Tabia ya Mungu na Kile Anacho na Alicho

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 232)

Mimi ni mwenye haki, Mimi ni mwaminifu, Mimi ndimi Mungu anayechunguza moyo wa ndani zaidi wa mwanadamu! Nitafichua mara moja aliye wa kweli na aliye wa uongo. Hakuna haja ya kuwa na hofu, vitu vyote hufanya kazi kwa wakati Wangu. Ni nani ananitaka kwa dhati, ni nani asiyenitaka kwa dhati—Nitawaambia. Kuleni tu vizuri, kunyweni vizuri, njoo mbele Yangu na Nikaribieni nami Nitafanya kazi Yangu Mwenyewe. Msiwe na hamu sana ya matokeo ya haraka, kazi Yangu si kitu ambacho kinaweza kufanywa mara moja. Ndani yake kuna hatua Zangu na hekima Yangu, hivyo hekima Yangu inaweza kufichuliwa. Nitawawezesha kuona ni nini kinachofanywa kwa mikono Yangu—kuadhibu uovu na kuzawadia mema. Mimi hakika Simpendelei mtu yeyote. Ninakupenda kwa dhati wewe unayenipenda kwa dhati, na ghadhabu Yangu daima itakuwa pamoja na wale wasionipenda kwa dhati, ili kwamba waweze kukumbuka daima kwamba Mimi ni Mungu wa kweli, Mungu anayechunguza moyo wa ndani zaidi wa mwanadamu. Usitende kwa njia moja mbele ya wengine na utende kwa namna nyingine bila wao kufahamu; Ninaona wazi kila kitu unachofanya na ingawa unaweza kuwadanganya wengine huwezi kunidanganya Mimi. Ninaona yote waziwazi. Haiwezekani kwako kuficha chochote; vyote vimo mikononi Mwangu. Usifikiri kuwa wewe ni mjanja sana, kwa kufanya hesabu zako ndogondogo zikufaidi. Nakwambia: Haijalishi mwanadamu anaweza kubuni mipango kiasi kipi, iwe elfu kadhaa ama elfu nyingi, mwishowe hawezi kuepuka kutoka kwenye kiganja cha mkono Wangu. Vitu na matukio yote huendeshwa katika mikono Yangu, sembuse mtu mmoja! Usijaribu kuepuka au kujificha, usijidanganye au kuficha. Je, huwezi kuona kwamba uso Wangu mtukufu, hasira Yangu na hukumu Yangu imefichuliwa hadharani? Nitahukumu mara moja na bila huruma wale wote ambao hawanitaki Mimi kwa dhati. Huruma Yangu imefika mwisho na hakuna tena iliyobaki. Usiwe mnafiki tena na acha njia zako za kishenzi.

Mwanangu, tahadhari; tumia muda zaidi mbele Zangu nami Nitakuwa msaada wako. Usiogope, toa upanga Wangu mkali wenye makali kuwili, na—kulingana na mapenzi Yangu—pigana na Shetani mpaka mwishoni, Nitakulinda; usiwe na wasiwasi. Mambo yote yaliyofichwa yatafunguliwa na kufichuliwa. Mimi ni Jua ambalo linatoa nuru, likimulika giza lote bila huruma. Hukumu Yangu imeshuka kabisa na kanisa ni uwanja wa vita. Nyote mnapaswa kuwa tayari na mnapaswa kutoa nafsi zenu zote kwa vita vya mwisho vya uamuzi; Mimi hakika Nitakulinda ili uweze kunipigania vita vizuri, vya ushindi.

Kuwa makini, mioyo ya watu leo ni yenye udanganyifu na haitabiriki na hawapaswi kuaminiwa. Ni Mimi tu Niliye upande wako kabisa. Hakuna udanganyifu ndani Yangu; Niegemee Mimi tu! Hakika wana Wangu watashinda katika vita vya mwisho vya uamuzi na bila shaka Shetani atajitokeza na kushambulia katika uchungu wake wa kifo. Usiogope! Mimi ni nguvu yako, Mimi ni kila kitu chako. Usifikiri juu ya mambo mara kwa mara, huwezi kushughulikia mawazo mengi sana. Nimesema hapo awali, Sitawavuta tena katika njia kwa kuwa hakuna muda wa kupoteza hata kidogo. Sina wakati wa kuwahitaji msikilize kwa makini tena na kuwakumbusha—haiwezekani! Malizeni tu maandalizi yenu kwa ajili ya vita. Mimi nakuwajibikia kikamilifu; vitu vyote viko mikononi Mwangu. Hivi ni vita vya kufa na kupona na yatakuwa mapambano ya kufa na kupona. Lakini unapaswa kutambua kwamba Mimi ni mshindi milele na Asiyeshindwa, na kwamba Shetani bila shaka ataangamia. Hii ni mbinu Yangu, kazi Yangu, mapenzi Yangu na mpango Wangu!

Imekamilika! Yote yamekamilika! Usiwe mwoga au mwenye hofu. Mimi pamoja na wewe na wewe pamoja na Mimi tutakuwa wafalme milele na milele! Maneno ambayo Nimesema hayatabadilika milele na matukio yatawafika hivi karibuni. Kesheni! Mnapaswa kutafakari vizuri kila neno; msiwe na mashaka kuyahusu tena. Lazima muwe wazi kuyahusu! Kumbuka—tumia muda zaidi mbele Zangu!

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 44

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 233)

Nimeanza kuchukua hatua ya kuadhibu wale ambao hufanya uovu, wale ambao hushika madaraka, na wale ambao hutesa wana wa Mungu. Kuanzia sasa kuendelea, mkono wa amri Zangu za utawala utakuwa daima juu ya wale wanaonipinga mioyoni mwao. Fahamu hili! Huu ndio mwanzo wa hukumu Yangu, na hakuna huruma itakayoonyeshwa kwa yeyote wala hakuna atakayesamehewa, kwani Mimi ni Mungu asiyependelea ambaye hutenda haki, na ingekuwa vyema kwenu nyote kutambua hili.

Si kwamba Nataka kuadhibu wale ambao hufanya uovu, badala yake ni adhabu inayoletwa kwao na uovu wao wenyewe. Mimi si mwepesi wa kumwadhibu yeyote, wala simtendei mtu yeyote isivyo haki—Ninatenda haki kwa wote. Hakika Mimi nawapenda Wanangu na kwa hakika Ninawachukia wale waovu wanaoniasi; hii ndiyo kanuni nyuma ya matendo Yangu. Kila mmoja wenu anapaswa kuwa na umaizi wa amri Zangu za utawala. Iwapo sivyo, hamtakuwa na hofu hata kidogo na mtakuwa wazembe mbele Yangu, na hamtajua kile Ninachotaka kukamilisha, kile Ninachotaka kufanya kuwa kamili, kile Ninachotaka kupata ama ufalme Wangu unahitaji mtu wa aina gani.

Amri Zangu za utawala ni:

1. Haijalishi wewe ni nani, ukinipinga Mimi katika moyo wako, utahukumiwa.

2. Kwa wale ambao Nimechagua, watafundishwa nidhamu mara moja kwa wazo lolote lisilo sahihi.

3. Nitawaweka wale wasioniamini upande mmoja. Nitawaruhusu wazungumze na kutenda kwa uzembe hadi mwisho kabisa ambapo Nitawaadhibu kabisa na kupambana nao.

4. Kwa wale ambao wananiamini, Nitawatunza na kuwalinda nyakati zote. Nyakati zote Nitawapa uzima kwa kutumia njia ya wokovu. Watu hawa watakuwa na upendo Wangu na hakika hawataanguka ama kupoteza njia yao. Udhaifu wowote ambao wako nao utakuwa wa muda, na kwa hakika Sitaukumbuka.

5. Kwa wale ambao wanaonekana kuamini lakini ambao kwa kweli hawaamini—kumaanisha wale ambao wanaamini kuna Mungu lakini hawamtafuti Kristo, lakini ambao pia hawapingi—watu wa aina hii ni wa kusikitisha zaidi, na kupitia vitendo Vyangu Nitawafanya waone kwa dhahiri. Kupitia matendo Yangu, Nitawaokoa watu wa aina hizi na kuwarudisha.

6. Wazaliwa wa kwanza ambao walikuwa wa kwanza kukubali jina Langu watabarikiwa! Hakika Nitawapa baraka bora zaidi na mtakuwa na furaha hadi kuridhika kwa mioyo yenu; hakuna atakayethubutu kuizuia. Kila kitu kimetayarishwa kabisa kwa ajili yenu, kwani hii ni amri Yangu ya utawala.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 56

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 234)

Wamebarikiwa wale ambao wamelisoma neno Langu na kuamini kwamba litatimizwa—Sitakutendea vibaya, lakini Nitafanya yale unayoamini yatimizwe ndani yako. Hii ni baraka Yangu ikija kwako. Neno Langu linapiga siri zilizofichwa ndani ya kila mtu. Kila mtu ana majeraha ya mauti, na Mimi ni tabibu mzuri ambaye anayaponya—njoo tu katika uwepo Wangu. Kwa nini Nilisema kuwa katika siku zijazo hakutakuwa na huzuni tena na hakutakuwa na machozi tena? Ni kwa sababu ya hili. Ndani Yangu, kila kitu kinatimizwa, lakini ndani ya wanadamu, vitu vyote ni vipotovu na bure, na vyote ni vidanganyifu kwa wanadamu. Katika uwepo Wangu utapokea vitu vyote, na utaona na pia kufurahia baraka zote ambazo hungewahi kufikiria. Wale wasiokuja mbele Yangu bila shaka ni waasi, na hakika ndio wanaonipinga Mimi. Hakika Sitawaacha kwa urahisi; Nitamwadibu vikali mtu wa aina hii. Kumbuka hili! Wale wanaokuja mbele Yangu zaidi watapata zaidi, lakini haitakuwa zaidi ya neema. Baadaye, watapata baraka nyingi hata zaidi.

Tangu uumbaji wa ulimwengu Nimeanza kuamulia kabla na kuchagua kundi hili la watu, yaani, ninyi leo. Tabia yako, ubora wa tabia, sura, kimo, familia ambayo ulizaliwa kwayo, kazi yako na ndoa yako, nafsi yako yote, hata rangi ya nywele zako na ngozi yako, na wakati wa kuzaliwa kwako vyote vilipangwa na mikono Yangu. Hata mambo unayofanya na watu unaokutana nao kila siku hupangwa na mikono Yangu, sembuse ukweli kwamba kukuleta katika uwepo Wangu leo kwa kweli ni mpango Wangu. Usijitupe katika vurugu; unapaswa kuendelea kwa utulivu. Kile Ninachokuruhusu kufurahia leo ni mgawo ambao wewe unastahili, na Nilikipangia kabla katika uumbaji wa dunia. Wanadamu wote ni waliozidi sana—wao huwa vichwa ngumu sana au wasio na aibu kabisa. Hawawezi kufanya mambo kulingana na mpango Wangu na mpangilio. Usifanye hilo tena. Ndani Yangu vyote vinakombolewa; usijifunge mwenyewe, kwani utayapoteza maisha yako. Kumbuka hili!

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 74

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 235)

Mimi ni Mungu Mwenyewe wa pekee, hata zaidi Mimi pekee ndimi nafsi ya Mungu, na Mimi, ukamilifu wa mwili, ni hata zaidi dhihirisho kamili la Mungu. Yeyote asiyethubutu kuniheshimu Mimi, yeyote anayethubutu kuonyesha dharau machoni pake, yeyote anayethubutu kusema maneno ya chuki dhidi Yangu hakika atakufa kutokana na laana na ghadhabu Yangu (kutakuwa na kulaani kwa sababu ya ghadhabu Yangu). Na yeyote ambaye hatathubutu kuwa mwaminifu au na upendo Kwangu, yeyote anayethubutu kujaribu kunihadaa hakika atakufa katika chuki Yangu. Haki yangu, uadhama na hukumu yangu vitadumu milele na milele. Mwanzoni, Nilikuwa mwenye upendo na rehema, lakini hii si tabia ya uungu Wangu kamili; haki, uadhama na hukumu ni tabia Yangu tu—Mungu Mwenyewe mkamilifu. Wakati wa Enzi ya Neema Nilikuwa mwenye upendo na rehema. Kwa sababu ya kazi Niliyopaswa kumaliza Nilikuwa na fadhila na rehema, lakini baadaye hakukuwa na haja ya fadhila yoyote au rehema (hakujakuwepo na yoyote tangu wakati huo). Yote ni haki, uadhama na hukumu na hii ni tabia kamili ya ubinadamu Wangu wa kawaida pamoja na uungu Wangu kamili.

Wale ambao hawanijui wataangamia katika kuzimu na wale ambao wana uhakika kunihusu wataishi milele, ili watunzwe na kulindwa ndani ya upendo Wangu. Punde Ninenapo neno moja, ulimwengu mzima na miisho ya dunia hutetemeka. Ni nani anayeweza kusikia maneno Yangu na asitetemeke kwa hofu? Nani hawezi kukuza moyo ambao unanicha? Nani hawezi kujua haki Yangu na uadhama kutokana na matendo Yangu? Na nani hawezi kuona uweza Wangu na hekima ndani ya matendo Yangu? Yeyote asiyezingatia kwa hakika atakufa. Hii ni kwa sababu wale wasiozingatia ni wale wanaonipinga na wasionijua; wao ni malaika wakuu na ndio watukutu zaidi. Jichunguzeni: Yeyote aliye mtukutu, anayejidai na mwenye majivuno hakika ni mlengwa wa chuki Yangu na ataangamia!

Sasa Natamka amri za kiutawala za ufalme Wangu: Vitu vyote vimo ndani ya hukumu Yangu, vitu vyote vimo ndani ya haki Yangu, vitu vyote vimo ndani ya uadhama Wangu, na haki inatendwa kwa wote. Wale ambao husema wananiamini Mimi ilhali wananipinga mioyoni mwao, au ambao mioyo yao imeniacha watafukuzwa, lakini yote ni kwa wakati Wangu mzuri. Wale ambao huzungumza kwa kejeli kunihusu, lakini kwa njia ambayo watu hawatambui, watakufa mara moja (watafariki katika roho, mwili na nafsi). Kwa wale ambao huwadhulumu ama kuwadharau wale Ninaowapenda, ghadhabu Yangu itawahukumu mara moja. Hii ni kusema kwamba wale ambao wana mioyo ya wivu kwa wale Ninaowapenda na kufikiri kuwa Mimi si mwenye haki watakabidhiwa kwa wale ambao Ninawapenda ili kuwahukumu. Wale wote wenye tabia nzuri, wanyenyekevu (pamoja na wale ambao hawana hekima) na ambao ni watiifu kwa dhati Kwangu watabaki wote katika ufalme Wangu. Wale ambao hawajapitia katika mafunzo, kumaanisha watu ambao ni waaminifu wanaokosa hekima na ufahamu, watakuwa na uwezo katika ufalme Wangu. Hata hivyo wao pia wamepitia ushughulikiwaji na kuvunjwa. Kwamba hawajapitia mafunzo si hakika, lakini badala yake kupitia mambo hayo Nitaonyesha kila mtu uweza Wangu na hekima Yangu. Nitawafukuza wale ambao bado wananishuku sasa, Sitaki hata mmoja wao (Ninawachukia sana wale ambao bado wananishuku wakati kama huu). Kwa matendo ambayo Mimi hufanya katika ulimwengu wote, Nitawaonyesha watu waaminifu matendo Yangu ya kustaajabisha, papo kukuza busara zao, ufahamu na utambuzi, na Mimi mara moja Nitasababisha watu wadanganyifu kuharibiwa kwa ajili ya matendo Yangu ya kustaajabisha. Wazaliwa wote wa kwanza waliokuwa wa kwanza kulikubali jina Langu (kumaanisha wale watakatifu wasio na dosari, watu waaminifu) watakuwa wa kwanza kuingia katika ufalme na kutawala mataifa yote na watu wote pamoja na Mimi, kutawala kama wafalme katika ufalme na pamoja kuhukumu mataifa yote na watu wote (kumaanisha wazaliwa wote wa kwanza katika ufalme, na sio wengine). Wale walio katika mataifa yote na watu wote ambao wamekwisha kuhukumiwa na wametubu wataingia katika ufalme Wangu na kuwa watu Wangu, na wale ambao ni wakaidi na wasiotubu watatupwa katika shimo la kuzimu (ili waangamie milele). Hukumu katika ufalme itakuwa mara ya mwisho na itakuwa utakaso Wangu kwa kina duniani. Hakutakuwa tena na udhalimu wowote, huzuni yoyote, machozi yoyote na hata zaidi hakutakuwa na dunia. Kila kitu kitakuwa dhihirisho la Kristo, kila kitu kitakuwa ufalme wa Kristo. Utukufu ulioje! Utukufu ulioje!

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 79

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 236)

Sasa Nawatangazia rasmi amri Zangu za utawala (zinaanza kazi kuanzia siku zilipotangazwa rasmi, kutoa kuadibu tofauti kwa watu tofauti):

Natimiza ahadi Zangu, na kila kitu kiko mikononi Mwangu: Yeyote aliye na shaka hakika atauwawa. Hakuna nafasi ya huruma yoyote; wataangamizwa mara moja, hivyo kuondoa chuki kutoka moyoni Mwangu. (Kuanzia sasa inathibitika kwamba yeyote anayeuwawa lazima asiwe mshiriki wa ufalme Wangu, na lazima awe wa ukoo wa Shetani.)

Kama wana wazaliwa wa kwanza, mnapaswa kushika nyadhifa zenu wenyewe na kutimiza wajibu wenu wenyewe vizuri, na wala msiwe wadadisi. Ni sharti mjitolee kwa mpango Wangu wa usimamizi, na popote muendapo, ni sharti muwe na ushuhuda mzuri Kwangu na mlitukuze jina Langu. Msitende vitu vya aibu; kuweni mfano kwa wana Wangu wote na watu Wangu. Msiwe waasherati hata kwa muda kidogo: Lazima muonekane kila mara mbele ya kila mtu mkiwa na utambulisho wa wana wazaliwa wa kwanza, na msiwe watumwa; badala yake, mnapaswa kutembea kwenda mbele kwa kujiamini. Nawaomba mlitukuze jina Langu, sio kulitia aibu jina Langu. Wale ambao ni wana wazaliwa wa kwanza wa kiume kila mmoja wao ana kazi yake binafsi, na hawawezi kufanya kila kitu. Hili ndilo jukumu Nililowapa, na halipaswi kuepukwa. Lazima mjitolee kwa mioyo yenu yote, kwa akili zenu zote na nguvu zenu zote, kwa kutimiza kile ambacho Nimewaaminia.

Kuanzia siku hii na kuendelea, katika ulimwengu wote mzima, jukumu la kuwachunga wana Wangu wote na watu Wangu wote litakabidhiwa kwa wana Wangu wazaliwa wa kwanza kutimiza, na Nitamwadhibu yeyote ambaye hawezi kujitolea moyo na akili yake yote kulitimiza. Hii ndiyo haki Yangu. Sitawaacha wala sitawahurumia hata wana Wangu wazaliwa wa kwanza.

Ikiwa kuna yeyote kati ya wana Wangu wote au kati ya watu Wangu wote anayemdhihaki na kumtusi mmoja wa wana Wangu wazaliwa wa kwanza, Nitamwadhibu vikali, kwa sababu wana Wangu wazaliwa wa kwanza wananiwakilisha Mimi Mwenyewe; kile ambacho mtu anawafanyia, ananifanyia Mimi pia. Hii ndiyo kali zaidi kati ya amri Zangu za utawala. Nitawaruhusu wazaliwa Wangu wa kwanza, kulingana na matamanio yao, watoe haki Yangu dhidi ya yeyote kati ya wana Wangu wote na watu Wangu anayeikiuka amri hii.

Taratibu Nitamtenga yeyote anayenitazama kipuuzi na anayelenga tu chakula Changu, mavazi na usingizi, anayeshughulikia tu mambo Yangu ya nje na haudhukuru mzigo Wangu, na hatilii maanani kutimiza kazi zake inavyostahili. Hili linaelekezwa kwa wote walio na masikio.

Yeyote amalizaye kunifanyia huduma lazima aondoke kwa utiifu bila vurugu yoyote. Kuwa makini, la sivyo Nitakushughulikia. (Hii ni amri ya ziada).

Wana Wangu wazaliwa wa kwanza watachukua fimbo ya chuma kuanzia sasa na kuendelea na kuanza kutekeleza mamlaka Yangu kutawala mataifa na watu wote, kutembea kati ya mataifa na watu wote na kuzitekeleza hukumu Zangu, haki, na uadhama kati ya mataifa yote na watu. Wana Wangu wote na watu Wangu wote wataniogopa, watanipa sifa, watanishangilia, na kunitukuza bila kukoma kwa sababu mpango wangu wa usimamizi umekamilika na wana Wangu wazaliwa wa kwanza wa kiume wanaweza kutawala nami.

Hii ni sehemu ya amri Zangu za utawala; baada ya hili, Nitawaambia kuyahusu kazi inapoendelea. Kutokana na amri za utawala zilizoko hapo juu, mtaona kasi ambayo kwayo Nafanya kazi Yangu, na vile vile ni hatua ipi ambayo kazi Yangu imefika. Hili litakuwa thibitisho.

Nimeshamhukumu Shetani. Kwa sababu mapenzi Yangu hayapingwi na kwa sababu wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume wametukuzwa pamoja na Mimi, tayari Nimetumia haki Yangu na uadhama juu ya dunia na vitu vyote ambavyo ni mali ya Shetani. Sikiinui kidole wala kumsikiliza Shetani kabisa (kwa sababu hastahili hata kuzungumza na Mimi). Nazidi tu kufanya kile Ninachotaka kufanya. Kazi Yangu inaendelea kwa ulaini, hatua kwa hatua, na mapenzi Yangu hayapingwi duniani kote. Hili limemwaibisha Shetani kwa kiwango na ameangamizwa kabisa, lakini hili peke yake halijatimiza mapenzi Yangu. Naruhusu pia wana Wangu wazaliwa wa kwanza kutekeleza amri Zangu za utawala juu ya mambo yote yaliyo ya Shetani. Kwa upande mmoja, kile Ninachomruhusu Shetani aone ni hasira Yangu kuelekea kwake; kwa upande, mwingine Namruhusu auone utukufu Wangu (kuona kwamba wana Wangu wazaliwa wa kwanza ndio mashahidi wakubwa sana kwa udhalilishaji wa shetani). Simwadhibu Mimi mwenyewe; badala yake, bali Naruhusu wana Wangu wazaliwa wa kwanza wa kiume kutekeleza haki Yangu na uadhama. Kwa sababu Shetani alikuwa anawanyanyasa wana Wangu, kuwatesa wana Wangu na kuwaonea wana Wangu, leo, baada ya huduma yake kuisha, Nitawaruhusu wana Wangu wazaliwa wa kwanza waliokomaa washughulike nalo. Shetani amekuwa hana nguvu dhidi ya maangamizi. Kiharusi cha mataifa yote duniani ndio ushuhuda mzuri zaidi; watu kupigana na nchi zikiwa vitani ni onyesho la wazi kabisa la kuanguka kwa ufalme wa Shetani. Sababu iliyofanya Sikuonyesha ishara na maajabu yoyote hapo zamani ilikuwa ili kumletea Shetani fedheha na kulitukuza jina Langu hatua kwa hatua. Wakati shetani ameangamizwa kabisa Naanza kuonyesha nguvu Zangu: kile Ninachosema kinatokea, na vitu vya kuvuka mipaka ambavyo havina usawa na fikira za kibinadamu vitatimia (hivi vinarejelea baraka zinazokuja karibuni). Kwa sababu Mimi ndimi Mungu Mwenyewe wa vitendo na Sina kanuni, na kwa sababu Nazungumza kulingana na mabadiliko katika mpango Wangu wa usimamizi, kwa hivyo kile Nilichosema zamani si lazima kiwe cha kutumika sasa. Msishikilie mawazo yenu wenyewe! Mimi siye Mungu anayezingatia amri; Kwangu, kila kitu ni huru, cha kuvuka mipaka, na kimeachiliwa kabisa. Labda kilichosemwa jana kimepitwa na wakati leo, au huenda kikawekwa kando leo (hata hivyo, amri Zangu za utawala, kwa sababu zimetangazwa rasmi hazitabadilika kamwe). Hizi ndizo hatua katika mpango Wangu wa usimamizi. Msishikilie kanuni. Kila siku kuna mwanga mpya na kuna ufunuo mpya, na huo ndio mpango Wangu. Kila siku mwanga wangu utafichuliwa kwako na sauti Yangu itaachiliwa kwa ulimwengu dunia. Je, unaelewa? Huu ni wajibu wako, jukumu ambalo Nimekuaminia. Ni lazima usilipuuze hata kidogo. Nitawatumia mpaka mwisho watu Ninaowaidhinisha, na hili halitabadilika kamwe. Kwa sababu Mimi ni mwenyezi Mungu, Najua ni mtu wa aina gani anayepaswa kufanya kitu kipi, na vile vile ni mtu wa aina gani anaweza kufanya kitu kipi. Huu ndio uweza Wangu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 88

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 237)

Kila sentensi Ninayotamka huwa na mamlaka na hukumu na hakuna mtu anayeweza kuzibadilisha. Mara tu maneno Yangu yanapotoka, mambo yatafanyika kwa mujibu wa maneno Yangu, na hii ndiyo tabia Yangu. Maneno Yangu ni mamlaka na yeyote anayeyarekebisha hukosea kuadibu Kwangu na ni lazima Nimwangamize. Hali ikiwa mbaya hayo husababisha uharibifu katika maisha yao wenyewe nao huenda kuzimu, au huenda jahanamu. Hii ndiyo njia ya pekee ambayo kwayo Ninawashughulikia wanadamu na mwanadamu hawezi kuibadilisha—hii ni amri Yangu ya utawala. Kumbuka hili! Hakuna mtu anayeruhusiwa kuikosea amri Yangu; lazima hili lifanyike kulingana na mapenzi Yangu! Zamani Nilikuwa mpole sana kwenu nanyi mlikabiliwa na maneno Yangu tu. Maneno Niliyonena kuhusu kuwaangamiza watu hayajatokea bado. Lakini kuanzia leo, majanga yote (haya yanayohusiana na amri Zangu za utawala) yatatokea moja baada ya lingine ili yawaadhibu wale wote wasiotii mapenzi Yangu. Lazima kuwe na ujio wa ukweli, vinginevyo watu hawataweza kuona ghadhabu Yangu lakini watapotoshwa tena na tena. Hii ni hatua ya mpango Wangu wa usimamizi nayo ni njia ambayo kwayo Mimi kushughulikia hatua inayofuata ya kazi Yangu. Nawaambieni hivi mapema ili muweze kuepuka kufanya makosa na kupitia mateso milele. Hiyo ni kusema, kuanzia leo Nitawafanya watu wote isipokuwa wana Wangu wazaliwa wa kwanza wachukue nafasi zao kwa mujibu wa mapenzi Yangu, na Nitawaadhibu mmoja baada ya mwingine. Sitamsamehe hata mmoja wao. Hebu thubutu tu kuwa wapotovu tena! Hebu thubutu tu kuwa mwasi tena! Nimesema mbeleni kuwa Mimi ni mwenye haki kwa wote bila hisia yoyote, na huu ni mfano kwamba tabia Yangu haipaswi kukosewa. Hii ni nafsi Yangu. Hakuna mtu anayeweza kubadilisha jambo hili. Watu wote husikia maneno Yangu na watu wote huuona uso Wangu mtukufu. Watu wote wanapaswa kunitii kabisa na kwa ukamilifu—hii ni amri Yangu ya utawala. Watu wote katika ulimwengu mzima na katika miisho ya dunia wanapaswa kunisifu na kunitukuza, kwa maana Mimi ni Mungu Mwenyewe wa pekee, kwa maana Mimi ni nafsi ya Mungu. Hakuna mtu anayeweza kubadili maneno na matamshi Yangu, usemi na mwenendo Wangu, kwa kuwa haya ni mambo Yangu peke Yangu, na kile ambacho Nimemiliki tangu milele na kile ambacho kitakuwepo milele.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 100

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 238)

Kazi Niliyopanga inaendelea kusonga mbele bila kukoma hata kwa muda kidogo. Baada ya kuingia katika Enzi ya Ufalme, na baada ya kukuingiza katika ufalme Wangu kama watu Wangu, Nitakuwa na madai mengine ya kuweka dhidi yenu; hiyo ni kusema, Nitaanza kutangaza rasmi mbele yenu katiba ambayo Nitatumia kuongoza enzi hii:

Kwa sababu mnaitwa watu Wangu, mnapaswa kuwa na uwezo wa kulitukuza jina Langu, yaani, kuwa na ushuhuda wakati wa majaribio. Mtu yeyote akijaribu kunirairai na kunificha ukweli, au kushiriki katika shughuli zisizo za heshima nyuma Yangu, bila ubaguzi Nitamfukuza nje, aondolewe kutoka katika nyumba Yangu akisubiri Mimi nimshughulikie. Wale ambao hawajakuwa waaminifu na wasio na upendo wa mtoto kwa mzazi Kwangu zamani, na leo hii wanainuka tena kunihukumu hadharani, wao pia watafukuzwa kutoka kwa nyumba Yangu. Wale ambao ni watu Wangu lazima wajali kuhusu mizigo Yangu kila mara na vile vile kutafuta kujua maneno Yangu. Ni watu kama hawa tu ndio Nitakaowapa nuru, na wao kwa hakika wataishi chini ya uongozi Wangu na nuru, na kamwe hawatakutana na kuadibu. Wale ambao, kwa kutojali mizigo Yangu, wanamakinika na kupanga mustakabali yao wenyewe, yaani, wale ambao hawalengi kwa matendo yao kukidhi Moyo Wangu bali wanataka kuomba omba vya bure, viumbe hawa walio kama waombaji, Ninakataa kata kata kuwatumia, kwa sababu tangu walipozaliwa hawajui chochote kuhusu maana ya kujali mizigo Yangu. Wao ni watu wasiokuwa na akili ya kawaida; watu kama hawa wanaugua kutokana na “utapiamlo” wa ubongo, na wanahitaji kwenda nyumbani wapate “lishe.” Siwahitaji watu wa aina hii. Miongoni mwa watu Wangu, kila mtu atatakiwa kuzingatia kunijua kama wajibu wa lazima unaotakiwa kutekelezwa mpaka mwisho, kama kula, kuvaa, na kulala, mambo ambayo mtu kamwe hawezi kusahau hata kwa muda mfupi, ili kwamba mwishowe kunijua litakuwa jambo la kawaida kama vile kula, jambo ambalo wewe hufanya bila jitihada yoyote, kwa mkono uliozoea. Kuhusu maneno Ninayoyanena, kila neno lazima lichukuliwe kwa uhakika mkubwa na lichukuliwe kikamilifu; hakuwezi kuwa na hatua nusu za uzembe. Yeyote asiyekuwa makini na maneno Yangu ataonekana kama ananipinga Mimi moja kwa moja; mtu yeyote asiyeyala maneno Yangu, au hatafuti kuyajua, ataonekana kama ambaye hanizingatii, na moja kwa moja atafagiliwa nje ya mlango wa nyumba Yangu. Kwa maana, kama Nilivyosema zamani, Ninachotaka sio watu wengi ila wateule wachache. Kati ya watu mia, kama mmoja tu anaweza kunijua kupitia maneno Yangu, basi bila kusita Ningewatupilia mbali wengine wote ili Nizingatie kumpa nuru na mwangaza mmoja huyu. Kutokana na hili unaweza kuona kuwa, si lazima iwe ukweli kwamba idadi kubwa pekee ndio inaweza kunidhihirisha, kuishi kulingana na Mimi. Ninachotaka ni ngano (hata ingawa viini vya mbegu huenda havijajaa) na sio magugu (hata wakati viini vya mbegu vimejaa vya kutosha kutamanika). Na kuhusu wale wasiojali kuhusu kutafuta lakini badala yake kuwa na tabia za kuzembea, wanapaswa kuondoka kwa hiari yao wenyewe; Mimi sitaki kuwaona tena, wasije wakaleta aibu kwa jina Langu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 5

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 239)

Kwa kuwa wewe ni mmoja wa watu wa nyumba Yangu, na kwa kuwa wewe ni mwaminifu katika ufalme Wangu, yote unayofanya lazima yafikie viwango ambavyo Ninahitaji. Sisemi kwamba uwe tu kama wingu linalofuata upepo, bali uwe kama theluji inayong’aa, na uwe na hali kama yake na hata zaidi uwe na thamani yake. Kwa sababu Nilitoka katika nchi takatifu, si kama yungiyungi, ambalo lina jina tu na halina dutu kwa sababu lilikuja kutoka katika matope na si kutoka nchi takatifu. Wakati ambapo mbingu mpya inashuka duniani na nchi mpya kuenea juu ya anga ndio pia wakati hasa ambao Ninafanya kazi kirasmi miongoni mwa binadamu. Ni nani kati ya wanadamu anayenijua Mimi? Ni nani aliyeona wakati wa kuwasili Kwangu? Ni nani ameona kwamba Mimi sina jina tu, bali zaidi ya jina Nina dutu? Mimi huyasongeza mawingu meupe kwa mkono wangu na kwa karibu Naichunguza anga; katika anga, hakuna kitu kisichopangwa kwa mkono wangu, na chini ya anga, hakuna mwanadamu asiyechangia juhudi yake ndogo kwa ukamilishaji wa shughuli Yangu kuu. Mimi Simwekei mwanadamu madai mazito duniani, kwa maana Mimi daima Nimekuwa Mungu wa vitendo, na kwa sababu Mimi ni Mwenyezi Aliyeumba mwanadamu na Anayemjua mwanadamu vizuri. Watu wote wako machoni pa Mwenyezi. Hata wale walio katika pembe zote mwisho wa dunia watawezaje kuepuka uchunguzi wa Roho Yangu? Ingawa mwanadamu “anajua” Roho Wangu, yeye pia huikosea Roho Wangu. Maneno Yangu yanaweka wazi uso mbaya wa wanadamu wote, na kuweka wazi mawazo ya ndani kabisa ya watu wote, na kusababisha wote duniani kufanywa wazi na mwanga Wangu na kuanguka chini ndani ya uchunguzi Wangu. Ijapokuwa mwanadamu anaanguka chini, moyo wake hauthubutu kwenda mbali Nami. Miongoni mwa viumbe, ni nani asiyekuja kunipenda kwa sababu ya matendo Yangu? Ni nani asiyekuwa na hamu kwa ajili ya kuyasikia maneno Yangu? Ni nani asiyezaliwa ndani mwake na hisia za ibada kwa sababu ya upendo Wangu? Ni kwa sababu tu ya ufisadi wa Shetani ndio maana mwanadamu anashindwa kuufikia ulimwengu kama Ninavyomhitaji kufika. Hata viwango vya chini kabisa ambavyo Mimi Namhitaji kufika huzalisha mashaka ndani yake, bila kutaja chochote cha leo, enzi ambayo Shetani anaendesha ghasia na ni mdhalimu mkuu, au wakati ambapo mwanadamu amekanyagwa sana na Shetani mpaka mwili wake mzima umejaa uchafu. Ni lini ambapo kutojali kwa mwanadamu kuhusu moyo Wangu kwa sababu ya upotovu wake hakujanisababishia Mimi huzuni? Je, inawezekana kwamba Mimi namwonea Shetani huruma? Je, inawezekana kwamba Mimi Nimekosea katika upendo wangu? Wakati mwanadamu ananikaidi, Moyo wangu unaomboleza kwa siri; wakati mwanadamu ananipinga, Ninamwadibu; wakati Ninamwokoa mwanadamu na kumfufua kutoka wafu, Mimi Huwalisha kwa uangalifu wanaponyenyekea mbele zangu, Moyo Wangu unatulia tuli na mara moja Ninahisi mabadiliko makubwa mbinguni na duniani na vitu vyote. Wanadamu wanaponisifu Mimi, itawezekanaje Nisiwe na furaha? Wakati mwanadamu ananishuhudia na kupatwa na Mimi, itawezekanaje Nisitukuzwe? Inawezekana kwamba kila anachofanya mwanadamu hakiongozwi na kutolewa na Mimi? Wakati ambapo Sitoi mwelekeo, wanadamu wanazembea na kuwa wanyamavu, na, nyuma Yangu, wao wanashiriki katika zile shughuli chafu “zenye kusifika.” Je, unafikiri kwamba mwili Ninaouvaa, haufahamu chochote kuhusu matendo yako, tabia zako, na maneno yako? Nimestahimili mvua na upepo kwa miaka mingi, na vile vile Nimepitia machungu ya ulimwengu wa binadamu, lakini ukitafakari kwa karibu, hakuna kiasi cha mateso kinachoweza kumfanya mwanadamu aliye katika nyama za mwili kupoteza matumaini ndani Yangu, kama vile hakuna utamu wowote unaoweza kumfanya mwanadamu wa mwili awe bila hisia, mwenye kuvunjika moyo au mwenye kunipuuza Mimi. Je, upendo wa mwanadamu Kwangu una mipaka kwa hali ya kutokuwa na maumivu au kutokuwa na utamu?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 9

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 240)

Leo, sababu Nimewaongoza hadi hapa, Nimefanya mipango ya kufaa, na Nina malengo Yangu Mwenyewe. Ningewaeleza kuyahusu leo, mngeweza kweli kuyajua? Nayajua vizuri mawazo ya akili ya mwanadamu na matakwa ya moyo wa mwanadamu: Nani hajawahi kutafuta njia ya kujitoa mwenyewe? Nani hajawahi fikiria matarajio yake mwenyewe? Lakini hata kama mwanadamu ana akili tajiri na ya asili nani aliweza kutabiri kwamba, kufuatia enzi, sasa kungekuwa kulivyo? Hili kweli ni tunda la juhudi zako binafsi? Haya ni malipo ya kazi yako ya bidii? Hii ndiyo picha nzuri iliyoonwa na akili yako? Nisingewaongoza wanadamu wote, nani angeweza kujitenga na mipango Yangu na kupata njia nyingine ya kutoka? Ni fikira akilini mwa mwanadamu na tamaa yake ambayo yamemleta hadi leo? Watu wengi wanaishi maisha yao yote bila kutimiziwa kwa matakwa yao. Kweli hili ni kwa sababu ya kosa katika fikira zao? Maisha ya watu wengi yamejawa na furaha na ridhaa isiyotarajiwa. Kweli ni kwa sababu wanatarajia kidogo sana? Je, nani kati ya wanadamu wote hatunzwi mbele ya macho ya Mwenyezi? Nani haishi maisha kati ya majaaliwa ya Mwenyezi? Je, maisha na kifo cha mwanadamu hutokea kwa chaguo lake mwenyewe? Je, mwanadamu anadhibiti hatima yake? Wanadamu wengi wanalilia kifo, lakini kiko mbali nao; watu wengi wanataka kuwa watu wenye nguvu maishani na wanahofia kifo, lakini bila kujua kwao, siku ya kufa kwao inasogea karibu, ikiwatumbukiza ndani ya dimbwi la kifo; watu wengi wanatazama angani na kutoa pumzi kwa undani; watu wengi wanalia sana, wakiomboleza; watu wengi wanaanguka kuwapo majaribu; na watu wengi wanakuwa wafungwa wa majaribu. Ingawa Sijitokezi binafsi kumruhusu mwanadamu kunitazama vizuri, watu wengi wanaogopa kuona uso Wangu, wanaogopa sana Nitawapiga chini, kwamba Nitawaangamiza. Mwanadamu kweli ananijua Mimi ama hanijui? Hakuna anayeweza kusema kwa hakika. Sivyo? Mnaniogopa na pia kuadibu Kwangu, lakini bado mnasimama na kunipinga wazi na kunihukumu hadharani. Sivyo? Kwamba mwanadamu hajawahi kunijua ni kwa sababu hajawahi kuuona uso Wangu ama kuisikia sauti Yangu. Hivyo, hata kama Niko ndani ya moyo wa mwanadamu, je, kuna wale ambao Sionekani mwenye ukungu na asiye dhahiri katika mioyo yao? Kuna wale Ninaoonekana vizuri ndani ya mioyo yao? Sitamani wale walio watu Wangu pia kutoniona vizuri, na hivyo Naanza kazi hii kubwa.

Nakuja kwa utulivu miongoni mwa wanadamu, na Ninaondoka polepole. Je, kuna aliyewahi kuniona? Je, jua linaweza kuniona kwa sababu ya miali yake inayowaka? Je, mwezi unaweza kuniona kwa sababu ya uangavu wake wa kung’aa? Je, nyota zinaweza kuniona kwa sababu ya mahali pao angani? Nikujapo, mwanadamu hajui, na mambo yote yanabakia gizani, na Niondokapo, bado mwanadamu hafahamu. Nani anaweza kuwa na ushuhuda Kwangu? Inaweza kuwa sifa ya watu wa dunia? Inaweza kuwa mayungiyungi yanayochanua porini? Inaweza kuwa ndege wanaoruka angani? Inaweza kuwa simba wanaonguruma milimani? Hakuna anayeweza kunishuhudia kikamilifu. Hakuna anayeweza kufanya kazi Nitakayoifanya! Hata kama wangefanya kazi hii, ingekuwa na athari gani? Kila siku Naona vitendo vyote vya watu wengi, na kila siku Nachunguza mioyo na akili za watu wengi; hakuna aliyewahi kutoroka hukumu Yangu, na hakuna aliyewahi kuachana na uhalisi wa hukumu Yangu. Nasimama juu ya mawingu na kuangalia kwa umbali: Nimewaangamiza watu wengi, lakini pia watu wengi wanaishi katika huruma, na wema Wangu. Nyinyi pia hamuishi chini ya hali kama hizi?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 11

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 241)

Duniani, Mimi ni Mungu wa vitendo Mwenyewe katika mioyo ya watu; mbinguni, Mimi Ndiye Mkuu wa viumbe vyote. Nimepanda milima na kuvuka mito, na Nimeingia na kutoka katikati ya binadamu. Nani anathubutu kwa uwazi kumpinga Mungu wa vitendo Mwenyewe? Nani anathubutu kutoka kati ya ukuu wa Mwenyezi? Nani anayethubutu kudai kuwa Mimi, bila shaka, Niko mbinguni? Tena, nani ambaye anathubutu kudai kuwa Mimi, bila kukosea, Niko duniani? Hakuna binadamu kati ya wote anayeweza kujieleza kwa ufasaha na undani mahali ambapo Mimi Naishi. Inawezekana kuwa kwamba, wakati Mimi niko mbinguni, Mimi ni Mungu Mwenyewe asiye wa kawaida? Inawezekana kuwa kwamba, wakati Mimi niko hapa duniani, Ninakuwa Mungu wa vitendo Mwenyewe? Kwamba Mimi ni Mtawala wa viumbe vyote, au kwamba Mimi ninapitia mateso ya ulimwengu wa mwanadamu—hakika hivi haviwezi kuamua iwapo Mimi ni Mungu wa vitendo Mwenyewe? Kama mwanadamu anadhani hivyo, si yeye ni mpumbavu asiye na matumaini ya kubadilika? Mimi niko mbinguni; Mimi pia Niko duniani; Mimi ni miongoni mwa maelfu ya vitu vya uumbaji, na pia miongoni mwa umati. Mwanadamu anaweza kunigusa kila siku; zaidi ya hayo, anaweza kuniona kila siku. Kulingana na binadamu, Mimi huonekana kuwa wakati mwingine Nimejificha na wakati mwingine Naonekana; Mimi kwa kweli nipo, lakini pia naonekana kutokuwepo. Ndani Mwangu kuna siri kubwa sana zisizoweza kufahamika na binadamu. Ni kana kwamba watu wote wananitazama kwa njia ya hadubini ili kugundua siri hata zaidi ndani Mwangu, wakiwa na matumaini ya kuondoa hisia za wasiwasi katika nyoyo zao. Lakini hata watumie darubini ya nguvu kivipi, binadamu watawezaje kuziweka wazi siri zilizo ndani Mwangu?

Wakati watu Wangu, kupitia kwa kazi Yangu, wanatukuzwa pamoja na Mimi, wakati huo maficho ya joka kubwa jekundu yatafichuliwa, matope yote na uchafu kufagiliwa mbali, na maji machafu, yaliyokusanyika kwa miaka mingi, kukaushwa na moto Wangu unaochoma, yasikuwepo tena. Hapo joka kubwa jekundu litaangamia katika ziwa la moto wa jehanamu. Je, kweli unayo nia ya kusalia chini ya ulinzi Wangu ili usinyakuliwe na joka? Je, kweli unachukia mbinu yake ya udanganyifu? Ni nani anayeweza kutoa ushahidi thabiti kwa ajili Yangu? Kwa ajili ya jina Langu, kwa ajili ya Roho Wangu, na kwa sababu ya mpango Wangu mzima wa usimamizi, ni nani anayeweza kutoa nguvu zake zote? Leo, wakati ambao ufalme upo katika ulimwengu wa wanadamu, ni wakati ambao Nimekuja binafsi miongoni mwa binadamu. Kama haingekuwa hivyo, je, kuna yeyote ambaye anaweza kujitokeza aende kwenye uwanja wa vita kwa niaba Yangu bila hofu yoyote? Ndipo ufalme uweze kuchukua mkondo, ili moyo Wangu uweze kuridhika, na tena, ili siku Yangu iweze kuja, ili wakati uweze kuja ambapo mambo mengi ya uumbaji yamezaliwa upya na kukua kwa wingi, ili kwamba mwanadamu aweze kuokolewa kutoka kwenye bahari ya mateso, ili siku inayofuata iweze kuja, na ili iwe ni ya ajabu, yenye kutoa maua na kushamiri, na tena, ili starehe ya siku za usoni itimizwe, binadamu wote wanajitahidi kwa nguvu zao zote, bila kuwacha chochote katika kujitoa sadaka wenyewe kwa ajili Yangu. Je, hii si ishara kwamba ushindi tayari ni Wangu, na alama ya kukamilika kwa mpango Wangu?

Wanadamu wanavyozidi kukaa katika siku za mwisho, ndivyo watakavyozidi kuhisi utupu wa dunia na ndivyo watakavyopungukiwa na ujasiri wa jinsi ya kuishi. Kwa sababu hii, watu wasiohesabika wamekufa katika hali ya kuvunja matumaini, wengine wengi wamevunjwa matumaini katika jitihada zao, na wengine wengi kuteseka wenyewe kuwa kunyanyaswa katika mikono ya shetani. Mimi Nimewaokoa watu wengi, Nimewapa wengi msaada, na mara nyingi, wakati binadamu wamepoteza mwanga, Mimi Nimewaongoza kurudi katika nafasi ya mwanga, ili wapate kunijua wakiwa kwenye mwanga, na kunifurahia katika furaha. Kwa sababu ya ujio wa mwanga Wangu, kuabudu hukuzwa katika mioyo ya watu wanaokaa katika ufalme Wangu, kwa maana Mimi ni Mungu wa kupendwa na binadamu, Mungu ambaye ubinadamu unajishika katika hali ya upendo, na mwanadamu anajazwa na maono ya kudumu ya umbo Langu. Hata hivyo, baada ya yote, hakuna mtu anayeelewa ikiwa hii ni kazi ya Roho au ni kazi ya mwili. Itawachukua watu maisha yote kupitia jambo hili moja. Wanadamu hawajawahi kunichukia ndani ya vina vya mioyo yao; badala yake, wananishikilia katika vina vya roho zao. Hekima yangu inaibua upendezewaji wake, maajabu Ninayotenda ni ukuu machoni pake, maneno Yangu yanastaajabisha akili yake, na bado yeye ana mapenzi tele kwayo. Uhalisi Wangu unawaacha wanadamu wasijue la kufanya, wakipigwa na butwaa na kukanganyikiwa, na bado wako tayari kuukubali. Je, hiki si kipimo cha mwanadamu jinsi alivyo hasa?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 15

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 242)

1. Mwanadamu hapaswi kujiinua, wala kujisifu. Anapaswa kumwabudu na kumsifu Mungu.

2. Unapaswa kufanya chochote ambacho kina manufaa kwa kazi ya Mungu, na hupaswi kufanya chochote ambacho kitaleta madhara kwa maslahi ya kazi ya Mungu. Unapaswa kulitetea jina la Mungu, ushuhuda Wake, na kazi ya Mungu.

3. Pesa, vitu vya dunia, na mali zote ambazo zipo katika nyumba ya Mungu ni sadaka ambazo zinapaswa kutolewa na mwanadamu. Sadaka hizi hazipaswi kufurahiwa na binadamu yeyote ila kuhani na Mungu Mwenyewe, kwani sadaka zinazotolewa na binadamu ni za kufurahiwa na Mungu, Mungu anashiriki tu sadaka hizi na kuhani, na hakuna mwingine yeyote aliyehitimu wala kuwa na haki ya kufurahia sehemu yoyote ya sadaka hizi. Sadaka zote zinazotolewa na mwanadamu (ikiwemo pesa, vifaa na vitu vinavyoweza kufurahiwa) vyote vinatolewa kwa Mungu, na sio kwa mwanadamu. Kwa hivyo, vitu hivi havipaswi kufurahiwa na mwanadamu; kama mwanadamu angekuwa anavifurahia vitu hivi, basi angekuwa anaiba sadaka. Yeyote yule atakayefanya hili ni msaliti kama Yuda, kwa kuwa, sio tu kwamba Yuda alikuwa msaliti, bali pia Yuda alijitwalia vilivyokuwa katika mfuko wa pesa ili kutumia.

4. Mwanadamu ana tabia potovu na, zaidi ya hayo, amejawa na hisia. Kwa hivyo, ni marufuku kabisa kwa watu wa jinsia mbili tofauti kufanya pamoja kazi wakati wa kumtumikia Mungu bila kuwepo na mtu mwingine. Yeyote yule atakayepatikana na kosa hili atafukuzwa, bila ubaguzi—na hakuna atakayeepuka hili.

5. Hupaswi kumhukumu Mungu, au kujadili kiholela mambo yanayomuhusu Mungu. Unapaswa kutenda vile mwanadamu anavyopaswa kutenda, na kuzungumza jinsi mwanadamu anavyopaswa kuzungumza, na hupaswi kuvuka upeo wako wala kuvuka mipaka yako. Uchunge ulimi wako na uwe mwangalifu kwa hatua zako. Yote haya yatakuzuia kufanya jambo lolote linaloweza kuikosea tabia ya Mungu.

6. Unapaswa kufanya yale yanayopaswa kufanywa na mwanadamu, na utekeleze wajibu wako, na utimize majukumu yako, na ushikilie wajibu wako. Kwa sababu unaamini katika Mungu, unapaswa kutoa mchango wako kwa kazi ya Mungu; kama huwezi, basi wewe hufai kula na kunywa maneno ya Mungu, na hufai kuishi katika nyumba ya Mungu.

7. Katika kazi na mambo yanayohusiana na kanisa, mbali na kumtii Mungu, katika kila kitu unapaswa kufuata maagizo ya mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Hata ukiukaji mdogo tu haukubaliki. Lazima uwe mkamilifu katika kutii kwako, na hupaswi kuchunguza kati ya mazuri na mabaya; yaliyo mazuri au mabaya hayakuhusu. Unapaswa kujishughulisha tu na utiifu kamili.

8. Watu wanaoamini katika Mungu wanapaswa kumtii na kumwabudu. Hupaswi kumsifu au kumwabudu mtu yeyote; hupaswi kumpa Mungu nafasi ya kwanza, binadamu unayemheshimu nafasi ya pili, kisha wewe mwenyewe nafasi ya tatu. Mtu yeyote asishikilie nafasi yoyote moyoni mwako, na hupaswi kuwachukulia watu—hasa wale unaowaheshimu—kuwa katika kiwango sawa na Mungu, kuwa sawa na Yeye. Mungu hawezi kustahimili hili.

9. Mawazo yako yanapaswa kuwa juu ya kazi ya kanisa. Unapaswa kuweka kando matarajio ya mwili wako, uwe na msimamo thabiti kuhusu mambo ya kifamilia, na ujitoe kwa moyo wako wote kwa kazi ya Mungu, na uiweke kazi ya Mungu kwanza kisha maisha yako katika nafasi ya pili. Huu ndio mwenendo mwema wa mtu mtakatifu.

10. Jamaa zako (watoto, mke au mume, dada zako au wazazi wako na kadhalika) wasio wa imani yako hawapaswi kulazimishwa kuja kanisani. Nyumba ya Mungu haina ukosefu wa washirika, na hakuna haja ya kuijaza na watu wasiokuwa na maana katika nyumba Yake. Wale wote wasioamini kwa moyo mchangamfu, hawapaswi kuongozwa kuingia kanisani. Amri hii inaelekezwa kwa watu wote. Kuhusu jambo hili mnapaswa kuchunguza, kufuatilia na kukumbushana, na hakuna anayepaswa kukiuka amri hii. Hata wakati jamaa zako wasio wa imani yako wanapoingia kanisani kwa i shingo upande, hawapaswi kupatiwa jina jipya wala kupewa vitabu vya kanisa; watu kama hao si wa nyumba ya Mungu, na kuingia kwao kanisani kunapaswa kukomeshwa kwa njia yoyote ile inayofaa. Ikiwa matatizo yataletwa kanisani kwa sababu ya uvamizi wa mapepo, basi wewe mwenyewe utafukuzwa au kuwekewa vikwazo. Kwa ufupi, kila mmoja ana jukumu katika suala hili, ingawa pia hupaswi kuwa mzembe, wala kutumia jambo hili ili kulipiza kisasi chako binafsi.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Amri Kumi za Utawala Ambazo Lazima Wateule wa Mungu katika Enzi ya Ufalme Wazitii

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 243)

Watu lazima wafuate majukumu mengi wanayostahili kuyatekeleza. Hili ndilo watu wanalopaswa kufuata, na wanalostahili kufanya. Mruhusu Roho Mtakatifu afanye linalostahili kufanywa na Roho Mtakatifu; mwanadamu hawezi kulichangia lolote. Mwanadamu sharti ashike yale ambayo lazima yatendwe na mwanadamu, ambayo hayana uhusiano na Roho Mtakatifu. Si lolote bali lile ambalo lazima litendwe na mwanadamu, na lazima lifuatwe kama amri, kama ufuasi wa sheria za Agano la Kale. Ingawa sasa si Enzi ya Sheria, bado kuna maneno mengi yanayolingana na Enzi ya Sheria ambayo yanahitaji kufuatwa, na hayatendwi tu kwa kutegemea kuguswa na Roho Mtakatifu, lakini ni yale yanayostahili kufuatwa na wanadamu. Kwa mfano:

Hupaswi kuihukumu kazi ya Mungu wa vitendo.

Hupaswi kumpinga mtu anayeshuhudiwa na Mungu.

Mbele za Mungu, utahifadhi nafasi yako, na hutakuwa mwovu.

Unapaswa kuwa na kiasi katika usemi, na maneno na matendo yako lazima yafuate mipangilio ya mwanadamu aliyeshuhudiwa na Mungu.

Unapaswa kuheshimu ushuhuda wa Mungu. Usipuuze kazi ya Mungu wala maneno kutoka kinywa chake.

Usiige sauti na malengo ya matamshi ya Mungu.

Kwa nje, usifanye lolote linalodhihirisha kumpinga mtu anayeshuhudiwa na Mungu.

Haya ndiyo yanayopaswa kufuatwa na kila mmoja. Katika kila enzi, Mungu hutaja amri nyingi zinazoambatana na amri na zinazopaswa kufuatwa na mwanadamu. Kupitia hili, anazuia tabia ya mwanadamu, na kugundua uaminifu wake. Chukua maneno “Heshimu baba yako na mama yako” ya enzi ya Agano la Kale, kwa mfano. Maneno haya hayatumiki leo; wakati huo, yalizuia tu baadhi ya tabia ya nje ya mwanadamu, yalitumika kuonyesha uaminifu wa imani ya mwanadamu kwa Mungu, na yalikuwa alama ya wale waliomwamini Mungu. Ingawa sasa ni Enzi ya Ufalme, bado kuna amri nyingi ambazo mwanadamu lazima azifuate. Amri za kale hazitumiki; leo, kuna mazoea mengi, mwafaka kwa mwanadamu kutekeleza, na ambayo ni muhimu. Hayahusishi na kazi ya Roho Mtakatifu na lazima yatendwe na mwanadamu.

Katika Enzi ya Neema, mazoea mengi ya Enzi ya Sheria yaliondolewa kwa sababu sheria hizi hazikufaa hasa ya kazi ya wakati huo. Baada ya kuondolewa, mazoea mengi yaliwekwa ambayo yalifaa enzi hiyo, na ambayo yamekuwa sheria nyingi za sasa. Mungu wa leo alipokuja, kanuni hizi zilitupiliwa mbali, na hazikuhitajika kufuatwa tena, na mazoea mengi ambayo yalifaa kazi ya wakati huu yakawekwa. Leo, mazoea haya sio sheria, lakini ili kufikia athari; zinafaa kwa leo—na kesho, pengine, zitakuwa kanuni. Kwa ujumla, unafaa kuzingatia yale ambayo yatafanikisha kwa kazi ya leo. Usizingatie kesho: Yanayofanywa leo ni kwa ajili ya leo. Pengine kesho kutakuwa na mazoea mazuri ambayo utahitajika kutekeleza—lakini usizingatie hayo sana, yafuate yanayofaa kufuatwa leo ili uepuke kumpinga Mungu. Leo, hakuna lolote muhimu analopaswa kufuata mwanadamu zaidi ya yafuatayo:

Usijaribu kumbembeleza Mungu anayesimama mbele ya macho yako, au kumficha jambo lolote.

Usizungumze uchafu ama matamshi ya kiburi mbele ya Mungu aliye mbele yako.

Usimdanganye Mungu mbele ya macho yako kwa maneno mazuri wala kwa maneno ya kuridhisha ili uweze kujipatia uaminifu Wake.

Usitende bila heshima mbele za Mungu. Tii yote yatokayo kinywani mwa Mungu, wala usikatae, usipinge, ama kusaili maneno Yake.

Usitafsiri unavyoona kuwa sawa, maneno yanayonenwa kutoka kinywani mwa Mungu. Chunga ulimi wako ili usikutie katika mtego wa hila danganyifu za yule mwovu.

Unapaswa kulinda nyayo zako ili kuepuka kupita mipaka uliyowekewa na Mungu. Kufanya hivyo kutakusababisha uzungumze maneno ya majivuno na yenye fahari kuu kutoka kwa mtazamo wa Mungu, na hivyo kufanya uchukiwe na Mungu.

Usieneze maneno kutoka kinywa cha Mungu ovyo ovyo, usije ukadhihakiwa na wengine na kufanywa kuwa mjinga na mapepo.

Tii kazi yote ya Mungu wa leo. Hata ikiwa hauifahamu, usiihukumu; unachoweza kufanya ni kutafuta na kushiriki.

Hakuna mtu atapatendea dhambi mahali pa Mungu pa asili. Huwezi kufanya lolote zaidi ya kumtumikia Mungu wa leo kutoka katika nafasi ya mwanadamu. Huwezi kumfundisha Mungu wa leo kutoka kwa nafasi ya mwanadamu—kufanya hivyo ni kupotoka.

Hakuna anayeweza kusimama kwa niaba ya mtu aliyeshuhudiwa na Mungu; katika maneno yako, matendo, na mawazo yako ya ndani, unasimama katika nafasi ya mwanadamu. Hili ni la kufuatwa, ni wajibu wa mwanadamu, hakuna anayeweza kulibadilisha, na kufanya hivyo ni ukiukaji wa amri za utawala. Inapaswa kukumbukwa na kila mtu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Amri za Enzi Mpya

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 244)

Kuna mambo mengi ambayo Ninatumai kuwa mtaweza kuyafikia. Hata hivyo, matendo yenu na maisha yenu yote hayawezi kuridhisha matakwa Yangu kikamilifu, kwa hiyo ni lazima Niseme kile hasa Ninachotaka kusema na kuwafafanulia mapenzi Yangu. Kwa kuwa utambuzi wenu ni mdogo na ufahamu wenu pia ni mdogo, mpo karibu kabisa kukosa kuijua tabia Yangu na kiini Changu pia, na hivyo ni suala la dharura kwamba Niwafahamishe kuyahusu. Haijalishi hapo awali ulielewa kwa kiwango kipi, au kama uko tayari kujaribu kuelewa masuala haya, bado ni lazima Niyaelezee kwenu kwa undani. Masuala haya si mageni kabisa kwenu, lakini bado mnakosa uelewa mwingi, ufahamu mwingi, kwa maana iliyoko ndani yao. Wengi wenu mna ufahamu mdogo tu, na wa sehemu na ambao haujakamilika kwa hilo. Ili kuwasaidia kutenda ukweli kwa njia bora zaidi, yaani, kuweka maneno Yangu katika matendo kwa njia bora zaidi, Nafikiri kwamba ni masuala haya ambayo ni lazima kwanza myajue. Vinginevyo, imani yenu itabakia kuwa isiyo na uhakika, ya kinafiki, na iliyojawa na mambo ya kidini. Kama huielewi tabia ya Mungu, basi hautaweza kufanya kazi unayopaswa kufanya kwa ajili Yake. Kama hujui dutu ya Mungu, basi hautaweza kumwonyesha heshima na uchaji, lakini badala yake kutakuwa tu na uzembe wa kutokujali, na kuepuka kusema ukweli wote, na hata zaidi, kufuru isiyoweza kurekebishwa. Ingawa kuielewa tabia ya Mungu kwa kweli ni muhimu sana, na maarifa ya dutu ya Mungu hayawezi kupuuzwa, hakuna yeyote ambaye amewahi kuchunguza kwa umakini au kudadisi masuala haya. Ni wazi kuona kwamba nyote mmetupilia mbali amri za utawala Nilizotoa. Kama huielewi tabia ya Mungu, basi kuna uwezekano mkubwa zaidi kwa wewe kuikosea tabia Yake. Kuikosea tabia Yake ni sawa na kuchochea hasira ya Mungu Mwenyewe, ambapo matunda ya mwisho ya matendo yako yatakuwa ni ukiukaji wa amri za utawala. Sasa unapaswa kutambua kwamba unapoelewa kiini cha Mungu, vivyo hivyo utaweza kuielewa tabia Yake—na unapoielewa tabia Yake, vivyo hivyo utakuwa umeelewa amri za utawala. Bila shaka, mengi ya yale yaliyoko katika amri za utawala yanahusisha tabia ya Mungu, lakini tabia Yake yote haijaonyeshwa ndani ya amri za utawala; kwa hivyo, ni lazima mpige hatua zaidi katika kuongeza ufahamu wenu wa tabia ya Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 245)

Tabia ya Mungu ni mada ambayo inaonekana kuwa ya dhahania sana kwa kila mtu na aidha ambayo haikubaliwi kwa urahisi, kwani tabia Yake ni tofauti na hulka ya binadamu. Mungu, pia, ana hisia za raha, hasira, huzuni, na furaha, lakini hisia hizo zinatofautiana na zile za binadamu. Mungu Mwenyewe ana milki na nafsi Yake. Kila kitu Anachokidhihirisha na kukifichua ni viwakilishi vya dutu Yake na utambulisho Wake. Kila Alicho na anacho, pamoja na dutu na utambulisho Wake vyote ni vitu ambavyo haviwezi kubadilishwa na binadamu yeyote. Tabia Yake inajumuisha upendo Wake kwa binadamu, faraja kwa binadamu, chuki kwa binadamu, na hata zaidi, uelewa wa kina wa binadamu. Hulka ya binadamu, hata hivyo, inaweza kuwa yenye matumaini chanya, changamfu, au isiyo na hisia. Tabia ya Mungu ni ile ambayo inamilikiwa na Mtawala wa vitu vyote na viumbe vyote vyenye uhai, na Bwana wa viumbe vyote. Tabia Yake inawakilisha heshima, nguvu, uadilifu, ukuu, na zaidi ya yote, mamlaka ya juu kabisa. Tabia Yake ni ishara ya mamlaka, ishara ya kila kitu kilicho cha haki, cha kuvutia, ishara ya kila kitu kilicho chema na kizuri. Zaidi ya hayo, tabia Yake ni ishara ya Yeye kutoweza kushindwa au kushambuliwa na giza au na nguvu yoyote ya adui, pamoja na ishara ya Yeye kutoweza kukosewa (wala Hatavumilia kukosewa) na kiumbe chochote kilichoumbwa. Tabia Yake ni ishara ya nguvu za kiwango cha juu zaidi. Hakuna mtu au watu wenye uwezo au wanaoweza kutatiza kazi Yake au tabia Yake. Lakini sifa bainifu za mwanadamu ishara tu ya mamlaka madogo ya mwanadamu juu ya mnyama. Mwanadamu ndani yake na kwake hana mamlaka, hana uhuru, na hana uwezo wa kuenda zaidi ya nafsi, lakini katika kiini chake ni mtu ambaye anajinyenyekeza chini ya kila aina ya watu, matukio, na vitu. Furaha ya Mungu inatokana na kuwepo na kuzuka kwa haki na nuru; kwa sababu ya uharibifu wa giza na uovu. Anafurahi kwa sababu Ameleta nuru na maisha mazuri kwa wanadamu; Furaha Yake ni furaha ya haki, ishara ya kuwepo kwa yote ambayo ni chanya na, hata zaidi, ishara ya fanaka. Ghadhabu ya Mungu ni n kwa sababu ya madhara ambayo kuwepo na kuingiliwa kwa dhulma kunaleta juu ya binadamu Wake, kwa sababu ya kuwepo kwa uovu na giza, kwa sababu ya kuwepo kwa vitu vinavyofukuza ukweli, na hata zaidi kwa sababu ya kuwepo kwa vitu vinavyopinga vitu vilivyo vyema na vizuri. Hasira Yake ni ishara ya kwamba vitu vyote hasi havitakuwepo tena, na hata zaidi ya hayo, ni ishara ya utakatifu Wake. Huzuni Yake ni kwa sababu ya wanadamu, ambao Amekuwa na matumaini nao lakini ambao wameanguka katika giza, ni kwa sababu kazi Afanyayo kwa mwanadamu haifikii matarajio Yake, na kwa sababu binadamu Awapendao hawawezi wote kuishi katika mwanga. Anahisi huzuni kwa sababu ya wanadamu wasio na hatia, kwa sababu ya yule ambaye ni mwaminifu lakini ni mjinga, na kwa sababu yule mwanadamu mzuri lakini ana upungufu katika maoni yake mwenyewe. Huzuni Yake ni ishara ya wema Wake na huruma Yake, ishara ya uzuri na ukarimu. Furaha yake, bila shaka, inatokana na kuwashinda maadui Zake na kupata imani nzuri ya mwanadamu. Zaidi ya hayo, inatokana na kuondolewa na kuangamizwa kwa nguvu zote za adui na kwa sababu wanadamu wamepokea maisha mazuri na yenye amani. Furaha ya Mungu ni tofauti na raha ya binadamu; badala yake, ni ile hisia ya kupokea matunda mazuri, hisia ambayo ni kubwa zaidi kuliko raha. Furaha Yake ni ishara ya wanadamu kuwa huru dhidi ya mateso kuanzia wakati huu na kuendelea, na ni ishara ya wanadamu kuingia katika ulimwengu wenye mwanga. Hisia za mwanadamu, kwa upande mwingine, zote huibuka kwa ajili ya masilahi yake mwenyewe, na wala si kwa ajili ya haki, mwangaza, au kile ambacho ni cha kupendeza, sembuse neema inayotolewa na Mbingu. Hisia za wanadamu zina ubinafsi na zinamilikiwa na ulimwengu wa giza. Hisia hizo hazipo kwa ajili ya mapenzi, sembuse mpango wa Mungu, na kwa hiyo mwanadamu na Mungu hawawezi kamwe kuzungumziwa kwa njia sawa. Mungu ni mkuu milele na Anaheshimiwa milele, ilhali mwanadamu siku zote ni wa chini, siku zote hana thamani. Hii ni kwa sababu daima Mungu anajitoa na kugharimika kwa ajili ya wanadamu, ilhali mwanadamu daima anatafuta na kujitahidi kwa ajili yake mwenyewe. Mungu daima anajitaabisha kwa ajili ya kuwepo kwa wanadamu, ilhali mwanadamu hachangii chochote kamwe kwa ajili ya haki au nuru, na hata kama mwanadamu atafanya jitihada ya muda, yeye ni dhaifu sana hawezi kustahimili dhoruba hata kidogo, kwani jitihada za mwanadamu siku zote ni kwa ajili yake mwenyewe na wala si kwa ajili ya wengine. Mwanadamu siku zote ni mbinafsi, wakati Mungu hana ubinafsi milele. Mungu ndiye chanzo cha vyote vilivyo vya haki, vyema, na vizuri, huku naye mwanadamu ni yule anayerithi na kudhihirisha vyote vyenye sura mbaya na vyenye maovu. Mungu hatawahi kubadilisha dutu Yake ya haki na uzuri, ilhali mwanadamu anaweza kabisa, wakati wowote, kuisaliti haki na kujiweka mbali na Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 246)

Kila sentensi Niliyoizungumza ina tabia ya Mungu ndani yake. Mtafanya vizuri endapo mtatafakari kuhusu maneno Yangu kwa umakini, na kwa kweli mtafaidi pakubwa kutoka kwa maneno hayo. Dutu ya Mungu ni ngumu sana kuielewa, lakini Ninaamini kwamba angalau nyinyi nyote mna mawazo fulani kuhusu tabia ya Mungu. Ninatumai, basi, kwamba mtanionyesha Mimi na kufanya mengi zaidi ya yale ambayo hayakosei tabia ya Mungu. Kisha Nitatulizwa moyo. Kwa mfano, mweke Mungu moyoni mwako kila wakati. Unapochukua hatua, fanya hivyo kulingana na maneno Yake. Tafuta nia Zake katika kila kitu, na usifanye kile ambacho kitavunjia heshima na kumdhalilisha Mungu. Hata zaidi usimweke Mungu nyuma ya akili yako ili ujaze utupu wa siku zijazo katika moyo wako. Ukifanya hivyo, basi utakuwa umeikosea tabia ya Mungu. Tena, ikitokea kwamba hutawahi kutamka matamshi ya kukufuru au kulalamika dhidi ya Mungu maisha yako yote, na tena ikitokea kwamba unaweza kufanya kikamilifu kila kitu ambacho Amekuaminia wewe na pia kutii maneno Yake yote katika maisha yako yote, basi utakuwa umeweza kuepuka kuasi dhidi ya amri za utawala. Kwa mfano, kama umewahi kusema “Kwa nini sifikirii kwamba Yeye ni Mungu?” “Nafikiri kwamba maneno haya ni nuru kiasi tu ya Roho Mtakatifu,” “Katika maoni yangu, si kila kitu ambacho Mungu anakifanya lazima ni sahihi,” “Ubinadamu wa Mungu hauna ukuu zaidi kuliko wangu,” “Maneno ya Mungu hayaaminiki kabisa,” au matamshi mengine kama hayo ya kuhukumu, basi Nakusihi wewe ukiri na kutubu dhambi zako mara nyingi zaidi. Vinginevyo, hutawahi kuwa na fursa ya msamaha, kwani humkosei mwanadamu, ila Mungu Mwenyewe. Unaweza kuamini kwamba wewe unamhukumu mtu tu, lakini Roho wa Mungu haichukulii hivyo. Wewe kutoheshimu mwili Wake ni sawa na kumvunjia Yeye heshima. Kama hali ni hivi, basi si ni kweli kwamba umeikosea tabia ya Mungu? Lazima ukumbuke kwamba kila kitu kinachofanywa na Roho wa Mungu kinafanywa ili kulinda kazi Yake katika mwili na ili kazi hii ifanywe vizuri. Ukiyapuuza haya, basi Nasema kwamba wewe ni mtu ambaye kamwe hataweza kufaulu katika kumwamini Mungu. Kwani umechochea hasira ya Mungu, kwa hivyo Atatumia adhabu inayofaa ili kukufunza adabu.

Kupata kujua dutu ya Mungu si jambo dogo. Lazima uelewe tabia Yake. Katika njia hii, polepole na bila kujua, utaanza kujua dutu ya Mungu. Wakati umeingia katika maarifa haya, utajikuta unasonga mbele kwenye hali ya juu na nzuri zaidi. Mwishowe, utakuja kujisikia aibu kwa nafsi yako ya kuchukiza, kiasi kwamba unahisi hakuna mahali pa kujificha. Wakati huo, kutakuwa na machache zaidi na zaidi katika mwenendo wako ya kukosea tabia ya Mungu, moyo wako utakuwa karibu zaidi na zaidi na ule wa Mungu, na polepole upendo wako Kwake utaongezeka ndani ya moyo wako. Hii ni ishara ya wanadamu kuingia katika hali nzuri. Lakini kufikia sasa bado hamjapata hili. Mnaposhughulika huku na kule kwa ajili ya majaaliwa yenu, ni nani anayependa kujaribu kujua dutu ya Mungu? Kama hali hii itaendelea, mtakiuka amri za utawala bila kujua, kwani mnafahamu kidogo sana kuhusu tabia ya Mungu. Kwa hivyo, je, si kile ambacho mnafanya sasa kinaweka msingi wa makosa yenu dhidi ya tabia ya Mungu? Kwamba Ninawaambia muielewe tabia ya Mungu haipingani na kazi Yangu. Kwani mkikosea amri za utawala mara nyingi, basi ni nani kati yenu anayeweza kutoroka adhabu? Je, basi kazi Yangu haingekuwa bure kabisa? Kwa hivyo, Ningali Nawaambia kwamba, pamoja na kuchunguza mienendo yenu binafsi, muwe waangalifu zaidi na hatua mnazochukua. Haya ndiyo yatakuwa mahitaji ya juu zaidi Ninayotoa kwenu, na Ninatumai kwamba nyote mtayafikiria kwa umakini na kuyaona kuwa muhimu kabisa. Endapo siku itafika ambapo matendo yenu yatanichochea Mimi hadi kuwa katika hali iliyojaa hasira, basi matokeo yatakuwa ya kwenu peke yenu kuyafikiria, na hakutakuwa na mwingine yeyote atakayechukua adhabu hiyo kwa niaba yenu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 247)

Watu husema Mungu ni Mungu wa haki, na kwamba mradi tu mwanadamu atamfuata mpaka mwisho, basi Hatakuwa na upendeleo kwa mwanadamu, kwani Yeye ni mwenye haki. Je, mwanadamu akimfuata mpaka mwisho kabisa, Mungu anaweza kumtupa mwanadamu nje? Sina upendeleo kwa mwanadamu yeyote, na Huwahukumu wanadamu wote kwa tabia Yangu ya haki, ilhali kuna mahitaji yanayofaa Ninayohitaji kutoka kwa mwanadamu, na Ninahitaji yakamilishwe na wanadamu wote, bila kujali ni nani. Sijali jinsi sifa zako zilivyo nyingi au za kuheshimiwa; najali tu kama utatembea kwa njia Yangu, na kama unapenda na una kiu ya ukweli. Kama huna ukweli, na unaleta aibu katika jina Langu, na matendo yako ni kinyume cha njia Yangu, kufuata tu bila kujali, basi wakati huo nitakupiga na kukuadhibu kwa uovu wako, na utakuwa na nini la kusema? Utaweza kusema Mungu si mwenye haki? Leo kama umezingatia maneno ambayo nimenena, basi wewe ni mtu ambaye Namkubali. Unasema umeteseka kila wakati ukimfuata Mungu, kwamba umemfuata Yeye katika hali ngumu na mbaya, na umeshiriki Naye nyakati nzuri na mbaya, lakini hujaishi kulingana na maneno yaliyosemwa na Mungu; unataka tu kukimbia huku na kule kwa ajili ya Mungu na kujitumia kwa ajili ya Mungu kila siku, na hujafikiria kuishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana. Unasema pia, “Kwa vyovyote, naamini Mungu ni mwenye haki. Nimeteseka kwa ajili Yake, nikashughulika kwa ajili Yake, kujitoa kikamilifu Kwake, na nimefanya bidii ingawa sijapata kutambuliwa; Yeye hakika atanikumbuka.” Ni ukweli kwamba Mungu ni mwenye haki, na haki hii haijatiwa doa na uchafu wowote: Haina mapenzi ya binadamu, na haijatiwa doa na mwili, ama kitendo chochote cha binadamu. Wale wote ambao ni waasi na wako kwa upinzani, na hawazingatii njia Zake wataadhibiwa; hakuna atakayesamehewa, na hakuna atakayeepuka! Watu wengine husema, “Leo ninakimbia kwa ajili Yako; mwisho ukifika, utaweza kunipa baraka kidogo?” Sasa Nakuuliza, “Umezingatia maneno Yangu?” Haki unayoongelea inategemea matendo. Unafikiria kwamba Mimi ni mwenye haki, na asiye na mapendeleo kwa binadamu wote, na kwamba wale wanifuatao hadi mwisho wataokolewa na kupata baraka Yangu. Kuna maana ya ndani kwa maneno Yangu kwamba “wale wote wanifuatao hadi mwisho wataokolewa”: Wale wanifuatao mpaka mwisho ndio Nitakaowapata, ni wale, baada ya kushindwa Nami, watautafuta ukweli na kufanywa wakamilifu. Ni hali gani umepata? Umepata kunifuata hadi mwisho, lakini nini kingine? Je, umezingatia maneno Yangu? Umekamilisha moja kati ya tano ya mahitaji Yangu, ilhali huna mpango wa kumaliza manne yaliyobaki. Umepata ile njia rahisi, na ukaifuatilia ukiwa na mtazamo wa kutumaini kuwa utabahatika. Kwa mtu kama wewe, haki Yangu ni kuadibu na hukumu, ni adhabu ya haki, na ni adhabu ya haki kwa watenda maovu wote; wale wote wasiotembea kwa njia Yangu wataadhibiwa, hata kama watafuata mpaka mwisho. Hii ndio haki ya Mungu. Wakati tabia hii ya haki inapodhihirishwa katika adhabu ya mwanadamu, mwanadamu atakosa la kusema, na kujuta kwamba, alipokuwa akimfuata Mungu hakutembea katika njia Yake. “Wakati huo niliteseka kidogo tu nikimfuata Mungu, lakini sikutembea katika njia ya Mungu. Kuna udhuru gani? Hakuna namna ila kuadibiwa!” Ila kwa akili yake anafikiria, “Nimefuata hadi mwisho, hata Ukiniadibu haitakuwa adabu kali, na baada ya kuadibu kwa kuchosha, bado Utanihitaji. Najua Wewe ni mwenye haki, na Hutanifanyia hivyo milele. Mimi si kama wale watakaofagiliwa nje; wale watakaofagiliwa watapokea adabu kuu, na adabu Yangu itakuwa kidogo.” Adabu ya Mungu ya tabia ya haki si unavyosema. Sio kwamba wale ambao wanatubu dhambi zao kila wakati wataadibiwa kwa huruma. Haki ni utakatifu, na ni tabia ambayo haivumilii makosa ya mwanadamu, na yale yote ambayo ni machafu na hayajabadilika ndiyo shabaha ya chukizo kwa Mungu. Haki ya Mungu si sheria, lakini amri ya utawala: Ni amri ya utawala katika ufalme, na hii amri ya utawala ni adhabu ya haki kwa yeyote asiye na ukweli na hajabadilika, na hakuna kiwango cha wokovu. Mwanadamu akiwekwa kulingana na aina, wazuri watazawadiwa na wabaya kuadhibiwa. Ndio wakati hatima ya mwanadamu itawekwa wazi, na ndio ni wakati ambao kazi ya wokovu itafika mwisho, baada ya hapo, kazi ya kuokoa binadamu haitafanyika tena, na adabu italetwa kwa wale waliotenda maovu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matukio Aliyopitia Petro: Ufahamu Wake wa Adabu na Hukumu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 248)

Mimi ni moto uteketezao na Sivumilii kosa. Kwa sababu wanadamu wote waliumbwa na Mimi, chochote Nisemacho na kufanya, watu lazima watii na hawawezi kukiasi. Watu hawana haki ya kuingilia kazi Yangu, na wao hasa siyo wenye sifa zinazostahili kuchambua kilicho cha kweli au chenye makosa katika kazi Yangu na maneno Yangu. Mimi ni Bwana wa uumbaji, na viumbe wanapaswa kutimiza kila kitu Ninachohitaji kwa moyo wa kunicha Mimi; hawapaswi kutoa sababu ili kunishawishi Mimi na wao hasa hawapaswi kunipinga. Ninatumia mamlaka Yangu kuwatawala watu Wangu, na wale wote ambao ni sehemu ya uumbaji Wangu wanapaswa kuyatii mamlaka Yangu. Ingawa leo ninyi ni, jasiri na wenye kiburi mbele Yangu, ninyi hukaidi maneno ambayo Nawafunzia, na hamwogopi, Mimi hukumbana tu na uasi wenu na uvumilivu. Singekasirika na kuathiri kazi Yangu kwa sababu mabuu wadogo sana walipindua uchafu katika rundo la samadi. Mimi huvumilia kuendelea kuwepo kwa kila kitu ambacho Mimi huchukia kabisa na mambo ambayo Mimi huchukia kabisa kwa ajili ya mapenzi ya Baba Yangu, mpaka matamshi Yangu yawe kamili, mpaka dakika Yangu ya mwisho kabisa. Usijali! Siwezi kuzama katika kiwango sawa na buu asiyefaa kutajwa, na Sitafananisha kiwango cha ujuzi na wewe. Nakuchukia kabisa, ilhali Naweza kuvumilia. Wewe hunikaidi Mimi, ilhali huwezi kuepuka siku ya Mimi kukuadibu ambayo Baba Yangu ameniahidi Mimi. Je, buu aliyeumbwa anaweza kufananishwa na Bwana wa uumbaji wote? Katika majira ya kupukutika kwa majani, majani yaangukayo hurudi kwa mizizi yake, wewe hurudi kwa nyumba ya “baba” yako, na Mimi hurudi ubavuni pa Baba Yangu. Mimi huandamana na upendo mwema wa Baba Yangu, na wewe hufuatwa na kuvyogwa kwa baba Yako. Nina utukufu wa Baba Yangu, na wewe una aibu ya baba yako. Mimi hutumia kuadibu ambako Nimeshikilia kwa muda mrefu kuandamana na wewe, na wewe hukutana na kuadibu Kwangu na mwili wako uliooza ambao tayari umekuwa mpotovu kwa makumi ya maelfu ya miaka. Nimehitimisha kazi Yangu ya maneno ndani yako, ikiandamana na uvumilivu, na umeanza kutimiza wajibu wa kupitia msiba kutoka kwa maneno Yangu. Mimi hufurahia sana na kufanya kazi katika Israeli; wewe hulia na kusaga meno yako na huishi na kufa matopeni. Nimepata tena umbo Langu la asili na Sibaki tena ndani ya uchafu na wewe, huku umepata tena ubaya wako wa asili na bado unafukua kila mahali katika lundo la samadi. Wakati ambapo kazi na maneno Yangu yatakamilika, itakuwa siku ya furaha Kwangu. Wakati ambapo upinzani na uasi wako utakwisha, itakuwa siku ya kulia kwako machozi. Sitakuonea huruma, na hutaniona Mimi tena. Sitakuwa tena na mazungumzo na wewe, na hutakutana na Mimi tena. Nitachukia uasi wako, na utakosa kupendeza Kwangu. Nitakupiga wewe, na utanikosa Mimi. Nitaondoka kwako kwa furaha, na utafahamu deni lako Kwangu. Sitakuona wewe tena, lakini wewe kila mara utanitarajia Mimi. Nitakuchukia kwa sababu unanipinga Mimi sasa, na utanikosa Mimi; kwa sababu Nakuadibu sasa. Siko radhi kuishi ubavuni pako, lakini utalitamani sana kwa uchungu na kulia machozi katika milele, kwa sababu utajuta kila kitu ambacho umenifanyia Mimi. Utahisi majuto kwa ajili ya uasi na upinzani wako, hata utalala kifudifudi chini kwa majuto na kuanguka chini mbele Yangu na kuapa kutonitii tena. Katika moyo wako, hata hivyo, utanipenda Mimi tu, ilhali hutaweza kamwe kusikia sauti Yangu, Nitakufanya ujionee haya.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Majani Yaangukayo Yatakaporudi kwa Mizizi Yake, Utajuta Maovu Yote Ambayo Umefanya

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 249)

Huruma Yangu inaonyeshwa kwa wale wanaonipenda Mimi na kujinyima. Kwa sasa, adhabu itakayowapata waovu, ni thibitisho hasa la tabia Yangu ya haki na, hata zaidi, ushuhuda wa ghadhabu Yangu. Maafa yatakapokuj, njaa na tauni zitawapata wale wote wanaonipinga na watalia. Wale ambao wametenda aina zote za uovu, lakini ambao wamenifuata kwa miaka mingi, hawataepuka kulipia dhambi zao; wao pia, watatumbukia katika maafa, ambayo yameonekana kwa nadra kotekote katika mamilioni ya miaka, na wataishi katika hali ya taharuki na woga daima. Na wale kati ya wafuasi Wangu ambao wamekuwa waaminifu Kwangu watafurahi na kushangilia ukuu Wangu. Watakuwa na ridhaa isiyo na kifani na kuishi kwa raha ambayo Sijawahi kuwapa wanadamu. Kwa sababu Ninathamini matendo mema ya mwanadamu na kuchukia matendo yake maovu. Tangu Nilipoanza kuwaongoza wanadamu, Nimekuwa nikitamani kwa hamu kupata kundi la watu wenye nia moja na Mimi. Wale ambao hawana nia moja na Mimi, wakati huo huo, Siwasahau kamwe; Ninawachukia kabisa moyoni Mwangu daima, Nikisubiri nafasi ya kutoa adhabu kwao, jambo ambalo Nitafurahia kuona. Sasa siku Yangu imefika hatimaye, na Sihitaji kusubiri zaidi!

Kazi Yangu ya mwisho si kwa ajili ya kumwadhibu mwanadamu tu bali pia kwa ajili ya kupanga hatima ya mwanadamu. Aidha, ni kwa ajili ya kupokea shukrani kutoka kwa kila mtu kwa yale yote ambayo Nimefanya. Ninataka kila mtu aone kwamba yale yote ambayo Nimefanya ni sahihi na kwamba yote ambayo Nimefanya ni dhihirisho la tabia Yangu; si kwa uwezo wa mwanadamu, sembuse ulimwengu, ambao uliwaleta wanadamu. Kinyume na hili, mimi Ndiye Ninalisha kila kiumbe miongoni mwa vitu vyote. Bila uwepo Wangu, wanadamu wataangamia tu na kusumbuka kutokana na mashambulizi ya misiba. Hamna mwanadamu atakayeona uzuri wa jua na mwezi au dunia ya kijani kibichi; wanadamu watakumbana tu na usiku wenye baridi na bonde kali la uvuli wa mauti. Mimi tu Ndiye wokovu wa wanadamu. Mimi tu ndiye tumaini la wanadamu na zaidi ya hayo; Mimi tu Ndiye mwamba wa uwepo wa wanadamu wote. Bila Mimi, wanadamu watasimama kabisa mara moja. Bila mimi, wanadamu watakumbana na msiba mkuu na kukanyagwa na mapepo wa aina yote, hata kama hamna anayenisikiliza. Nimefanya kazi ambayo haiwezi kufanywa na yeyote yule ila mimi, tumaini Langu la pekee ni kwamba mwanadamu anaweza kunilipa kwa kutenda matendo kiasi mema. Ingawa wanaoweza kunilipa ni wachache, bado Nitahitimisha safari Yangu duniani na Nianze hatua ifuatayo ya kazi Yangu inayotokea, kwa sababu kukimbia kimbia Kwangu miongoni mwa wanadamu kwa miaka hii mingi imekuwa na matokeo mazuri, na Nimefurahishwa sana. Sijali kuhusu idadi ya watu ila kuhusu matendo yao mazuri. Kwa hali yoyote ile, Ninatumaini kwamba mtatayarisha matendo mema ya kutosha kwa ajili ya hatima yenu wenyewe. Huo ndio wakati Nitakaporidhika; la sivyo, hakuna yeyote miongoni mwenu atakayepuka maafa yatakayowafikia. Maafa haya hutoka Kwangu na bila shaka Mimi ndiye Niliyeyapanga. Ikiwa hamwezi kuonekana kuwa wema mbele Yangu, basi hamtaweza kuyaepuka maafa. Katikati ya dhiki, matendo yenu hayatafikiriwa kuwa yanafaa kabisa, kwa kuwa imani na upendo wenu vilikuwa tupu, na mlijionyesha tu kuwa ama waoga au wagumu. Kuhusu hili, Nitafanya hukumu ya mazuri au mabaya tu. Shaka Yangu inaendelea kuwa jinsi kila mmoja wenu hutenda na kujionyesha, kwa msingi ambao Nitatumia kufanya uamuzi kuhusu hatima yenu. Hata hivyo, ni sharti Niseme wazi kwamba: Sitawahurumia tena wale ambao hawakuwa waaminifu Kwangu kabisa wakati wa dhiki, kwa sababu huruma Yangu ina mipaka. Zaidi ya hayo, Simpendi yeyote yule ambaye amewahi kunisaliti Mimi, wala Sipendi kujihusisha na wale ambao hawawajali wenzao. Bila kujali huyo mtu ni nani, hii ndiyo tabia Yangu. Ni lazima Niwaambie hili: Yeyote atakayeuhuzunisha moyo Wangu hatapokea huruma kutoka Kwangu mara ya pili, na yeyote ambaye amekuwa mwaminifu Kwangu atadumu moyoni Mwangu milele.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Tayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 250)

Mungu alipokuja duniani Yeye hakuwa wa ulimwengu na Yeye hakuwa mwili ili apate kuufurahia ulimwengu. Mahali ambapo kufanya kazi kungefichua tabia Yake vizuri sana na pawe mahali pa maana zaidi ni mahali Alipozaliwa. Kama ni nchi takatifu au yenye uchafu, na bila kujali Anapofanya kazi, Yeye ni mtakatifu. Kila kitu duniani kiliumbwa na Yeye; Ni kwamba tu kila kitu kimepotoshwa na Shetani. Hata hivyo, vitu vyote bado ni Vyake; vyote viko mikononi Mwake. Kuja Kwake katika nchi yenye uchafu kufanya kazi ni kufichua utakatifu Wake; Yeye hufanya hivi kwa ajili ya kazi Yake, yaani, Yeye huvumilia aibu kubwa kufanya kazi kwa njia hii ili kuwaokoa watu wa nchi hii yenye uchafu. Hii ni kwa ajili ya ushuhuda na ni kwa ajili ya wanadamu wote. Kile aina hii ya kazi inawaruhusu watu kuona ni haki ya Mungu, na ina uwezo zaidi wa kuonyesha mamlaka ya juu kabisa ya Mungu. Ukuu na uadilifu Wake vinaonyeshwa kupitia wokovu wa kundi la watu wa hali ya chini ambao hakuna mtu anayewapenda. Kuzaliwa katika nchi yenye uchafu haimaanishi kabisa kuwa Yeye ni duni; inawaruhusu tu viumbe vyote kuuona utuu Wake na upendo wake wa kweli kwa wanadamu. Zaidi Anavyofanya kwa njia hii, zaidi inavyofichua upendo Wake safi zaidi kwa mwanadamu, upendo wake usio na dosari. Mungu ni mtakatifu na mwenye haki. Hata ingawa Alizaliwa katika nchi yenye uchafu, na ingawa Anaishi na watu hao ambao wamejawa uchafu, kama vile Yesu alivyoishi na wenye dhambi katika Enzi ya Neema, si kazi Yake yote kwa ajili ya kuishi kwa wanadamu wote? Je, si yote ni ili mwanadamu aweze kuupata wokovu mkuu? Miaka elfu mbili iliyopita Aliishi na wenye dhambi kwa miaka kadhaa. Hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya ukombozi. Leo, Anaishi na kikundi cha watu wachafu, wa hali ya chini. Hii ni kwa ajili ya wokovu. Je, si kazi Yake yote ni kwa ajili yenu, wanadamu hawa? Kama haingekuwa ili kuwaokoa wanadamu, kwa nini Angeishi na kuteswa pamoja na wenye dhambi kwa miaka mingi sana baada ya kuzaliwa horini? Na kama si kuwaokoa wanadamu, kwa nini Angerudi katika mwili mara ya pili, kuzaliwa katika nchi hii ambako mapepo hukusanyika, na kuishi na watu hawa ambao wamepotoshwa kwa kina na Shetani? Je, si Mungu ni mwaminifu? Ni aina gani ya kazi Yake ambayo haijakuwa kwa ajili ya wanadamu? Ni aina gani ambayo haijakuwa kwa ajili ya kudura yako? Mungu ni mtakatifu. Hili haliwezi kubadilika! Yeye hanajisiwi na uchafu, ingawa Amekuja katika nchi yenye uchafu; yote haya yanamaanisha tu kwamba upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wenye kuwajali wengine sana, mateso na aibu Anayoyavumilia ni makubwa sana! Hamjui kwamba Yeye hupitia aibu kubwa sana kwa ajili yenu wote na kwa ajili ya kudura yenu? Je, hamjui hivyo? Yeye hawaokoi watu wakuu au wana wa familia tajiri na zenye uwezo, lakini Yeye huwaokoa hasa wale ambao ni wa hali za chini na wanaodharauliwa na wengine. Je, si haya yote ni utakatifu Wake? Je, si haya yote ni haki Yake? Afadhali Azaliwe katika nchi yenye uchafu na kuteseka aibu yote kwa ajili ya kuishi kwa wanadamu wote. Mungu ni halisi sana—Hafanyi kazi ya uwongo. Je, si kila hatua ya kazi Yake imefanyika kwa utendaji hivi? Ingawa watu wote wanamkashifu na kusema kuwa Anakaa mezani pamoja na wenye dhambi, ingawa watu wote wanamdhihaki na kusema kuwa Anaishi na wana wa uchafu, na watu wa hali ya chini sana, bado Anajitolea bila ubinafsi, na bado Anakataliwa kwa njia hii kati ya wanadamu. Je, si mateso Anayoyahimili ni makubwa zaidi kuliko yenu? Je, si kazi Yake ni zaidi ya gharama ambayo mmelipa?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 251)

Mungu amejinyenyekeza Mwenyewe kwa kiwango fulani, kufanya kazi Yake katika watu hawa wachafu na wapotovu, na kukikamilisha kikundi hiki cha watu. Mungu hakupata mwili tu ili kuishi na kula kati ya watu, kuwalisha watu, kutoa wanachohitaji watu. Jambo muhimu zaidi ni kwamba Yeye hufanya kazi Yake kubwa ya wokovu na ushindi kwa watu hawa walio na upotovu usiovumilika. Alikuja katika kiini cha joka kubwa jekundu ili kuwaokoa watu hawa wapotovu mno, ili watu wote waweze kubadilishwa na kufanywa wapya. Tatizo kubwa ambalo Mungu huvumilia siyo tu shida ambayo Mungu mwenye mwili huvumilia, lakini hasa ni kwamba Roho wa Mungu hupitia udhalilishaji uliokithiri—Yeye hujinyenyekeza na kujificha Mwenyewe sana kiasi kwamba Yeye huwa mtu wa kawaida. Mungu alipata mwili na kuchukua mfano wa mwili ili watu waone kwamba Ana maisha ya kawaida ya binadamu, na kwamba ana mahitaji ya kawaida ya binadamu. Hili linatosha kuthibitisha kwamba Mungu amejinyenyekeza Mwenyewe kwa kiwango fulani. Roho wa Mungu hufanyika katika mwili. Roho Wake ni wa juu sana na mkuu, lakini Yeye huchukua mfano wa mwanadamu wa kawaida, wa mwanadamu asiye muhimu ili kufanya kazi ya Roho Wake. Ubora wa tabia, umaizi, hisi, ubinadamu, na maisha ya kila mmoja wenu vinaonyesha kwamba hamfai kweli kupokea kazi ya Mungu ya aina hii. Hakika hamfai kumruhusu Mungu kuvumilia shida kama hiyo kwa ajili yenu. Mungu ni mkubwa sana. Yeye ni mkuu sana, na watu ni duni sana na wa hali ya chini, lakini Yeye bado huwafanyia kazi. Yeye hakupata mwili tu ili kuwaruzuku watu, kuzungumza na watu, Yeye hata huishi pamoja na watu. Mungu ni mnyenyekevu sana, wa hupendeka sana.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Wale Wanaolenga Kutenda tu Ndio Wanaoweza Kukamilishwa

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 252)

Mungu amevumilia sana kulala bila kupata usingizi kwa ajili ya kazi ya binadamu. Kutoka vina vya juu hadi vya chini, Amepanda kwenda katika kuzimu ambapo mwanadamu anaishi kupitisha siku Zake na mwanadamu, hajawahi kulalamikia uchakavu walionao wanadamu, hajawahi kumlaumu kwa ukaidi wake, lakini Anavumilia mateso makuu kadri Anavyofanya kazi Yake. Inawezekanaje Mungu awe wa kuzimu? Inawezekanaje Aishi maisha Yake kuzimu? Lakini kwa ajili ya binadamu wote, ili binadamu wote waweze kupata pumziko mapema zaidi, Amestahimili fedheha na kupitia udhalimu kuja duniani, na Aliingia mwenyewe “jahanamu” na “kuzimu,” katika tundu la duma, kumwokoa mwanadamu. Mwanadamu amestahili vipi kumpinga Mungu? Ana sababu gani tena ya kumlaumu Mungu? Anawezaje kuwa na ujasiri wa kumwangalia Mungu tena? Mungu wa mbinguni Amekuja katika nchi hii chafu zaidi ya uovu, na Hajawahi kutangaza manung’uniko au malalamiko Yake kuhusu mwanadamu, lakini badala yake Anakubali kimyakimya maangamizi[1] na ukandamizaji wa mwanadamu. Kamwe Hajawahi kujibu matakwa ya mwanadamu yasiyokuwa na msingi, hajawahi kutaka mambo mengi yanayomuelemea mwanadamu, na hajawahi kumwekea mwanadamu matakwa yasiyokuwa na msingi; Anafanya tu kazi yote inayotakiwa na mwanadamu bila malalamiko: kufundisha, kutia mwanga, kukaripia, usafishaji wa maneno, kukumbusha, kusihi, kufariji, kuhukumu na kufunua. Ni hatua gani Alizozichukua ambazo si kwa ajili ya maisha ya mwanadamu? Ingawa Ameondoa matarajio na majaliwa ya mwanadamu, ni hatua zipi zilizochukuliwa na Mungu ambazo hazikuwa kwa ajili ya majaliwa ya mwanadamu? Ni ipi kati ya hatua hizo ambayo haijawahi kuwa kwa ajili ya mwanadamu kuendelea kuishi? Ni ipi kati ya hatua hizo haijakuwepo kwa ajili ya kumweka mwanadamu huru dhidi ya mateso haya na kunyanyaswa na nguvu za giza ambazo ni nyeusi kama usiku? Ni ipi kati ya hatua hizo si kwa ajili ya mwanadamu? Ni nani awezaye kuujua moyo wa Mungu, ambao ni sawa na mama mwenye upendo? Ni nani awezaye kuujua moyo wa Mungu wenye shauku? Moyo wa upendo na matarajio ya shauku ya Mungu vimelipwa kwa mioyo ya baridi, na usugu, na macho yanayoonyesha kutojali, kwa makaripio ya kujirudia na matusi ya mwanadamu, kwa maneno ya mkato na dhihaka na udhalilishaji, vimelipwa kwa dhihaka ya mwanadamu, kwa kukanyagwa na kukataliwa, kwa kutokuwa na ufahamu, na kupiga kite, na farakano, na uepukaji, kwa uongo, mashambulizi na ukali. Maneno ya wema ya Mungu yamekutana na nyuso kali na ufidhuli wa vidole elfu moja vinavyotikisika. Mungu anaweza tu kustahimili, Akiwa Ameinamisha kichwa, Akiwahudumia watu kama ng’ombe aliye radhi kufungwa.[2] Miezi na jua nyingi sana, Amekabiliana na nyota mara nyingi sana, Ameondoka alfajiri na kurudi jioni mara nyingi sana, na kurushwarushwa na kugeuzwa, Akivumilia maumivu makubwa mara elfu moja kuliko maumivu Aliyoyapata Alipokuwa Anaondoka kwa Baba Yake, Akivumilia mashambulizi na “kuvunja” kwa mwanadamu, na “kumshughulikia” na “kumpogoa” mwanadamu. Unyenyekevu na kufichika kwa Mungu vimelipwa kwa upendeleo[3] wa mwanadamu, kwa mitazamo na vitendo vya mwanadamu visivyokuwa vya haki, na kutojulikana Kwake, ustahimilivu, na uvumilivu vimelipizwa kwa jicho la tamaa la mwanadamu, mwanadamu hujaribu kumkanyaga Mungu hadi afe, bila majuto, na anajaribu kumkanyagia Mungu ardhini. Mtazamo wa mwanadamu kwa namna anavyomtendea Mungu ni wa “ujanja adimu,” na Mungu, ambaye anaonewa na kudharauliwa na mwanadamu, anakandamizwa chini ya makumi ya maelfu ya watu huku mwanadamu mwenyewe akisimama juu, kana kwamba angekuwa mfalme wa ngome, kana kwamba anataka kuchukua mamlaka kamili,[4] “kuendesha mahakama akiwa nyuma ya skrini,” kumfanya Mungu kuwa makini na mwenye kanuni “mwongozaji nyuma ya matukio,” ambaye haruhusiwi kupigana au kusababisha shida; lazima Mungu achukue nafasi ya “Mtawala wa Mwisho,” ni lazima Awe “kibaraka,”[5] bila uhuru wowote. Matendo ya mwanadamu hayaelezeki, sasa ana sifa gani ya kutaka hili au lile kuhusu Mungu? Ana sifa gani ya kutoa mapendekezo kwa Mungu? Anafaa kwa kiasi gani kumtaka Mungu amhurumie juu ya udhaifu wake? Anafaa kwa kiasi gani kupokea huruma ya Mungu? Anafaa kwa kiasi gani kupokea ukarimu wa Mungu kila mara? Anafaa kwa kiasi gani kupokea msamaha wa Mungu kila mara? Dhamiri yake ipo wapi? Alivunja moyo wa Mungu muda mrefu uliopita, ni muda mrefu toka ameuacha moyo wa Mungu katika vipande. Mungu alikuja miongoni mwa wanadamu Akiwa na nguvu nyingi na mwenye shauku kubwa, Akitegemea kwamba mwanadamu atakuwa mkarimu Kwake, hata kama ni kwa wema kiasi kidogo tu. Bado moyo wa Mungu haujafarijiwa na mwanadamu, yote Aliyoyapokea ni mashambulizi na mateso ya kuongezeka haraka;[6] moyo wa mwanadamu ni wenye tamaa sana, tamaa yake ni kubwa sana, hawezi akatosheka, siku zote ni mwenye fitina na jasiri pasi busara, hawezi kamwe kumpatia Mungu uhuru au haki ya kuzungumza, na anamwacha Mungu bila budi ila kukubali unyanyasaji, na kumruhusu mwanadamu kumtawala vyovyote apendavyo.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi na Kuingia (9)

Tanbihi:

1. “Maangamizi” inatumiwa kuweka wazi kutotii kwa wanadamu.

2. “Anaweza tu kustahimili, Akiwa Ameinamisha kichwa, Akiwahudumia watu kama ng’ombe aliye radhi kufungwa” ni kwa asili sentensi moja, lakini hapa imegawanywa mara mbili ili kuyafanya mambo wazi zaidi. Sentensi ya kwanza inahusu matendo ya mwanadamu, huku ya pili inaonyesha mateso aliyoyapitia Mungu, na kwamba Mungu ni mnyenyekevu na Aliyefichika.

3. “Upendeleo” unahusu tabia ya watu ya ukaidi.

4. “Kuchukua mamlaka kamili” inahusu tabia ya watu ya ukaidi. Wanajitukuza, huwafunga wengine, wakiwafanya wawafuate na kuteseka kwa ajili yao. Wao ni majeshi ambayo ni ya uadui kwa Mungu.

5. “Kibaraka” inatumiwa kuwadhihaki wale ambao hawamjui Mungu.

6. “Kuongezeka haraka” inatumiwa kuonyesha tabia duni ya watu.


Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 253)

Kila kitu ambacho Mungu hufanya ni cha vitendo, na hakuna Anachofanya ambacho ni kitupu. Mungu huja kati ya wanadamu, Akijinyenyekeza kuwa mtu wa kawaida. Haondoki baada ya kufanya tu kazi kidogo na kunena maneno machache; badala yake, kwa kweli Yeye huja kati ya wanadamu ili kupitia mateso ya ulimwengu. Analipa gharama ya uzoefu Wake mwenyewe wa kuteseka ili kulipia hatima ya wanadamu. Je, si hii ni kazi ya vitendo? Wazazi wanaweza kulipa gharama ya dhati kwa ajili ya watoto wao, na hii inawakilisha uaminifu wao. Kwa kufanya hivi, Mungu mwenye mwili bila shaka anakuwa mnyoofu na mwaminifu kabisa kwa wanadamu. Kiini cha Mungu ni uaminifu; Yeye hufanya Anachosema, na chochote Afanyacho hutimizwa. Kila kitu Anachowafanyia wanadamu ni cha kweli. Yeye haneni tu maneno; Anaposema kuwa atalipa gharama, Yeye kwa kweli hulipa gharama. Anaposema kwamba Atapitia mateso ya wanadamu na kuteseka badala yao, kwa kweli Yeye huja kuishi kati yao, Akihisi na kupitia mateso haya Yeye binafsi. Baada ya hapo, vitu vyote ulimwenguni vitakiri kuwa kila kitu ambacho Mungu hufanya ni sahihi na chenye haki, kwamba vyote ambavyo Mungu hufanya ni halisi: Hiki ni kipande cha ushahidi chenye nguvu. Wanadamu watakuwa na hatima nzuri katika siku zijazo, na wale wote watakaobaki watamsifu Mungu; watasifu sana kwamba matendo ya Mungu kweli yalifanywa kutokana na upendo Wake kwa wanadamu.

Asili ya Mungu ya uzuri na wema inaweza kuonekana katika umuhimu wa kupata mwili Kwake. Lolote Afanyalo ni la kweli; lolote Asemalo ni la dhati na halisi. Vitu vyote Anavyokusudia kuvifanya hufanywa kwa vitendo, na Yeye huvilipia gharama halisi; Yeye haneni tu maneno. Kwa hiyo, Mungu ni Mungu mwenye haki; Mungu ni Mungu mwaminifu.

Neno, Vol. 3. Mihadhara ya Kristo wa Siku za Mwisho. Kipengele cha Pili cha Umuhimu wa Kupata Mwili

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 254)

Njia ya uzima si kitu ambacho mtu yeyote anaweza kumiliki, wala si kitu ambacho kila mtu anaweza kufikia kwa urahisi. Hii ni kwa sababu uzima unaweza kutoka tu kwa Mungu, ambayo ni kusema, ni Mungu Mwenyewe pekee ndiye Anayemiliki kiini cha uzima, na ni Mungu Mwenyewe pekee aliye na njia ya uzima. Na hivyo Mungu tu ndiye chanzo cha uzima, na kijito cha maji ya uzima kinachotiririka nyakati zote. Tangu uumbaji wa dunia, Mungu amefanya kazi kubwa sana inayobeba pamoja nayo uzima uhai wa uzima, Amefanya kazi nyingi ambayo inamletea mwanadamu uzima, na Amelipa gharama kubwa inayomwezesha mwanadamu apate uzima. Hii ni kwa sababu Mungu Mwenyewe ni uzima wa milele, na Mungu Mwenyewe ndiye njia ambayo kwayo mwanadamu anaweza kufufuliwa. Mungu kamwe hajawahi kosa kuwepo moyoni mwa mwanadamu, na Anaishi miongoni mwa wanadamu wakati wote. Yeye ndiye nguvu ya kuendesha maisha ya mwanadamu, chanzo cha kuendelea kuishi kwa mwanadamu, na rasilmali kubwa ya kuwepo kwa mwanadamu baada ya kuzaliwa. Yeye huwasababisha watu kuzaliwa upya, na kuwawezesha kuishi kwa ushupavu katika jukumu lao binafsi. Akitegemea uwezo Wake, na nguvu Yake ya uzima isiyozima, mwanadamu ameishi kwa kizazi baada ya kizazi, huku nguvu ya uzima wa Mungu imekuwa ikitoa utegemezi miongoni mwa binadamu, na Mungu amelipa gharama ambayo hakuna mtu wa kawaida amewahi kulipa. Nguvu za Mungu za maisha zinaweza kutawala juu ya nguvu zozote; hata zaidi ya hayo, zinapita mamlaka yoyote. Uzima Wake ni wa milele, nguvu Zake ni za ajabu, na nguvu Zake za uzima haziwezi kuzidiwa na kiumbe yeyote au nguvu za adui. Nguvu za uzima wa Mungu zipo na hung’aa kwa mwangaza ulio mzuri sana, bila kujali muda au mahali. Mbingu na dunia zinaweza kupitia mabadiliko ya ajabu, lakini uzima wa Mungu ni ule ule daima. Mambo yote yanaweza kupita, lakini uzima wa Mungu bado utakuwepo. Hii ni kwa sababu Mungu ndiye chanzo cha kuwepo kwa vitu vyote, na mzizi unaotegemewa na kila kitu ili kiendelee kuishi. Asili ya maisha ya mwanadamu hutoka kwa Mungu, kuwepo kwa mbingu ni kwa sababu ya Mungu, na kuwepo kwa ardhi kunatokana na nguvu ya uhai wa Mungu. Hakuna kitu kinachomiliki nguvu kinachoweza kuzidi ukuu wa Mungu, na hakuna kitu chenye nguvu kinachoweza kuvunja mipaka ya mamlaka ya Mungu. Kwa njia hii, bila kujali wao ni nani, kila mtu lazima ajiwasilishe kwa utawala wa Mungu, kila mtu lazima aishi chini ya amri za Mungu, na hakuna mtu anayeweza kutoroka kutoka katika utawala Wake.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 255)

Kama kweli unataka kupata njia ya uzima wa milele, na kama wewe unayo tamaa katika utafutaji wako kwa ajili yake, basi kwanza ulijibu swali hili: Mungu yuko wapi leo? Labda utajibu kwamba Mungu anaishi mbinguni, bila shaka—Hangekuwa akiishi nyumbani kwako, sivyo? Labda unaweza kusema, kawaida Mungu anaishi kati ya mambo yote. Au unaweza kusema kwamba Mungu anaishi katika moyo wa kila mtu, au kwamba Mungu yuko katika ulimwengu wa kiroho. Mimi sipingi lolote kati ya haya, lakini lazima nifafanue suala hilo. Sio sahihi kabisa kusema kwamba Mungu anaishi katika moyo wa mwanadamu, wala si makosa kabisa. Hayo ni kwa sababu, miongoni mwa wanaomuamini Mungu, wapo ambao imani yao ni ya kweli na wale ambao imani yao ni ya uwongo, kuna wale ambao Mungu amewaridhia na wale ambao Amewachukia, wapo wanaomridhia na wale anaowachukia, na wapo ambao anawafanya kuwa wakamilifu na wale anaowaondoa. Na kwa hivyo Ninasema kwamba Mungu anaishi ndani ya mioyo ya watu wachache tu, na watu hawa bila shaka ni wale wanaomwamini Mungu kweli, wale ambao Mungu anawakubali, wale wanaompendeza Yeye, na wale ambao Yeye huwakamilisha. Wao ni wale wanaoongozwa na Mungu. Kwa kuwa wanaongozwa na Mungu, kwa hivyo ni watu ambao tayari wamesikia na kuona njia ya Mungu ya uzima wa milele. Wale ambao imani yao kwa Mungu ni ya uongo, wale ambao hawajaidhinishwa na Mungu, wale ambao wanadharauliwa na Mungu, wale ambao wamechujwa na Mungu—wamefungwa katika kukataliwa na Mungu, wamefungwa kubaki bila njia ya maisha, na wamefungwa kubaki wajinga wa kujua aliko Mungu. Kwa upande mwingine, wale ambao Mungu anaishi katika mioyo yao wanajua aliko Mungu. Wao ndio watu ambao Mungu amewapa njia ya uzima wa milele, na wao ndio wanaomfuata Mungu. Je, unajua, sasa, aliko Mungu? Mungu yuko katika moyo wa mwanadamu na upande wa mwanadam. Hayupo tu katika ulimwengu wa kiroho, na juu ya vitu vyote, lakini hata zaidi Yupo duniani ambapo mwanadamu huishi. Na hivyo kuwasili kwa siku za mwisho kumechukua hatua za kazi ya Mungu katika eneo jipya. Mungu ana ukuu juu ya vitu vyote katika ulimwengu, na Yeye ndiye mhimili mkuu wa mwanadamu katika moyo wake, na zaidi ya hayo, Yuko miongoni mwa mwanadamu. Ni kwa njia hii pekee Anaweza kuleta njia ya uzima kwa mwanadamu, na kumleta mwanadamu katika njia ya uzima. Mungu amekuja duniani, na Anaishi kati ya wanadamu, ili wanadamu wanaweza kupata njia ya uzima, na hivyo binadamu anaweza kuwepo. Wakati huo huo, Mungu pia naamuru vitu vyote katika ulimwengu, ili viweze kushirikiana na usimamizi Wake miongoni mwa wanadamu. Na hivyo, kama wewe unakiri tu kwamba Mungu yuko mbinguni na katika moyo wa mwanadamu, lakini usikiri ukweli wa kuwepo kwa Mungu miongoni mwa watu, basi kamwe hutapata uzima, na kamwe hutapata njia ya kweli.

Mungu Mwenyewe ni uzima, na ukweli, na uzima Wake na ukweli vipo pamoja. Wale ambao hawana uwezo wa kupata ukweli hawatapata uzima kamwe. Bila mwongozo, usaidizi, na utoaji wa ukweli, utapata tu barua, mafundisho, na, zaidi ya hayo, kifo. Maisha ya Mungu ni ya milele, na ukweli wake na maisha hupatana. Kama huwezi kupata chanzo cha ukweli, basi huwezi kupata lishe ya maisha; kama huwezi kupata starehe ya maisha, basi utakuwa hakika huna ukweli, na hivyo mbali na mawazo na dhana, ukamilifu wa mwili wako hautakuwa chochote ila mwili, mwili wako unaonuka. Ujue kwamba maneno ya vitabu hayahesabiki kama maisha, kumbukumbu za historia haziwezi kupokelewa kama ukweli, na mafundisho ya siku za nyuma hayawezi kutumika kama sababu ya maneno ya sasa anayosema Mungu. Kinachoonyeshwa tu na Mungu anapokuja duniani na kuishi miongoni mwa binadamu ni ukweli, maisha, mapenzi ya Mungu, na njia Yake ya sasa ya kufanya kazi. Kama wewe utatumia rekodi ya maneno yaliyosemwa na Mungu wakati wa enzi zilizopita leo, basi wewe ni mtafutaji wa mambo ya kale, na njia bora ya kukueleza wewe ni mtaalamu wa urithi wa kihistoria. Kwa sababu wewe daima unaamini katika athari ya kazi ambayo Mungu alifanya katika nyakati zilizopita, unaamini tu katika kivuli cha Mungu kilichoachwa tangu Alipofanya kazi hapo awali miongoni mwa wanadamu, na unaamini tu katika njia ambayo Mungu aliwapa wafuasi Wake katika nyakati za awali. Huamini katika mwelekeo wa kazi ya Mungu leo, huamini katika uso wa utukufu wa Mungu leo, na huamini katika njia ya sasa ya kweli iliyotolewa na Mungu. Na hivyo wewe ni mwotaji wa mchana ambaye hana ufahamu kamwe na hali ya mambo ya sasa. Kama sasa bado wewe unafuata maneno yasiyokuwa na uwezo wa kuleta maisha kwa binadamu, basi wewe ni kipande cha ukuni uliokauka kisicho na matumaini[a], kwa maana wewe ni mwenye kushikilia ukale mno, asioweza kubadilika, huwezi kusikiza wosia!

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Tanbihi:

a. Kipande cha gogo lililokufa: Nahau ya Kichina yenye maana “-siyoweza kusaidiwa.”


Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 256)

Mungu Mwenyewe ni ukweli, Mwenyewe anao ukweli, na Yeye ndiye chanzo cha ukweli. Kila kitu chanya na kila ukweli unatoka Kwake. Anaweza kutoa hukumu juu ya wema na ubaya wa mambo yote na matukio yote; Anaweza kutoa hukumu juu ya mambo ambayo yametukia, mambo ambayo yanatukia sasa, na mambo ya baadaye ambayo bado hayajajulikana kwa mwanadamu. Yeye ndiye hakimu wa pekee Anayeweza kutoa hukumu juu ya wema na ubaya wa mambo yote, na hii inamaanisha kuwa wema na ubaya wa mambo yote unaweza kuhukumiwa na Yeye tu. Anajua sheria za mambo yote. Huu ndio mfano halisi wa ukweli, jambo ambalo linamaanisha kwamba Yeye Mwenyewe anacho kiini cha ukweli. Ikiwa mwanadamu angeuelewa ukweli na kupata ukamilifu, basi angekuwa na uhusiano wowote na mfano halisi wa ukweli? Mwanadamu anapokamilishwa, yeye huwa na ufahamu sahihi wa yote ambayo Mungu hufanya sasa na mambo Anayohitaji, naye huwa na njia sahihi ya kutenda; mwanadamu pia huyaelewa mapenzi ya Mungu na hujua tofauti kati ya mema na mabaya. Lakini kuna mambo kadhaa ambayo mwanadamu hawezi kuyafikia, mambo ambayo anaweza kuyajua tu baada ya Mungu kumwambia kuyahusu—je, mwanadamu anaweza kujua mambo ambayo bado hayajajulikana, mambo ambayo bado Mungu hajamwambia? (Hawezi.) Mwanadamu hawezi kufanya utabiri. Aidha, hata kama mwanadamu angeupata ukweli kutoka kwa Mungu, na awe na uhalisi wa ukweli, na ajue kiini cha ukweli mwingi, na awe na uwezo wa kutofautisha mema na mabaya, basi angekuwa na uwezo wa kudhibiti na kutawala vitu vyote? (La.) Hiyo ndiyo tofauti. Viumbe walioumbwa wanaweza tu kuupata ukweli kutoka kwa chanzo cha ukweli. Je, wanaweza kuupata ukweli kutoka kwa mwanadamu? Mwanadamu anaweza kuwapa ukweli? Mwanadamu anaweza kumtunza mwanadamu? Hawezi, na hiyo ndiyo tofauti. Unaweza kupokea tu, siyo kutoa—je, unaweza kuitwa mfano halisi wa ukweli? Kiini cha mfano halisi wa ukweli ni kipi hasa? Ni chanzo kinachoutoa ukweli, chanzo cha utawala na mamlaka juu ya vitu vyote, na pia ni viwango na sheria ambazo kwazo vitu vyote na matukio yote yanahukumiwa. Huu ndio mfano halisi wa ukweli.

Neno, Vol. 4. Kuwafichua Wapinga Kristo. Kipengele cha Nane: Wangefanya Wengine Wawatii Wao Pekee, Sio Kweli au Mungu (Sehemu ya Tatu)

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 257)

Katika kuonyesha Kwake ukweli, Mungu huonyesha tabia na kiini Chake; havionyeshwi kulingana na mihutasari ya wanadamu ya mambo mbalimbali chanya na njia za kuzungumza ambazo wanadamu wanatambua. Maneno ya Mungu ni maneno ya Mungu; maneno ya Mungu ni ukweli. Hayo ndiyo msingi na sheria ambayo kwayo wanadamu wanapaswa kuishi, na hizo zinazodaiwa kuwa kanuni zinazotokana na binadamu zimelaaniwa na Mungu. Hazikubaliwi na Yeye, sembuse kuwa asili au msingi wa matamshi Yake. Mungu huonyesha tabia Yake na kiini Chake kupitia maneno Yake. Maneno yote yaliyotolewa na maonyesho ya Mungu ni ukweli, kwa maana Yeye anacho kiini cha Mungu, na Yeye ndiye uhalisi wa mambo yote chanya. Ukweli kwamba maneno ya Mungu ni ukweli haubadiliki kamwe, bila kujali jinsi wanadamu hawa wapotovu wanavyoyachukulia au kuyafafanua, wala jinsi wanavyoyaona au kuyaelewa. Haijalishi ni maneno mangapi ya Mungu ambayo yamezungumzwa, na bila kujali jinsi binadamu hawa wapotovu na wenye dhambi wanavyoyashutumu kwa kiasi kipi, hata kiasi kwamba hawayasambazi, na hata kufikia kiwango ambacho yanadharauliwa na wanadamu wapotovu—hata katika hali hizi, bado kuna ukweli ambao hauwezi kubadilishwa: Hizi zinazodaiwa kuwa mila na desturi ambazo wanadamu huthamini haziwezi kuwa vitu chanya na haziwezi kuwa ukweli, hata sababu zilizopo hapo juu zikizingatiwa. Hili haliwezi kubadilika. Tamaduni za jadi za wanadamu na njia za kuishi hazitakuwa ukweli kwa sababu ya mabadiliko au kupita kwa wakati, na wala maneno ya Mungu hayatakuwa maneno ya mwanadamu kwa sababu ya shutuma na kusahau kwa wanadamu. Kiini hiki hakitabadilika kamwe; ukweli ni ukweli kila wakati. Kuna ukweli ndani ya hili: Hiyo misemo yote inayofupishwa na wanadamu inatoka kwa Shetani—ni fikira na mawazo ya wanadamu, hata inatokana na hamaki ya binadamu, na haihusiani hata kidogo na mambo chanya. Maneno ya Mungu, kwa upande mwingine, ni maonyesho ya kiini na hadhi ya Mungu. Yeye huyaonyesha maneno haya kwa sababu gani? Kwa nini Ninasema maneno hayo ni ukweli? Sababu ni kwamba Mungu anatawala juu ya sheria, kanuni, vyanzo, viini, uhalisi na siri zote za vitu vyote, na vimefumbatwa mkononi Mwake, na ni Mungu pekee Anayejua kanuni, uhalisi, ukweli, na siri zote za vitu vyote; Anajua asili ya vitu hivyo na vyanzo vyao ni nini hasa. Kwa hivyo, ni ufafanuzi wa vitu vyote uliotajwa katika maneno ya Mungu pekee ndio sahihi kabisa, na mahitaji kwa wanadamu yaliyo ndani ya maneno ya Mungu ndicho kiwango pekee kwa wanadamu—kigezo pekee ambacho mwanadamu anapaswa kuishi kwa kufuata.

Neno, Vol. 4. Kuwafichua Wapinga Kristo. Kipengele cha Tisa (Sehemu ya Kwanza)

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 258)

Kuanzia wakati unapokuja ulimwenguni humu ukilia, unaanza kutimiza majukumu yako. Kwa ajili ya mpango wa Mungu na kutawaza Kwake, unafanya wajibu wako na kuanza safari yako ya maisha. Haijalishi ulikokulia kulivyo, na haijalishi safari iliyo mbele yako ilivyo, kwa vyovyote vile, hakuna anayeweza kuepuka mipango na mipangilio ya Mbinguni, na hakuna anayeweza kudhibiti hatima yake mwenyewe, kwani ni Yeye tu aliye na mamlaka juu ya vitu vyote ndiye Anayeweza kufanya kazi hiyo. Tangu kuwepo kwa mwanadamu hapo mwanzo, Mungu daima amekuwa Akifanya kazi Yake kwa namna hii, Akiusimamia ulimwengu, na kuelekeza sheria za mabadiliko kwa vitu vyote na mweleke wa kusonga kwao. Kama vitu vyote, mwanadamu kwa ukimya na bila kujua anastawishwa kwa utamu na mvua na umande kutoka kwa Mungu; kama vitu vyote, mwanadamu bila kujua, anaishi chini ya mpango wa mkono wa Mungu. Moyo na roho ya mwanadamu vimo katika mshiko wa Mungu, na kila kitu cha maisha yake kinatazamwa machoni pa Mungu. Bila kujali kama unaamini haya yote au la, chochote na vitu vyote, viwe vilivyohai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilishwa, kufanywa vipya, na kupotea kulingana na fikira za Mungu. Hivi ndivyo ambavyo Mungu anashikilia mamlaka juu ya vitu vyote.

Usiku unapoingia polepole, mwanadamu huwa hafahamu, kwani moyo wa mwanadamu hauwezi kujua jinsi giza linavyoingia au ni wapi linakotokea. Usiku unapotoweka polepole, mwanadamu hukaribisha mwanga wa mchana, lakini kuhusu mahali ambapo nuru imetokea, na jinsi imeliondoa giza la usiku, mwanadamu anajua machache, na hata anafahamu mchache zaidi Mabadiliko haya ya kawaida ya mchana na usiku humpitisha mwanadamu kutoka kipindi kimoja hadi kingine, kutoka kipindi kimoja cha kihistoria hadi kingine, wakati huu wote zinahakikisha kwamba kazi ya Mungu katika kila kipindi na mpango Wake wa kila enzi unatekelezwa. Mwanadamu amepitia vipindi hivi vyote tofauti akimfuata Mungu, lakini bado hafahamu kwamba Mungu ana ukuu juu ya hatima ya vitu vyote na viumbe hai, wala jinsi Mungu anavyopanga na kuelekeza vitu vyote. Hili ni jambo ambalo limekwepa ufahamu wa binadamu tangu enzi za kale mpaka leo. Kuhusu sababu, siyo kwa sababu matendo ya Mungu hayafahamiki, au kwa sababu mpango wa Mungu bado haujakamilika, lakini ni kwa sababu moyo na roho ya mwanadamu viko mbali sana na Mungu, kiasi cha kwamba, mwanadamu anabaki katika huduma ya Shetani wakati ule ule anapomfuata Mungu—na hata halitambui hili. Hakuna anayetafuta kwa bidii nyayo za Mungu na kuonekana kwa Mungu, na hakuna aliye tayari kuishi katika utunzaji na ulinzi wa Mungu. Badala yake wako tayari kutegemea upotoshaji wa Shetani, yule mwovu, ili kubadilishwa kufuatana na dunia hii na kanuni za kuishi ambazo wanadamu waovu wanafuata. Katika hatua hii, moyo na roho ya mwanadamu vinakuwa ushuru ambao mwanadamu anatoa kwa shetani na kuwa riziki ya Shetani. Hata zaidi, moyo wa binadamu na roho yake zimekuwa mahali ambapo Shetani anaweza kuishi na uwanja wake wa kuchezea unaofaa. Kwa njia hii, mwanadamu bila kujua anapoteza ufahamu wake wa kanuni za mwenendo wa mwanadamu, na wa thamani na umuhimu wa kuwepo kwa binadamu. Sheria za Mungu na agano kati ya Mungu na mwanadamu polepole vinakuwa giza katika moyo wa mwanadamu, na anaacha kumtafuta au kumsikiliza Mungu. Wakati unavyopita, mwanadamu haelewi tena kwa nini Mungu alimuumba, wala haelewi maneno yanayotoka katika kinywa cha Mungu na yote yanayotoka kwa Mungu. Kisha mwanadamu anaanza kupinga sheria na amri za Mungu, na moyo wake na roho yake vinakufa ganzi…. Mungu amempoteza mwanadamu ambaye Alimuumba hapo mwanzo, na mwanadamu amepoteza asili aliyokuwa nayo hapo awali: Hii ndio huzuni ya jamii hii ya binadamu. Kwa hakika, tangu mwanzo hadi sasa, Mungu ameandaa janga kwa ajili ya wanadamu, ambapo mwanadamu ndiye mhusika mkuu na mwathirika. Na hakuna anayeweza kujibu kuhusu mwelekezi wa janga hili ni nani.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Ndiye Chanzo cha Uzima wa Mwanadamu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 259)

Mungu aliuumba ulimwengu huu na kumleta mwanadamu ndani yake, kiumbe hai ambaye Alimtia uhai ndani yake. Kisha, mwanadamu akaja kuwa na wazazi na jamaa na hakuwa mpweke tena. Tangu mwanadamu alipotazama kwa mara ya kwanza ulimwengu huu unaoonekana, alikusudiwa kuishi ndani ya utaratibu wa Mungu. Ni pumzi ya uhai inayotoka kwa Mungu ambayo inamtegemeza kila kiumbe hai katika kipindi cha ukuaji wake hadi kufikia utu uzima. Wakati wa mchakato huu, hakuna anayehisi kwamba mwanadamu anakua chini ya uangalizi wa Mungu, lakini badala yake anaamini kwamba mwanadamu anafanya hivyo chini ya utunzaji wa upendo wa wazazi wake, na kwamba ni silika yake mwenyewe ya maisha ambayo inaongoza mchakato huu wa kukua kwake. Hii ni kwa sababu mwanadamu hajui ni nani aliyetoa maisha yake, au ni wapi yalikotoka, sembuse hata jinsi ambavyo silika ya maisha inavyoweza kusababisha miujiza. Anajua tu kwamba chakula ndicho msingi wa kuendelea kwa maisha yake, kwamba uvumilivu ndio chanzo cha kuwepo kwake, na kwamba imani zilizopo katika akili yake ndio mtaji ambao kuishi kwake kunategemea. Mwanadamu hajui kabisa kuhusu neema na riziki zitokazo kwa Mungu, na kwa njia hii yeye hupoteza. uzima aliopewa na Mungu bila azma…. Hakuna hata mmoja wa wanadamu hawa amepoteza maisha ambayo Mungu amempa. Mungu anaendelea tu kufanya kazi juu ya mwanadamu, Akiwa hana matarajio yoyote kutoka kwake, kama jinsi ambavyo Amepanga. Anafanya hivyo kwa matumaini kwamba siku moja, mwanadamu ataamka kutoka katika ndoto yake na kwa ghafla atambue thamani na maana ya maisha, gharama aliyolipa Mungu kwa yote ambayo Amempa, na shauku ambayo kwayo Mungu anamngojea mwanadamu ageuke amrudie Yeye. Hakuna mtu yeyote ambaye amewahi kuchunguza siri zinazoongoza asili na kuendelea kwa maisha ya mwanadamu. Ni Mungu tu, ambaye Anaelewa yote haya, kwa ukimya Anavumilia mapigo na maumivu ambayo binadamu, ambaye amepokea kila kitu kutoka kwa Mungu lakini hana shukrani, anampa Yeye. Mwanadamu hufurahia yote ambayo maisha huleta kwa hakika, na, vivyo hivyo, ni “jambo la hakika,” kwamba Mungu anasalitiwa na mwanadamu, Anasahaulika na mwanadamu, na kutozwa kwa nguvu na mwanadamu. Je, inaweza kuwa kwamba mpango wa Mungu una umuhimu kama huo kweli? Je, inaweza kuwa kwamba mwanadamu, kiumbe huyu aliye hai ambaye alitoka katika mkono wa Mungu, ni wa maana namna hiyo kweli? Mpango wa Mungu kwa hakika ni muhimu kabisa; hata hivyo, kiumbe chenye uhai kilichoumbwa na mkono wa Mungu kipo kwa ajili ya mpango Wake. Kwa hivyo, Mungu hawezi kuuharibu mpango Wake kwa sababu Anaichukia jamii hii ya wanadamu. Ni kwa ajili ya mpango Wake na kwa ajili ya pumzi aliyotoa ndiyo maana Mungu anavumilia mateso yote, sio kwa ajili ya mwili wa mwanadamu ila ni kwa sababu ya uhai wa mwanadamu. Yeye anafanya hivyo ili kurudisha pumzi Aliyopulizia ndani ya mwanadamu, wala si kuchukua tena mwili wa mwanadamu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Ndiye Chanzo cha Uzima wa Mwanadamu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 260)

Wote wanaokuja katika ulimwengu huu lazima wapitie maisha na kifo, na wengi wao walipitia mzunguko wa kifo na kuzaliwa upya. Wale wanaoishi watakufa hivi karibuni na wafu watarejea karibuni. Yote haya ni mchakato wa maisha uliopangwa na Mungu kwa kila kiumbe hai. Hata hivyo, mchakato huu na mzunguko huu hasa ni ukweli ambao Mungu anataka binadamu auone: kwamba maisha aliyopewa mwanadamu na Mungu hayana mwisho, na hayazuiliwi na maumbile ya nje, wakati, au nafasi. Hivyo ndivyo lilivyo fumbo la maisha aliyopewa mwandamu na Mungu, na ni udhihirisho kwamba maisha yalikuja kutoka Kwake. Ingawa watu wengi wanaweza kukosa kuamini kwamba maisha ya mwanadamu yalitoka kwa Mungu, mwanadamu bila kujua anafurahia yote yatokayo kwa Mungu, iwe anaamini au anakana uwepo Wake. Siku moja Mungu kwa ghafla Akibadili moyo na Atake kurudisha yote yaliyomo duniani na Achukue uzima Aliotoa, basi yote duniani yataisha. Mungu hutumia uzima Wake kukimu vitu vyote vilivyo hai na visivyo hai, na kuleta vyote kwenye utaratibu mzuri kupitia nguvu na mamlaka Yake. Huu ni ukweli ambao hauwezi kufikirika au kueleweka na yeyote, na kweli hizi zisizoeleweka kwa fikira zetu ni udhihirisho halisi wa, na ushahidi wa, nishati uhai ya Mungu. Sasa hebu Niwaambie siri: Ukubwa wa maisha ya Mungu na nguvu za maisha Yake haziwezi kueleweka na kiumbe yeyote aliyeumbwa. Hivi ndivyo hali ilivyo sasa, kama ilivyokuwa zamani, na itakuwa hivyo kwa wakati ujao. Siri ya pili Nitakayotoa ni hii: Chanzo cha uzima kwa viumbe vyote hutoka kwa Mungu; bila kujali jinsi wanavyoweza kuwa tofauti katika maumbile au muundo, na haijalishi wew ni kiumbe hai wa aina gani, hakuna kiumbe anayeweza kwenda kinyume na njia ya maisha iliyowekwa na Mungu. Kwa vyovyote vile, kile Ninachotaka ni mwanadamu aweze kuelewa hili: Bila utunzaji, ulinzi, na utoaji wa Mungu, mwanadamu hawezi kupokea yote aliyokusudiwa kupokea, bila kujali jinsi anavyojaribu kwa bidii au jinsi anavyopambana kwa kwa sulubu. Bila ruzuku ya uzima kutoka kwa Mungu, mwanadamu anapoteza thamani ya kuishi na maana ya maisha. Je, Mungu angewezaje kumruhusu mwanadamu, ambaye bila umakini amepoteza thamani ya maisha Yake, Asiwe na wasiwasi kiasi hicho? Kama vile Nilivyosema hapo awali: Usisahau kwamba Mungu ndiye chanzo cha uhai wako. Ikiwa mwanadamu atashindwa kuthamini yote ambayo Mungu Amemfanyia, si tu kwamba Mungu atachukua kile Alichotoa hapo mwanzo, lakini pia Atamfanya mwanadamu amlipe fidia mara mbili ya gharama zote Alizotoa.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Ndiye Chanzo cha Uzima wa Mwanadamu

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 261)

Kila kitu cha ulimwengu huu kinabadilika haraka sawasawa na mawazo ya Mwenyezi, na chini ya macho Yake. Mambo ambayo wanadamu hawajawahi kuyasikia yanaweza kuja kwa ghafla, ilhali vitu ambavyo wanadamu wamevimiliki kwa muda mrefu vinaweza kutoweka bila wao kujua. Hakuna anayeweza kutambua mahali alipo Mwenyezi, sembuse mtu yeyote anayeweza kuhisi kule kwenda zaidi ya uwezo wa binadamu na ukuu wa nguvu za maisha za Mwenyezi. Yeye ni Mkuu kwa kuwa Anaweza kutambua kile ambacho wanadamu hawawezi. Yeye ni Mkuu kwa kuwani Yeye anayekataliwa na wanadamu na bado Anawaokoa wanadamu. Yeye anajua maana ya uzima na mauti na, isitoshe, Anajua sheria za kuishi ambazo wanadamu, ambao wameumbwa, wanapaswa kuzifuata. Yeye ndiye msingi wa kuwepo kwa mwanadamu, na Yeye ndiye Mkombozi anayewafufua wanadamu tena. Anailemea mioyo yenye furaha kwa huzuni, na kuiinua mioyo yenye huzuni kwa furaha, yote ni kwa ajili ya kazi Yake, na kwa ajili ya mpango Wake.

Binadamu, wakiwa wamepotoka kutoka kwa ugavi wa uzima wa Mwenye Uweza, hawajui kusudi la kuwepo, lakini wanaogopa kifo hata hivyo. Hawana msaada au tegemeo, lakini bado hawako tayari kufumba macho yao, na wanajikaza kuitegemeza miili yao, isiyo na hisia yoyote ya kiroho, na kujikokota kuishi maisha duni duniani humu. Wewe unaishi hivyo, bila tumaini, kama wafanyavyo wengine, bila lengo. Ni Yule Mtakatifu wa ngano pekee ndiye Atakayewaokoa watu ambao, wakiwa wanaomboleza katikati ya mateso yao, wanangoja kwa hamu kubwa kuja Kwake. Imani kama hiyo imebaki bila kutimizwa kwa muda mrefu ndani ya wale wasio na fahamu. Hata hivyo, bado wanaitamani sana. Mwenye Uweza ana rehema kwa watu hawa ambao wameteseka sana; wakati huo huo, Anawachukia watu hawa wasio na fahamu zozote kabisa, kwani inabidi Asubiri kwa muda mrefu sana kabla ya kupokea jibu kutoka kwa watu. Anataka kutafuta, kutafuta moyo wako na roho yako, na kukuletea maji na chakula, ili uzinduke na usiwe na kiu au njaa tena. Unapochoka na unapohisi kiasi fulani cha ukiwa wa dunia hii, usijihisi umepotea, usilie. Mwenyezi Mungu, Mwangalizi, atakumbatia kuja kwako wakati wowote. Anakesha kando yako. Anakusubiri urejee, akisubiri siku utakayorejesha kumbukumbu yako ghafla: utakapotambua kwamba ulitoka kwa Mungu, na kwamba, wakati fulani usiojulikana ulipoteza mwelekeo wako, wakati fulani usiojulikana ulilala usingizi njiani, na wakati fulani usiojulikana ulikuwa na “baba”; unapotambua, zaidi ya hayo, kwamba Mwenye Uweza amekuwa akikesha daima, Akisubiri hapo kwa muda mrefu sana, sana kwa ajili ya kurudi kwako. Amekuwa akitamani kwa hamu kubwa, akisubiri itikio lisilo na jibu. Kukesha Kwake ni kwa thamani isiyokadirika, na ni kwa ajili ya moyo wa mwanadamu na roho ya mwanadamu. Pengine kukesha Kwake hakuna kikomo, au pengine kumefika mwisho. Lakini unapaswa kujua hasa ulipo moyo wako na ilipo roho yako sasa hivi.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kutanafusi kwa Mwenye Uweza

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 262)

Kama washiriki wa jamii ya wanadamu na Wakristo waaminifu, ni jukumu na wajibu wetu sote kutoa akili na miili yetu kwa ajili ya kutimiza agizo la Mungu, kwa maana asili yetu yote inatoka kwa Mungu, na tunaishi kwa sababu ya ukuu wa Mungu. Kama akili na miili yetu haipo kwa ajili ya agizo la Mungu na kwa ajili ya kusudi la haki ya wanadamu, basi roho zetu hazitastahili mbele ya wale waliokufa kishahidi kwa ajili ya agizo la Mungu, na zaidi sana hazistahili kwa Mungu, aliyetupa kila kitu.

Mungu aliumba ulimwengu huu, Alimuumba mwanadamu huyu na, zaidi ya hayo, Alikuwa muasisi wa utamaduni wa kale wa Kigiriki na ustaarabu wa binadamu. Ni Mungu pekee Anayewafariji wanadamu hawa, na ni Mungu pekee Anayewajali wanadamu hawa usiku na mchana. Ukuaji na maendeleo ya binadamu hayatenganishwi na ukuu wa Mungu, na historia na mustakabali wa mwanadamu hauwezi kuepuka mipango inayofanywa na mikono ya Mungu. Kama wewe ni Mkristo wa kweli, basi kwa hakika utaamini kwamba kupanda na kushuka kwa nchi ama taifa lolote kunafanyika chini ya mipango ya Mungu. Mungu pekee ndiye Anayejua hatima ya nchi ama taifa lolote, na ni Mungu pekee ndiye Anayedhibiti mwenendo wa wanadamu hawa. Ikiwa wanadamu wanataka kuwa na hatima nzuri, ikiwa nchi inataka kuwa na hatima nzuri, basi mwanadamu lazima amsujudie Mungu katika ibada, na aje mbele za Mungu akitubu na kuungama, kama sivyo majaliwa na hatima ya mwanadamu hayataepuka kumalizika kwa janga.

Angalia nyuma wakati Nuhu alipojenga safina: Wanadamu walikuwa wamepotoka sana, walikuwa wamepotea kutoka katika baraka za Mungu, hawakuwa wanatunzwa na Mungu tena, na walikuwa wamepoteza ahadi za Mungu. Waliishi gizani, bila mwangaza wa Mungu. Hivyo wakawa waasherati kwa asili, wakajiachilia katika mkengeuko wa kutisha. Watu kama hao hawangeweza tena kupokea ahadi za Mungu; hawakufaa kushuhudia uso wa Mungu, wala kusikia sauti ya Mungu, kwani walikuwa wamemwacha Mungu, waliweka kando yote Aliyowapa, na kusahau mafunzo ya Mungu. Mioyo yao ilienda mbali zaidi na zaidi kutoka kwa Mungu, na ilivyofanya hivyo, wakawa wapotovu zaidi ya mantiki na ubinadamu wote na wakazidi kuwa waovu. Hivyo walisogelea kifo zaidi, na kukabiliwa na ghadhabu na adhabu ya Mungu. Ni Nuhu tu aliyemwabudu Mungu na kuepukana na uovu, na hivyo aliweza kusikia sauti ya Mungu, na kusikia maagizo ya Mungu. Alijenga safina kulingana na maagizo ya neno la Mungu, na akakusanya aina zote za viumbe hai. Na kwa njia hii, wakati kila kitu kilikuwa kimetayarishwa, Mungu aliangamiza dunia. Nuhu tu na wanachama saba wa familia yake walinusurika maangamizi, kwani Nuhu alimwabudu Yehova na kuepukana na uovu.

Kisha angalia enzi ya sasa: Hawa watu wenye haki kama Nuhu, ambao wangeweza kumwabudu Mungu na kuepuka uovu, wamekoma kuwepo. Lakini bado Mungu ana fadhili kwa mwanadamu huyu, na Anamsamehe mwanadamu wakati huu wa enzi ya mwisho. Mungu anawatafuta wale wanaotamani Aonekane. Anawatafuta wale wanaoweza kuyasikia maneno Yake, wale ambao hawajasahau agizo Lake na wanatoa mioyo na miili yao Kwake. Anawatafuta wale walio watiifu kama watoto wachanga mbele Zake, na hawampingi. Kama hujazuiliwa na nguvu zozote katika ibada yako Kwake, basi Mungu atakutazama kwa upendeleo na Ataweka baraka Zake juu yako. Kama wewe ni wa cheo cha juu, mwenye sifa ya kuheshimika, mwenye maarifa mengi, mwenye mali nyingi, na kuungwa mkono na watu wengi, lakini mambo haya hayakuzuii kuja mbele za Mungu kuukubali wito Wake na agizo Lake, kufanya kile Mungu anachokuambia ufanye, basi yote unayoyafanya yatakuwa yenye umuhimu zaidi duniani na yenye haki zaidi kwa binadamu. Ukiukataa wito wa Mungu kwa sababu ya hadhi yako na malengo yako mwenyewe, yote utakayoyafanya yatalaaniwa na hata kudharauliwa na Mungu. Pengine wewe ni rais, ama mwanasayansi, ama mchungaji, ama mzee, lakini bila kujali ukuu wa ofisi yako, ukitegemea maarifa yako na uwezo katika shughuli zako, basi daima utakuwa wa kushindwa na kamwe utanyimwa baraka za Mungu, kwa sababu Mungu hakubali chochote unachofanya, na Hakubali kwamba kazi yako ni yenye haki, wala kukubali kwamba unafanya kazi kwa manufaa ya wanadamu. Atasema kwamba kila kitu unachofanya, ni kutumia maarifa na nguvu za wanadamu ili kumwondolea mwanadamu ulinzi wa Mungu, ambapo ni kukataa baraka za Mungu. Atasema kuwa unamwongoza mwanadamu kuelekea gizani, kuelekea kifo, na kuelekea mwanzo wa maisha yasiyo na mipaka ambapo mwanadamu amempoteza Mungu na baraka Zake.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 2: Mungu Ana Mamlaka Juu ya Hatima ya Wanadamu Wote

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 263)

Tangu uvumbuzi wa wanadamu wa sayansi ya kijamii, akili ya mwanadamu imechukuliwa na sayansi na maarifa. Kisha sayansi na maarifa zikawa zana za kuwatawala wanadamu, na hakuna tena nafasi ya kutosha kwa mwanadamu kumwabudu Mungu, na hakuna hali nzuri zaidi kwa kumwabudu Mungu. Nafasi ya Mungu ikashuka chini kabisa katika moyo wa mwanadamu. Bila Mungu mioyoni mwao, ulimwengu wa ndani wa mwanadamu ni giza, usio na tumaini na ni mtupu. Na hivyo kukatokea wanasayansi wa jamii, wataalamu wa historia na wanasiasa wengi kueleza nadharia ya sayansi ya jamii, nadharia ya mageuko ya binadamu, na nadharia nyingine zinazopinga ukweli kwamba Mungu alimuumba mwanadamu, ilikujaza mioyo na akili za wanadamu. Na kwa njia hii, wanaoamini kwamba Mungu aliumba kila kitu wanakuwa wachache zaidi, na wale wanaoamini nadharia ya mageuko wanakuwa hata wengi kwa nambari. Watu zaidi na zaidi wanachukulia rekodi za kazi ya Mungu na maneno Yake wakati wa enzi ya Agano la Kale kuwa hadithi na hekaya. Katika mioyo yao, watu wanakuwa wasiojali adhama na ukuu wa Mungu, wasiojali kwamba Mungu yupo, na kanuni kwamba Mungu ana ukuu juu ya vitu vyote. Kuendelea kuishi kwa wanadamu na hatima ya nchi na mataifa si muhimu tena kwao, na mwanadamu anaishi katika ulimwengu ulio mtupu unaojishughulisha tu na kula, kunywa, na kutafuta raha. … Ni watu wachache wanaojishughulisha kutafuta mahali ambapo Mungu anafanya kazi Yake leo, au kutafuta jinsi Anavyosimamia na kupanga hatima ya mwanadamu. Na kwa njia hii, bila ya mwanadamu kujua, ustaarabu wa mwanadamu unashindwa zaidi na zaidi kuendana na matakwa ya mwanadamu, na hata kuna watu wengi zaidi ambao wanahisi kwamba, kuishi katika ulimwengu kama huu, hawana furaha kuliko wale ambao tayari wamekufa. Hata watu wa nchi zilizokuwa na ustaarabu wa hali ya juu wanatoa malalamiko kama hayo. Kwani bila mwongozo wa Mungu, hata kama watawala na wanasosholojia wataumiza akili zao ili kuhifadhi ustaarabu wa mwanadamu, haitakuwa na mafanikio. Hakuna anayeweza kujaza utupu katika moyo wa mwanadamu, kwani hakuna anayeweza kuwa uzima wa mwanadamu, na hakuna nadharia ya kijamii inayoweza kumwokoa kutokana na utupu unaomtesa. Sayansi, maarifa, uhuru, demokrasia, starehe na faraja, haya yote yanamletea mwanadamu faraja ya muda tu. Pamoja na mambo haya, mwanadamu bado haepuki kutenda dhambi na kulalamika kuhusu ukosefu wa haki kwa jamii. Mambo haya hayawezi kupunguza tamaa ya mwanadamu na hamu ya kuchunguza. Kwa sababu mwanadamu aliumbwa na Mungu na kujitoa kwao na uchunguzi usio na maana wa mwanadamu vitamwongoza tu kwenye dhiki zaidi. Mwanadamu daima atakuwa katika hali ya hofu isiyoisha, hatajua jinsi ya kuukabili mustakabali wa wanadamu, ama jinsi ya kuikabili njia iliyo mbele, hadi kufikia kiwango ambacho mwanadamu hata anaogopa sayansi na maarifa, na hata zaidi anahofia hisia ya utupu iliyo ndani yake. Katika ulimwengu huu, bila kujali kama unaishi katika nchi huru ama isiyo na haki za binadamu, huwezi kabisa kuponyoka majaliwa ya mwanadamu. Kama wewe ni kiongozi ama anayeongozwa, huwezi kabisa kuponyoka hamu ya kuchunguza majaliwa, mafumbo, na hatima ya wanadamu, sembuse kuwa na uwezo wa kutoroka hisia ya utupu inayotatiza. Matukio kama haya, yaliyo kawaida kwa wanadamu wote, yanaitwa matukio ya kijamii na wanasosholojia, lakini hakuna mtu mkuu anayeweza kuja kutatua shida kama hizi. Mwanadamu, hata hivyo, ni mwanadamu. Nafasi na maisha ya Mungu hayawezi kubadilishwa na mwanadamu yeyote. Mwanadamu hahitaji tu jamii iliyo na haki, ambapo kila mtu analishwa vyema na ana uhuru na usawa, lakini wokovu wa Mungu na utoaji Wake wa uzima kwa mwanadamu. Ni pale tu mwanadamu anapopokea utoaji wa Mungu wa uzima na wokovu Wake ndipo mahitaji yao, shauku yao ya kuchunguza, na utupu wa mioyo yao utaweza kutatuliwa. Ikiwa watu wa nchi ama taifa hawawezi kupokea wokovu na utunzaji wa Mungu, basi nchi ama taifa kama hilo litatembelea njia inayoelekea uharibifuni, inayoelekea gizani, na litaangamizwa na Mungu.

Pengine nchi yako inafanikiwa kwa sasa, lakini ukiruhusu watu wako waende mbali na Mungu, basi nchi yako itazidi kujipata bila baraka za Mungu. Ustaarabu wa nchi yako utazidi kukanyagiwa chini, na kabla ya muda mrefu watu watamwasi Mungu na kuilaani Mbingu. Kwa njia hii, bila mwanadamu kujua, hatima ya nchi itaharibiwa. Mungu ataziinua nchi zenye nguvu ili kukabiliana na nchi hizo zilizolaaniwa na Mungu, na Anaweza hata kuzifuta kutoka kwa uso wa dunia. Kupanda na kushuka kwa nchi ama taifa kunategemea kama viongozi wao wanamwabudu Mungu, na kama wanawaongoza watu wao karibu na Mungu na kumwabudu. Lakini, katika enzi hii ya mwisho, kwa sababu wale wanaomtafuta na kumwabudu Mungu kwa kweli wanazidi kuwa wachache, Mungu anatoa upendeleo wa pekee kwa nchi ambazo Ukristo ni dini ya serikali. Anazikusanya nchi hizo pamoja ili kuunda kambi ya ulimwengu yenye haki, wakati nchi zisizomwamini Mungu na zile nchi ambazo hazimwabudu Mungu wa kweli zinakuwa wapinzani wa kambi hiyo ya haki. Kwa njia hii, Mungu hana tu mahali miongoni mwa wanadamu pa kufanyia kazi Yake, lakini pia Anapata nchi zinazoweza kutumia mamlaka ya haki, Akiruhusu vizuizi na vikwazo kuwekwa kwa nchi hizo zinazompinga Mungu. Lakini licha ya hayo, bado hakuna watu zaidi wanaokuja kumwabudu Mungu, kwa sababu mwanadamu amepotea mbali sana kutoka Kwake, na mwanadamu amemsahau Mungu kwa muda mrefu sana, na katika dunia hii kumebaki tu nchi ambazo zinatenda haki na kupinga udhalimu. Lakini hii ipo mbali na kufikia matakwa ya Mungu, kwa kuwa hakuna viongozi wa nchi watakaomruhusu Mungu awaongoze watu wao, na hakuna chama cha kisiasa cha nchi kitakachokusanya pamoja watu wake ili wamwabudu Mungu; Mungu amepoteza nafasi Yake inayostahili katika moyo wa kila nchi, taifa, chama tawala, na hata katika moyo wa kila mtu. Ingawa baadhi ya nguvu za haki zipo katika ulimwengu huu, utawala wowote ambao Mungu hana nafasi ndani ya moyo wa mwanadamu ni mdhaifu sana, na uwanja wa kisiasa, ambao hauna baraka za Mungu, upo katika mkanganyiko na hauwezi kustahimili hata pigo moja. Kwa wanadamu, kutokuwa na baraka za Mungu ni sawa na kutokuwa na jua. Bila kujali jinsi watawala wanavyotoa michango kwa bidii kwa watu wao, bila kujali ni mikutano mingapi ya haki ambayo wanadamu wanafanya pamoja, hakuna hata moja kati ya haya litakaloweza kugeuza wimbi hilo au kubadilisha hatima ya wanadamu. Mwanadamu anaamini kwamba nchi ambayo watu wanalishwa na kuvishwa, ambayo watu wanaishi pamoja kwa amani, ndio nchi nzuri, na yenye uongozi mzuri. Lakini Mungu hafikirii hivyo. Anaamini kuwa nchi ambayo hakuna mtu anayemwabudu ndiyo Atakayoiangamiza. Njia ya mwanadamu ya kufikiria ni tofauti kabisa na ya Mungu. Kwa hiyvo, kama mkuu wa nchi hamwabudu Mungu, basi majaliwa ya nchi hii yatakuwa mabaya sana, na nchi hii haitakuwa na hatima.

Mungu hashiriki katika siasa za mwanadamu, lakini majaliwa ya nchi ama taifa yanadhibitiwa na Mungu, Mungu anadhibiti dunia hii na ulimwengu mzima. Majaliwa ya mwanadamu na mpango wa Mungu vimeunganishwa kwa karibu, na hakuna mtu, nchi au taifa linaloweza kuepuka ukuu wa Mungu. Ikiwa mwanadamu anatamani kujua hatima yake, basi lazima aje mbele za Mungu. Mungu atawafanya wanaomfuata na kumwabudu kufanikiwa, na Atawashusha na kuwaangamiza wale wanaompinga na kumkataa.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 2: Mungu Ana Mamlaka Juu ya Hatima ya Wanadamu Wote

Maneno ya Mungu ya Kila Siku  (Dondoo 264)

Katika upana wa ulimwengu na anga, viumbe wasiohesabika wanaishi na kuzaliana, hufuata sheria ya mzunguko wa maisha na kufuata sheria isiyobadilika. Wanaokufa huenda na hadithi za walio hai, na walio hai hurudia historia hii yenye huzuni ya wale waliokufa. Na kwa hivyo wanadamu hawawezi kujizuia ila kujiuliza wenyewe; Kwa nini tunaishi? Na kwa nini inatulazimu kufa? Nani anayeitawala dunia hii? Na ni nani aliyemuumba mwanadamu huyu? Je, kweli wanadamu waliumbwa na mazingira asilia? Je, kweli wanadamu wana uamuzi juu ya hatima yao? … Kwa maelfu ya miaka wanadamu wameyauliza haya maswali, tena na tena. Kwa bahati mbaya, jinsi wanadamu wanavyopagawa na haya maswali, ndivyo kiu yao ya sayansi huendelea kukua. Sayansi hupatiana kutosheleza kwa muda na raha ya muda ya mwili, ila haitoshi kumpa mwanadamu uhuru kutokana na upweke, ukiwa, na hofu isiyodhihirika na kutosaidika ndani ya moyo wake. Wanadamu hutumia ujuzi wa kisayansi ambao wanaweza kuona kwa macho na kuelewa kwa akili yao ili kuutuliza moyo wao. Ilhali maarifa kama hayo ya kisayansi hayatoshi kuwazuia wanadamu kutafiti siri. Wanadamu hawajui kabisa Mkuu wa ulimwengu na vitu vyote ni nani, sembuse kujua mwanzo na mustakabali wa wanadamu. Wanadamu wanaishi tu, bila budi, katikati ya hii sheria. Hakuna anayeweza kuiepuka wala kuibadilisha kwani katika vitu vyote na katika mbingu kuna Mmoja kutoka milele hadi milele ambaye ni Mkuu wa kila kitu. Ni Yeye ambaye Hajawahi kuonekana na mwanadamu, ambaye wanadamu hawajawahi kumjua, ambaye wanadamu hawajawahi kuamini kuwepo Kwake, na bado ni Yeye Aliyewapulizia pumzi mababu wa wanadamu na kuwapa wanadamu uhai. Ni Yeye ndiye Huruzuku na kustawisha wanadamu kwa kuishi kwao, na huwaongoza wanadamu hadi siku ya leo. Aidha, Yeye na Yeye pekee ni wa kutegemewa na wanadamu ili kuendelea kuishi. Ni Mkuu wa kila kitu na Hutawala viumbe vyote vyenye uhai chini ya dunia. Huamrisha misimu yote minne, na ni Yeye huita upepo, jalidi, theluji na mvua. Huwapa wanadamu mwangaza wa jua na huleta machweo ya jioni. Ni Yeye Aliyeumba mbingu na ardhi, Akampa mwanadamu milima, maziwa na mito na kila kitu kilicho na uhai ndani yake. Matendo Yake yako kila mahali, nguvu Zake ziko kila mahali, busara Zake ziko kila mahali na mamlaka Yake yako kila mahali. Kila mojawapo ya hizi sheria na kanuni ni mfano mzuri wa matendo Yake, na kila mojawapo inafichua hekima na mamlaka Yake. Nani anayeweza kujiondoa kutoka kwa ukuu Wake? Na ni nani anayeweza kujitoa mwenyewe katika njia Zake? Kila kitu kinaishi chini ya uangalizi Wake, zaidi ya hayo, kila kitu huishi chini ya ukuu Wake. Matendo na nguvu Zake huwaacha wanadamu bila chaguo ila kutambua ukweli kwamba ni Yeye pekee Anayeishi na Ana ukuu juu ya kila kitu. Hakuna kitu chochote ila Yeye kinachoweza kuamuru dunia, wala kuwajibikia wanadamu bila kukoma. Bila kujali kama unaweza kutambua vitendo vya Mungu, bila kujali kama unaamini katika kuwepo kwa Mungu, hakuna shaka kuwa hatima yako inaegemea katika mipango ya Mungu, na hakuna shaka kuwa Mungu atakuwa na ukuu juu ya kila kitu. Uwepo na utawala Wake haviwezi kutabiriwa ikiwa vinatambulika na kufahamika na binadamu au la. Ni Yeye pekee Anayejua kuhusu yaliyopita ya mwanadamu, yaliyopo na yanayojiri, na Yeye pekee ndiye mwamuzi wa hatima ya wanadamu. Haijalishi kama unaukubali huu ukweli, haitachukua muda mrefu kabla mwanadamu kushuhudia haya yote kwa macho yake mwenyewe, na huu ni ukweli ambao hivi karibu Mungu Ataudhihirisha. Wanadamu huishi na hufa chini ya macho yake Mungu. Wanadamu anaishi kwa ajili ya usimamizi wa Mungu, na macho Yake yanapofumba kwa mara ya mwisho, hiyo pia ni kwa ajili ya usimamizi huo huo. Tena na tena, mwanadamu huja na kwenda, nyuma na mbele. Bila mapendeleo, yote ni sehemu ya mamlaka ya Mungu na muundo Wake. Usimamizi wa Mungu unaendelea mbele kwa kudumu; haujawahi kusimama. Atawafanya wanadamu wafahamu uwepo Wake, waamini katika mamlaka Yake, watazame matendo Yake, na warudi katika ufalme Wake. Huu ndio mpango Wake, na kazi ambayo Amekuwa akiitekeleza kwa maelfu ya miaka.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 3: Mwanadamu Anaweza tu Kuokolewa Katikati ya Usimamizi wa Mungu

Iliyotangulia: Kujua Kazi ya Mungu (II)

Inayofuata: Siri Kuhusu Biblia

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp