7 Mwili Mtakatifu wa Kiroho wa Mwenyezi Mungu Umeonekana

1 Mwenyezi Mungu! Mwili Wake mtukufu waonekana wazi wazi, mwili mtakatifu wa kiroho watokea na Yeye ndiye Mungu Mwenyewe kamili! Dunia na mwili vyote vimegeuzwa na mabadiliko Yake juu ya mlima ambaye ni nafsi ya Mungu. Amevaa taji la dhahabu kichwani, mavazi Yake ni meupe kabisa, kifuani ana ukanda wa dhahabu na vitu vyote katika dunia ni mahali pa kuweka miguu yake. Macho Yake ni kama mwale wa moto, na upanga mkali wenye makali kuwili uko ndani ya kinywa Chake na Ana nyota saba katika mkono Wake wa kuume. Njia ya kwenda kwa ufalme ni ng’avu bila kikomo na utukufu Wake watokea na kuangaza; milima huwa na furaha na maji hucheka, jua, mwezi na nyota zote zazunguka kwa mpango wao wa taratibu, ukimkaribisha Mungu wa kweli na wa kipekee, ambaye kurudi kwake kwa ushindi kunaashiria ukamilisho wa miaka elfu sita ya mpango Wake wa usimamizi.

2 Mwenyezi Mungu amekaa juu ya kiti Chake kitukufu cha enzi! Zote zaruka na kucheza kwa furaha! Shangilia! Imbeni! Bendera ya ushindi ya Mwenyezi inainuliwa juu ya mlima mwadhimu, mtukufu wa Sayuni! Mataifa yote yanashangilia, watu wote wa mataifa wanaimba, Mlima Sayuni unacheka kwa furaha, utukufu wa Mungu umetokea! Hata katika ndoto Sijawahi kufikiri kwamba Ningeuona uso wa Mungu lakini leo Nimeuona. Uso kwa uso na Yeye kila siku, nauweka wazi moyo wangu Kwake. Yeye kwa ukarimu hutoa vyote vinavyoliwa na kunywewa. Maisha, maneno, matendo, mawazo, nia—mwanga Wake mtukufu huwatia nuru wote. Yeye huongoza kila hatua ya njia, na kama moyo wowote ni muasi basi hukumu Yake itatokea mara moja.

3 Kula pamoja na Mungu, kukaa pamoja, kuishi pamoja, kuwa pamoja na Yeye, kutembea pamoja, kufurahia pamoja, kupata utukufu na baraka pamoja, kushiriki ufalme na Mungu, na kuwa pamoja katika ufalme—oo, ni furaha iliyoje! Oo, ni utamu ulioje! Uso kwa uso kila siku, kuzungumza kila siku, kuzungumza mara kwa mara, kupata nuru upya na ufahamu mpya kila siku. Macho yetu ya kiroho yanafunguliwa na tunaona kila kitu, siri zote za kiroho zinafichuliwa kwetu. Maisha matakatifu si ya kujali. Kimbia kwa haraka na usisite, songa mbele mfululizo, kuna maisha ya ajabu zaidi mbele. Usiridhike tu na ladha tamu lakini siku zote tafuta kuingia ndani ya Mungu. Yeye anajumuisha yote na mkarimu, na Ana kila aina ya vitu ambavyo tumekosa. Shirikiana kwa vitendo, ingia ndani Yake na hakuna kitu kitakachokuwa kama awali tena. Maisha yetu yatakuwa ya uvukaji mipaka na hakuna mtu, jambo, au kitu kitakachoweza kutuvuruga.

Umetoholewa kutoka katika “Sura ya 15” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 6 Mwenyezi Mungu Aonekana Kama Jua la Haki

Inayofuata: 8 Mwenyezi Mungu Atawala Kama Mfalme

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp