mungu anafanya, mapenzi Yake ni yapi—ndio maana uelewa wa binadamu kumhusu Mungu ni finyu mno. Kwa maneno mengine, wakati Mungu anaficha nafsi Yake, Yeye pia Anasimama kando ya mwanadamu kila wakati, akionyesha waziwazi mapenzi Yake, tabia Yake na kiini chake halisi siku zote. Kimsingi, nafsi ya Mungu pia iko wazi kwa watu lakini kutokana na upofu na kutotii kwa binadamu, siku zote hawawezi kuuona kuonekana kwa Mungu. Hivyo kama hali iko hivyo, basi si kuelewa tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe kunafaa kuwa rahisi mno kwa kila mmoja? Hili ni swali gumu sana kujibu, sivyo? Mnaweza kusema ni rahisi, lakini wakati watu wengine wanatafuta kumjua Mungu, hatimaye hawamjui Yeye au kupata uelewa wa wazi kumhusu Yeye—siku zote ni jambo lililojaa ukungu na lisiloeleweka. Lakini mkisema si rahisi, hilo si sahihi vilevile. Baada ya kuwa mlengwa wa kazi ya Mungu kwa muda mrefu, kila mmoja anafaa, kupitia uzoefu wake, kuwa amepitia kwa kweli mambo mbalimbali na Mungu. Anafaa kuwa amehisi Mungu angalau kwa kiwango fulani katika moyo wake au awe amekuwa na mawasiliano ya kiroho na Mungu, na anafaa angalau kuwa alikuwa na ufahamu kiasi tambuzi kuhusu tabia ya Mungu au kupata uelewa fulani kumhusu Yeye. Kuanzia wakati binadamu alianza kumfuata Mungu hadi sasa, mwanadamu amepokea mengi mno, lakini kutokana na sababu za aina zote—uhodari wa kimasikini ya kibinadamu, kutojua, uasi, na nia mbalimbali—wanadamu wamepoteza mambo mengi mno. Je, Mungu hajampatia mwanadamu mali ya kutosha? Ingawaje Mungu huficha nafsi Yake kutoka kwa wanadamu, Anawatosheleza mahitaji yao kwa kile Anacho na alicho, na hata maisha Yake; maarifa ya binadamu ya Mungu hayafai kuwa vile yalivyo tu sasa. Ndiyo maana Nafikiri inahitajika kuwa na ushirika zaidi na nyinyi kuhusu mada ya kazi ya Mungu, kuhusu tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe. Kusudio ni ili miaka elfu ya utunzaji na fikira ambayo Mungu amemwagia binadamu isije ikaisha bure bilashi, na ili mwanadamu aweze kuelewa kwa dhati na kutambua mapenzi ya Mungu kwake. Ni ili watu waweze kusonga mbele kwenye hatua mpya ya maarifa yao kumhusu Mungu. Itaweza pia kumrudisha Mungu katika nafasi Yake inayofaa kwenye mioyo ya watu yaani kumfanyia Yeye haki.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 23)

Amri ya Mungu kwa Adamu

Mwa 2:15-17  Naye Yehova Mungu akamchukua mtu huyo, na kumweka ndani ya bustani ya Edeni ili ailime na kuihifadhi. Yehova Mungu akamwamrisha mtu huyo, akisema, Unaweza kula kwa uhuru matunda kutoka miti yote ya bustani: Lakini kutoka mti wa maarifa ya mema na maovu, usiyale: kwa kuwa katika siku ambapo utakula matunda kutoka mti huo bila shaka utakufa.

Je, mlielewa chochote kutoka kwenye mistari hii? Je, ni vipi ambavyo sehemu hii ya maandiko inavyo wafanya kuhisi? Kwa nini “Amri ya Mungu kwa Adamu” ilidondolewa kutoka kwa maandiko? Je, kila mmoja wenu sasa anayo picha ya Mungu na Adamu katika akili yenu? Mnaweza kujaribu kufikiria: Kama ni nyinyi mliokuwa katika tukio hilo, je, Mungu katika moyo wenu angekuwa vipi? Ni hisia gani ambazo picha hii zinafanya mhisi? Hii ni picha ya kusisimua na ya kutuliza moyo. Ingawaje kunaye Mungu tu na binadamu ndani yake, ule ukaribu kati yao unastahili kuonewa wivu: Upendo mwingi wa Mungu amepewa binadamu kwa ukarimu, unamzunguka binadamu; binadamu ni mnyofu na asiye na hatia, aliye huru kabisa na asiyejali chochote, anayeishi kwa furaha kwa uangalizi wa jicho la Mungu; Mungu anaonyesha hali ya kujali binadamu huku naye binadamu anaishi katika ulinzi na baraka za Mungu; kila kitu binadamu anachofanya na kusema kinaunganishwa kwa karibu na Mungu na hakiwezi kutofautishwa.

Mnaweza kusema kwamba hii ndiyo amri ya kwanza ya Mungu aliyoitoa kwa binadamu tangu kumuumba yeye. Je, amri hii ina nini? Amri hii inayo mapenzi ya Mungu, lakini pia inayo wasiwasi Wake kwa wanadamu. Hii ndiyo amri ya kwanza ya Mungu na pia ndio mara ya kwanza Mungu anakuwa na wasiwasi kuhusu binadamu. Hivi ni kusema, Mungu analo jukumu kwa binadamu tangu ule wakati alipomuumba yeye. Jukumu Lake ni lipi? Lazima amlinde binadamu, kumwangalia binadamu. Anatumai kwamba binadamu anaweza kuamini na kutii maneno Yake. Hili pia ndilo tarajio la kwanza la Mungu kwa binadamu. Na ni kwa tarajio hili kwamba Mungu anasema yafuatayo: “Unaweza kula kwa uhuru matunda kutoka miti yote ya bustani: Lakini kutoka mti wa maarifa ya mema na maovu, usiyale: kwa kuwa katika siku ambapo utakula matunda kutoka mti huo bila shaka utakufa.” Maneno haya rahisi yanawakilisha mapenzi ya Mungu. Yanafichua pia kwamba moyo wa Mungu tayari umeanza kuonyesha hali ya kujali binadamu. Miongoni mwa mambo yote, ni Adamu pekee aliyeumbwa kwa taswira ya Mungu; Adamu alikuwa kiumbe wa pekee aliye hai aliye na pumzi ya uhai ya Mungu; angeweza kutembea na Mungu, kuzungumza na Mungu. Na ndiyo maana Mungu alimpa amri kama hiyo. Mungu aliweka wazi katika amri hii kile binadamu anaweza kufanya, na vilevile akaweka wazi kile asichoweza kufanya.

Katika maneno haya machache rahisi, tunauona moyo wa Mungu. Lakini ni aina gani ya moyo tunaouona? Je, kunao upendo katika moyo wa Mungu? Je, upendo huo unao hali yoyote ya kujali ndani yake? Upendo wa Mungu na kujali kwake katika mistari hii hakuwezi kutambulika na kuthaminiwa tu na watu, lakini unaweza pia kuhisiwa vizuri na kwa kweli. Hayo ni kweli? Kwa vile nimesema tayari mambo haya, bado mnafikiria kwamba haya ni maneno machache tu rahisi? Si rahisi hivyo, kweli? Mngeweza kuona hivi awali? Kama Mungu mwenyewe angekuambia maneno hayo machache mngehisi vipi ndani yenu? Kama wewe si mtu mwenye utu, kama moyo wako ni baridi kama barafu, basi usingehisi chochote, usingethamini upendo wa Mungu, na usingejaribu kuuelewa moyo wa Mungu. Lakini kama wewe ni mtu mwenye dhamiri, mwenye ubinadamu, basi utahisi tofauti. Utahisi joto, utahisi kuwa umetunzwa na umependwa, na utahisi furaha. Je, hayo ni kweli? Unapohisi mambo haya, utatenda vipi kwa Mungu? Utahisi ukiwa umeunganishwa kwa Mungu? Utampenda na kumheshimu Mungu kutoka kwenye sakafu ya moyo wako? Moyo wako utakuwa karibu zaidi na Mungu? Unaweza kuona kutoka kwa haya namna ambavyo upendo wa Mungu ulivyo muhimu kwa binadamu. Lakini kile kilicho muhimu zaidi ni kuthamini na kufahamu kwa binadamu upendo huu wa Mungu. Kwa hakika, Mungu hasemi mambo mengi yanayofanana kwenye awamu hii ya kazi Yake? Lakini je, watu wa leo wanauthamini moyo wa Mungu? Je, mnaweza kung’amua mapenzi ya Mungu Niliyoyazungumzia muda mfupi uliopita? Hamwezi hata kutambua mapenzi ya Mungu wakati yanaonekana waziwazi, yanaweza kushikika na ni halisi. Na ndiyo maana Nasema hamna maarifa na uelewa halisi wa Mungu. Je, haya si kweli?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 24)

Mungu Amuumba Hawa

Mwa 2:18-20  Yehova Mungu akasema, Si vizuri kuwa mtu huyo akuwe peke yake; nitamuumbia msaidizi anayefanana na yeye. Na kutoka kwa ardhi Yehova Mungu akaumba wanyama wote wa msituni, na ndege wote wa angani; na akawaletea kwa Adamu ndiyo aone majina ambayo angewapa: na chochote ambacho Adamu alikiita kiumbe hai, hilo ndilo likawa jina lake kuanzia hapo. Naye Adamu akawapa wanyama wote wa kufugwa majina, na ndege wa hewani, na wanyama wote wa mwituni; lakini kwa Adamu hakupatikana msaidizi ambaye alifanana na yeye.

Mwa 2:22-23  Nao ubavu, ambao Yehova Mungu aliuchukua kutoka kwa Adamu, yeye akaufanya uwe mwanamke, na akampeleka kwa Adamu. Naye Adamu akasema, Huyu sasa ni mfupa wa mifupa yangu, na nyama ya nyama zangu: ataitwa Mwanamke, kwa kuwa amechukuliwa kutoka kwa Mwanamume.

Kuna msitari mmoja muhimu kwenye sehemu hii ya Maandiko: “chochote ambacho Adamu alikiita kiumbe hai, hilo ndilo likawa jina lake kuanzia hapo.” Kwa hivyo ni nani aliyepatia viumbe wote haya majina yao? Alikuwa Adamu, si Mungu. Msitari huu unamwambia mwanadamu ukweli: Mungu alimpa binadamu werevu alipomuumba Yeye. Hivi ni kusema kwamba, werevu wa binadamu ulitoka kwa Mungu. Hili ni kweli. Lakini kwa nini? Baada ya Mungu kumuumba Adamu, Adamu alienda shuleni? Je, alijua namna ya kusoma? Baada ya Mungu kuwaumba viumbe hai mbalimbali, je, Adamu aliwatambua viumbe hawa wote? Je, Mungu alimwambia majina ya viumbe hao? Bila shaka, Mungu pia hakumfunza namna ya kutunga yale majina ya viumbe hawa. Huo ndio ukweli! Basi alijua vipi namna ya kupatia viumbe hawa hai majina yao na aina gani ya majina ya kuwapatia? Haya yote yanahusiana na swali kuhusu ni nini ambacho Mungu aliongezea kwa Adamu alipomuumba yeye. Ukweli unathibitisha kwamba wakati Mungu alipomuumba binadamu Alikuwa ameongezea werevu kwake. Huu ni ukweli muhimu sana. Je, nyinyi nyote mmesikiliza kwa makini? Kunao ukweli mwingine muhimu ambao unafaa kuwa wazi kwenu? Baada ya Adamu kuwapatia viumbe hai majina yao, majina haya yalipangwa kwenye msamiati wa Mungu. Kwa nini Ninasema hivyo? Hii pia inahusisha tabia ya Mungu, na lazima Niielezee.

Mungu alimuumba binadamu, Akapumua maisha ndani yake, na pia Akampa baadhi ya werevu Wake, uwezo Wake, na kile Anacho na alicho. Baada ya Mungu kumpa binadamu mambo haya yote, binadamu aliweza kufanya baadhi ya mambo haya kwa uhuru na kufikiria pekee yake. Kama kile binadamu anaunda na kufanya ni kizuri machoni mwa Mungu, basi Mungu anakikubali na haingilii kati. Kama kile binadamu anafanya ni sahihi, basi Mungu atakiacha tu kiwe hivyo milele. Kwa hivyo kauli hii “chochote ambacho Adamu alikiita kiumbe hai, hilo ndilo likawa jina lake kuanzia hapo” inaonyesha nini? Inaopendekeza kwamba Mungu hakufanya marekebisho yoyote kwa majina ya wale viumbe mbalimbali hai. Jina lolote lile ambalo Adamu alimwita, Mungu alisema “Ndiyo” na akasajili jina hilo hivyo. Je, Mungu alionyesha maoni yoyote? La, hilo ni hakika. Kwa hivyo, mnaona nini hapa? Mungu Alimpa binadamu werevu naye binadamu akautumia werevu wake aliopewa na Mungu kufanya mambo. Kama kile binadamu anafanya ni kizuri machoni mwa Mungu, basi kinathibitishwa, kutambulika, na kukubalika na Mungu bila ya utathmini au upinzani wowote. Hili ni jambo ambalo hakuna mtu wala roho wa maovu, wala Shetani, anaweza kufanya. Je, mnauona ufunuo wa tabia ya Mungu hapa. Je, mwanadamu, mwanadamu aliyepotoshwa, au Shetani anaweza kuwakubali wengine kuwawakilisha katika kufanya mambo huku wakitazama? Bila shaka la! Je, wanaweza kupigania cheo na yule mtu mwingine au nguvu nyingine ambayo ni tofauti na wao? Bila shaka wangefanya hivyo! Na kwa muda huo, kama angekuwa ni mtu aliyepotoshwa au Shetani aliyekuwa na Adamu, bila shaka wangekataa kile ambacho Adamu alikuwa akifanya. Ili kuthibitisha kwamba wanao uwezo wa kufikiria kwa uhuru na wanayo maono yao binafsi na ya kipekee, wangekataa kabisa kila kitu alichofanya Adamu: “Unataka kukiita hivyo? Kwa kweli, sitakiita hivyo, nitakiita hivi; ulikiita Tom lakini mimi nitakiita Harry. Lazima nionyeshe ustadi wangu.” Haya ni aina gani ya asili? Hii ni asili ya kiburi kisicho na mipaka? Lakini Mungu anayo tabia kama hii? Je, Mungu alikuwa na upinzani wowote usiokuwa wa kawaida kwa mambo haya ambayo Adamu alifanya? Jibu ni bila shaka la! Kati ya tabia ambayo Mungu anafichua, hakuna hata chembe ya ubishi, ya kiburi, au kujigamba kwa nafsi. Hilo liko wazi kabisa hapa. Hili ni jambo dogo tu, lakini kama huelewi kiini cha Mungu, kama moyo wako hautajaribu kujua namna ambavyo Mungu anatenda na mwelekeo wa Mungu ni ipi, basi hutajua tabia ya Mungu au kuyaona maonyesho na ufunuo wa tabia ya Mungu. Je, hayo si kweli? Je, unakubali kile Nimetoka tu kukuelezea? Kwa kujibu matendo ya Adamu, Mungu hakutangaza kwa sauti kwamba, “Umefanya vyema. Umefanya sahihi Ninakubali.” Katika Moyo Wake, hata hivyo, Mungu aliidhinisha, akathamini, akashangilia kile Adamu alikuwa amefanya. Hili ndilo jambo la kwanza tangu uumbaji ambalo binadamu alikuwa amemfanyia Mungu akifuata maagizo Yake. Ni jambo ambalo binadamu alifanya badala ya Mungu na kwa niaba ya Mungu. Mbele ya macho yake, hili lilitokana na werevu Aliokuwa amempa binadamu. Mungu aliliona kama jambo zuri, kitu kizuri. Kile ambacho Adamu alifanya wakati huo kilikuwa maonyesho ya kwanza ya werevu wa Mungu kwa binadamu. Hili lilikuwa onyesho zuri kutoka kwa maoni ya Mungu. Kile Ninachotaka kuwaambia nyinyi hapa ni kwamba nia ya Mungu katika kuongezea sehemu ya kile Anacho na alicho na werevu wake kwa binadamu ilikuwa ili mwanadamu aweze kuwa kiumbe hai anayemwonyesha Yeye. Kwa kiumbe hai kama huyo kufanya mambo hayo kwa niaba yake, ilikuwa ndicho hasa kile Mungu alikuwa akitamani kuona.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 25)

Mungu Awatengenezea Adamu na Hawa Nguo za Ngozi

Mwa 3:20-21  Adamu akampa mke wake jina la Hawa; kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa mama ya wote wenye uhai. Pia Yehova Mungu akawatengenezea Adamu na mke wake nguo za ngozi; na akawavisha.

“Pia Yehova Mungu akawatengenezea Adamu na mke wake nguo za ngozi; na akawavisha,” Katika tukio hili, ni wajibu gani ambao tunamwona Mungu akiuchukua Anapokuwa na Adamu na Hawa? Na ni katika aina gani ya uajibu ambao Mungu anajitokeza katika ulimwengu akiwa tu na wanadamu wawili? Kutekeleza wajibu wa Mungu? Kaka na dada kutoka Hong Kong, tafadhali jibuni. (Kutekeleza wajibu wa mzazi.) Kaka na dada kutoka Korea Kusini, ni wajibu wa aina gani mnafikiria Mungu anatekeleza hapa? (Kiongozi wa familia.) Kaka na dada kutoka Taiwan, mnafikiria nini? (Wajibu wa mtu katika familia ya Adamu na Hawa, wajibu wa mwanafamilia.) Baadhi yenu mnafikiria kuwa Mungu anajitokeza kama mwanafamilia wa Adamu na Hawa, huku baadhi wakisema kwamba Mungu anajitokeza kama kiongozi wa familia na wengine wanasema kwamba Anajitokeza kama mzazi. Haya yote yanafaa sana. Lakini ni nini hasa Ninachotilia mkazo hapa? Mungu aliwaumba watu hawa wawili na kuwashughulikia kama mtu na mwandani Wake. Akiwa ndiye mwanafamilia pekee wao, Mungu aliangalia kuishi kwao na pia akakidhi mahitaji yao ya kimsingi. Hapa, Mungu anajitokeza kama mzazi wa Adamu na Hawa. Huku Mungu akifanya haya, binadamu haoni namna ambavyo Mungu alivyo mkuu; haoni mamlaka ya juu zaidi ya Mungu, hali Yake ya mafumbo, na hasa haoni hasira au adhama Yake. Kile anachoona tu ni unyenyekevu wa Mungu, upendo Wake, kujali Kwake binadamu na jukumu Lake na utunzaji Wake kwake yeye. Mwelekeo na njia ambayo Mungu alishughulikia Adamu na Hawa ni sawa na namna ambavyo wazazi wa kibinadamu wanavyoonyesha hali ya kuwajali watoto wao binafsi. Ni kama pia namna ambavyo wazazi wa kibinadamu wanavyopenda, kuangalia, na kutunza watoto wao binafsi wa kiume na kike—halisia, namna ya kuonekana, na kushikika. Badala ya kujiweka Yeye Mwenyewe katika cheo cha juu na cha utukufu, Mungu mwenyewe alitumia ngozi kutengeneza nguo za binadamu. Haijalishi kama koti hili la manyoya lilitumika kufunika uchi wao au wao kujikinga dhidi ya baridi. Kwa ufupi, nguo hii iliyotumika kuufunika mwili wa binadamu ilitengenezwa na Mungu mwenyewe kwa mikono Yake mwenyewe. Badala ya kuitengeneza tu kupitia kwa fikira au kwa mbinu za kimiujiza kama watu wanavyofikiria, Mungu alikuwa amefanya kitu cha halali kwa binadamu ambacho binadamu anafikiria Mungu hawezi na hafai kufanya. Kitu hiki kinaweza kuwa rahisi ambacho baadhi huenda hata wasifikirie kwamba kinastahili kutajwa, lakini kinawaruhusu pia wale wote wanaomfuata Mungu lakini awali walikuwa na mawazo yasiyoeleweka kuhusu Yeye kuweza kupata maono kuhusu ukweli na uzuri Wake, na kuuona uaminifu Wake na asili Yake ya unyenyekevu. Kinawafanya watu wenye kiburi kisicho na kifani wanaofikiria kwamba wako juu na wanao utukufu kuinamisha vichwa vyao kwa aibu mbele ya ukweli na unyenyekevu wa Mungu. Hapa, ukweli na unyenyekevu wa Mungu unawezesha zaidi watu kuona namna ambavyo Anapendeka. Kwa kinyume cha mambo, yule Mungu mkubwa sana, Mungu anayependeka na yule Mwenyezi Mungu katika mioyo ya watu ni mdogo sana, asiyevutia, na asiyeweza kuhimiliwa hata mara moja. Unapouona mstari huu na kuisikia hadithi hii, unamkasirikia Mungu kwa sababu Alifanya kitu kama hiki? Baadhi ya watu wanaweza kufanya hivyo, lakini kwa wengine itakuwa ni tofauti kabisa. Watafikiri Mungu ni mkweli na anapendeka, na hasa ni ule ukweli na uzuri wa Mungu ndiyo unaowafurahisha. Kwa kadri wanavyoona ule upande wa kweli wa Mungu, ndipo wanapothamini uwepo wa kweli wa upendo wa Mungu, umuhimu wa Mungu katika mioyo yao, na namna anavyosimama kando yao kila muda.

Kwa wakati huu, tunafaa kuunganisha mazungumzo yetu na sasa. Kama Mungu angeweza kufanya mambo haya madogo mbalimbali kwa binadamu Aliowaumba hapo mwanzo kabisa, hata vitu vingine ambavyo watu hawangethubutu kufikiria ama kutarajia, basi naye Mungu angewafanyia watu leo mambo kama hayo? Baadhi ya watu husema, “Ndiyo!” Kwa nini hivyo? Kwa sababu kiini cha Mungu si bandia, uzuri Wake si bandia. Kwa sababu kiini cha Mungu kwa kweli kipo, na si kitu kilichoongezewa tu na wengine na bila shaka si kitu ambacho kinabadilika na mabadiliko ya muda, mahali, na enzi. Ukweli na uzuri wa Mungu unaweza kwa kweli kuonyeshwa kupitia kufanya jambo ambalo watu wanafikiria si la kipekee na ni dogo, jambo ambalo ni dogo sana kiasi cha kwamba watu hata hawafikirii angeweza kufanya. Mungu si mnafiki. Hakuna kupiga chuku, kufunika ukweli, majivuno au kiburi katika tabia na kiini Chake. Siku zote Hajigambi, lakini badala yake Anapenda, Anaonyesha hali ya kujali, Anaangalia, na kuwaongoza wanadamu Aliowaumba kwa uaminifu na dhati. Haijalishi ni kiwango kipi ambacho watu wanaweza kuthamini, kuhisi, au kuona, Mungu kwa hakika anafanya mambo haya. Je, kujua kwamba Mungu anacho kiini kama hicho kunaweza kuathiri upendo wa watu kwake Yeye? Kutaweza kushawishi namna wanavyomcha Mungu? Ninatumai utakapoelewa upande halisi wa Mungu utaweza kuwa hata karibu zaidi na Yeye na kuweza kuthamini hata zaidi na kwa kweli upendo Wake na utunzaji Wake kwa wanadamu, huku wakati huohuo pia kumpa moyo wako na kutowahi tena kuwa na shaka au wasiwasi wowote kwake Yeye. Mungu anafanya kimyakimya kila kitu kwa ajili ya binadamu, akifanya kimyakimya kupitia ukweli, uaminifu, na upendo Wake. Lakini siku zote Hana hofu au majuto yoyote kwa yale yote Anayofanya, wala hahitaji mtu yeyote kumlipa Yeye kwa njia yoyote au kuwa na nia za kuwahi kupokea kitu kutoka kwa wanadamu. Kusudio tu la kila kitu Alichowahi kufanya ni ili Aweze kupokea imani na upendo wa kweli kutoka kwa wanadamu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 26)

Mungu Anuia kuangamiza Ulimwengu kwa Gharika, Amwagiza Nuhu Kuijenga Safina

Mwa 6:9-14  Hivi ni vizazi vyake Nuhu: Nuhu alikuwa mtu mwenye haki na mtimilifu katika vizazi vyake, naye Nuhu alitembea na Mungu. Naye Nuhu akapata watoto watatu wa kiume, Shemu, Hamu, na Yafethi. Dunia pia ilikuwa potovu mbele za Mungu, nayo dunia ilijaa vurugu. Naye Mungu akaiangalia dunia, na, tazama, ilikuwa imepotoka; kwa sababu kila aliye na mwili alikuwa amejipotoshea njia yake duniani. Naye Mungu akasema kwake Nuhu, Mwisho wa wote walio na mwili umefika mbele zangu; kwa kuwa dunia imejawa na vurugu kupitia kwao; na, tazama, nitawaangamiza pamoja na dunia. Ujitengenezee safina ya mbao wa mvinje; utatengeneza vyumba ndani ya safina, na uipake lami ndani na nje.

Mwa 6:18-22  Lakini na wewe nitaliimarisha agano langu; na utaingia ndani ya safina, wewe, na wana wako, na mke wako, na wake zao wana wako pamoja na wewe. Na kwa kila kilicho na uhai chenye mwili, utawaleta wawili wa kila aina katika safina, kuwaweka hai pamoja nawe; watakuwa wa kiume na wa kike. Kila ndege arukaye kwa aina yake, na mifugo kwa aina yake, kila kinachotambaa duniani kwa aina yake, wawili wa aina yote watakuja kwa wewe, ili uwaweke hai. Na ujichukulie chakula cha kila aina kinacholika, nawe ukikusanye kwako; na kitakuwa kwa ajili ya chakula cha ninyi, na cha wao. Nuhu alifanya hivyo; kulingana na vyote ambavyo Mungu alimwamrisha, alifanya hivyo.

Je sasa mnaelewa kwa jumla Nuhu ni nani baada ya kuzisoma fahamu hizi? Nuhu ni mtu wa aina gani? Maandishi asilia ni: “Nuhu alikuwa mtu mwenye haki na mtimilifu katika vizazi vyake.” Kulingana na uelewa wa watu wa kisasa, mtu mwenye haki wakati huo wa nyuma alikuwa mtu wa aina gani? Mtu mwenye haki anafaa kuwa mtu mtimilifu. Je, mnajua kama mtu huyu mtimilifu ni mtimilifu machoni mwa binadamu au ni mtimilifu machoni mwa Mungu? Bila shaka mtu huyu mtimilifu ni mtu mtimilifu machoni mwa Mungu na wala si machoni mwa binadamu. Haya yote ni kweli! Hii ni kwa sababu binadamu ni kipofu na hawezi kuona, na Mungu tu ndiye anayeiangalia nchi nzima na kila mmoja wetu, Mungu pekee ndiye anayejua Nuhu ni mtu mtimilifu. Hivyo basi, mpango wa Mungu wa kuuangamiza ulimwengu kwa gharika ulianza pindi tu Alipomuita Nuhu.

Kwamba Nuhu aliitwa ni ukweli mdogo, lakini hoja kuu ya kile tunachozungumzia sasa—tabia ya Mungu, mapenzi Yake kiini Chake halisi katika rekodi hii—si rahisi. Ili kuelewa dhana hizi mbalimbali za Mungu lazima kwanza tuelewe ni mtu wa aina gani ambaye Mungu hutamani kuita, nakupitia hii, tuweze kuelewa tabia yake, mapenzi yake na kiini chake halisi. Kufanya hivi ni muhimu. Hivyo katika macho ya Mungu, mtu huyu ni wa aina gani ambaye yeye humwita? Huyu lazima awe ni mtu anayeweza kuyasikiza maneno Yake. Wakati huohuo, lazima mtu huyu awe yule wa kuwajibika, mtu atakayetekeleza neno la Mungu kwa kuliona kuwa jukumu na wajibu ambao anahitajika kukamilisha. Basi mtu huyu anahitajika kuwa mtu anayemjua Mungu? La. Hapo nyuma, Nuhu hakuwa ameyasikia sana mafundisho ya Mungu wala kupitia kazi yoyote ile ya Mungu. Hivyo basi, maarifa ya Nuhu kumhusu Mungu yalikuwa madogo mno. Ingawaje imerekodiwa hapa kwamba Nuhu alitembea na Mungu, aliwahi kuiona nafsi ya Mungu? Jibu ni bila shaka la! Kwa sababu katika siku hizo, wajumbe wa Mungu tu ndio waliowaendea watu. Ingawa waliweza kuwakilisha Mungu katika kusema na kufanya mambo, walikuwa wakipitisha tu mapenzi na nia Zake. Nafsi ya Mungu haikufichuliwa kwa binadamu uso kwa macho. Kwenye sehemu hii ya maandiko, chote tunachoona tu ni kile ambacho mtu huyu Nuhu alilazimika kufanya na maagizo ya Mungu kwake yalikuwa gani. Hivyo basi ni kiini kipi kilichoonyeshwa na Mungu hapa? Kila kitu anachofanya Mungu kimepangiliwa kwa uhakika. Anapoona jambo au hali ikitokea, kutakuwa na kiwango cha kulipima jambo hilo katika macho Yake, na kiwango hiki kitaamua kama Ataanza mpango wa kulishughulikia au namna ya kuchukulia jambo na hali hii. Yeye anajali na ana hisia kwa kila kitu. Kwa hakika ni kinyume kabisa cha mambo. Kunao mstari hapa ambao Mungu alimwambia Nuhu: “Mwisho wa wote walio na mwili umefika mbele zangu; kwa kuwa dunia imejawa na vurugu kupitia kwao; na, tazama, nitawaangamiza pamoja na dunia.” Katika maneno ya Mungu wakati huu, Alisema kwamba Angeangamiza binadamu tu? La! Mungu Alisema kwamba Angeangamiza viumbe wote hai wenye mwili. Kwa nini Mungu alitaka kuangamiza? Kunao ufunuo mwingine wa tabia ya Mungu hapa: Katika macho ya Mungu, kunayo mipaka ya subira yake kwa kupotoka kwa binadamu, kwa uchafu, vurugu, na kutotii kwa mwili wote. Mipaka Yake ni ipi? Ni kama vile alivyosema Mungu: “Mungu akaiangalia dunia, na, tazama, ilikuwa imepotoka; kwa sababu kila aliye na mwili alikuwa amejipotoshea njia yake duniani.” Kauli hii “kwa sababu kila aliye na mwili alikuwa amejipotoshea njia yake duniani” inamaanisha nini? Inamaanisha kiumbe yeyote hai, wakiwemo wale waliofuata Mungu, wale walioita jina la Mungu, wale waliowahi kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Mungu, wale waliomtambua Mungu kwa vinywa vyao na hata kumsifia Mungu—pindi tabia yao ilipojaa upotovu na kufikia macho ya Mungu, basi ingemlazimu kuwaangamiza. Hiyo ndiyo ilikuwa mipaka ya Mungu. Hivyo basi ni hadi kiwango kipi Mungu alibakia kuwa mwenye subira kwa binadamu na upotovu wa mwili wote? Hadi katika kiwango ambacho watu wote, wawe wafuasi wa Mungu au wasioamini, walikuwa hawatembelei njia sahihi. Hadi kiwango ambacho binadamu alikuwa hajapotoshwa tu katika maadili na mwenye wingi wa maovu, lakini pia pale ambapo hakukuwa na mtu aliyesadiki uwepo wa Mungu, tupilia mbali yeyote aliyesadiki kuwa ulimwengu unatawaliwa na Mungu na kwamba Mungu anaweza kuwaletea watu nuru na njia sahihi. Hadi kiwango ambacho binadamu aliudharau uwepo wa Mungu, na hakumruhusu Mungu kuwepo. Pindi upotovu wa mwanadamu ulipofikia kiwango hiki, Mungu asingeweza tena kuwa na subira Ni nini kingechukua nafasi yake? Kuja kwa hasira ya Mungu na adhabu ya Mungu. Huu haukuwa ufunuo kiasi wa tabia ya Mungu? Katika enzi hii ya sasa, yupo bado binadamu mwenye haki katika macho ya Mungu? Yupo bado binadamu mtimilifu katika macho ya Mungu? Enzi hii ndiyo ile ambayo tabia ya miili yote duniani imepotoka mbele ya macho ya Mungu? Katika siku na enzi hii, mbali na wale Mungu anataka kuwafanya kuwa kamili, wale wanaoweza kumfuata Mungu na kuukubali wokovu Wake, huoni kwamba watu wote wa mwili wanapatia changamoto ile mipaka ya subira ya Mungu? Si kila kitu kinachofanyika kando yenu, kila mnachoona kwa macho yenu, na kusikia kwa masikio yenu, na kupitia ninyi binafsi kila siku katika ulimwengu huu kimejaa vurugu? Katika macho ya Mungu, si ulimwengu kama huu, enzi kama hii, inafaa kukomeshwa? Ingawaje usuli wa enzi ya sasa ni tofauti kabisa na usuli wa enzi ya Nuhu, hisia na hasira Alizo nazo Mungu kwa kupotoka kwa binadamu inabakia ileile sawa na ilivyokuwa wakati huo. Mungu anaweza kuwa mwenye subira kwa sababu ya kazi Yake, lakini kulingana na hali na masharti ya aina yote, ulimwengu huu unafaa kuwa uliangamizwa kitambo katika macho ya Mungu. Hali imepita na kupitiliza ile iliyokuwa hapo nyuma wakati ulimwengu uliangamizwa na gharika. Lakini tofauti ni nini? Hili ndilo jambo jingine linalohuzunisha moyo wa Mungu zaidi, na pengine kitu ambacho hakuna yeyote kati yenu anaweza kutambua.

Alipokuwa akiuangamiza ulimwengu kwa gharika, Mungu angemwita Nuhu ili kuijenga safina na kufanya baadhi ya kazi ya matayarisho. Mungu angemwita binadamu mmoja—Nuhu—kumfanyia misururu hii ya mambo. Lakini kwenye enzi ya sasa, Mungu hana mtu yeyote wa kumuita. Kwa nini hivyo? Kila mmoja aliyeketi hapa pengine anaelewa na kujua sababu vizuri sana. Je, mngependa Mimi niweze kuiweka wazi? Kuitaja kwa sauti huenda kukawaaibisha na kufanya kila mmoja kukasirika. Baadhi ya watu wanaweza kusema: “Ingawaje sisi si watu wenye haki na wala sisi si watu watimilifu kwenye macho ya Mungu, kama Mungu atatuelekeza sisi kufanya kitu, bado tutaweza kukifanya. Kabla, Aliposema janga kuu lilikuwa likija, tulianza kutayarisha chakula na vitu ambavyo tungehitaji wakati wa janga hilo. Si haya yote yalifanywa kulingana na mahitaji ya Mungu? Si tulikuwa tukishirikiana kwa hakika na kazi ya Mungu? Mambo haya tuliyofanya hayawezi kulinganishwa na kile Nuhu alifanya? Kwani kufanya kile tulichofanya si utiifu wa kweli? Kwani hatukuwa tunafuata maagizo ya Mungu? Kwani hatukufanya kile Mungu alichosema kwa sababu tunayo imani katika maneno ya Mungu? Basi kwa nini Mungu angali na huzuni? Kwa nini Mungu anasema Hana mtu wa kumwita?” Kunao tofauti wowote kati ya vitendo vyenu na vile vya Nuhu? Tofauti ni nini? (Kutayarisha chakula leo kwa minajili ya janga kulikuwa nia yetu binafsi.) (Matendo yetu hayawezi kufikia yale ya “haki,” ilhali Nuhu ni mtu mwenye haki mbele ya macho ya Mungu.) Kile mlichosema hakiko mbali sana na ukweli. Kile alichofanya Nuhu ni tofauti sana kulingana na kile watu wanafanya sasa. Wakati Nuhu alipofanya kama vile Mungu alivyomwagiza hakujua nia za Mungu zilikuwa nini. Hakujua ni nini ambacho Mungu Alitaka kukamilisha. Mungu alikuwa amempa tu amri, Akamwagiza afanye kitu, lakini bila ya maelezo mengi, na akaendelea mbele na kukifanya. Hakujaribu kuelewa kwa siri nia za Mungu zilikuwa nini, wala hakumpinga Mungu au kuwa na fikira mbili kuhusu jambo hilo. Alienda tu na kuifanya vilivyo kwa moyo safi na rahisi. Chochote ambacho Mungu alimruhusu kufanya alifanya, na kutii na kusikiliza neno la Mungu vyote vilikuwa ni imani yake ya kufanya mambo. Hivyo ndivyo alivyokuwa mnyofu na mwepesi wa kushughulikia kile ambacho Mungu alimwaminia kufanya. Kiini chake—kiini cha vitendo vyake kilikuwa ni utiifu, sio kutarajia kwa kukisia, sio kupinga, na zaidi; kutofikiria kuhusu maslahi yake binafsi na faida zake na hasara zake. Zaidi ya hayo, wakati Mungu aliposema Angeuangamiza ulimwengu kwa mafuriko, Nuhu hakuuliza ni lini au kuuliza kile kitakachovifanyikia vitu, na bila shaka hakumuuliza Mungu namna hasa alivyopanga kuangamiza ulimwengu. Alifanya tu kama Mungu alivyomwagiza. Njia yoyote ile aliyotaka Mungu, safina hiyo iweze kujengwa na hasa kujengwa na nini, alifanya tu vile ambavyo Mungu alimwomba na pia akaanza kazi mara moja. Alitenda kulingana na maagizo ya Mungu kwa mwelekeo wa kutaka kutosheleza Mungu. Je, alikuwa akifanya hivyo kujisaidia yeye kuepuka janga? La. Je, alimwuliza Mungu ni baada ya muda gani zaidi kabla ulimwengu ungeangamizwa? Hakuuliza. Je, alimwuliza Mungu au alijua ingechukua muda gani kuijenga safina? Hakujua hilo pia. Alitii tu, akasikiliza, na kufanya hivyo inavyohitajika. Watu wa sasa si sawa: Pindi tu taarifa fulani inapojitokeza kupitia kwa neno la Mungu, pindi tu watu wanapohisi ishara ya kutatizwa au matatizo, wote watachukua hatua mara moja, haijalishi ni nini, au gharama husika, ili kutayarisha kile ambacho watakula, kunywa, na kutumia athari za baadaye, hata kupanga njia za wao kutoroka wakati janga litakapovamia. Hata ya kuvutia zaidi ni kwamba, wakati huu muhimu, akili za binadamu zinakuwa zenye “manufaa sana.” Katika hali ambazo Mungu hajanipa maagizo yoyote, binadamu anaweza kupanga kila kitu kwa njia inayofaa Mngeweza kutumia neno “sahihi” ili kuielezea. Na kuhusiana na kile Mungu anachosema, nia za Mungu ni nini, au kile Mungu anataka ni nini, hakuna anayejali na hakuna anayejaribu kukitambua. Je, hii siyo tofauti kubwa zaidi kati ya watu wa leo na Nuhu?

Katika rekodi hii ya hadithi ya Nuhu, mnaona sehemu ya tabia ya Mungu? Kunacho mpaka kwa subira ya Mungu kwa upotovu, uchafu, na vurugu la binadamu. Anapofikia ule mpaka, Hatawahi tena kuwa na subira na badala yake Ataanza usimamizi Wake mpya na mpango mpya, kuanza kufanya kile ambacho lazima Afanye, kufichua matendo Yake na upande ule mwingine wa tabia Yake. Kitendo hiki Chake si cha kuonyesha kwamba lazima Asiwahi kukosewa na binadamu au kwamba Yeye amejaa mamlaka na hasira, na wala si kuonyesha kwamba Anaweza kuangamiza binadamu. Ni kwamba tabia Yake na kiini chake takatifu ambacho hakiwezi tena kuruhusu, hakina tena subira kwa aina hii ya binadamu kuishi mbele Yake, kuishi chini ya utawala Wake. Hivyo ni kusema, wakati wanadamu wote wako dhidi Yake, wakati hakuna mtu yeyote Anayeweza kuokoa katika ulimwengu mzima, Hatakuwa tena na subira kwa binadamu kama hawa, na Ataweza, bila ya utundu wowote, kutekeleza mpango Wake—kuangamiza binadamu wa aina hii. Kitendo kama hicho cha Mungu kinaamuliwa na tabia Yake. Hii ni athari inayohitajika, na athari ambayo kila kiumbe aliyeumbwa chini ya utawala wa Mungu lazima ashuhudie. Je, haya hayaonyeshi kwamba katika enzi ya sasa, Mungu hawezi kusubiri kukamilisha mpango Wake na kuokoa watu Anaotaka kuokoa? Katika hali hizi, Mungu anajali kuhusu nini zaidi? Si vile wale wasiomfuata Yeye kabisa au wale wanaompinga Yeye kwa vyovyote vile wanamshughulikia Yeye au kumpinga Yeye, au namna ambavyo mwanadamu anamdanganya Yeye. Anajali tu kuhusu kama wale wanaomfuata Yeye, walengwa wa wokovu Wake katika mpango Wake wa usimamizi, wamewekwa kamili na Yeye, na kama wametimiza utoshelezi Wake. Kuhusiana na watu wale wengine bali na wale wanaomfuata Yeye, Anawatolea tu adhabu kidogo mara kwa mara ili kuonyesha ghadhabu Yake. Kwa mfano tsunami, mitetemeko ya ardhi, kuibuka kwa volkano na kadhalika. Wakati huohuo, Anawalinda kwa dhati na kuwashughulikia wale wanaomfuata Yeye na karibu wanaokolewa na Yeye. Tabia ya Mungu ni hii: Kwa mkono mmoja, Anaweza kuwapatia watu Anaonuia kutekeleza subira na ustahimilivu kamili wa kupindukia na kuwasubiria wao kwa muda mrefu Anavyoweza; kwa mkono mwingine, Mungu anachukia na kuchukizwa kwa dhati na watu wa aina ya Shetani wasiomfuata Yeye na wanaompinga Yeye. Ingawaje Hajali kama hawa watu wa aina ya Shetani wanamfuata au wanamwabudu Yeye, bado Anawachukia wao huku akiwa na subira na wao katika moyo Wake, na Anapoamua mwisho wa hawa watu wa aina ya Shetani, Yeye pia anasubiria kufika kwa hatua za mpango Wake wa usimamizi.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 27)

Baraka za Mungu kwa Nuhu Baada ya Gharika

Mwa 9:1-6  Naye Mungu akawabariki Nuhu na wana wake, na akasema kwao, Ninyi Zaeni, na muongezeke, na muijaze tena dunia. Na wanyama wote wa dunia watawaogopa na kuwa na hofu nanyi, na ndege wote wa angani, na vyote vitembeavyo duniani, na kila samaki wa baharini; wamewekwa katika mikono yenu. Kila kisongacho kilicho na uhai kitakuwa chakula chenu, jinsi ambavyo nimewapa mboga ndivyo ninavyowapa vitu vyote. Lakini nyama iliyo na uhai, ambayo ni damu yake, ninyi msiile. Na bila shaka nitahitaji damu yenu ya uhai wenu, nitaihitaji kwa mkono wa kila mnyama, na kwa mkono wa mwanadamu, nitahitaji uhai wa mwanadamu kwa mkono wa ndugu wa kila mwanadamu. Yeyote ambaye atamwaga damu ya mwanadamu, damu yake itamwagika na mwanadamu: kwa kuwa Mungu alimfanya mwanadamu kwa mfano wake.

Baada ya Nuhu kukubali maagizo ya Mungu na kujenga safina na kuishi katika siku zile husika Mungu alitumia gharika ili kuangamiza ulimwengu, familia yake nzima ya wanane ilinusurika. Mbali na familia ya Nuhu ya wanane, wanadamu wote waliangamizwa, na viumbe wote nchini wakaangamizwa. Kwa Nuhu, Mungu alimpa baraka, na akasema baadhi ya mambo kwake na watoto wake wa kiume. Mambo haya yalikuwa yale ambayo Mungu alikuwa akimpa yeye na pia baraka zake kwake yeye. Hizi ndizo baraka na ahadi Mungu humpa yule ambaye anaweza kumsikiliza Yeye na kuyakubali maagizo Yake, na pia namna anavyotuza watu. Hivi ni kusema, haijalishi kama Nuhu alikuwa binadamu mtimilifu au alikuwa binadamu mwenye haki mbele ya macho ya Mungu, na haijalishi ni kiwango kipi alichomjua Mungu, kwa ufupi, Nuhu na watoto wake wa kiume watatu wote waliyasikiliza maneno ya Mungu, wakaratibu na kazi ya Mungu, na kufanya kile walichofaa kufanya kulingana na maagizo ya Mungu. Kutokana na hayo, walimsaidia Mungu kuweza kubakiza binadamu na aina mbalimbali za viumbe walio na uhai baada ya kuangamizwa kwa ulimwengu na gharika, na hivyo wakawa wamefanya mchango mkubwa kwa hatua iliyofuata ya mpango wa usimamizi wa Mungu. Kwa sababu ya kila kitu alichokuwa amefanya, Mungu alimbariki. Pengine kwa watu wa leo, kile alichofanya Nuhu hakikuwa sana na thamani ya kutajwa. Baadhi wanaweza hata kufikiria: Nuhu hakufanya chochote; Mungu alikuwa ameamua akilini Mwake kumhifadhi, hivyo kwa hakika angehifadhiwa. Kuwepo kwake si kwa sababu yake. Hili ndilo jambo ambalo Mungu alitaka lifanyike, kwa sababu binadamu ni mtulivu. Lakini hicho sicho Mungu alikuwa anafikiria. Kwa Mungu, haijalishi kama mtu ni mkubwa au asiye wa maana, mradi tu aweze kumsikiliza Yeye, kutii maagizo Yake na kile anachomwaminia na aweze kushirikiana na kazi Yake, mapenzi Yake, na mpango Wake, ili mapenzi Yake na Mpango Wake iweze kukamilika vizuri, basi mwenendo wake unastahili kukumbukwa na Yeye na kustahili kupokea baraka Zake. Mungu huthamini sana watu kama hao, na Yeye Hupenda sana vitendo vyao na upendo wao na huba yao Kwake. Huu ndio mwelekeo wa Mungu. Hivyo kwa nini Mungu alimbariki Nuhu? Kwa sababu hivi ndivyo Mungu anavyoshughulikia vitendo kama hivyo na utiifu wa mwanadamu.

Kuhusiana na baraka za Mungu kwa Nuhu, baadhi ya watu watasema: “Kama binadamu atamsikiliza Mungu na kumtosheleza Mungu, basi Mungu anafaa kumbariki binadamu. Je, hilo halifanyiki hivyo bila kusema?” Tunaweza kusema hivyo? Baadhi ya watu husema: “La.” Kwa nini hatuwezi kusema hivyo? Baadhi ya watu husema: “Binadamu hastahili kufurahia baraka za Mungu.” Hilo si sahihi kabisa. Kwa sababu wakati mtu anapokubali kile Mungu amemwaminia, Mungu anacho kiwango cha kuhukumu kama vitendo vya mtu huyu ni vizuri au vibaya na kama mtu huyu amemtii, na kama mtu huyu ametosheleza mapenzi ya Mungu na kama kile anachofanya kimeruhusiwa. Kile anachojali Mungu ni kuhusu moyo wa mtu huyu, si vitendo vyake vya juujuu. Si jambo kwamba Mungu anafaa kubariki mtu mradi tu afanye hivyo, licha ya namna anavyofanya hivyo. Huku ni kutoelewa kwa watu kumhusu Mungu. Mungu huangalia tu mwisho wa matokeo ya mambo, lakini Anatilia mkazo zaidi kuhusu namna moyo wa mtu ulivyo na namna mwelekeo wa mtu ulivyo wakati wa maendeleo ya mambo, na Anaangalia kama kunao utiifu, utiliaji maanani, na tamanio ya kumtosheleza Mungu ndani ya moyo wake. Nuhu alijua kiasi kipi kumhusu Mungu wakati huo? Kiasi hicho kilikuwa kingi kama mafundisho ya dini mnayojua sasa? Kuhusu dhana za ukweli kama vile dhana na maarifa ya Mungu, alipokea kunyunyizia na uchungaji kama ninyi? La, hakupokea! Lakini kunao ukweli mmoja ambao haupingiki: Katika fahamu, akili, na hata kina cha mioyo ya watu wa leo, dhana zao na mwelekeo wao kwa Mungu umejaa ukungu na haueleweki. Mnaweza hata kusema kwamba sehemu fulani ya watu inashikilia mwelekeo mbaya kwa uwepo wa Mungu. Lakini katika moyo wa Nuhu na fahamu yake, uwepo wa Mungu ulikuwepo na bila shaka, na hivyo basi utiifu wake kwa Mungu ulikuwa haujatiwa doa wala toa na ungeweza kustahimili majaribio. Moyo wake ulikuwa safi na wazi kwa Mungu. Hakuhitaji maarifa ya mafundisho ya dini mengi mno ili kujishawishi kufuata kila neno la Mungu, wala hakuhitaji ukweli mwingi kuthibitisha uwepo wa Mungu, ili akubali kile Mungu alimwaminia na kuweza kufanya chochote kile ambacho Mungu angemruhusu kufanya. Hii ni tofauti muhimu kati ya Nuhu na watu wa leo, na pia ndio ufasili wa kweli hasa kuhusu binadamu mtimilifu alivyo machoni mwa Mungu. Kile anachotaka Mungu ni watu kama Nuhu. Yeye ni aina ya mtu anayesifiwa na Mungu, na pia hasa mtu wa aina ile ambaye Mungu hubariki. Mmepokea nuru yoyote kutoka haya? Watu huangalia watu kutoka nje, huku naye Mungu anaangalia mioyo ya watu na kiini chao. Mungu hamruhusu yeyote kuwa na moyo wowote wa kukosa ari au shaka kwake Yeye, wala Hawaruhusu watu kushuku au kumjaribu Yeye kwa njia yoyote ile. Hivyo, ingawaje watu wa leo wako uso kwa uso na neno la Mungu, au mnaweza hata sema kwamba wako uso kwa uso na Mungu, kutokana na kitu kilicho ndani ya mioyo yao, uwepo wa kiini chao potovu, na mwelekeo wao wenye ukatili kwake Yeye, wamezuiliwa kutoka kwa imani yao ya kweli kwa Mungu na kuzibwa kutoka kwa utiifu wao kwake Yeye. Kwa sababu ya haya, ni vigumu sana kwao kutimiza baraka sawa ambazo Mungu alikabidhi Nuhu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 28)

Mungu Atumia Upinde wa Mvua Kama Ishara ya Agano Lake na mwanadamu

Mwa 9:11-13  Na nitaweka agano langu na ninyi, wala miili yote haitaondolewa tena na maji ya gharika; wala hakutakuwa na gharika tena kuiharibu dunia. Naye Mungu akasema, Hii ni alama ya agano ambayo naifanya kati ya Mimi na ninyi na viumbe vyote vyenye uhai vilivyo nanyi, kwa vizazi vya kudumu: naweka upinde wangu mawinguni, na utakuwa alama ya agano kati ya Mimi na dunia.

Kisha, hebu tuangalie sehemu hii ya maandiko kuhusu namna Mungu alivyounda upinde wa mvua kama ishara ya Agano lake na binadamu.

Watu wengi zaidi wanajua upinde wa mvua ni nini na wamesikia baadhi ya hadithi zinazohusiana na pinde za mvua. Kuhusiana na hadithi ile ya upinde wa mvua kwenye biblia, baadhi wa watu wanaisadiki, baadhi wanaichukulia tu kama hadithi ya kale, huku wengine hawaisadiki kamwe. Haijalishi ni nini, kila kitu kilichofanyika kuhusiana na upinde wa mvua ndicho kila kitu ambacho Mungu Alifanya hapo awali, na mambo yaliyofanyika katika mchakato huu wa usimamizi wa Mungu wa binadamu. Mambo haya yamerekodiwa vivyo hivyo kwenye Biblia. Rekodi hizi hazituambii chochote kuhusu hali ya Mungu ilivyokuwa wakati huo au nia zake nyuma ya maneno haya ambayo Mungu alisema. Zaidi, hakuna anayeweza kutambua ni nini Mungu alikuwa akihisi Aliposema maneno hayo. Hata hivyo, hali ya akili ya Mungu kuhusiana na hiki kitu chote inafichuliwa katikati ya mistari ya maandishi. Ni kana kwamba fikira zake wakati huo zinatoka kwenye ukurasa kupitia kila neno na kauli ya neno la Mungu.

Fikira za Mungu ni kile ambacho watu wanafaa kujali kuhusu na kile wanafaa kujaribu kujua zaidi. Hii ni kwa sababu fikira za Mungu zinahusiana kwa karibu na uelewa wa binadamu wa Mungu na uelewa wa binadamu wa Mungu ni kiungo muhimu sana kwa kuingia kwa binadamu katika maisha. Hivyo ni nini alichokuwa akifikiria Mungu wakati huo mambo haya yalipofanyika?

Hapo mwanzo, Mungu aliumba binadamu ambao katika macho Yake walikuwa wazuri sana na karibu na Yeye, lakini waliangamizwa na gharika baada ya kuasi dhidi Yake. Je, ilimwumiza Mungu kwamba binadamu kama hao walitoweka tu papo hapo hivyo? Bila shaka Aliumizwa! Kwa hivyo Maonyesho Yake ya maumivu haya yalikuwa nini? Ilirekodiwa vipi kwenye Biblia? Ilirekodiwa kwenye Biblia kama: “Na nitaweka agano langu na ninyi, wala miili yote haitaondolewa tena na maji ya gharika; wala hakutakuwa na gharika tena kuiharibu dunia.” Sentensi hii rahisi inafichua fikira za Mungu. Kuangamizwa huku kwa ulimwengu kulimpa Yeye maumivu sana. Kwa maneno ya binadamu, Alikuwa na huzuni sana. Tunaweza kufikiria: Ni vipi ambavyo dunia iliyokuwa imejaa maisha inavyofanana baada ya kuangamizwa na gharika? Ni vipi ambavyo dunia iliyokuwa imejaa binadamu inavyofanana hivi sasa? Hakuna makazi ya binadamu, hakuna viumbe walio hai, maji kila mahali na machafuko kabisa juu ya maji. Hilo ndilo lililokuwa onyesho la kusudio la asili ya Mungu wakati alipoumba ulimwengu? Bila shaka la! Nia asilia ya Mungu ilikuwa ni kuyaona maisha katika maeneo yote, kuwaona wanadamu Aliowaumba wakimwabudu Yeye, si tu kwa Nuhu kuwa mtu pekee anayemwabudu, au kuwa wa pekee ambaye angejibu mwito Wake ili kukamilisha kile alichoaminiwa kufanya. Wakati binadamu walitoweka, Mungu hakuona kile alichonuia awali lakini kinyume cha mambo. Ni vipi ambavyo moyo Wake usingekuwa katika maumivu? Hivyo Alipokuwa akifichua tabia Yake na kuelezea hisia Zake, Mungu alifanya uamuzi. Ni aina gani ya uamuzi Alifanya? Kuunda uta mawinguni (kumbuka: upinde wa mvua tunaouona) kama agano na binadamu, ahadi kwamba Mungu hangemwangamiza mwanadamu kwa gharika tena. Wakati huohuo, ulikuwa pia ni kuwaambia watu kwamba Mungu aliwahi kuangamiza ulimwengu kwa gharika, kumfanya mwanadamu kukumbuka milele ni kwa nini Mungu alifanya kitu kama hicho.

Je, kuangamizwa kwa ulimwengu wakati huu kulikuwa ni jambo alilotaka Mungu? Bila shaka lilikuwa ni jambo asilotaka Mungu Huenda tukaweza kufikiria sehemu ndogo ya picha ile ya kusikitikia ya ulimwengu baada ya kuangamizwa kwa ulimwengu lakini hatuwezi kukaribia kufikiria namna hali ilivyokuwa wakati huo mbele ya macho ya Mungu. Tunaweza kusema kwamba, haijalishi kama ni watu wa sasa au wa wakati huo, hakuna yeyote anayeweza kufikiria au kutambua ni vipi Mungu alikuwa akihisi Aliposhuhudia tukio hilo, picha hiyo ya ulimwengu baada ya kuangamizwa kwake kwa gharika. Mungu alilazimishwa kufanya haya kutokana na kutotii kwa binadamu, lakini maumivu ambayo moyo wa Mungu ulipitia kutokana na maangamizo haya ya ulimwengu kwa gharika ni uhalisia ambao hakuna anayeweza kuufikiria au kuutambua. Ndiyo maana Mungu aliweka agano na mwanadamu, ambalo lilikuwa ni kuambia watu kukumbuka kwamba Mungu aliwahi kufanya kitu kama hiki, na kuapa kwamba Mungu asingewahi kuangamiza ulimwengu kwa njia hii tena. Katika agano hili, tunauona moyo wa Mungu—tunaona kwamba moyo wa Mungu ulikuwa katika maumivu Alipoangamiza binadamu hawa. Katika lugha ya binadamu, wakati Mungu aliangamiza mwanadamu na Akaona mwanadamu akitoweka, moyo Wake ulikuwa ukiomboleza na kuvuja damu. Je, hivyo sivyo tunavyoweza kuifafanua kwa njia bora zaidi? Maneno haya yanatumika na binadamu kuonyesha hisia za binadamu, lakini kwa sababu lugha ya binadamu inao ukosefu mwingi, kuitumia kufafanua hisia za Mungu hakuonekani kuwa mbaya sana kwangu Mimi, na wala si kubwa mno. Angaa inawapa uelewa sahihi kabisa, wa kufaa zaidi, wa hali ya Mungu ilivyokuwa wakati huo. Sasa mtafikiria nini mtakapouona upinde wa mvua tena? Angaa mtakumbuka namna ambavyo Mungu aliwahi kuwa katika huzuni kwa sababu ya kuangamiza ulimwengu kwa gharika. Mtakumbuka namna, hata kama Mungu aliuchukia ulimwengu huu na kudhalilisha binadamu hawa, Alipowaangamiza wanadamu Alioumba kwa mikono Yake mwenyewe, moyo Wake ulikuwa ukisononeka, ukipambana kuachilia, ukihisi kusita, na kuhisi vigumu kuvumilia mambo. Tulizo lake pekee lilikuwa katika familia ya wanane ya Nuhu. Ulikuwa ni ushirikiano wa Nuhu uliofanya jitihada Zake za kipekee za kuumba viumbe wote kuwa cha thamani. Kwa wakati ambao Mungu alikuwa akiteseka, hili ndilo jambo tu ambalo lingeweza kusawazisha maumivu Yake. Kuanzia hapo, Mungu aliweka matarajio Yake yote ya binadamu kwa familia ya Nuhu, akitumai kwamba wangeishi chini ya baraka Zake na si laana Yake, akitumai kwamba wasingewahi kumwona Mungu akiuangamiza ulimwengu kwa gharika na pia akitumai kwamba wasingeangamizwa.

Ni sehemu gani ya tabia ya Mungu tunayofaa kuelewa kutoka hapa? Mungu alikuwa amemdharau binadamu kwa sababu binadamu alikuwa na uadui na Yeye, lakini ndani ya moyo Wake, utunzaji Wake, kujali Kwake, na huruma Yake kwa binadamu vilibakia vilevile. Hata wakati alipowaangamiza wanadamu, moyo Wake hukubadilika. Wakati binadamu walikuwa wamejaa upotovu na kutotii Mungu hadi katika kiwango fulani, Mungu alilazimika, kwa sababu ya tabia Yake na kiini Chake, na kulingana na kanuni Zake, kuangamiza binadamu hao. Lakini kwa sababu ya kiini cha Mungu, bado Alisikitikia binadamu, hata Akataka kutumia njia mbalimbali za kuwakomboa wanadamu ili waweze kuendelea kuishi. Badala yake, binadamu alimpinga Mungu, akaendelea kutomtii Mungu, na kukataa kukubali wokovu wa Mungu, yaani, alikataa kukubali nia Zake nzuri. Haijalishi ni vipi Mungu aliwaita wao, aliwakumbusha, akawatosheleza haja zao, akawasaidia wao, au akawavumilia wao, binadamu hakutambua haya, wala hakutilia maanani. Katika maumivu Yake, Mungu bado hakusahau kumpa binadamu uvumilivu Wake wa kiwango cha juu zaidi, akisubiri binadamu kugeuka na kubadilika. Baada ya Yeye kufikia kikomo Chake, Alifanya kile Alicholazimika kufanya bila ya kusita. Kwa maneno mengine, kulikuwa na kipindi cha muda mahususi na mchakato kutoka pale ambapo Mungu alipanga kuangamiza wanadamu hadi katika mwanzo rasmi wa kazi Yake ya kuwaangamiza wanadamu. Mchakato huu ulikuwepo kwa kusudio la kumwezesha binadamu kugeuka, na ndio uliokuwa fursa ya mwisho ya Mungu kumpa binadamu. Hivyo ni nini ambacho Mungu alifanya kwenye kipindi hiki kabla ya kuangamiza wanadamu? Mungu alifanya kiwango kikubwa cha kazi ya kukumbusha na kazi ya kusihi. Haijalishi ni maumivu kiasi kipi na huzuni ambayo ilikuwa ndani ya moyo wa Mungu, Aliendelea kufanyisha zoezi utunzaji Wake, wasiwasi, na huruma nyingi juu ya binadamu. Tunaona nini kutoka kwa haya? Bila shaka, tunaona kwamba upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wa kweli na si tu jambo ambalo Analizungumzia tu bila matendo. Ni jambo hakika, linaloweza kushikika na kutambulika, si bandia, halijatiwa najisi, halidanganyi wala halisingizii. Mungu kamwe hatumii uongo au kuunda taswira za bandia ili kufanya watu kuona kwamba Yeye anapendeka. Kamwe hatumii ushuhuda wa uongo ili kuwafanya kuona uzuri Wake, au kuringia uzuri wake na utakatifu Wake. Je, dhana hizi za tabia ya Mungu zinastahili upendo wa binadamu? Kwani nazo hazistahili kuabudiwa? Kwani nazo hazistahili kupendwa sana? Kwa sasa, Ningependa kuwauliza: Baada ya kuyasikia maneno haya, mnafikiri kwamba ukubwa wa Mungu ni maneno matupu tu kwenye kipande cha karatasi? Je, uzuri wake Mungu ni maneno matupu tu? La! Bila shaka la! Mamlaka ya juu, ukubwa, utakatifu, uvumilivu, upendo, wa Mungu na kadhalika—kila utondoti wa kila mojawapo ya vipengele vya tabia ya Mungu na kiini Chake unapata maonyesho ya vitendo kila wakati Anapoanza kazi Yake, zikiwa katika mapenzi Yake kwa binadamu, na pia zikitimizwa na kuonyeshwa kwa kila mtu. Licha ya kama umewahi kuzihisi awali, Mungu anamtunza kila mtu katika kila njia inayowezekana, kwa kutumia moyo Wake wa dhati, hekima, na mbinu mbalimbali ili kupashana mioyo ya kila mtu, na kuzindua roho ya kila mmoja. Huu ni ukweli usiopingika.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 29)

Mungu aliwaumba wanadamu; licha ya kama wamepotoka au kama wanamfuata Yeye, Mungu hushughulikia binadamu kama wapendwa Wake wanaothaminiwa zaidi—au kama vile binadamu wangesema, watu walio wapenzi Wake sana—na wala si kama vikaragosi Wake. Ingawaje Mungu anasema Yeye ndiye muumba na kwamba binadamu ni uumbaji Wake, hali ambayo inaweza kuonekana ni kana kwamba kuna tofauti kiasi katika mpangilio wa cheo, uhalisia ni kwamba kila kitu ambacho Mungu amefanya kwa mwanadamu kinazidi kabisa uhusiano wa asili hii. Mungu anampenda mwanadamu, anamtunza mwanadamu, na anaonyesha kwamba anamjali mwanadamu, pamoja na kumkimu mwanadamu bila kuacha na bila ya kusita. Kamwe hahisi katika moyo Wake kwamba hii ni kazi ya ziada au ni kitu kinachostahili sifa nyingi. Wala Hahisi kwamba kuokoa binadamu, kuwatosheleza, na kuwapatia kila kitu, ni kutoa mchango mkuu kwa binadamu. Anamkimu tu mwanadamu kimyakimya na kwa unyamavu, kwa njia Yake mwenyewe na kupitia kwa kiini Chake na kile Anacho na alicho. Haijalishi ni toleo kiasi kipi na ni msaada kiasi kipi ambao wanadamu wanapokea kutoka kwa Yeye, Mungu siku zote hajawahi kufikiri kuhusu au kujaribu kutaka sifa yoyote. Hii inaamuliwa na kiini cha Mungu, na pia hasa ni maonyesho ya kweli pia ya tabia ya Mungu. Na ndio maana, haijalishi kama iko kwa Biblia au kitabu chochote kingine, hatujawahi kumpata Mungu akionyesha fikira Zake, na hatujawahi kumpata Mungu akifafanua au akitangazia wanadamu ni kwa nini Anafanya mambo haya, au ni kwa nini Anamjali sana mwanadamu, ili kumfanya mwanadamu kumshukuru Yeye au kumsifu Yeye. Hata wakati Amejeruhiwa, wakati moyo Wake umo katika maumivu makali, Hajawahi kusahau jukumu Lake kwa mwanadamu au wasiwasi Wake kwa mwanadamu, huku haya yote yakiendelea, Anavumilia madhara na maumivu akiwa pekee katika ukimya. Kinyume cha mambo ni kwamba, Mungu anaendelea kumkimu mwanadamu kama Anavyofanya siku zote. Ingawaje mwanadamu mara nyingi humsifia Mungu au huwa na ushuhuda Kwake, hakuna kati ya tabia hii ambayo imedaiwa na Mungu. Hii ni kwa sababu Mungu hajawahi kunuia mambo yoyote mazuri Anayomfanyia binadamu yeye pia naye kumfanyia vivyo hivyo kama ishara ya shukrani au ili iweze kuonekana kwamba anafanyiwa mazuri aliyofanya. Kwa mkono mwingine, wale wanaomcha Mungu na kujiepusha na maovu, wale wanaomfuata Mungu kwa kweli, wanaomsikiliza Yeye, na walio waaminifu Kwake yeye, na wale wanaomtii Yeye—hawa ndio watu ambao mara nyingi watapokea baraka za Mungu, na Mungu atawakabidhi baraka hizo bila kusita. Isitoshe, baraka ambazo watu hupokea kutoka kwa Mungu mara nyingi zinazidi kufikiria kwao na pia zinazidi kitu chochote ambacho binadamu wanaweza kubadilishana na yale waliyofanya au gharama waliyolipia. Wakati mwanadamu anafurahia baraka za Mungu, Je, yupo yeyote anayejali ni nini Mungu anafanya? Je, yupo yeyote anayeonyesha wasiwasi wowote kuhusu vile ambavyo Mungu anahisi? Je, yupo yeyote anayethamini maumivu ya Mungu? Jibu la uhakika la maswali haya ni: La! Je, mwanadamu yeyote, akiwemo Nuhu, anaweza kuthamini yale maumivu ambayo Mungu alikuwa akihisi wakati huo? Je, mtu yeyote anaweza kufahamu ni kwa nini Mungu alianzisha agano kama hilo? Hakuna anayeweza! Mwanadamu hathamini maumivu ya Mungu si kwa sababu hawezi kuelewa maumivu ya Mungu, na si kwa sababu ya nafasi iliyopo kati ya Mungu na mwanadamu au tofauti kati ya hadhi yao; badala yake, ni kwa sababu mwanadamu hata hajali kuhusu hisia zozote za Mungu. Mwanadamu anafikiria Mungu yuko huru—Mungu hahitaji watu wa kujali kuhusu Yeye, kumwelewa au kumwonyesha namna anavyomfikiria. Mungu ni Mungu, hivyo Hana maumivu, hana hisia; Hatakasirika, Hahisi huzuni, hata Halii. Mungu ni Mungu, hivyo Hahitaji maonyesho yoyote ya kihisia na Hahitaji faraja yoyote ya kihisia. Kama Hahitaji mambo haya katika hali fulani, basi Atatatua mwenyewe na Hatahitaji usaidizi wowote kutoka kwa mwanadamu. Lakini kinyume chake ni kuwa, ni wale binadamu wanyonge, wanaohitaji tulizo, toshelezo, himizo la Mungu na hata pia kwake Yeye kuweza kutuliza hisia zao wakati wowote mahali popote. Fikira kama hiyo inajificha ndani kabisa ya mioyo ya mwanadamu: Binadamu ndiye mnyonge; wanahitaji Mungu ili awatunze kwa kila njia, wanastahili utunzaji wote wanaopokea kutoka kwa Mungu, na wanafaa kudai kutoka kwa Mungu chochote kile wanachohisi kinafaa kuwa ni chao. Mungu ndiye mwenye Nguvu; Anacho kila kitu, na Anahitaji kuwa mlezi wa mwanadamu na Anayetoa baraka. Kwa sababu Yeye tayari ni Mungu, Yeye Mwenyezi na Hahitaji katu chochote kutoka kwa mwanadamu.

Kwa vile binadamu hatilii maanani ufunuo wowote wa Mungu, hajawahi kuhisi huzuni, maumivu au furaha ya Mungu. Lakini kinyume chake ni kwamba, Mungu anajua maonyesho yote ya binadamu kama vile anavyojua sehemu ya kiganja cha mkono Wake. Mungu hutosheleza mahitaji ya kila mtu siku zote na pahali pote, akiangalia fikira zinazobadilika za kila mmoja na hivyo basi kuwatuliza na kuwahimiza, na kuwaongoza na kuwaangazia. Kuhusu mambo yote ambayo Mungu amemfanyia mwanadamu, na gharama zote Alizolipia kwa sababu yao, watu wanaweza kupata kifungu kutoka kwa Biblia au kutoka kwa chochote ambacho Mungu amesema mpaka sasa kinachoelezea waziwazi kwamba Mungu atadai kitu kutoka kwa binadamu? La! Kinyume cha mambo, haijalishi ni vipi watu wanapuuza kufikiria kwa Mungu, Bado Anawaongoza kwa marudio wanadamu, Anamkimu kwa kurudia mwanadamu na kumsaidia, kuwaruhusu kufuata njia za Mungu ili waweze kupokea hatima nzuri ambayo Amewatayarishia. Inapokuja kwa Mungu, kile Anacho na alicho, neema Yake, rehema Yake, na tuzo Zake zote, zitakabidhiwa bila ya kusita kwa wale wanaompenda na kumfuata Yeye. Lakini hajawahi kufichua kwa mtu yeyote maumivu aliyopitia Yeye au hali ya akili Yake, na katu halalamiki kuhusu yeyote ambaye hamtilii Yeye maanani au hajui mapenzi Yake. Anavumilia tu haya yote kimyakimya, akisubiria siku ambayo mwanadamu ataweza kuelewa.

Kwa nini Nasema mambo haya hapa? Ni nini mnachoona kutoka kwa mambo haya Niliyosema? Kuna kitu katika kiini na tabia ya Mungu ambacho ndicho rahisi zaidi kupuuza, kitu ambacho kinamilikiwa tu na Mungu na wala si mtu yeyote, wakiwemo wale wengine wanafikiria kwamba ni watu wakubwa, watu wazuri, au Mungu wa kufikiria kwao. Kitu hiki ni nini? Ni kule kutokuwa na nafsi kwa Mungu. Tunapozungumzia kutokuwa na nafsi, unaweza kufikiria kwamba pia wewe huna nafsi, kwa sababu inapokuja kwa watoto wako, haujadiliani juu ya bei na wao na wewe ni mkarimu sana kwao, au unafikiria kwamba wewe huna nafsi sana inapokuja kwa wazazi wako. Haijalishi ni nini unafikiria, angaa unayo dhana ya neno “kutokuwa na nafsi” na unalifikiria kama neno zuri, na kwamba kuwa mtu asiye na nafsi ni jambo la kipekee. Wakati huna nafsi, unafikiri kuwa wewe ni mkubwa. Lakini hakuna mtu anayeweza kuona kutokuwa na nafsi kwa Mungu miongoni mwa viumbe wote, miongoni mwa watu, hafla, na vitu, na kupitia kazi ya Mungu. Kwa nini hali iko hivi? Kwa sababu binadamu ni mchoyo sana! Kwa nini Ninasema hivyo? Mwanadamu anaishi katika ulimwengu wa uyakinifu. Unaweza kumfuata Mungu, lakini huoni wala kushukuru namna ambavyo Mungu anakukimu, anavyokupenda na anavyoonyesha kwamba anakujali. Kwa hivyo unaona nini? Unaona watu wako wa ukoo wanaokupenda au kukupenda sana. Unayaona mambo ambayo ni ya manufaa kwa mwili wako, unajali kuhusu watu na vitu unavyopenda. Huku ndiko kutokuwa na nafsi kwa binadamu kunakodaiwa. Watu kama hao “wasiokuwa na nafsi” hata hivyo, huwa hawajali katu kuhusu Mungu anayewapa maisha. Kinyume na Mungu, kutokuwa na nafsi kwa binadamu kunakuwa cha nafsi na yenye uchoyo. Kutokuwa na nafsi ambako binadamu anasadiki katika ni ulio mtupu na usio halisi, uliotiwa madoa, usiolingana na Mungu, na usiohusika na Mungu. Kutokuwa na nafsi kwa binadamu ni kwa ajili yake, huku kutokuwa na nafsi kwa Mungu ni ufunuo wa kweli wa kiini Chake. Ndipo hasa kutokana na kujitolea nafsi kwa Mungu ndipo binadamu anapokea mfululizo usiosita wa ujazo kutoka kwake. Huenda msiathirike sana na mada hii Ninayozungumza kuhusu leo na unaweza kuwa tu unatikisa kichwa chako kwa kukubaliana nami, lakini wakati unapojaribu kufurahia moyo wa Mungu katika moyo wako, utaweza kwa kutojua kugundua: Miongoni mwa watu wote, masuala, na mambo unaweza kuhisi katika ulimwengu huu ni kutokuwa na nafsi tu kwa Mungu ambako ni kweli na dhabiti, kwa sababu ni upendo wa Mungu tu kwako ndio ambao hauna masharti na hauna madoa. Mbali na Mungu, kutokuwa na kile kinachodaiwa kutokuwa na nafsi wa mtu mwingine ni bandia, cha juujuu, kisicho na msingi; kina kusudio, nia fulani, kinatekeleza shughuli ya masikilizano, na hakiwezi kupimwa kamwe. Mnaweza hata kusema kwamba ni ki chafu, na cha kudharauliwa. Je, mnakubali?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Maneno ya Mungu ya Kila Siku (Dondoo 30)

Mwa 9:11-13  Na nitaweka agano langu na ninyi, wala miili yote haitaondolewa tena na maji ya gharika; wala hakutakuwa na gharika tena kuiharibu dunia. Naye Mungu akasema, Hii ni alama ya agano ambayo naifanya kati ya Mimi na ninyi na viumbe vyote vyenye uhai vilivyo nanyi, kwa vizazi vya kudumu: naweka upinde wangu mawinguni, na utakuwa alama ya agano kati ya Mimi na dunia.

Mwishoni mwa hadithi ya Nuhu, tunaona kwamba Mungu alitumia mbinu isiyo ya kawaida kuelezea hisia Zake wakati huo. Mbinu hii ni maalumu sana, na ni kuweka agano na binadamu. Ni mbinu inayotangaza mwisho wa matumizi ya gharika na Mungu katika kuangamiza ulimwengu. Kutoka nje, kuweka agano kunaonekana kuwa jambo lililo la kawaida sana. Si jambo lolote zaidi ya kutumia maneno kufunga wahusika ili wasitende vitendo vitakavyokiuka agano, ili kusaidia kutimiza kusudio la kulinda maslahi ya pande zote mbili. Kwa umbo, ni jambo la kawaida sana, lakini kutoka kwa motisha zilizopo na maana ya Mungu kufanya kitu hiki, ni ufunuo wa kweli wa tabia ya Mungu na hali Yake ya akili. Endapo utayaweka maneno haya kando na kuyapuuza, kama Sitawahi kukuambia ukweli wa mambo, basi binadamu hawatawahi kwa hakika kujua kufikiria kwa Mungu. Pengine katika kufikiria kwako Mungu alikuwa akitabasamu wakati alipofanya agano hili, au pengine maonyesho Yake yalikuwa mazito, lakini haijalishi ni watu wanavyofikiria Mungu alikuwa na maonyesho gani ya kawaida kabisa, hakuna ambaye angeweza kuuona moyo wa Mungu au maumivu Yake, na hata upweke Wake. Hakuna mtu anayeweza kumfanya Mungu kumwamini au anayestahili kuaminiwa na Mungu, au kuwa mtu Anayeweza kueleza fikira Zake au kuwa mwandani Wake wa kuambia maumivu Yake. Ndiyo maana Mungu hakuwa na chaguo ila kufanya kitu kama hicho. Kwa juujuu, Mungu alifanya jambo rahisi la kuwaaga binadamu wale wa awali, kuhitimisha hali ya kale ilivyokuwa na kufikia hitimisho halisi katika kuangamiza Kwake kwa ulimwengu akitumia gharika. Hata hivyo, Mungu alikuwa ameyazika maumivu kutoka muda huu ndani kabisa ya moyo Wake. Kwa wakati ambao Mungu hakuwa na yeyote wa kuita mwandani, aliunda agano na wanadamu, akiwaambia kwamba asingeuangamiza ulimwengu kwa gharika tena. Wakati upinde wa mvua unapojitokeza ni kukumbusha watu kwamba, kitu kama hicho kiliwahi kufanyika, kuwapa onyo watu dhidi ya kufanya maovu. Hata katika hali hiyo ya maumivu, Mungu hakusahau kuwahusu wanadamu na bado akaonyesha kujali kwingi sana kwao. Je, huu si upendo na kutokuwa na nafsi kwa Mungu? Lakini nao watu wanafikiria nini wakati wanapoteseka? Kwani huu si wakati ambao wanamhitaji Mungu zaidi? Katika nyakati kama hizi, siku zote watu humkokota Mungu katika mambo yao ili Mungu aweze kuwapa tulizo. Haijalishi ni lini, Mungu hatawahi kuwavunja moyo watu wake, na siku zote Atawaruhusu watu kutoka katika changamoto zao na kuishi katika mwangaza. Ingawaje Mungu anawakimu wanadamu, ndani wa moyo wa binadamu, Mungu si chochote wala lolote ila tembe ya kumhakikishia tu mambo, dawa ya tulizo. Wakati Mungu anateseka, wakati moyo Wake una majeraha, kuwa na kiumbe aliyeumba au mtu yeyote wa kuwa mwandani wake au wa kumtuliza Yeye kwa kweli kwake Mungu ni tamanio tu la kibadhirifu asiloweza kutegemea. Siku zote binadamu hatilii maanani hisia za Mungu, hivyo Mungu siku zote haulizii wala hatarajii kuwa kuna mtu anayeweza kumtuliza Yeye. Anatumia mbinu Zake mwenyewe kueleza hali Yake. Watu hawafikirii kwamba ni jambo kubwa kwa Mungu kupitia mateso fulani, lakini unapojaribu tu kuelewa Mungu kwa kweli, unapoweza kushukuru kwa dhati, nia nzuri za Mungu katika kila kitu anachofanya, ndipo unapoweza kuhisi ukubwa wa Mungu na kutokuwa na nafsi kwake. Ingawaje Mungu aliunda agano na wanadamu kutumia upinde wa mvua, hakuwahi kuambia yeyote kwa nini alifanya hivi, kwa nini alianzisha agano hili, kumaanisha hakuwahi kuambia mtu fikira Zake halisi. Hii ni kwa sababu hakuna mtu anayeweza kufahamu kina cha upendo ambao Mungu anao kwa wanadamu Aliowaumba kwa mikono Yake mwenyewe, na hakuna pia mtu anayeweza kutambua ni kiasi kipi cha maumivu moyo Wake uliteseka wakati Alipoangamiza binadamu. Hivyo basi, hata kama Angeambia watu namna Anavyohisi, hawawezi kumwamini. Licha ya kuwa katika maumivu, angali Anaendelea na hatua inayofuata ya kazi Yake. Siku zote Mungu Anautoa upande wake bora zaidi na mambo bora zaidi kwa wanadamu huku yeye Mwenyewe Akistahimili kimyakimya mateso yote. Mungu kamwe hafichui mateso haya. Badala yake, Anayavumilia na kusubiri kwa kimya. Ustahimilivu wa Mungu si wa kimya tu, usio na hisia, au usio na suluhu, wala si ishara ya unyonge. Ni kwamba upendo na kiini cha Mungu siku zote yamekuwa bila nafsi. Huu ni ufunuo wa kiasili wa kiini na tabia Yake na maonyesho halisi wa utambulisho wa Mungu kama Muumba wa kweli.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Iliyotangulia: Hatima na Matokeo

Inayofuata: Kumjua Mungu (II)

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp