Je, Mwokozi Atakaporudi, Bado Ataitwa Yesu?

23/04/2023

Katika siku za mwisho, Mwokozi Mwenyezi Mungu tayari amekuja duniani, Ameonyesha ukweli, na kuonekana na kufanya kazi ili kuwaokoa wanadamu kikamilifu. Tangu kitabu Neno Laonekana katika Mwili kilipowekwa mtandaoni kwa ajili ya ulimwengu, watu kutoka kila sehemu wameona kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu ni ukweli na wamesikia sauti ya Mungu. Huenda hawajauona uso wa Mwenyezi Mungu, lakini wana hakika kwamba maneno Yake yote ni maneno ya Roho Mtakatifu, kwamba huyu ni Mungu anayezungumza na wanadamu, na Neno kuonekana katika mwili. Hatimaye wameshuhudia kuonekana kwa Mwana wa Adamu na kazi Yake, na wamepata nyayo za Mungu. Wakiwa na msisimko, wote wanakwenda kila mahali kwa haraka kueneza habari, wanamkubali Mwenyezi Mungu kwa shangwe, na kuja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Wao hula na kunywa maneno ya sasa ya Mungu kila siku, wakipata nuru zaidi wanaposoma, na kufurahia kunyunyiziwa na kuchungwa na maneno ya Mungu. Wao hujifunza ukweli na imani yao inakua. Wanafanya hima kueneza jina la Mwenyezi Mungu, wakitoa ushuhuda kwamba Mwokozi amekuja ulimwenguni kuwaokoa mwanadamu. Wamejawa na imani na nguvu na wao hupata faraja kutoka katika maneno ya Mwenyezi Mungu. Wana lengo sahihi katika ufuatiliaji na mwelekeo wao maishani, na wanajitolea kwa dhati kwa ajili ya Mungu, na kutoa ushuhuda kwa Mungu. Watu wengi ulimwenguni kote wanazidi kuchunguza njia ya kweli. Sasa kwa kuwa maafa ya kila aina yanaanza kuja kwa wingi, kila mtu analazimika kutafuta njia ya kweli, nyayo za Roho Mtakatifu, na kuonekana kwa Mwokozi na kazi Yake. Huu ni mwelekeo usioepukika. Katika jumuiya za kidini kutoka kila nchi ulimwenguni, wengi wanakubali njia ya kweli na kumgeukia Mwenyezi Mungu kila siku. Kanisa la Mwenyezi Mungu linaanzishwa katika nchi nyingi, na kutimiza kikamilifu mstari huu katika Isaya: “Na itatimia katika siku za mwisho, kwamba mlima wa nyumba ya Yehova utawekwa imara juu ya milima, na utainuliwa juu zaidi ya vilima; na mataifa yote yatamiminika kwenda kwake(Isaya 2:2). Ingawa wengi wanachunguza kwa hamu njia ya kweli, kuna wengine ambao wamethibitisha kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu ni ukweli, kwamba yana mamlaka na nguvu, lakini wanapoona kwamba Mwenyezi Mungu ana sura ya mtu wa kawaida, kwamba hajaonekana akiwa na umbo la kiroho la Bwana Yesu wala hajafanya miujiza, wanakwama katika hilo na kukataa kumkubali. Na baadhi ya watu wanaona bila shaka yoyote kwamba maneno yote ya Mwenyezi Mungu ni ukweli, lakini kwa sababu hayajaandikwa ndani ya Biblia, hawawezi kuwa na hakika kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Bwana Yesu aliyerudi. Hapa ndipo wanapokwama, na hawamkubali. Bado kuna wengine wanaokiri kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli na yanatoka kwa Mungu, lakini wanapoona kwamba Biblia inasema “Yesu Kristo ni yuyo huyo jana, na leo na daima” (Waebrania 13:8), wanaamini jina Yesu halitabadilika kamwe. Wanafikiri kwamba Mwenyezi Mungu haitwi Yesu, na Biblia haikutaja kamwe jina Mwenyezi Mungu, kwa hivyo hawakubali kwamba Yeye ndiye Mwokozi aliyeshuka. Wanafikiri kwamba kumkubali Mwenyezi Mungu kutakuwa kumsaliti Bwana Yesu, kwa hivyo wanakwama katika hilo, na hawamkubali. Hali hizi zote tatu zinarejelea tatizo moja la msingi: Mwenyezi Mungu anaonekana tu kama mtu wa kawaida, na kila kitu Anachosema ni ukweli, na Ana nguvu na mamlaka, lakini Yeye haitwi Yesu na hajaonekana katika umbo la kiroho la Yesu, hivyo hawakubali kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Bwana Yesu aliyerudi. Hili linaeleweka kwa kuzingatia tu fikira na mawazo ya mwanadamu, lakini kuonekana kwa Mungu na kazi Yake vina mafumbo makubwa ambayo wanadamu hawawezi kuyafahamu. Bila kutafuta ukweli, na kuamua mambo kulingana na maneno ya Mungu na ukweli wa kazi Yake, mtu hawezi kupata jibu sahihi. Kushikilia maandishi halisi ya Biblia na mawazo yao kwa upofu, kukataa kumkubali Kristo anayeonyesha ukweli kutaleta matokeo yasiyowazika. Hii ni sawa tu na wale katika imani ya Kiyahudi waliokataa kuukubali ukombozi wa Bwana Yesu na wakalaaniwa. Somo hili la kuhuzunisha limekuwa mbele yetu kwa muda mrefu. Sasa kwa kuwa Mwokozi amekuja, tunaweza kufikiri matokeo ya kushindwa kutafuta ukweli yatakuwaje. Je, Mwokozi bado ataitwa “Yesu” atakaporudi? Nitashiriki ufahamu wangu mdogo kuhusu mada hii.

Kwanza tunahitaji kuelewa jinsi ya kuthibitisha kuwa huyu ni Mwokozi aliyeshuka. Hatuwezi tu kuongozwa na iwapo ana jina la Bwana Yesu, na iwapo anafanana na Bwana Yesu. Kilicho muhimu ni kama Anaweza kuonyesha ukweli na kufanya kazi ya Mungu, na iwapo Anaweza kuwatakasa na kuwaokoa wanadamu. Almradi Anaweza kuonyesha ukweli, kuonyesha sauti ya Mungu na kufanya kazi ya kuwaokoa wanadamu, haijalishi Anaitwaje au Anaonekana wa kawaida kiasi gani. Tunaweza kuwa na hakika huyu ni Mungu katika mwili, Bwana Yesu aliyerudi. Yeye ni Mwokozi aliyekuja duniani. Tukiongozwa tu na jina Lake au sura Yake ya nje ni rahisi sana kukosea. Sote tunajua kwamba Mungu alitumia jina Yehova katika Enzi ya Sheria, na jina Yesu katika Enzi ya Neema. Hakuitwa tena Yehova, badala yake aliitwa Yesu, lakini Bwana Yesu alikuwa Yehova Mungu mwenye mwili. Alikuwa Yehova Mungu aliyevaa mwili kama Mwana wa Adamu, Aliyekuja kwa binadamu ili kuonekana na kufanya kazi. Bwana Yesu na Yehova Mungu walishiriki Roho mmoja, na walikuwa Mungu mmoja. Njia ya toba na mafumbo ya ufalme yaliyofichuliwa na Bwana Yesu, pamoja na kazi Yake ya ukombozi, vilithibitisha kabisa alikuwa Mungu katika mwili, kuonekana kwa Mungu mmoja wa kweli, na Mwokozi. Wale waliokuwa katika dini ya Kiyahudi hawakuweza kuona hilo wakati huo. Ingawa wengi wao walitambua kwamba njia ya Bwana Yesu ilikuwa na nguvu na mamlaka, kwa sababu Yeye hakuitwa “Masihi,” na Alionekana kama mtu wa kawaida, walimkana na kumhukumu. Bila kujali jinsi njia ya Bwana Yesu ilivyokuwa ya hali ya juu, hawakuitafuta au kuichunguza, bali walimshtaki kwa kukufuru, na hata kumfanya Asulubishwe. Walilaaniwa na kuadhibiwa na Mungu. Walikosea wapi? Hawakujua kupata mwili kulikuwa nini, na hawakujua uungu wa Mungu mwenye mwili ulidhihirishwa kwa kuonyesha ukweli, kwa hivyo bila kujali Mwana wa Adamu alionyesha ukweli kiasi gani au kazi Yake ilikuwa kuu kiasi gani, hawakuweza kumkubali Yeye kama Mungu. Walimfafanua kama mwanadamu; walikuwa na hakika kabisa juu ya hili na walikataa kuamini. Kutokana na hilo, walikosa wokovu wa Mungu na kuishia kuadhibiwa na kulaaniwa. Je, huo si upumbavu na ujinga wa kibinadamu? Na sasa, ingawa wengi katika ulimwengu wa dini wanatambua kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu ni ukweli na yanatoka kwa Mungu, bado wanashikilia maana ya juu ya Maandiko, wakifuata fikira na mawazo yao, na kusisitiza kwamba Mungu anaitwa Yesu na hilo halitabadilika kamwe, na Ataitwa hivyo Atakaporudi. Kwa kuwa Mwenyezi Mungu haitwi Yesu, na hakuja juu ya wingu kwa mfano wa Yesu, wanakataa kabisa kukubali kwamba Yeye ni Bwana Yesu aliyerudi. Je, hawafanyi kosa sawa na la Wayahudi? Kwa sababu hiyo, bado hawajamkaribisha Bwana, hivyo wataanguka katika maafa makubwa, watajipiga vifua, wakilia, na kusaga meno yao. Matumaini yao ya kumkaribisha Bwana na kunyakuliwa kabla ya maafa hayatatimizwa kabisa. Je, hilo halisikitishi? Je, ni kweli kwamba jina la Mungu la Yesu halitabadilika kamwe? Je, hili linaungwa mkono na Biblia, na neno la Mungu? Kwa kweli, Biblia ilitabiri zamani kwamba Bwana atakuja akiwa na jina jipya. Kitabu cha Isaya kinatabiri waziwazi: “Na Watu wa Mataifa wataiona haki yako, nao wafalme wote watauona utukufu wako; na wewe utaitwa kwa jina jipya, jina ambalo kinywa cha Yehova kitalitamka(Isaya 62:2). Na kitabu cha Ufunuo kinasema: “Yule ambaye anashinda nitamfanya awe nguzo katika hekalu lake Mungu Wangu, na hatatoka nje tena: na nitaandika kwake jina lake Mungu wangu, na jina la mji wake Mungu Wangu, ambao ni Yerusalemu mpya, ambao hukuja chini kutoka kwa Mungu Wangu mbinguni: na nitaandika kwake jina langu jipya(Ufunuo 3:12). Mistari hii miwili inataja waziwazi Mungu kuwa na jina jipya. Kwa kuwa ni jina jipya, ambalo hajawahi kuwa nalo hapo awali, ni hakika kwamba Bwana atakaporudi hataitwa Yesu. Basi jina Lake jipya ni lipi? Ni Mwenyezi Mungu. Hii inalingana kikamilifu na unabii wa Ufunuo: “Mimi ndiye Alfa na Omega, Mwanzo na tena mwisho, ambaye yuko, na ambaye alikuweko, na ambaye atakuja, Mwenyezi(Ufunuo 1:8). “Haleluya: kwani Bwana Mungu mwenye uenzi hutawala(Ufunuo 19:6). Na katika mistari mingine mingi kama vile Ufunuo 4:8, 11:17, na 16:7, jina “Mwenye enzi” limetajwa. Bila shaka, Bwana anaporudi katika siku za mwisho, anaitwa Mwenye enzi, Mwenyezi Mungu. Hakuna shaka juu ya hili. Imani hii kwamba jina la Mungu la Yesu halitabadilika kamwe, kwamba Mwokozi wetu wa siku za mwisho ataitwa Yesu, ni dhana ya kibinadamu tu ambayo haipatani kabisa na ukweli.

Sasa, wengine wanaweza kuuliza kwa nini Mungu alibadilisha jina Lake. Hilo lina maana gani? Mwenyezi Mungu amefichua mafumbo haya yote ya ukweli. Hebu tuangalie maneno ya Mwenyezi Mungu ili kuelewa hili vyema zaidi. Mwenyezi Mungu anasema, “Wengine wanasema kwamba jina la Mungu halibadiliki, hivyo, mbona basi jina la Yehova likawa Yesu? Ilitabiriwa kuja kwa Masihi, hivyo mbona basi mwanadamu kwa jina Yesu alikuja? Mbona jina la Mungu lilibadilika? Kazi kama hiyo haikufanyika muda mrefu uliopita? Hawezi Mungu leo kufanya kazi mpya? Kazi ya jana inaweza kubadilishwa, na kazi ya Yesu inaweza kufuata baada ya hiyo ya Yehova. Haiwezi kazi ya Yesu kurithiwa na kazi nyingine? Ikiwa jina la Yehova linaweza kubadilishwa kuwa Yesu, basi jina la Yesu haliwezi kubadilishwa pia? Hakuna jambo lolote hapa lisilo la kawaida; ni kwamba tu watu ni punguani sana. Mungu daima atakuwa Mungu. Bila kujali mabadiliko ya kazi Yake na jina Lake, tabia na maarifa Yake hayabadiliki milele. Ikiwa unaamini kwamba Mungu anaweza tu kuitwa na jina Yesu, basi unajua machache sana(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Jinsi Gani Ambavyo Mwanadamu Ambaye Amemwekea Mungu Mipaka katika Fikira Zake Anaweza Kupokea Ufunuo wa Mungu?).

Katika kila enzi, Mungu Anafanya kazi mpya na huitwa kwa jina jipya; Je, anawezaje kufanya kazi sawa katika enzi tofauti? Itakuwaje Yeye kugandamana na yale ya zamani? Jina la Yesu lilichukuliwa kuwa la kazi ya ukombozi, hivyo bado Yeye Anaweza kuitwa kwa jina moja wakati Atarudi katika siku za mwisho? Je, bado Yeye Atafanya kazi ya ukombozi? Ni kwa nini Yehova na Yesu ni kitu kimoja, ilhali wanaitwa kwa majina tofauti katika enzi hizi tofauti? Je, si kwa sababu enzi za kazi Yao ni tofauti? Jina moja linawezaje kumwakilisha Mungu kwa ukamilifu wake? Kwa njia hii, lazima Mungu aitwe kwa jina tofauti katika enzi tofauti, lazima Atumie jina kubadilisha enzi na kuwakilisha hiyo enzi, kwa kuwa hakuna jina moja linaweza kumwakilisha Mungu mwenyewe kikamilifu. Na kila jina linaweza tu kuwakilisha kipengele cha wakati cha tabia ya Mungu katika enzi fulani; yote linahitaji kufanya ni kuwakilisha kazi Yake. Kwa hivyo, Mungu Anaweza kuchagua jina lolote ambalo linafaa tabia yake kuwakilisha enzi nzima(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maono ya Kazi ya Mungu (3)).

‘Yehova’ ni jina Nililolichukua wakati wa kazi Yangu kule Uyahudi, nalo linamaanisha Mungu wa Wayahudi (Wateule wa Mungu) Anayeweza kumhurumia mwanadamu, kumlaani mwanadamu, na kuyaongoza maisha ya mwanadamu. Linamaanisha Mungu anayemiliki nguvu kuu na Amejawa na hekima. ‘Yesu’ ni Imanueli, nalo linamaanisha sadaka ya dhambi iliyojawa na upendo, Amejawa na huruma, naye Anamkomboa mwanadamu. Alifanya kazi ya Enzi ya Neema, naye Anawakilisha Enzi ya Neema, na Anaweza tu kuwakilisha sehemu moja ya mpango wa usimamizi. … Yesu pekee ndiye Mkombozi wa wanadamu. Yeye ni sadaka ya dhambi ambayo ilimkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi. Yaani, jina la Yesu lilitoka katika Enzi ya Neema, nalo lilikuwepo kwa ajili ya kazi ya wokovu katika Enzi ya Neema. Jina la Yesu lilikuwepo ili kuwawezesha watu wa Enzi ya Neema kuzaliwa upya na kuokolewa, nalo ni jina mahsusi la wokovu wa binadamu wote(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya “Wingu Jeupe”).

Iwapo mwanadamu bado anatamani kuwasili kwa Yesu Mwokozi katika siku za mwisho, na bado anamtarajia Afike katika mfano aliochukua kule Uyahudi, basi mpango wote wa usimamizi wa miaka elfu sita ungekoma katika Enzi ya Ukombozi, nao usingeweza kuendelea zaidi. Siku za mwisho, hata zaidi, zisingeweza kufika, nayo enzi isingekomeshwa. Hiyo ni kwa sababu Yesu Mwokozi ni kwa ajili ya ukombozi na wokovu wa wanadamu peke yake. Nililichukua jina la Yesu kwa sababu ya watenda dhambi wote katika Enzi ya Neema, nalo si jina ambalo kwalo Nitawaangamiza wanadamu wote. Ingawa Yehova, Yesu, na Masihi yote yanawakilisha Roho Wangu, majina haya yanaashiria tu enzi tofauti katika mpango Wangu wa usimamizi, nayo hayaniwakilishi katika ukamilifu Wangu. Majina wanayoniita watu duniani hayawezi kueleza kwa ufasaha tabia Yangu nzima na yote Niliyo. Ni majina tofauti tu ambayo Ninaitwa katika enzi tofauti. Na hivyo, enzi ya mwisho—enzi ya siku za mwisho—itakapofika, jina Langu litabadilika tena. Sitaitwa Yehova, au Yesu, wala Masihi, lakini nitaitwa Mwenyezi Mungu Mwenyewe mwenye nguvu, na chini ya jina hili Nitatamatisha enzi nzima(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya “Wingu Jeupe”).

Sasa nadhani tunaweza kuona umuhimu wa Mungu kubadilisha jina Lake. Mungu daima ni mpya, kamwe Hazeeki, na kazi Yake daima husonga mbele. Jina Lake linaendelea kubadilika kadiri enzi inavyobadilika, na kazi Yake inapobadilika. Katika kila hatua ya kazi Yake, na kila enzi mpya, Mungu huchukua jina lenye maana maalum ili kuwakilisha kazi anayofanya na tabia Anayoonyesha katika enzi hiyo. Tunapoona hivyo, hatutamwekea Mungu mipaka ya kuwa na majina mawili tu ya Yehova na Yesu. Hatutamwekea Mungu mipaka kulingana na fikira na mawazo yetu. Sote tunajua kwamba kile Mungu anacho na alicho vinajumuisha vitu vyote. Yeye ni mwenye hekima na uweza! Hakuna lugha ya binadamu inayoweza kueleza haya, hivyo jina moja au mawili yanawezaje? Hakuna idadi ya majina ambayo inaweza kuwakilisha kikamilifu kile Mungu anacho na alicho. Hii ndiyo sababu Mungu huchukua jina tofauti katika kila enzi. Mungu Aliitwa Yehova katika Enzi ya Sheria, na Alitoa sheria na amri kwa jina hilo. Aliongoza maisha ya wanadamu duniani, Akawaruhusu kujua dhambi ni nini, jinsi wanavyopaswa kuishi, na jinsi wanavyopaswa kumwabudu Yehova Mungu. Yehova ni jina ambalo Mungu aliteua kwa ajili ya Enzi ya Sheria, na liliwakilisha tu kazi Yake katika enzi hiyo, na tabia Zake za rehema, uadhama, na ghadhabu Alizoonyesha wakati huo. Mwishoni mwa Enzi ya Sheria, watu walizidi kupotoshwa na Shetani, na walizidi kuwa wenye dhambi. Hakuna aliyeweza kufuata sheria. Iwapo hilo lingeendelea, wote wangehukumiwa na kuuawa chini ya sheria. Ili kuwakomboa wanadamu, Mungu binafsi alifanyika mwili kama Mwana wa Adamu ili kufanya kazi, kufanya kazi ya ukombozi Akitumia jina Yesu. Alianzisha Enzi ya Neema na kutamatisha Enzi ya Sheria. Bwana Yesu aliwaletea wanadamu njia ya toba na akasamehe dhambi zetu, na kutupa amani na furaha, na neema ya ajabu. Hatimaye, Alisulubishwa, na kuwakomboa wanadamu wote. Yesu ni jina la Mungu lililoteuliwa kwa ajili ya Enzi ya Neema, na liliwakilisha kazi Yake ya ukombozi katika enzi hiyo pamoja na tabia Yake ya upendo na rehema. Kutoka katika hatua hizi mbili za kazi ya Mungu tunaweza kuona kwamba kila jina Lake lina umuhimu maalum. Yanawakilisha kazi na tabia ya Mungu katika enzi hiyo mahususi. Hebu tufikirie hilo. Iwapo Bwana Yesu angeendelea kutumia jina Yehova katika Enzi ya Neema, kazi ya Mungu ingekoma katika Enzi ya Sheria. Kisha wanadamu wapotovu wasingekombolewa, na sote tungehukumiwa na kuuawa chini ya sheria kwa ajili ya dhambi zetu. Tusingeweza kufika leo. Ni vivyo hivyo katika siku za mwisho—kama Bwana Yesu angerudi akitumia jina Yesu, kazi ya Mungu ingebaki tu katika hatua ya ukombozi, na watu wangeweza tu kupata ukombozi wa Bwana Yesu na msamaha wa dhambi. Asili ya dhambi tuliyo nayo sote isingeweza kutatuliwa. Tusingekuwa na njia ya kuepuka dhambi na kutakaswa, na tusingestahili kamwe ufalme wa mbinguni. Bwana Yesu alitabiri kurudi Kwake katika siku za mwisho mara nyingi, kwamba Ataonyesha ukweli na kufanya kazi ya hukumu ili kuwatakasa wanadamu, kuwaokoa wanadamu kikamilifu kutokana na dhambi, na kutupeleka katika ufalme wa Mungu. Kama tu Bwana Yesu alivyosema, “Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno Yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa Mimi, na hayakubali maneno Yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho(Yohana 12:47-48). “Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati Yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, Atawaongoza hadi kwenye ukweli wote(Yohana 16:12-13). Kwa hivyo katika siku za mwisho, Mungu anapoanzisha enzi mpya na kazi Yake mpya, Je, kwa kweli bado ataitwa Yesu? La, hasha. Bwana Yesu amerudi katika siku za mwisho kufanya kazi kama Mwenyezi Mungu, Akianzisha Enzi ya Ufalme na kuhitimisha Enzi ya Neema. Anaonyesha ukweli ili kufanya kazi ya hukumu inayoanza na nyumba ya Mungu, ili kuwaokoa wanadamu kikamilifu kutokana na dhambi na kutokana na nguvu za Shetani, na kukamilisha kundi la washindi. Baada ya hapo, Atashusha maafa makubwa ili kuadhibu uovu na kutuza wema, kuondoa kabisa enzi nzee yenye uovu na giza, na kisha ufalme wa Kristo utatimizwa duniani. Hii inatimiza kikamilifu unabii wa Ufunuo: “Mimi ndiye Alfa na Omega, Mwanzo na tena mwisho, ambaye yuko, na ambaye alikuweko, na ambaye atakuja, Mwenyezi(Ufunuo 1:8). “Haleluya: kwani Bwana Mungu mwenye uenzi hutawala(Ufunuo 19:6).

Mwenyezi Mungu anasema, “Nilijulikana kama Yehova wakati mmoja. Pia niliitwa Masihi, na wakati mmoja watu waliniita Yesu Mwokozi kwa sababu walinipenda na kuniheshimu. Lakini leo Mimi si yule Yehova au Yesu ambaye watu walimfahamu nyakati zilizopita—Mimi ni Mungu ambaye Amerejea katika siku za mwisho, Mungu ambaye Ataikamilisha enzi. Mimi ni Mungu Mwenyewe ambaye Anainuka kutoka mwisho wa dunia, Nimejawa na tabia Yangu nzima, na Nimejawa na mamlaka, heshima na utukufu. Watu hawajawahi kushirikiana na Mimi, hawajawahi kunifahamu, na daima hawaijui tabia Yangu. Tangu uumbaji wa dunia hadi leo, hakuna mtu yeyote ambaye ameniona. Huyu ni Mungu anayemtokea mwanadamu katika siku za mwisho lakini Amejificha kati ya wanadamu. Anaishi kati ya wanadamu, ni wa kweli na halisi, kama jua liwakalo na moto unaochoma, Aliyejaa nguvu na kujawa mamlaka. Hakuna mtu au kitu chochote ambacho hakitahukumiwa kwa maneno Yangu, na mtu au kitu chochote ambacho hakitatakaswa kupitia moto unaowaka. Hatimaye, mataifa yote yatabarikiwa kwa ajili ya maneno Yangu, na pia kupondwa na kuwa vipande vipande kwa sababu ya maneno Yangu. Kwa njia hii, watu wote katika siku za mwisho wataona kuwa Mimi ndiye Mwokozi aliyerejea, Mimi ndiye Mungu Mwenyezi ambaye Anawashinda binadamu wote, nami Nilikuwa sadaka ya dhambi kwa mwanadamu wakati mmoja, lakini katika siku za mwisho Ninakuwa pia miale ya Jua linalochoma vitu vyote, na pia Jua la haki Linalofichua vitu vyote. Hivyo ndivyo ilivyo kazi Yangu ya siku za mwisho. Nilichukua jina hili nami Ninamiliki tabia hii ili watu wote wapate kuona kuwa Mimi ni Mungu mwenye haki, na Mimi ni jua linachoma, na moto unaowaka. Ni hivyo ili watu wote waweze kuniabudu, Mungu pekee wa kweli, na ili waweze kuuona uso Wangu wa kweli: Mimi si Mungu wa Wayahudi tu, na Mimi si Mkombozi tu—Mimi ni Mungu wa viumbe vyote katika mbingu na dunia na bahari(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya “Wingu Jeupe”).

Maneno ya Mwenyezi Mungu ni dhahiri kabisa. Yehova, Yesu, na Mwenyezi Mungu ni majina ya Mungu mmoja wa kweli. Anatumia majina tofauti katika Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Ingawa kazi Yake na jina Lake hubadilika kulingana na enzi, na Anaonekana kwa njia tofauti, kiini Chake hakibadiliki kamwe, na tabia Yake, na kile Anacho na alicho havitabadilika kamwe. Yeye ni Mungu mmoja milele, Roho mmoja, anayefanya kazi ya kuwaongoza, kuwakomboa na kuwaokoa wanadamu kikamilifu. Katika siku za mwisho, anapata mwili kama Mwenyezi Mungu, na ingawa Yeye Haitwi Yesu na anaonekana kama mtu wa kawaida, Ameonyesha ukweli wote unaowatakasa na kuwokoa wanadamu, na kufanya kazi ya hukumu inayoanza na nyumba ya Mungu. Yeye huwakumu na kuwafunua watu kwa maneno Yake, Akifichua kupotoshwa kwetu kwa kina na Shetani na asili yetu ya kishetani, na kutuonyesha vipengele vyote vya ukweli ambavyo tunahitaji ili kutakaswa na kuokolewa. Wateule Wake hula na kunywa maneno Yake kila siku, hukubali kuhukumiwa, kuadibiwa, kushughulikiwa, kujaribiwa, na kusafishwa na maneno Yake, na tabia zao potovu zinatakaswa na kubadilishwa polepole. Wanaondokana polepole na uovu na nguvu za Shetani, na kuokolewa kikamilifu na Mungu. Tayari Mwenyezi Mungu amekamilisha kundi la washindi kabla ya maafa, na kuonyesha kikamilifu hekima na uweza wa Mungu. Wakati wa kazi ya Mwenyezi Mungu, licha ya kuteswa kikatili na kukamatwa bila kikomo na vikosi vya kishetani vya Chama cha Kikomunisti pamoja na kushutumiwa na kukufuriwa vikali na nguvu za wapinga Kristo, injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu imeenea kutoka Mashariki hadi Magharibi, na kupitia ulimwengu mzima. Hii inaonyesha kwamba kazi kuu ya Mungu inakamilika, kwamba Mwenyezi Mungu anamshinda kabisa Shetani na kupata utukufu wote! Maafa makubwa tayari yameanza na ulimwengu wa kidini umevurugika, lakini wengi wao bado wanashikilia kwa ukaidi jina la Bwana Yesu, wakingoja Aje juu ya wingu. Bila kujali Mwenyezi Mungu anaonyesha ukweli kiasi gani, na kazi Yake ni kuu kiasi gani, wanakataa kukiri na kukubali hayo. Hata wanashutumu na kupinga vikali kuonekana Kwake na kazi Yake. Je, wana tofauti gani na wale Mafarisayo walioshikilia jina la Masihi, na kumpinga Bwana Yesu vikali? Je, wote kimsingi si watu wanaomsulubisha Mungu msalabani? Wanashikilia jina la Bwana Yesu bure, lakini wanampinga na kumhukumu Mwenyezi Mungu vikali. Je, unafikiri ni nini kinawasubiri mwishoni?

Ili kuhitimisha, hebu tutazame video ya maneno ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anasema, “Je, mngependa kujua kiini cha sababu ya Mafarisayo kumpinga Yesu? Je, mnataka kujua dutu ya Mafarisayo? Walikuwa wamejawa na mawazo makuu kuhusu Masiha. Kilicho zaidi, waliamini tu kuwa Masiha angekuja, ilhali hawakutafuta ukweli wa uzima. Na hivyo, hata leo bado wanamngoja Masiha, kwani hawana maarifa ya njia ya uzima, na hawajui ukweli ni nini. Ni vipi, hebu nielezeni, watu wapumbavu, wakaidi na washenzi kama hawa wangeweza kupata baraka za Mungu? Wangewezaje kumwona Masiha? Walimpinga Yesu kwa sababu hawakujua mwelekeo wa kazi ya Roho Mtakatifu, kwa sababu hawakuijua njia ya ukweli uliozungumziwa na Yesu, na zaidi, kwa sababu hawakumwelewa Masiha. Na kwa kuwa hawakuwa wamewahi kumwona Masiha na hawakuwa wamewahi kuwa pamoja na Masiha, walifanya kosa la kuning’inia bila mafanikio kwa jina la Masiha huku wakipinga dutu ya Masiha kwa kila njia iwezekanayo. Mafarisayo hawa kwa dutu walikuwa wakaidi, wenye kiburi na hawakutii ukweli. Kanuni ya imani yao kwa Mungu ni: Haijalishi mahubiri Yako ni makubwa vipi, haijalishi mamlaka Yako ni makubwa vipi, Wewe si Kristo iwapo Huitwi Masiha. Je, maoni haya si ya upuuzi na ya kudhihaki? Nawauliza tena: Je, si rahisi sana kwenu kufanya makosa ya Mafarisayo wa mbeleni zaidi, kwa kuwa hamna ufahamu hata kidogo kumhusu Yesu? Je, unaweza kuitambua njia ya ukweli? Je, unaweza kutoa uhakika kweli kuwa hutampinga Kristo? Je, una uwezo wa kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu? Kama hujui iwapo utampinga Kristo, basi Nasema kuwa tayari unaishi kwenye ukingo wa kifo. Wale wote ambao hawakumfahamu Masiha walikuwa na uwezo wa kumpinga Yesu, wa kumkataa Yesu, wa kumpaka Yeye tope. Watu wote wasiomwelewa Yesu wako na uwezo wa kumkana, na kumtusi. Zaidi, wako na uwezo wa kuona kurejea kwa Yesu kama uwongo wa Shetani, na watu zaidi watamshutumu Yesu aliyerudi kwa mwili. Je, haya yote hayawafanyi muogope? Mtakachokumbana nacho kitakuwa kumkufuru Roho Mtakatifu, kuharibiwa kwa maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa, na kukataliwa kwa dharau ya yale yote ambayo yamedhihirishwa na Yesu. Mnaweza kupata nini kutoka kwa Yesu kama mmetatizwa kwa namna hii? Mtaielewaje kazi ya Yesu atakaporudi kwa mwili kwa wingu jeupe, kama mnakataa katakata kuona makosa yenu? Nawaambieni hili: Watu wasioukubali ukweli, ilhali wanangoja kufika kwa Yesu juu ya wingu jeupe kwa upofu, kwa hakika watamkufuru Roho Mtakatifu, na ni kundi ambalo litaangamizwa(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kufikia Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu, Mungu Atakuwa Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia).

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Kupata Mwili Ni Nini?

Sote tunajua kwamba miaka elfu mbili iliyopita, Mungu alikuja mwilini katika ulimwengu wa mwanadamu kama Bwana Yesu ili kuwakomboa...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp