Sura ya 38

Kulingana na tabia za asili za wanadamu, yaani, uso wa kweli wa mwanadamu, kuweza kuendelea hadi sasa kwa kweli hakujakuwa jambo rahisi, na ni kupitia hili tu ndipo nguvu kuu ya Mungu imedhihirika. Kwa kuzingatia kiini cha mwili pamoja na upotovu wa joka kuu jekundu hadi sasa, ikiwa si kwa uongozi wa Roho wa Mungu, mwanadamu angewezaje kusimama leo? Mwanadamu hastahili kuja mbele ya Mungu, lakini Anawapenda wanadamu kwa ajili ya usimamizi Wake na ili kazi Yake kuu iweze kukamilika kabla ya muda mrefu sana. Kwa kweli, hakuna mtu anayeweza kulipa upendo wa Mungu kwa wanadamu katika maisha yao yote. Labda wengine wanataka kulipa neema ya Mungu kwa kuyatoa maisha yao, lakini Nakwambia: Mwanadamu hastahili kufa mbele ya Mungu, na kwa hiyo kifo cha mwanadamu ni bure. Kwa sababu kwa Mungu kifo cha mwanadamu hakistahili hata kutajwa, wala hakina thamani ya senti moja, na ni kama kifo cha chungu duniani. Ninashauri binadamu wasiwe wa kuweka thamani kubwa sana juu yao wenyewe, na msifikirie kuwa kufa kwa ajili ya Mungu kunabeba uzito wa mlima mkubwa. Kwa Kweli, kifo cha mwanadamu ni suala jepesi kama unyoya. Hakistahili kutambuliwa. Lakini tena, mwili wa mwanadamu umeandikiwa kufa kwa asili, na hivyo mwishoni, maumbile ya mwili yanapaswa kuishia duniani. Huu ni ukweli mwaminifu, na hakuna anayeweza kuukanusha. Hii ni “sheria ya asili” ambayo Ninaipata kutoka kwa jumla ya uzoefu wa maisha ya mwanadamu, na hivyo Mungu amefafanua mwisho wa mwanadamu kwa njia hii, bila mtu yeyote kutambua. Je, unaelewa? Si ajabu Mungu anasema “Ninadharau uasi wa wanadamu. Sijui kwa nini; inaonekana ni kana kwamba Nimemchukia mwanadamu tangu mwanzo, na bado Ninahisi huruma kubwa kwake. Hivyo ndivyo watu daima wamekuwa na mitazamo miwili kunihusu—kwa kuwa Nampenda mwanadamu, na pia Namchukia.”

Nani asiyemtukuza Mungu kwa kuwepo Kwake au kuonekana Kwake? Kwa wakati huu, ni kana kwamba Nimesahau kabisa uchafu na udhalimu ndani ya mwanadamu. Kujidai kwa wanadamu, kujikweza, kutotii, kutojali, na uasi wake wote—Nayasukuma haya yote nyuma ya mawazo Yangu ili kuyasahau. Mungu hazuiliwi kwa sababu ya nafsi kama hiyo ya wanadamu. Kwa kuwa Mungu na Mimi “tunashiriki mateso haya haya,” nami pia Nitajiondoa kwenye shida hii ili Nisizuiliwe zaidi na mwanadamu. Kwa nini ujisumbue na hilo? Kwa kuwa mwanadamu hayuko radhi kujiunga na nyumba ya Mungu pamoja nami, Nitawezaje kutumia nguvu Zangu kuwakomesha? Sifanyi mambo kulazimisha nguvu Zangu kwao, na si ajabu, kwa sababu Nilizaliwa katika jamii ya Mungu, bila shaka mwanadamu na Mimi daima ni tofauti. Hili limesababisha kushindwa mno kwa leo. Lakini Naendelea kuepukana na udhaifu wa mwanadamu; Nina chaguo gani? Je, si hili ni kwa sababu Mimi sina uwezo? Si ajabu Mungu anataka “kustaafu” kutoka katika “wakala” wa wanadamu, na anataka “pensheni” Yake. Nanena kutoka kwa mtazamo wa mwanadamu, na mwanadamu hasikilizi, lakini Ninenapo kama Mungu, je, bado haasi? Labda siku itakuja ambapo Mungu kwa kweli “atastaafu” ghafla kutoka katika “wakala” wa wanadamu, na wakati huo utakapokuja, neno la Mungu litakuwa kali zaidi. Leo, inaweza kuwa kwa sababu Yangu kwamba Mungu huzungumza kwa njia hii, na siku hiyo ikifika, Mungu hatakuwa kama Mimi tena, kwa subira “kusimulia hadithi kwa watoto katika shule ya chekechea.” Labda kile Ninachosema hakifai kabisa, lakini Mungu yuko tayari kulegeza mshiko Wake kwa mwanadamu kidogo tu kwa sababu ya Mungu mwenye mwili; vinginevyo, ingekuwa mbaya sana kutafakari. Kama vile Mungu alisema, “Nililegeza fumbato Langu kwao kwa kiasi fulani, kuwaruhusu kujiingiza katika tamaa zao za mwili, na hivyo walithubutu kuwa jeuri, bila kizuizi, na inaweza kuonekana kuwa hawanipendi kweli, kwa vile wote wanaishi katika mwili.” Kwa nini Mungu anasema hapa “kujiingiza katika tamaa zao,” na “kuishi katika mwili” hapa? Ukweli usemwe, mwanadamu kwa kawaida ataelewa maneno kama haya bila ufafanuzi Wangu. Labda watu wengine wanasema hawaelewi, lakini Nitakwambia kuwa unajua ukweli, na unajifanya tu hujui. Nakukumbusha: Kwa nini Mungu anasema “Naomba tu mwanadamu kushirikiana na Mimi”? Kwa nini Mungu anasema kwamba asili ya mwanadamu ni ngumu kubadilika? Kwa nini Mungu anadharau asili ya mwanadamu? Na asili ya mwanadamu ni nini hasa? Je, si asili ya mwanadamu? Nani amefikiria maswali haya? Pengine hili ni somo jipya kwa mwanadamu, lakini bila kujali, Ninamsihi mwanadamu kulizingatia sana, vinginevyo utamchukiza Mungu kila mara kwa sababu ya maneno kama vile “asili ya mwanadamu haibadiliki.” Kuna maana gani katika kutenda kinyume Chake kwa njia hiyo? Je, huko si kutafuta shida? Je, mwishowe, si kama tu kurusha yai kwenye jiwe?

Kwa kweli, majaribu na vishawishi vyote vinavyomjia mwanadamu ni masomo ambayo Mungu anahitaji kwa mwanadamu. Kulingana na nia ya asili ya Mungu, mwanadamu anaweza kufikia mambo haya, hata ikiwa atalazimika kutoa dhabihu kile anachopenda, lakini, kwa sababu mwanadamu daima anajipenda, hivyo anashindwa kushirikiana na Mungu kikweli. Mungu hataki mengi kutoka kwa mwanadamu. Yote ambayo Mungu anataka kwa mwanadamu yanahitaji kutimizwa kwa urahisi na kwa furaha; ni vile tu mwanadamu hayuko radhi kupitia shida. Kama mtoto, angeweza kuishi kwa uangalifu ili kupata senti chache kuwaheshimu wazazi wake na kutimiza wajibu anaopaswa kutimiza. Lakini anaogopa kwamba hatakula vizuri vya kutosha na kwamba mavazi yake yatakuwa ya kawaida sana, kwa hiyo kwa sababu moja au nyingine, anachukua upendo na utunzaji wa wazazi wake na kuvitupa mbali sana katika mawingu, kana kwamba ataanza kufanya hili baada ya kupata kiasi kikubwa cha fedha. Lakini Naweza kuona kutokana na hili kwamba wanadamu hawana ukarimu wa kuwapenda wazazi wao—hawana sifa ya kuwa wana. Pengine hili ni kali mno, lakini Siwezi kuzungumza upuuzi kinyume na ukweli. Siwezi “kuwaiga wengine” kumpinga Mungu kwa kujiridhisha Mwenyewe. Ni kwa sababu tu hakuna mtu hapa duniani aliye na muelekeo wa kuwa mwana mwenye upendo kama Mungu alivyosema: “Mbinguni, Shetani ni adui Yangu, duniani, mwanadamu ni adui Yangu. Kwa sababu ya muungano kati ya mbingu na dunia, vizazi vyao tisa vinapaswa kuchukuliwa kuwa na hatia kwa kuhusishwa.” Shetani ni adui wa Mungu; sababu ya kusema hivyo ni kwa kuwa hamlipi Mungu kwa neema na fadhili Zake, lakini badala yake “hupiga kasia kinyume na mkondo,” na kwa kufanya hivyo hatimizi “ukarimu wa kuwa mwana” kwa Mungu. Je, watu hawako hivi pia? Hawaonyeshi heshima ya kuwa watoto kwa “wazazi” wao na hawalipi malezi na msaada wa “wazazi” wao. Hili linatosha kuonyesha kwamba watu wa dunia ni jamaa wa Shetani mbinguni. Mwanadamu na Shetani ni wa moyo mmoja na akili moja dhidi ya Mungu, na kwa hiyo si ajabu Mungu anajumuisha vizazi tisa kama wenye hatia kwa kuhusishwa na hakuna anayeweza kusamehewa. Katika siku za nyuma, Mungu alikuwa na mtumishi mnyenyekevu kusimamia wanadamu, lakini hakusikia, na akafanya kulingana na silika yake ya kuasi dhidi Yake. Je, si wanadamu waasi pia wanapiga hatua mbele kwenye njia hii? Haijalishi ni kiasi gani Mungu anakaza “viti,” watu kamwe hawatikisiki na hawawezi kugeuka. Kwa maoni yangu, kama mwanadamu ataendelea kwa njia hii, ataharibiwa, na labda ni wakati huu ndio utaelewa maana halisi ya maneno haya: “mwanadamu hawezi kutenganishwa na asili yake ya zamani?” Mungu amemkumbusha mwanadamu mara nyingi: “Kwa sababu ya uasi wa mwanadamu, Nimemwacha.” Kwa nini Mungu anasema hivi tena na tena? Je, Mungu anaweza kuwa katili hivyo? Kwa nini Mungu anasema pia “Mimi si mwanadamu hasa”? Kwa siku nyingi zilizotulia, ni nani ambaye amechunguza kweli masuala haya kwa kina? Nawahimiza wanadamu waweke juhudi zaidi katika maneno ya Mungu na wasiyachukulie kwa wepesi; hili halina faida kwako, au kwa wengine. Ni vyema kutosema kile ambacho hakihitajiki kusemwa, na kutofikiri juu ya kile ambacho hakihitajiki kuzingatiwa. Je, hilo si rahisi zaidi? Je, ni kosa gani linaweza kutokana na hili? Kabla ya Mungu kutangaza mwisho wa kazi Yake duniani, hakuna mtu ataacha “kusonga”; hakuna mtu atakayejitoa kabisa katika wajibu wake. Sasa sio wakati; usijifanye kuwa kiongozi kwa Mungu, au mtangulizi. Nadhani ni mapema sana kukoma sasa na kuacha kusonga mbele—unaonaje?

Mungu humleta mwanadamu katika kuadibu, na Huwaingiza katika mazingira ya kifo, lakini kwa upande mwingine, ni nini ambacho Mungu anataka mwanadamu afanye duniani? Kujifanya kama kabati la nguo nyumbani? Haliwezi kuliwa au kuvaliwa, bali kutazamwa tu. Ikiwa ni hivyo, kwa nini utumie michakato mingi migumu, kuwafanya watu wateseke sana katika mwili? Mungu Asema, “Ninawasindikiza hadi kwenye ‘uwanja wa kunyongwa,’ kwani hatia ya wanadamu inatosha kustahili kuadibu Kwangu.” Kwa wakati huu, je, Mungu huwaruhusu watu watembee wenyewe hadi kwenye uwanja wa kunyongwa? Kwa nini hakuna mtu anayewaombea msamaha? Basi, mwanadamu anapaswa kushirikiana jinsi gani? Je, mwanadamu anaweza kufanya mambo kweli bila kuathiriwa na hisia, kama Mungu Anavyofanya hukumu Zake? Ufanisi wa maneno haya hasa unategemea matendo ya mwanadamu. Kama baba anavyopata pesa, ikiwa baadaye mama hajui jinsi ya kushirikiana, bila kujua jinsi ya kusimamia nyumba, basi nyumba hiyo itakuwa katika hali gani? Angalia hali ya kanisa sasa; Je, nyinyi kama viongozi mtafikiria nini? Nyinyi mnaweza kuwa na mkutano ambapo kila mtu anaweza kuzungumza kuhusu fikira zao kibinafsi. Mama hufanya machafuko ya vitu nyumbani, kwa hiyo watoto wa familia hii watakuwa kama nani? Mayatima? Waombaji? Si ajabu Mungu alisema: “Watu wote wanadhani kwamba Mimi ni uungu unaokosa ‘ubora wa akili,’ lakini ni nani anayeweza kuelewa kwamba Naweza kubaini kila kitu katika ubinadamu?” Kuhusu hali dhahiri kama hiyo, hakuna haja ya kuzungumza kutoka kwa uungu Wake. Kama vile Mungu asemavyo, “hakuna haja ya kugonga msumari kwa nyundo kubwa.” Kwa wakati huu, pengine kuna watu ambao wana uzoefu wa vitendo na kaulimbiu ya Mungu ya: “Miongoni mwa wanadamu, hakuna wanaonipenda.” Wakati huu, ni vile tu alivyosema Mungu: “Watu wote wanainamisha vichwa vyao kwa kusita kwa sababu ya hali ya sasa, lakini mioyo yao bado haijaridhika.” Maneno haya ni kama darubini. Katika siku za karibu za usoni, mwanadamu ataingia katika hali nyingine. Hii inaitwa kutorekebishika. Je, mnaelewa? Hilo ndilo jibu kwa maswali haya mawili ya Mungu: “Je, watu hawaepuki dhambi tu kwa sababu wanaogopa Nitaondoka? Je, si kweli kwamba hawalalamiki tu kwa sababu wanaogopa kuadibu?” Kwa kweli, sasa watu ni wazembe kidogo na wanaonekana wamechoka sana, na hawajali kabisa kutilia maanani kazi ya Mungu, na wanajishughulisha tu na utaratibu na mipango ya miili yao. Je, huu si ukweli?

Iliyotangulia: Sura ya 36

Inayofuata: Sura ya 39

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp