H. Juu ya Kumcha Mungu na Kuepuka Uovu

415. Ili kuwa kiumbe halisi aliyeumbwa, sharti ujue Muumba ni nani, uumbaji wa mwanadamu una umuhimu gani, jinsi ya kutekeleza majukumu ya kiumbe, na jinsi ya kumwabudu Bwana wa uumbaji wote, lazima aelewe, ashike, ajue, na kujali kuhusu nia za Muumba, mapenzi Yake, na mahitaji Yake, na lazima atende kulingana na njia ya Muumba—kumcha Mungu na kuepuka maovu.

Kumcha Mungu kuna maana gani? Na mtu anawezaje kuepuka maovu?

“Kumcha Mungu” hakumaanishi woga na hofu isiyoelezeka, wala kukwepa, wala kuweka umbali, wala si ibada ya sanamu ama ushirikina. Bali, ni kuheshimu, kuthamini, kuamini, kuelewa, kujali, kutii, kujiweka wakfu, kupenda, pamoja na ibada isiyo na masharti na isiyo na malalamiko, kulipa na kunyenyekea. Bila ya ufahamu halisi wa Mungu, binadamu hawatakuwa na heshima ya kweli, imani ya kweli, ufahamu wa kweli, kujali au utiifu wa kweli, bali tu hofu na wasiwasi, mashaka pekee, kutokuelewa, kukwepa, na kuepuka; bila maarifa halisi ya Mungu, binadamu hawatakuwa na utakatifu na malipo halisi; bila ujuzi wa kweli wa Mungu, binadamu hawatakuwa na ibada ya kweli na kujisalimisha, wataabudu tu sanamu kwa upofu na ushirikina; bila maarifa halisi juu ya Mungu, binadamu hawawezi kutenda kulingana na njia ya Mungu, ama kumcha Mungu, ama kuepuka maovu. Badala yake, kila tendo na tabia ambayo mwanadamu atajihusisha uasi na ukaidi, na shutuma za kukashfu na hukumu za uwongo kumhusu Yeye, na mienendo miovu inayoenda kinyume na ukweli na maana halisi ya maneno ya Mungu.

Mara tu wanadamu wanapokuwa na imani ya kweli kwa Mungu, watakuwa wa kweli katika kumfuata Yeye na kumtegemea; ni kwa kumwamini na kumtegemea Mungu pekee ndipo binadamu anaweza kuwa na uelewa na ufahamu wa kweli; kukiwa na ufahamu wa kweli wa Mungu kutatokea kumjali Yeye kwa kweli; ni kwa kumjali Mungu kwa kweli pekee ndipo binadamu watakuwa na utiifu wa kweli kwa Mungu; na ni kwa utiifu wa kweli kwa Mungu pekee ndipo binadamu wataweza kujiweka wakfu kwa kweli; na ni kwa kujiweka wakfu kwa kweli kwa Mungu pekee ndipo binadamu wataweza kuwa na malipo yasiyo na masharti na yasiyo na malalamiko; ni kwa kuamini tu na kutegemea kwa kweli, kuelewa na kujali kwa kweli, kutii kwa kweli, kujiweka wakfu kwa kweli na kulipa, ndipo binadamu watakuja kujua kwa kweli tabia na kiini cha Mungu, na kujua utambulisho wa Muumba; ni pale tu watakapopata kumjua Muumba ndipo binadamu wataamsha ndani yao ibada ya kweli na kujisalimisha; watakapokuwa na ibada ya kweli na kujisalimisha kwa Muumba tu ndipo binadamu wataweza kwa kweli kuweka kando njia zao ovu, hivyo ni kusema, watajiepusha na maovu.

Hii inajumuisha mchakato mzima wa “kumcha Mungu na kujiepusha na maovu,” na pia ni maudhui ya jumla katika kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hii ndiyo njia ambayo ni lazima ipitiwe ili kufikia kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

416. Kwanza kabisa tunajua kwamba tabia ya Mungu ni ukuu, ni ghadhabu. Yeye si kondoowa kuchinjwa na yeyote; na hata zaidi Yeye si kikaragosiwa kudhibitiwa na watu watakavyo. Yeye pia si hewa tupu ya kuamrishwa huku na kule na watu. Kama kweli unasadiki kwamba Mungu yupo, unapaswa kuwa na moyo unaomcha Mungu, na unapaswa kujua kwamba kiini cha Mungu hakipaswi kughadhabishwa. Ghadhabu hii inaweza kusababishwa na neno; pengine fikira; pengine aina fulani ya tabia mbaya; pengine tabia ya upole, tabia inayoweza kuruhusiwa machoni pake na maadili ya mwanadamu; au pengine inasababishwa na mafundisho, aunadharia. Hata hivyo, punde unapomghadhabisha Mungu, fursa yako inapotea na siku zako za mwisho zinakuwa zimewasili. Hili ni jambo baya sana! Kama huelewi kwamba Mungu hawezi kukosewa, basi pengine humchi Mungu, na pengine unamkosea Yeye kila wakati. Kama hujui jinsi ya kumcha Mungu, basi huwezi kumcha Mungu, na hutaweza kujua namna ya kujiweka kwenye njia ya kutembea katika njia ya Mungu—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Punde unapofahamu, unaweza kuwa na ufahamu kwamba Mungu hawezi kukosewa, kisha utajua ni nini maana ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

417. Ingawa sehemu ya kiini cha Mungu ni upendo, na Anaitoa rehema yake kwa kila mtu, watu hupuuza na kusahau ukweli kwamba kiini Chake halisi ni heshima vilevile. Kwamba Ana upendo haimaanishi kwamba watu wanaweza kumkosea Yeye wapendavyo na Hana hisia zozote, au miitikio yoyote. Kwamba Ana rehema haimaanishi kwamba Hana kanuni zozote katika jinsi Anavyowatendea watu. Mungu yu hai; kwa kweli Yupo. Yeye si kikaragosi kilichofikiriwa au kitu kingine tu. Kwa kuwa Yeye yuko, tunapaswa kusikiliza kwa makini sauti ya moyo Wake wakati wote, kuzingatia makini mtazamo Wake, na kuzielewa hisia Zake. Hatupaswi kutumia mawazo ya watu kumfafanua Mungu, na hatupaswi kulazimisha mawazo na matamanio ya watu kwa Mungu, na kumfanya Mungu atumie mtindo na kufikiri kwa mwanadamu katika jinsi Anavyowatendea wanadamu. Ukifanya hivyo, basi unamghadhabisha Mungu, unaijaribu hasira ya Mungu, na unapinga heshima ya Mungu! Hivyo basi, baada ya kuelewa ukali na uzito wa suala hili, Ninasihi kila mmoja wenu aliye hapa kuwa makini na wenye busara katika vitendo vyenu. Kuwa makini na wenye busara katika kuongea kwenu. Na kuhusu jinsi mnavyomtendea Mungu, kadiri mnavyokuwa waangalifu na wenye busara zaidi, ndivyo ilivyo bora! Wakati huelewi mtazamo wa Mungu ni nini, usizungumze kwa uzembe, usiwe mzembe katika vitendo vyako, na usipachike majina ovyo ovyo. Na hata zaidi, usikimbilie kufanya hitimisho kiholela. Badala yake, unafaa kusubiri na kutafuta; hili pia ndilo dhihirisho la kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Ikiwa wewe unaweza kufikia kiwango hiki zaidi ya yote, na kuwa na mtazamo huu zaidi ya yote, basi Mungu hatakulaumu kwa upumbavu wako, ujinga wako, na ukosefu wa kuelewa sababu za mambo. Badala yake, kwa sababu ya hofu yako ya kumkosea Mungu, heshima yako kwa mapenzi ya Mungu, na mtazamo wako wa kutaka kumtii, Mungu atakukumbuka, atakuongoza na kukupa mwanga, au kuvumilia uchanga na ujinga wako. Kinyume chake, endapo mtazamo wako Kwake utakuwa usio na heshima—kumhukumu Mungu kiholela, kukisia kiholela, na kufafanua mawazo ya Mungu—Mungu atakupa hukumu, nidhamu, au hata adhabu; au Atakupa kauli. Pengine kauli hii inahusisha matokeo yako. Hivyo basi, Ningali bado nataka kutilia mkazo jambo hili kwa mara nyingine tena: Unapaswa uwe makini na mwenye busara katika kila kitu kinachotoka kwa Mungu. Usiongee kwa uzembe, na usiwe mzembe katika matendo yako. Kabla ya kusema chochote, unafaa kufikiria: Je, kufanya hivi kutamghadhabisha Mungu? Je, kufanya hivi ni kumcha Mungu? Hata katika masuala mepesi, bado unafaa kujaribu kuelewa hakika maswali haya, yafikirie kwa kweli. Ikiwa unaweza kwa kweli kutenda kulingana na kanuni hizi katika nyanja zote, katika mambo yote, kila wakati, na kukubali mtazamo kama huu hasa wakati huelewi kitu, basi Mungu atakuongoza daima na kukupatia njia ya kufuata.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

418. Ninawasihi muwe na ufahamu bora zaidi wa yaliyomo katika amri za utawala, na mfanye bidii kuijua tabia ya Mungu. Vinginevyo, mtapata ugumu sana wa kufunga vinywa vyenu, ndimi zenu zitaropoka kwa uhuru kwa maneno ya kujigamba, na bila kujua mtaikosea tabia ya Mungu na kujipata kwenye giza, mkipoteza uwepo wa Roho Mtakatifu na mwangaza. Kwa sababu ninyi hamna kanuni katika matendo yenu, kwa sababu mnafanya na kusema yale msiyopaswa, basi mtapata adhabu inayowafaa. Lazima ujue kwamba ingawa wewe ni mpotovu katika maneno yako na matendo yako, Mungu ana kanuni katika hayo yote. Sababu ya wewe kupokea adhabu ni kwa sababu umemkosea Mungu na wala si binadamu. Kama, katika maisha yako, unatenda makosa mengi dhidi ya tabia ya Mungu, basi utalazimika kuwa mtoto wa kuzimu. Kwa binadamu inaweza kuonekana kwamba umetenda matendo machache tu yasiyolingana na ukweli na si chochote zaidi. Je, una habari, hata hivyo, kwamba machoni pa Mungu, tayari wewe ni mmoja ambaye kwako hakuna tena sadaka ya dhambi? Kwani umevunja amri za utawala za Mungu zaidi ya mara moja na hujaonyesha ishara yoyote ya kutubu, kwa hivyo huna chaguo lolote ila kutumbukia kuzimu mahali ambapo Mungu anamwadhibu mwanadamu. Idadi ndogo ya watu, wakati wanamfuata Mungu, walifanya baadhi ya matendo ambayo yalikiuka kanuni, lakini baada ya kupogolewa na kupewa mwongozo, waligundua upotovu wao wenyewe hatua kwa hatua, kisha wakaingia kwenye njia sahihi ya ukweli, na wamebaki na msingi mzuri leo. Watu kama hao ndio watakaobaki mwishoni. Hata hivyo, ni wale walio waaminifu ndio Ninaowatafuta; ikiwa wewe ni mtu mwaminifu na ni mtu ambaye unatenda kulingana na kanuni, basi unaweza kuwa msiri wa Mungu. Kama katika matendo yako huikosei tabia ya Mungu, na unatafuta mapenzi ya Mungu na una moyo wa kumcha Mungu, basi imani yako iko kwenye kiwango kinachotakiwa. Yeyote asiyemcha Mungu na asiye na moyo unaotetemeka kwa hofu kuna uwezekano wa kukiuka kwa urahisi amri za utawala za Mungu. Wengi wanamtumikia Mungu kwa nguvu ya shauku zao, lakini hawana ufahamu wa amri za utawala za Mungu, sembuse hata ufahamu wowote wa maana ya maneno Yake. Na kwa hivyo, kwa nia zao nzuri, mara nyingi wanaishia kufanya mambo ambayo yanatatiza usimamizi wa Mungu. Katika hali mbaya zaidi, wanafukuzwa kutoka kwenye nyumba ya Mungu, wakinyimwa nafasi yoyote zaidi ya kumfuata, na watatupwa kuzimu, hatimaye hawatakuwa na uhusiano mwingine wowote na nyumba ya Mungu. Watu hawa wanafanya kazi katika nyumba ya Mungu kwa nguvu ya nia zao nzuri zisizojua wanaishia kuikasirisha tabia ya Mungu. Watu huleta njia zao za kuwahudumia wakuu na mabwana katika nyumba ya Mungu na kujaribu kuzifanya zitumike, wakidhania kwa kiburi kwamba njia kama hizo zinaweza kutumika hapa kiurahisi. Hawakuwahi kufikiria kwamba Mungu hana ile tabia ya mwanakondoo bali ile ya simba. Kwa hiyo, wale wanaojihusisha na Mungu kwa mara ya kwanza wanashindwa kuwasiliana na Yeye, kwani moyo wa Mungu ni tofauti na ule wa binadamu. Ni baada tu ya kuelewa ukweli mwingi ndipo utakapoweza kuendelea kumjua Mungu. Maarifa haya si tu maneno wala mafundisho, lakini yanaweza kutumika kama hazina ya kuingia katika matumaini ya kumkaribia Mungu, na uthibitisho kwamba Anafurahishwa na wewe. Kama unakosa uhalisia wa maarifa, na haujajiandaa na ukweli, basi huduma yako ya dhati itakuletea tu kuchukiwa na kudharauliwa na Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maonyo Matatu

419. Kama huielewi tabia ya Mungu, basi hautaweza kufanya kazi unayopaswa kufanya kwa ajili Yake. Kama hujui dutu ya Mungu, basi hautaweza kumwonyesha heshima na uchaji, lakini badala yake kutakuwa tu na uzembe wa kutokujali, na kuepuka kusema ukweli wote, na hata zaidi, kufuru isiyoweza kurekebishwa. Ingawa kuielewa tabia ya Mungu kwa kweli ni muhimu sana, na maarifa ya dutu ya Mungu hayawezi kupuuzwa, hakuna yeyote ambaye amewahi kuchunguza kwa umakini au kudadisi masuala haya. Ni wazi kuona kwamba nyote mmetupilia mbali amri za utawala Nilizotoa. Kama huielewi tabia ya Mungu, basi kuna uwezekano mkubwa zaidi kwa wewe kuikosea tabia Yake. Kuikosea tabia Yake ni sawa na kuchochea hasira ya Mungu Mwenyewe, ambapo matunda ya mwisho ya matendo yako yatakuwa ni ukiukaji wa amri za utawala. Sasa unapaswa kutambua kwamba unapoelewa kiini cha Mungu, vivyo hivyo utaweza kuielewa tabia Yake—na unapoielewa tabia Yake, vivyo hivyo utakuwa umeelewa amri za utawala. Bila shaka, mengi ya yale yaliyoko katika amri za utawala yanahusisha tabia ya Mungu, lakini tabia Yake yote haijaonyeshwa ndani ya amri za utawala; kwa hivyo, ni lazima mpige hatua zaidi katika kuongeza ufahamu wenu wa tabia ya Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu

420. Mungu ni Mungu aliye hai, na kama vile watu hutenda tofauti katika hali tofauti, mtazamo wa Mungu kuelekea maonyesho haya hutofautiana kwa sababu Yeye si kikaragosi, wala Yeye si hewa tupu. Kupata kuujua mtazamo wa Mungu ni jambo lenye thamani kwa wanadamu. Watu wanapaswa kujifunza jinsi, kwa kuujua mtazamo wa Mungu, wanaweza kujua tabia ya Mungu na kuuelewa moyo Wake kidogo kidogo. Wakati unapokuja kuuelewa moyo wa Mungu kidogo kidogo, hutahisi kwamba kumcha Mungu na kuepuka maovu ni jambo gumu kutimiza. Kilicho zaidi ni kwamba, unapomwelewa Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kufanya hitimisho kuhusu Yeye. Unapoacha kufanya hitimisho kuhusu Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kumkosea Yeye, na bila kujua Mungu atakuongoza kuwa na maarifa Yake, na hivyo basi utamcha Mungu katika moyo wako. Utaacha kumfafanua Mungu kwa kutumia mafundisho, zile barua, na nadharia ambazo umejifunza. Badala yake, kwa kutafuta nia za Mungu katika mambo yote na siku zote utaweza bila kufahamu kuwa mtu anayefuata moyo wa Mungu.

Kazi ya Mungu haionekani na haiwezi kuguswa na wanadamu, lakini kwa jinsi Mungu anavyohusika, matendo ya kila mtu, pamoja na mtazamo wao Kwake—haya hayatambuliki tu na Mungu, lakini yanaonekana pia. Hili ni jambo ambalo kila mmoja anafaa kutambua na kuwa wazi kulihusu. Unaweza kuwa ukijiuliza siku zote: “Je, Mungu anajua kile ninachofanya hapa? Je, Mungu anajua kile ninachofikiria sasa hivi? Pengine Anajua, pengine Hajui.” Kama utakuwa na mtazamo wa aina hii, kumfuata na kumwamini Mungu ilhali unatilia shaka kazi Yake na uwepo Wake, basi hivi karibuni au baadaye siku itawadia ambapo utamghadhabisha, kwa sababu tayari unaelea kwenye ukingo wa mteremko wa hatari. Nimeona watu ambao wamemwamini Mungu kwa miaka mingi, lakini bado hawajapata uhalisi wa ukweli, wala hata hawaelewi mapenzi ya Mungu. Maisha yao na kimo chao havipigi hatua yoyote, wakishikilia tu mafundisho duni kabisa. Hii ni kwa sababu watu hawa hawajawahi kuchukulia neno la Mungu kama maisha yao binafsi, na hawajawahi kukabiliana na kukubali uwepo Wake. Je, unafikiri kwamba Mungu anapowaona watu kama hao, Anajawa na furaha? Je, wanamfariji Yeye? Katika hali hiyo, ni njia ya imani ya watu kwa Mungu ambayo huamua hatima yao. Kuhusu jinsi watu wanavyomwamini Mungu ndivyo inavyoamua hatima yao. Kuhusu jinsi watu wanavyotafuta na jinsi watu wanavyomkaribia Mungu, mitazamo ya watu ni ya muhimu sana. Usimpuuze Mungu kama vile Yeye ni rundo la hewa tupu linalozunguka nyuma ya kichwa chako. Daima mfikirie Mungu wa imani yako kama Mungu aliye hai, Mungu halisi. Yeye hayupo kule juu kwenye mbingu ya tatu bila chochote cha kufanya. Badala yake, Yeye hutazama kila mara ndani ya moyo wa kila mtu, Akiangalia kile unachotaka kufanya, katika kila neno dogo na kila tendo dogo, Akiangalia jinsi unavyotenda na mtazamo wako kwa Mungu ni upi. Iwe uko radhi kujitolea kwa Mungu au la, tabia yako yote na fikira zako na mawazo yako ya ndani zaidi yako mbele za Mungu, na yanaangaliwa na Yeye. Ni kulingana na tabia yako, kulingana na vitendo vyako, na kulingana na mwelekeo wako kwa Mungu, ambapo maoni Yake kwako, na mwenendo Wake kwako, vinaendelea kubadilika. Mimi Ningependa kutoa ushauri fulani kwa baadhi ya watu. Msijiweke kwenye mikono ya Mungu kama watoto wachanga, kana kwamba Yeye Anapaswa kukupenda sana, kana kwamba Hawezi kamwe kukuacha, na kana kwamba mwelekeo Wake kwako ni imara na usingeweza kubadilika, na Ninawashauri muache kuota ndoto! Mungu ni mwenye haki katika kumtendea kila mtu, na Yeye ni mwaminifu katika mtazamo Wake kwa kazi ya kuwashinda na kuwaokoa watu. Huu ndio usimamizi Wake. Anamtendea kila mmoja kwa umakinifu, na wala si kama kiumbe cha kufugwa cha kucheza nacho. Upendo wa Mungu kwa binadamu si ule wa kudekeza au kupotosha; rehema na uvumilivu Wake kwa wanadamu si wa kuendekeza au kutojali. Kinyume cha mambo, upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wa kutunza, kuhurumia, na kuheshimu maisha; rehema na uvumilivu Wake vyote vinaonyesha matarajio Yake kwa binadamu; rehema na uvumilivu Wake ndivyo ambavyo binadamu anahitaji ili kuishi. Mungu yuko hai, na kwa hakika Mungu yupo; Mtazamo Wake kwa wanadamu ni wa kanuni, sio sheria ya kiitikadi hata kidogo, na unaweza kubadilika. Mapenzi Yake kwa ubinadamu yanabadilika polepole na kurekebishwa kulingana na wakati, na hali, na mtazamo wa kila mtu. Kwa hiyo, unapaswa kujua ndani ya moyo wako kwa uwazi kabisa kwamba kiini cha Mungu hakibadiliki, na kwamba tabia Yake itajidhihirisha kwa nyakati tofauti na katika mazingira tofauti. Huenda usifikirie kwamba hili si suala zito, na unatumia mawazo yako binafsi kufikiria jinsi Mungu anapaswa kufanya mambo. Lakini kuna nyakati ambapo kinyume kabisa cha mtazamo wako ni kweli, na kwamba kwa kutumia mawazo yako binafsi katika kumjaribu na kumpima Mungu, tayari umemghadhabisha. Hii ni kwa sababu Mungu hafanyi kazi kama unavyofikiria wewe, Naye Mungu hatalishughulikia suala hili kama vile unavyosema Atalishughulikia. Kwa hivyo, Ninakukumbusha uwe makini na mwenye hekima katika mtazamo wako kwa kila kitu, na ujifunze namna ya kufuata kanuni ya kutembea kwenye njia ya Mungu katika mambo yote—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Lazima uimarishe uelewa thabiti katika masuala ya mapenzi ya Mungu na mtazamo wa Mungu; lazima utafute watu walio na nuru ili wakujulishe mambo haya, na ni lazima utafute kwa bidii. Usimwone Mungu wa imani yako kama kikaragosi—ukimhukumu upendavyo, ukifanya hitimisho kiholela kuhusu Yeye, na kumtendea kwa mtazamo usio na heshima. Katika mchakato wa wokovu wa Mungu, Anapoamua matokeo yako, bila kujali kama Yeye atakupa rehema, au uvumilivu, au hukumu na kuadibu, kwa vyovyote vile, mtazamo Wake kwako unabadilika. Inategemea mtazamo wako kwa Mungu, na uelewa wako kuhusu Mungu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

421. Mungu daima yumo mioyoni mwa wale wanaomwamini Mungu kwa kweli na daima wana moyo wa kumcha Mungu, moyo wa kumpenda Mungu. Wale wanaomwamini Mungu lazima wayafanye mambo kwa moyo wa uangalifu na wenye busara, na yote wanayoyafanya yanapasa kulingana na matakwa ya Mungu na yaweze kuuridhisha moyo wa Mungu. Hawapaswi kuwa wabishi, wakifanya watakavyo, hayo hayafai katika utaratibu mtakatifu. Watu hawawezi kuipunga bendera ya Mungu kwa madaha na kucharuka kila mahali, wakienda kwa mikogo na kutapeli kotekote; kutenda haya ni tendo la uasi la juu zaidi. Familia zina masharti yao na mataifa yana sheria zao; je, hali sio hivi hata zaidi katika nyumba ya Mungu? Je, matarajio sio makali hata zaidi? Je, hakuna amri nyingi hata zaidi za utawala? Watu wana uhuru wa kutenda watakayo, lakini amri za usimamizi za Mungu haziwezi kubadilishwa kwa hiari. Mungu ni Mungu asiyewaruhusu watu kumkosea; Yeye ni Mungu anayewaua watu. Je, watu kweli hawajui hili tayari?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Onyo kwa Wale Wasiotenda Ukweli

422. Katika kila enzi ya kazi ya Mungu, Yeye huwapa watu baadhi ya maneno Anapofanya kazi ulimwenguni, na kuwaambia kuhusu ukweli fulani. Kweli hizi zinatumika kama njia ambayo watu wanapaswa kuifuata, njia ambayo wanapaswa kuitembea, njia inayowawezesha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, na njia ambayo watu wanapaswa kuiweka katika vitendo na kuitii katika maisha yao na kwenye mkondo wa safari zao za maisha. Ni kwa sababu hizi ambapo Mungu anampa binadamu maneno haya. Binadamu anapaswa kuyatii maneno haya yanayotoka kwa Mungu, na kuyatii ni kupokea uzima. Kama mtu hataweza kuyatii, na hayaweki kwenye matendo, na haishi kwa kudhihirisha maneno ya Mungu katika maisha yake, basi mtu huyo hauweki ukweli katika matendo. Na kama hawaweki ukweli katika matendo, basi hawamchi Mungu na hawaepuki maovu, wala hawawezi kumtosheleza Mungu. Kama mtu hawezi kumtosheleza Mungu, basi hawezi kupokea sifa ya Mungu; mtu wa aina hii hana matokeo.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

423. Kutembea katika njia ya Mungu hakuhusu kuangalia sharia kwa juujuu. Badala yake, kunamaanisha kwamba unapokabiliwa na suala, kwanza kabisa, unaliangalia kama ni hali ambayo imepangwa na Mungu, wajibu uliopewa wewe na Yeye, au kitu ambacho Amekuaminia wewe, na kwamba unapokabiliana na suala hili, unapaswa kuliona kama jaribio kutoka kwa Mungu. Wakati unapokabiliwa na suala hili, lazima uwe na kiwango, lazima ufikirie kwamba suala hilo limetoka kwa Mungu. Lazima ufikirie ni vipi ambavyo utashughulikia suala hili kiasi cha kwamba utaweza kutimiza wajibu wako, na kuwa mwaminifu kwa Mungu; namna ya kuifanya bila kumkasirisha Mungu; au kuikosea tabia Yake. … Kwa sababu ili kutembea katika njia ya Mungu, hatuwezi kuachilia chochote kinachotuhusu sisi wenyewe, au kinachofanyika karibu nasi, hata yale mambo madogo madogo. Haijalishi kama tunadhani tunapaswa kuyazingatia au la, maadamu jambo lolote linatukabili, tusiliache litupite. Mambo yote yanayotutokea yanapaswa kuonwa kama majaribio ya Mungu kwetu. Je, una maoni gani kuhusu mtazamo huu? Kama una mtazamo wa aina hii, basi inathibitisha ukweli mmoja kwamba: Moyo wako unamcha Mungu, na moyo wako upo tayari kujiepusha na maovu. Kama una shauku kama hii ya kumridhisha Mungu, basi kile ambacho unaweka katika vitendo hakiko mbali na kiwango cha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Mara nyingi wale wanaoamini kwamba masuala ambayo hayatiliwi maanani na watu, masuala ambayo kwa kawaida hayatajwi—haya ni mambo madogo tu, na hayana chochote kuhusiana na kuweka ukweli katika matendo. Wakati watu hawa wanakabiliwa na suala kama hilo, hawalifikirii sana na wanaliachilia tu. Lakini ukweli wa mambo ni kwamba, suala hili ni somo ambalo unapaswa kujifunza, somo kuhusu namna ya kumcha Mungu, na namna ya kujiepusha na maovu. Zaidi ya hayo, kile unachopaswa kuzingatia zaidi ni kujua kile ambacho Mungu anafanya wakati suala hili linapokukabili. Mungu yuko kando yako, Anatazama kila neno na tendo lako, na Anatazama kila kitu unachofanya, na ni mabadiliko gani yanayotokea katika mawazo yako—hii ni kazi ya Mungu. Baadhi ya watu wanasema: “Ikiwa hiyo ni kweli, basi ni kwa nini siihisi?” Huihisi kwa sababu jinsi ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu haijawa ndiyo njia ya muhimu zaidi kwako kuishikilia. Kwa hivyo, huwezi kuihisi kazi ya Mungu isiyoeleweka kwa binadamu, ambayo inajidhihirisha kulingana na fikira tofauti na vitendo tofauti vya watu. Wewe upo makini! Suala kubwa ni lipi? Swala dogo ni lipi? Masuala yanayohusu kutembea katika njia ya Mungu hayagawanywi katika masuala makubwa au madogo, yote ni yenye umuhimu—je, mnaweza kulikubali hilo? (Tunaweza kulikubali). Kuhusiana na masuala ya kila siku, kuna yale ambayo watu wanayaona kuwa makubwa sana na muhimu, na mengine yanaonekana kuwa mambo madogo madogo tu. Mara nyingi watu wanayaona masuala haya makubwa kuwa ndiyo ya muhimu zaidi, na wanayachukulia kwamba yametumwa na Mungu. Hata hivyo, kwenye mkondo wa masuala haya makubwa yanayojitokeza, kutokana na kimo kidogo cha watu, na kutokana na kiwango duni cha watu, mara nyingi binadamu haendani sawa na nia za Mungu, hawezi kupata ufunuo wowote, na hawezi kufaidi maarifa yoyote halisi yenye thamani. Kuhusu masuala madogo, haya yanapuuzwa tu na watu, na kuachwa yaondoke moja kwa moja. Kwa hivyo, watu wamepoteza fursa nyingi sana za kuchunguzwa na kujaribiwa mbele za Mungu. Je, inamaanisha nini ikiwa kila mara unapuuza watu, matukio, masuala, na hali ambazo Mungu amekuandalia? Inamaanisha kwamba kila siku, hata kila wakati, unakana ukamilishaji wa Mungu kwako, na uongozi wa Mungu. Kila Mungu anapopanga hali hizi kwako, Yeye anakuangalia kwa siri, Anauchunguza moyo wako, Anaziangalia fikira na hali zako, Anaangalia namna unavyofikiria, Anaangalia namna unavyochukua hatua. Kama wewe ni mtu asiyejali—mtu ambaye hajawahi kujali kuhusu njia ya Mungu, neno la Mungu, au ukweli—basi hutajali, hutatilia maanani kile ambacho Mungu anataka kukamilisha, na yale ambayo Mungu anakuhitaji wewe uyafanye wakati Anapopanga hali hizi kwako. Wala hutajua jinsi watu, matukio na vitu ambavyo unakumbana navyo vinavyohusiana na ukweli au mapenzi ya Mungu. Baada ya kukabiliana na hali nyingi kama hizi na majaribio mengi kama haya, ikiwa Mungu haoni matokeo yoyote ndani yako, je, Atafanyaje? Baada ya kukabiliwa na majaribio mara kwa mara, hujamheshimu Mungu kama Aliye mkuu moyoni mwako, wala hujachukulia zile hali ambazo Mungu amekuandalia kwa uzito—na hujazichukulia kama majaribio au mitihani kutoka kwa Mungu. Badala yake unakataa fursa ambazo Mungu amekupa wewe moja baada ya nyingine, na unaziacha zitokomee mara kwa mara. Je, huku si kutokutii kwa hali ya juu ambako watu wanaonyesha? (Ndiyo, ni kutokutii.) Je, Mungu atahuzunika kwa mambo haya? (Ndiyo, Atahuzunika). Sivyo, Mungu hatahuzunika! Mnaposikia Nikiongea hivi mnashtuka kwa mara nyingine tena. Huenda ukawa unafikiria: “Je, haikusemwa hapo awali kwamba Mungu anahuzunika siku zote? Je, Mungu hatahuzunika? Ni lini basi Mungu atahuzunika?” Kwa ufupi, Mungu hatahuzunika kuhusu jambo hili. Kwa hivyo, mtazamo wa Mungu ni upi katika aina hii ya tabia iliyoelezwa hapo juu? Wakati watu wanakataa majaribio na mitihani ambayo Mungu anawapa, wakati wanapoikwepa, kuna mtazamo mmoja tu ambao Mungu anao kwa watu kama hao. Je, mtazamo huo ni upi? Mungu anawadharau watu wa aina hio kutoka kwenye kina cha moyo Wake. Kuna safu mbili za maana ya neno “kudharau.” Je, Ninaelezeaje hilo kutoka kwa mtazamo Wangu? Neno “dharau” linabeba maana ya kukataa na kuchukia. Na je, safu ya pili ya maana ni ipi? Hiyo ndiyo sehemu inayomaanisha kukata tamaa juu ya kitu fulani. Ninyi nyote mnajua maana ya “kukata tamaa”, sivyo? Kwa ufupi, “kudharau” ni neno ambalo linawakilisha mwitikio na mtazamo wa mwisho wa Mungu kwa wale watu ambao wana tabia kama hiyo; ni chuki na karaha ya hali ya juu kwao, na hivyo inapelekea uamuzi wa kukata tamaa juu yao. Huu ndio uamuzi wa mwisho wa Mungu kwa mtu ambaye hajawahi kutembea katika njia ya Mungu, ambaye hajawahi kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

424. Kumcha Mungu na utiifu wa Ayubu kwa Mungu ni mfano kwa wanadamu, na ukamilifu na unyofu wake ulikuwa ndio kilele cha ubinadamu unaofaa kumilikiwa na binadamu. Ingawa hakumwona Mungu, alitambua kwamba Mungu kwa kweli alikuwepo, na kwa sababu ya utambuzi huu alimcha Mungu, na kutokana na uchaji wake kwa Mungu, aliweza kumtii Mungu. Alimpa Mungu uhuru wa kuchukua chochote alichokuwa nacho, hata hivyo hakuwa na manung’uniko, na akaanguka chini mbele za Mungu na kumwambia kwamba, kwa wakati huu, hata kama Mungu angeuchukua mwili wake, angemruhusu yeye kufanya hivyo kwa furaha, bila malalamiko. Mwenendo wake wote ulitokana na ubinadamu wake mkamilifu na mnyofu. Hivi ni kusema, kutokana na kutokuwa na hatia kwake, uaminifu, na wema wake, Ayubu alikuwa thabiti katika kutambua na kuhisi uwepo wa Mungu, na juu ya msingi huu aliweza kujiwekea mahitaji yake mwenyewe na kudhibiti mawazo yake, tabia, mwenendo, na kanuni za kutenda mbele za Mungu kulingana na mwongozo wa Mungu kwake na matendo ya Mungu ambayo alikuwa ameyaona kati ya vitu vyote. Baada ya muda, uzoefu wake ulimsababisha yeye kuwa na hali halisi na ya kweli ya kumcha Mungu na kumfanya pia kujiepusha na maovu. Hiki ndicho kilikuwa chanzo cha uadilifu ambao Ayubu alishikilia kwa uthabiti. Ayubu alikuwa na ubinadamu wenye uaminifu, unyofu, na mwema, na alikuwa na uzoefu halisi wa kumcha Mungu, kumtii Mungu na kujiepusha na maovu, pamoja na maarifa kwamba “Yehova alinipa, na Yehova amechukua.” Ni kwa sababu tu ya mambo haya ndiyo aliweza kusimama imara na kutoa ushuhuda katikati ya mashambulizi hayo makali ya Shetani, na ni kwa sababu tu ya hayo ndiyo aliweza kutomkasirisha Mungu na kutoa jibu la kumridhisha Mungu wakati majaribio ya Mungu yalipomjia.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II

425. Ayubu alikuwa hajauona uso wa Mungu, wala kusikia matamshi yaliyonenwa na Mungu, na sembuse yeye binafsi alipitia kazi ya Mungu, lakini kumcha kwake Mungu na ushuhuda aliokuwa nao wakati wa majaribu unashuhudiwa na kila mmoja, na unapendwa, unafurahiwa, na kupongezwa na Mungu, na watu wanayaonea wivu na kuvutiwa nayo, na hata zaidi ya hayo, wanaimba sifa zao. Hakukuwa na chochote kikubwa au kisicho cha kawaida kuhusu maisha yake: Kama tu mtu yeyote wa kawaida, aliishi maisha yasiyo ya kina, akienda kufanya kazi wakati wa macheo na akirudi nyumbani kupumzika wakati wa magharibi. Tofauti ni kwamba wakati wa miongo kadhaa ya kawaida ya maisha yake, alipata utambuzi katika njia ya Mungu, na akatambua na kuelewa nguvu kuu na ukuu wa Mungu kuliko mtu mwingine yeyote aliyewahi kuwa nao. Hakuwa mwerevu zaidi kuliko mtu yeyote wa kawaida, maisha yake hayakuwa yenye ushupavu sana, wala, aidha, hakuwa na ustadi maalum usioonekana. Hata hivyo, kile alichokuwa nacho, kilikuwa ni hulka iliyokuwa na uaminifu, ukarimu na unyofu, na hulka iliyopenda kutopendelea, haki, na iliyopenda mambo chanya—hakuna kati ya mambo haya yanayomilikiwa na watu wengi wa kawaida. Alitofautisha kati ya upendo na chuki, alikuwa na hisia ya haki, hakukubali kushindwa na alikuwa hakati tamaa, na alikuwa mwangalifu sana katika kufikiria kwake. Hivyo, kwawakati wake wa kawaida duniani aliyaona mambo yote yasiyo ya kawaida ambayo Mungu alikuwa amefanya, na aliuona ukuu, utakatifu, na haki ya Mungu, aliona kujali kwa Mungu, neema Yake, na ulinzi Wake kwa binadamu, na aliuona utukufu na mamlaka ya Mungu mkuu zaidi. Sababu ya kwanza iliyomfanya Ayubu aweze kupata mambo haya yaliyokuwa zaidi ya mtu yeyote wa kawaida ilikuwa kwamba alikuwa na moyo safi, na moyo wake ulimilikiwa na Mungu na kuongozwa na Muumba. Sababu ya pili ilikuwa ni ufuatiliaji wake: ufuatiliaji wake wa kuwa mtu asiye na kasoro na mkamilifu, na wa kuwa mtu aliyekubaliana na mapenzi ya Mbinguni, aliyependwa na Mungu, na aliyejiepusha na uovu. Ayubu alimiliki na kufuatilia mambo haya huku akiwa hawezi kumwona Mungu au kusikia maneno ya Mungu; ingawa alikuwa hajawahi kumwona Mungu, alikuwa amejua mbinu ambazo kwazo Mungu hutawala juu ya vitu vyote, na kuelewa hekima ambayo Mungu anatumia ili kufanya hivyo. Ingawa alikuwa hajawahi kusikia maneno ambayo yalikuwa yametamkwa na Mungu, Ayubu alijua kwamba matendo ya kumthawabisha binadamu na kuchukua kutoka kwa binadamu yote yalitoka kwa Mungu. Ingawa miaka ya maisha yake haikuwa tofauti na ile ya mtu wa kawaida, hakuruhusu kutokuwa wa ajabu kwa maisha yake kuathiri maarifa yake ya ukuu wa Mungu juu ya vitu vyote, au kuathiri kufuata kwake kwa njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Machoni pake, sheria za mambo yote zilijaa matendo ya Mungu, na ukuu wa Mungu ungeweza kuonekana katika sehemu yoyote ya maisha ya mtu. Hakuwa amemwona Mungu lakini aliweza kutambua kwamba matendo ya Mungu yako kila mahali, na katika wakati wake wa kawaida duniani, kwa kila upande wa maisha yake aliweza kuona na kutambua matendo ya kipekee na ya ajabu ya Mungu, na aliweza kuona mipangilio ya ajabu ya Mungu. Hali ya kujificha na ukimya wa Mungu haukuzuia utambuzi wa Ayubu wa matendo ya Mungu, wala haukuathiri maarifa yake kuhusu ukuu wa Mungu juu ya vitu vyote. Maisha yake ya kila siku, yalikuwa na utambuzi, wa ukuu na mipangilio ya Mungu, ambaye Amejificha miongoni mwa vitu vyote. Katika maisha yake ya kila siku alisikia pia na kuelewa sauti ya moyo wa Mungu na maneno ya Mungu, ambaye yuko kimya miongoni mwa vitu vyote ilhali Anaeleza sauti ya moyo Wake na maneno Yake kwa kutawala sheria za vitu vyote. Unaona, basi, kwamba ikiwa watu wana ubinadamu na ufuatiliaji kama wa Ayubu, basi wanaweza kupata utambuzi na maarifa kama ya Ayubu, na kupata ule ufahamu na maarifa sawa kuhusu ukuu wa Mungu juu ya vitu vyote kama Ayubu. Mungu hakuwa Amemtokea Ayubu au kuongea na yeye, lakini Ayubu aliweza kuwa mkamilifu na mnyofu, na pia aliweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kwa maneno mengine, bila ya Mungu kumtokea au kuzungumza na mwanadamu, matendo ya Mungu katika vitu vyote na ukuu Wake juu ya vitu vyote yanatosha kwa mwanadamu ili kuweza kuwa na ufahamu wa uwepo, nguvu na mamlaka ya Mungu, nguvu na mamlaka ya Mungu yanatosha kumfanya mwanadamu afuate njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II

426. “Kumcha Mungu na kujiepusha na maovu” na kumjua Mungu ni uhusiano usiogawanyishwa na uliounganishwa kwa nyuzi zisizohesabika, na uhusiano kati yao ni dhahiri. Iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kujiepusha na maovu, lazima kwanza amche Mungu kwa kweli; iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kumcha Mungu kwa kweli, lazima awe na maarifa ya kweli kuhusu Mungu; Iwapo mtu anataka kupata maarifa ya Mungu, lazima kwanza apate uzoefu wa maneno ya Mungu, aingie katika uhalisi wa maneno ya Mungu, apitie kuadibu na nidhamu ya Mungu, kuadibu na hukumu Yake; ikiwa mtu anataka kupata uzoefu maneno ya Mungu, lazima aje ana kwa ana na maneno ya Mungu, aje ana kwa ana na Mungu, na kumwomba Mungu Ampe fursa ya kupitia maneno ya Mungu katika kila aina ya mazingira yanayowahusisha watu, matukio na vitu; iwapo mtu anataka kuja ana kwa ana na Mungu na maneno ya Mungu, lazima kwanza awe na moyo wa kweli na wenye uaminifu, awe tayari kuukubali ukweli, kukubali kupitia mateso, awe na azimio na ujasiri wa kujiepusha uovu, na azimio la kuwa kiumbe halisi…. Kwa njia hii, ukiendelea mbele hatua kwa hatua, utamkaribia Mungu zaidi, moyo wako utakuwa safi zaidi, na maisha yako na thamani ya kuwa hai, pamoja na maarifa yako kumhusu Mungu, yatakuwa ya maana zaidi na yatakuwa hata yenye kung’aa zaidi. Mpaka siku moja, utahisi kuwa Muumba sio fumbo tena, kwamba Muumba hajawahi kufichwa kutoka kwako, kwamba Muumba hajawahi kuificha sura Yake kutoka kwako, kwamba Muumba hayuko mbali na wewe hata kidogo, kwamba Muumba siye Yule tena ambaye unamtamani kila mara katika mawazo yako lakini kwamba huwezi kumfikia kwa hisia zako, kwamba Anasimama kwa kweli kama mlinzi kulia na kushoto kwako, Akiruzuku maisha yako, na kudhibiti majaliwa yako. Hayuko katika upeo wa mbali, wala Hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ndiye kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho. Mungu kama huyo Anakuruhusu umpende kutoka moyoni, umshikilie, umweke karibu, umtamani, uhofu kumpoteza, na kutokuwa tayari kumkana tena, kumwasi tena, ama kumwepuka tena ama kumweka mbali. Kile unachotaka ni kumjali tu, kumtii, kulipia kila kitu Anachokupa, na kujisalimisha katika utawala Wake. Haukatai tena kuongozwa, kuruzukiwa, kutazamwa, na kutunzwa na Yeye, haukatai tena kile Anachoamuru na kupangilia kwa ajili yako. Unachotaka tu ni kumfuata, kutembea kando Yake iwe ni kushoto ama kulia Kwake, kile unachotaka ni kumkubali kama uzima wako wa pekee, kumkubali kama Bwana wako wa pekee, Mungu wako wa pekee.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Dibaji

427. Watu wanapopitia uzoefu wa kazi ya Mungu, ufahamu wao wa kwanza kumhusu ni kwamba Yeye ni asiyeeleweka, ni mwenye hekima na wa ajabu na wanamcha bila kujua na kuihisi siri ya kazi Anayoifanya, ambayo inapita akili ya mwanadamu. Watu wanataka tu kuwa na uwezo wa kukidhi matakwa Yake, kuridhisha matamanio Yake; hawatamani kumpita Yeye, kwa sababu kazi Anayoifanya inazidi fikira za mwanadamu na haiwezi kufanywa na mwanadamu kama mbadala. Hata mwanadamu mwenyewe hayajui mapungufu yake, wakati Amefungua njia mpya na kumleta mwanadamu katika dunia mpya zaidi na nzuri zaidi, na hivyo mwanadamu amefanya maendeleo mapya na kuwa na mwanzo mpya. Kile ambacho watu wanahisi kumhusu Mungu, sio matamanio, au sio matamanio tu. Uzoefu wake wa kina ni kicho na upendo, hisia zake ni kwamba Mungu kweli ni wa ajabu sana. Anafanya kazi ambayo mwanadamu hawezi kufanya na kusema mambo ambayo mwanadamu hawezi kusema. Watu ambao wamepitia kazi ya Mungu daima wana hisia isiyoweza kuelezeka. Watu wenye uzoefu wa kina wa kutosha wanaweza kuelewa ukweli wa Mungu; wanaweza kuhisi uzuri Wake, kwamba kazi Yake ni ya hekima sana, ya ajabu sana, na hivyo hii inazalisha nguvu isiyokoma ndani yao. Si woga au upendo wa mara moja moja na heshima, bali hisia za ndani za upendo wa Mungu na uvumilivu kwa mwanadamu. Hata hivyo, watu ambao wamepata uzoefu wa kuadibu na hukumu Yake wanahisi kuwa Yeye ni mkuu na Asiyekosewa. Hata watu ambao wamepitia uzoefu mkubwa wa kazi Yake pia hawawezi kumwelewa; watu wote wanaomcha wanajua kwamba kazi Yake hailingani na fikira za watu lakini siku zote inakwenda kinyume na fikira zao. Haihitaji watu wamtamani kabisa au wawe na mwonekano wa kunyenyekea Kwake; badala yake, wanapaswa kufikia uchaji wa kweli na utiifu wa kweli. Katika kazi Zake nyingi, mtu yeyote mwenye uzoefu wa kweli anahisi heshima Kwake, ambayo ni ya juu kuliko matamanio. Watu wameiona tabia Yake kwa sababu ya kazi Yake ya kuadibu na hukumu, na kwa hiyo wanamcha mioyoni mwao. Mungu anapaswa kuogopwa na kunyenyekewa, kwa sababu nafsi Yake na tabia Yake si sawa na za viumbe vilivyoumbwa, na ziko juu ya zile za viumbe vilivyoumbwa. Mungu hategemei chochote ili kuwepo na ni wa milele, Yeye siye kiumbe Aliyeumbwa, na ni Mungu tu anayestahili uchaji na utiifu; mwanadamu hana sifa ya kupewa hivi. Hivyo, watu wote waliopitia uzoefu wa kazi Yake na kweli wanamjua wanampatia heshima. Hata hivyo, wale ambao hawaachi mawazo yao kumhusu, yaani, wale ambao hawamwoni kuwa Mungu, hawana uchaji wowote Kwake, na hata ingawa wanamfuata hawajashindwa; ni watu wasiotii kwa asili yao. Anafanya kazi hii ili apate matokeo kwamba viumbe vyote vilivyoumbwa viweze kumcha Muumba, vimwabudu Yeye, na kujikabidhi katika utawala Wake bila masharti. Haya ni matokeo ya mwisho ambayo kazi Yake yote inalenga kuyapata. Ikiwa watu ambao wamepitia kazi hiyo hawamchi Mungu, hata kidogo, kama kutotii kwao kwa zamani hakutabadilika kabisa, basi watu hawa ni hakika wataondolewa. Kama mtazamo wa mwanadamu kwa Mungu ni kumtamani au kuonyesha heshima kwa mbali na sio kumpenda, hata kidogo, basi haya ndiyo matokeo ambayo mtu asiye na moyo wa kumpenda Mungu yamefikia, na mtu huyo anakosa vigezo vya kukamilishwa. Ikiwa kazi nyingi sana haziwezi kupata upendo wa kweli wa mtu, hii ina maana kwamba mtu huyo hajampata Mungu na kwa uhalisi hatafuti kuujua ukweli. Mtu ambaye hampendi Mungu hapendi ukweli na hivyo hawezi kumpata Mungu, sembuse kupata kukubaliwa na Mungu. Watu kama hao, bila kujali jinsi wanavyopata uzoefu wa Roho Mtakatifu, na bila kujali jinsi gani wanapitia uzoefu wa hukumu, bado hawawezi kumcha Mungu. Hawa ni watu ambao asili yao haiwezi kubadilishwa, ambao wana tabia ya uovu uliokithiri. Wale wote ambao hawamchi Mungu wataondolewa, na kuwa walengwa wa hukumu, na kuadhibiwa kama tu wale ambao wanafanya uovu, watateseka hata zaidi ya wale ambao wamefanya matendo maovu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu

Iliyotangulia: G. Juu ya Jinsi ya Kutimiza Wajibu wa Mtu vya Kutosha

Inayofuata: I. Kuhusu Jinsi ya Kuchagua Njia ya Mtu katika Imani

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp