Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu
Kila mmoja anapaswa kuchunguza upya jinsi ambavyo anamwamini Mungu katika maisha yake yote, ili muweze kuona kama katika mchakato wa kumfuata Mungu, unaweza kuelewa kwa kweli, umefahamu kwa kweli, na umefikia kumjua Mungu kweli, na kama unajua kwa kweli ni mtazamo gani ambao Mungu anao kwa aina tofauti za wanadamu, na kama unaelewa kwa kweli kazi ambayo Mungu Anaifanya juu yako na jinsi Mungu Anavyofafanua kila tendo lako. Huyu Mungu, Ambaye yuko kando yako, Akiongoza mwelekeo wa maendeleo yako, Akishikilia ukuu juu ya hatima yako, na kukupa mahitaji yako—je, ni kwa kiasi gani, katika uchanganuzi wa mwisho, unaelewa na je, ni kwa kiasi gani unajua kwa uhakika kumhusu Yeye? Je, unajua Anachofanyia kazi kwako kila siku? Je, unajua kanuni na makusudi ambayo kwayo Yeye anazingatia katika kila tendo Lake? Je, unajua jinsi Anavyokuongoza? Unajua mbinu Anazotumia kukupa mahitaji yako? Unajua mbinu ambazo Anatumia kukuongoza? Je, unajua kile Anachotaka kupata kutoka kwako na kile Anachotaka kutimiza kwako? Je, unajua mtazamo Anaochukua katika namna nyingi ambazo unatenda? Je, unajua kama wewe ni mtu Anayependwa na Yeye? Je, unajua chanzo cha furaha, hasira, huzuni na uchangamfu Wake, na fikira na mawazo yanayohusiana na hayo, na kiini Chake? Je, unajua, hatimaye, huyu Mungu ni Mungu wa aina gani ambaye unamwamini? Je, maswali haya na mengine ya aina hii, ni kitu ambacho hujawahi kuelewa ama kuwaza kuyahusu? Katika kufuatilia imani yako kwa Mungu, je, umewahi, kuondoa hali za kutomwelewa Yeye, kupitia ufahamu wako wa kweli na katika uzoefu halisi wa maneno ya Mungu? Je, baada ya kupokea kuadibu na maonyo ya Mungu, umefikia utiifu wa kweli na kujali kwa kweli? Je, wakati wa kuadibu kwa Mungu na hukumu, umepata kutambua uasi na asili ya kishetani ya mwanadamu na kupata ufahamu kidogo kuhusu utakatifu wa Mungu? Je, chini ya uongozi na nuru ya maneno ya Mungu, umeanza kuwa na mtazamo mpya wa maisha? Katika majaribu yaliyotumwa na Mungu, je, umepata kuhisi kutovumilia Kwake makosa ya mwanadamu na pia kile Anachohitaji kutoka kwako na vile Anavyokuokoa? Iwapo hujui kutomwelewa Mungu ni nini, au jinsi ya kumaliza kutoelewa huku, basi mtu anaweza kusema hujawahi kuingia katika ushirika wa kweli na Mungu na hujawahi kumwelewa Mungu, ama angalau mtu anaweza kusema kuwa hujawahi kuwa na nia ya kumwelewa Yeye. Ikiwa hujui nidhamu ya Mungu na kuadibu ni nini, basi kwa hakika hujui kujitiisha na kujali ni nini, ama angalau hujawahi kujinyenyekeza kwa Mungu kwa kweli au kumjali. Ikiwa hujawahi kupitia kuadibu na hukumu ya Mungu, basi kwa hakika hutaweza kujua utakatifu Wake ni nini, na unaweza hata kuwa na ufahamu kidogo kuhusu uasi wa mwanadamu ni nini. Ikiwa hujawahi kuwa na mtazamo sahihi wa maisha, au lengo sahihi katika maisha, lakini bado uko katika hali ya kuchanganyikiwa na kutokuwa na uamuzi juu ya njia yako ya maisha ya baadaye, hata kufikia hatua ya kusita kusonga mbele, basi ni dhahiri kuwa hujawahi kupokea nuru na uongozi wa Mungu, na mtu anaweza tu kusema kuwa hujawahi kweli kuruzukiwa au kujazwa zaidi na maneno ya Mungu. Ikiwa bado hujapitia majaribio ya Mungu, basi ni hakika kuwa bila shaka hutajua kutovumilia kwa Mungu makosa ya mwanadamu ni nini, wala hutaelewa kile ambacho Mungu Anahitaji hatimaye kutoka kwako, ama kweli kuruzukiwa au kujazwa zaidi na maneno ya Mungu. Ikiwa bado hujapitia majaribio Ikiwa bado hujapitia majaribio. Haijalishi ni kwa miaka mingapi mwanadamu ameamini katika Mungu, iwapo hajawahi kupitia ama kutambua chochote katika maneno ya Mungu, basi kwa hakika hatembei katika njia ya wokovu, imani yake katika Mungu kwa hakika haina chochote, maarifa yake kumhusu Mungu pia kwa hakika ni sufuri, na ni hakika kuwa hana ufahamu wowote kuhusu kumcha Mungu ni nini.
Kile Mungu alicho nacho na uwepo wa Mungu, kiini cha Mungu, tabia ya Mungu—yote yamewekwa wazi katika maneno Yake kwa binadamu. Anapopitia maneno ya Mungu, katika mchakato wa kuyaweka katika vitendo mwanadamu atapata kuelewa kusudi la maneno Anayonena Mungu, na kuelewa chanzo na usuli wa maneno ya Mungu, na kuelewa na kufahamu maneno ya Mungu. Kwa binadamu, haya ni mambo yote ambayo mwanadamu lazima ayapitie, ayatambue, na kuyafikia ili kuufikia ukweli na uzima, kutambua nia za Mungu, kubadilishwa katika tabia yake, na kuweza kutii ukuu na mipango ya Mungu. Katika wakati huo ambao mwanadamu anapitia, anafahamu, na kuvifikia vitu hivi, atakuwa kupata kumwelewa Mungu polepole, na kwa wakati huu pia atakuwa amepata viwango tofauti vya maarifa kumhusu Yeye. Ufahamu huu na maarifa haya hayatoki katika kitu ambacho mwanadamu amefikiria au kutunga, ila kutoka kwa kile ambacho anafahamu, anapitia, anahisi, na anashuhudia ndani yake mwenyewe. Ni baada tu ya kufahamu, kupitia, kuhisi, na kushuhudia vitu hivi ndipo ufahamu wa mwanadamu kumhusu Mungu utapata ujazo, ni maarifa haya tu anayoyapata kwa wakati huu ndio yaliyo halisi, ya kweli na sahihi, na mchakato huu—wa kupata kuelewa kwa kweli na ufahamu wa Mungu kwa kuelewa, kupitia, kuhisi, na kushuhudia maneno Yake—sio kingine ila ushirika wa kweli kati ya mwanadamu na Mungu. Katikati ya aina hii ya ushirika, mwanadamu anakuja kuelewa kwa kweli na kufahamu nia za Mungu, anakuja kuelewa kwa kweli na kujua kile Mungu alicho na uwepo wa Mungu, anakuja kuelewa kujua kwa kweli kiini cha Mungu, anakuja kuelewa na kujua tabia ya Mungu polepole, anafikia uhalisi wa kweli, na ufafanuzi sahihi, kuhusu ukweli wa utawala wa Mungu juu ya vitu vyote vilivyoumbwa, na kupata mambo ya muhimu na ufahamu wa utambulisho wa Mungu na nafasi Yake. Katika ushirika kama huo, mwanadamu anabadilika, hatua kwa hatua, mawazo yake kuhusu Mungu hayamfikirii Yeye kwa mawazo yaliyoundwa, ama kutawaliwa na wasiwasi wake mwenyewe kumhusu Yeye, ama kutomwelewa, ama kumshutumu, ama kutoa hukumu Kwake, ama kuwa na mashaka Naye. Kwa sababu hii, mwanadamu atakuwa na kiwango kidogo cha kutomwelewa Mungu, atakuwa na vipingamizi vichache kwa Mungu, na kutakuwa na matukio machache ambayo mwanadamu atamwasi Mungu. Kwa upande mwingine, kujali na utiifu wa mwanadamu kwa Mungu, utaongezeka kwa kiasi kikubwa, na uchaji wake kwa Mungu utakuwa wa kweli zaidi na pia wa kina zaidi. Katikati ya ushirika kama huo, sio tu kwamba mwanadamu atapata kuruzukiwa ukweli na ubatizo wa maisha, bali pia kwa wakati huo huo atapata maarifa ya kweli ya Mungu. Katika aina hii ya ushirika, sio tu kwamba mwanadamu atapata kubadilishwa tabia yake na kupata wokovu, bali pia kwa wakati huo atafikia uchaji na ibada ya kweli ya kiumbe aliyeumbwa kwa Mungu. Baada ya kuwa na aina hii ya ushirika, imani ya mwanadamu katika Mungu haitakuwa tena ukurasa tupu wa karatasi, ama ahadi ya maneno matupu, ama aina ya kufuata kwa upofu na kuabudu sanamu; ni; katika aina hii ya ushirika pekee ndio maisha ya mwanadamu yatakua kuelekea ukomavu siku baada ya siku, na ni wakati huu ndio tabia yake itabadilika polepole, na imani yake kwa Mungu, hatua kwa hatua, itatoka kwenye imani isiyo dhahiri na imani isiyo na uhakika mpaka kufikia utiifu wa kweli na kujali, na kuwa na uchaji wa kweli, na mwanadamu pia, katika mchakato wa kumfuata Mungu, ataendelea polepole kutoka kwenye mtazamo baridi mpaka kufikia mtazamo wa kiutendaji, kutoka kuwa yule aliye hasi mpaka kuwa chanya; ni kwa aina hii ya ushirika pekee ndipo mwanadamu atafikia kuelewa kwa kweli na ufahamu wa Mungu, kufikia maarifa ya kweli ya Mungu. Kwa sababu watu wengi hawajawahi kuingia katika ushirika wa kweli na Mungu, ufahamu wao kuhusu Mungu unakomea kiwango cha nadharia, katika kiwango cha barua na mafundisho. Hivyo ni kusema, watu wengi, haijalishi ni miaka mingapi wamemwamini Mungu, inapokuja katika suala la kumjua Mungu bado wako mahali pale pale walipoanzia, wamekwama katika msingi wa aina za ibada za kitamaduni, na mitego yao ya hadithi za kutumia rangi na ushirikina wa kikabaila. Ikiwa maarifa ya mwanadamu kumhusu Mungu yanasalia katika hatua ya awali, hii ina maana kwamba hayapo kabisa. Mbali na uthibitisho wa mwanadamu kuhusu nafasi na utambulisho wa Mungu, imani ya mwanadamu kwa Mungu bado iko katika hali ya kutoeleweka na kutokuwa na uhakika. Hii ikiwa hivyo, je, ni kiwango gani ambacho mwanadamu anaweza kuwa nacho kuhusu uchaji wa kweli kwa Mungu?
Haijalishi jinsi unavyoamini kwa uthabiti kuwepo kwa Mungu, hii haiwezi kuchukua nafasi ya ujuzi wako kuhusu Mungu, wala uchaji wako kwa Mungu. Haijalishi kiwango ambacho umefurahia baraka Zake na neema Yake, hii haiwezi kuchukua nafasi ya ufahamu wako wa Mungu. Haijalishi ni kiwango gani unataka kuweka wakfu kila kitu chako na kugharimika kwa ajili Yake, hii haiwezi kuchukua nafasi ya maarifa yako kuhusu Mungu. Ama labda umeyazoea sana maneno ambayo Amenena mpaka unayajua kimoyomoyo na unaweza kuyasema kwa haraka; hata hivyo, hii haiwezi kuchukua nafasi ya maarifa yako kuhusu Mungu. Haijalishi jinsi ambavyo mwanadamu amedhamiria kumfuata Mungu, ikiwa hajawahi kuwa na ushirika wa kweli na Mungu, ama kuwa na uzoefu wa kweli wa maneno ya Mungu, basi ufahamu wake wa Mungu utakuwa mtupu tu au ndoto isiyo na mwisho; kwa kuwa yale yote ambayo unaweza kuwa “umekumbana” nayo katika Mungu kwa kupita, au kukutana Naye uso kwa uso, bado ufahamu wako kuhusu Mungu utakuwa sifuri, na uchaji wako kwa Mungu utakuwa ni maneno matupu tu au mawazo ya kufikirika.
Watu wengi wanashikilia kusoma maneno ya Mungu siku baada ya siku, kiasi kwamba wanaweka akilini kwa umakini vifungu vyote vinavyotambuliwa sana humo kama vitu vyao vyenye thamani zaidi, na hata zaidi wanayahubiri maneno ya Mungu kila mahali, wakiwatolea na kuwasaidia wengine kwa njia ya maneno Yake. Wanafikiri kuwa kufanya hivi ni kuwa na ushuhuda kwa Mungu, kuwa na ushuhuda kwa maneno Yake, kwamba kufanya hivi ni kufuata njia ya Mungu; wanafikiri kuwa kufanya hivi ni kuishi kulingana na maneno ya Mungu, kwamba kufanya hivi ni kuleta maneno Yake katika maisha yao halisi, kuwa kufanya hivi kutawawezesha kupokea pongezi ya Mungu, na kuokolewa na kukamilishwa. Lakini, hata wanapohubiri maneno ya Mungu, hawazingatii maneno ya Mungu katika matendo, ama kujaribu kujilinganisha na yale yanayofichuliwa katika maneno ya Mungu. Badala yake, wanayatumia maneno ya Mungu ili kupata kuheshimiwa na kuaminiwa na wengine kwa hila, kuingia katika usimamizi wao wenyewe, na kubadhiri na kuiba utukufu wa Mungu. Wanatarajia, kwa ubatili, kutumia nafasi waliyopata kwa kueneza maneno ya Mungu ili kupewa kazi ya Mungu na pongezi Yake. Ni miaka mingapi imepita, lakini sio tu kwamba watu hao hawajaweza kupata kusifiwa na Mungu katika hatua ya kuyahubiri maneno ya Mungu, na sio tu kwamba hawajaweza kugundua njia ambayo wanapaswa kuifuata katika hatua ya kushuhudia maneno ya Mungu, na sio tu kwamba hawajaweza kujisaidia ama kujipatia wao wenyewe katika hatua ya kuwapa na kuwasaidia wengine kwa njia ya maneno ya Mungu, na pia sio tu kwamba hawajaweza kumjua Mungu, ama kuamsha ndani yao uchaji wa kweli wa Mungu, katika mchakato wa kufanya haya yote; bali pia, kwa upande mwingine, kutoelewa kwao kuhusu Mungu kunaongezeka kwa kina zaidi, kutoamini kwao kuhusu Mungu kunazidi kuongezeka zaidi, na mawazo yao kumhusu Yeye yanazidi kutokuwa sahihi. Wakijazwa na kuongozwa na nadharia za kuhusu maneno ya Mungu, wanaonekana kana kwamba zimekuwa sehemu yao kabisa, kana kwamba wanapitia ujuzi wao kwa urahisi bila juhudi, kana kwamba wamepata kusudi lao katika maisha, wito wao, na kana kwamba wamepata maisha mapya na kuokolewa, kana kwamba, maneno ya Mungu yakiwatoka kwa haraka kwenye ulimi kwa kukariri, wameupata ukweli, wamefahamu nia za Mungu, na kugundua njia ya kumjua Mungu, ni kana kwamba, katika mchakato wa kuhubiri maneno ya Mungu, wanakuja kila wakati uso kwa uso na Mungu. Pia, mara nyingi “wanasukumwa” na vipindi vya kulia, na kila wakati wanaongozwa na “Mungu” katika maneno ya Mungu, wanaonekana kuwa wanashikilia bila kukoma kujali Kwake kwa dhati na nia njema, na wakati huo huo wanashikilia wokovu wa Mungu kwa mwanadamu na usimamizi Wake, kuja kujua kiini Chake, na kuelewa tabia Yake ya haki. Kulingana na msingi huu, wanaonekana kuamini hata kwa uthabiti zaidi katika kuwepo kwa Mungu, kuwa na ufahamu zaidi wa hali Yake ya kuinuliwa, na kuhisi hata kwa undani zaidi ukuu Wake na uweza Wake mkuu. Wakiwa wamejawa na ufahamu wao wa kijuujuu wa maneno ya Mungu, itaonekana kuwa imani yao imekua, kuamua kwao kupitia mateso kumetiwa nguvu, na maarifa yao kwa Mungu yamekuwa na kina. Ila hawajui kwamba, ni mpaka watakapopitia maneno ya Mungu kwa kweli, maarifa yao yote kuhusu Mungu na mawazo yao kumhusu Yeye yanatoka kwa mawazo yao wenyewe na dhana zao wenyewe. Imani yao haingeweza kustahimili jaribio la aina yoyote kutoka kwa Mungu, kile wanachoita maisha yao ya kiroho na kimo havingeweza kustahimili majaribu au ukaguzi wa Mungu, azimio lao ni kama ngome iliyojengwa juu ya mchanga, na yale yanayoitwa maarifa yao ya Mungu pia sio zaidi ya ubunifu wa mawazo yao. Kwa hakika, watu hawa, ambao, ni kana kwamba, wameweka juhudi kubwa katika maneno ya Mungu, hawajawahi kutambua imani ya kweli ni nini, utiifu wa kweli ni nini, kujali kwa kweli ni nini, ama maarifa ya kweli ya Mungu ni nini. Wanachukua nadharia, mawazo, maarifa, karama, utamaduni, ushirikina na hata tabia nzuri za binadamu, na kuyafanya kuwa “mtaji na silaha” za kumwamini Mungu na kumfuata Yeye, na hata kuzifanya kuwa misingi ya imani yao kwa Mungu na katika kumfuata Yeye. Wakati uo huo, pia wanachukua mtaji huu na silaha hizi na kuzifanya kuwa hirizi za kichawi ambazo kupitia kwazo wanamjua Mungu, wanazitumia kukabiliana na kushughulika na ukaguzi, majaribio, kuadibu, na hukumu ya Mungu. Mwishowe, wanachopata bado hakijumuishi chochote zaidi ya hitimisho kumhusu Mungu dhana za kidini, ushirikina wa kikabaila, na mambo yote ambayo yanavutia, yanayostaajabisha, na yenye ugumu kuelewa. Mbinu zao za kumjua na kumfafanua Mungu zimetiwa muhuri katika muundo sawa na ule wa watu wanaoamini tu katika Mbingu iliyo Juu, ama Mtu Mzee aliye Angani, wakati uhalisi wa Mungu, kiini Chake, tabia Yake, kile Alichonacho na uwepo Wake, na kadhalika—yote ambayo yanahusiana na Mungu Mwenyewe wa kweli—ni mambo ambayo maarifa yao yameshindwa kuyafahamu, ambayo hayana hata uhusiano kabisa na yako mbali navyo kabisa. Kwa njia hii, ingawa watu hawa wanaishi chini ya utolewaji na ustawishaji wa maneno ya Mungu, hawawezi hata hivyo kutembea kwa kweli katika njia ya kumcha Mungu na kuepuka maovu. Sababu ya kweli ya hili ni kwamba hawajawahi kupata kumfahamu Mungu, wala hawajawahi kuwa na mawasiliano ya kweli ama ushirika Naye, kwa hivyo haiwezekani kwao kufikia maelewano ya pamoja na Mungu, ama kuamsha ndani mwao imani ya kweli katika kumfuata, au kumwabudu Mungu. Kwamba wanapaswa kuzingatia maneno ya Mungu, kwamba wanapaswa kumtazama Mungu—mwelekeo na mtazamo huu umewahukumu kurudi mikono mitupu kutoka kwa jitihada zao, umewahukumu kwa milele yote wasiweze kamwe kutembea katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Lengo ambalo wanalenga, na mwelekeo wanaoelekea, inamaanisha kuwa wao ni maadui wa Mungu milele, na kwamba hata milele hawatawahi kuweza kupokea wokovu.
Iwapo, katika tukio la mwanadamu ambaye amemfuata Mungu kwa miaka mingi na kufurahia ruzuku ya maneno Yake kwa miaka mingi, kama ufafanuzi wake kuhusu Mungu kimsingi utakuwa sawa na ule wa mtu anayesujudu kwa heshima mbele ya sanamu, basi hii ingeashiria kwamba mtu huyu hajapata uhalisi wa maneno ya Mungu. Hii ni kwa sababu hajaingia katika uhalisi wa maneno ya Mungu, na kwa sababu hii uhalisi, ukweli, nia, na matakwa juu ya wanadamu, yote ambayo yamo katika maneno ya Mungu, hayana uhusiano wowote na mtu huyo. Hivyo ni kusema, haijalishi jinsi mtu kama huyo anavyoweza kufanya kazi kwa bidii katika maana ya juu juu ya maneno ya Mungu, yote ni bure: kwani yale anayofuata ni maneno tu, kwa hivyo yale atakayopata yatakuwa pia ni maneno tu. Haijalishi kama maneno yanayonenwa na Mungu ni ya juu juu au ya kina katika mwonekano wa nje, yote ni ukweli ambao ni wa lazima kwa mwanadamu anapoingia katika uzima; ni chemichemi ya maji ya uzima yanayomwezesha kuishi katika roho na mwili. Yanatosheleza kile ambacho mwanadamu anahitaji ili awe hai; ni kanuni na mfumo wa imani wa kuendesha maisha yake ya kila siku; ni njia, lengo, na mwelekeo ambao ni lazima aupitie ili kupokea wokovu; ni kila ukweli ambao anapaswa awe nao kama kiumbe aliyeumbwa mbele za Mungu; na kila ukweli kuhusu jinsi mwanadamu anavyomtii na kumwabudu Mungu. Ni dhamana ambayo inahakikisha kudumu kwa uwepo wa mwanadamu, ni mkate wa kila siku wa mwanadamu, na pia ni nguzo ya msaada inayowezesha mwanadamu kuwa na nguvu na kusimama. Zimejawa na uhalisi wa ukweli ambao kupitia kwazo mwanadamu aliyeumbwa anaishi ubinadamu wa kawaida, zimejawa na ukweli ambao mwanadamu anatumia kutoka kwenye upotovu na kuepuka mitego ya Shetani, zimejaa mafunzo maonyo, uhamasishaji na faraja isiyokwisha ambayo Muumba anampa binadamu aliyeumbwa. Ni ishara ambayo inawaongoza na kuwaelimisha wanadamu kuelewa yale yote yaliyo chanya, ni dhamana inayohakikisha kuwa wanadamu wataishi kwa kudhihirisha na kumiliki yale yote yaliyo ya haki na mema, kigezo ambacho watu, matukio, na vitu vyote vinapimwa, na pia alama ya usafiri inayowaongoza wanadamu kuuelekea wokovu na njia ya mwanga. Na katika uzoefu wa kivitendo wa maneno ya Mungu pekee ndipo mwanadamu anaweza kupewa ukweli na uzima; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kupata kuelewa ubinadamu wa kawaida ni nini, maisha yenye umuhimu ni nini, kiumbe halisi ni nini, utiifu wa kweli kwa Mungu ni nini; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kuelewa anavyofaa kumjali Mungu, jinsi ya kutimiza wajibu ya kiumbe aliyeumbwa, na jinsi ya kumiliki mfano wa mwanadamu halisi; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kuelewa maana ya imani ya kweli na ibada ya kweli; ni hapa tu ndipo mwanadamu anaweza kuelewa nani ndiye Mtawala wa mbingu na nchi na vitu vyote; ni hapa tu ndipo mwanadamu anapoweza kuja kuelewa njia ambayo kwayo Yule ambaye ni Mtawala wa vitu vyote Anatawala, Anaongoza, na kuutosheleza uumbaji; na ni katika hili tu ndipo mwanadamu anaweza kuja kuelewa na kufahamu njia ambayo kwayo Yule ambaye ni Mtawala wa vitu vyote Anakuwepo, Anadhihirika na kufanya kazi. Akitenganishwa na uzoefu wa kweli wa maneno ya Mungu, mwanadamu hana maarifa ya kweli ama ufahamu katika maneno ya Mungu na ukweli. Mwanadamu wa aina hii ni maiti inayoishi tu, ganda lililoisha, na ufahamu wote unaohusiana na Muumba hauna uhusiano wowote na yeye. Machoni pa Mungu, mwanadamu kama huyo hajawahi kumwamini, ama kuwahi kumfuata, na hivyo Mungu hamtambui yeye kama mwumini Wake wala mfuasi Wake, ama hata kama kiumbe halisi aliyeumbwa.
Ili kuwa kiumbe halisi aliyeumbwa, sharti ujue Muumba ni nani, uumbaji wa mwanadamu una umuhimu gani, jinsi ya kutekeleza majukumu ya kiumbe, na jinsi ya kumwabudu Bwana wa uumbaji wote, lazima aelewe, ashike, ajue, na kujali kuhusu nia za Muumba, mapenzi Yake, na mahitaji Yake, na lazima atende kulingana na njia ya Muumba—kumcha Mungu na kuepuka maovu.
Kumcha Mungu kuna maana gani? Na mtu anawezaje kuepuka maovu?
“Kumcha Mungu” hakumaanishi woga na hofu isiyoelezeka, wala kukwepa, wala kuweka umbali, wala si ibada ya sanamu ama ushirikina. Bali, ni kuheshimu, kuthamini, kuamini, kuelewa, kujali, kutii, kujiweka wakfu, kupenda, pamoja na ibada isiyo na masharti na isiyo na malalamiko, kulipa na kunyenyekea. Bila ya ufahamu halisi wa Mungu, binadamu hawatakuwa na heshima ya kweli, imani ya kweli, ufahamu wa kweli, kujali au utiifu wa kweli, bali tu hofu na wasiwasi, mashaka pekee, kutokuelewa, kukwepa, na kuepuka; bila maarifa halisi ya Mungu, binadamu hawatakuwa na utakatifu na malipo halisi; bila ujuzi wa kweli wa Mungu, binadamu hawatakuwa na ibada ya kweli na kujisalimisha, wataabudu tu sanamu kwa upofu na ushirikina; bila maarifa halisi juu ya Mungu, binadamu hawawezi kutenda kulingana na njia ya Mungu, ama kumcha Mungu, ama kuepuka maovu. Badala yake, kila tendo na tabia ambayo mwanadamu atajihusisha uasi na ukaidi, na shutuma za kukashfu na hukumu za uwongo kumhusu Yeye, na mienendo miovu inayoenda kinyume na ukweli na maana halisi ya maneno ya Mungu.
Mara tu wanadamu wanapokuwa na imani ya kweli kwa Mungu, watakuwa wa kweli katika kumfuata Yeye na kumtegemea; ni kwa kumwamini na kumtegemea Mungu pekee ndipo binadamu anaweza kuwa na uelewa na ufahamu wa kweli; kukiwa na ufahamu wa kweli wa Mungu kutatokea kumjali Yeye kwa kweli; ni kwa kumjali Mungu kwa kweli pekee ndipo binadamu watakuwa na utiifu wa kweli kwa Mungu; na ni kwa utiifu wa kweli kwa Mungu pekee ndipo binadamu wataweza kujiweka wakfu kwa kweli; na ni kwa kujiweka wakfu kwa kweli kwa Mungu pekee ndipo binadamu wataweza kuwa na malipo yasiyo na masharti na yasiyo na malalamiko; ni kwa kuamini tu na kutegemea kwa kweli, kuelewa na kujali kwa kweli, kutii kwa kweli, kujiweka wakfu kwa kweli na kulipa, ndipo binadamu watakuja kujua kwa kweli tabia na kiini cha Mungu, na kujua utambulisho wa Muumba; ni pale tu watakapopata kumjua Muumba ndipo binadamu wataamsha ndani yao ibada ya kweli na kujisalimisha; watakapokuwa na ibada ya kweli na kujisalimisha kwa Muumba tu ndipo binadamu wataweza kwa kweli kuweka kando njia zao ovu, hivyo ni kusema, watajiepusha na maovu.
Hii inajumuisha mchakato mzima wa "kumcha Mungu na kujiepusha na maovu," na pia ni maudhui ya jumla katika kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hii ndiyo njia ambayo ni lazima ipitiwe ili kufikia kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.
“Kumcha Mungu na kujiepusha na maovu” na kumjua Mungu ni uhusiano usiogawanyishwa na uliounganishwa kwa nyuzi zisizohesabika, na uhusiano kati yao ni dhahiri. Iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kujiepusha na maovu, lazima kwanza amche Mungu kwa kweli; iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kumcha Mungu kwa kweli, lazima awe na maarifa ya kweli kuhusu Mungu; Iwapo mtu anataka kupata maarifa ya Mungu, lazima kwanza apate uzoefu wa maneno ya Mungu, aingie katika uhalisi wa maneno ya Mungu, apitie kuadibu na nidhamu ya Mungu, kuadibu na hukumu Yake; ikiwa mtu anataka kupata uzoefu maneno ya Mungu, lazima aje ana kwa ana na maneno ya Mungu, aje ana kwa ana na Mungu, na kumwomba Mungu Ampe fursa ya kupitia maneno ya Mungu katika kila aina ya mazingira yanayowahusisha watu, matukio na vitu; iwapo mtu anataka kuja ana kwa ana na Mungu na maneno ya Mungu, lazima kwanza awe na moyo wa kweli na wenye uaminifu, awe tayari kuukubali ukweli, kukubali kupitia mateso, awe na azimio na ujasiri wa kujiepusha uovu, na azimio la kuwa kiumbe halisi…. Kwa njia hii, ukiendelea mbele hatua kwa hatua, utamkaribia Mungu zaidi, moyo wako utakuwa safi zaidi, na maisha yako na thamani ya kuwa hai, pamoja na maarifa yako kumhusu Mungu, yatakuwa ya maana zaidi na yatakuwa hata yenye kung’aa zaidi. Mpaka siku moja, utahisi kuwa Muumba sio fumbo tena, kwamba Muumba hajawahi kufichwa kutoka kwako, kwamba Muumba hajawahi kuificha sura Yake kutoka kwako, kwamba Muumba hayuko mbali na wewe hata kidogo, kwamba Muumba siye Yule tena ambaye unamtamani kila mara katika mawazo yako lakini kwamba huwezi kumfikia kwa hisia zako, kwamba Anasimama kwa kweli kama mlinzi kulia na kushoto kwako, Akiruzuku maisha yako, na kudhibiti majaliwa yako. Hayuko katika upeo wa mbali, wala Hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ndiye kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho. Mungu kama huyo Anakuruhusu umpende kutoka moyoni, umshikilie, umweke karibu, umtamani, uhofu kumpoteza, na kutokuwa tayari kumkana tena, kumwasi tena, ama kumwepuka tena ama kumweka mbali. Kile unachotaka ni kumjali tu, kumtii, kulipia kila kitu Anachokupa, na kujisalimisha katika utawala Wake. Haukatai tena kuongozwa, kuruzukiwa, kutazamwa, na kutunzwa na Yeye, haukatai tena kile Anachoamuru na kupangilia kwa ajili yako. Unachotaka tu ni kumfuata, kutembea kando Yake iwe ni kushoto ama kulia Kwake, kile unachotaka ni kumkubali kama uzima wako wa pekee, kumkubali kama Bwana wako wa pekee, Mungu wako wa pekee.
Agosti 18, 2014