Sababu ya Kweli ya Kazi Isiyofaa

15/01/2018

Xinyi Mji wa Xi’an, Mkoa wa Shaanxi

Katika ziara zangu za karibuni kwa makanisa, mara nyingi niliwasikia viongozi na wafanyakazi wakisema kwamba watu wengine, baada ya kuhudhuria ushirika na mimi, waligeuka hasi, wanyonge na walikosa motisha ya kuendelea kutafuta. Wengine walisema ilikuwa vigumu sana kumwamini Mungu na walimwelewa Mungu visivyo. Wengine walisema kwamba hali zao zilikuwa nzuri kabla ya wao kukutana na mimi, lakini punde tu waliponiona, walihisi shinikizo kubwa mno na wasio na raha. … Niliposikia haya yote, nilihuzunika, na nilihisi kukosewa vibaya—kila wakati nilipokuja kushiriki na wao ningeishi kwa baadhi ya siku, na, ili kutatua shida zao, nilipitia na kudondoa kama mifano vifungu vingi vya neno la Mungu, nikizungumza hadi nilipokauka mdomo, na wakati huo wote nikifikiri kwamba juhudi zangu zilikuwa zimetoa matokeo mazuri. Sikuwahi kufikiri kwamba mambo yangegeuka kuwa hivi. Mbona hili lilifanyika. Niliweka swali hili katika mawazo yangu nilipomwomba Mungu, “Ee Mungu, hakika mimi ni mwenye makosa kwa ajili ya yote ambayo yamefanyika, lakini sijui nilikosea wapi. Naomba mwongozo Wako, ili niweze kutambua zaidi makosa yangu. Niko tayari kusubiri kupokea nuru Yako.”

Baada ya kumaliza sala yangu, nilianza kutafakari kuhusu ushirika na ndugu zangu: Walipoeleza masuala kuhusu mipango ya kazi ningechangua asili yao yenye kiburi na kueleza kinaganaga kuhusu matokeo ya kiburi, nikisema kwamba kiburi chote bila kuepukika kingekabiliwa na adhabu. Nilipoona kwamba matatizo yalikuwa yakiibuka katika mchakato wa uchaguzi, ningezungumza kuhusu jinsi kuchagua watu wasiofaa kungekatiza kuendelea kwa kazi ya kanisa na kuharibu maisha ya ndugu zetu. Kwa njia hii, Mungu angekuja kutuchukia na tungeondolewa. Nilipoona ndugu wakizembea kazini, ningeibua watu fulani waliokuwa wametimuliwa kama mfano. Ningewaambia kwamba walikuwa wanageuka kuwa wadanganyifu na kwamba hili lilikuwa sawa na kumsaliti Mungu. Kama hawangebadili mienendo yao, jaala yao ingekuwa sawa na watu waliokuwa wameshindwa. Wakati hawakutaka kueneza injili, ningejadili jinsi matendo kama hayo yaliasi dhidi ya na kumpinga Mungu. … Ee Mungu! Nilikuwa nikitumia ukweli katika hali gani ili kutatua matatizo yao? Nilikuwa nikitumia tishio kabisa! Chini ya mwongozo wa Mungu, niliwaza kuhusu kifungu kifuatacho kutoka kwa mahubiri, “Huduma inayolingana na mapenzi ya Mungu inahitaji kwamba katika vitu vyote na kuhusu masuala yote tunapaswa kumsifu Mungu, kutoa ushuhuda kwa Mungu, kuwasiliana kwa karibu mapenzi ya Mungu, kuwasiliana kwa karibu maombi ya Mungu, na kuwaruhusu wengine kutenda kwa mujibu wa neno la Mungu. Hatupaswi kuwafanya watu kutenda kulingana na kanuni, amri na misemo ya mwanadamu. Ushirika wako unapaswa kuwawezesha watu kuja mbele za Mungu na kutii mapenzi Yake, kutenda kulingana na neno la Mungu na, hatimaye, kuja kumjua Mungu na kumtii” (Ushirika kutoka kwa Aliye Juu). Wakati huo, nilipitia ufunuo wa ghafla. Mungu huwaaminia viongozi kazi ya kumsifu Mungu, kutoa ushuhuda kwa Mungu, kuwasiliana kwa karibu mapenzi na maombi ya Mungu, kuwaruhusu wengine kutenda kwa mujibu wa maombi ya Mungu na, hatimaye, kuja kumwelewa na kumtii Mungu. Katika kutatua masuala ya ndugu zangu, mimi, hata hivyo, nilizungumza mara chache kuhusu maombi ya Mungu, mapenzi Yake ama matamanio Yake. Pia nilitumia ukweli mara chache kuwasiliana kwa karibu kuhusu hali za ndugu zangu. Badala yake, bila huruma nilichangua asili yao na njia ambayo kwayo walitenda. Ningetaja matokeo yanayowezekana ya matendo yao ili kuwatisha kujijua. Hili lilisababisha ndugu zangu kutoweza kutambua mapenzi ya Mungu, kutokuwa na kujifahamu kwa kweli na kutoweza hata zaidi kuona nia yenye ari ya wokovu wa Mungu na upendo kwa wanadamu. Kutokana na hilo, waliishi katika hali za kila aina zisizo za kawaida. Ilikuwa hapo tu ndipo nilitambua kuwa nilikuwa nikitenda mambo katika uaminifu wa kijinga kwa tamaa zangu mwenyewe. Nilikuwa nikimpinga Mungu! Kuwaongoza ndugu zangu kwa njia hii, sio tu kwamba sikuweza kuwasaidia kumwelewa na kumtii Mungu, kwa kweli nilikuwa nikiwasababisha kuelewa visivyo na kuingia katika mgongano zaidi na Mungu. Kwa njia hii, walitengana na Mungu zaidi na zaidi na kutenda dhambi zaidi. Licha ya ukweli kwamba nilitatua masuala ya ndugu zangu kulingana na neno la Mungu na kila kitu nilichosema kilikuwa kweli, kwa kweli, sikuwa nikifanya kazi kwa njia ya kutoa maoni yanayosaidia. Kwa kweli, kile nilichokuwa nikifanya kilikuwa bure kabisa. Njia hii ya kufanya kazi ingekuwa ya uharibifu mkubwa kwa kazi ya kanisa. Ilikuwa hapo ndipo nilitambua kwamba njia nzuri zaidi ya kuwasaidia ndugu zangu ilikuwa kuwaruhusu kuelewa mapenzi ya Mungu kupitia neno la Mungu, kutambua nia yenye ari ya wokovu wa Mungu, kupata kujua kiini cha asili yao wenyewe na, kwa kufanya hivyo, kujifunza kujichukia wenyewe, kutenda kulingana na maombi ya Mungu na, hatimaye, kupata kujua na kumtii Mungu. Hii ndiyo maana ya kweli ya huduma kulingana na mapenzi ya Mungu na huduma ya aina hii tu ndiyo inafikiri mapenzi ya Mungu.

Namshukuru Mungu kwa kunionyesha sababu ya kweli mbona kazi yangu ilikuwa isiyofaa. Baadaye, kwa fahamu nilifanya kazi kuwasiliana kwa karibu mapenzi na matakwa ya Mungu kulingana na hali za ndugu zangu. Nilijadiliana mbona Mungu aliwataka watende kwa njia Aliyotaka, jinsi nia Zake zenye ari zilidhihirika katika maisha yao na ni matokeo ya aina gani Alitarajia kuwa nayo. Pia nilijadili jinsi wangefanya kazi na Mungu ili kuwa katika kukubaliana na mapenzi Yake. … Baada ya kuwasiliana kwa karibu hivi, niliona baraka za Mungu kwa kweli: Ndugu zangu walianza kuelewa mapenzi ya Mungu na kushuhudia wokovu wa Mungu. Walipata kuelewa kwamba gharama ambayo Mungu amelipa kwa ajili ya watu wote ni isiyoweza kufahamika. Walianza kuelewa asili yao asi, walikuwa tayari kutafuta ukweli na walihisi kutiwa hamasa kutimiza wajibu wao.

Ukweli ulivyojifichua, nilikuwa na hisia ya kina ya asili ya kweli kabisa ya upendo wa Mungu. Nilipofanya kazi kulingana na mapenzi yangu mwenyewe, nikimpinga Mungu katika huduma yangu Kwake, Mungu mara moja alifichua upungufu na kasoro yangu na Akasahihisha makosa yote katika kazi yangu. La sivyo, kwa kweli sijui matendo yangu yangewaongoza ndugu zangu wapi au kwa muda upi ningekuwa nimewanasa. Mwenyezi Mungu, asante kwa kazi Yako halisi na ya kweli, ambayo iliniruhusu kuona matendo Yako ya ajabu na wokovu ambao Uliniletea. Kuanzia sasa kuendelea, naapa kuwa mwenye kushika sana ukweli na kufanya kazi kwa bidii zaidi ili kutimiza matakwa Yako, ili kutafuta na kuelewa mapenzi Yako na kutimiza uwezo wa kufanya kazi kulingana na tamanio Lako katika vitu vyote, kutekeleza huduma kwa mujibu wa mapenzi Yako.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Nilifurahia Karamu Kubwa

Xinwei Mkoa wa Zhejiang Juni 25 na 26, mwaka wa 2013 zilikuwa siku zisizosahaulika. Eneo letu lilipata tukio kubwa, viongozi wengi na...

Pambano la Kuwa Mtu Mwaminifu

Mwenyezi Mungu anasema, “Ufalme Wangu unawahitaji wale ambao ni waaminifu, wasio wanafiki, na wasio wadanganyifu. Je, si watu wenye moyo...

Kuishi Mbele za Mungu

Na Yongsui, Korea ya Kusini Mwenyezi Mungu anasema, “Ili kuingia katika uhalisi, mtu lazima apindue vitu vyote kuelekea maisha halisi....

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp