Utambulisho wa Asili wa Mwanadamu na Thamani Yake: Je, Viko Namna Gani?
Mlitengwa kutoka kwa matope na kwa vyovyote vile, mlichaguliwa kutoka kwa mashapo, wachafu na mliochukiwa na Mungu. Mlikuwa wa Shetani na wakati mmoja mlikanyagwa na kuchafuliwa na yeye. Hii ndiyo maana inasemwa kuwa mlitengwa kutoka kwa matope, na nyinyi si watakatifu, lakini badala yake nyinyi ni vitu visivyo binadamu ambavyo Shetani kwa muda mrefu alikuwa amevifanya vipumbavu. Haya ndiyo maelezo sahihi zaidi yenu. Lazima mtambue kuwa nyinyi ni uchafu unaopatikana katika maji yaliyotuama na matope, kinyume na ushikaji unaofaa kama samaki na uduvi, kwa maana hakuna starehe inayoweza kupatikana kutoka kwenu. Kuzungumza waziwazi, nyinyi ni wanyama wa chini sana wa tabaka la chini zaidi, wanyama wabaya zaidi kuliko nguruwe na mbwa. Kusema kweli, kuwahutubia kwa maneno kama haya si kupita kiasi au kutia chumvi, bali ni njia ya kurahisisha suala hilo. Kuwahutubia kwa maneno kama haya kwa kweli ni njia ya kuwaheshimu. Utambuzi wenu, hotuba, mwenendo kama watu, na vitu yote katika maisha yenu—ikiwa ni pamoja na hali yenu katika matope—vinatosha kuthibitisha kwamba utambulisho wenu ni “wa kipekee.”