519 Kupata Ukweli Kuna Maana Gani?

1 Kuufikia ukweli kunamaanisha kuwa unaelewa mapenzi Yake kupitia katika kila neno ambalo Anasema. Mara unapoelewa, unaliweka katika vitendo. Unaishi kwa kudhihirisha neno la Mungu, na kulifanya kuwa uhalisia wako. Ni hapo tu, ndipo unaweza kusema kwamba unaufahamu ukweli kwa kweli. Ni wakati tu unapokuwa na ufahamu wa kina wa neno la Mungu ndipo unaweza kuushika ukweli kwa kweli. Neno la Mungu ni ukweli. Hata hivyo, kusoma maneno ya Mungu haimaanishi kwamba utaelewa maana yake hasa na kuupata ukweli. Kula na kunywa maneno ya Mungu ama kutakuletea ukweli au kukuletea barua na mafundisho. Hujui ni nini maana ya kuupata ukweli. Unaweza kuyashikilia maneno ya Mungu katika kiganja cha mkono wako; lakini baada ya kuyasoma, bado unashindwa kuyaelewa mapenzi ya Mungu, unapata tu barua na mafundisho kiasi.

2 Kwanza kabisa, unapaswa kutambua kwamba neno la Mungu sio halisi vile; Neno la Mungu ni lenye kina kabisa. Hata sentensi moja itahitaji maisha yako yote kuielewa kikamilifu. Unasoma maneno ya Mungu, lakini huelewi mapenzi ya Mungu; huelewi madhumuni ya maneno Yake, asili yake, matokeo yanayotafuta kutimiza, au kile yatakachotimiza. Wewe huelewi chochote kuhusu mambo haya, kwa hivyo unawezaje kuuelewa ukweli? Unaweza kuwa umepindua kurasa za kitabu mara nyingi; unaweza kuwa umekisoma mara nyingi. Labda unaweza kukariri vifungu vyake vingi kwa moyo, lakini bado hujabadilika; bado hujafanya maendeleo yoyote. Uhusiano wako na Mungu uko mbali na na wenye kufarakana kama ulivyokuwa. Bado kuna vizuizi kati yako na Mungu, kama hapo awali. Bado unaendelea kuwa na shaka Kwake. Sio tu kwamba humfahamu Mungu, lakini unampinga na hata kumkufuru. Unatoa visingizio kwa Mungu na una dhana juu Yake. Katika hali hii, unawezaje kusema kwamba umepata ukweli?

Umetoholewa kutoka katika “Ni Wale wenye Uhalisi wa Ukweli Pekee Ndio Wanaoweza Kuongoza” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 518 Kuelewa Ukweli Si Jambo Rahisi

Inayofuata: 520 Mungu Atawabariki Wale Wanaofuatilia Ukweli kwa Dhati

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp