249 Mungu Amenipa Upendo Mwingi Sana

1

Ee Mungu! Hukumu Yako ni ya kweli kabisa, imejaa haki na utakatifu.

Ufunuo Wako kuhusu ukweli wa upotovu wa wanadamu umenifichua kabisa.

Nafikiri juu ya jinsi nilivyojitumia na kujishughulisha kwa miaka mingi ili tu kupata baraka Zako.

Nilimwiga Paulo, kufanya kazi kwa bidii, ili niweze kujitokeza kwa umati.

Maneno Yako ya hukumu yalinifanya nione jinsi nilivyokuwa mbinafsi na wa kudharauliwa.

Ninaanguka chini nikiwa na aibu na fedheha, sistahili hata kuutazama uso Wako.

Mara nyingi nimekumbuka njia ambayo nimeitembea.

Ni Wewe uliyenitunza na kunilinda, Ukiniongoza katika kila hatua ya njia hadi kufikia sasa.

Naona jinsi inavyokugharimu kuniokoa, yote ni upendo Wako.

2

Ee Mungu! Kwa kupitia hukumu Yako, nimeonja upendo Wako wa kweli.

Ni hukumu Yako ambayo huniruhusu kujijua mwenyewe na kutubu kwa kweli.

Mimi ni mpotovu sana kiasi kwamba nahitaji sana Unihukumu na kunitakasa

Bila hukumu Yako, ningetapatapa gizani tu.

Ni maneno Yako ambayo yameniongoza kwenye njia ya maisha ya nuru.

Nahisi kuwa kukupenda na kuishi kwa ajili Yako ni ufuatiliaji wa maana zaidi.

Mara nyingi sana nimekumbuka njia ambayo nimeitembea.

Hukumu Yako na kuadibu Kwako ni baraka Zako na upendo wa kweli.

Nitaelewa ukweli na kufikia mapenzi halisi zaidi Kwako. Niko tayari bila kujali nitateseka kiasi gani.

Iliyotangulia: 248 Upendo wa Kweli wa Mungu

Inayofuata: 250 Upendo wa Mungu Ni Halisi Kweli

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp