Mwanadamu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu
Mwanadamu amekuwa akiishi katika funiko la ushawishi wa giza, huku akiwa amezuiliwa bila ya kuachiliwa na ushawishi wa Shetani. Nayo tabia ya mwanadamu, baada ya kutengenezwa na Shetani, inaendelea kuongezeka kuwa potovu. Mtu anaweza kusema kwamba binadamu huishi daima na tabia yake potovu ya kishetani, asiweze kumpenda Mungu kikweli. Kwa sababu ya hili, kama mwanadamu anataka kumpenda Mungu, lazima anyang’anywe kujidai kwake, kujigamba, kiburi, majivuno, na sifa nyingine kama hizo zinazomilikiwa na tabia ya Shetani. La sivyo, upendo wake si safi, ni upendo wa kishetani, na ule ambao hauwezi kabisa kupokea idhini ya Mungu. Bila kukamilishwa, kushughulikiwa, kuvunjwa, kupogolewa, kufundishwa nidhamu, kuadibiwa, au kusafishwa na Roho Mtakatifu moja kwa moja, hakuna yeyote anayeweza kumpenda Mungu kwa kweli. Ukisema kwamba sehemu ya tabia yako inamwakilisha Mungu na hivyo basi unaweza kumpenda Mungu kwa kweli, basi wewe ndiwe unayezungumza maneno ya kiburi na ni mtu wa upuuzi. Binadamu kama hao ni malaika mkuu! Asili ya ndani ya binadamu haiwezi kumwakilisha Mungu kwa njia ya moja kwa moja. Lazima binadamu aiondoe asili yake ya ndani kupitia kwa ukamilifu wa Mungu, na kisha kupitia kutunza na kutosheleza mapenzi ya Mungu tu, na hata zaidi kupitia kwa kazi ya Roho Mtakatifu, ndipo kuishi kwa kudhihirishwa kwake kunaweza kuidhinishwa na Mungu. Hakuna mtu anayeishi katika mwili anayeweza kumwakilisha Mungu moja kwa moja, isipokuwa awe mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Hata hivyo, hata kwa mtu wa namna hii, tabia yake na kile anachoishi haviwezi kusemwa kabisa kumwakilisha Mungu; mtu anaweza tu kusema kwamba kile anachoishi kinaongozwa na Roho Mtakatifu. Tabia ya mtu kama huyo haiwezi kumwakilisha Mungu.
Ingawa tabia ya mwanadamu imeamriwa na Mungu—hili halina shaka na linaweza kuchukuliwa kuwa jambo chanya—limechakatwa na Shetani. Kwa hivyo, tabia nzima ya mwanadamu ni tabia ya Shetani. Mtu anaweza Kusama kuwa Mungu, katika tabia yake, ni mnyofu katika kutekeleza mambo, na kwamba yeye pia anatenda kwa njia hii; yeye pia an tabia kama hii, na hivyo basi anasema kwamba tabia yake inamwakilisha Mungu. Huyu ni binadamu wa aina gani? Je, tabia potovu ya kishetani inaweza kumwakilisha Mungu? Yeyote yule anayetangaza kwamba tabia yake ni wakilishi kwa Mungu, huyo mtu anamkufuru Mungu na kumtukana Roho Mtakatifu! Tukiangalia namna ambavyo Roho Mtakatifu hufanya kazi, kazi ambayo Mungu anafanya hapa ulimwenguni ni kwa ajili ya kushinda pekee. Hii ndiyo maana, nyingi ya tabia potovu za kishetani za mwanadamu bado hazijatakaswa, na ndiyo maana mienendo ya maisha ya mwanadamu bado ni taswira ya Shetani. Ndicho ambacho mwanadamu anaamini kuwa kizuri na kinawakilisha matendo ya mwili wa mwanadamu, au, ili kuiweka kwa usahihi zaidi, kinamwakilisha Shetani na hakiwezi kabisa kumwakilisha Mungu. Hata kama binadamu tayari anampenda Mungu hadi kufikia kiwango ambacho anaweza kufurahia maisha ya mbinguni hapa ulimwenguni, anaweza kutamka kauli kama vile: “Eh Mungu! Siwezi kukupenda vya kutosha,” na kwamba amefikia eneo la juu zaidi, huwezi kusema kwamba anaishi kwa kumdhihirisha Mungu au kumwakilisha Mungu, kwani kiini cha binadamu ni tofauti na kile cha Mungu. Binadamu hawezi kamwe kuishi kwa kumdhihirisha Mungu, sembuse kuwa Mungu. Kile ambacho Roho Mtakatifu anamwelekeza binadamu kuishi kwa kudhihirisha ni kulingana tu na kile ambacho Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu.
Vitendo vyote na matendo ya Shetani vinaonyeshwa kupitia kwa binadamu. Sasa vitendo vyote na matendo yote ya binadamu ni maonyesho ya Shetani na hivyo basi haviwezi kumwakilisha Mungu. Binadamu ni mfano halisi wa Shetani, na tabia ya mwanadamu haiwezi kuiwakilisha tabia ya Mungu. Baadhi ya wanadamu ni wenye tabia nzuri; Mungu anaweza kufanya baadhi ya kazi kupitia kwa tabia hiyo nayo kazi yao inatawaliwa na Roho Mtakatifu. Ilhali tabia yao haiwezi kumwakilisha Mungu. Kazi ambayo Mungu hufanya ndani yao ni kule tu kufanya kazi na pamoja na kupanua kile ambacho tayari kimo ndani yao. Wawe ni manabii au wanadamu wanaotumiwa na Mungu kutoka kwa enzi zilizopita, hakuna yeyote anayeweza kumwakilisha Mungu moja kwa moja. Binadamu wote huja kumpenda Mungu kwa sababu tu ya shurutisho kutoka kwa mazingira yao, na hakuna kati yao ambaye hujitahidi kushiriki kwa hiari yake. Ni mambo gani chanya? Yote ambayo hutoka kwa Mungu moja kwa moja ni chanya. Hata hivyo, tabia ya mwanadamu imechakatwa na Shetani na haiwezi kumwakilisha Mungu. Ni Mungu mwenye mwili tu—mapenzi Yake, nia Yake ya kuteseka, haki, utiifu, unyenyekevu na kujificha Kwake—hivi vyote humwakilisha Mungu moja kwa moja. Hii ni kwa sababu Alipokuja, Hakuwa na asili ya dhambi na alikuja moja kwa moja kutoka kwa Mungu bila ya kuchakatwa na Shetani. Yesu yuko tu katika mfano wa mwili wenye dhambi na hawakilishi dhambi; kwa hivyo, vitendo Vyake, matendo na maneno, hadi wakati wa kabla ya kukamilisha Kwake kazi kwa njia ya kusulubiwa (pamoja na wakati wa kusulubiwa Kwake), vyote vinawakilisha Mungu moja kwa moja. Mfano wa Yesu unatosha kuthibitisha kwamba binadamu yeyote aliye na asili ya dhambi hawezi kumwakilisha Mungu, na kwamba dhambi ya binadamu inamwakilisha Shetani. Hiyo ni kusema kwamba dhambi haimwakilishi Mungu na Mungu hana dhambi. Hata kazi inayofanywa ndani ya binadamu na Roho Mtakatifu inaweza tu kuchukuliwa kuwa imetawaliwa na Roho Mtakatifu na haiwezi kusemwa kwamba ilifanywa na binadamu kwa niaba ya Mungu. Lakini kwa kadiri ambavyo binadamu anahusika, si dhambi yake wala tabia yake inamwakilisha Mungu. Kwa kuangalia kazi ambayo Roho Mtakatifu amefanya ndani kwa mwanadamu kutoka zamani hadi sasa, mtu anaona kwamba mwanadamu anacho kile anachoishi kwa kudhihirisha kwa sababu Roho Mtakatifu amefanya kazi juu yake. Ni wachache sana wanaoweza kuishi kwa kudhihirisha ukweli baada ya kushughulikiwa na kufundishwa nidhamu na Roho Mtakatifu. Ambayo ni kusema kwamba, kazi ya Roho Mtakatifu tu ndiyo iliyopo; ushirikiano kwa upande wa binadamu haupo. Je, unaliona suala hili kwa uwazi zaidi sasa? Kwa hiyo basi, ni nini unachofaa kufanya ili kufanya kazi kwa bidii pamoja na Yeye huku Roho Mtakatifu akiwa kazini na, kwa kufanya hivyo, kutimiza wajibu wako?