Kupata Ahueni kwa Njia ya Kumwamini Mungu

14/01/2018

Zhuanbian Mji wa Shanghai

Ingawa nilikuwa nikimfuata Mungu kwa miaka mingi, nilikuwa karibu sijafanya maendeleo yoyote na kuingia kwangu katika maisha, na hii ilinifanya nihisi kuwa na wasiwasi sana. Hasa wakati niliposikia rekodi ya mahubiri juu ya kuingia kwa maisha, na kusikia mtu aliyetumiwa na Roho Mtakatifu akizungumza na ndugu wa kiume na wa, nilihisi nikiwa nimejawa na wasiwasi nikimsikia akisema jambo kama hili, “Nyinyi sasa mnamwamini Mungu na mmeonja uzuri wa ukimbizaji wa ukweli. Nyinyi mmeanza kuingia kwa njia sahihi na mmejaa imani katika ukimbizaji wenu wa wokovu.” Nikawaza, “Watu hawa wamemwamini Mungu kwa muda mfupi sana lakini wameingia tayari na wamejaa imani sana kuhusu kuokolewa. Na bado niko hapa nikiwa nimemwamini Mungu hadi sasa na bado sijaipata ukweli na tabia yangu katika maisha haijapitia mabadiliko yoyote kamwe, bila kujali kuwa nilikuwa nimeingia kwa njia sahihi. Ni rahisi kuongelea kufikia wokovu kuliko kukuweka katika vitendo!” Niliwaza jinsi hao wa hapo juu walifanya ushirika kwamba ukweli ungeweza kutatua upotovu wote wa wanadamu, lakini sikuwa nimepitia jambo hili kamwe. Hata nilihisi kwamba ukweli ungeweza kutatua upotovu wa watu wengine lakini sio wangu mwenyewe, kwa hiyo nilipoteza imani katika ukimbizaji wangu wa ukweli na wa wokovu. Ingawa nilikuwa na ufahamu kwamba hali yangu mwenyewe haikuwa sahihi, hapakuwa na njia yoyote ambayo ningeweza kuiepuka, hivyo ningeweza tu kumlilia Mungu kwa msaada. Baadaye, maneno Yake yalinipatia nuru, yakinifanya nione ni kwa nini nilikuwa nimemwamini Mungu kwa miaka mingi hivyo na bado sikuwa nimeendelea katika maisha, na kwa nini hali yangu haikuwa imepitia mabadiliko yoyote. Mungu pia aliniweka kwa njia ya kutenda na kuingia katika ukweli.

Maneno ya Mungu yanasema: “Ukuaji katika maisha ya mwanadamu na mabadiliko katika tabia zake hupatikana kwa kuingia ndani ya ukweli na, zaidi ya hili, kwa kuingia katika uzoefu wa kina(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Tofauti Kati ya Huduma ya Mungu Mwenye Mwili na Wajibu wa Mwanadamu). “Iwapo utalenga tu ujuzi katika nadharia na kuishi tu katika sherehe za dini bila ya kuingia ndani ya uhalisi, bila kuingia kwenye maisha halisi, basi hutaweza kamwe kuingia katika uhalisi, hutaweza kujijua mwenyewe, kuujua ukweli, au kumjua Mungu, na utakuwa kipofu na mjinga milele(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kujadili Maisha ya Kanisa na Maisha Halisi). Ni kwa njia ya kupatiwa nuru na maneno ya Mungu tu nilipoona kwamba tabia yangu haikuwa imepitia mabadiliko yoyote licha ya miaka mingi niliyokuwa nimemwamini Yeye, na kwamba hii ilikuwa hasa kwa sababu wakati niliposoma maneno ya Mungu nilizingatia tu kuelewa maana halisi, maana ya nadharia, na nilikuwa na ufahamu wa kufikiria tu. Sikuwa nazingatia kuweka ukweli katika matendo au kuingia katika uhalisi, wala sikuwa nikizingatia kupitia maneno ya Mungu kwa njia ya uzoefu wa kiutendaji. Kufikiria nyuma kwa miaka hii ya imani yangu kwa Mungu, bila kujali ni kipengele gani cha ukweli, sikuwahi kamwe kutafuta kuwa na ufahamu wa kina zaidi kuuhusu au kupata ufahamu wa kiini cha ukweli, sembuse mimi kupanga kuingia katika matendo kwa utondoti, ambayo kwayo ningeweza kupata kipengele cha kweli. Badala yake, nilifikiri ilitosha tu kuwa na maarifa na ufahamu wa kinadharia. Kwa mfano, katika maisha halisi siku zote nilijitahidi kwa ajili ya umaarufu na mapato, daima nilitaka kuwafanya wengine wanisikilize mimi, kuwafanya waniheshimu mimi na kuniidhinisha. Baada ya kufichua upotovu huu, nilifikiri tu kwa muda, na kuomba mbele ya Mungu, nikikubali upotovu wangu mwenyewe na nikijua kwamba yalikuwa ni maonyesho ya kiburi, na bila chochote zaidi. Matokeo yalikuwa kwamba, bila kujali ni mara ngapi nilihisi majuto au kukiri dhambi zangu mbele ya Mungu, na nilikuwa nimeandikiwa kurudia makosa yale yale ya zamani. Ndani ya mazingira yaliyopangwa na Mungu, kwa kuomba na kutafuta nilipata kujua kwamba Mungu alikuwa akitumia mazingira haya kushughulikia upotovu wangu. Baada ya kuja kwa ufahamu huu, hata hivyo, nilikubali tu kwamba majaribio yote ya Mungu na usafishwaji, ushughulikiaji wote wa Mungu nami na kunipogoa kulikuwa ni wokovu Wake, ulikuwa ni upendo Wake, kwamba moyo wa Mungu ni mzuri daima. Lakini sikutilia maanani hata kidogo katika kutenda ukweli ili kutatua upotovu wangu mwenyewe. Matokeo yake yalikuwa kwamba, ingawa nilipitia shida kiasi, sikuwa nimepitia mabadiliko yoyote kama matokeo. Baada ya kusikia mahubiri hayo, nilihisi kuwa ushirika huu ndio hasa niliouhitaji, kwamba ulikuwa umeniruhusu kuuelewa ukweli ambao sikuwa nimeuelewa hapo awali. Lakini yote niliyoyafanya yalikuwa tu kukumbuka maudhui ya ushirika kichwani mwangu na kisha kutoyazingatia, matokeo yake yakiwa ni kwamba ufahamu huo mdogo ulitoweka baada ya muda, na mimi kutokuwa nimepata chochote kamwe.

Kukabiliana na ukweli, niliona kwamba sikuwa nikitafuta ukweli kabisa. Nilikuwa nimemwamini Mungu kwa miaka mingi lakini sikuwa nimetia juhudi zozote katika kutenda ukweli au kuingia katika uhalisi, kwa kiasi kwamba nilikuwa bado sijapata ukweli, wala tabia yangu haikuwa imepitia mabadiliko yoyote. Huu wote ulikuwa ndio ufunuo wa tabia ya haki ya Mungu, kama Mungu alivyosema zamani sana: “Lazima ufanye juhudi ya kuishi kwa kudhihirisha maneno ya Mungu ili yaweze kuonekana katika matendo yako. Kama unayo maarifa ya mafundisho ya dini pekee, basi imani yako kwa Mungu itakuwa kazi bure. Kama wewe utatenda pia na kuishi kwa kudhihirisha neno Lake basi imani yako inaweza kuchukuliwa kuwa kamili na kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu(“Unapaswa Kuishi Kwa Ajili Ya Ukweli Kwa Maana Unamwamini Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Mungu ni mwenye haki. Mungu hajawahi kumtendea mtu yeyote bila haki, na hajawahi kumpa mwanadamu kimchezo, sembuse kumpa mwanadamu bila masharti. Mimi huwa sitendi ukweli, sijafanya jitihada zozote kuishi kwa kudhihirisha maneno Yake, matokeo yake yakiwa kwamba leo, ni lazima nivune kama nilivyopanda. Wakati huu sikuweza kujizuia kuhisi majuto makubwa, nikijuta kwa uchungu kwamba, ingawa nilikuwa nimepitia kazi ya Mungu, nilikosa kuingia kwangu mwenyewe, ili kwamba leo bado sikuwa na chochote cha kuonyesha licha ya imani yangu na kwa kweli sikuwa nimefikia wokovu wa Mungu. Na bado sikutaka kuendelea kuharibika tabia kwa namna hiyo, lakini badala yake nilitaka kuanza mwanzo, kufanya jitihada katika matendo yangu na kutekeleza maneno ya Mungu kwangu.

Baadaye, nilianza kujifundisha kutenda ukweli na kuingia katika uhalisi. Sikuwa tena kama nilivyokuwa nilipokuwa nikitaka watu wengine kunisikiliza, kuniheshimu na kuniidhinisha, kuomba tu na kukiri kwa Mungu. Badala yake, nilikuja mbele ya Mungu kutafuta ukweli, kutafuta maneno ya Mungu ili kuyala na kuyanywa ambayo yalihusiana hasa na suala hili na kukubali hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu, nikitatua upotovu wangu mwenyewe kwa njia hii. Nilipotenda na kuingia kwa namna hiyo, Mungu alinionyesha neema ya pekee ambayo iliniwezesha kutambua kwamba nilikuwa nikishindana na Mungu kwa cheo Chake, nikiwafanya watu kuniabudu kana kwamba nilikuwa babu yao wa zamani, au kuniabudu kama kwamba mimi nilikuwa Mungu. Niliona kuwa nilikuwa ibilisi Shetani mwenye asili na kiini sawa kabisa na vile vya joka kubwa jekundu, na karaha na chuki kwa asili yangu mwenyewe zilipanda bila kujua. Baadaye, nilijiandaa na ukweli kuhusu kumwinua Mungu, kuhusu kumshuhudia Mungu, na kwa hakika nilijifundisha kwa ajili ya kuingia. Kwa njia ya matendo haya, niliona hata kwa dhahiri zaidi ubaya na chukizo langu nikiwa mwenye kupayukapayuka na kuwaambia watu ni nini kilichokuwa nini. Nilijichukia na kujilaani hata zaidi, na nikawa radhi kuunyima mwili na kutenda ukweli ili kumridhisha Mungu. Baada ya kujifunza kwa njia hii kwa muda, nilitambua kwamba maonyesho yangu mwenyewe ya tabia yangu ya kiburi yalipungua sana.

Katika uhusiano wa kawaida baina ya watu, siku za nyuma nilijua nilipaswa kutenda uvumilivu, subira, kutumia hekima, kuwa na kanuni, na kuwa mtu mwaminifu. Lakini kwa hakika sikuwahi kuingia katika vipengele hivi vitano kamwe. Kwa hiyo, wakati wa kupatana na ndugu wa kiume na wa kike, mara nyingi kulitokea ndani yangu chuki bila sababu kuwaelekea kwa sababu ya jambo lisilo na maana au kufichua kwao upotovu, kwa kiasi kwamba sikuwa na njia ya kupatana nao. Sasa, naleta ufahamu wangu wa zamani katika maisha halisi ili kujifundisha na kutenda. Ninapowachukiza wengine kwa sababu ya maonyesho yao ya upotovu, huwa ninaomba kwa Mungu na kutafuta ukweli, nikiuliza jinsi napaswa kuelewa jambo hili ambalo nimelipata, na jinsi ninavyopaswa kutenda na kuingia katika maneno ya Mungu. Chini ya mwongozo wa Mungu, ilitokea kwangu kwamba kila mtu yuko katika mchakato wa kutafuta mabadiliko, kwa hiyo bila shaka kutakuwa na maonyesho ya upotovu, kwamba labda fulani hafahamu upotovu anaoufichua, au labda anatawalwa bila kujua na asili yake mwenyewe na hatendi kwa njia hii dhidi yangu kwa makusudi. Ilikuwa sawa tu na wakati ambapo tabia yangu ya kiburi kwa kawaida ilikuwa ni chukizo kwa wengine, lakini mimi mwenyewe nilibaki kutojua. Haya yote ni madhara yanayofanywa kwa mtu na Shetani. Ni Shetani anayepaswa kuchukiwa, na mtu hapaswi kuwa na maoni kuhusu ndugu zake wa kiume na wa kike. Nilipofikiria jinsi hii, chuki na vinyongo nilivyoshikilia ndani yangu vilipotea mara moja, na vilibadilishwa na chuki kwa Shetani na huruma na msamaha kwa ndugu zangu wa kiume na wa kike, hata kutaka kupata fursa zinazofaa za kuwasaidia wengine. Nilipojaribu kwa hiari kuwasaidia watu wengine, niligundua kwamba uhusiano wangu nao ulikuwa wa kirafiki zaidi na nilipata ladha ya furaha ambayo hutoka kwa kuwasaidia wengine.

Nilipojifundisha kuingia katika maneno ya Mungu na kutenda ukweli, sio tu kuwa nilipata ujuzi kiasi na kuingia katika vipengele vyote vya ukweli, pia niliona kazi za ajabu za Mungu. Nilihisi uongozi na mwongozo wa Mungu na kuonja uhakika, amani na furaha ambazo kutenda ukweli kulikuwa kumeupa moyo wangu. Nilihisi kuwa hakukuwa kitu kilichokuwa kitupu kuhusu maisha, kwamba kulikuwa na somo la kujifunza kila siku, kwamba kulikuwa na maoni mapya na ufahamu kila siku, kwamba niliweza kuona Mungu akiniokoa kila siku, kuhisi kwamba kutafuta ukweli kulikuwa kwa maana sana, kwamba ukweli kwa kweli unaweza kuwaokoa na kuwabadili watu!

Mara nilipokuwa na kipande hiki kidogo cha uzoefu na ufahamu wa kibinafsi, nilihisi kuwa njia yangu mwenyewe ya kumwamini Mungu ilikuwa imepata ahueni, nisihisi kuwa singeweza kuupata wokovu kamwe tena. Naamini kwamba, almradi nafanya kazi na Mungu, daima kujiandaa na ukweli na kutenda na kuingia katika ukweli, bila shaka nitafikia mabadiliko katika tabia yangu potovu. Ninaamini kwamba kazi ya Mungu inaweza kumwokoa mwanadamu na maneno ya Mungu yanaweza kumbadilisha mtu: nina imani hii kwa sababu nimeionja tayari. Kuanzia leo kwendelea, napenda kutafuta ukweli na kutenda ukweli miguu yangu ikiwa imewekwa sakafuni kwa udhabiti. Napenda Mungu aendelee kuniongoza, kunifanya kufikia mabadiliko katika tabia yangu hivi karibuni, kuishi kwa kudhihirisha namna ya mtu wa kweli ili kuwa na ushuhuda wa Mungu, kuwa na ushuhuda wa kazi ya Mungu kuniokoa, kuwa na ushuhuda wa nguvu za Mungu kumwokoa mwanadamu, na kuwa na ushuhuda wa matendo ya ajabu ya Mungu!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Nimebahatika Kumhudumia Mungu

Na Gensui, Korea ya Kusini Mwenyezi Mungu anasema, “Ni kupitia nini ndiyo ukamilishaji wa Mungu kwa mwanadamu hutimizwa? Kupitia tabia Yake...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp