Neno la Mungu Laniongoza Kushinda Vishawishi

24/12/2019

Na Tian’na, Hong Kong

Ninapofungua kurasa za makala ya maneno ya Mungu, “Je, Ulikuwa Unajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu” sina budi kukumbuka uzoefu wangu miaka miwili iliyopita wa kuondokana na vifungo vya uvumi na kurudi mbele za Mungu.

Mimi na familia yangu sote tunaishi Hong Kong. Baba mkwe wangu na shemeji yangu (kaka mdogo wa mume wangu) wote wanamwamini Bwana Yesu. Shemeji yangu ni mchungaji kanisani, kwa hivyo ndugu kutoka kanisani mara nyingi wangekuja nyumbani kwetu kututembelea ambapo waliomba pamoja na kuimba nyimbo za kumsifu Bwana. Na kisha mnamo Desemba 2014, rafiki yangu mzuri aliniambia kuwa yeye pia alimwamini Bwana. Huku nikishawishiwa na familia na marafiki zangu, nilivutiwa kwa kiasi fulani na imani katika Bwana. Nilikutana na Dada Peipei, mshiriki mwingine wa kanisa, siku moja muda mfupi baadaye. Alikuwa mpole na mwema. Alifurahi sana alipogundua kuwa baadhi ya familia na marafiki zangu walimwamini Bwana na akanialika nimtembelee nyumbani kwake, ambako alinitambulisha kwa Dada Chen Hui. Katika kipindi cha mikutano kadhaa, Dada Chen alishiriki nami ukweli kuhusu Mungu kuumba vitu vyote na ukuu Wake juu ya kila kitu na pia asili ya Shetani, na kadhalika. Mambo ambayo aliniambia yalinivutia sana na kuniacha nikihisi furaha sana. Nilipenda sana kuwasikiza wakishiriki uzoefu na ufahamu wao kuhusu imani, na nilitaka sana kushiriki furaha hii na wengine. Siku moja, huku nikishindwa kujizuia, nilishiriki na familia yangu shauku yangu ya kuwa muumini. Habari hiyo ilienea haraka kwa shemeji yangu; alipiga simu na kuuliza ni kwa nini nilimwamini Mungu ghafla na akasema pia, “Kuna kanisa linaloitwa Umeme wa Mashariki, na wako kila mahali wakishuhudia kwamba Bwana Yesu tayari amerudi. Wameiba watafutaji wengi waliojitolea kwa dhati kutoka katika kila dhehebu. Usikose kutilia jambo hilo maanani; usijihusishe nao.” Kisha akaniuliza tena na tena iwapo watu wanaoshiriki injili pamoja nami walikuwa wamenipa kitabu, na akanisihi mara kadhaa niwe mwangalifu zaidi kuhusiana na chochote kinachohusiana na imani. Maneno ya shemeji yangu yalizidi kuzungukazunguka kichwani mwangu, yakiniacha nikihisi wasiwasi. Kwa upande mmoja, shemeji yangu alipinga mimi kutafuta kanisa lingine, lakini kwa upande mwingine, nilifurahia sana kile ambacho Dada Chen alikuwa nacho cha kusema kuhusu kuamini katika Mungu. Sikujua cha kufanya, na sikujua iwapo nilipaswa kuendelea kuwasiliana na Dada Chen.

Kwa hivyo, nilianza kutafuta mtandaoni mahubiri ya wachungaji ili niyasikilize. Niliona habari nyingi mtandaoni kuhusu Umeme wa Mashariki, lakini sikuzitilia maanani sana; nililenga kabisa kupata mahubiri mazuri. Nilisikiliza na kulinganisha mahubiri mengi na mwishowe, nilidhani kwamba mahubiri ya Dada Chen na ya wale wengine yalikuwa bora zaidi, kwa sababu yalishiriki zaidi juu ya kumshuhudia Mungu, na kuyasikiliza kulinipa ufahamu mzuri zaidi kuhusu Mungu. Baada ya kufikiria juu yake kiasi, niliamua kuendelea kusikiliza ushirika wa Dada Chen. Katika siku zilizofuata, aliniambia hadithi za Musa kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri, Abrahamu kumtoa Isaka, Bwana Yesu kusulubishwa kwa ajili ya wanadamu, uzoefu wa Petro, Lazaro kufufuliwa na kumtukuza Mungu, na zaidi. Hadithi hizi nzuri za Biblia zilinivutia sana na zilinipa ufahamu wa kina kuhusu kazi ambayo Mungu amefanya. Kila baada ya mkutano nilingojea uliofuata kwa hamu.

Mwezi mmoja baadaye wakati wa mkutano, Dada Chen alinisomea vifungu kadhaa vya Biblia na kifungu cha maneno ya Mwenyezi Mungu. Katika Biblia inasema: “Lakini kama jinsi zilivyokuwa zile siku za Nuhu, ndivyo pia kuja kwa Mwana wa Adamu kutakuwa. Kwani kama katika zile siku kabla ya gharika walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, hadi siku ambapo Nuhu aliingia katika safina, Na hawakujua hadi gharika ilipokuja, na kuwachukua wote; ndivyo itakavyokuwa pia kuja kwa Mwana wa Adamu(Mathayo 24:37–39). Mwenyezi Mungu asema, “Angalia nyuma wakati wa safina ya Nuhu: Wanadamu walikuwa wapotovu sana, walikuwa wamepotea kutoka katika baraka za Mungu, hawakuwa wanatunzwa na Mungu tena, na walikuwa wamepoteza ahadi za Mungu. Waliishi gizani, bila mwangaza wa Mungu. Hivyo wakawa waasherati kwa asili, wakajiachilia katika mkengeuko wa kutisha. Watu kama hao hawangeweza tena kupokea ahadi za Mungu; hawakufaa kushuhudia uso wa Mungu, wala kusikia sauti ya Mungu, kwani walikuwa wamemwacha Mungu, kuweka kando yote Aliyowapa, na kusahau mafunzo ya Mungu. Mioyo yao ilipotea mbali zaidi na zaidi na Mungu, na ilivyofanya hivyo, wakawa wapotovu zaidi ya mantiki na ubinadamu wote na wakazidi kuwa waovu. Hivyo walikaribia kifo zaidi, na kukabiliwa na ghadhabu na adhabu ya Mungu. Ni Nuhu tu aliyemwabudu Mungu na kuepukana na uovu, na hivyo aliweza kusikia sauti ya Mungu, na kusikia maelekezo ya Mungu. Alijenga safina kulingana na maelekezo ya neno la Mungu, na kukusanya aina yote ya viumbe hai. Na kwa njia hii, wakati kila kitu kilikuwa kimetayarishwa, Mungu aliangamiza dunia. Nuhu tu na wanachama saba wa familia yake walinusurika maangamizi, kwani Nuhu alimwabudu Yehova na kuepukana na uovu.

Kisha angalia enzi ya sasa: Hawa watu wenye haki kama Nuhu, ambao wangeweza kumwabudu Mungu na kuepuka uovu, wamekoma kuwepo. Lakini bado Mungu ana fadhili kwa mwanadamu huyu, na Anamsamehe mwanadamu wakati huu wa enzi ya mwisho. Mungu anawatafuta wanaomtaka Yeye ajitokeze. Anawatafuta wale wanaoweza kuyasikia maneno Yake, wale ambao hawajasahau agizo Lake na wanatoa mioyo na miili yao Kwake. Anawatafuta wale walio watiifu kama watoto wachanga mbele Yake, na hawampingi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 2: Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote). Dada Chen alisema katika ushirika wake: “Watu wa siku za Nuhu walikuwa ‘wakila na kunywa, kuoa na kuolewa’; walikuwa wazinzi na wapotovu, na hawakusikiza neno la Mungu wala kumwabudu Mungu. Badala yake, waliabudu sanamu na walikuwa wenye dhambi kupita kiasi. Ili kuwaokoa watu wa wakati huo, Mungu alimwagiza Nuhu ajenge safina na awaambie watu kwamba mafuriko yatauharibu ulimwengu. Lakini hata baada ya Nuhu kuhubiri jambo hili kwa zaidi ya miaka mia moja, hakuna mtu aliyeamini maneno ya Mungu na hakuna mtu aliyetubu kwa Mungu. Kwa hivyo, Mungu alitumia gharika kuu kuwaangamiza watu wa wakati huo. Watu wa siku za mwisho ni wapotovu hata zaidi kuliko watu wa wakati wa Nuhu. Jamii nzima imekosa maadili na inazidi kukengeuka kila siku. Kiwango cha talaka kinasalia kuwa cha juu, uhalifu ni jambo la kawaida, pamoja na ponografia, kamari na dawa za kulevya zimepotosha roho za watu. Watu wanazidi kuwa wajanja, wachoyo, waovu, wenye hila na wabinafsi. Hakuna anayejali kuwa na dhamiri au kuwa mtu mzuri na mwaminifu, lakini wanatilia maanani kula, kunywa, na kustarehe, na kubadili mamlaka na ngono, au ngono na mamlaka. Watu wamechoshwa na ukweli na wanatukuza uovu. Wanatamani furaha ya kutenda dhambi, na kwa muda mrefu wamefikia kiwango ambacho kinastahili maangamizo na Mungu. Ishara hizi zote zinaonyesha kuwa siku za mwisho zimewadia. Sasa Bwana Yesu amerudi na mwili Wake wa pili unaishi ulimwenguni. Amenena ukweli wote kwa ajili ya utakaso na wokovu wa wanadamu; Amekuja kutuokoa kabisa, sisi watu wapotovu sana. Upendo na huruma za Mungu kwa wanadamu ni kubwa sana!” Kumsikia dada huyo akisema maneno haya kulinifurahisha na nilijiwazia: “Sisi sote ni watu waovu sana na tulipaswa kuangamizwa na Mungu zamani. Ni kwa msaada tu wa huruma za Mungu kwamba tuna bahati ya kuja ndani ya nyumba ya Mungu, kusoma maneno ambayo Mungu amenena, na kupata nafasi ya kumjua Mungu. Baraka kubwa iliyoje!” Nilimshukuru Mungu tena na tena kwa kuniongoza na kuniruhusu nijue kazi ya Mungu ya siku za mwisho na kupata fursa ya wokovu. Nilipokuwa tu karibu kuondoka, dada huyo alinipa kitabu cha maneno ya Mungu. Huku nikishika kitabu hicho kwa mikono yote miwili, niliguswa sana kiasi kwamba nilianza kulia. Niliamua kumfuata Mungu kadiri ya uwezo wangu.

Siku moja baada ya kuwasha kompyuta yangu, niliona tovuti ambayo ilisema jambo kuhusu Umeme wa Mashariki. Huku nikisukumwa na udadisi, nilibofya kwenye kiungo na nikaona propaganda mbaya kuhusu Umeme wa Mashariki kutoka kwa serikali ya CCP na jumuia ya dini. Nilipogundua kuwa “Umeme wa Mashariki” lililotajwa kwenye tovuti hiyo lilikuwa kazi ya Mwenyezi Mungu ambayo Dada Chen alikuwa amenihubiria, nilishtuka na nikahisi wasiwasi sana: Yawezekana kwamba nilikuwa nimepotea katika imani yangu? Napaswa kufanya nini? Hata hivyo, nilikumbuka jinsi kila nilipowasiliana na Dada Chen na wale wengine, wote walikuwa wenye upendo sana kwangu na hawakuwa kama ilivyosemwa mtandaoni. Nilikumbuka nilipoanza kusoma neno la Mungu na niliguswa na upendo wa Mungu—maneno hayo yalikuwa na mamlaka na nguvu, kwa hivyo yangewezaje kutokuwa maonyesho na sauti ya Mungu? Kisha nilitoa maneno ya Mungu kwa kusudi la kuyasoma, lakini sikuweza kupata tena hisia za kuguswa ambazo nilikuwa nazo mwanzoni—Mungu alikuwa amenifichia uso Wake. Niliyoweza tu kuona ni karatasi nyeupe na maneno meusi. Kila propaganda hasi niliyokuwa nimeona mtandaoni ilinijia ghafla akilini mwangu moja moja. Sikujua la kufanya. Niliendelea kujiuliza: “Je, napaswa kuamini haya, au la? Je, Umeme wa Mashariki ni kazi ya Mungu? Na ikiwa Umeme wa Mashariki kwa kweli ni kazi ya Mungu? Nisipotenda imani hii, si nitapoteza tu nafasi yangu ya kumjua Mungu na kuokolewa? Lakini iwapo ni bandia na niifuate tu bila kufikiria, si hiyo itamaanisha kwamba nimedanganywa? Napaswa kuendelea kuichunguza au la?” Maswali haya yaliendelea kunisumbua na hata yaliniacha bila tamaa ya kufanya kazi. Nilitaka sana kujadili jambo hilo na familia yangu na kuwaomba ushauri, lakini nilifikiria jinsi shemeji yangu alivyonisihi mara kwa mara juu ya kutahadhari, na kwamba nisizunguke tu nikitafuta makanisa mengine. Ikiwa kwa kweli imani yangu ilikuwa na makosa, si wangenikemea zaidi? Kwa hivyo, nilitupilia mbali wazo la kulijadili na familia yangu ingawa hali yangu ya akili ilikuwa katika kiwango cha chini kabisa, nilikuwa katika uchungu mwingi wa kihisia, na nilichanganyikiwa sana. Nilihisi kutokuwa kabisa na furaha na amani niliyohisi siku chache kabla ya kushirikiana na dada.

Bila mahali pa kugeukia, nilijaribu kumwomba na kumtafuta Mungu, kumwaminia Mungu kila ugumu na wahaka uliokuwa moyoni mwangu, na kuomba sana nuru Yake. Baada ya kusali, nilikumbuka ghafla kitu ambacho Dada Chen aliniambia wakati mmoja: Bwana Yesu alipozaliwa, kwa sababu Mfalme Herode aliogopa kupoteza ufalme wake wakati huo, aliamuru wavulana wote katika jiji lote ambao walikuwa chini ya umri ya miaka miwili wauawe. Bwana Yesu aliposhiriki mafundisho Yake, viongozi wa dini ya Kiyahudi walitangaza msimamo dhidi Yake na kumshutumu kwa hasira kwa sababu waliogopa kwamba waumini wangemfuata Bwana Yesu, na kwamba wangepoteza hadhi zao. Walijua vizuri kuwa hakuna mtu wa kawaida ambaye angeweza kufanya miujiza ambayo Bwana Yesu alifanya, lakini walimkashifu kimakusudi, wakisema kwamba Alikuwa akitoa pepo kwa msaada wa Beelzebuli. Pia walimshutumu Bwana Yesu kwa kukufuru. Mwishowe, walishirikiana na serikali ya Kirumi ili kumsulubisha Bwana Yesu. Na siku hizi, matendo ya serikali ya CCP na jumuia ya dini ya kumlaani Mwenyezi Mungu kwa hasira ni sawa kabisa na yale yaliyofanywa na serikali ya Roma na viongozi wa Uyahudi katika Enzi ya Neema dhidi ya Bwana Yesu. Njia ya kweli imepatwa na ukandamizaji tangu nyakati za zamani. Kila wakati Mungu anapokuja kufanya kazi, Yeye hupitia mateso kutoka kwa ulimwengu wa dini pamoja na mamlaka yaliyomo. Hata hivyo, hakuna mtu anayeweza kuzuia kazi ya Mungu. Mwishowe, Bwana Yesu bado alimaliza kazi ya kusulubishwa na kuwaokoa wanadamu na injili Yake ilienea ulimwenguni kote. Na siku hizi, serikali ya China na jumuia ya dini imebuni uvumi mwingi sana mtandaoni ambao unamlaani Mwenyezi Mungu na kazi Yake, lakini injili Yake ya ufalme bado imeenea haraka. Hii isingekuwa kazi ya Mungu, isingeondolewa na serikali ya China hapo zamani? Kisha wazo lilinijia akilini kuwa kila wakati nilipokuwa nimekutana na Dada Chen na wengine, wote walikuwa wakweli kwangu, na ushirika wao wote ulimtukuza Mungu na ulimshuhudia Mungu. Hawakuwahi kuzungumza juu ya mambo ya dunia au juu ya mambo ambayo hayana faida kwa maisha ya watu. Yote yalikuwa yametoa mwongozo mzuri na msaada kwangu. Baada ya muda mfupi, shaka zilizokuwa moyoni mwangu ziliondolewa kwa kiasi fulani, hivyo nilimwomba Mungu tena kwa moyo wa kutafuta: “Mungu! Ikiwa kwa kweli ni Wewe ambaye Umerudi, tafadhali niongoze nijue kazi Yako na kurudi mbele Yako.” Bila shaka, Mungu alisikia maombi yangu.

Chini ya mwongozo wa Roho Mtakatifu, nilifungua kitabu cha maneno ya Mungu, Neno Laonekana katika Mwili na nikaona makala haya, “Je, Ulikuwa Unajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu” ambapo Mwenyezi Mungu alisema, “Mnapaswa kujua kwamba bila kuwepo kwa mwili huu, wanadamu wote wangetazamia msiba usioepukika na kupata kuwa ngumu kuponyoka adhabu kali zaidi ya Mungu katika siku za mwisho. Bila kuzaliwa kwa mwili huu wa kawaida, nyinyi nyote mngekuwa katika hali ambayo uhai wala kifo havitakuja bila kujali jinsi mtakavyovitafuta; bila kuwepo kwa mwili huu, basi siku hii hamngeweza kupokea ukweli na kuja mbele ya kiti cha Mungu cha enzi. Badala yake, mngeadhibiwa na Mungu kwa sababu ya dhambi zenu zinazohuzunisha. Je, mnajua? Kama sio kwa kurudi kwa Mungu kwa mwili, hakuna ambaye angepata nafasi ya wokovu; na isipokuwa kwa kuja kwa mwili huu, Mungu angekuwa ameimaliza kitambo enzi ya zamani. Hivyo basi, mnaweza bado kuukataa kupata mwili kwa mara ya pili kwa Mungu? Sababu mnaweza kufaidika sana kutoka kwa huyu mwanadamu wa kawaida, basi mbona hamumkubali kwa urahisi?” “Kazi ya Mungu ni ile usiyoweza kuelewa. Kama huwezi kufahamu kama uamuzi wako ni sahihi wala kujua kama kazi ya Mungu inaweza kufaulu, basi mbona usijaribu bahati yako na kuona iwapo huyu mwanadamu wa kawaida ni wa msaada mkubwa kwako, na iwapo Mungu amefanya kazi kubwa.” Shukrani ziwe kwa Mungu! Nilihisi mtulivu zaidi baada ya kusoma maneno ya Mungu—yalikuwa sahihi kabisa! Niligundua kwamba kwa kuwa sikuifahamu vyema kazi ya Mungu na sikuweza kuelewa kikamilifu mambo hayo yaliyokuwa mtandaoni, mbona nisijaribu bahati yangu? Mbona nisiendelee kwenda ndani zaidi katika uchunguzi wangu na kisha nifikie uamuzi? Ikiwa kweli ni kuonekana kwa Mungu na kazi Yake, basi nikikataa, si huko ni kumkataa Mungu? Si hayo yatakuwa majuto ya maisha? Niliamua kwenda kumwona Dada Chen siku iliyofuata na kuendelea na utafutaji na uchunguzi wangu.

Nilipomwona Dada Chen nilishiriki uzoefu wangu katika siku chache zilizopita na nikamuuliza kilichokuwa kikiendelea kwa kweli na Umeme wa Mashariki. Alinisomea vifungu viwili vya maneno ya Mungu: “Watu wote wanapotilia maanani, wakati vitu vyote vinafanywa upya na kuhuishwa, wakati kila mtu anamtii Mungu bila shaka, na yuko tayari kubeba jukumu zito la mzigo wa Mungu—hapa ndipo wakati umeme wa mashariki unatoka, ukiangaza yote kutoka Mashariki hadi Magharibi, ukiyatisha yote ya ulimwengu na ujaji wa mwanga huu; na wakati huu, Mungu tena huanza maisha Yake mapya. … Ambayo ni kusema, katika Mashariki ya dunia, kutoka wakati ushuhuda kwa Mungu Mwenyewe huanza, hadi wakati Yeye huanza kufanya kazi, mpaka wakati uungu huanza kushika madaraka makuu pande zote duniani—huu ni mwale unaong’aa wa umeme wa mashariki, ambao daima umemulika kwa ulimwengu mzima. Wakati ambapo nchi duniani zinakuwa ulimwengu wa Kristo ndio wakati ambapo ulimwengu mzima unatiwa nuru. Sasa ndio wakati ambapo umeme wa mashariki unatoka: Mungu mwenye mwili Anaanza kufanya kazi, na, zaidi ya hayo, Anaongea moja kwa moja katika uungu. Inaweza kusemwa kwamba Mungu anapoanza kuongea duniani ni wakati ambapo umeme wa mashariki unatoka. Kwa usahihi zaidi, wakati ambapo maji ya uhai yanatiririka kutoka katika kiti cha enzi—wakati ambapo matamshi kutoka katika kiti cha enzi huanza—bila shaka ni wakati ambapo matamshi ya Roho saba huanza kirasmi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ufafanuzi wa Mafumbo ya “Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima”, Sura ya 12). “Wakati nuru ya Mashariki inapong’aa polepole tu ndipo giza kote duniani litaanza kugeuka na kuwa nuru, na hapo tu ndipo mwanadamu atatambua kwamba Nilishatoka Israeli zamani na Nimeanza kuchomoza upya Mashariki. Niliwahi kushuka Israeli na baadaye Niliondoka kutoka huko, Siwezi tena kuzaliwa Israeli kwa mara nyingine, kwa kuwa kazi Yangu inauongoza ulimwengu mzima na, zaidi ya hilo, umeme unamulika moja kwa moja kutoka Mashariki kwenda Magharibi. Hii ndiyo sababu Nimeshuka Mashariki na kuwaletea watu wa Mashariki Kanaani. Ningependa kuwaleta watu kutoka dunia nzima waje katika nchi ya Kanaani, na kwa hiyo Naendelea kutoa maneno Yangu katika nchi ya Kanaani ili kuudhibiti ulimwengu mzima. Kwa wakati huu, hakuna nuru katika dunia nzima isipokuwa katika Kanaani, na watu wote wamehatarishwa na njaa na baridi. Niliipa Israeli utukufu Wangu kisha Nikauchukua na baadaye Nikawaleta Waisraeli Mashariki, na vilevile binadamu wote Mashariki. Nimewaleta wote kwenye nuru ili waweze kuungana tena nayo, na kushirikiana na nuru, na wasilazimike kuitafuta tena. Nitawaacha wote wanaotafuta waione nuru tena na kuuona utukufu Niliokuwa nao katika Israeli; Nitawaacha waone kwamba tayari Nimeshuka juu ya wingu jeupe miongoni mwa wanadamu, kuwaacha waone mawingu mengi meupe na vishada vingi vya matunda, na, zaidi ya hayo, Nitawaacha wamwone Yehova Mungu wa Israeli. Nitawaacha waone Mkuu wa Wayahudi, Masihi aliyengojewa kwa hamu, na kuonekana kamili kwa Mimi niliyeteswa na wafalme kotekote katika enzi. Nitafanya kazi katika ulimwengu mzima na Nitatekeleza kazi kubwa, Nikifichua utukufu Wangu wote na matendo Yangu yote kwa mwanadamu katika siku za mwisho. Nitaonyesha uso Wangu uliojaa utukufu kwa wale ambao wameningoja kwa miaka mingi, kwa wale ambao wametamani kuniona Nikija juu ya wingu jeupe, kwa Israeli ambayo imengoja Nionekane kwa mara nyingine, na kwa wanadamu wote wanaonitesa, ili wote wajue kwamba Niliuchukua utukufu Wangu zamani na kuuleta Mashariki, Ili usiwe katika Uyahudi tena. Kwani siku za mwisho tayari zimewadia!(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni).

Kisha akashiriki hili katika ushirika: “Tunaweza kuona kutoka katika maneno ya Mungu kwamba kazi na maneno ya Mungu katika siku za mwisho ni umeme unaotokea Mashariki. Jina ‘Umeme’ linamaanisha mwanga, na ‘mwanga’ linamaanisha maneno ya Mungu; yaani, kurudi kwa Mungu katika siku za mwisho ni kupata mwili Kwake kama Mwana wa Adamu, Akionekana na kufanya kazi kwanza katika Mashariki, nchini China, Akinena maneno na kufanyiza kundi la washindi. Na kisha injili Yake ya siku za mwisho inaenea haraka kwenda Magharibi, ili watu wote ulimwenguni kote waweze kupata wokovu wa Mungu wa siku za mwisho. Hii inatimiza yaliyosemwa katika Mathayo 24: 27: ‘Kwa kuwa kama umeme unavyotokea mashariki, na kumulika pia magharibi; ujio wa Mwana wa Adamu utakawa hivyo pia.’ Aidha, wakati wa Mungu wa kufanya kazi katika siku za mwisho ni mfupi na unakwenda haraka, kama umeme tu. Kwa zaidi ya miongo miwili mifupi, injili ya Mungu ya ufalme tayari imeenea kote bara China na inaenea katika nchi kote ulimwenguni. Umeme wa Mashariki ni neno la Mungu na kazi ya siku za mwisho, ukweli ulioonyeshwa na Mungu. Mwenyezi Mungu ni Mwana wa Adamu ambaye anaonekana mbele ya mwanadamu katika siku za mwisho, kama ilivyotabiriwa katika Biblia; Anatekeleza kazi mpya katika siku za mwisho. Wote ambao hawakubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho wataondolewa na kazi ya Roho Mtakatifu.” Niliposikia haya tu ndipo niligundua kuwa Umeme wa Mashariki unarejelea kazi ya Mungu, unarejelea ukweli ulioonyeshwa na Mungu, na ni kuonekana kwa Mungu katika siku za mwisho! Mungu alionekana kwanza na akaanza kufanya kazi nchini China, mamlaka ya kisiasa yanayomkana Mungu. Kwanza Alishinda na kulikamilisha kundi la watu wakawa washindi nchini China, na kisha Akaeneza jambo hili hadi Magharibi na hata ulimwenguni kote, ili watu wateule wa Mungu kutoka mataifa yote na maeneo yote waweze kukubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho na kupata utakaso na wokovu wa Mungu, Akifanikisha kikamilifu mpango wa Mungu wa usimamizi wa miaka elfu sita. Si huu ni udhihirisho wa hekima Yake? Mungu Mwenyewe asingeyanena maneno ili kufunua siri hizi, nisingeweza kuelewa kamwe!

Dada Chen aliendelea na ushirika wake: “Hata hivyo, viongozi wa madhehebu yote walipokabiliwa na kuonekana kwa Mungu na kazi ya Yake, sio tu kwamba walishindwa kutafuta na kuchunguza, lakini walimshutumu, wakampinga na kumkufuru Mungu vikali; walieneza uvumi waziwazi kuliharibia jina Kanisa la Mwenyezi Mungu na waliungana na serikali ya CCP imkanayo Mungu ili kuwaonea, kuwakamata na kuwatesa wale wanaomfuata Mwenyezi Mungu ili kujaribu kuzuia injili ya Mwenyezi Mungu ya ufalme isienee, kuiharibu kazi ya Mungu ya siku za mwisho na kuwazuia waumini kumrudia Mwenyezi Mungu. Kama tu serikali ya Warumi na viongozi wa Kiyahudi ambao walimpinga, kumshutumu na kumsulubisha Bwana Yesu, wote ni pepo wa kishetani wanaochukia ukweli, kumchukia Mungu, na ni maadui wa Mungu. Wanajua kuwa maneno yote yaliyosemwa na Mwenyezi Mungu ni ukweli na kwamba yana mamlaka na nguvu. Mara maneno haya yatakapoenea ulimwenguni, wote wanaopenda ukweli na kuonea kiu kuonekana kwa Mungu watamgeukia Mwenyezi Mungu na kumwabudu. Kisha, hakuna mtu atakayeendelea kuwafuata. Kwa hivyo, sasa kwa kuwa Mungu amepata tena mwili ili kufanya kazi ya kuwaokoa wanadamu, serikali inayomkana Mungu ya CCP na nguvu za mpinga Kristo za jumuia ya dini zinajaribu sana kuizuia na kuiharibu kazi ya Mungu. Wanatumia kila aina ya njia zinazostahili dharau kuwafunga na kuwadanganya watu, ili kuwazuia wasitafute na kuichunguza njia ya kweli. Ni kama tu wewe kukuza mashaka juu ya kazi ya Mungu baada ya kuona uvumi huo mtandaoni—lengo la Shetani ni kutufanya tumshuku Mungu. Anataka tumkane na kumsaliti Mungu, tupoteze wokovu Wake na kurudi chini ya utawala wake, ili afikie lengo lake baya la kuwadhibiti na kuwadhuru watu kabisa. Kama maneno ya Mungu yanavyofichua: ‘Mungu anafanya kazi, Mungu anamtunza mtu, anamwangalia mtu, na Shetani anafuata hatua Yake yote. Yeyote anayefadhiliwa na Mungu, Shetani pia anatazama, akifuata nyuma. Iwapo Mungu anamtaka mtu huyu, Shetani atafanya kila kitu kwa uwezo wake kumzuia Mungu, akitumia mbinu mbalimbali mbovu kujaribu, kusumbua na kuharibu kazi anayofanya Mungu ili kufikia lengo lake lililofichwa. Lengo lake ni nini? Hataki Mungu awe na mtu yeyote; anataka wale wote ambao Mungu anataka, kuwamiliki, kuwatawala, kuwaelekeza ili wamwabudu, ili watende maovu pamoja naye. Je, hii siyo nia ya husuda ya Shetani?(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IV). Tunapaswa kung’amua udanganyifu wa Shetani kulingana na maneno ya Mungu; tunapaswa kuona waziwazi asili mbaya ya Shetani ya kuwa adui wa Mungu na kuwazuia watu kumrudia Mungu. Tunapaswa kuona nia yake mbaya ya kuwamiliki na kuwameza watu wazima, ili tusikose nafasi ya kuokolewa na Mungu.” Kupitia kusoma maneno ya Mungu na kusikiliza ushirika wa dada huyo, nilielewa kwa kweli kwamba uvumi wote huo uliopo mtandaoni ulikuwa umetoka kwa Shetani. Niliona kuwa ni vishawishi na hila ambazo Shetani ameweka ili kuwazuia watu wasichunguze njia ya kweli na kumrudia Mungu. Iwapo ningekosa utambuzi juu yake, basi ningetekwa nyara na Shetani. Ushirika wa dada huyo ulinipa ufahamu wa kweli kuhusu Umeme wa Mashariki, kwamba ni kuonakena kwa Mungu na kazi Yake. Sasa nina utambuzi juu mbinu zinazostahili dharau ambazo nguvu za kishetani za serikali ya CCP na jumuia ya dini zinatumia kumshambulia Mungu; pia nimeona kuwa njia ya kweli imekuwa ikikandamizwa tangu nyakati za zamani. Jambo la kushangaza ni kwamba, vurugu la Shetani lilinipa ufahamu mkubwa zaidi kuhusu kazi ya Mungu na pia liliniwezesha kupata utambuzi wa kweli kuhusu Shetani, na kumkataa. Kwa kweli hekima ya Mungu inatekelezwa kwa kutegemezwa kwa mbinu za Shetani. Shukrani ziwe kwa Mungu!

Nilipofika nyumbani nilianza kutazama video za Kanisa la Mwenyezi Mungu mtandaoni. Nilitazama mfululizo wa video kumi za kwaya kwa kufuatanisha na vile vile masimulizi ya maneno ya Mungu na filamu kadhaa za injili. Kila kitu kilichoelezwa na video na filamu hizi zote kilikuwa ukweli na walichoshuhudia ni kuonekana kwa Mungu na kazi Yake ya siku za mwisho. Ziliniruhusu nione uhalisi na uzuri wa Mungu, na kupata maarifa kiasi kuhusu tabia ya Mungu yenye haki. Kuona kwamba maneno yote yaliyonenwa na Mwenyezi Mungu ni ukweli na kwamba yanaweza kuwabadilisha, kuwasafisha na kuwaokoa watu kwa kweli kuliniruhusu nipate njia ya ufalme wa mbinguni—kulinipa tumaini la wokovu. Shemeji yangu alipopata habari kwamba nilikuwa nimekubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, alikuja mara kadhaa kunigombeza, na hata aliwakusanya watu kadhaa kanisani ili wafanye hivyo pia. Pia alikariri habari nyingi hasi kutoka mtandaoni ili kujaribu kunikanganya na kunifanya niache imani yangu katika Mwenyezi Mungu. Hata hivyo, nilikuwa na hakika kabisa kuhusu kazi ya Mwenyezi Mungu na uvumi huo haukuwa na athari kwangu. Ninapokumbuka yaliyopita, ni mwongozo wa Mungu ambao kwa kweli uliniruhusu nielewe baadhi ya ukweli; nilijitenga na pingu na vifungo vya uvumi hatua kwa hatua na kuanzisha msingi juu ya njia ya kweli. Shukrani ziwe kwa Mungu kwa wokovu na ulinzi Wake kwangu, na kwa kunielekeza kuingia katika nyumba ya Mungu!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Kuwa katika Hatari Kubwa

Nilikubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho zaidi ya mwezi mmoja uliopita. Mchungaji na wazee hawajaacha kunisumbua na kuwashawishi...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp