85 Njia Yote Pamoja na Wewe

1

Naelea na kuzurura katika dunia, nikihisi kupotea na mnyonge ndani.

Ninapoamshwa na maneno Yako ya upole, naona kuonekana kwa mwanga.

Maneno Yako yanauangaza moyo wangu, yote ni ukweli na halisi sana.

Nikitafakari mienendo yangu, yote ni maonyesho ya tabia yangu potovu.

Naanguka chini zaidi kwa majuto, nikiwa radhi kutubu na kujifanya upya.

Hukumu Yako inafichua kuwa upotovu wangu ni wa kina sana, Umeniongoza kila hatua ya njia.

Wakati niko mbali, Unaniita, na kuniongoza kutoka majaribuni.

Ninaasi na kisha Unajificha, na natumbukia katika dhiki na uchungu.

Moyo wangu unapokugeukia tena, Unatabasamu, ukinishika kwa karibu.

Shetani anaponidanganya na kuniumiza, Unaniokoa haraka na kuponya majeraha yangu.

Ninapoanguka katika mfumbato wa Shetani, Uko pamoja nami na sihisi mpweke.

Naamini kuwa asubuhi itakuja, mbingu itakuwa samawati tena.

2

Maneno na kazi Yako huniongoza, upendo Wako hunivuta nikufuate Wewe.

Nafurahia maneno Yako kila siku, Wewe ni rafiki yangu wa kila siku.

Ninapohisi dhaifu na mnyonge, maneno Yako ni lishe na nguvu yangu.

Ninapoteseka ama ninapoanguka, maneno Yako ni mkono uniinuao.

Shetani anaponizunguka, maneno Yako yananipa hekima na nguvu.

Ninapokabiliwa na majaribu, maneno Yako yananiongoza nisimame kama shahidi.

Maneno Yako yanaandama nami na kuniongoza, moyo wangu una upendo na utulivu.

Upendo Wako ni halisi sana, moyo wangu umejaa shukrani.

Naimba sifa Zako kwa sauti, Umeniokoa kutoka kwa madhara ya Shetani.

Nakuimbia Wewe, Umenitakasa na kuniokoa.

Bila hukumu Yako, singekuwa hapa sasa.

Ee, Mungu wa vitendo mwenye mwili, Umewaokoa wanadamu.

Mwenyezi Mungu, tutakupenda daima, Unastahili sana upendo wa mwanadamu!

Iliyotangulia: 84 Nataka Kupenda Mungu Zaidi

Inayofuata: 86 Ni Mungu Mwenyezi Anipendaye

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp