Bahati na Bahati Mbaya

29/01/2018

Na Dujuan, Japani

Nilizaliwa katika familia fukara katika kijiji cha mashambani. Tangu niwe mtoto, niliishi maisha magumu na nilidharauliwa na wengine. Wakati mwingine sikujua hata kama ningepata chakula changu cha kufuatia, sembuse kumbwe na vitu vya watoto kuchezea. Kwa kuwa familia yangu ilikuwa fukara, nilipokuwa mdogo, ningevaa nguo zilizokuwa zikivaliwa na dadangu mkubwa awali. Nguo zake mara nyingi zilikuwa kubwa sana kwangu. Kama matokeo, nilipoenda shuleni, watoto wengine wangenicheka na hawangecheza na mimi. Utoto wangu ulikuwa mchungu sana. Kuanzia wakati huo kuendelea, ningejiambia kwa siri: Mara nitakapokuwa mtu mzima, nitakuwa mtu wa sifa na kupata pesa nyingi. Sitaruhusu wengine kunidharau tena. Kwa sababu familia yangu haikuwa na fedha, nililazimika kuacha shule kabla ya shule ya upili. Nilienda mji wa jimbo ili kufanya kazi katika kiwanda cha dawa. Ili kupata pesa zaidi, mara nyingi ningefanya kazi hadi saa tatu au nne usiku. Hata hivyo, fedha nilizopata hazikuwa za kutosha kufikia malengo yangu. Baadaye, niliposikia kwamba dada yangu alikuwa na uwezo wa kupata katika siku tano pesa nilizopata kwa mwezi kutokana na kuuza mboga, niliacha kazi yangu katika kiwanda cha dawa na nilikwenda kuuza mboga. Baada ya muda, nilipata kwamba ningeweza kupata hata pesa nyingi zaidi kwa kuuza matunda, kwa hiyo niliamua kuanza biashara kuuza matunda. Baada ya kuolewa na mume wangu, tulianzisha biashara ya mkahawa. Nilidhani kuwa kwa vile sasa nilikuwa na mkahawa, ningeweza kupata hata pesa zaidi. Mara nilipoweza kupata kiasi kikubwa cha mapato, kwa kawaida, ningeweza kushinda pendo na staha ya wengine. Watu wengine wangeanza kuniheshimu na wakati huo huo, ningeweza kuishi maisha bora zaidi. Hata hivyo, baada ya kuendesha biashara hiyo kwa kipindi cha muda, niligundua kuwa kwa hakika sikuwa natengeneza fedha nyingi. Nilianza kupata wasiwasi. Ni lini ningeweza kuishi maisha ambayo wengine wangependa?

Mnamo mwaka 2008, kwa bahati nilisikia rafiki akisema kuwa kufanya kazi kwa siku moja huko Japani ilikuwa sawa na kufanya kazi kwa siku kumi nchini China. Nilipopata habari hii, nilifurahi sana. Nilihisi kuwa hatimaye, nilikuwa nimepata nafasi nzuri ya kupata pesa. Nilifikiri kuwa ni lazima nipate faida zaidi kwa kutoa kile kidogo zaidi. Kila nilichohitaji kufanya ni kwenda Japani kufanya kazi na ningeweza kufidia gharama zangu. Ili kufanikisha ndoto zetu, mimi na mume wangu hatukujali ada ya wakala ingekuwa kiasi gani. Tuliamua kwenda Japani mara moja. Baada ya kufika Japani, tuliweza kupata kazi haraka sana. Kila siku, mimi na mume wangu tulifanya kazi kwa saa 13 au 14. Dhiki ya kazi ilikuwa nyingi sana. Nilikuwa nimechoka kabisa siku nzima. Baada ya kazi, kile nilichotaka kufanya ilikuwa kulala na kupumzika. Sikutaka hata kula. Niliona vigumu kuvumilia maisha ya upesi sana kama hayo. Hata hivyo, mara nilipofikiri kuhusu fedha ambazo ningepata baada ya kujitahidi kwa miaka michache, nilijihimiza: Ingawa ni magumu na yenye uchovu sasa hivi, baadaye, maisha yangu yatakuwa ya ajabu. Lazima niendelee. Matokeo yake, kila siku nilifanya kazi kwa bidii kabisa ni kama kwamba mimi nilikuwa mashine ya kutengeneza fedha. Kufikia mwaka wa 2015, niliporomoka kwa ajili ya mzigo wa kazi nzito. Nilikwenda kwa hospitali kwa ajili ya uchunguzi na daktari aliniambia kuwa nilikuwa na gegedu iliyochomoka na kwamba ilikuwa ikiufinya mshipa wangu. Kama ningeendelea kufanya kazi nilivyokuwa nikifanya kazi, hatimaye ningekuwa mgonjwa kitandani na singeweza kujitunza mwenyewe. Habari hii ilinigonga kama radi kutoka anga lisilo na mawingu. Nilikuwa mdhaifu sana wakati huo huo. Maisha yangu yalikuwa yameanza tu kuwa bora zaidi, na nilikuwa nikiikaribia ndoto yangu zaidi. Sikuwahi kudhani kwamba ningekuwa mgonjwa. Nilikataa kufa moyo. Nilifikiri: “Mimi bado ni mdogo. Nahitaji tu kujikaza kisabuni na kupita haya. Nisipopata pesa zaidi sasa, wakati nitakapokwenda nyumbani, sitakuwa na pesa nyingi. Je! Hiyo haitakuwa aibu zaidi?” Matokeo yake, nilijikaza kisabuni na kuukokota mwili wangu dhaifu kurudi kazini. Hata hivyo, baada ya siku chache, nilikuwa mgonjwa sana kiasi kwamba singeweza kuinuka.

Nilihisi huzuni sana nilipokuwa nikilala kitandani katika hospitali bila mtu yeyote wa kunitunza. “Je, ninaishiaje kuwa katika hali hii? Inawezekana kuwa mimi hakika siwezi kutoka kitandani?” Kwa kweli nilikuwa na matumaini ya kuwa na mtu kando na mimi. Kwa bahati mbaya, mume wangu alikuwa kazini na mtoto wangu alikuwa shuleni. Bosi wangu na wenzangu walizingatia faida tu. Wao kimsingi hawakujali kunihusu. Wadi ilikuwa imejaa kila aina ya wagonjwa. Sikuweza kujizuia ila kufikiri kwa undani: Watu wanaishikwa sababu ipi? Mtu anawezaje kuishi maisha yenye maana? Pesa inaweza kununua furaha kweli? Nilitafakari kile nilichokuwa nacho baada ya miaka 30 ya kujitahidi. Nilifanya kazi katika kiwanda cha dawa, nikauza matunda, niliendesha mkahawa na nikaja Japani kufanya kazi. Hata ingawa nilipata pesa kiasi kwa miaka hii yote, hata hivyo, nilivumilia huzuni sana. Nilikuwa nimedhani kwamba mara ningefika Japani, ningeweza kufanikisha ndoto zangu haraka sana. Baada ya miaka michache huko Japani, niliporejea China, ningeweza kuanza maisha mapya kama mtu tajiri na kuonewa kijicho na watu wengine. Hata hivyo, sasa nilikuwa mgonjwa kitandani na nilikumbwa na uwezekano wa kuwa singeweza tena kuwa na uwezo wa kujitunza mwenyewe na kwamba ningeshinda katika kiti cha gurudumu kwa nusu ya pili ya maisha yangu…. Nilipowaza hili, nilianza kuomboleza kwamba nilikuwa nimehatarisha hata maisha yangu mwenyewe ili kupata fedha na kusonga mbele katika maisha. Kadri nilivyofikiri juu ya hili, ndivyo machozi ya uchungu yalivyoanza kumwagika usoni mwangu. Katika uchungu, sikuweza kujizuia ila kulia: Mungu! Niokoe mimi! Kwa nini maisha ni katili hivi?

Wakati tu nilipokuwa katika maumivu na sikuwa na uwezo, ndio wakati ambao wokovu wa Mwenyezi Mungu ulinijia na “ugonjwa” wangu ukawa “baraka” yangu. Ni bahati kuu iliyoje kwamba nilijua kuhusu dada watatu kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu. Kwa kuwa walikuwa wamewasiliana nami, nilielewa kule ambako ugonjwa wangu ulikuwa unatoka na nilijua kule ambako mateso yangu yalikuwa yanatoka. Kama mtu ambaye hakuwa na imani yoyote kabla, sasa nilikuwa mtu ambaye alikuwa na mwelekeo wa maisha na nilijua nani nilipaswa kuishi kwa sababu yake. Dada huyo alisoma kifungu cha maneno ya Mwenyezi Mungu kwa ajili yangu: “Uchungu wa kuzaliwa, kufa, magonjwa na uzee uliopo katika maisha yote ya mwanadamu ulitoka wapi? Ni kwa sababu ya nini ndio watu walikuwa na vitu hivi mwanzo? Je, mwanadamu alikuwa na vitu hivi alipoumbwa mara ya kwanza? Hakuwa navyo, sivyo? Hivyo, vitu hivi vilitoka wapi? Vitu hivi vilikuja baada ya wanadamu kujaribiwa na Shetani na miili yao ikasawijika. Uchungu wa mwili, mateso yake na utupu wake, na pia masuala yenye taabu sana ya dunia ya binadamu yote yalikuja baada ya wanadamu kupotoshwa na Shetani, kutoka wakati Shetani alipoanza kuwatesa watu; matokeo yalikuwa kwamba walisawijika zaidi na zaidi. Maradhi ya wanadamu yakawa makubwa zaidi na mateso yao yakawa makali zaidi. Watu zaidi walihisi utupu na tanzia ya dunia ya binadamu na vilevile kutoweza kwao kuendelea kuishi hapo, na walihisi matumaini madogo zaidi kwa dunia. Yote haya yalikuja baada ya kupotoshwa na Shetani(“Umuhimu wa Mungu Kuuonja Mateso ya Dunia” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Mmoja wa akina dada hao aliniambia kuwa wakati mwanadamu alipoumbwa mwanzoni, mwanadamu hakuwa na maumivu ya kuzaliwa, kifo, ugonjwa na uzee wala hakuwa na wasiwasi na shida. Badala yake, aliishi maisha yasiyo na mawazo katika Bustani ya Edeni, akifurahia mambo yote mazuri ambayo Mungu alimpa mwanadamu. Hata hivyo, mwanadamu alimsaliti Mungu na hakumsikiliza tena Mungu kuanzia wakati mwanadamu alipodanganywa na kupotoshwa na Shetani. Mungu hakumchunga tena, kumlinda na kumbariki mwanadamu na aliishi chini ya umiliki wa Shetani. Aliishi kulingana na sheria za Shetani. Alianza kuishi kwa ajili ya umaarufu, hali, pesa. Kwa hiyo sisi wanadamu tulipanga njama dhidi ya sisi kwa sisi. Tulipigana kwa ukali. Tulidanganyana, na hata tuliuana. Hapa ndipo ambapo ugonjwa wetu, shida katika maisha yetu, na maumivu na huzuni ndani ya mioyo yetu vilikuwa vinatoka. Maumivu na dhiki hii husababisha kila mtu kuhisi kwamba maisha duniani ni machungu sana, yenye kuchosha na magumu. Mambo haya yote yalitokea baada ya Shetani kumdanganya mwanadamu. Ni Shetani ndiye anayetuumiza. Baada ya kusikiliza kile ambacho dada alikuwa nacho kusema, nilikuja kuelewa: Mwanzoni, tulikuwa tunaishi chini ya baraka za Mungu. Maisha yetu yalikuwa yenye furaha na hapakuwa na ugonjwa au shida. Baada ya Shetani kutupotosha, tulipoteza ulinzi wa Mungu na tukaanza kuwa wagonjwa na tukaanza kuvumilia kila aina ya mateso. Wakati huo, nilihisi kweli kwamba Shetani alikuwa mwenye kuchukiwa sana. Nilielewa pia kwamba maumivu niliyokuwa nikiteseka miaka hii yote yalitokea kwa Shetani.

Dada huyo aliendelea kuwasiliana na mimi: “Mungu hawezi kuvumilia kumwona mwanadamu akiendelea kupotoshwa na kuumizwa na Shetani. Yeye amepata mwili mara mbili miongoni mwa wanadamu ili kutukomboa na kutuokoa. Hasa katika siku za mwisho, Kristo mwenye mwili ameonyesha mamilioni ya maneno; ni ukweli unaowaruhusu watu kujiweka huru dhidi ya kupotoshwa na Shetani, watakaswe na kuokolewa kikamilifu. Mradi tu tunamsikiliza Mungu na kuuelewa ukweli ndani ya neno la Mungu, tutaweza kutofautisha na kuona wazi njia zote na namna ambazo Shetani huwapotosha wanadamu. Tutaweza kung’amua asili ovu ya Shetani na kuwa na nguvu ya kumwacha Shetani, kutupa madhara ya Shetani, kurudi mbele ya Mungu, kupata wokovu wa Mungu na hatimaye, kuletwa na Mungu katika hatima nzuri.” Niliposikia kwamba Mungu alikuwa amekuja binafsi kuwaokoa wanadamu, nilikuwa na hisia nyingi. Kwa kuwa sikutaka Shetani aendelee kunidhuru, niliwaambia dada zangu kuhusu maumivu yangu na shaka: “Sielewi tu. Ni kwa nini nahisi maumivu mengi kutoka kutafuta kuwa bora zaidi kuliko kila mtu mwingine? Inawezekana kuwa hii ni kutokana na Shetani pia?” Dada huyo alinisomea zaidi ya maneno ya Mungu: “Mtu yeyote aliye mkubwa ama maarufu, watu wote kwa hakika, chochote wanachofuata maishani kinahusiana tu na haya maneno mawili: ‘umaarufu’ na ‘faida.’ Watu hufikiri kwamba punde tu wanapata umaarufu na faida, wanaweza basi kuyatumia kwa faida yao kufurahia hadhi ya juu na utajiri mwingi, na kufurahia maisha. Baada ya wao kuwa na umaarufu na faida, wanaweza basi kuyatumia kwa faida yao katika kutafuta kwao raha na kufurahia kwao kwa fidhuli mwili. Watu kwa hiari, lakini bila kujua, wanachukua miili na akili zao na vyote walivyonavyo, siku zao za baadaye, na kudura zao na kuzikabidhi zote kwa Shetani ili kupata umaarufu na faida wanayotaka. Watu kweli hufanya hivi kamwe bila kusita kwa muda, kamwe bila kujua haja ya kupata tena yote. Je, watu bado wanaweza kujidhibiti baada ya wao kumkimbilia Shetani na kuwa mwaminifu kwake kwa njia hii? Bila shaka, la. Wanadhibitiwa na Shetani kikamilifu na kabisa. Pia kikamilifu na kabisa wamezama katika bwawa na hawawezi kujinusuru. Baada ya mtu kukwama katika umaarufu na faida, hatafuti tena kile kilichong’aa, kile chenye haki ama yale mambo ambayo ni mazuri na mema. Hii ni kwa sababu nguvu za ushawishi ambazo umaarufu na faida yanayo juu ya watu ni kubwa mno, na vinakuwa vitu vya watu kutafuta katika maisha yao yote na pia milele bila kikomo. Hili si ukweli?(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI). Ufunuo wa neno la Mungu ulinifanya kuwa na mwanga wa ghafla wa utambuzi. Nilikuwa kielelezo bora zaidi cha mtu aliyekuwa mtumwa na Shetani, mtu ambaye alikuwa akijiharibu mwenyewe kwa njia ya kutafuta umaarufu na faida. Nilikuwa nimejipoteza mwenyewe katika kutafuta kuwa bora zaidi kuliko wengine na kupata pesa nyingi za kuonewa kijicho. Mimi kimsingi nikawa mashine ya kuunda fedha. Kwa sababu ya umaarufu na mali nilikuwa nimeitoa kafara afya yangu mwenyewe. Kwa kweli nilikuwa mtumwa wa umaarufu na faida. Nikiongozwa na mtazamo wa maisha ya kupata pesa na kuwa kitu cha kuonewa kijicho, nilijitahidi kutimiza malengo yangu hadi mwili wangu ulikuwa huwezi kustahimili tena. Tamaa hizi za umaarufu na faida zilinisababishia mateso mengi ya kimwili na ya kihisia. Isingekuwa ufunuo wa maneno ya Mwenyezi Mungu, nisingeweza kamwe kujua kwamba mambo niliyokuwa nikitaka yalikuwa mabaya. Kwa kweli, ilikuwa moja ya njia za Shetani za kumuumiza mwanadamu.

Hatua kwa hatua, akina dada hao walivyokuja kunitembelea mara kwa mara na kuwasilisha maneno ya Mwenyezi Mungu kwangu, nilikuwa na uhakika zaidi na zaidi ya kazi ya Mwenyezi Mungu. Wakati huo huo, nilikuwa bora zaidi katika kutofautisha mbinu na njia ambazo Shetani humdhuru mwanadamu. Katika wakati huu, niliona hali ya mmoja wa wenzi wangu wa kike. Ili kupata pesa, yeye na mumewe walikuja Japani kufanya kazi. Hata ingawa wote walikuwa wamepata pesa fulani, mumewe alianza kuwa na shida fulani za kimwili. Hakuwa na budi ila kurudi nyumbani kwa ajili ya matibabu. Matokeo yake ni kwamba aliopatikana kuwa na saratani ya hatua za mbele zaidi. Baada ya wao kujua kuhusu hili, hawakutaka tena kuja Japani tena kupata pesa. Familia nzima ilikuwa inaishi katika hofu na huzuni. Mwenyezi Mungu alisema: “Watu huishi maisha yao wakitafuta pesa na umaarufu; wanashikilia nyuzi hizi, wakifikiri kwamba ndizo mbinu zao pekee za msaada, ni kana kwamba wakiwa nazo wangeendelea kuishi, wangejitoa kwenye hesabu ya wale watakaokufa. Lakini pale tu wanapokuwa karibu kufa ndipo wanapotambua namna ambavyo vitu hivi vilivyo mbali na wao, namna walivyo wanyonge mbele ya kifo, namna wanavyosambaratika kwa urahisi, namna walivyo wapweke na wasivyoweza kusaidika, na hawana popote pa kugeukia. Wanatambua kwamba maisha hayawezi kununuliwa kwa pesa au umaarufu, kwamba haijalishi mtu ni tajiri vipi, haijalishi cheo chake kilivyo cha hadhi, watu wote ni maskini kwa njia sawa na wanaofanya mambo bila mpango mbele ya kifo. Wanatambua kwamba pesa haiwezi kununua maisha, kwamba umaarufu hauwezi kufuta kifo, kwamba si pesa wala umaarufu vinaweza kurefusha maisha ya mtu kwa hata dakika moja, hata sekunde moja(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III). Bahati mbaya ya wenzi wangu ilinifanya nihisi hata zaidi kuwa maisha kweli yalikuwa ya thamani. Wakati uo huo, ningeweza kuona jinsi Shetani alikuwa anatumia “umaarufu” na “faida” kuyaumiza maisha ya watu wengi. Katika wakati huu wa sasa, nilihisi kuwa mwenye bahati sana kuwa niliweza kupokea kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Kama singesoma neno la Mwenyezi Mungu, singewahi kuweza kuelewa ukweli wa jinsi Shetani anamuumiza mwanadamu. Karibuni, ningekuwa nimemezwa nikiwa hai na Shetani.

Baadaye, akina dada kutoka kanisa mara nyingi wangekuja nyumbani kwangu kuniona. Kwa kuwa sikuweza kusogeza nyonga zangu, akina dada hao wangesaidia kuchua misuli na kufanya baadhi ya mwumiko kwangu. Mmoja wa akina dada hao aliyekuwa amefundishwa kitabibu aliniambia kuwa ikiwa ningefinya eneo maalum la tiba vitobo, ingeletea afueni kwa hali yangu. Pia Wangechukua hatua na kunisaidia na kazi zangu za nyumbani. Walinitunza a walikuwa jamaa zangu wa familia. Kama mgeni katika nchi ya kigeni, sikuwa na rafiki duniani. Leo kweli nilihisi kuguswa kwamba dada hawa walinitunza bora zaidi kuliko vile jamaa zangu wangefanya. Niliwashukuru tena na tena. Hata hivyo, dada zangu waliniambia, “Maelfu ya miaka iliyopita, Mungu alituamulia kabla na kutuchagua. Sasa, ametupangia sisi kuzaliwa katika siku za mwisho na kukubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho. Pamoja, tunatembea njia hii. Hii ndiyo amri ya Mungu. Kwa kweli tulikuwa familia muda mrefu uliopita. Ni kwamba tu tulikuwa tumetenganishwa na ni sasa tu ndiyo tumepatana.” Mara dada zangu waliposema hivi, sikuweza kudhibiti tena hisia zangu na nikawakumbatia machozi yakitiririka usoni mwangu. Wakati huu, nilihisi ukaribu na dada zangu ambao siwezi kuelezea. Moyo wangu ulikuwa na shukrani zaidi kwa Mwenyezi Mungu.

Bila kujua, nilikuwa napata afueni zaidi na zaidi. Baada ya kupitia maumivu na mateso ya tukio hili la ugonjwa, nilitafakari juu ya jinsi nilivyokuwa chini ya udhibiti wa mtazamo wa maisha ya Shetani usio sahihi wa “kujitahidi kuwa bora zaidi kuliko kila mtu mwingine.” Muda huu wote, nilijitahidi kujitokeza miongoni wa wenzangu na kuishi maisha yenye wingi ili wengine wangenipenda na kunitamani. Hata hivyo, sijawahi kufikiri nini nitapata badala yake yalikuwa maumivu na huzuni. Sikupata hata amani na furaha kidogo. Nimeonja mchakato huu wa maumivu na siko tayari kupigana dhidi ya hatima wala siko tayari kutafuta umaarufu na faida. Haya siyo maisha ninayotaka. Mimi si kama mashine ya kutengeneza fedha kwa kasi tena. Badala yake, ninaishi maisha ya kawaida kila siku. Bali na kwenda kazini, mara kwa mara ninahudhuria mikutano, kusoma neno la Mungu na kushiriki uzoefu wangu mwenyewe na ufahamu na kaka na dada zangu. Mimi pia hujifunza kuimba nyimbo za neno la Mungu na kuishi kwa furaha. Nimepata aina ya uhakika na amani ambayo sikuwahi kuonja kabla moyoni mwangu. Siku moja nilisoma kifungu kinachofuata cha maneno ya Mungu: “Wakati mtu hana Mungu, wakati mtu hawezi kumwona Mungu, wakati hawezi kutambua waziwazi ukuu wa Mungu, kila siku inakosa maana, inakosa thamani, na kuwa yenye taabu. Popote pale mtu yupo, kazi yoyote ile anayofanya, mbinu za mtu za kuzumbua riziki na kutafuta shabaha zake huweza kumletea kitu kimoja ambacho ni kuvunjika moyo kusikoisha na mateso yasiyopona, kiasi cha kwamba mtu hawezi kuvumilia kuangalia nyuma. Ni pale tu mtu anapokubali ukuu wa Muumba, ananyenyekea katika mipango na mipangilio Yake, na kutafuta maisha ya kweli ya binadamu, ndipo mtu atakapokuwa huru kwa utaratibu dhidi ya kuvunjika moyo na kuteseka, kutupilia mbali utupu wote wa maisha(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III). Kutoka kwa maneno ya Mungu, nilielewa kwamba maana ya kuwepo kwa mwanadamu ni kuishi kulingana na maneno ya Mungu na kutii sheria na mipangilio ya Muumba. Haya ni maisha ya kweli ya binadamu. Mambo ambayo mwanadamu anaweza kupata katika maisha yake hayategemei kujishughulisha kwake akiharakisha huku na kule na kufanya kazi kwa wayowayo. Badala yake, yanategemea amri ya Mungu na kuamuru kabla kwa Mungu kabla. Wakati uo huo, nilielewa pia kwamba haijalishi kiasi cha utajiri ambao mtu hukusanya kwa ajili yote ni mali tu ya kidunia. Hukuja nayo wakati ulizaliwa na huwezi kuichukua pamoja nawe baada ya kufa. Baada ya kupata ufahamu huu, nilikuwa tayari kutii amri ya Mungu na mipangilio. Niliaminisha nusu ya pili ya maisha yangu kwa Mungu kabisa. Mimi sikutafuta tena upendo wa wengine. Badala yake, nilitafuta kuwa mtu anayemtii Mungu. Sasa, ninafanya kazi saa tatu hadi nne kwa siku. Bosi wangu ni Mjapani. Ingawa hatuwezi kuwasiliana kupitia maneno, bosi wangu ananitunza. Kila wakati ananiuliza kufanya kitu fulani, yeye hutumia maneno rahisi kueleza ujumbe wake kwangu. Yeye kamwe hanipi msongo. Ninahisi hata zaidi sasa kwamba, mradi tu mwanadamu anamtii Mungu, atakuwa na uwezo wa kuishi maisha yenye starehe na yenye furaha.

Kila wakati ninapokuwa peke yangu, mara kwa mara natafakari juu ya mchakato wa kuja kwangu mbele ya Mungu. Kama haingekuwa kwa ajili ya ugonjwa wangu ambao umenizuia kutafuta umaarufu na kupata, bado ningekuwa mashine ya kutengeneza fedha duniani. Ningekuwa kipofu kwa hili mpaka uharibifu wa Shetani uniue. Shetani alinidhuru mimi kwa kutumia umaarufu, faida, na magonjwa. Kinyume na hilo, Mwenyezi Mungu alitumia ugonjwa yangu kunileta mbele Yake. Kupitia kwa maneno Yake, niliona wazi kwamba Shetani anahusika na upotovu wa mwanadamu. Niliona pia wazi jinsi ilivyo vibaya na cha kudharauliwa kwa Shetani kutumia umaarufu na faida kuwameza watu. Hatimaye nilikuwa katika nafasi ya kutupa mbali pingu za umaarufu na faida na kuanzisha mtazamo sahihi wa maisha. Roho yangu iliwekwa huru. Mungu ni mwenyezi sana na mwenye busara! Ninashukuru kwamba Mungu amenipenda na kuniokoa.

Iliyotangulia: Mungu Yuko Kando Yangu
Inayofuata: Toba ya Afisa

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mungu Yuko Kando Yangu

Na Guozi, MarekaniNilizaliwa katika familia ya Kikristo, na nilipokuwa na umri wa mwaka mmoja, mama yangu alikubali kazi mpya ya Bwana Yesu...

Toba ya Afisa

Na Zhenxin, Uchina Mwenyezi Mungu anasema, “Tangu uumbaji wa dunia hadi sasa, yote ambayo Mungu amefanya katika kazi Yake ni upendo, bila...

Kurejea Kutoka Ukingoni

Na Zhao Guangming, ChinaMwanzoni mwa miaka ya 1980, nilikuwa katika miaka yangu 30 nami nilikuwa nikifanyia kazi kampuni ya ujenzi....

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp