“Njiwa Mjumbe” Aleta Habari Muhimu

24/12/2019

Na Su Jie, China

Siku moja mnamo mwaka wa 1999 baada ya mkutano mmoja kukamilika, mchungaji alinijia na kuniambia, “Su Jie, kuna barua yako hapa.” Mara tu nilipoiona, nilijua kuwa ilikuwa imetoka katika kanisa ambalo nilikuwa nimelianzisha kule Shandong. Nilichukua barua hiyo na nilipokuwa njiani kuelekea nyumbani, nilijiuliza huku nikitembea, “Barua hii ni nene sana, yawezekana kwamba wamekabiliwa na matatizo fulani?”

Nilikuwa mwenye hamu sana kuifungua barua hiyo baada ya kufika nyumbani na ndani yake nilisoma: “Dada Su, amani iwe nawe katika Bwana! Ninaandika ili kukuarifu habari fulani za kushangaza: Bwana Yesu Mwokozi wetu ambaye tumemtamani sana siku zote amerudi. Tayari Amerudi mwilini na anafanya hatua ya kazi ya kuwahukumu na kuwatakasa watu kupitia maneno Yake nchini China; Amemaliza Enzi ya Neema na kuanza Enzi ya Ufalme. … Natumaini kuwa utakubali kazi mpya ya Mungu na kwenda sambamba na nyayo za Mungu. Chochote ufanyacho, usikose nafasi hii ya wokovu wa Mungu wa siku za mwisho.” Mara niliposoma hadi hapo, nilishtuka: Hawakuwa wamekabiliwa na matatizo yoyote kwa kweli, lakini waliliamini Umeme wa Mashariki! Nilikuwa mwenye hamu kujua ni nani aliyeandika barua hii, kwa hiyo nilifungua ukurasa wa mwisho kwa haraka. Ilitokea kuwa Ndugu Meng ndiye aliyeiandika, na saini za ndugu wengine wote wa kanisa pia zilikuwa mwishoni. Baada ya kusoma barua hiyo nzima nilipigwa na bumbuazi. Niliikazia macho kwa muda bila kuonyesha mawazo kabla ya kupata tena utambuzi na kujiuliza: “Umeme wa Mashariki linashuhudia kwamba Bwana amerudi, na wameiba kondoo wengi wazuri na kondoo wengi viongozi kutoka kwa madhehebu kadhaa. Kamwe sikuwahi kufikiria kwamba Ndugu Meng wa kutoka kanisa la Shandong angeliamini Umeme wa Mashariki pia. Ndugu wote wa kanisa hili wameibiwa na Umeme wa Mashariki—je, nini kinaweza kufanywa?” Wazo hili liliponijia nilihisi wasiwasi hata zaidi, lakini kusafiri kwenda Shandong kulikuwa mbali sana na nilikuwa nimebanwa na kazi yangu hapa. Singeweza kwenda wakati huo. Kwa ajili ya kushindwa la kufanya, niliweza tu kumlilia na kumwomba Bwana: “Bwana! Ndugu hawa hawajakuamini kwa muda mrefu sana na bado hawana msingi thabiti. Tafadhali walinde….”

Baada ya hayo, nilitafuta katika Biblia na kuanza kuwaandikia barua ya kwanza ili kuwajibu. Katika barua hiyo nilisema: “Ndugu katika Yesu Kristo, ninawashauri kwa heshima muwe waangalifu. Paulo alisema: ‘Nashangaa kwamba mmejiondoa upesi hivi kwake yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kuelekea injili nyingine: Ambayo si nyingine; lakini kunao wengine ambao wanawasumbua na ambao wanataka kupotosha injili ya Kristo. Ila ingawa sisi, au malaika kutoka mbinguni, atahubiri injili yoyote nyingine kwenu isipokuwa hiyo ambayo tumehubiri kwenu, yeye na alaaniwe. Jinsi tulivyosema awali, ndivyo nisemavyo sasa tena, mtu yeyote akiwahubiria injili nyingine kando na ile mliyoipokea, yeye amelaaniwa’ (Wagalatia 1:6-9). Ndugu, kuwaleta mbele za Bwana hakukuwa kazi rahisi; je, mnawezaje kumsaliti Bwana haraka sana hivi? Kimo chenu ni kidogo sana—msisikilize tu njia nyingine kwa ukunjufu! Lazima mnisikilize kwa sababu kile nilichoshiriki nanyi ndiyo njia ya kweli. Bwana Yesu Kristo tu ndiye Mwokozi wetu. Lazima mdumishe jambo hili milele….” Ni baada tu ya kumaliza kuandika na kuangalia barua hiyo ya kurasa nane ndipo tu nilihisi utulivu. Nilijiwazia: Niliandika yote ambayo nilipaswa kuandika, nikatafuta maoni katika maandiko yote ambayo nilipaswa kutafuta maoni kutoka, na nikaandika maneno yote ya ushauri na ya kutia moyo ambayo nilipaswa kuandika. Naamini kwamba baada ya wao kusoma barua hii, hakika watajibu na kukubali makosa yao.

Wiki mbili baadaye, nilipokea jibu hili: “Dada Su, hatuwezi kuzungumzia yote ambayo tumeona na kusikia kwa sababu Mwenyezi Mungu tunayemwamini ndiye Bwana Yesu aliyerudi. Tunadumisha njia ya kweli na kusonga mbele; hatujamsaliti Bwana hata kidogo, lakini tunafuata nyayo za Bwana. Ulitaja maneno haya kutoka kwa Paulo: ‘Nashangaa kwamba mmejiondoa upesi hivi kwake yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kuelekea injili nyingine: Ambayo si nyingine; lakini kunao wengine ambao wanawasumbua na ambao wanataka kupotosha injili ya Kristo’ (Wagalatia 1:6-7). Kuna sababu ya kile ambacho Paulo alisema. Tunahitaji tu kuchunguza Biblia ili kujua kwamba 'injili nyingine' ambayo Paulo alizungumzia wakati huo iliwahusu Mafarisayo kuwasihi watu wadumishe sheria ya Yehova; haikuwahusu watu wa siku za mwisho kueneza injili ya ufalme, kushuhudia kwamba Bwana amerudi katika mwili na anafanya kazi Yake ya hukumu akianza na nyumba ya Mungu. Paulo alipoandikia makanisa ya Wagalatia barua hii, hakuna mtu yeyote aliyekuwa akihubiri injili ya ufalme ya Mungu. Kwa hiyo, 'injili nyingine' ambayo Paulo alizungumzia haihusu Bwana kurudi na kufanya kazi Yake ya hukumu ya siku za mwisho akianza na nyumba ya Mungu. Hatua hii ya kazi ya hukumu ambayo Bwana sasa amerudi kutekeleza inatimiza unabii huu uliopo katika Kitabu cha Ufunuo: ‘Na nikamwona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu, akiwa na injili ya daima kuwahubiria hao wanaoishi katika ulimwengu, na kwa kila taifa, na ukoo, na lugha, na watu, Akisema kwa sauti kuu, Mwogopeni Mungu, na kumpa utukufu; kwa kuwa saa ya hukumu yake imekuja(Ufunuo 14:6-7). Hapa 'injili ya milele' inahusu injili ya ufalme. Zaidi ya hayo, wokovu huu wa mwisho ulifichuliwa zamani na Roho Mtakatifu kwa wanafunzi wa Bwana Yesu. Kama Petro alivyosema: ‘Kwa maana muda umekuja ambao lazima hukumu ianze katika nyumba ya Mungu(1 Petro 4:17). ‘Ninyi mnaohifadhiwa na nguvu zake Mungu kupitia imani hadi kwa wokovu ambao uko tayari kufichuliwa katika muda wa mwisho’ (1 Petro 1:5). Sister Su, si kurudi kwa Bwana ni kitu ambacho sisi kama waumini tunatamani sana? Sasa Bwana amerudi kweli; lazima tuwe watafutaji wanyenyekevu. Hatuwezi kabisa kuwa kama Mafarisayo katika jinsi ambavyo walimtendea Bwana Yesu, kupata mwili kwa Mungu kwa mara ya kwanza, kutumia ufahamu wa Bibilia na fikra zao na mawazo yao pasipo kufikiria ili kuwekea kazi mpya ya Mungu mipaka, kumlaani na kumpinga Bwana kwa sababu ya Bwana Yesu kutotii sheria, na kisha kumsulubisha Bwana. Mafarisayo walimwamini tu Yehova Mungu lakini hawakukubali kupata mwili kwa Yehova Mungu—kazi ya Bwana Yesu—na mwishowe walishutumiwa na kulaaniwa na Bwana. Je, si somo hili kali linastahili kutafakari kwetu? Hakuna mtu anayeweza kukataa kuwa Bwana Yesu ni Mwokozi wetu. Lakini ikiwa tunamkubali tu Bwana Yesu lakini hatukubali kurudi kwa Bwana, je, sisi si sawa na Mafarisayo? Je, basi hatujakuwa watu wanaomwamini Mungu lakini wanampinga? Zaidi ya hayo, Dada Su, hatuwezi kufanya kama unavyosema kwa sababu tu ulituhubiria injili ya Bwana. Tunayemwamini ni Mungu. Petro na mitume wengine hapo nyuma walisema, ‘Tunapaswa kumtii Mungu badala ya wanadamu’ (Matendo 5:29). Na katika maswala yanayohusu kuja kwa Bwana hatuwezi hasa kuwasikiliza wanadamu wengine tu. Tayari tumebainisha kuwa neno la Mwenyezi Mungu ndiyo sauti ya Mungu. Tunatumaini kwamba utalichunguza jambo hilo pia.”

Nilipokuwa nikisoma barua hiyo niligadhabika, na sikusadiki hata kidogo. Nilichukua ghafla kitabu changu cha marejeo cha biblia na kufungua ukurasa wa utangulizi wa Kitabu cha Wagalatia. Nilisoma kwa makini na nikshangaa sana: Kwa kweli jambo hili lilikuwa kweli! “Injili nyingine” ambayo Paulo alizungumzia kweli iliwahusu Mafarisayo kuwafanya watu wafuate sheria za Yehova; bila shaka, haikuhusu kazi ya Bwana ya hukumu kuanza na nyumba ya Mungu baada ya kurudi Kwake. Miaka hiyo yote, ilikuwaje kwamba sikuwa nimefahamu kamwe kuwa huu ndio ulikuwa muktadha wa aya hiyo? Si ajabu hawakusadiki. Lakini wazo lingine lilinijia: Hata kama kile nilichokisema kilikuwa si sahihi, hilo bado haliwezi kudhibitisha kwamba Bwana amerudi, kama wanavyohubiri. Nilisoma barua hiyo tena kuanzia mwanzo hadi mwisho na kadiri nilivyozidi kuisoma, ndivyo nilivyozidi kughadhabika. Niliwaza, “Sikuwahi kutarajia kwamba baada ya kuondoka kwa muda mfupi sana hivyo, wangekuwa na ujasiri wa kuwa wajeuri kwangu na hata kuthubutu … kuthubutu kuniita Mfarisayo. Nawachukia Mafarisayo kuliko mtu yeyote. Je, ningewezaje kumpinga Bwana kama jinsi Mafarisayo walivyofanya? Nimejitahidi sana kwa miaka mingi sana, nikifanya kazi kwa bidii mchana na usiku kwa ajili ya waumini. Je, wangewezaje kutojua hilo?” Kadiri nilivyozidi kufikiria kuhusu jambo hilo ndivyo nilivyozidi kufadhaika na nikawaza: "La, ninawezaje kushindwa kwa maneno na waumini wachache ambao bado ni washamba? Nimesoma Biblia mara nyingi sana—haiwezekani kuwa siwezi kushinda mjadala huu.”

Kwa hiyo, nilichomoa kalamu yangu tena na kuwaandikia barua ya pili, nikisema: “Kina ndugu, amani iwe nanyi katika Bwana! Kusoma barua yenu kulinifadhaisha sana. Siwasihi mfanye kama ninavyosema—mmeelewa nia yangu visivyo kabisa. Ninaogopa kuwa mtaondoka kutoka kwa njia ya Bwana Yesu kwa sababu Bwana Yesu alisema: ‘Basi iwapo mtu yeyote atawaambia, Tazameni, Kristo yuko huku, au yuko pale; msiamini hili. Kwa kuwa wataibuka Makristo wasio wa kweli, na manabii wasio wa kweli, nao wataonyesha ishara kubwa na vioja; ili kwamba, ikiwezekana, watawadanganya walio wateule zaidi(Mathayo 24:23-24). Paulo pia alisema: ‘Sasa tunawaomba, ndugu, kwa kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, na kwa kukusanyika kwetu Kake. Kuwa msidhoofike upesi kimawazo, au msihangaike, kwa roho, au kwa neno, au kwa waraka unaofikiriwa kutoka kwetu, kama kwamba siku yake Kristo ishafika. Mtu yeyote asiwadanganye kwa namna yoyote’ (2 Wathesalonike 2:1-3). Ndugu wapendwa, nawashauri katika jina la Bwana Yesu kwamba kutakuwa na siku za hatari mbeleni katika siku za mwisho, na kwamba lazima msimwamini mtu yeyote anayehubiri kuhusu kuja kwa Bwana. Lazima tuwe waangalifu sana na kuzingatia maneno ya Bwana, tusije tukachukua njia isiyo sahihi na kumkasirisha Bwana! "

Wiki mbili baadaye nilipokea barua nyingine kutoka kwao, ambayo ilisema: "Dada Su, maandiko uliyotupa hayana makosa, lakini lazima tuelewe wazi kuhusu maana halisi ya Bwana Yesu ndani ya maneno haya na tusielewe visivyo mapenzi ya Bwana. Bwana Yesu alituambia waziwazi kwamba Makristo wa uwongo watajitokeza Bwana atakapokuja katika siku za mwisho, na kwamba Makristo wa uwongo watajifanya wakitumia jina la Bwana, na kuonyesha miujiza ili kuwadanganya watu. Kwa kusema hili, Bwana anatuambia tutende utambuzi; Hasemi kwamba wale wote wanaohubiri kuhusu kuja kwa Bwana ni waongo. Ikiwa, kama unavyosema, wale wote wanaohubiri kuhusu kuja kwa Bwana ni waongo na lazima tujihadhari nao na kuwakataa, basi je, si huenda hatutamfungia mlango Bwana Yesu aliyerudi mwilini? Tunasema hili kwa sababu Bwana alisema atarudi tena. Ni wazi kwamba, mtazamo wa aina hiyo haukubaliani na mapenzi ya Bwana. Kwa mintarafu ya kutofautisha kati ya Kristo wa kweli na Makristo wa uwongo, tumekunukulia kifungu cha maneno ya Mwenyezi Mungu na tunatumaini kuwa utakisoma vizuri. Mwenyezi Mungu alisema: ‘Kama, wakati wa zama hizi, kutatokea mtu mwenye uwezo wa kuonyesha ishara na maajabu, na kutoa mapepo, kuponya wagonjwa, na kufanya miujiza mingi, na kama mtu huyu anadai kwamba yeye ni Yesu ambaye amekuja, basi hii itakuwa ni ghushi ya roho wachafu, na kumuiga Yesu. Kumbuka hili! Mungu Harudii kazi ile ile. Hatua ya kazi ya Yesu tayari imekwisha kamilika, na Mungu Hataichukua tena hatua hiyo ya kazi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuijua Kazi ya Mungu Leo). Kazi ya Mungu haiwezi kuwa isiyobadilika daima. Kazi ya Mungu ni mpya kila wakati, kamwe si nzee, na kamwe haijirudii. Kama tu jinsi kazi ya Mungu katika Enzi ya Sheria na Enzi ya Neema ilivyokuwa hatua mbili tofauti za kazi. Katika siku za mwisho, tayari Mungu ametekeleza hatua moja ya kazi ya kuwahukumu na kuwatakasa watu kupitia maneno Yake kulingana na mahitaji ya wanadamu. Hii ni hatua ya kuwatakasa na kuwaokoa watu kikamilifu. Ni mpya zaidi, ya fahari zaidi, na ya vitendo zaidi kuliko kazi ya hapo awali. Kutoka kwa kila hatua ya kazi ya Mungu, tunaweza kuona ukweli ambao Yeye huonyesha na vile vile hekima, mamlaka na nguvu ya kazi Yake. Lakini Makristo wa uwongo wana pepo waovu na hawana asili ya Mungu. Wanakosa ukweli kabisa na kwa hiyo hawawezi kuonyesha ukweli, na hawawezi kuonyesha uweza wa Mungu, hekima na tabia ya Mungu. Ni wazi kwamba Makristo wa uwongo hawawezi kufanya kazi ya Mungu hata kidogo. Makristo wa uwongo wanaweza tu kuiga kazi ambayo Bwana Yesu tayari amefanya, kuwaponya wagonjwa, kufukuza pepo na kuonyesha miujiza kadhaa ya kawaida ili kujifanya Kristo katika juhudi ya kuwadanganya watu. Dada, tunahitaji ufahamu halisi wa maneno ya Bwana; hatuwezi kuelewa vibaya mapenzi ya Bwana, sembuse kujikata pua ili kuunga wajihi kwa sababu tu Makristo wa uwongo wanajitokeza katika siku za mwisho. Hatuwezi hata kutochunguza kazi ya kurudi kwa Bwana.… ”

Hata ingawa ushirika wote wa kina ndugu katika barua hiyo ulikuwa na msingi, sikuwa na nia yoyote ya kuutafuta au kuutafakari. Nilijali tu kuhusu ikiwa walikubali maandiko ambayo nilikuwa nimeyapata na kumgeukia Bwana au la. Niliwaza kuhusu mijadala hii miwili katika barua zetu na kuona kuwa walikuwa hawajasadiki hata kidogo. Kinyume chake, nilikuwa nimewaruhusu wanishawishi kiasi kwamba sikuheshimiwa hata kidogo. Niliharakisha kumwomba Bwana na kisha kuchukua Biblia na vitabu vyangu vyote vya kiroho, na kuviweka kwenye kitanda changu. Niliendelea kuvisomasoma, nikitaka kupata msingi wa kuvikanusha. Chumba kilikuwa kimya kabisa isipokuwa sauti ya kuchakarisha ya mimi kugeuza kurasa. Usiku uliingia kabla ya mimi kugundua na bado sikuwa nimepata chochote. Nilikuwa nimechoka sana kiasi kwamba nilishusha pumzi zito na kuwaza: “Kwa kweli si rahisi kufikiria jibu la barua hii.” Nilichoweza tu kufanya ni kuchukua kalamu yangu na kuandika: “Ndugu, kusoma barua yenu kumeniacha na hisia kwamba ninyi tena si wanakondoo wachanga wazuri kama mlivyokuwa hapo nyuma. Hata hamnisikizii, mnasisitiza kuondoka kutoka kwa njia ya Bwana, na ninyi hamkubaliani nami. Nadhani kwamba mienendo yenu inamhuzunisha Bwana, na mimi pia nina huzuni sana. Naomba Bwana Yesu awaguse na naomba barua hii iwawezeshe kurudi nyuma hivi karibuni. Amina!”

Baada ya majuma kadhaa nilipokea jibu lingine kutoka kwao, lakini nilisikitishwa kwamba hawakuwa wamerudi nyuma kwa sababu ya upendo wangu na kuwatia moyo. Kinyume chake, walisema kwa ukali na kwa hakika: “Dada Su, ulitubadili dini, hiyo ni kweli, lakini Yule tunayepaswa kumshukuru kwa ajili ya jambo hili ni Bwana, kwa sababu ilikuwa ni Mungu aliyetukusanya, kondoo hawa waliopotea na kuzurura, kuwa kundi kwa usaidizi wako. Ulikuwa tu mtumishi anayetunza kundi, lakini ni Bwana Yesu tu ndiye mchungaji wetu wa kweli. Kama Bwana Yesu alivyosema: ‘Mimi ndiye mchungaji mzuri, nami nawajua kondoo Wangu, na wale ambao ni Wangu wananijua(Yohana 10:14). Bwana anamwaminiai kila mtu anayemfanyia kazi kondoo. Jukumu la mtu ni kuwatunza tu na Bwana atakaporudi, anapaswa kurudisha kundi Kwake. Dada Su, sote tunajua mfano wa 'wapangaji waovu' ambao Bwana Yesu alizungumzia katika Biblia. Ili kumiliki mali kwa nguvu, wapangaji waliwapiga watumishi waliokuja kukusanya matunda, na mwenye nyumba alipomtuma mtoto wake wa kiume, walimuua mtoto huyo ili kumiliki mali hiyo. Mwenye nyumba atakaporudi, je, atawatendeaje wapangaji hawa waovu? Lazima tusiwe kama wao. Bwana sasa amerudi, na tunapaswa kukabidhi kondoo wa Bwana kwa Bwana. Hii ndiyo mantiki ambayo lazima tuwe nayo.”

Barua hii ilinishangaza sana. Nilijiwazia: “Je, wanawezaje kupata ufahamu mwingi hivyo haraka? Ni muda wa miaka mbili tu umepita tangu niende Shandong na kuanzisha kanisa hilo. Nilipoondoka walikuwa bado kama 'watoto wachanga' katika imani yao. Kamwe sikuwahi kufikiria kuwa miezi michache tu baada ya kukubali Umeme wa Mashariki maneno yao yangekuwa na nguvu nyingi sana, au kwamba wangeweza kupata vifungu sahihi hivi vya Biblia ili kunishawishi, kwamba ningeachwa bila neno la kuwajibu.” Wakati huo nilisikitishwa sana na kuhisi kwamba kina ndugu hawa walikuwa wamekuwa thabiti katika azma yao ya kufuata Umeme wa Mashariki, kwamba hawakuwa na mipango ya kurudi nyuma. Nilijua kuwa singeweza kuwashawishi warudi. Huku nikihisi dhaifu na hafifu kabisa, niliwatumia barua ya nne kwa kusita, ambamo nilisema: “Shauri yenu. Kama ilivyoandikwa katika Biblia, tangu nyakati za zamani, kwamba kile kinachotoka kwa Mungu kitafanikiwa na kile kinachotokana na mwanadamu kitashindwa. Msiniandikie barua tena. Natumaini kwamba mnaweza kushikilia imani yenu na upendo wenu kwa Yesu Kristo."

Baada ya kukataa kazi ya Mungu ya siku za mwisho ambayo ndugu wa Shandong walikuwa wameshiriki nami, roho yangu ilikuwa imehuzunika na kudhoofika zaidi, na hali yangu ya jumla ilikuwa imefifia. Hata ingawa nilifunga na kuomba na kutafakari jinsi ambavyo naweza kuwa nilitenda dhambi dhidi ya Bwana mara nyingi, sikuweza kamwe kuelewa mapenzi ya Bwana, na sikuweza kabisa kuhisi uwepo wa Bwana. Ilikuwa katika kipindi hiki ndipo wachungaji na wazee walitoa mashtaka ya uongo dhidi yangu ili kushindania pesa kutoka kwa sadaka, na walinifukuza kutoka kanisa kwa mafanikio. Nilikuwa mwenye taabu sana na sikujua cha kufanya. Mara nyingi ningeenda kando ya mto na kuimba wimbo “Bwana, Wewe Ndiye Rafiki Yangu wa Karibu Zaidi” huku nikilia. Nilitamani sana Bwana arudi haraka ili Aweze kuniokoa kutoka kwa matatizo yangu.

Siku moja miezi sita baadaye nilipokuwa nikitayarisha chakula cha mchana, nilimsikia mama mkwe wangu akiita jina langu kutoka nje ya mlango wa mbele. Nilipoufungua mlango, nilimwona mwanamke mwembamba mchanga mwenye sura ya kupendeza akiwa amesimama nyuma ya mama mkwe wangu. Mama mkwe wangu alisema, “Dada huyu mdogo amekuja kukuona. Alikuwa na anwani lakini hakuweza kukupata, kwa hiyo alikwenda kanisani. Alisema kwamba alihitaji kukuona kwa haraka, kwa hiyo niliharakisha kumleta.” Nilimtathmini dada huyu kwa uangalifu na kujiwazia: “Je, ni kwa nini sielekei kumfahamu?” Aliponiona, alinijia, akanishika mkono na kusema kwa msisimko: “Kwa hiyo wewe ndiye Dada Su. Hatimaye nimekupata!” Kwa sababu ya kupigwa na bumbuazi na matendo yake, nilimtazama kwa mshangao na kumuuliza: “Je, wewe ni nani? Sidhani kwamba tumewahi kukutana?” Jibu lake la shauku lilikuwa: “Dada, jina langu la ukoo ni Wang. Niko hapa kwa sababu ya Ndugu Meng na Dada Zhao kutoka Shandong. Ndugu Meng na wengine waliandika barua kwa Kanisa la Mwenyezi Mungu hapa na kututaka tufikirie jinsi ya kukupata, lolote litokealo. Walituaminia wajibu wa kushiriki nawe injili ya Mungu ya ufalme kwa sababu wana shughuli nyingi sana na kwa kweli hakukuwa na wakati kwao kuja wenyewe. Sijui barua hii imepitia mikono mingapi ya watu, lakini imesambazwa mara kadhaa kabla ya kutufikia. Nimekuja hapa mara nyingi sana nikiuliza kukuhusu. Haikuwa rahisi kukupata.” Aliposema jambo hilo, dada huyo mdogo alisongwa roho na kuweka barua hiyo mikononi mwangu. Niliichukua na kuisoma: “Dada Su ni muumini wa kweli. Tafadhali, lazima umtafute na ushiriki naye injili ya Mungu ya ufalme….” Kusoma maneno haya kuliuchangamsha moyo wangu na machozi yangu hayakuweza kuacha kutiririka. Mama mkwe wangu aliguswa na kusema: “Kwa kweli jambo hili ni kwa msaada wa Bwana! Huu kweli ni upendo wa Bwana!” Huku nikimtazama dada huyu mdogo, mkarimu na mwaminifu, nilifikiria tena kuhusu maneno yenye kugusa, na ya dhati katika barua hiyo na niliweza kuhisi uharaka ambao kina ndugu walikuwa nao ili kushiriki nami injili ya kurudi kwa Bwana. Welewa wangu kutoka ndani ya nafsi yangu uliniambia kwamba upendo huu ulitoka kwa Mungu. Ni Mungu tu ndiye huthamini kila nafsi kwa njia hii na kujali sana kila mtu ambaye anamwamini Mungu kwa kweli. Na kwa hiyo, niliamua kwamba mara hii nitatafuta na kuchunguza kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Sikuweza kukataa tena tena. Nilimwambia kwa shauku: “Dada, ingia ndani uketi." Alikubali kwa kichwa kwa furaha, macho yake bado yaking'aa kwa machozi.

Tulikula, na kisha nilimpigia simu mfanyakazi mwenzangu Dada Zhang aje pia. Mume wangu alisikia kwamba tutakuwa na ushirika na akaomba siku ya kupumzika kazi pia. Dada huyo mchanga aliuliza kwa uchangamfu: “Dada, katika barua ya Ndugu Meng walisema kwamba walikuwa wamekuandikia barua kadhaa kuhusu kazi ya Mungu ya siku za mwisho, lakini hukuikubali. Najiuliza maoni yako juu ya jambo hili ni gani? Dada, ikiwa una matatizo yoyote, tafadhali yashiriki; tunaweza kufanya ushirika na kutafuta pamoja.” Nilisema: “Kwa kuwa unauliza, nitatoa hisia zangu na kushiriki nawe. Nimekuwa nikiogopa kudanganywa na Makristo wa uwongo wanaojitokeza katika kipindi cha siku za mwisho na kwa hiyo nimeshikilia kwamba 'wale wote wanaohubiri juu ya kuja kwa Bwana ni wa uwongo,' kwa hiyo sijachunguza kamwe kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Baadaye, nilifikiria kuhusu yale ambayo Ndugu Meng na wale wengine walisema katika barua zao, na kufikiria jinsi yalivyoleta maana. Kukataa injili yoyote ya kurudi kwa Bwana pasipo kufikiria kwa sababu Makristo wa uwongo wanajitokeza katika siku za mwisho kwa kweli ni kujikata pua ili kuunga wajihi wetu. Hata hivyo, ikiwa tunataka kukaribisha kurudi kwa Bwana, hatuwezi kuwa wasioweza kutambua kati ya Kristo wa kweli na Makristo wa uwongo. Kwa kuwa upo hapa, tafadhali fanya ushirika nasi kuhusu jambo hili.” Dada Zhang, mume wangu na mama mkwe wangu pia walikubali kwa vichwa vyao.

Kisha dada huyo alitusomea kifungu cha maneno ya Mungu, ambapo Mwenyezi Mungu alisema: “Kuchunguza kitu cha aina hii sio vigumu, lakini kunahitaji kila mmoja wetu ajue ukweli huu: Yeye Aliye mwili wa Mungu Atakuwa na dutu ya Mungu, na Yule Aliye Mungu katika mwili Atakuwa na maonyesho ya Mungu. Kwa maana Mungu Hupata mwili, Ataleta mbele kazi Anayopaswa kufanya, na kwa maana Mungu Amepata mwili, Ataonyesha kile Alicho na Ataweza kuuleta ukweli kwa mwanadamu, kumpa mwanadamu uhai, na Amwonyeshe mwanadamu njia. Mwili usio na dutu ya Mungu kwa kweli sio Mungu mwenye mwili; kwa hili hakuna tashwishi. Kupeleleza kama kweli ni mwili wa Mungu mwenye Mwili, mwanadamu lazima aamue haya kutoka kwa tabia Yeye huonyesha na maneno Yeye hunena. Ambayo ni kusema, kama ni mwili wa Mungu mwenye mwili au la, na kama ni njia ya kweli au la, lazima iamuliwe kutokana na dutu Yake. Hivyo, katika kudadisi[a] iwapo ni mwili wa Mungu mwenye mwili, cha msingi ni kuwa makini kuhusu dutu Yake (Kazi Yake, maneno Yake, tabia Yake, na mengine mengi), bali sio hali ya sura Yake ya nje. Mwanadamu akiona tu sura Yake ya nje, na aipuuze dutu Yake, basi hilo linaonyesha upumbavu na ujinga wa mwanadamu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Dibaji). Baada ya kusoma maneno ya Mungu, dada huyu mdogo alisema katika ushirika: "Tunaweza kuona kutoka katika maneno ya Mwenyezi Mungu kuwa cha muhimu katika kutambua kati ya Kristo wa kweli na Makristo wa uwongo ni kuangalia asili zao. Hili linaweza kutambuliwa kutoka kwa kazi, maneno na tabia yao. Bwana Yesu alisema wakati mmoja: ‘Mimi ndiye njia, ukweli na uhai(Yohana 14:6). Bila shaka, kwa kuwa Yeye alikuwa Mungu katika mwili, Aliweza kuonyesha ukweli na kufanya kazi ya Mungu Mwenyewe; Aliweza pia kuonyesha tabia ya Mungu Mwenyewe na kile Anacho na alicho. Kama tu katika Enzi ya Neema, Bwana Yesu alionyesha ukweli mwingi, Akaonyesha tabia ya huruma na upendo hasa, na kutimiza kazi ya kuwakomboa wanadamu wote. Kutoka kwa kazi na maneno ya Bwana Yesu, na kutoka kwa tabia Aliyoonyesha, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yesu Kristo alikuwa ukweli, njia, na uzima, ya kwamba alikuwa Mungu Mwenyewe mwenye mwili. Sasa Mwenyezi Mungu amekuja na kuonyesha ukweli wote ili kuwatakasa na kuwaokoa wanadamu; Amefanya kazi ya siku za mwisho ya kuwahukumu na kuwaadibu watu. Maneno ya Mwenyezi Mungu yanafichua ukweli wa wanadamu kupotoshwa na Shetani na asili na kiini cha mwanadamu. Yanatuambia vipengele vyote vya ukweli kama vile kupata wokovu ni nini, mabadiliko ya tabia ni nini na njia ya kuyafanikisha, na vile vile hatima ya baadaye ya wanadamu ni gani na mwisho utakuwa vipi kwa kila aina za watu. Maneno Yake pia yanafichua siri za mpango wa usimamizi wa Mungu wa miaka elfu sita na kupata mwili, pia yanaonyesha tabia ya asili ya Mungu, nafsi Yake, na kile Anacho na alicho. Alimradi tusome maneno ya Mungu kwa bidii, tutaweza kuona kwamba maneno yaliyotamkwa na Mwenyezi Mungu ndiyo sauti ya Roho wa ukweli, njia ya hukumu katika siku za mwisho. Kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho imetimiza unabii katika Biblia, kama vile, ‘Lazima hukumu ianze katika nyumba ya Mungu(1 Petro 4:17). ‘Wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote(Yohana 16:13) na ‘Yeye ambaye ananikataa mimi, na hayakubali maneno yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho(Yohana 12:48). Ukweli ambao Mwenyezi Mungu ameonyesha, kazi ya kuwahukumu, kuwaadibu na kuwatakasa watu ambayo Amefanya, na tabia inayoonyeshwa na haki ambayo Mwenyezi Mungu ameonyesha yote yanathibitisha kikamilifu kwamba Mwenyezi Mungu ni onyesho la Kristo wa siku za mwisho. Lakini kinyume chake, Makristo wa uwongo hawana asili ya Mungu. Wengi wao wana pepo waovu au ni pepo fidhuli sana na pepo wabaya wasio na mantiki kabisa. Hawawezi kuonyesha ukweli ili kutoa riziki kwa watu, wala hawawezi kufanya kazi ya hukumu ili kuwatakasa watu. Wanaweza tu kuwadanganya wale watu wapumbavu, wasiojua, waliokanganyikiwa ambao wanataka kujaza tumbo zao kwa mkate ili kuzuia njaa kwa kuwaonyesha ishara na maajabu rahisi. Kwa hiyo, ni rahisi sana kwetu kutambua kati ya Kristo wa kweli na Makristo wa uwongo kwa kutumia kanuni hii moja: Kristo ndiye ukweli, njia na uzima. Jambo hili linakubaliana kabisa na mapenzi ya Mungu."

Nilipokuwa nikisikiliza ushirika wa dada huyo, nilifikiria haya tena na tena: "Nimemwamini Bwana miaka hii yote lakini kamwe sijawahi kusikia ushirika wa aina hii. Sasa maneno ya Mwenyezi Mungu yanazungumza kuhusu kutambua kati ya Kristo wa kweli na Makristo wa uwongo kikamilifu sana; inaonekana kana kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu yanaweza kwa kweli kuwa sauti ya Roho Mtakatifu. Ee Bwana! Siku zote nimekuwa nikingojea kwa hamu kurudi Kwako, lakini miaka hii michache iliyopita nimesisitiza tu kujihadhari dhidi ya Makristo wa uwongo na sijakuwa na moyo wa kutosha wa kutafuta. Sijawahi kuchunguza kurudi Kwako kufanya kazi ya hukumu katika siku za mwisho kama Kanisa la Mwenyezi Mungu linavyoshuhudia, lakini nilipinga na kulaani jambo hilo pasipo na kufikiria. Bwana, je, nimekupuuza kwa kweli?” Wazo hili liliufanya moyo wangu uanze kupiga kwa kasi. Nilihisi hali ya hofu na sikuweza tena kuketi nikiwa nimetulia, kwa hiyo niliinuka na kwenda jikoni ili kujifanya kuleta maji, nikijaribu kujituliza kidogo. Huku nikimimina maji, nilitafakari: “Dada huyu ni mchanga sana, lakini ushirika wake kuhusu ukweli ni wa vitendo sana. Kina ndugu wa Shandong pia walipiga hatua haraka sana baada ya kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu. Ufahamu wao kuhusu Biblia na maarifa kuhusu kazi ya Mungu yalikuwa bora zaidi kuliko yangu. Njia hii inawaruhusu watu kuelewa ukweli na kupata maarifa kuhusu kazi ya Mungu. Je, hii si kazi ya Mungu?” Nilipofikiria haya yote, nilihisi kusisimka na kujuta pia. Nilikumbuka kuhusu nilipokuwa nikiwaandikia kina ndugu barua hizo huko Shandong. Nilikuwa nikitia tahabibu kalamu yangu, nikiwakaripia kwa sauti ya majivuno. Na katika mtazamo wangu wa kurudi kwa Bwana, si kwamba tu nilishindwa kutafuta ukweli na kukubali ushirika wa kina ndugu, lakini badala yake, niliendelea kuukanusha na kuukata. Nilijichukulia kuwa bwana wa ukweli na kuwataka ndugu wote wanisikilize, pia nilifikiria kuwa nilikuwa nikifanya kila linalowezekana kutetea njia ya kweli. Kamwe haikuwahi kunijia mawazoni kwamba nilikuwa nikimpinga Mungu. Kwa hiyo, je, jambo hilo halinifanyi kuwa Mfarisayo wa siku hizi? Wakati huo, nilihisi kana kwamba nilikuwa nimeloweshwa kwa maji baridi kutoka utosini hadi vidoleni; nilihisi legevu na dhaifu kote. Mikono yangu yote miwili ilikuwa ikitetemeka bila kudhibitika na niliendelea kurudia kucheza picha za mimi kumpinga Mungu akilini mwangu tena na tena…. Sikuweza kujizuia tena—machozi yalianza kutiririka kutoka kwa macho yangu. Nilijichukia kwa kuwa mwenye majivuno sana na kuwa kipofu. Baada ya muda mrefu, nilifuta machozi yangu na kurudi chumbani nikiwa na trei ya glasi za maji. Dada huyo alinitazama na kuniuliza kwa kujali: “Dada, je, unakubali ushirika huu?" Nilishusha pumzi na kusema kwa kujilaumu: “Baada ya kusikiliza maneno ya Mwenyezi Mungu na ushirika wako hivi sasa, ninahisi kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Bwana Yesu aliyerudi. Nimesubiri kila siku kurudi kwa Bwana lakini sikudhani kamwe kuwa sasa Bwana amerudi, kwa kweli ningetekeleza wajibu wa Mfarisayo. Kwa kweli nimefanya uovu mkubwa! Nimemkataa Mungu.” Kisha nilianza kulia sana kiasi kwamba singeweza kuzungumza.

Baadaye, baada ya muda fulani kutumika kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu, mimi, Dada Zhang, mama mkwe wangu, na mume wangu tulikuwa na hakika kabisa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Bwana Yesu aliyerudi. Nilifurahia sana kiasi kwamba niliwatumia ndugu wa Shandong barua ya tano kwa msisimko: “Ndugu wapendwa! Namshukuru Mungu kwamba kupitia ninyi kushiriki nami injili ya Mungu ya ufalme mara nyingi, sasa nimekubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho na nimekuwa mshiriki wa Kanisa la Mwenyezi Mungu. Ingawa nimeikubali baadaye kuwaliko, sitaki kuachwa nyuma. Nitatia bidii yangu yote ili niwafikie….” Wakati huo, nilihisi kana kwamba moyo wangu ulikuwa ukirudi Shandong pamoja na barua ili kukusanyika pamoja kwa karibu na ndugu zangu waliokuwa huko. Shukrani ziwe kwa Mungu kwa upendo Wake!

Tanbihi:

a. Nakala halisi ya mwanzo inasema “na kwa.”

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Sauti Hii Yatoka Wapi?

Na Shiyin, ChinaNilizaliwa katika familia ya Kikristo, na jamaa wangu wengi ni wahubiri. Nilimwamini Bwana pamoja na wazazi wangu tangu...

Nimekaribisha Kurudi Kwa Bwana

Na Chuanyang, Vereinigte StaatenMajira ya baridi kali ya mwaka wa 2010 huko Amerika yaliniacha nikihisi baridi sana. Kando na baridi kali...

Bwana Ameonekana Mashariki

Na Qiu Zhen, ChinaSiku moja, dadangu mdogo alinipigia simu akisema kwamba alikuwa amerudi kutoka kaskazini na kwamba alikuwa na jambo...

Kukutana na Bwana Tena

Na Jianding, AmerikaNilizaliwa katika familia ya Kikatoliki, na tangu nikiwa na umri mdogo mamangu alinifunza kusoma Biblia. Wakati huo,...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp